Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104809 articles
Browse latest View live

Lulu Michael Afunguka Baada ya Mtu Kumzushia Kuwa Alihusika Kusababisha Ajali iliyotokea Jana..' Adai Mungu Atawalipa'

$
0
0
Wengi wamefurahia ushindi wa Waigizaji wa Tanzania Lulu pamoja na Richie kwenye tuzo za Africa Magic Viewer’s Choice Awards 2016 na sasa tumeendelea kushuhudia comments na post mbalimbali kwenye mitandao ya kijamii baada ya ushindi huo ambapo uhuru ambao kila mmoja anao kuandika chochote kwenye mitandao hii unaweza kufikia kukwaza watu wengine
Lulu ambaye alishinda tuzo ya Movie bora Afrika Mashariki kupitia movie yake ya ‘Mapenzi’ alihuzunishwa na post moja iliyoandikwa kwenye mtandao wa Instagram ikisema >>> ‘Jamani umbea mtamu khaaaa, yani umbea mtamu kama kuku jamani, bwana leo kuna mtu kanifata DM kanipa Umbea na mimi sitaki kuongeza chumvi
Haya soma mwenyewe, mambo Duller? naomba unifiche jina langu, ni kweli kabisa Lulu anahusika na ajali iliyotokea jana watu wakafa wengi, mimi nipo Nigeria, alimuomba rafiki yangu Mnigeria ampeleke kwa mganga mkubwa hata wa kitoa kafara yeye atafanya, kwa mganga akaambiwa aongee yote chini ya mti na dawa akapewa ya kutupa njia panda yoyote usiku wa manane
Ajali iliyotokea Dar es salaam
Ajali iliyotokea Dar es salaam
Haya nimeambiwa na Mnigeria ambaye kampeleka ambaye ni Bwanaangu, sasa jana baada ya kumuonyesha picha ya ajali iliyotokea akasema sawa kabisa huyo ni Lulu sababu aliambiwa asipitishe siku mbili majini hayatakaa Tanzania zaidi ya siku mbili
lulu 12
Baada ya Lulu kuiona hii post aliichukua kama ilivyo na kuiweka kwenye page yake ya Instagram na kuandika yafuatayo… ‘Jamani mpaka sasa hivi mshaongea vitu vingi sana na nimekaa kimya, okay kwa hili siwezi kujua ni watu kiasi gani wataamini na wengine hawataamini, kilichonifanya nipate tuzo au mafanikio ni Mungu, juhudi zangu pamoja na watu walionipigia kura
Sijawahi na wala sina fikra za kutumia nguvu yoyote ya ziada kupata mafanikio, kama mnahisi maneno na uongo vinaweza kunirudisha nyuma kwa hali yoyote nawaombeeni muishi maisha mengi muone Mungu anavyozidi kuniinua, wewe uliyepost na huyo aliyekutumia msg sibishani na nyie ila imani yangu ntaongea na Mungu wangu tu, mtajutia mlichokifanya hata kama ikiwa baada ya miaka 50 mana najua Mungu anajibu kwa wakati
Lulu 11
Chanzo:Millard Ayo

TRA: Zanzibar kichaka cha kukwepa kodi

$
0
0

Wakati Rais John Magufuli akipambana na wakwepa kodi ili kuhakikisha uchumi wa nchi unakuwa, takwimu za zinaonyesha uwapo wa wafanyabiashara wanaopitisha bidhaa za magendo kwa njia ya panya kati ya mianya 509, Zanzibar inaongoza kwa kuwa na mianya 422,  huku Tanzania Bara ikiwa na mianya 87.

Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, kuhusu mwenendo wa ukusanyaji wa mapato, matumizi ya mashine za kielektroniki katika ukusanyaji kodi (EFD), kusitishwa kwa bei elekezi na usajili wa vyombo vya moto, Kaimu Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Alphayo Kidata, alisema bidhaa hizo hupitishwa Bandari ya Tanga na Mtwara zikitokea Zanzibar.

Alisema hali hiyo isipodhibitiwa haraka inaweza kusababisha madhara kwa sababu licha ya Bandari ya Dar es Salaam kuchangia mapato kwa kudhibiti wafanyabaishara wanaokwepa kodi katika kipindi kifupi cha uongozi wa Rais Magufuli, bado kuna haja ya kuandaliwa mazingira rafiki yatakayowabana wakwepa kodi wanaotumia njia hizo za panya.

Alisema licha ya Bandari ya Dar es Salaam na mashine za EFDs, kuchangia kuongezeka kwa mapato, pia mamlaka hiyo imeboresha mfumo wa udhibiti wa ukwepaji kodi kwa wafanyabaishara hasa katika kipindi hiki cha uongozi wa Rais Magufuli.

“Mianya ya panya ni mingi na inabidi idhibitiwe haraka, tukiangalia mara moja, Zanzibar kuna mianya 422 inayopitisha bidhaa za magendo, wakati Tanzania Bara ni 87, tusiridhike na kiwango hicho kidogo ila iwekezwe nguvu kubwa kumaliza tatizo hilo,” alisema Kidata.

Akitoa mchanganuo wa makusanyo ya kodi ya ndani, alisema kwa Februari mamlaka hiyo imekusanya Sh. trilioni 1.040 kwa Tanzania Bara na Visiwani sawa na asilimia 101.18 ya lengo la serikali kufikisha Sh. trilioni  1.028.
Alisema kwa Januari, TRA ilikusanya kiasi cha Sh. trilioni 1.079  kwa Tanzania Bara na Visiwani sawa na asilimia 102 ya lengo la serikali kufikisha Sh.trillioni 1.059.

Alifafanua kuwa kwa kipindi cha Julai mwaka jana hadi Februari mwaka huu mapato yamefika Sh. trilioni 8.569 sawa na asilimia 99 ya makusanyo yote ya ndani.

Kwa mujibu wa Kidata, makusanyo hayo yametokana na ari na udhubutu ambao mamlaka hiyo imeweka katika kusimamia na kuhakikisha inaendelea kuziba mianya ya ukwepaji kodi ma kuweka mazingira  rafiki kwa wafanyabiashara kwa kutumia mifumo mbalimbali.

