Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live

Breaking Newa: Rais Magufuli Aivunja Bodi ya TCRA na Kumsimamisha Kazi Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka Hiyo Dr Ally Yahaya Simba

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ameivunja Bodi ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) na kumsimamisha kazi Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka hiyo Dkt. Ally Yahaya Simba kutokana na kutosimamia ipasavyo Mkataba wa utekelezaji wa mfumo wa usimamizi wa mawasiliano ya simu (TTMS), na kusababisha nchi kupoteza mapato ya takriban shilingi bilioni 400 kwa mwaka.

Rais Magufuli amechukua hatua hiyo leo tarehe 26 Aprili, 2016 Ikulu Jijini Dar es salaam baada ya kufanya kikao cha kazi kati yake na viongozi na wataalamu kutoka Wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi, Wizara ya fedha na Mipango na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU).

Tarehe 22 Machi, 2013 Mamlaka ya Mawasiliano nchini (TCRA) iliingia mkataba na kampuni ya SGS juu ya uwekaji, uendeshaji na uhamishaji wa mapato ya simu ambapo kampuni hiyo ilipaswa kutekeleza vipengele vitano lakini mpaka sasa kampuni ya SGS haijaanza kutekeleza kipengele kidogo kinachohusiana na uthibiti wa mapato ya simu za ndani (Offnet), hali ambayo imesababisha serikali kukosa mapato yanayokadiriwa kuwa shilingi bilioni 400 kwa mwaka.

Pamoja na kuivunja bodi ya TCRA inayoongozwa na Profesa Haji Semboja na Kumsimamisha kazi Mkurugenzi Mkuu wa TCRA Dkt. Ally Yahaya Simba, Rais Magufuli pia amemuagiza Waziri wa Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi Profesa Makame Mbarawa Mnyaa kumteua Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka hiyo mara moja.

Aidha, Rais Magufuli amewataka Waziri Prof. Mbarawa, Katibu Mkuu na Naibu Katibu katika wizara hiyo kuchukua hatua mara moja ili mfumo wa ukusanyaji wa mapato ya simu kwa simu za ndani (Offnet) uanze kufanya kazi, na nchi ipate mapato yanayostahili kukusanywa.

“Waziri hakikisha unachukua hatua mara moja, nataka tukusanye mapato yote ya serikali yanayostahili na sitasita kuchukua hatua  dhidi ya yoyote atakayekwamisha jambo hili” Amesisitiza Rais Magufuli.

Gerson Msigwa

Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU
Dar es salaam
26 Aprili, 2016

Tanzia: Mke wa Rais Mstaafu wa Kenya Mama Lucy Kibaki Afariki Dunia

$
0
0
Mke wa Rais mstaafu  wa    Kenya, mama Lucy Kibaki amefariki dunia . Lucy alifariki katika hospitali ya Bupa Cromwell mjini London alikokuwa amelazwa.

Alisafrishwa hadi mjini Landon wiki moja iliopita kwa matibabu.

Akithibitisha kifo chake rais wa Kenya Uhuru Kenyatta amesema kuwa kenya imesikitishwa na kifo cha mama Lucy mke wa aliyekuwa rais wa Kenya Mwai Kibaki.

Katika taarifa iliotumwa katika vyombo vya habari Uhuru amesema bi Lucy amekuwa mgonjwa kwa kipindi cha mwezi mmoja .

Amesema kuwa Kenya imempoteza mwanamke aliyechangia mengi katika maendeleo ya taifa la Kenya hususan katika vita dhidi ya ugonjwa wa ukimwi.

Rais ametuma risala za rambi rambi kwa mtangulizi wake Mwai Kibaki pamoja na familia yake.

Chanzo:BBC

Wastara Juma Aeleza Kwanini Ndoa yake na Mbunge Imevunjika Ndani ya Siku 80, Pia Kukatwa Mguu

$
0
0
Mwigizaji Wastara anavyo vichwa vya habari Tanzania kutokana na ndoa yake kuvunjika ndani ya siku 80 akiwa kaolewa na Mbunge wa Zanzibar, hii ndio ndoa yake iliyowahi kukaa kwa muda mfupi zaidi… kaongelea pia mguu wake kutaka kukatwa na mengine kwenye hii video hapa chini.

