Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live

Edward Lowassa Azidiwa Nguvu...Magufuli Azidi Kupigilia Msumari...Aombwa Kustaafu Siasa

$
0
0
Ushauri wa kwa Lowassa, ni heri nusu shari kuliko shari kamili, bora astaafu siasa apumzike kwa heshima watanzania tutamkumbuka kwa kuleta changamoto katika siasa za nchini hii.

Lakini kwa kasi hii ya Magufuli haiwezi, kama ataendelea na ndoto zake kuutaka urais 2020 atakuja kuaibika kwa kupata kura chache pengine huenda asifikishe hata robo ya kura alizozipata 2015.
Magufuli ni habari nyingine kabisa amefunika kila upande, nyota yake inag'aa Tanzania nzima, wananchi wote wamemkubali hata Mbowe na wabunge wa upinzani wamekubali kuwa hakuna kama Magufuli.

Bora Lowassa akasoma alama za nyakati la sivyo ataendelea kuisoma namba JPM

Jaji Warioba Azungumzia Uchaguzi Mkuu wa 2015

$
0
0
Waziri Mkuu mstaafu, Joseph Warioba amesema Uchaguzi Mkuu wa mwaka jana (2015) ulifanyika kwa haki huku akitaka vyama vya siasa kuwa na demokrasia ndani yao, kuhakikisha wanayotaka Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) iwafanyie, wao pia wayafanye kwenye vyama vyao.

Amesema nchi inatakiwa kuangalia na kujadili uchaguzi usiwe bidhaa inayotafutwa kwa fedha kama ambavyo ilijitokeza katika uchaguzi wa mwaka jana ambao rushwa ilitumika kwa kiwango kikubwa.

Akizungumza katika mdahalo wa kitaifa kuhusu uchaguzi mkuu uliofanyika mwaka jana, Warioba pia ametoa angalizo kwa asasi za kiraia kuwa makini na wafadhili wao kuepuka kuingiza matakwa yao (wafadhili) kwenye siasa za ndani.

Mdahalo huo uliofanyika jana jijini Dar es Salaam, ulioandaliwa na Mpango wa Elimu ya Demokrasia Tanzania (REDET) na Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu, (LHRC).

Akiwasilisha mada, Warioba ambaye amepongeza utendaji wa Rais John Magufuli, alisema uchaguzi mkuu ulikuwa na hamasa ambayo haijapata kutokea lakini ulikuwa huru na ulimalizika kwa amani na utulivu .

Alisema akiwa mmoja wa waangalizi aliyewahi kusimamia chaguzi za Zambia, Malawi, Nigeria, Ghana, Ethiopia na Sudan, anafahamu masuala ya uangalizi na kutoa ripoti. Alisema ni kweli uchaguzi ulienda vizuri. Alisema alipoangalia maoni ya waangalizi wa nje alishangaa kwa mara ya kwanza kusifu mchakato mzima wa uchaguzi.

Alisema licha ya kuwapo kwa upungufu mdogo, waangalizi hao walisifu mchakato mzima na zaidi alishangaa kuona waangalizi ambao wagumu kusifia ; mfano Umoja wa Ulaya (EU), waliridhishwa na uchaguzi huo.

Vyama, asasi vyamulikwa
Hata hivyo alisema, katika kukuza demokrasia kwenye vyama, yapo matatizo na ipo kazi ya kufanya kwa kuwa rushwa imekuwa ikitumika kwa kuwepo matumizi mabaya ya madaraka.

Alisema bila kuleta demokrasia ndani ya chama, ni vigumu kufanikiwa katika kukuza demokrasia nchini.

“Ni rahisi kulaumu Tume ya Uchaguzi (NEC) lakini ndani ya vyama hawafuati yale wanayotaka NEC iwafanyie hivyo lazima kuwe na demokrasia ndani ya chama kwani kukiwa na vyama bila demokrasia hatupati nchi yenye demokrasia hivyo wanasiasa tupige kelele ndani ya vyama siyo NEC,”alisisitiza.

Kwa upande wa asasi za kiraia kuwa walifanya kazi ipasavyo lakini alishauri elimu kwa mpigakura iwekwe kwenye mtaala wa shule nchini na isisubiri kutolewa wakati wa uchaguzi.

Asasi na wafadhili
Akizungumzia nafasi ya asasi za kiraia, alisema zipo baadhi katika kutoa elimu, ziligeuka wanaharakati na kufikia kuhamasisha wachague chama au mgombea yupi .

Alisema walifanya hivyo ikidaiwa ni matakwa ya wafadhili jambo alilosema kwamba ni hatari masharti ya wafadhili kuingilia siasa za nchi.

Wanahabari
Jaji Warioba alizungumzia pia ushiriki wa vyombo vya habari katika uchaguzi huo na kusema vyote vilikuwa na upendeleo. Alisema hata magazeti yaliyosifika kwamba hayana upendeleo, yalizidi na mpaka sasa vyombo hivyo vina upande wake.

Alitaja baadhi ya mambo ya kuboresha ni mfumo wa kisheria na kitaasisi kwa kuboresha katiba kukuza demokrasia.

Alisema ushindi wa rais uhojiwe mahakamani na kuwepo kwa kura za uwiano kwa wabunge kuleta usawa wa kijinsia pamoja na vyama vidogo vya siasa kukua.

