Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104799 articles
Browse latest View live

Video:Bob Junior Kakubali Alikamatwa na Kulala Polisi.. Chanzo Je? Stori Iko Hapa

$
0
0
Ni headlines zilizochukua nafasi kubwa katika mitandao mbalimbali  hivi karibuni kuhusiana na msanii Bob Junior kukamatwa na jeshi la polisi, sasa basi msanii huyo yuko uraiani na hapa amefunguka mengi ambayo tulikuwa hatuyafahamu kuhusu kukamatwa kwake.

Angalia Video Hapa:
Chanzo:Millard Ayo

HIZI ni Dalili za Mwanamke Anayekupenda Kwa Dhati Toka Moyoni, ila Hawezi Kukuambia

$
0
0
Kumekuwa na imani potofu kwa wanawake kwamba hawawezi kumwambia ukweli mwanaume anampenda kwanza mpaka mwanaume aanze lakini ukweli usiopingika ni kwamba wao pia hupendi na mara nyingi wao wakianza kupenda hupenda kweli kufikia stage hata ya kuhisi kuumwa. Hizi ni dalili za mwanamke anaekupenda ila anagoma kukwambia tu.

1. KUKUTEGA ILIKUJUA THAMANI YAKE KWAKO
Hufanya mambo ambayo yatamfanya kuona kama unampenda na kumthamini au la mfano wa mambo hayo ni kama kujifanya anaumwa na kauangalia respond yako kwake ni kiasi gani unamjali na kiasi gani utahangaika kwa ajili yake.

2.HUWA ANAPENDA KUKUGUSA SEHEMU YAKO YA MWILI.
Haoni aibu kugusa sehemu ya mwili wako. Msichana anayependa haoni aibu kukushika mkono ama kukutomasa au hata kukumbatia.Kwa kufanya hivyo hujua kuwa kwa asilimia kubwa hisia za kushikana kwenu kutamrahishishia kazi ya kuwa na wewe.

3. KUPENDA KUCHEKA TENA MUDA MWINGINE KWA NGUVU
Kucheka kwa nguvu hata kwa kitu kisicho chekesha endapo wewe umezungumza. Mara nyingi ataonesha uso wa furaha hata kama si furaha ya kweli.

4. WIVU
Hujisikia wivu anapokuona na wasichana wengine. Ukiwa unachart nao na ukiwaita majina ya kimahaba. Hapendi na hupenda yale afanyiwe yeye tu hata kama sio mpenzi wako.

5.HUKUMBUKA MATUKIO MUHIMU YOTE KUHUSU WEWE
Anakumbuka siku zako muhimu. Hukumbuka kama vile siku yako ya kuzaliwa hatoweza kuisahau kufanya ipite bila kukutakia heri ya siku ya kuzaliwa kama sivyo ukifauli mtihani au chochote katika maisha yako atakuwa mbele kukupongeza.

6. HUPENDA KUANGALIANANA WEWE MUDA MWINGI
Eye contact hupendelea sana kukuangalia machon muda wote ambao mtakuwa mkizungumza pamoja akidhani kuwa utamuelewa ni kiasi gani anakupenda kupitia vile anavyokuangalia. Ila wengine huona aibu kuwatazama wavulana wanaowapenda hivyo huweka jicho la wizi na kukuvizia.

8. HUPENDA KUKAANA WEWE MUDA MWINGI NA KUKUJUAZAIDI
Hupenda kukaa muda mwingi na wewe. Hawezi kupoteza hata sekunde ukimuhitaji kwa mazungumzo. Anajisikia furaha kukaa na wewe muda mrefu bila kuchoka. Anaweza akaacha kila kitu anachokifanya ili ajumuike na wewe na akikaa na wewe hupendelea sana mwanzoni kukujua wewe zaidi na hukujengea mazingira ya wewe uwemuwazi ili umwambie mengi kuhusu wewe na pia akiwa na wewe atakuwa muwazi zaidi hadi mavazi aliyovaa hupenda sana kujua yako na kukuambia yake na hupenda kujua ni mavazi gani yeye akivaa anakuvutia zaidi na atajitahidi kuwa anavaa ya style hiyo kukufurahisha.

9.YUPO TAYARI KUSACRIFICE
Kama msichana anakupenda yupo tayari kusacrifice. Ni kitu ambacho hakuna mtu ambaye anaweza akafanya kwa mtu mwingine. Utamuona vipi huyo msichana alivyo kwako na kwa wengine. Yaani yupo tayari akose lakini wewe upate na kwa mwingine anaweza akamwambia hana alichoombwa lakini akakupa wewe kama pesa na vitu vingine.

10. HUPENDA KUTATUA MIKWARUZANO YENU KWA AMANI
Mikwaruzano ikitokea katika urafiki wenu hayupo tayari kukupoteza kabla hajakwambia nakupenda.Kwa kuwa anakupenda endapo ikitokea mikwaruzano basi atafanya juu chini kuyaweka mambo sawa ili asikukose.