Tazama Video Hapa Chini:

Chanzo:Millard Ayo

Mr Blue Aibuka na Kumtuhumu Mh Sugu Kumuibia Wimbo wa Freedom..Ushahidi Kamili Huu Hapa

$
0
0
Msanii wa Bongefleva ambaye jina lake lilianza kushine kwenye game ya muziki wa Bongofleva toka akiwa na umri mdogo Mr. Blue, amerudi kwenye headlines baada ya kupost kupitia account yake ya instagram na kuelezea hisia zake kuhusu wimbo mpya alioutoa Mr. II Sugu kuwa ni wimbo ambao alimshirikisha na anashangaa kuona mambo yapo tofauti.

Katika post ya instagram Mr. Blue aliandika

“Ndugu zangu nipeni ushauri kwa hili niliona nikae kimya ila limeniuma sana kwa kweli ..!! SUGU namuheshimu km kaka yangu kimuziki na kiumri pia ..sasa kuna nyimbo nilimshirikisha inaitwa “Freedom” tulifanya pale kwa makochali na hiyo ndo picha ya ushahidi na nyimbo ipo youtube kwa wasioisikia..sasa kinachonishangaza leo kuona ameitoa verse yangu na kuweka verse zake mbili na kaishoot mpaka video na nyimbo imekuwa yake tena bila kunitaarifu mimi mwenyewe au ridhaa yoyote kutoka kwangu je hii ni haki kweli??? Maana mtu ukiongea unaonekana unatafuta kiki au sijui nn…mi imeniuma kwa kweli jamani je mnanishauri nini ndugu zangu….????”

Hii ndio video mpya Mr. II aliyoitoa leo April 25 2016 ‘Freedom’ na chini yake nimekuwekea wimbo wa Mr Blue Feat. Sugu
Wimbo wa mr Blue

MJ Records Wazungumzia Ukweli Kuhusu Wimbo Freedom Ulioleta Mgogoro Kati ya Sugu na Mr Blue

$
0
0
Mr Blue analalamika kuwa Sugu ameupora wimbo wake ‘Freedom’ aliokuwa amemshirikisha kwa kutoa verse zake na kuufanyia video iliyotoka jana.

Lakini katika kila malalamiko, ni vyema kusikiliza pande zote zinazohusika kwenye jambo husika ili kuupata ukweli. MJ Records walioutayarisha wimbo huo wamezungumza kuelezea mambo yalikuwaje.

Producer mkuu wa studio hiyo, Marco Chali ameiambia Bongo5 kuwa beat ya wimbo huo ilitengenezwa na mdogo wake, Daxo Chali aliyetengeneza chorus yake na alimpa msanii wake Lizzy aliyeingiza.

“Ngoma ilikuwa ipo tayari na ilikuwa inasubiria verse tu kadhaa halafu ilikuwa ni ngoma yake [Daxo]. Kwahiyo jamaa [Blue] akawa ameipenda tukampa akasema atamshirikisha Mr Two,” amesema Marco.

Walipoifanya, Blue aliiamua kuiachia kupitia Mkito peke yake kwa maana kwamba hakuiachia ngoma rasmi. Anasema baada ya muda Sugu alimpigia simu kumuomba kuwa afanye version nyingine ya wimbo huo na aifanyie kabisa na video.

Anadai alimuambia Sugu aongee na Daxo waliyekubali kuufanya tena hadi video ikafanyika huku yeye [Marco] akiwa hajui chochote kilichoendelea baada ya hapo. Na Marco anasema pia hakuhusika kwenye uingizaji wa sauti zote mbili zaidi ya kuzifanyia mixing peke yake.

Marco amesema anadhani wawili hao [Sugu na Blue] waliongea kuhusu hatua hiyo na kwamba wao kama studio hawakuwa na kipingamizi chochote kuhusu kurudiwa kwa wimbo huo kwasababu walitaka wimbo ufike mahali.

Hata hivyo Marco amedai kuwa wote wawili [Sugu na Blue] hawakulipia wimbo huo na kwamba MJ Records iliwapa kwasababu ya ‘love’ tu. Marco anasema anashangaa kuona Mr Blue sasa hivi anatoa malalamiko hayo.

“Ni kwasababu mimi nilipenda tu kutoa studio bure kwanini usijitahidi ukapeleka hiyo nyimbo ikafika sehemu ikafahamika, at least pia akili za watu zilizotumika watu wazione. Na ndio hicho kitu naona ni kizuri, yeye kwa mfano angefanya hata video, sidhani kama Sugu angerudia huo wimbo,” ameongeza Marco.