Naye Kamishna wa  Kodi za Ndani wa TRA, Yusuph Salum, alielezea mikakati ya mamlaka hiyo kwa Machi hadi Juni mwaka huu, kuwa wataendelea  kudhibiti mianya ya ukwepaji kodi, kufichua wakwepa kodi, kupambana na rushwa,   pamoja na kupanua wigo wa kodi kwa kusajili wafanyabishara ambao hawajasajiliwa kama  washereheshaji na wanataaluma.

Kadhalika, alisema TRA itasimamia kwa karibu matumizi ya mashine za EFDs na utoaji wa risiti na itafuatilia na kudai malimbikizo ya kodi kutoka kwa wadaiwa sugu pamoja na kuendeleza ukaguzi wa kodi kwa wafanyabaishara. 

“TRA iko katika mchakato wa mwisho wa kubadilisha mfumo wa kusimamia mapato ya ndani, hivyo kupitia bajeti ya serikali ya 2017/17, kutakuwapo na utaratibu mpya utakaochangia ukuaji wa mapato,”alisema Salum.

Kwa upande wake Kamishna wa Idara ya Forodha, Akonary Kaima, aliongeza kuwa matumizi  ya bei elekezi katika mchakato wa uthaminishaji wa bidhaa bandarini ni kinyume cha sheria ya Jumuiya ya Afrika Mashariki, hivyo TRA itaendelea na shughuli za kiforodha kulingana na sheria bila kuathiri eneo jingine.

“Kwa sababu TRA, itadhibiti ukaguzi na uthaminishaji halisi, kila mfanyabaishara anatakiwa kulipa ushuru na kodi kulingana na thamani ya bidhaa husika,”alisema.

Alifafanua kuwa, kuna magari yaliyoingia nchini na kusajiliwa bila kufuata taratibu za forodha na  kusababisha yamilikiwe kinyume cha taratibu, hivyo wamiliki wajisalimishe TRA, kufanyiwa uhakiki ikiwa ni pamoja na kuyalipia kodi.

Forbes rates Dangote richer than Trump, Abramovich, Oprah put together

$
0
0
Aliko Dangote, president of Dangote group, is now richer than Donald Trump, Republican front runner; Roman Abramovich, owner of Chealsea football club and Oprah Winfrey, the richest black woman, put together.

Dangote, who came in at the 51st position of the 2016 ranking by Forbes Magazine, is also richer than the combination of all other Nigerians who made the list.

Despite losing $300 million from $15.7 billion (N3.1 trillion) to about $15.4 billion, (N3.05 trillion) in the latest rankings, Dangote remains the richest black billionaire anywhere on the planet.

At $15.4 billion, the 58-year-old is richer than Abramovich ($7.6 billion), Oprah ($6.2 billion) and Trump $4.5 billion.

The Nigerians who made the list are Mike Adenuga ($10 billion), Femi Otedola ($1.8 billion), Folorunsho Alakija ($1.6 billion) and Abdulsamad Rabiu ($1.1 billion), who came in at 103, 1,011, 1,121 and 1,577 respectively.

Bill Gates remains the richest person in the world with a net worth of $75 billion, “despite being $4.2 billion poorer than a year ago. He has been No. 1 one for 3 years in a row and topped the list 17 out of 22 years”.

Amancio Ortega moves up to the second spot for the first time, displacing Mexico’s Carlos Slim, who slips number four, while Warren Buffett remained steady in third position.

Facebook’s Mark Zuckerberg had the best year of all billionaires, the 31-year-old adding $11.2 billion to his fortune and moved up 10 places from 16 to the sixth spot.

The global economic volatility and plunge in commodity prices also affected the billionaires’ list, as the 16 billionaires fell of the list.

“Volatile stock markets, cratering oil prices and a stronger dollar led to a dynamic reshuffling of wealth around the globe and a drop in ten-figure fortunes for the first time since 2009,” Forbes said.

“For our 30th annual guide to the world’s richest, we found 1,810 billionaires, down from a record 1,826 a year ago. Their aggregate net worth was $6.48 trillion, $570 billion less than last year.

“It was also the first time since 2010 that the average net worth of a billionaire dropped – it is now $3.6 billion, $300 million less than last year.”

Alakija was negatively affected by the fall in oil prices, while Dangote took a hit due to a fall in the Nigerian currency, naira.

“Her first company was a fashion label that catered to Nigeria’s elite women, including the wife of former military president, Ibrahim Babangida, who awarded Alakija’s company an oil prospecting license. Alakija’s net worth has fallen in the past year as a result of lower oil prices,” Forbes said.

As Africa’s largest cement producer, Dangote owns about 90 percent of publicly-traded Dangote Cement through a holding company, a percentage that exceeds the 80 percent ownership ceiling set by the Nigerian Stock Exchange.

In 2015, Dangote and 61 others were richer than 3.5 billion people around the world.

Soma Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Ijumaa ya March 11, Ikiwemo ya Lowassa Bado ni Shida CCM

$
0
0
Soma Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Ijumaa ya March 11, Ikiwemo ya Lowassa Bado ni Shida CCM

Marekani Yatia Mguu Tanzania....Yataifisha Mali za Mtanzania Kigogo wa Madawa Ya Kulevya

$
0
0
Serikali ya Marekani imeamua kutaifisha mali za mfanyabiashara wa dawa zilizopigwa marufuku za kulevya kutoka Tanzania, Ali Khatib Haji Hassan, maarufu kwa jina la “Shikuba” na mtandao wake na kupiga marufuku kampuni za nchi hiyo kujihusisha na biashara zake.

Shikuba, ambaye amekuwa akihusishwa na biashara kubwa ya usafirishaji dawa za kulevya kati ya Afrika Mashariki, Asia, Ulaya na Marekani, alikamatwa mwaka 2014 nchini Tanzania akihusishwa na shehena ya kilo 210 za heroin zilizokamatwa mkoani Lindi mwaka 2012.