NEC kulalamikiwa
Alisema lazima kuwa na tume inayoaminika na wote ambayo haitawekwa wanasiasa.

Akizungumzia suala la gharama za uchaguzi,Warioba alisema sheria ipo lakini haitekelezwi kwani vyama vikubwa vinapata faida kuliko vidogo .

Alisema uchaguzi mkuu wa mwaka jana ulikuwa ni wa fedha hivyo kugeuka bidhaa kwa wenye fedha kushinda.

Alisema athari zilizojitokeza katika uchaguzi mkuu ni lugha iliyotumika ya kukebehi ,kukejeli na matusi ikiunganishwa na ushabiki hali iliyoacha makovu na uhasama katika jamii na miongoni mwa viongozi .

Alisema kumekuwa na nyufa katika taifa kwa kuwepo rushwa na ubaguzi kwani rushwa imekuwepo katika ngazi zote za mchakato wa uchaguzi kuanzia uteuzi wa wagombea ndani ya vyama mpaka kutangaza matokeo.

Alisema kumekuwa na ubaguzi wa kila aina ikiwemo ukabila, dini na kikanda ambao nyuma ulijulikana kijiografia lakini sasa zinatumika kisiasa .

Alisema zipo nyufa mpya zinazoanza kujitokeza baina ya wazee na vijana.

Mdahalo huo uliokuwa na kaulimbiu ya ‘Tathmini ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania mwaka 2015: Mchango wa waangalizi wa ndani kuelekea uchaguzi bora, huru na haki’, mgeni rasmi alikuwa Waziri wa Katiba na Sheria, Dk Harrison Mwakyembe.

Mwakyembe alisema takwimu za mwaka 2013-2014 zinaonesha kuwa kwa ujumla demokrasia nchini inazidi kuimarika na kushamiri.

Waziri alisema inaonesha kuwa Tanzania ilikuwa nchi ya 83 ikiwa na alama 50.5 kwa kukidhi vigezo vya demokrasia, ikilinganishwa na Kenya iliyochukua nafasi ya 93 ikiwa na alama 48.1. Zambia ilichukua nafasi ya 94 alama 48.1; Nigeria nafasi ya 107, alama 40.6 na Afrika ya Kusini ikichukua nafasi ya 71 alama 54.7.

Utata ACT – Wazalendo..Zitto Kabwe Adaiwa Kumpindua Mwigamba ili Achukue Nafasi yake

$
0
0
Mwigamba, Katibu Mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo ameng’atuka rasmi nafasi hiyo kwa madai kuwa anaenda masomoni, anaandika Pendo Omary.

Anna Mghwira, Mwenyekiti wa chama hicho ameliambia MwanaHALISI Online kuwa, Samson Mwigamba ataanza masomo ya shahada ya Uzamili ya Biashara (MBA) katika Chuo Kikuu cha Kenyata tawi la Arusha kuanzia mwezi Mei mwaka huu.

“Kufuatia hatua hii ameomba aruhusiwe kung’atuka nafasi yake ya Katibu Mkuu wa chama. Katika kikao chake cha dharura kilichofanyika jana katika Hotel ya Kebby’s Jijini Dar es Salaam, Kamati ya Uongozi Taifa imeridhia ombi la Katibu Mkuu,” amesema Mghwira.

Mghwira amesema kufuatia hatua ya kung’atuka kwa Mwigamba, Kamati ya Uongozi ya chama hicho imeiagiza kamati ya Mafunzo na Uchaguzi ianze mchakato wa kumpata katibu mkuu mpya kwa kuzingatia katiba na kanuni za uchaguzi wa chama.

Aidha, Mwigamba amesema hatua hiyo haimzuii kushiriki katika shughuli zingine za chama atakapohitajika na akawa na muda wa kutosha.

“Mimi ni mwanachama mwanzilishi wa ACT- Wazalendo. Nikipata nafasi nitaendelea kukitumikia chama. Japo nimekuwa kiongozi wa chama katika mazingira magumu. Kuanzisha chama bila mapato inakulazimu kuchangisha watu na wakati mwingine vyama kuwekwa mifukoni mwa watu,” amesema Mwigamba.

Haya yanajiri ikiwa ni miezi takribani mitano tangu gazeti la Mawio lililofutwa na serikali kuandika juu ya uwezekano wa Mwigamba kuondolewa katika cheo hicho ili Zitto Kabwe aweze kuteuliwa kuwa Katibu Mkuu kumwezesha kufanya kazi za utendaji za siku kwa siku ndani ya chama.

Iliandikwa kuwa Mkuu huyo wa chama ameandaa na kuratibu mkakati wa kumg’oa kwenye uongozi Katibu Mkuu, Mwigamba.

Taarifa zilisema kuwa Zitto anampindua Mwigamba ili achukue wadhifa huo, baada ya kubaini cheo cha kiongozi mkuu wa chama, hakina nguvu kiutendaji.

Vyanzo vyetu ndani ya ACT Wazalendo viliarifu kuwa kama mkakati huo ungefanikiwa Zitto angekuwa katibu mkuu, nafasi yake ya “ukuu wa chama” atapewa Mghwira.

Taarifa zilizoandikwa na Mawio zilidai kuwa kuwa mkakati huo ulianza katikati ya Septemba 2015 na ulipaswa kukamilika ndani ya miezi minne.