11. HUPENDA KUKUNUNULIAZAWADI ZA MITEGO

Mwanamke anaekupenda hupenda kujua mengi sana kuhusu wewe na hapo inamsaiia kukununulia zawadi za mitego kama boxer , na mara nyingi hupenda rangi nyeupe, au kukununulia perfume , sabuni ya kuoge ya manukato,soksi, vest, bukta, saa,raba, t-shirt. Na kama mkitoka wote mkaenda shopping ataakutega kwa kukuonyesha vitu na wewe ukionekana umependa kitu hatonunua siku hiyo ila atanunua siku inayofuata na kukuletea kama suprise.

12. KUPENDA MLE WOTE

Mwanamke anaekupenda ili akujue zaidi hupendelea msosi mle sehemu mmoja na kama ikitokea mwanaume hawezi kuhama sehemu anayokula mwanamke yupo radhi kubadili na kumfuata mwanaume hatakama sehemu hiyo yeye haipendi na kama unakula kwako basi atakutega na kuja kupika kwako ili mle na atakuwa anapenda kununua vitu vya kupika ili tu akutekena uone upendo wake.

NB: Kuwa makini, sio kila mwanamke atakaye onesha dalili hizi anakupenda kwa dhati, wengine hutaka kukuweka mtu kati ili akugagadue mpunga wako tuuu a.k.a gold digger.

Napingana na Mhe. EDWARD Lowassa, Anaposema Rais Magufuli Hana Maono...

$
0
0
Katika moja ya thread nimesoma ndani ya jamii forums, inasema Mh Dk Magufuli ni rais asie na maono. Usemi huu umenifanya kuunganisha dots nakatuni za mwana siasa fulani ndan ya ccm ambaye ni kijana na ambaye ilisemekana kwamba alikuwa akiandaliwa as plan B ikiwa Mh Lowasa angekosa kuchaguliwa ndani ya ccm.

Ukweli ni kwamba kunauwezekano mkubwa mguno na kelele zimeanza toka kwa mh Lowasa ni dalili kuna mahali ameshaguswa na anaanza kusikia maumivu makali, ambayo kelele zake nikusema Mh Rais hana maono.

Swali gumu ambalo mimi na wewe mtanzania mwenzangu yatupasa kujiuliza kwa makini. Nikwanini huyu mh ameamua kuja na msemo huu wa rais wetu hana maono? Nilazima uwe na jicho la tatu,lanne mpaka saba kujuwa nini Mh Lowasa ali manisha!

Rais wa Tz nimiongoni wa viongoz wa africa amekataa ufalme na utukufu wanapata marais wa africa na badala yake amewageuza masikini na watu wenye kipato cha chini kuwa ndio wa falme na wenye thamani kwa wenye navyo. Kwa kiongoz wa africa lazima uambiwe huna maono!
Pili Mh Rais ktk hali isiyokuwa yakawaida kwa kiongoz wa africa, amewaambia matajiri walipe kodi na hataki mawe ya almas na kadi za kupewa michango toka kwa matajiri hili pia africa lazima uwe huna maono.
Tatu mh Rais amekataa sherehe na tafrija za kifahari kama rais nakupeleka mapesa yote kwa madawati na wagonjwa kwenye ma hosp. Kwa afrika huyu sio tu hana maono ila ni chizi hajuwi kuila nchi.

Mh Magufuli amekataa kujinufaisha yeye na familia yake kwa mara nyingine tena huyu hawez kuwa na maono, wakat wenzake wanawapa tenda na miradi mikubwa familia zao yeye anatoa tenda kwa mashirika yenye viwango na ubora wa kimataifa no more richmond. Lazima lowasa mguno wake uwe mkubwa eti Rais hana maono!
Kuzuwia safari za nje na kukata matumiz ya ovyo ambayo hata Rwanda anaiga ni lazima lowasa aseme mkubwa hana maono.

Tusi hili ambalo limejificha ktk lugha nyepesi ndio mwanzo na mwisho wa matusi kwa Rais wetu maana baada yajipu kutumbuliwa atakuwa raia mwema mwenye mapenz mema kwa mifugo yake Monduli.

Napenda kumwambia mh Lowasa wa tanzania sio wajinga kiasi hiko anafikiri, wala watu hawajapofuka kwa vijisent vyake taifa hili limepata mwana mapinduzi wa kweli ndani ya chama cha mapinduzi. Hatuna rais asie na maono kama ukawa! Ila tuna genius president ambaye dunia nzima wanamtaja. Ukienda Europ wanalitaja jina Maguful, Africa chanel zote kubwa anatajwa, Asia ndio usiseme, Amerika yote na Australia New president of Tz ndio habari ya mjini. Kwanini? Kwasababu anamaono ambayo hata wazungu wanaogopa. Mungu ibariki Tz pamoja na rais wa jamuhur ya muungano wa Tz Dk Magufuli. Amen

By TumainiE

Mama Diamond Atoa Siri ya Zari

$
0
0
Mama mzazi wa staa wa Afro-Pop, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, Sanura Kassim ‘Sandra’ ametoboa siri ya mkaza mwanaye, Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’ kushindwa kuishi Bongo na badala yake kukimbilia nchini Afrika Kusini ‘Sauz’.