“Na yeye aliposema kwamba anataka afanye video, namaanisha kwamba walishaongea na Blue kwamba yeye afanye video. Halafu Daxo wasije kumweka tena kwenye matatizo akaonekana kwamba ni producer mzinguaji ni vitu ambavyo havitamsababishia biashara na dogo mwenyewe ndio anataka kutoka. Na anajua wazi kuwa ni watu wazima wameongea kule,” amesisitiza Marco.

Kwa upande wake Daxo Chali amethibitisha alichosema kaka yake.

“Mr Blue Hajanilipa Hela Yoyote Kama Hilo Swala Ndio Mnataka Kujua , Na Mr Blue Na Sugu Wote Wameikuta Beat Studio Ikiwa Na Chorus Ambayo Mimi Ndio NimeAndika Na Kumuweka Msanii Wangu Na Idea Ya Wimbo Ni Ya Kwangu Pia,” ameandika kwenye post yangu ya Instagram.

“So Mr Blue Hakuiwekea Mkazo FREEDOM Then Sugu Akaomba Afanye Version Yake. Mimi Sioni Kama Kuna Tatizo Hapo, Labda Kama Angefanya Msanii Ambaye Hayupo Kwenye Wimbo Wa Kwanza. Wamalize Tofauti Zao Tu.”

Naye Sugu amedaiwa kujibu malalamiko ya Blue kwa ujumbe huo chini kwenye WhatsApp

Tahadhari ya Kuwepo Kwa Mvua Kubwa na Upepo Mkali...

$
0
0
Mamlaka ya Hali ya Hewa imetoa tahadhari kuhusu mvua kubwa na upepo, Soma Hapa chini:

Lugumi yazua Balaa Lingine..Maofisa wa Polisi Wahaha Kuunganisha Mitambo ya Alama za Vidole ifanyaje Kazi

$
0
0
Sakata la mkataba kati ya Jeshi la Polisi Tanzania na Kampuni ya Lugumi Enterprises wa kufunga vifaa 108 vya kuchukua alama za vidole katika vituo vya polisi, limezua balaa lingine kufuatia madai kwamba, maofisa wa polisi wameanza kupita katika vituo wilayani na mikoani kukagua na kuunganisha mitambo hiyo ili iweze kufanya kazi.

Taarifa zilizopatikana kutoka ndani ya jeshi  hilo zinadai kuwa, zoezi hilo limeanza huku kukiwa na usiri mkubwa.

Habari kutoka makao makuu ya polisi zinasema kuwa, maofisa wa polisi walitawanywa vituo mbalimbali nchini wakifuatilia kwa karibu suala hilo ambalo linalitikisa vichwa vya viongozi serikalini.

Aidha, gazeti hili likiwa Kituo Kikuu cha Polisi Mkoa wa Pwani, Ijumaa iliyopita lilishuhudia maofisa wa polisi wakiwa na wataalam kutoka makao makuu ya jeshi hilo jijini Dar na kuambiwa walikwenda kwalengo la kuunganisha mashine hizo ili zianze kufanya kazi.

Baadhi ya polisi kituoni hapo waliozungumza kwa masharti ya kutotajwa majina kwa kuwa siyo wasemaji, walidai kuwa kutofanya kazi kwa mashine hizo kulizorotesha shughuli za upelelezi hasa namna ya kuwatafuta wahalifu sugu wanaofanya uhalifu mkoa mmoja na kuhamia mwingine bila kujulikana.

Wakifafanua umuhimu wa mitambo hiyo, polisi hao walisema mhalifu, hasa jambazi anapokamatwa katika kituo chochote cha polisi, akifikishwa wilayani au mkoani hupigwa picha na kuchukuliwa alama za vidole na kuingizwa katika mtandao, hivyo kuwa rahisi kujua kama alishawahi kufanya uhalifu popote nchini.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani, ACP Bonaventura Mshongi alipoulizwa kama amepokea ugeni wa polisi kutoka makao makuu kwa ajili ya kufuatilia mashine hizo, alikiri kupata wageni ofisini kwake. Hata hivyo, hakuwa tayari kufafanua walichokifuata.

Tayari bunge limeunda kamati ndogo yenye wabunge tisa iliyopewa kazi ya kuchunguza kwa kina mkataba huo, kwa mujibu wa Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), Aeshi Hilary.

Hilary alisema kuundwa kwa kamati hiyo kumetokana na uamuzi wa Spika wa Bunge, Job Ndugai ambaye ameielekeza kwenda kuchunguza kwa kina mkataba huo na kupewa siku 30 za kufanya kazi hiyo kisha taarifa itatolewa bungeni.