Waliopewa jukumu la kusimamia mradi huo wametakiwa kuukamilisha “mapema,” ikiwezekana na uwe tayari ifikapo Januari 2016.

Zitto alitajwa kuandaa na kuratibu mkakati huo, baada ya kubaini nafasi yake ndani ya chama (kiongozi mkuu) ambayo kazi yake ni kueneza sera na kutoa ushauri ndani ya chama, haina nguvu kama nafasi aliyonayo Mwigamba ya ukatibu mkuu.

Katibu Mkuu ndiye msimamizi mkuu wa utendaji siku katika chama.

Licha ya kutowekwa wazi, vyanzo vya taarifa viliarifu kuwa zitto akiwa Katibu Mkuu ataweza kuhusika moja kwa moja na fedha za ruzuku ambazo chama kingepata kama kingekuwa na sifa ya kupewa fedha hizo kutoka serikalini kulingana na matokeo ya uchaguzi mkuu

Wako Wapi Salum Mwalim, John Mnyika na Tundu Lissu?

$
0
0
Kwa muda sasa sijawasikia hawa makamanda Salum Mwalim, John Mnyika, Tundu Lissu, hata ukipita Makao Makuu ya Chadema pale Ufipa ni ngumu kuwapata.

Tulizoe kusikia na kuona matamko yao kila baada ya muda kupitia kwa Tumaini Makene ambaye naye hajulikani alipo.

Je Kasi ya Magufuli Imewanjamazisha au ndio Ukiona Kobe Kainama Ujue Anatunga Sheria....?

Nafasi za Kazi Tembelea www.ajirayako.com

Msafara wa Naibu Waziri wa Ofisi ya Rais (Tamisemi), Seleman Jafo Wapotea Dodoma

$
0
0
Msafara wa Naibu Waziri wa Ofisi ya Rais (Tamisemi), Seleman Jafo leo asubuhi ulipotea njia kutokana na watumishi wa Manispaa ya Dodoma kutojua eneo ambalo waziri huyo alikuwa analitembelea.

Waziri Jafo alikuwa amepanga kufanya ziara kwenye Shule ya Msingi ya Nzuguni B kwa lengo la kuangalia mapungufu, hasa tatizo la uhaba wa madawati, lakini hakufika kama alivyotarajia kutokana na watumishi hao kutojua eneo ambalo shule hiyo iko.

Shule hiyo haijawahi kutembelewa na ofisa elimu tangu mwaka 2007 licha ya kuwa kilomita 6 kutoka katikati ya mji.

Naibu Waziri alikasirishwa na kitendo hicho akawataka watumishi wa idara ya Elimu wajipime kama wanastahili kuendelea kufanya kazi.

“Mstahiki Meya, mimi niliona wazi kuwa watumishi wako wananipoteza," alisema Waziri Jafo.

"Nimechukia sana na hawa watu. Tatizo lao ni kwamba hawajawahi kuja katika shule hii tangu mwaka 2007, lakini wamekaa ofisini tu. Ikiwezekana waondolewe na kupelekwa vijijini,” alisema Jafo.

Mzee Mengi na Jacqueline Maisha ni Motomoto...Wakubwa Wanafaidi Sana

$
0
0
Kweli pesa ni kila kitu.Hizi ndio pesa na raha yake,sio wale watani zangu wa Nyanda za Juu Kusini,unakuwa na pesa halafu mke unamuweka kama "msukule" anakaa tu dukani siku nzima.

Bata mara moja moja kama hivi si haba,unakula bata na watoto na wife hapa na pale..Mambo ya kuja Dsm kwa kupanda fuso peleka huko...


UKAWA Yazidi Kuitesa CCM Dar es Salaam...Huyu Ndio Naibu Meya Mpya wa Jiji la Dar es Salaam

$
0
0
Diwani  wa Kata ya Kiwalani, Mussa Kafana (Cuf), ameibuka mshindi katika uchaguzi wa Naibu Meya wa Jiji la Dar es Salaam, kwa kumbwaga mpinzani wake kwa kura nne.

Uchaguzi huo ulifanyika jana katika ukumbi wa Karimjee, baada ya madiwani wa jiji hilo, ambao pia ni wajumbe wa Baraza la Halmashauri ya jiji hilo kuapishwa.

Akitangaza matokeo ya uchaguzi huo, Kaimu Mkurugenzi wa jiji hilo, Sarah Yohana alisema, Kafana ameibuka mshindi kwa kura 10 huku mpinzani wake Mariam Lulida (CCM) akipata kura sita. 

“Kura zilizopigwa ni 16 na hakuna iliyoharibika. Namtangaza Mussa Kafana kuwa Naibu Meya wa Jiji la Dar es Salaam,” alisema Yohana. 

Awali Meya wa jiji hilo, Isaya Mwita alisema, baraza hilo lina jukumu la kuhakikisha linatekeleza majukumu yake ipasavyo na kila mjumbe kupitia chama chake anapaswa kutoa mchango utakaoweza kulibadilisha Jiji la Dar es Salaam.

Akizungumza baada ya kutangazwa kuwa mshindi, Kafana aliwashukuru wajumbe wa baraza hilo huku akiahidi kushirikiana nao bila kubagua itikadi za vyama vyao, kwani wanafanya kazi kwa ajili ya wananchi na si vyama vyao. 

Alisema kwa sasa vyama havina nafasi bali maendeleo ya wananchi wa jiji hilo ndio muhimu.