Taarifa iliyotolewa juzi na kitengo cha udhibiti wa mali za nje cha Wizara ya Fedha ya Marekani imeeleza kuwa serikali imemtambua Shikuba kama kinara wa usafirishaji wa dawa za kulevya kwa mujibu wa Sheria ya Utambuzi wa Vinara wa Dawa za Kulevya wa Nje (Foreign Narcotics Kingpin Designation Act) ya Marekani.

“Hassan (pichani) ni kinara mkubwa wa kimataifa wa dawa za kulevya ambaye anasafirisha mamilioni ya tani za heroine na cocaine kwenda barani Afrika, Asia, Amerika Kaskazini kwa kutumia mtandao wake uliopo Afrika Mashariki,” inasema taarifa hiyo ya Serikali ya Marekani iliyotolewa Washington juzi.

“Kutokana na uamuzi wa leo (juzi), mali zote za Hassan na mtandao wake ambazo ziko ndani ya mamlaka ya Marekani au kwenye mikono ya raia wa Marekani zinataifishwa.”

Sheria hiyo ya Marekani ilipitishwa mwaka 1999 na kuanza kazi mwaka uliofuatia, ikiwa na lengo la kudhibiti wasafishaji wa dawa za kulevya, biashara na shughuli zao kuingia kwenye mfumo wa kifedha wa nchi hiyo na kudhibiti biashara na miamana baina ya wasafirishaji wa dawa hizo na kampuni za Marekani na raia wake.

Kwa mujibu wa gazeti la The New York Times, sheria hiyo imekuwa ikitumiwa na Marekani kufuatilia wahalifu kadhaa wanaojihusisha na biashara hiyo duniani.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo ya Marekani, Hassan amekuwa akijaribu mara kadhaa kurubuni viongozi wa Serikali za Afrika kuepuka kukamatwa na kufunguliwa mashtaka kutokana na biashara zake haramu.

“Uamuzi wa leo unaweka vikwazo kwa Ali Khatib Haji Hassan na mtandao wake kusafirisha heroine na cocaine duniani na kumzuia kutumia faida haramu kurubuni maofisa wa Serikali za Afrika,” anasema kaimu mkurugenzi wa OFAC, John E. Smith katika taarifa hiyo.

“Wasafirishaji wa dawa za kulevya kama Mtandao wa Usafirishaji Dawa za Kulevya wa Hassan ni tishio kubwa kwa uthabiti wa mfumo wa kimataifa wa fedha na kanda, na Hazina inaendelea kuwa thabiti katika kuuanika na kufuatilia na wale wanaochochea biashara hiyo duniani.”

Tangu mwaka 2006, amekuwa akiongoza wanachama wa mtandao wake kutuma shehena za dawa hizo kwenda sehemu kadhaa duniani kama China, Ulaya na Marekani.

Hassan alikuwa msambazaji wa kwanza kwa wasafirishaji dawa za kulevya wa Tanzania ambao mara kwa mara walikuwa wakipokea maelfu ya kilo za heroine kutoka pwani ya Makran nchini Pakistan na Iran.

Hassan, pia alisimamia mtandao wa wasafirishaji hao barani Amerika Kusini na kuzisafirisha hadi Afrika Mashariki, zikiwa njiani kwenda Ulaya na China.

Akizungumzia hatua hiyo, aliyekuwa Kamishna wa Kikosi cha Kupambana na Dawa za Kulevya nchini, Godfrey Nzowa alisema Hassan alikamatwa Januari mwaka 2014 Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere (JNIA) baada ya mbinu nyingi kugonga mwamba.

“Mtandao wa Shikuba ulikamatwa mapema kabla yake na ilituchukua muda mrefu kumkamata baada ya mbinu zetu nyingi kugonga mwamba,” alisema.

Kuhusu sheria, Kamanda Nzowa alisema iwapo itahakikishwa kuwa Hassan amepata mali zake kwa njia ya kuuza dawa za kulevya, zitataifishwa kama walivyofanya Marekani.

Sifa za Wanaume Katika Mahusiano na Mapenzi Kutokana na Majina yao

$
0
0
Majina ya wanaume na Sifa zao katika mahusiano yao na mapenzi

1. Dennis-mapenzi ya tamthiliya

2. Nicolas-muongo

3. Albert-domo zege ila mjanja mjanja

4. Mathias-anapenda mwanamke kwa muda mrefu

5. Joseph/Josephat-kicheche

6. Jeryson-anapenda mademu ila wanawake wanamkataa

7. Shadrack-anapenda sifa kwa mademu

8. Richard-ana wapenzi wengi ila msiri

9. Mathew-anapendwa na wanawake ila domo zege

10. Thomas-anapendwa na mademu ila hajatulia

11. Prosper-hajui habari za mapenzi

12. Fidelis-mtaalam wa kutongozea mademu wenzie(kuwadi)

13. Peter-maneno mengi ila vitendo sifuri

14. Christopher-wanapenda kutongoza hovyo ingawaje wana mpenzi mwaminifu

15. Elvis-Handsome ila hapendwi na mademu

16. Edward/Eddy -serious sana kwenye mapenzi

17. Mussa-mwepesi kutongoza na mwepesi kuwacha

18. Ally-wasiri sana kwenye mapenzi

19. Mohammed-anapenda watu waliomzidi umri

20. Nickson-wakiingia kwenye mapenzi wanatendwa vibaya

21.Frederick-anapenda sifa kwa wanawake ili apendwe

22. Jimmy-wana mapenzi ya kejeli

23. Elias-anapenda mademu ila anaogopa kuwaambia

24. Frank-huyu mpole, hajui kudanganya, wanawake wanajitongozesha wenyewe

25. Joachim-hana habari na nademu, anaamini ipo siku ataoa tu

26. Benjamin-anapenda achape tu atembee

27. Steven-hana habari kabisa na wanawake ila ana bahati ya kupendwa

28. Gerald-mpole na antulia na mpenzi mmoja kwa mda mrefu

29. Elisha-anapenda wanawake wanaochukiwa katika jamii

30. Benard-akipenda kapenda

31. Daudi-hawa kazi yao ni kuchafua wanawake wa mtaani na jamii inayozungukwa

32. Davis-anapenda sehemu sahihi lakini uacha na kupotea pabaya.

33. Daniel-ana maneno mengi sana na ni muongo

Donald Trump Hakamatiki Tena Urais Marekani, Hillary Clinton Ajipanga Upya...