Sandra au Mama D aliyasema hayo katika mahojiano maalum na Ijumaa Wikienda juu ya uhusiano wake na Zari kufuatia tetesi kuwa hawaivi ndipo akaweka mambo sawa.

Mama D alisema kuwa yeye na Zari wapo vizuri lakini kinachomfanya mkwewe huyo kushindwa kuishi naye Bongo ni kutokana na biashara zake kudoda nchini Afrika Kusini.

“Unajua anapokuwa huku (Bongo), biashara zake huwa zinayumba sana, wakati mwingine akipiga simu akiulizia biashara zinakwendaje anaambiwa hali ni mbaya au hazijaingiza chochote hapo ndipo huwa anachanganyikiwa.

“Kwa mfano hivi karibuni alipiga simu akaambiwa hakuna fedha kabisa na biashara haziendi. Kilichofuata ni kujiandaa na kumchukua Tiffah (Latifah Nasibu) kisha akaondoka zake.

“Hicho ndicho kinachomkimbiza Zari kuishi Bongo na si kweli kwamba hapapendi au kuna tatizo lolote,” alisema Mama D.

Chanzo:GPL

Mwigizaji Lulu Azuiwa Kuingia Ikulu Kuonana na Waziri Mkuu...Kisa Kizima Kipo Hapa...

$
0
0
Imefichuka! Baada ya kuitwa na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa kwa ajili ya kupongezwa kutokana na tuzo aliyopata nchini Nigeria, staa wa filamu, Elizabeth Michael ‘Lulu’ alijikuta akihaha baada ya kuzuiwa kuingia Ikulu kutokana na kutokuwa na kitambulisho cha chama cha waigizaji.

Chanzo makini kililiambia gazeti hili kwamba Lulu alijikuta katika wakati mgumu kwani utaratibu wa wasanii kuingia Ikulu umebadilika, tofauti na serikali iliyopita kwani kwa sasa, wasanii wa filamu ni lazima wapitie kwenye Shirikisho la Filamu ‘TAFF’ kisha wizarani ndipo waruhusiwe kuonana na mhusika aliyemuita au anayetaka kumuona.

“Shughuli ilikuwa ifanyike Alhamis, Lulu alipofika wizarani akakutana na utaratibu huo mpya, si unajua yeye siyo mwanachama wa chama chochote cha filamu, ndiyo ikabidi aelezwe jambo hilo,” kilisema chanzo hicho.

JFKutokana na utaratibu huo, Lulu akalazimika kurudi katika ofisi za mwenyekiti wa waigizaji mkoa wa Kinondoni (TDFAA),  Ally Baucha ambapo alichukua fomu ya uanachama na kuijaza na kuirejesha siku hiyohiyo ya Alhamis iliyopita ili aweze kwenda kuonana na Waziri Mkuu siku iliyofuata (Ijumaa). “Yaani Lulu alihangaika kweli siku hiyo kwani hata siku ya kupokelewa pale Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere hakuna msanii wa TAFF aliyekwenda  kumpokea hata mmoja wala viongozi wake, hivyo hata alipopata mwaliko wa Ikulu ikashindikana kuingia bila ya utambulisho wa uanachama wa shirikisho na chama cha waigizaji mkoa anaoishi wa Kinondoni,” kilisema chanzo hicho.

Baada ya kuzinyaka habari hizo paparazi wetu alimtafuta Mwenyekiti wa TDFAA, Ally Baucha ambapo alikiri kwamba ni kweli Lulu alikwenda kuchukua fomu harakaharaka na kuijaza na kuwa mwanachama ikiwa ni baada ya kupata mwaliko wa kwenda kupewa pongezi na Waziri Mkuu.
Naye Rais wa Shirikisho la Filamu Tanzania ‘TAFF’, Simon Mwakifwamba alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kwamba ni kweli kwa sasa hakuna msanii anayeruhusiwa kuingia Ikulu bila kupitia kwenye shirikisho na wizarani hata kama ameitwa na nani.

“Utaratibu umebadilika sasa, msanii hata kama ameitwa na kiongozi gani ni lazima afuate utaratibu huo ndivyo tulivyokubaliana, hivyo Lulu alishindwa kwenda moja kwa moja mpaka alipokwenda kujiunga kwanza na chama cha waigizaji na kutambulika na shirikisho ndipo nikawapeleka Ijumaa iliyopita na msanii mwenzake aliyeshinda tuzo pia, Single Mtambalike ‘Richie’ na kwenda kupongezwa kwa kutwaa tuzo hizo za kimataifa.

“Wasanii wanatakiwa kuufahamu utaratibu huo kwani hata wakipita moja kwa moja lazima watarudishwa tu kwenye shirikisho, wakati wao ukifika kama Lulu naamini watajiunga tu hatumlazimishi mtu,”alisema Mwakifwamba.