Kamati hiyo itawahoji mawaziri, viongozi wa jeshi la polisi waliopo na waliostaafu na wafanyabiashara waliotajwa pamoja na kampuni zilizoshiriki kufunga mashine hizo.

Naye Mkurugenzi wa Upelelezi na Makosa ya Jinai (DCI), Diwani Athuman alipotafutwa kwa njia ya simu na Uwazi, juzi (Jumapili), alisema hana taarifa hizo na badala yake akaelekeza atafutwe msemaji wa jeshi la polisi, Advera Bulimba ambaye mpaka gazeti hili linakwenda mitamboni, hakupatikana.

Mwaka 2011, Kampuni ya Lugumi  ilipewa zabuni ya kufunga mashine za kuchukua alama za vidole katika vituo vya polisi 108 nchini ambapo inadaiwa imeshalipwa Sh. bilioni 34 kati ya bilioni 37, sawa na asilimia 99 ya malipo yote.

Hata hivyo, kuna madai kwamba ni vituo 14 tu vilivyofungwa mashine hizo huku mashine moja pekee ikiwa ndiyo inayofanya kazi.

Chanzo:GPL

Nani wa Kutumbua Jipu Kwenye Wizara ya Ujenzi iliyokuwa Chini ya Rais Magufuli Wakati Huwo Akiwa Waziri?

$
0
0
Nani wa kutumbua jipu kwenye Wizara ya ujenzi iliyokuwa Chini ya Rais Magufuli wakati huwo akiwa Waziri... Ripoti ya Mkaguzi wa Serikali CAG imeonyesha ubadhirifu Mkubwa kwenye Wizara hiyo kuliko Wizara yeyote ile.

Watanzania mtapa kujua mengi nyakati muhimu zikifika, endeleeni na mahaba ya utamu wa karanga...

Gari Bovu haliwezi kuwa jipya kwa kutafuta Dereva mpya. Mabadiliko ya Taifa hili ni CCM kuondoka Madarakani.

Ndiyo maana Wamehakikisha Bunge halionyeshwi live kwakuwa wanajua Uchafu waliyoufanya utawekwa wazi na Watanzania hawatKuwa na habari nao kwakuwa watajua ukweli...

Kwanini hutaki Bunge lionyeshwe live kama wewe ni msafi? Na unapenda uwazi? TURUDISHIE BUNGE LETU LIVE TUWAONYESHE WATANZANIA MADUDU WANAVYODANGANYWA

Chanzo:Henry Kilewo

Video: Je, Umeiona Video ya Chura ya Snura? itazame Hapa

$
0
0

Video: Je, Umeiona Video ya Chura ya Snura? itazame Hapa Chini:

Sina Mpango wa Kurudiana na Siwema, Namsaidia tu – Nay wa Mitego

$
0
0
Rapa Nay wa Mitego amefunguka na kuzungumzia nini kinaendelea baada ya kutangaza kumsaidia aliyekuwa mpenzi wake Siwema ambaye amehukumiwa kwenda jela miaka miwili kwa kosa la kumtukana shabiki kwenye mtandao wa kijamii.

Nay na Siwema walifanikiwa kukaa kwenye uhusiano kwa kipindi kirefu na kufanikiwa kupata mtoto ambaye walimpa jina la Curtis kabla hawajatengana.

Akizungumza na Bongo5 Jumatatu hii, Nay wa Mitego alisema tayari ameshatuma wanasheria wake na wanaendelea kulishughulikia suala hilo kwa ukaribu zaidi.

“Nashukuru Mungu mambo bado yanaenda vizuri, wanasheria wangu wanalishughulikia hili suala kwa ukaribu zaidi. Naamini tunaweza kumsaidia. Lakini sio nataka kumsaidia kwa sababu ni mpenzi wangu, tayari tulishaachana na hatuwezi kurudiana,” alisema.

Aliongeza,
“Mimi sasa hivi nipo kwenye mahusiano na mtu mwingine, pia na yeye bila shaka alikuwa kwenye mahusiano. Kwa hiyo mimi nimemsaidia kibinadamu zaidi, kama alinikosea tayari yalishapita, hakuna aliyemkamilifu.”

Nimechoka Kudanganya Kila Siku - Mo Music Afunguka Ukweli....

$
0
0
Msanii Mo Music ambaye kwa sasa anatamba na wimbo wake wa 'Skendo' amefunguka na kusema kuwa kwa sasa amechoka kusema uongo na kuwadanganya mashabiki zake juu ya kazi zake na ukimya wake kwenye muziki.