$
0
0
Wagombea wawili wakuu wa urais wa vyama vya Republican, Dolald Trump na Democratic, Hillary Clinton nchini Marekani wameshinda kwenye kura za maoni katika majimbo ya Missisipi na Michigan.

Bilionea Trump amemshinda mpinzani wake wa karibu, Seneta Ted Cruz, ukiwa ni ushindi wake wa 13 kwenye kura za  mchujo za chama chake cha Republican.

Kabla ya ushindi huo, Trump alikuwa mbele kwa kura za wajumbe 384 dhidi ya 300 za Cruz.

Wadadisi wanasema ushindi huo umezima uvumi wa mwishoni mwa wiki iliyopita kuwa kampeni ya Trump ilikuwa imepoteza kasi.

Baada ya kupata ushindi huo, Trump alisema anakiongezea umaarufu Republican.

Mshindani wake mkuu, Seneta Ted Cruz naye alipata ushindi katika jimbo dogo la Idaho.

Naye Hillary ameshinda kwa urahisi kwenye jimbo hilo la Missisipi linalokaliwa na Wamarekani wengi wenye asili ya Afrika, dhidi ya mshindani wake wa karibu ndani ya chama chake, Bernie Sanders.

Kati ya wajumbe 36 wa jimbo hilo, Hillary amejinyakulia kura za wajumbe 21. Kwa ujumla, mke huyo wa rais wa zamani, anaongoza kwa wajumbe 1,155 mbele ya Sanders mwenye kura za wajumbe 502.

Ili mtu kuweza kuteuliwa kuwa mgombea, anahitaji kupata kura za wajumbe 2,383.

Trump ambaye hata hivyo, aliangushwa na Cruz kwenye jimbo la Idaho, aliwaambia wafuasi wake mjini Michigan kuwa kwa sasa ana uhakika wa kuwa Rais wa Marekani.

“Tupo mbele kwa kiasi cha asilimia 50 au zaidi. Hapo unazungumzia mamilioni ya watu.

Naamini kabisa kuwa hii ni habari kubwa kabisa kwenye siasa, na ninatarajia Warepublican wataipokea. Tuna Democrat wanakuja, tuna wagombea huru wanakuja, lakini hawana idadi hiyo na pengine kamwe hawatakuwa nayo,” alisema Trump.

Hillary Clinton ambaye ni waziri wa zamani wa mambo ya nje wa Marekani, alilichukua kwa urahisi jimbo la ghuba ya kaskazini la Missisipi, ambalo lina wafuasi wengi wa Democratic.

Tayari mke huyo wa rais wa 42 wa Marekani, amejikingia zaidi ya nusu ya kura wa wajumbe 2,382 zinazohitajika kuteuliwa kupeperusha bendera ya kuwania kiti hicho, akiwekeza zaidi kampeni zake kwenye uwezo wa Wamarekani kujiamini katika kuleta mabadiliko, mfano wa ilivyokuwa kampeni ya Rais Barack Obama.

“Usimruhusu mtu kukwambia kuwa hatuwezi tena kufanikiwa Marekani. Tunaweza, tunafanikiwa na tutafanikiwa. Lakini ili hilo liwe, hatuwezi kujenga kwenye kuta kongwe au kurejesha majira ya saa nyuma. Tunapaswa kujenga juu ya kile kinachoifanya Marekani kuwa taifa kubwa, nishati, matumaini, uwazi na ubunifu wetu,” aliwaambia wafuasi wake.

Sanders bado aonyesha dhamira

Licha ya kuwa hesabu za kura zinamuweka Hillary mahala pazuri zaidi mpinzani wake, Sanders ameibuka kuwa mwanasiasa mwenye dhamira ya dhati ya kusonga mbele.

Katika jimbo la Michigan, mzee huyo wa miaka 74 ambaye ana uzoefu wa harakati za kisiasa kwa zaidi ya miaka 50, amemuangusha Hillary kwa asilimia 2.

Anatajwa kuwavutia zaidi wapiga kura vijana kwa kampeni yake ya mapinduzi ya umma, usawa wa kiuchumi na mapambano dhidi ya kile anachokiita “mfumo wa kifisadi wa kisiasa”

“Watu wa Marekani wanasema kuwa wamechoka na mfumo wa kifisadi wa kampeni na ufadhili wa matajiri wakubwa, Wall Street na tabaka la mabilionea.

Wamechoka na uchumi unaoibiwa ambapo watu wa Michigan, Illinois, Ohio, wafanya kazi kwa masaa mengi kwa mshahara wa kiwango cha chini, wakiwa na wasiwasi na mustakabali wa watoto wao,” alisema mjini Michigan.

Wachambuzi wanasema iwapo Sanders hatafanikiwa kuitwaa tiketi ya Democratic kuwania urais, kama ambavyo amewahi kuikosa huko nyuma, athari yake kwenye siasa za sasa za Marekani ni kuweza kudharaulika.

Uchaguzi huo umefanyika siku chache baada ya wagombea wakuu wa Republican kushinda majimbo mawili kila mmoja katika kura ya mchujo.

Cruz ameshinda majimbo ya Kansas na Maine huku Trump, akitwaa majimbo ya Louisiana na Kentucky.

Trump ameshinda majimbo mengine kadhaa ya awali na anaongoza wapinzani wake katika Republican, jambo linalowatia wasiwasi vigogo wa chama hicho wakisema sera na kauli zake zinakwenda kinyume na maadili ya Marekani.

Cruz anasema yeye ndiye anaweza kuwa mgombea mbadala wa bilionea huyo wa New York.