Hivi karibuni, wasanii hao wawili walishinda Tuzo za African Movies Viewers Choice (AMVC) zilizofanyika nchini Nigeria ambapo  Lulu alishinda katika Kipengele cha Filamu Bora ya Afrika Mashariki (Mapenzi ya Mungu) huku Richie akichukua kwenye Kipengele cha Filamu Bora ya Kiswahili Afrika Mashariki (Kitendawili), tukio lililofanyika Nigeria wiki iliyopita.

Chanzo:Global Publishers

Pendeza na Kessy Products..Pata Dawa za Asili Zisizo na Madhara Wala Kemikali Yoyote

$
0
0

PENDEZA NA KESSY PRODUCT.
PATA DAWA ZA ASILI ZISIZO NA MADHARA WALA KEMIKALI YOYOTE,
NA MATOKEO KUANZIA WEEK (2) ADI (4) NAKUENDELEA

1) KUTOA MVI SUGU 80,000/
2) KUREFUSH NYWELE NA UKATIKAJI 80,000/
3) TENGENEZA SHEPU YAKO FIGA UMBO (8) KWA DAW...
@ KUPAK 70,000/
@ KUNYWA NA VIDONGE 130,000/
4) TENGENEZA MGUU KAMA CHUP YA BIA 60,000/
5) PUNGUZA KITAMBI NA MANYAMA UZEMBE
@) KUNYWAA 90,000/
@) KUPAKA 70,000/
6) PUNGUZA MWILI MZIMA PAMOJA NA KILO
@) MAJAN 130,000/
@) VIDONGE 150,000/
7) PUNGUZA MAZIWA NA YASIMAME 60,000/
8) ENGEZA MAZIWA NA SAIZ UNAYOPEND 60,000/
9) ONGEZA MWILI MZIMA NA KUKUPA HAMU YAKULA (WEMBAMB) 80,000/
10) TOA MICHIRIZI SUGU PIA NA ILE YAKUJIFUMGUA, 70,000/
11) TOA MAKOVU, CHUNUSI, WEUSI KATIKATI YA MAPAJA 50,000/
12) TOA NGIRI YA AINA ZOTE 70,000/
13) KUWA MWEUP MWILI MZIMA KUPAKA 80,000/PIA VIDONGE VIDONGE.
14) TOA VINYWELEO NA NDEVU 80,000/
15/ ONGEZA NGUVU ZA KIUME
@) JEL KUPAKA 60,000/
@) VIDONGE 80,000/
16) ONGEZA MAUMBIL KWA
@) HANDSM UP MASHIN 170,000/
@) JELI YAKUPAKA 100,000/
17) RUDISHA HAM YA TENDO 60,000/
18) RUDISHA USICHAN(BIKRA) 70,000/

TUPO DAR, K/KOO SINZA, MAPAMBAN, KWA MIKOAN T UTATUMA KWA MABAS, KWA ZENJ PIA KWA BOT ZA AZAM
CHAKUFANYA PIGA CM
0719955558.
0756259180.
0785371237.
AMA TU FOLLOW
@dr_kessy_product
@dr_kessy_product

Delivery kwa DAR ipo utaletewa popote ulipo

Njia Bora Kuliko zote ya Kuzuia Mimba Kwa Uzazi wa Mpangoa Kwa Wanawake Hii Hapa....

$
0
0
Elimu ya uzazi wa mpango bado haijawafikia vijana wengi sana hasa tanzania, wengi wao hudhani labda.

matumizi ya dawa na njia za uzazi wa mpango ni kwa ajili ya malaya, watu waliokwisha zaa na kadhalika. lakini hii sio kweli kwani njia hizi ni nzuri kwa rika zote yaani vijana na watu wazima ambao wanashiriki ngono ila kwa sasa hawako tayari kupata mtoto.

kutotumika kwa njia hizi kumesababishwa kuzaliwa kwa watoto wengi ambao hawakupangwa, kujiua kwa wasichana kwa kukwepa aibu na utoaji wa mimba wa mara kwa mara.

utafiti nilioufanya mwenyewe nimegundua kwamba msichana akiingia kwenye mahusiano kwa miaka mitatu bila kutumia njia yeyote ya uzazi wa mpango anaweza kutoa mimba nne mpaka tano lakini pia asilimia kubwa ya wanachuo wa tanzania ambao huingia kwenye mahusiano vyuoni hawawezi kumaliza chuo bila kutoa mimba hata moja.

kuna njia nyingi sana za uzazi wa mpango ikiwemo vitanzi, vijiti, kondomu,kutumia kalenda, sindano,vidonge, upasuaji wa kufunga mirija na kadhalika. kondomu ni njia bora sana kwani huzuia ukimwi na mimba pia lakini ukweli ni kwmba kama kondomu zingekua zinatumika vizuri basi hao watoto tusingewaona mtaani hivyo kama wewe hauko tayari kuzaa sasa hivi kwa sababu yeyote ile nakushauri utumie njia ya kijiti.