Naye Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Huduma za Sheria kutoka Ofisi ya Rais, Tamisemi, Eustard Ngate, alisema, Halmashauri ya jiji hilo ilishawahi kuvunjika mara mbili mwaka 1983 na mwaka 1996 kutokana na viongozi wake kushindwa kuwajibika hivyo hawategemei hilo litokee

Milioni 50 za Rais Magufuli Kila Kijiji Zazuzua Kizaazaa

$
0
0

WAZIRI wa Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu, Jenista Mhagama alisema serikali imeweka utaratibu mzuri wa fedha za ahadi ya Rais ya milioni 50 kila kijiji, ili Watanzania wote wanufaike bila kujali itikadi zao za kisiasa.


Alisema hayo bungeni mjini Dodoma jana wakati akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Buyungu, Kasuku Bilango(Chadema) aliyetaka kusikia kauli ya serikali juu ya mgawanyo wa fedha hizo akisema ipo mizengwe kwamba fedha hizo zitatolewa kwa wanachama wa CCM .


“Serikali itoe kauli fedha hizo zitatolewa kwa utaratibu gani,” alihoji.


Mhagama alisema fedha hizo ni ahadi ya Rais aliyotoa wakati wa kampeni za uchaguzi mkuu ambao Watanzania walichagua Serikali ya CCM.


Alisema serikali inatumikia Watanzania wote bila kujali itikadi za vyama vyao.


Alisema Baraza la Uwezeshaji Kiuchumi limeanza kutengeneza utaratibu wa namna ambavyo fedha hizo zitanufaisha Watanzania wote.


Alisisitiza kuwa serikali iko imara kuhakikisha fedha hizo zinanufaisha Watanzania wote.


Awali, Mbunge wa Viti Maalumu, Halima Bulembo (CCM), katika swali la msingi, alitaka kufahamu ni lini ahadi hiyo ya kutoa Sh milioni 50 kwa kila kijiji itatekelezwa.


Alitaka kufahamu pia vijana watapata mgao wao kwa asilimia ngapi.


Mbunge huyo pia alitaka kujua mikakati ya serikali katika kuwawezesha vijana wawe wajasiriamali kwa kuwapa mitaji, mikopo na vigezo gani vitakavyosimamia na kuwalinda na kuweka usawa wa upatikanaji wa ushiriki wao katika fursa hizo.


Akijibu swali hilo, Naibu Waziri wa Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu, Antony Mavunde alisema ahadi ya Rais ya Sh milioni 50 kwa kila kijiji itaanza kutekelezwa kwa mwaka wa fedha ujao 2016/2017.


Alisema utaratibu wa kugawa fedha hizo unaandaliwa na Baraza la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi kwa kushirikiana na Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa.

Video: Dudu Baya Adai Hajawai Tumia Madawa ya Kulevya, Bangi, Wala Kunywa Bia Lakini…

$
0
0
Msanii mkongwe wa muziki wa Hip Hop, Dudu Baya amefunguka kwa kusema kuwa katika maisha yake ya muziki hajawai tumia Madawa ya kulevya, kuvuta sigara wala kunywa bia.

Rapa huyo ameiambia Bongo5 kuwa yeye ameeputa kutumia madawa ya kulevya kwa kuwa amekuwa akiishi na watu ambao wameathirika.

“Mimi sivuti sigara, sinywi bia wala situmii Madawa ya kulevya na sijawai kushawishika,” alisema Dudu. Mimi ni mnywaji wa bapa (Konyagi), lakini sio vinywaji vingine,”
Chanzo:Bongo5

Baby Madaha: Nikikosa Kufanya Mapenzi na Mpenzi Wangu Siku Tatu tu Naugua....

$
0
0
STAA wa muziki Bongo, Baby Joseph Madaha ametoa kali ya mwaka baada ya kusema kuwa, starehe yake kubwa ni kuwa faragha na laazizi wake kiasi kwamba akipitisha siku tatu huwa anaugua.

Akibonga na paparazi wetu kuhusu maisha yake ya kimapenzi, Madaha alisema kuwa kila mtu kuna kitu anakipenda hivyo yeye ugonjwa wake ni huo wa kukutana faragha na baby wake na kupeana furaha.

“Kusema ukweli miongoni mwa vitu ambavyo vinanifanya nikose amani ni kutokutana na mpenzi wangu faragha kwa zaidi ya siku tatu, huwezi kuamini naugua kabisa,” alisema msanii huyo.

Asilimia 18 Ya Simu Za Kiganjani Zaonekana Ni Bandia ,huku Asilimia 79 Zikiwa Salama

$
0
0
MAMLAKA ya mawasiliano Tanzania (TCRA) imesema kuwa asilimia 79 ya simu za kiganjani zilizofanyiwa utafiti kwa kipindi cha desemba hadi February mwaka huu ziko salama na sio za bandia ,huku asilimia 18 zikionekana zikiwa za bandia hivyo kuwataka wananchi kutambua kuwa simu feki zilizoko sokoni ni chache tofauti na kipindi cha nyuma.

Pia imebainika kuwa asilimia kubwa ya nyumba zinazoungua na umeme ni kutokana na simu bandia ambazo betri zake au vifaa vyake hushindwa kuhimili  mionzi pindi zinapokuwa zinachajiwa hivyo kusababisha mlipuko wa moto na hivyo kuleta madhara .