Wagombea wengine 12 wa Republican walijotoa kwenye mbio hizo baada ya kufanya vibaya katika hatua za awali na hivyo kufanya uwanja kusaliwa na wanasiasa wanne.

Kwa upande wa Democratic, Hillary Clinton amemshinda Louisiana huku mpinzani wake seneta Bernie Sanders akishinda Kansas na Nebraska.

Akihutubia wapinzani wake amesema demokrasia ya Marekani haipaswi kuharibiwa na mabilionea.

Awali wagombea hao wa Democratic walichuana vikali katika mdahalo uliofanyika juzi huku kila mmoja akitamba kuwa katika nafasi nzuri ya kukabiliana na mgombea yoyote kutoka Republican.

Wagombea hao wanaotafuta tiketi ya kugombea urais wa Marekani wamesema wapo tayari kupambana na Trump.

Hillary na Sanders, walisema kwamba wako tayari kupambana na Trump kwenye uchaguzi mkuu ujao.

Wakizungumza wakati wa mdahalo uliofanyika mjini Flint katika jimbo la Michigan, walisema midahalo yao ni tofauti na ile ya Warepublican.

Wamedai hivi karibuni wamekuwa wakishambuliana na kurushiana matusi.

Sanders aliibua kicheko aliposema Warepublican wamedhihirisha waziwazi kwa nini utawala wake utalipa kipau mbele suala la kuwekeza kwa taasisi za kushughulikia afya ya akili.

Wakazi wa mji wa Flint, wengi wao wakiwa ni watu weusi maskini, wamekuwa wakikabiliana na mzozo wa maji yaliyo na kemikali za chuma.

Suala hilo limezua mtafaruku baina ya viongozi wa Serikali kwa miezi kadhaa.

Wanasiasa hao wawili, walimtaka Gavana wa Jimbo la Michigan, Rick Snyder kujiuzulu kufuatia kashfa hiyo.    

It Is Official: Diamond Platnumz Cries After Tiffah's DNA Results In S.Africa....His Mother Shocked

$
0
0
Tanzania’s superstar Diamond Platnumz is the biological father of Latifah Dangote, DNA tests conducted on Diamond, Zari Hassan and Latifah have confirmed.
Tanzania’s Amani newspaper reports that the Bongo Fleva giant bowed to pressure from sections of fans and critics who claimed there could be a possibility that he did not sire Latifah Dangote.

In a bid to put the confusion to bed, Diamond Platnumz, Zari Hassan and Latifah Dangote traveled to South Africa to conduct the DNA test on baby Tifah – ostensibly a faraway land that no Tanzanian paparazzi or snoops would get scoop.
An insider who is very close with the Utanipenda star shared exclusive details of what transpired in South Africa.

“Diamond and his family (Zari and Tifah) recently traveled to South Africa to conduct DNA test on baby Tifah,” said the source.

“He (Diamond) was bothered and disturbed by the constant persecution by fans who wanted a DNA test on baby Tifah. He was confused; he was in a dilemma. In a bid to clear the paternity issue, he asked Zari to accompany him to South Africa so that they could conduct DNA test on the baby before he leaves for the United States,” revealed the source.

DNA test results
“The DNA tests confirmed Nasib Abdul Juma (Diamond Platnumz) to be the biological father of Latifah Dangote. Diamond shed a lot of tears…It hurt him the more when some quotas referred to Ivan Ssemwanga (Zari’s ex-husband) as the little one’s father. Others claimed that Tifah was sired by a Tanzanian tycoon. A lot was said,” added the source.

Diamond’s mother shocked
Diamond’s mother Sanura Kasim ‘Sandra’ was shocked by the news as all through she had her doubts about her granddaughter’s paternity – doubts that were cultivated in her by social media discussions which largely claimed that her son Diamond was taking care of someone else’s child.

Diamond responds
“People talked a lot, created a lot of lies. I was not worried nonetheless. All through I knew the baby is mine; though just to make myself happier and more peaceful, I decided to conduct a DNA test on Tifah,” said Diamond.

“Tifah is my daughter, completely! I am extremely overjoyed by the results (DNA). That’s why I am now freer, happier and having a good time. When you happen to visit my office, you will notice I have hung framed photos of Tifah everywhere. I am not worried at all. I can now courageously face my critics,” affirmed Diamond Platnumz.

The Tanzanian top act also responded to why he shed tears.
“It (crying) is not an issue. What did you expect me to do after getting results that I dearly needed, especially at a time when sections of the society constantly claimed that I wasn’t my daughter’s biological father?”

Diamond says he embraced DNA testing of his child – a practice that he says is not popular among Tanzanians – because he wanted to be a hundred percent sure of his status as a father.
Diamond Platnumz and Zari Hassan welcomed Baby Latifah Dangote in August 6, 2015.
credit; citizentv

Dida wa Times FM Aeleza Kisa cha Kutukanwa na Mke Mdogo wa Mzee Yussuf

$
0
0
Mtangazaji wa Kipindi cha Mitikisiko ya Pwani kupitia Times FM, Khadija Shaibu ‘Dida’ amefunguka na kuzungumzia sababu ya kutukanwa katika mtandao wa kijamii na mke mdogo wa Mzee Yussuf, Chiku.

Mzee Yussuf Jumanne hii aliamua kuwaondoa wake zake wawili Leyla Rashid na Chiku katika mtandao wa Instagram baada ya kuwa wanatupiana maneno machafu kupitia mtandao huo hali ambayo inadaiwa ilikuwa inamchafua mume wao.

Akizungumza na Bongo5 Ijumaa hii, Dida amedai alitukanwa na Chiku ambaye ni mke mdogo wa Mzee Yussuf kwa madai alikuwa anampendelea mke mkubwa wa Mzee Yussuf, Leyla Rashid.