Mo Music akizungumza kwenye kipindi cha Planet Bongo kinachorushwa na ting'a namba moja kwa vijana alidai kuwa mara nyingi amekuwa akitoa ahadi zisizo timia kwa mashabiki wake kutokana na menejimenti yake kushindwa kazi yake, ikiwepo kumfanyia video pamoja na jambo ambalo limekuwa likimkwamisha na kumrudisha nyuma.

"Unajua uongozi wangu umefika sehemu ambayo kwa sasa kwangu kuvumilia imekuwa ni ngumu kwa sababu mwanzo walinichukua kama ndugu na tuliishi kama ndugu, kwa sasa nimefanya nao kazi huu mwaka wa tatu mimi napiga jalamba lakini sioni mafanikio yoyote kiuchumi, na mimi saizi ni majukumu mengi kuna watu wanasoma kwa ajili yangu mwenyewe natakiwa kuendesha maisha kwa kazi hivyo kazi zinapokuwa haziendi nazidi kukwama mimi" alisema Mo Music.

Mbali na hilo Mo Music anasema alifika hatua aliamua kufanya maamuzi magumu na kuwashirikisha wanafamilia wake na kuamua kwenda kuonana na uongozi wake ili yeye aendelee na kazi zake mwenyewe baada ya kuona hakuna jambo lolote ambalo linafanywa na uongozi wake huo katika kuhakikisha msanii huyo anazidi kusonga mbele.

"Unajua hata mimi nimechoka kusema uongo mbele za mashabiki zangu, kila siku mimi nilikuwa nikimfuata meneja wangu juu ya kufanya video ananiambia waambie tutafanya wiki ijayo so nilichoka na hali hiyo ya kusema uongo kila siku, ndiyo maana unaona mpaka sasa sina video ya kazi zangu kadhaa kwa sababu uongozi ulikuwa hauna uwezo wa kuendelea kunipeleka mbele zaidi, ndiyo maana unaona hata mzunguko wa nyimbo zangu kwenye vyombo vya habari ulikuwa unapungua siku hadi siku na mambo mengi kwenye muziki wangu yalikuwa yanakwama kwa sababu ya uongozi".

Kutokana na hali hiyo, Moe anaweka wazi maamuzi aliyoamua kuchukua kwa kusema "Kwa sasa nimeamua kwenda mwenywe sina uongozi na imani yangu nitasonga mbele zaidi kwani Mungu aliyenipa kipaji na mashabiki ndiyo wamefanya mimi kuwa Moe Music hivyo bila hata ya uongozi wa Aljazeera Entertainment imani yangu nitaweza kusimama na kusonga mbele zaidi.

Sikiliza na Download Hapa Wimbo Mpya wa Nuh Mziwanda Feat. Ali Kiba Unaoitwa JIKE SHUPA

$
0
0
Baada ya kimya Msanii Nuh Mzinda ameachia wimbo mpya unaitwa “Jike Shupa”, amemshirikisha Ali Kiba, Producer Mr T Touch.

Mwanamke Akikujibu SMS yako Hivi Acha Haraka Sana Kuchat Nae

$
0
0
Ukiona umemtumia mpenzi wako/mchumba wako/mchepuko wako/mke wako au hata rafiki wa kike wakati mwingine SMS ya kawaida tu kwaajili ya kumsalimia lakini yeye akakujibu moja kati ya majibu yafuatayo, tafadhali sana usiendelee kuchat nae maana kinachofuata hapo ni majanga tu.

KWA MFANO: 
1. Ukimtumia sms ''Mambo mpenzi wangu?'' akikujibu ''mambo mabaya'', usimuulize kwanini mambo mabaya, ukimuuliza atakwambia kuwa ''sina hela dear''

2. Ukimtumia sms ''Maisha yanasemaje kipenzi changu'' akikujibu ''maisha magumu hubby wangu we acha tu'' usimuulize kwanini, ukimuuliza kwanini atakwambia ''nimefulia mwenzio kama nini sijui''

3. Ukimtumia sms ''Mbona kimya sana mchumba wangu, umenitupa kiasi hicho'' akikujibu ''sijakutupa wangu yaani mambo hata hayaendi'' usimuulize kwanini mambo hayaendi, ukimuuliza atakwambia kuwa ''yaani sina kitu mpenzi wangu, simu ilikuwa haina hata hela ya kubeep''

4. Au ukiona mwanamke anaanza kwa kukwambia nikwambie kitu? We mkatalie kiutani utani tu, mwambie usiniambie, hata akikomaa vipi akwambie mwambie sitaki uniambie huku unafanya kama utani lakini moyoni unakuwa upo serious.