Hayo yalisemwa na meneja uhusiano wa mamlaka ya mawasiliano Tanzania Innocent Mungi alipokuwa akizungumza katika semina ya mfumo wa rajisi ya  namba za utambulisho wa simu za kiganjani iliyowashirikisha wadau na wafanyabiashara wa jijini hapa.

Alisema kuwa kutokana na elimu ambayo wameitoa kwa wafanyabiashara wa simu  hizo ya kuhakiki kwanza kabla ya kuwauzia wananchi imepunguza uingizaji wa simu feki na kwamba wamebaini kuwa asilimia 79 ni salama hazina matatizo ya aina yeyote.

Alidai kuwa kufuatia uzimaji wa simu bandia litakalofanyika juni 16 mamlaka hiyo imeweza kutoa elimu kwa wauzaji,watumiaji ili kuhakikisha kuwa wanabini simu zao kama ni salama ili kuweza kuepuka zoezi la kuzimiwa simu zao bila yawao kujiandaa.

“Wakati tumeanza kubaini zoezi la kutambua simu feki tulibaini kuwa asilimia 30 zilikuwa bandia ila kutokana na elimu iliyotolewa hadi February simu bandia zimepungua hadi kufikia asilimia 18 hii inaonyesha kuwa simu feki zilizoko sokoni ni chache mno “aliongeza .

Aidha Innocent alitaja faida za kuzimiwa simu bandia kuwa ni pamoja na kuongeza usalama mtandaoni kwa watumiaji wa simu ,kupunguza wizi wa simu  na kupunguza matukio ya uhalifu ambayo yamekuwa yakitumika mara nyingi kwa njia ya simu hizo pamoja na kuzuia matumizi ya simu zisizokuwa na viwango.

Awali mkurugenzi mkuu wa mamlaka hiyo Ally Simba aliwataka wananchi kufanya zoezi la kuhakiki simu zao kwa kufuata maelekezo sahii ili waweze kubaini simu feki kabla ya kuzimiwa simu hizo juni 16 ,kwani wengi wa watumiaji wa simu hawafuati malekezo ya kutambua simu bandia .

Simba aliseama kuwa ni vema wananchi wakatumia mfumo waliowekewa wa kubaini  simu zao kama ziko salama kwani ifikapo juni simu zote bandia zitazimwa na kuwataka wafanyabiashara nao wawe makini pindi wanaponunua mizigo yao ya bashara ili kuepuka hasara watakazozipata wao na pia hasara watakazopata wanunuzi wa simu hizo .

SIWEMA wa Nay wa Mitego Atupwa Jela Miaka 2..Kisa Mkasa Huu Hapa

$
0
0
Ni stori iliyoanza kuchukua headlines April 21, 2016 Ikiwa bado tunasubiria taarifa kamili kutoka Mahakamani, sasa Ayo TV ilimpata staa Nay wa Mitego kuthitibisha taarifa hizo za mzazi mwenza, Siwema kufungwa miaka miwili Jela.


Ni stori iliyoanza kuchukua headlines April 21, 2016 Ikiwa bado tunasubiria taarifa kamili kutoka Mahakamani, sasa  Ayo TV ilimpata staa Nay wa Mitego kuthitibisha taarifa hizo za mzazi mwenza,  Siwema kufungwa miaka miwili Jela.

Akizungumza staa huyo na ripota wa Ayo TV alisema…>>>’Taarifa nimezipokea ni kweli Mzazi mwenzangu amefungwa na ninakumbuka nilipoamka tu nikakutana na missed calls za ndugu zake kadhaa ambao wananifahamu nikahisi kuna kitu maana sio kawaida watu kunipigia mara kwa mara, kumpigia akaniambia Siwema amehukumiwa miaka miwili Jela sikuamini ikanibidi nimpigie tena ndugu wa karibu naye akanithitibishia hivyo‘ – Nay wa Mitego

‘Kosa unajua mimi nilishasahau kwamba kitu chochote kichotokea kipindi cha nyuma kwasababu ni muda kidogo na pia sikuwa naye kwenye mawasiliano ila niliachoambiwa kuwa amehukumiwa miaka miwili kutoka na kosa lake, nimejikuta nimekuwa mnyonge nimeingia imani kusikia habari hiyo’ – Nay wa Mitego

Unaweza ukabonyeza play kutazama interview ya Nay wa Mitego akizungumza kuhusu kufungwa kwa Mzazi mwenza miaka miwili Jela

Dogo Janja: Najuta Kutomaliza Shule..Stress na Umaarufu Vilinichanganya Sana....

$
0
0
Rapa wa Tip Top Connection, Dogo Janja amesema ana mpango wa kurudi shule kutokana na muziki wake pamoja na maisha kuhitaji elimu yakutosha.

Akizungumza katika kipindi cha 360 cha Clouds TV Ijumaa hii, Dogo Janja amesema kuna wakati anajuta kabisa kutomaliza shule.

“Kusema kweli najuta kutomaliza shule,” alisema Dogo Janja. “Msanii lazima uwe pande mbili, huwezi kuwa msanii wakati wote, kuna wakati utahitaji kufanya mambo mengine,”

Dogo Janja amesema muziki ndio kitu ambacho kilimsabisha ashindwe kuzingatia masomo.