“Kusema ukweli kila mtu anajua jinsi wake zake Mzee Yussuf, Leyla Rashid na Chiku pamoja na wifi yao walivyokuwa wanarushiana matusi. Lakini mimi kama mimi niliwaHi kuzungumza na Chiku na baadaYe Leyla, lakini nilianza Chiku. Kila mmoja alikuwa anaeleza tatizo nini na kwanini wamekuwa wakitukanana katika mitandao ya kijamii, hawaoni kama wanamuaibisha mume wao! Basi kila mmoja akawa anazungumza kwa pande wake, siku nimezungumza na Leyla akazungumza mambo mengi sana, sasa Chiku baada ya kusikia akawa ananitukana mimi kupitia mitandao,” amesema Dida.

“Mimi binafsi sikumjibu vibaya nikawa namuelewesha nini maana ya uke wenza lakini akawa anaendelea kunitukana. Nikasema Mzee Yussuf ndiye anaweza kumaliza tofauti zao, ngoja nimtafute ili nizungumze naye, akakubali lakini siku ambayo aliniambia nitaongea naye akaniambia amepata dharura na pia hawezi kuja na kuzungumzia mgogoro wa familia yake kwani ataumaliza mwenyewe,” alisema Diva.

Bongo5 ilijaribu kumtafuta Mzee Yussuf ili kuzungumzia suala hilo kwakuwa linamshushia heshima yake, lakini alikataa na kusema tayari ameshafunga ukurasa wa kuzungumzia masuala ya wake zake kwenye vyombo vya habari.

Pia Mzee Yussuf alidai tayari ameshawakataza wake zake kutumia mtandao wa Instagram kwa kuwa ndio chanzo cha ugomvi wao huku na yeye akijipanga kuondoka katika matumizi ya mtandao huo.

Hata hivyo Bongo5 haikuishia hapo, ilizungumza na mtu wa karibu wa Mzee Yussuf ambaye hakutaka kutajwa jina lake na kueleza jinsi mgogoro huo unavyomuumiza kichwa Mzee Yussuf.

“Kweli amewaambia hakuna mtu kutumia mitandao wa Instagram na atakayetumia kwa siri ndiyo talaka yake. Unajua haya mambo huwezi kujua nani ni mkorofi kwa sababu unashangaa tu mambo yamezuka na huwezi kuelewa chanzo chake ni nini. Lakini hii hali inamuumiza sana Mzee kusema kweli, sema watu wa nje wanamchukulia poa,” alisema.

Chanzo:Bongo5

Zitto Kabwe Amshukia Tena Magufuli, Hasara ya 36 Bilioni Toka Aingie Madarakani

$
0
0
Tshs bilioni 8 kila mwezi TANESCO bado wanalipa IPTL. Rais haijampendenza kumaliza ufisadi huu. IPTL nadhani ni Jipu la Mgongoni ( kwa kutumia maneno ya Hidaya wa Richard Mabala ).
Rais, kwa kutochukua kwake hatua, ameshaliingizia taifa hasara ya tshs 36 bilioni toka aingie madarakani".-Zitto Kabwe

Nilimpenda Jackie Cliff ila Sitarudiana Nae Tena-Juma Jux

$
0
0
Msanii Jux ambaye kwa sasa yupo kimahusiano na Vanessa Mdee, amefunguka na kuweka wazi sakata ambalo lilimkuta mpenzi wake wa zamani anayefahamika kama Jackie Cliff na mahusiano yake na model huyo.

Kupitia kipindi cha Mkasi kinachorushwa na EATV Jux alikiri wazi kuwa alikuwa akitoka kimapenzi na Jackie Cliff na kusema alikuwa anampenda sana licha ya bidada huyo kumzidi umri.
Jux alidai katika kipindi chote ambacho wapo katika mahusiano hakuwahi kutambua wala kuhisi kama Jackie Cliff alikuwa akijihusisha na biashara ya dawa za kulevya mpaka siku alipopata taarifa kuwa amekamatwa ndipo alipojua suala hilo.

"Kiukweli nilimpenda sana Jackie Cliff maana mara nyingi mimi napokuwa na mtu huwa napenda kweli sababu huwa nahitaji kutulia, lakini huwezi amini sikuwahi kutambua kama Jackie Cliff anafanya mambo hayo mpaka alipopata matatizo hayo ndiyo najua mimi, hivyo ilinipa wakati mgumu sana mimi kiasi kwamba nilikuwa sijielewi". Alisema Jux

Jux aliendelea kudai kuwa wakati Jackie Cliff anapata matatizo hayo yeye alikuwa amekuja likizo Tanzania hivyo ndiyo siku hiyo hiyo 'Producer' wake Manecky alipompigia simu na kumwambia aende studio na kumwambia anapaswa kufanya kitu ndipo hapo alianza kuandika na kufanya wimbo wa 'Nitasubiri' ambao anadai walishirikiana na watu wengine studio kuutengeneza na kuandika baadhi ya mashairi kwenye wimbo ule ambao ulikuwa maalum kwake.

"Huwezi amini siku ambayo Jackie alipata matatizo Manecky alinipigia simu na kuniambia njoo studio, nilipofika pale akaniambia lazima tufanye kitu ndiyo tukaanza kuandika na kutengeneza wimbo ule, lakini ikitokea ametoka saizi Jackie Cliff sitaweza kuwa naye tena sababu tayari nishaanza maisha mapya" alidai Jux

Wavaa Vimini Wavuliwa Nguo Hadharani Jijini Mbeya

$
0
0

Wasichana wanaovaa nguo fupi za kubana na wavulana wanaovaa milegezo  jijini Mbeya , juzi walipata wakati mgumu baada kundi la vijana kuwavua nguo zao na kuzichana hadharani, kutokana na gari la matangazo kupita jijini hapa likiwataka watu kuvaa nguo za heshima zinazoendana na maeneo husika.


Tangu Machi 7 hadi 9, gari la matangazo ya Kampuni ya Studio H ya Huruma lilipita mitaa mbalimbali ya jijini Mbeya, likiwataka wasichana kuacha kuvaa vimini na vijana kuacha kuvaa mlegezo.


Baada ya tangazo hilo, vijana walianza kuwavamia wasichana na wavulana waliovaa milegezo maeneo ya Uyole, Soweto, Kabwe na Mwanjelwa, huku wanawake waliokuwa wakiuza matunda wakiwarushia vitenge wasichana waliochaniwa nguo ili wajisitiri.