Njia hii ikoje?
kijiti cha plastiki chenye homoni za uzazi huwekwa kwenye mkono wa mwanamke, homoni ndani ya kijiti hicho huzuia mimba kwa kwa kuzuia yai kutoka kwenye kiwanda yaani ovari kwenda kwenye kizazi . kijiti hiki huwekwa bure kwenye hospitali zote za serikali tanzania.

kwanini njia hii ni bora kuliko zote?
1. Hurudisha uwezo wa kuzaa haraka: kama unatumia kijiti hata kama kiliwekwa wiki iliyopita, ukibadilisha mawazo ukataka mtoto kinatolewa na mwezi huohuo unapata mtoto, tofauti na njia ya sindano ambayo ukichomwa leo kuna uwezekano wa kukaa mpaka miaka miwili bila kupata mtoto.

2. Ni rahisi kutumia: kijiti hiki kikishawekwa hospitali huhitaji kukumbuka chochote tofauti na vidonge ambavyo wakati mwingine mtu huweza kusahau asimeze akajikuta amebeba mimba.

3. Inafanya kazi kwa muda mrefu sana; kama wewe ni binti mdogo au wewe ni mama ambaye una mtoto tayari na hauhitaji mtoto kwa sasa njia hii ni nzuri kuliko zote kwani huweza kuzuia mimba kwa miaka mitano mfululizo kwa asilimia mia.

4. Haiingilii utoaji wa maziwa ya mama; vidonge vya uzazi wa mpango vyenye homoni zote mbili yaani oestrogen na progesterone kitaalamu kama microgynon huweza kupunguza wingi wa maziwa kwani wingi wake kwenye mfumo wa binadamu husababisha kupungua kwa homoni ya maziwa kitaalamu kama prolactin hormone.

5. Haiongezi uzito; inaaminika vidonge vya uzazi wa mpango huongeza uzito kwa kuzuia kiasi kikubwa cha maji kisitoke ndani ya mwili kwa njia ya mkojo na pia kuongeza hamu ya kula, lakini utafiti kwa wanaotumia vijiti haujaonyesha madhara haya.

6. Muda zaidi wa kushiriki tendo la ndoa: matumizi ya kijiti huzuia kutoka kwa damu ya kila mwisho wa mwezi ambayo kwa wengine huambatana na maumivu makali na kukosa raha ya kushiriki tendo la ndoa hivyo ukitumia kijiti utapata faida hii.damu inaweza ikatoka hata mara mbili kwa mwaka tu.

7. Sio rahisi kwa watu wengine kujua: wasichana wengi hasa vijana hawapendi maisha yao ya ngono yafahamike, na hasa njia hizi za uzazi wa mpango watu wakijua unatumia wanakuona muhuni, kitu ambacho sio kweli, hivyo matumizi ya kijiti ni siri sana na sio rahisi kwa watu wengine kujua tofauti na vidonge ambavyo sio rahisi kuvificha.

Mwisho; utafiti unaonyesha utoaji wa mimba umewanyima wanawake wengi watoto, msanii maarufu wema sepetu ambaye kwa sasa anatafuta mtoto kwa shida sana aliwahi kukiri kwamba aliwahi kutoa mimba zamani kidogo na huenda anajutia maamuzi yake.hivyo kama wewe ni msichana mdogo na hutaki kuzaa kwa sasa au wewe ni mama hutaki mtoto mwingine kwa sasa tumia njia hii ya uzazi wa mpango itakusaidia sana

Idris Afunguka: Tumeamua Kuufanya Uhusiano Wetu na Wema ‘Private’ Kwa Sasa

$
0
0
Hutoona tena Idris Sultan na Wema Sepetu wakionesha upendo hadharani kama zamani kwakuwa wameamua kuuweka ‘private’ kwa sasa.

Mshindi huyo wa BBA 2014, ameiambia Bongo5 kuwa angependa zaidi kwa sasa kujikita kwenye kazi zake kuliko kuufanya uhusiano wao uwe mjadala mkubwa.

“Sipendi uhusiano wangu uwe kitu kikubwa kuliko kazi yangu kwa sasa,” alisema.

Hata hivyo kama wasemavyo wahenga kuwa penzi ni kikohozi huwezi kukificha, Wema ameonekana kutilia mkazo jinsi ambavyo anampenda staa huyo kwa comments za hapa na pale kwenye post za Instagram.


Unene Wamkosesha Raha Wema Sepetu, Aacha Kupost Picha zake Instagram Kwa Miezi Mitatu

$
0
0
Wema Sepetu ameacha kupiga picha na kuzitupia Instagram kutokana na kunenepa sana, na zoezi hilo litakwenda hadi hadi mwezi June.

Kupitia Instagram , Wema ameandika.