Ni mara chache sana mwanamke akikwambia kuwa mambo mabaya, maisha magumu au mambo hayaendi huwa na matatizo mengine kama kuumwa, misiba.... n.k lakini THE REST ni wapigaji mizinga tu. Akikwambia maisha magumu mjibu ''pole wangu, mambo mengine vipi?''

Ukipewa majibu kama hayo, chagua moja, either usiendelee kuchat nae mpaka badae kidogo au mbadilishie maada ili kukwepa huo mzinga ambao unakuja mbele yako.

ACT- Wazalendo Wamteua Juma Saanani Kuwa Kaimu Katibu Mkuu Kujaza Nafasi Iliyoachwa na Samson Mwigamba

$
0
0

MAAZIMIO YA HALMASHAURI KUU YA CHAMA CHA ACT-WAZALENDO KUFUATIA KIKAO CHAKE CHA

JUMATATU TAREHE 25 APRILI 2016


Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama cha ACT-Wazalendo ilifanya kikao chake cha kawaida jana (Jumatatu) tarehe 25 Aprili 2016 Jijini Dar es Salaam.


Pamoja na mambo mengine, Halmashauri Kuu:

1. Ilimteua Ndugu Juma Saanani kuwa Kaimu Katibu Mkuu wa Chama hadi pale uchaguzi mkuu wa ndani ya chama utakapofanyika.


Uteuzi huu unafuatia kung’atuka kwa aliyekuwa Katibu Mkuu Ndugu Samson Mwigamba anakwenda masomoni katika Chuo Kikuu cha Kenyatta.


Kabla ya uteuzi huu, Ndugu Juma Saanani alikuwa Naibu Katibu Mkuu wa Chama (Zanzibar).


2.Ilipitisha Mpango Mkakati wa Chama utakaongoza programu za chama kwa kipindi cha miaka mitano (2016-2020).


3.Aidha, kwa kuzingatia mamlaka yake kikatiba (Ibara ya 29 (25iv), Kiongozi wa Chama cha ACT-Wazalendo Ndugu Zitto Kabwe (MB) amemteua Ndugu Samson Mwigamba kuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama wa Chama na Kamati Kuu imekwisharidhia uteuzi huo.


Uteuzi huu umefanyika kwa kuzingatia kuwa Mwenyekiti wa Kamati halazimika kufanya kazi makao makuu na hivyo Ndugu Mwigamba ataendelea na masomo yake bila kikwazo.


Ado Shaibu

Katibu wa Itikadi, Uenezi na Mawasiliano kuwa Umma.

Jumanne, 26 Aprili 2016.

Rais Magufuli Aombwa Kuteketeza Meno ya Tembo yaliyohifadhiwa Ghalani

$
0
0

Wanahalakati wa Okoa Tembo wa Tanzania wamemshauri Rais John Magufuli kuteketeza shehena ya meno ya tembo yaliyohifadhiwa ghalani ili kuepuka gharama za uhifadhi na ulinzi.

Akizungumza leo jijini Dar es Salaam, mwenyekiti wa kampeni hiyo, Shubert Mwarabu amesema, endapo meno hayo yatauzwa yatachochea ujangili kwani itaibuka imani miongoni mwa watu kuwa meno hayo yana soko na faida.

"Taiwan na China ambao ni miongoni mwa wateja wakubwa wa meno hayo wamefunga biashara hiyo kwenye masoko ya ndani hivyo haina sababu kutafuta wateja bali yachomwe," alisema.

Mwarabu amesema ili kuthibitisha kuwa biashara hiyo ni haramu, serikali haina budi kuonesha mfano wa wazi kwa kuteketeza meno hayo.

Donald Trump Ashindwa Kutamka Jina la Tanzania..Ashutumiwa Kuwa na Ufahamu Mdogo wa Diplomasia ya Kimataifa

$
0
0
Mgombea wa urais kupitia chama cha Republican nchini Marekani ambaye amekuwa akiongoza kwenye kinyang’anyiro hicho, Donald Trump amejikuta akikosolewa vikali kuhusu upeo wake juu ya sera za nje pale aliposhindwa kulitamka bayana jina la Tanzania.