“Nilikuwa nikifungua radio au TV kote nazungumziwa, stress zikawa zinanichanganya nikawa sisomi, bila stress ningesoma na ningefaulu. Nampango wa kurudi shule za private, kwa sababu elimu ni kila kitu,” alisema Dogo Janja.

Pia Janjaro amewataka vijana walio mashuleni kuzingatia masomo yao kwa elimu ndio kila kitu katika maisha.

Lulu Michael Adaiwa Kutafuta Laana Kwa Mama Kanumba....Ashambuliwa kwa Maneno na Mashabiki Wake

$
0
0

KITENDO cha muigizaji wa filamu Bongo, Elizabeth Michael ‘Lulu’, kudaiwa kutoa maneno yenye kuonesha sawa na kumtusi mama mzazi wa marehemu Steven Kanumba, Flora Mtegoa, baadhi ya watu wamesema kuna dalili za msichana huyo kuitafuta laana.

Hivi karibuni, mama Kanumba aliliambia gazeti moja nchini (siyo ya Global Publishers) kuwa tabia ya mpenzi huyo wa zamani wa mwanaye imebadilika sana na kukosa maadili, kiasi cha kumuita yeye kuwa ni kubwa jinga.

“Hata kama siyo mama yake mzazi, lakini umri tu unatosha kumuonesha kuwa anahitaji kumheshimu, huwezi kumuita mtu aliyekuzidi kubwa jinga, vinginevyo ni utovu mkubwa wa nidhamu na kwa mujibu wa mila na desturi za Watanzania, huku ni kama kutafuta laana, mama Kanumba ni kama mzazi wake,” alisema msomaji mmoja wa gazeti hili, aliyejitambulisha kwa jina la Tabia Doffa wa Kimara.

Msomaji mwingine aliyepiga simu chumba cha habari kutoka Tanga, aliyelitaja jina lake kama Aesha, alisema kinachoonekana umaarufu umempa upofu, kiasi cha kushindwa kuwaheshimu watu wanaomzidi umri, tena mtu ambaye angeweza kuwa mama mkwe wake, ikizingatiwa kuwa Lulu alikuwa mpenzi wa Kanumba.

“Huyu mtoto umaarufu umempoteza, huwezi kutoa maneno kama hayo kumwambia mtu ambaye angeweza kuwa mkweo, hivi kama Kanumba angekuwa hai angeweza kumwambia namna hiyo? Hili ni tatizo la malezi, mambo mengine ya ustaa ni ulimbukeni tu, laana inamnyemelea huyu,” alisema Aesha.

Akizungumzia suala hilo, mama Kanumba alisema anasikitishwa sana na tabia ya msichana huyo, kwani kikubwa ambacho angefarijika kupata toka kwake ni heshima tu na wala si kingine chochote.

“Sielewi jambo gani limemtokea huyo binti mpaka kufikia hatua ya kuniita hivyo, lakini yote namwachia Mungu maana anajua anachokifanya,” alisema mama huyo huku akionekana kulengwa na machozi.

Kwa upande wake, alipoulizwa kuhusu kutoa kauli nzito kwa mama huyo, Lulu alisema hapendi kumzungumzia chochote kwani siyo staili yake kuzungumzia mambo ya wengine katika vyombo vya habari.

“Kama yeye amesema hivyo kwenye vyombo vya habari ni staili yake, mimi staili yangu ni ya kukaa kimya, sitaki kabisa kumzungumzia huyo mama,” alisema Lulu.

Chanzo:GPL

Ladies: Hizi ni Dalili Tisa Kuwa Wewe si ‘Main Chick’ Bali ni Mchepuko Wake tu!

$
0
0

Wanaume wengi ni wataalam wa kuwa na uhusiano na wanawake wengi kwa wakati mmoja. Sasa kwa msichana unayesoma makala hii, hizi ni dalili 9 kuwa huenda wewe si ‘baby number one’ wake bali ni mchepuko tu.

1. Mazungumzo mengi naye yanahusisha kufanya mapenzi tu

2. Hawezi kukualika kwenye mkusanyiko wa familia yake

3. Hapendi surprises – hapendi uende kwake bila kumwambia

4. Ni mkali sana kwenye simu yake, hawezi kukuruhusu uishike

5. Ni mgumu kukuonesha mahaba ukiwa naye hadharani

6. Anahofia kupiga selfie na wewe

7. Anapigiwa simu za ajabu ajabu

8. Hakuiiti wewe kama girlfriend wake. Akiwa na marafiki au
ndugu zake anakutambulisha kwa jina lako

9. Haongelei kuhusu mipango yenu ya baadaye

Wakati Tanzania Mirungi ni Haramu..Kenyatta Atoa Dola 10m za Kilimo Cha Mirungi

$
0
0

Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta ametangaza kwamba serikali yake itatenga dola za Kimarekani 10 milioni za kusaidia wakulima wa mirungi kwenye bajeti ya mwaka ujao wa kifedha.

Wakulima hao wameathirika sana kufuatia hatua ya baadhi ya nchi za Ulaya kupiga marufuku uuzaji wa mirungi, maarufu pia kama miraa, katika mataifa hayo.

Hutumiwa sana na watu wa jamii ya Wasomali na hutegemewa sana na jamii zianzoishi katika maeneo ya mashariki ya Mlima Kenya, miongoni mwa watu wa jamii ya Wameru.
Pesa hizo zitatolewa kupitia Wizara ya Kilimo.