About Yesterday… Tulivyoalikwa na Makamu wa Rais… Mama Kipenzi… Mama Darling…. Mama Samia Suluhu Hassan… Ni hii tu naipost sababu nampenda sana Huyu mwanamke… Ila sasa hivi sijui nijifungie tu ndani maana zoezi la mpaka June ni Kubwa…. Haiya na msisahau kunipa na ushauri wa dawa gani za kutumia nipungue sio kwa ubonge nilionao sasa… But nat my fault ni fault ya vile vitwins vyangu vile Weightloss imekuwa ni ngumu sana kwangu… Wat do I dooooo….?? Mashavu, Mamikono, Minyama… Mtumbo….!!! Nilisema mpaka June atleast nijitahidi kupungua ila sijui ni nini hiki… Hel

A.Y Afunguka Sababu ya Kumfanya Meneja wa Diamond Awe Meneja Wake Pia....Sababu Ipi Hiyo?

$
0
0
Mkongwe AY amefunguka sababu kubwa ya yeye kumfanya Salaam,meneja wa diamond kuwa meneja wake pia ni kutokana na kuzidiwa na majukumu.

A.Y amefunguka kuwa hajawai kuwa na meneja kwenye maisha yake ya muziki lakini amemchagua Salaam kwa kuwa anaujua utendaji wake kwani wamekuwa toka wadogo na anahisi anaweza kuvaa viatu hivyo.

“mpaka mimi nimefika hapa leo sikuwahi kuwa na meneja kwa hiyo naona kama kazi zinakuwa nyingi lazima nipate msaidizi mwingine,nikaona Salaam ndiye mtu anayeweza ku fit kwenye hivyo viatu” alifunguka A.Y na kubainisha kuwa amewahi kufanya kazi na meneja huyo lakini haikuwa rasmi.

Rais Magufuli Awakuna Waingereza

$
0
0
Balozi wa Uingereza nchini, Diana Melrose amewahakikishia wafanyabiashara wa Uingereza kwamba Tanzania ina mazingira mazuri ya uwekezaji na Serikali ipo tayari kushirikiana nao.

Melrose aliyasema hayo juzi wakati akizungumza na ujumbe wa wafanyabiashara wakiongozwa na Chama cha Wafanyabiashara wa Uingereza (London Chamber of Commerce), Kitengo cha Viwanda, Biashara na Uwekezaji.

Alisema amefanya mazungumzo na Rais John Magufuli hivi karibuni na kumuonyesha dhamira ya kuleta mabadiliko ili wananchi wapate huduma za jamii.

Makamu wa Rais wa London Chamber of Commerce, Subhash Thakrar alisema ili kukuza uchumi lazima kuwapo na kampuni nyingi zinazochipukia.

Mshauri wa kimataifa wa biashara kutoka Uingereza, David Billingsby alisema ziara hiyo itatoa fursa za mafanikio kwa biashara zitakazoshiriki.

Alitoa mfano kwa mshiriki ambaye mwaka jana alikuwa mtaji wa kuanzisha shule ya kimataifa.

Lowassa Afunguka Mazito Kuhusu Wanachama Wanaofukuzwa CCM Wakituhumiwa Kukisaliti Chama Kwa Kumuunga Mkono Yeye

$
0
0
Aliyekuwa mgombea urais kwa tiketi ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Edward Lowassa amewapa neno wanachama wa CCM wanaotaka kufukuzwa ndani ya chama hicho wakituhumiwa kumuunga mkono.

Akiongea hivi karibuni katika kikao cha Baraza Kuu la chama hicho kilichofanyika jijini Mwanza, Lowassa aliwasihi watu hao kujiondoa CCM na kujiunga na Chadema kwani kuna maisha mazuri zaidi ndani ya chama hicho kikuu cha upinzania.

“Lakini hivi karibuni kuna utaratibu wa kuwafukuza kwenye chama watu ambao waliniunga mkono. Wanafukuzwa wanaambiwa ‘ondokeni mfuateni Lowassa’.

"Nasikia kuna mipango mikubwa zaidi baada ya mwezi wa sita atakapokabidhiwa Rais Magufuli… kuna mipango mikubwa zaidi ya kuwaondoa kwenye chama,” alisema Lowassa.

“Sasa mimi nawaambia kwa niaba yetu. There is life outside CCM, nawaambia tena kwa ajili yenu, waje Chadema kuna maisha mazuri tu hapa. Wasibaki huko wananyanyaswa, wanabezwa wanafanya nini… waje tushirikiane tufanye kazi,” aliongeza.

Lowassa ambaye ni Waziri Mkuu Mstaafu alieleza kuwa CCM hivi sasa wanaumia kwa sababu kuondoka kwake na kujiunga na Chadema kuliiongezea nguvu kambi hiyo ya upinzani na kupunguza ruzuku kwa kiasi kikubwa kwa chama hicho tawala.