Drump ambaye Jumanne aliyopita alivuna ushindi wa kishindo kwenye majimbo yote manne yaliyopiga kura za mchujo alijikuta akitumbukia kwenye kadhia hiyo wakati akielezea vipaumbele vya Marekani kuelekea mataifa ya kigeni.

Alikuwa akigusia juu ya mashambulizi ya mabomu yaliyotokea katika ubalozi wa Marekani nchini Tanzania na Kenya na kusababisha uharibifu mkubwa wa mali huku watu kadhaa wakipoteza maisha.

Akiwa katika hali ya kujiamini, Trump alisema kuwa iwapo ataingia madarakani moja ya vipaumbele vyake ni kuendelea kutetea masilahi ya Marekani na kudhihirisha hilo aliamua kutolea mfano mashambulizi hayo ya kigaidi.

Lakini wakati akilitaja jina la Tanzania, mfanyabiashara huyo alijikuta akigusa hisia za wengi pale alipolitaja jina hilo kinyume na inavyotamkwa. “ Ona mashambulizi yaliyotokea katika miaka ya 1990 katika ubalozi wetu nchini Tan-ZAY-nee-uh”.

Matamshi hayo yalizusha mjadala mkubwa huku baadhi ya wakosoaji wake wakiingia kwenye mitandao ya kijamii na kuanza kumuelezea kama ni mtu asiyekuwa na upeo mkubwa kuhusu siasa za kimataifa.

Baadae kambi ya kampeni ya Trump ilitoa taarifa kwa vyombo vya habari ikisema kuwa kuteleza kwa mgombea wao katika matamshi ya jina halisi la Tanzania hakumaanishi kuwa uwezo wake kuhusu masuala ya usalama,diplomasia ya kimataifa na biashara ya kimataifa ni wa kutiliwa mashaka.

SOMA Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya April 29, Ikiwemo ya Magufuli Amtumbua Aliyesusa Mil 180

$
0
0

SOMA Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya April 29

Ni kweli Diamond na Zari Wanataka Kuachana? Ni kweli Diamond Kahamishia Majeshi kwa Mrembo Lyn?

$
0
0
Kinachoendelea sahizi instagram ni Mtifuano na ukorochoaji wa Maisha ya watu! Watu wapo busy,watu wapo katika pirika pirika za kutafuta ukweli kujua nini kinacho endelea kati ya Zari na Diamond na Diamond na Video queen wa Kwetu' Mama Diamond na mkwe wake na mawifi mtu!

Kama unavojua wabongo Umbea una nguvu kuliko Ripoti ya CAG insta kumechafuka.....Mama Diamond alianza kwa kufuta picha zote alizo post za Zari watu wakasema Mmmmmmmmh kuna kitu hapa,(mimi sidhani kama kufuta picha za mtu ni kitu kibaya lakini hakufuta za zari tuu mbona hata za wengine alifuta akaacha za Tiffa na Rommy tuu)

Wafuatiliaji wa mambo hawakuishia hapo wakasema Esma dada wa Diamond Ka muunfollow Zari (sina uhakika lakini Kwa usawahili wa huyu Dada nilishangaa kuona anapatana na Zari huyu ni mswahili mno na Diamond asipo kuwa Makini atamponza kwa uswahili wake)

Watu wakaendelea na story kwanini Zari hakutoa shout out kwa wimbo wa Raymond video ya Kwetu wakaguna wakasemaaa mmmmmmmmh hapa kuna kitu huenda Diamond anatoka na yule video queen wa hio video(Sioni tatizo tukumbuke Video ilitoka wakiwa bsy ulaya hata Mama Dai naye hajatoa Shout out kwenye video na hata picha alio post kuhusu hio video hamna)

Wafuatiliaji wa Mambo wakasema ishu ilianza kutokea world tour kuwa wakati wa kurudi kila mtu alipita njia yake Mama Diamond na Zari (mimi sioni Tatizo as long as Zari anaishi South Africa huenda alichukua ndege moja kwa moja hadi South na Mama Dai akaja bongo)

Juzi juzi hapa Dai na Zari wamepost picha zao wakionesha they are happy na mahusiano yao so Sidhani kama kuna kitu hicho ingawa leo bado hawajapost chochote

Kimbembe ni pale Mama Dai alipo like picha ya Video queen(anaesadikika kutoka na Dai)


Watu wakaendelea kupagawa na kuona kama yasemwayo yanaukweli baada ya video queen kupost picha hizi (Lakini ameshazifuta ila wajanja waliwahi)


MTAZAMO:
Kama Dai atakuwa kweli kaamua kuachana na Zari (Sidhani kama kitatokea) na kuja Kutoka na Video queen kwanza atakuwa amejishushia heshima yake hata kama Mama Dai ndo anampenda huyo video queen!, pili Dai atakufa Maskini maana wabongo huyo video queen atahamishia hadi ukoo wake pale white house sasa itakuwa bila bila Dai yupo na kijiji chake na huyu yupo na Kijiji chake!