Ofisa Habari Jiji la Mbeya, John Kilua alisema uongozi hauhusiki na tangazo hilo.


Hata hivyo, Ofisa wa Kampuni ya Studio H ya Huruma, Siyata Mbua alisema walitoa tangazo hilo baada ya kukamilika kwa makubaliano baina ya jiji na kampuni yake.


Mbua alisema kazi ya kuzuia nguo zisizo za heshma inahusu Serikali, lakini kampuni iliamua kujitolea kwa makubaliano na jiji kwa mwaka mmoja.


“Lengo ni kuwahamasisha wananchi wavae nguzo za heshima. Hatuwahamasishi vijana wawavamie watu, bali tunawataka kila mmoja avae nguo kulingana na maeneo anayofanyia kazi,”alisema. Mabua alisema lengo ni kuelimishana zaidi.


Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Ahmed Msangi alisema hajapata malalamiko na kuwataka vijana kuheshimu utu wao kwa kuvaa nguo za heshima.

Serikali Yakifunga Chumba cha Maiti Tumbi

$
0
0

Serikali imefunga kwa siku tatu Chumba cha kuhifadhia maiti cha Hospitali ya rufani ya Tumbi Mkoani Pwani kutokana na hali mbaya ya chumba hicho ukiwamo ubovu wa majokofu na huduma isiyoridhisha.


Akizungumza mara baada ya kufanya ziara hiyo Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinisia, Wazee na Watoto Mhe. Khamis Kigwangala amesema amechukua uamuzi huo baada ya kupokea maelezo kutoka kwa msimamizi wa chumba hicho.


Naibu waziri amesema amekuta changamoto kadhaa katika chumba hicho ikiwemo ubovu huo wa Mjaokofu hali inayosababisha maiti kulazwa sakafuni, na kupelekea kuharibika na kutoa harufu kali.


Katika hatua nyingine Naibu Waziri Kigwangala amemtaka Mkurugenzi mtendaji wa Shirika la Elimu Kibaha kuandika barua ndani ya msaa 24 ya kujieleza kwanini asifukuzwe kazi kutokana na kushindwa kutatua changamoto zinazoikabili hosptali teule ya Tumbi.


Naibu Waziri huyo amesema amebaini kuwa kuna tatizo la kiutawala hali inayosababisha utoaji wa huduma za kimatibabu kuwa wa kusuasua ikwamo kukosekana kwa maji,ubovu na uchakavu wa chumba cha upasuaji, ukosefu wa dawa na chupa za kuhifadhia damu.

Kampuni ya Magari ya Toyota Waja na Ubunifu Mpya...Watengeneza Gari la Mbao....

$
0
0
Toyota kutambulisha gari lilotengenezwa kwa mbao na teknolojia ya kiutamaduni ya nchini Japan isiyohusisha utumiaji wa misumari wala nati katika kuzishikilia mbao hizo.

Teknolojia hii imetokea wapi?

Huko nchini Japan kuna mahekalu ya kitamaduni ambayo huvunjwa na kujengwa upya kila baada ya miaka 20. Kitu cha pekee katika ujengaji wa hekalu hizo no utumiaji wa mbao usiohusisha utumiaji wa ata msumari mmoja katika ujenzi wake.

Teknolojia hiyo inatumika kwa miaka mingi katika ujengaji wa hekalu maarufu Japan – The Ise Grand Shrine
Ubomoaji na ujengaji wa mahekalu hayo umekuwa ukifanyika kwa takribani miaka 1,300 sasa, na huwa wanabomoa na kujenga tena ili kuhakikisha majengo hayo yanaendelea kuwa na nguvu na usalama. Teknolojia ya ujengaji huo inapitia kwa vizazi hadi vizazi, na sasa Toyota wanatumia teknolojia hiyo katika utengenezaji wa gari.

Wiki ya Ubunifu mjini Milani, Italia

Takribani mwezi kuanzia sasa kutakuwa na maonesho ya ubunifu katika jiji la Milani, (Design Week in Milan, Italy) na ndio Toyota wanategemewa kutambulisha gari hilo rasmi.’

Ubunifu wa gari hilo ambao wameuita Setsuna, unaonesha kitu ambacho wanaweza kukifanya baadae. Wanashiriki maonesho hayo ili pia kuweza kupata mitazamo kutoka wabunifu wengine.

Aina kadhaa za mbao zimetumika kutengeneza bodi la gari hilo, chasis, viti, uskani (steering wheel) na rim za matairi.

Je mbao hizo zimejishakaje kama misumari na ‘screw’ hazijatumika?


Ni uunganishaji wa sehemu zinazokutana kwa kutumia maumbo ya ‘concave’ na ‘convex’ (umbo la mbonyeo) ndio vinavyoshikanisha sehemu mbalimbali za gari hilo.

Lini magari la namna hiyo litaanza kupatikana?

Usitegemee kununua gari hilo siku ya karibuni… ni kitu wanachokifikira kukifanya lakini si leo. Na ata hiyo miaka ya mbele wakitumia teknolojia hii kutengeneza magari ya kuingia sokoni na kuuzika yatakuwa ni magari ya bei ghari sana.

Unaonaje Boeng nao wakitengeneza ndege ya mbao? :-) Sipandi ng’ooooo… Tuambie maoni yako :-)

Picha,Nicki Minaj na Meek Mill Walivyokanusha Taarifa za Kuachana

$
0
0
Nicki Minaj na Meek Mill wametumia mtandao wa snapchat  kukanusha kuwa wameachana.

Picha hii ni miongoni mwa picha zilizosamba mtandaoni zinamuonyesha Nicki Minaj akiwa na Meek Mill kwenye pozi flani la kimahaba.

Mwezi uliopita Meek Mill na Nicki Minaj waliripotiwa kuacha sababu ya kifungo cha ndani cha Meek Mill kinachomuweka nyumbani kwake Philadelphia.