Rais Kenyatta ametangaza hayo alipokuwa akitia saini mswada unaotambua mirungi kuwa mmea wa kuzalishia taifa mapato kuwa sheria.

Sheria hiyo itaifanya serikali kuweka mikakati ya kutangaza, kuzalisha na kusambaza na kuuza zao hilo.

Rais Kenyatta amesema kutaundwa pia jopo kazi la kuangazia changamoto zinazokabili sekta ya ukuzaji wa mirungi ambayo itatoa mapendekezo kwa serikali.

Umesikia Hii Kuhusu Wabakaji wa Watoto Wadogo Kuhasiwa Wanapokamatwa?

$
0
0

Sheria mpya imeidhinishwa nchini Kazakhstan inayoruhusu utumiaji wa kemikali kuhasi ili kuwaadhibu watu waliopatikana na hatia ya kufanya ngono na watoto.

Hatua hiyo ni mojwapo ya sheria mpya kulinda haki za watoto.

Afisi ya mwendesha mashtaka mkuu wa Kazakhstani imesema kuwa visa vya watu wanaopenda kufanya ngono na watoto vimeongezeka kwa asilimia 50 mwaka uliopita.

Lakini wataalam wanasema kuwa kuhasi hakuna madhara makubwa ,hakudumu,hulazimika kurejelewa na ni ghali .

Ofisi ya Waziri Mkuu Waamua Kutumia Bajaji na Piki Piki Kubana Matumizi...Mashangingi Sasa Basi

$
0
0

Dodoma. Kamati ya Katiba na Sheria ya Bunge imeipongeza Ofisi ya Waziri Mkuu kwa kutenga fedha ya kununulia bajaji na pikipiki zitakazotumiwa na watumishi kwa mwaka huu wa fedha, ikiwa ni mkakati wa kubana matumizi.

Wizara iliyo chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu ni ya Sera, Bunge, Vijana, Kazi, Ajira na Walemavu.

Akiwasilisha maoni ya kamati hiyo kwa bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu ya mwaka 2016/17, mwenyekiti wa kamati hiyo, Mohamed Mchengerwa amesema uamuzi wa namna hiyo unaendana na dhana ya kubana matumizi ya fedha ya Serikali ya Awamu ya Tano.

Hata hivyo, hotuba ya bajeti iliyosomwa na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa leo, haionyeshi pikipiki na bajaji hizo zinanuliwa kwa ajili ya wafanyakazi wa kada gani.

Ukimya Wa Msanii Alikiba Wawatesa Mashabiki Wake Kwenye Mitandao Ya Kijamii

$
0
0

Tupo kwenye ulimwengu ambao mitandao ya kijamii imegeuka kuwa kama chakula ambacho ni lazima ule kila siku. Kwa watu maarufu, mitandao imegeuka kuwa sehemu muhimu kwa wao kuwa karibu na mashabiki wao. 

Mashabiki wanatarajia kuona kila hatua ambayo msanii anaipitia katika shughuli zake za kila siku. Wanataka kuona si tu picha zake akiwa studio akirekodi muziki au jukwaani akitumbuiza, bali pia za maisha binafsi kama vile akiwa na familia au washkaji. 
Na kwa mashabiki, msanii wanayempenda akiwa kimya hata kwa siku moja tu, hukosa raha na kila wakati huchungulia kwenye akaunti yake kuangalia nini alichoweka. Kwao ni furaha kuona picha za staa huyo na pindi anapoamua kukaa kimya huwanyima kitu muhimu katika yao. Huo umekuwa ni kama ulevi na unaweza kushangaa kwanini mtu anajiskia hivyo lakini ukweli ni kwamba ‘this is real.’ 
Mashabiki wa Alikiba wanalalamika kuwa amekuwa kimya sana siku za hivi karibuni. Picha ya mwisho kwenye akaunti yake ya Instagram iliwekwa siku sita zilizopita. Wanahisi hawatetendei haki kwa ukimya wake na kwa sababu post zake ni kitu kinachowapa furaha, wameanza kukosa uvumilivu. 
Lakini mashabiki wanapaswa kufahamu kuwa wakati mwingine msanii anaweza asiwe na ‘mood’ ya kushare kila kitu kwenye mitandao ya kijamii. Ni kitu cha muhimu lakini sio lazima na ukiangalia post za nyuma, kama wasanii wengine Kiba amekuwa mstari wa mbele kuwaweka karibu mashabiki wake kwa posts za kikazi na familia. 
Na mara nyingi anapokaa kimya kwenye mitandao hiyo haiimanishi kuwa hana mambo anayofanya. Beyonce huamua kukaa kimya hata kwa mwezi mzima bila kuweka chochote Instagram. 
Nicki Minaj, Rihanna na wasanii wengi tu wamekuwa wakiamua kukaa kimya kwa sababu maalum. 
Nadhani ni muhimu kuacha kuifanya mitandao ya kijamii iwe kielelezo cha mambo yanayoendelea kwenye maisha yetu. 
Kwasababu kabla ya Instagram, Facebook au Twitter, maisha yalikuwa ya heri tu na mashabiki walizoea kuishi karibu na mastaa wanaowapenda hata kwa kusikiliza tu nyimbo zake.