Kingine ni kuwa Dai akae na dada zake na Mama ake awambie wapunguze uswahili kwa Zari! Utakuja kumponza Esma ni mswahili sana bora hata Halima! Esma yake yanamshinda anataka kuvuruga ya watu,pia Mama ake hata kama Insta kaikutia ukubwani Apunguze uswahili mwanae ashakuwa super star,yeye atulie afaidi matunda basi uswahili wakumuamlia atoke na nani ni ujinga na atampotezea mwanae Heshima!

Pamoja na kuwa zari ni mvumilivu namshauri Dai apunguze watu wakukaa nae Nyumbani kwake ana nyumba nyingi sio kila mtu lazima akae nae hata kama huruma sasa zinazidi! Ile ni nyumba yake na mke wake ndo maana ya mke,mama mkwe awe na nyumba yake,dada zake pia na ndugu wengine zari atakuwa anakosa uhuru ajifunze mbna Zari haleti ndugu zake! Ndoa ni kitu nyeti sana!

Napinga kwa asilimia 80% kuwa Dai anatka kumtosa Zari kwenda kwa video queen mtoto! Lakini ngoja tuone hii ngoma itaishia wapi

Reality Tv show ya Daimond huenda ikawa inatafutiwa Kiki kwa njia hii,mama Dai wabongo asha wajua kuwa akitoa Show yake hyo itauza maana wengi wanapenda umbea so huenda ni kiki

Mchezo huu hauhitaji hasira

Imeandikwa na Danya

TID Afunguka 'Nilikuwa Natoka na Wema Sepetu Alafu Akaniambia Hanitaki..Sasa Hivi Akitaka Kurudi Hakuna Nafasi Tena'

$
0
0
Akiwa Katika Kipindi cha Clouds 360 leo Mwanamuziki TID Amefunguka Kuhusu Kutoka na Wema Sepetu...

"Nilikuwa "namdate" Wema Sepetu akaniambia Sikutaakiiii....tangu kipindi hicho nimekuwa na Wasichana wengi...Ikitokea Wema Sepetu anataka kurudi hakuna nafasi Tena"I'm occupied".

Pia TID Amemuongelea Mwanamuziki Ommy Dimpoz na kusema kuwa yeye ndio aliyemtoa
 "Alikuja studio kwangu akiwa anavaa ndala na kupitia kwangu alijuana na watu muhimu kama Ali Kiba na Ruge Mutahaba". Anasema pia yeye anapenda na ni bora afanye video zake hapahapa Tanzania ili kuitangaza nchi yetu na vivutio vyake zaidi.

Mh Mbunge Sugu Amnunulia Mpenzi Wake Gari Mpya Aina ya Lexus..Yazua Gumzo Mtandaoni

$
0
0
Ripoti kutoka mitandaoni zinasema kuwa Muheshimiwa Mbunge Sugu Amemzawadia Gari aiana ya Toyota Lexus kama zawadi ya siku ya kuzaliwa kwa mpenzi wake ajulikanae kama Happiness, Sugu na mpenzi wake huyo mpya wamekuwa gumzo mitandaoni hasa baada ya aliyekuwa mpenzi wa Sugu wa zamani Faiza Ally kusema bado anampenda Sugu....Wadau wengi tunasubiri kuona Faiza atasema nini kuhusu hilo kwani amekuwa sio mvumilivu wa kukaa kimya kinapokuja suala la Sugu

Hizi Hapa ni Baadhi ya Comments kutoka kwa wadau mitandaoni:

mrs_j6316 @mwakobadoris :njoo umuone Mrs sugu au first lady was Mbeya yetu mpaka raha wallah afu ametulia hadi uso

full_mikuki :Maskini bahati hizi wengine acha tuzae tu

fine_mushy: Tenaaaaaa sio Harrier bubu Maana Kuna Harrier Kma Harrier mamaeeeee kitu LEXUS hiooooo

official_chagga_girl: Kuna watu wanakufaa ukoo,haaa haaa @tit4tati




Viewing all 104789 articles
Browse latest View live




Latest Images