Nay wa Mitego Amemdiss Gigy Money?Asema Hana Sura Nzuri Lakini Amejaliwa

$
0
0
Kumekuwepo na malalamiko kutoka kwa video Queen anayetamba kwa sasa Gigy Money kwenda kwa rapper wa Shika adabu yako Nay wa Mitego kuhusiana na uhusika wake kwenye video ya wimbo huo.

Gigy ameweka wazi kuwa alipewa Shilingi elfu ishirini tu kutoka kwa rapper huyo kama malipo ya kutokea kwenye video hiyo na pia amelalamika kuwa walikubaliana yeye aonekane kwenye kipande kinachohusu wanachuo lakini baadala yake ameoneshwa kwenye kipande kinachohusu mwanamke mwenye sura mbaya.

Mwanamuziki CHID BENZ Adai Yeye Ndio Baba wa Muziki wa Stamina na Sio Fid Q Kama Watu Wanavyodhania

$
0
0
Chid anadai amepata stori kutoka wa watu waliosoma na Stamina kwamba alikuwa akijiita Chid Benz na kuiga kila kitu alichokuwa akifanya na kudai hilo limedhihirika kwenye ngoma ya Like Father Like Son remix kwa kumpa kolabo.
“Stamina nimepewa stori zake, alikuwa anajiita Chid Benz kwao huko,alivyokuja mjini na kuona Chid Benz ana matatizo ndio akabadilisha na kusema Fid Q ndio kila kitu,sio mbaya lakini uhalisia utabaki kuwa mimi ndo nimemu inspire kuingia kwenye game” alisema Chid Benz.

Nikki Mbishi Amchana Dogo Young Dee Kiana Kuhusu Matumizi ya Madawa ya Kulevya

$
0
0
Katika pitapita zangu Insta leo, nimekutana na picha ya Nikki mbishi aliyopost leo akiwa na Becka Title wanakula ugali. Caption ya picha hiyo inasema hivi "Huwezi kuwa mjanja ikiwa unapotea kwa madawa ya kulevya, halafu ndugu zako na washkaji zako wa karibu wanakuchana unawaona masnitch. Oya baba Marietha @beckatitle_tz tule ugali kuku bila kusahau maji mengi. Acha wazee wa #UjanjaUjanja wapotee.
Hii inaashiria kuwa tayari Beckatitle ashammwagia Nikki Mbishi ubuyu kuhusu Young Dee(Mzee Wa UjanjaUjanja) kuhusu kupotea kwake na madawa. Its the high time dogo abadilike awachane na madawa.

Freeman Mbowe: Nawaletea Katibu Mkuu Makini Wakuvaa Viatu vya Dr Slaa

$
0
0
MWENYEKITI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe, amevunja ukimya na kusema atawasilisha jina makini la mrithi wa nafasi ya aliyekuwa Katibu Mkuu wa chama hicho, Dk. Willibrod Slaa.

Akizungumza na MTANZANIA mjini hapa jana, baada ya kumalizika kikao cha kwanza cha Kamati Kuu, Mbowe alisema sifa za kiongozi anayepaswa kushika wadhifa huo zinafahamika.

Alisema wajumbe na wanachama wa Chadema watarajie kumpokea mtu makini ambaye jina lake atalipendekeza kisha kupigiwa kura na wajumbe wa Baraza Kuu kesho.
“Sifa za Katibu Mkuu zinajulikana, nawaomba wanachama na wajumbe kutulia, jina watakutana nalo ukumbuni muda ukifika… nina imani litakuwa jina la mtu makini,” alisema.

Mbowe alisema chama hicho kinakutana kwa mara ya kwanza tangu kumalizika kwa Uchaguzi Mkuu wa Rais mwaka jana, hivyo wana mambo mengi ya kujadili, ikiwa ni pamoja na kupanga mikakati mipya ya kuwafikia wafuasi wao.

Katika hatua nyingine, chama hicho kimesema kitamtambulisha Katibu Mkuu mpya rasmi Jumapili wakati wa mkutano wa hadhara utakaofanyika viwanja wa Furahisha jijini hapa.

Akizungumza na waandishi wa habari jana, Ofisa Habari wa chama hicho, Tumaini Makene, alisema majina mawili yatawasilishwa katika Baraza Kuu litakalokaa usiku wa Jumamosi kwa ajili ya kupitisha jina moja.

Alisema majina yatakayowasilishwa hayatakuwa na uhusiano au urafiki wowote na Mwenyekiti Mbowe.

“Tayari viongozi wa kitaifa wamewasili Mwanza, Sekretarieti imekutana kwa ajili ya kuandaa ajenda ambazo zitajadiliwa na Kamati Kuu yenye wajumbe 36.

“Siku inayofuata Baraza Kuu litakaa usiku kwa ajili kumpata Katibu Mkuu, hii ni nafasi nyeti sana ndiyo maana hata wenzetu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wanafuatilia kwa ukaribu kujua nani atapewa mikoba ya Dr Slaa.

Mwanamuziki Bob Junior Akamatwa na Polisi Kwa Tuhuma za Kushirikiana na Majambazi

$
0
0

Msanii wa muziki wa bongo fleva Bob Junior amekamatwa na jeshi la Polisi nyumbani kwao magomeni mapipa Jijni Dar es salaam majira ya saa sita mchana wa leo.

Kwa mujibu wa chanzo cha  habari ambaye ni rafiki wa karibu wa Bob Junior ameiambia Mtembezi.com kuwa Polisi wamemkamata Msanii huyo kwa kile walichodai kuwa wamepata taarifa kuwa Bob Junior anashirikiana na kikundi cha majambazi.

Rafiki huyo wa karibu na Bob Junior, ameiujuza mtembezi.com kuwa Msanii huyo amekuwa akipigiwa simu tangu juzi kutoka kituo cha polisi cha magomeni usalama kwamba kuna lalamiko la mtu anaye dai kutekwa na kikundi cha majambazi ambacho msanii huyo anashirikiana nacho.
Viewing all 104809 articles
Browse latest View live


Latest Images