Huyu Hapa Ndio Msanii Mpya wa Diamond Kwenye Lebo ya WCB.. Anaitwa Raymond Sikiliza Wimbo Wake Uliotambulishwa leo

$
0
0
Kipaji cha Raymond kilianza kuonekana mwaka 2011 baada ya kushiriki kwenye mashindano ya FreeStyle  mkoa wa Mbeya na kuwa mshindi wa kwanza,alipokuja Dar akaibuka pia mshindi ndipo TipTop Connection ilipomchukua na kuwa chini yake,Raymond ameshaonekana kwenye majukwaa mengi hasa kwenye show za Madee,Kutokana na ukaribu wa Lebo ya TipTop Connection na WCB,Menejimenti zimekaa chini na kukubaliana kumtoa kupitia lebo ya WCB.

Sasa leo ndio katambulishwa rasmi ktka vituo mbalimbali vya redio na hapa anakukaribisha kuisikiliza hii single yake mpya iitwayo Kwetu

JIPU JIPYA..Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali PAC Yakataa Ripoti ya Matumizi ya Fedha za NEC...

$
0
0
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali PAC leo imekataa Ripoti ya Mapato na Matumizi ya Fedha ya Tume ya Uchaguzi nchini, NEC

Kamati ya kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali PAC leo imekataa Ripoti ya Mapato na Matumizi ya Fedha ya Tume ya Uchaguzi Nchini NEC baada ya kubaini kuwepo kwa mapungufu na ubadhilifu mkubwa wa Fedha na kuisababishia Serikali hasara.
Hatua hiyo imekuja baada ya kubaini kuwepo kwa mapungufu na ubadhilifu mkubwa wa Fedha na kuisababishia Serikali hasara ya fedha zilizotolewa kwa Tume hiyo katika Bajeti ya mwaka 2015/2016.
Taarifa hiyo imetolewa leo Jijini Dar es salaam na wajumbe wa kamati hiyo ambao walikutana na Tume ya Taifa ya Uchaguzi nchini NEC kwa lengo lakujadili na kupokea taarifa ya fedha ya Mapato na Matumizi ya NEC kwa mwaka wa Fedha 2015/2016.
Baada ya wajumbe hao kutoridhishwa na ripoti hiyo ya tume na kugundua bado kuna upotevu mkubwa na ubadhirifu wa fedha za serikali kwenye tume hiyo hadi kufikia kuwapo kwa deni la fedha takribani shilingi bilioni mbili milioni mia nane na ishirini na tatu
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Uchaguzi NEC Ramadhani Kailima amekiri mapungufu hayo ndani ya tume.
Akitoa maazimio ya kikao hicho kati ya Tume ya Uchaguzi na Kamati ya Hesabu za Serikali Mwenyekiti Msaidizi wa Kamati hiyo Mheshimiwa Aeshi Hilaly amekataa kupokea Ripoti hiyo na kuwataka watendaji wa NEC kuifanyia masahihisho Ripoti hiyo na kuipeleka kwa CAG.

Mkuu Mpya Wa Mkoa wa Kagera Meja Jenerali mstaafu Salum Mustafa Kijuu Atoa Onyo Kali Kwa Majambazi na Wahalifu.

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Kagera Meja Jenerali mstaafu Salum Mustafa Kijuu amewataka watu wote wanaopindisha sheria, majambazi na wahalifu wote kutafuta kazi nyingine halali za kufanya.

Meja Kijuu aliyasema hayo baada ya kula kiapo cha utiifu na uadilifu kuwatumikia wananchi wa mkoa wa Kagera mkoa ambao upo pembezoni mwa nchi unaokabiliwa na matukio ya mara kwa mara ya uhalifu.

''Namshukuru Mheshimiwa Rais kwa imani kubwa aliyonayo kwangu na nitafanya kazi kwa kuzingatia yale ambayo ameyasema na kuhakikisha maendeleo yanapatikana''-Amesema Meja Kijuu

''Sitakubali watu wazurure hovyo na kuacha kufanya kazi za uzalishaji na nitahakikisha napambana na wahalifu wote kwa uwezo wote nilionao"-Amesisitiza Meja Kijuu.

Aidha Rais Magufuli aliwaapisha wanajeshi wastaafu Meja Jenerali Mstaafu, Ezekiel Elias Kyunga, aliyekuwa Chuo cha Kamanda na Unadhimu (JWTZ) ambaye sasa ni Mkuu wa Mkoa wa Geita, Jenerali Mstaafu Salum Mustafa Kijuu, aliyekuwa Mkuu wa Kamandi ya Nchi Kavu ni Mkuu wa Mkoa wa Kagera.

Wengine ni Meja Jenerali Mstaafu Raphael Muhuga, aliyekuwa Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa(JKT) sasa ni Mkuu wa Mkoa wa Katavi na Brigedia Jenerali Mstaafu Emmanuel Maganga, aliyekuwa Makao Makuu ya Jeshi sasa ni Mkuu wa Mkoa wa Kigoma lengo la Rais kuweka wanajeshi katika mikoa ya pembezoni ni kuleta usalama na kuimarisha amani katika mikoa hiyo.