Rais Magufuli Awageukia Watumishi HEWA Ndani ya CCM

$
0
0

Rais John Magufuli juzi aliwazungumzia makada walioihama CCM wakati wa mchakato wa Uchaguzi Mkuu uliopita, alipoeleza kuwa kuondoka kwao pengine kulimsaidia kupata ushindi.


Bila kutaja majina ya waliokihama chama, Magufuli alisema ni vyema wana CCM wakasahau tofauti zilizojitokeza wakati wa uchaguzi huo na kuganga yajayo.


Rais alisema hayo kwenye mkutano na viongozi wa CCM wa mikoa na wilaya zote nchini, uliofanyika juzi Ikulu jijini Dar es Salaam.


Alisema kuna mengi yalitokea wakati wa uchaguzi huo na yalikidhoofisha chama na hivyo kuna haja ya kuyasahau yaliyopita na kuangalia mbele katika kukijenga chama.


“Lakini inawezekana wale walioamua kwenda kule walisaidia mimi kushinda,”alisema bila ya kufafanua.


Baadhi ya wana CCM waliokihama chama hicho wakati wa uchaguzi huo ambao ulikuwa na ushindani mkubwa kuanzia ndani ya chama hicho ni pamoja na mawaziri wakuu wa zamani, Edward Lowasa aliyehamia Chadema, Frederick Sumaye, ambaye kwanza alitangaza kujiunga na upinzani bila ya kutaja chama na mapema mwaka huu kukabidhiwa kadi ya Chadema.


Mwingine ni aliyekuwa kada mkongwe wa CCM, Kingunge Ngombale Mwiru, Balozi Juma Mwapachu, mawaziri, wabunge na madiwani, wengi wakijiunga na Chadema, ambayo ilimsimamisha Lowassa kuwa mgombea wake wa urais akiungwa mkono na vyama vya NLD, NCCR-Mageuzi na CUF vilivyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa).


Lowassa alionekana kuwa kinara kwenye harakati za urais ndani ya CCM, akichuana vikali na Bernard Membe, lakini jina lake halikufikishwa kwenye Kamati Kuu, ambayo ilitangaza majina matano, akiwamo Magufuli, yaliyopelekwa Halmashauri Kuu ya chama hicho.


Kitendo hicho kilifanya wajumbe wa Halmashauri Kuu kumpinga waziwazi mwenyekiti wa CCM, Jakaya Kikwete na baada ya juhudi za wazee wa chama hicho, hali ilitulia na Magufuli akaongoza kwa kura nyingi. Baadaye Lowassa alitangaza kuhamia Chadema na kufuatiwa na wanachama kadhaa.


Alipotangazwa mshindi wa Uchaguzi Mkuu, Magufuli alisema wakati akihutubia wanaCCM kwenye ofisi ndogo ya chama hicho Lumumba jijini, alisema uchaguzi huo ulikumbwa na hujuma zilizofanywa na wanafiki waliojificha ndani ya chama hicho.


Alisema ni vema wanafiki hao wakajisalimisha kwa kutubu kwa kuwa wamekigharimu chama hicho na kusababisha kiwe kwenye wakati mgumu.


Dk Magufuli alisema anaona ni bora kuishi na mchawi kuliko mnafiki, na kumuomba Kikwete asiwahurumie wanaokihujumu chama. 


CCM walikidhoofisha chama 

Juzi, akizungumza kwenye mkutano huo na viongozi wa CCM ambao katika hali isiyokuwa ya kawaida hawakuvaa sare zao za chama, Magufuli alisema waliokidhoofisha chama ni wana CCM wenyewe na ndiyo maana wapinzani walitumia udhaifu huo kukisaliti.


“Tulithamini fedha kuliko chochote. Wala hatukuuliza hizi fedha zimetoka wapi. Tuliowapa miradi, walituchezea, tumejikaanga CCM kwa mafuta yetu wenyewe. Kama tulifanya makosa, tusifanye tena,” alisema.


Aliwataka viongozi hao wa CCM kuanza kuzungukia maeneo yao ili kuwashukuru wananchi kwa ushindi na kukiimarisha chama.


“Kwa kifupi, nyinyi ndiyo Serikali. Kiongozi yeyote mnayemuona hatekelezi ilani yake, huyo hafai kwenye safari hii. Mimi niwaahidi hatutasita kuchukua hatua kwa wale mtakaoona hawafai,” alisema.


Awali Katibu Mkuu wa chama hicho, Abdulrahman Kinana alisema Kamati Kuu ya CCM imepokea ripoti ya uchaguzi huo wa Oktoba 25 kutoka mikoa yote na wiki ijayo itafanyika tathmini ya maandalizi, mchakato wa kuwapata wagombea, matokeo, upigaji kura na utangazaji wa matokeo.


Azungumzia Watumishi Hewa  CCM

Kadhalika, Magufuli alimtaka Kinana kuanza kuchukua hatua za kuondoa wafanyakazi hewa ndani ya chama hicho.


“Na mimi nina uhakika katibu mkuu hata kwenye chama wapo wafanyakazi hewa kwa sababu watu ni wale wale, ni Watanzania wale wale. Kwa hiyo na wewe uanze kuchukua hatua dhidi ya wafanyakazi hewa walioko kwenye chama,” alisema.


Alisema Serikali inatumia zaidi ya Sh583 bilioni kulipa mishahara, lakini mpaka sasa kuna wafanyakazi 7,700 hewa wakati uchambuzi bado ukiendelea. 
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live




Latest Images