Tumeukamata Mtandao wa Wizi wa Magari Dar es Salaa...Kamanda Sirro Afunguka

$
0
0
Jeshi la Polisi kanda maalum ya Dar es salaam imetoa taarifa ya kufanikiwa kukamata mtandao wa wezi wa magari yanayoibiwa kutoka Dar es salaam na kwenda mikoani.

Akiongea na vyombo vya Habari jijini Dar es salaam leo Kamishna wa polisi kanda maalum ya Dar es salaam Simon Sirro amesema jeshi hilo limeendesha Operation mbili ikiwa ni pamoja na kuukamata mtandao huo wa wezi wa Magari na kuwakamata Wanaume na Wanawake wanaofanya biashara ya ukahaba Jijini Dr Es Salaam.

Kamishna Siro amesema jumla ya magari 24 ya wizi na watuhumiwa 50 wa makosa ya wizi wa magari wamekamatwa ambapo magari hayo yalikuwa yakipelekwa kuuzwa katika mikoa ya kanda ya ziwa.

Aidha Kamishna Sirro ameitaja operesheni ya kuwakamata wanawake na wanaume wanaouza miili yao pamoja na kununua kuwa imewanasa jumla ya watu 287 katika siku kumi zilizopita.

Paul Makonda Aanza Kazi Kama Mkuu wa Mkoa...Atoa Agizo Kwa Wakuu wa Idara za Halmashauri Kumfikishia Ripoti Jinsi Walivyojipanga Ndani ya Masaa 24

$
0
0
MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda amewagiza wakuu wa idara wa Halmashauri za Jiji la Dar es Salaam kutoa ripoti za matatizo ya wananchi na jinsi walivyojipanga ndani ya masaa 24.
Makonda ameyasema hayo wakati akizungumza na watendaji wa halmashauri hizo ikiwa ni siku ya kwanza kuingia katika ofisi ya Mkuu wa Mkoa baada ya kuapishwa jana, Makonda amesema wananchi wa Dar es Salaam wanakabiliwa na changamoto za ulinzi,maji,biashara pamoja na elimu  hivyo lazima matatizo hayo yapate ufumbuzi katika kusaidia wananchi kuondokana na changamoto hizo.

Makonda amesema kuwa kwa muda alioutoa wa masaa 24 ni mkubwa hivyo lazima wafanye kazi hiyo jinsi walivyojipanga katika kutatua changamoto hizo.
Amesema wakati umefika katika kuwatumikia wananchi kuwaondolea  kero zao ambazo zinafanya kuwa na malalamiko yasioisha.

Makonda amesema amekutana na Kamanda wa Polis wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Kamishina wa Jeshi la Polisi, Simon Sirro kuzungumzanaye juu ya suala la ulinzi na usalama  kwa wananchi.

Aidha amesema kuwa kukutana huko sio mara ya kwanza ataendelea ikiwa ni lengo la kuwatumikia wananchi pamoja na kutatua kero zao.

Rais Magufuli: IPTL ni Mkataba wa Ovyo, Serikali Haitaendelea Nao.....

$
0
0
Rais Magufuli amesema kuwa IPTL ni mkataba wa hovyo na Serikali yake hautaendelea nao.

Rais John Magufuli ameyasema hayo wakati akizindua ujenzi wa kituo cha kufua umeme wa Megawati 240 cha Kinyerezi II Dar leo.

Wasanii wa Bongo Movie Wampongeza Paul Makonda kwa Kuteuliwa kuwa RC Dar

$
0
0
Ma-Star wa Bongo Movia wamemuangushia party ya nguvu Mkuu wa Mkoa mpya wa Dsm ndugu Paul Makonda baada ya kuteuliwa na kuapishwa kuwa mkuu wa mkoa wa Dsm.

Party hiyo ilijumuisha mastaa kibao wa mjini wakiongozwa na STEVE NYERERE, RICHI RICHIE na JB






HATIMAYE Tarehe ya Kufanyika Uchaguzi wa Meya Dar es Salaam Yatajwa.....

$
0
0
Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam imetangaza Machi 22 kuwa ndiyo kitafanyika kikao cha Baraza la Madiwani wa Dar es Salaam kujadili ajenda moja ya uchaguzi wa meya.

Uchaguzi huo umeahirishwa mara tatu kwa sababu mbalimbali, ikiwamo zuio batili la mahakama lililowekwa na makada wa CCM, katika Mahakama Hakimu Mkazi wa Kisutu.

 Hata hivyo, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Tamisemi), George Simbachawene hivi karibuni, alisema zuio hilo ni batili na kuagiza Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam kufanya uchaguzi huo kabla ya Machi 25.

Kaimu Mkurugenzi wa jiji hilo, Sarah Yohana alisema jana  kuwa uchaguzi huo utafanyika Machi 22 kuanzia saa 4.00 asubuhi ukumbi wa Karimjee.

Alisema maandalizi ya uchaguzi huo yamekamilika, ikiwamo kusambaza barua kwa viongozi wa vyama husika na wajumbe watakaoshiriki kikao hicho
Viewing all 104799 articles
Browse latest View live


Latest Images