Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live

Chief Kiumbe Akinipa Ndinga Sikatai-Young Killer

$
0
0
Young Killer alisema haya kupitia kipindi cha eNEWS na kusema kuwa yeye kuwataja madoni kwenye wimbo wake haina maana kuwa amewashawishi ili wampe kitu, bali amefanya hivyo kwa mapenzi yake mwenyewe na kudai hata kama ikitokea kweli akapewa ndiga haiwezi kukataa.

Mbali na hilo Young Killer amesema kuwa moja ya sababu kubwa kuwataja majina watu hao ni kwasababu wamemsaidia kimawazo, kwa kipindi ambacho alikuwa kimya hivyo amefanya hivyo kama kuwakumbuka na kuweka kumbukumbuka kwa kile walichomsaidia.

Lulu Michael Awapa Makavu Mastaa Wapenda Kiki

$
0
0
STAA wa sinema za Kibongo, Elizabeth Michael ‘Lulu’ amefunguka kuwa mastaa wengi wanapenda kiki kuliko kusaka fedha kitu ambacho yeye hakifanyi.

Akizungumza na gazeti hili, pasipo kuwataja majina, Lulu alisema anashangazwa na tabia ya mastaa wengi kuwa ‘bize’ kutafuta kiki kwenye mitandao mbalimbali ya kijamii badala ya kukutana pamoja na kufikiria ni kitu gani wanaweza kufanya ili waendelee kimaisha.

“Jamani mimi nashangaa siku hizi huku mjini mastaa wanatafuta kiki sana kuliko kufikiria mbinu ya kusaka hela yaani ni shida kabisa, tubadilike jamani, muda unakwenda,” alisema Lulu.

Kiba Apata Mpenzi Mwingine, Asema: Nikimrudia Jokate Nisutwe

$
0
0
Siku chache baada ya kusaini mkataba wa kimataifa na Kampuni ya Sony, Staa wa Bongo Fleva, Ali Saleh Kiba ‘King Kiba’ amedaiwa kufunguka kuwa, kamwe hawezi kurudiana na aliyekuwa mpenzi wake na akifanya hivyo asutwe mchana kweupe.
kiba na jokateeKiba na Jokate.

TUJIUNGE NA CHANZO
Chanzo makini ambacho kipo karibu na msanii huyo kimeeleza kuwa, staa huyo amegundua alipotea njia kwenye penzi la Jokate hivyo hana sababu ya kurudi nyuma kwani huu ndiyo wakati wake wa kufanya mambo makubwa.
“Jamaa tangu asaini mkataba mpya na Sony, hataki kuutia doa. Amesema anataka kutusua kimataifa zaidi hivyo anaona akirudi kwa Jokate ni kama atakuwa amerudi alikotoka kisanii.
“Unajua amejifunza mambo mengi kipindi yupo na Jokate, hataki tena kurudi kule kwani kusaini kwake mkataba mkubwa anataka kuendane na maisha yake binafsi,” kilisema chanzo chetu.
jokate12Jokate Kidoti ‘Jojo’

CHANZO CHAZIDI KUTIRIRIKA
Kama hiyo haitoshi, chanzo hicho kilizidi kutiririka kuwa, mbali na kula mkataba mnono, Kiba tayari amempata mpenzi mpya ambaye wanaendana kwa kila kitu hivyo anaona ni wakati mzuri wa kufaidi maisha ya uhusiano sambamba na maisha yake kimuziki.
“Ni mtoto f’lani mwenye maadili. Kama unavyojua Kiba ni mtoto wa Kiislamu, safari hii ameona achukue binti mwenye imani kama yake ili aweze kufika mbali maana japo hana mpango wa ndoa kwa sasa lakini anataka mtu ambaye ataishi naye kwa muda mrefu,” kilisema chanzo hicho.

KUFANYA MAMBO MAKUBWA
Chanzo hicho kilizidi kuweka bayana kuwa, Kiba ameapa kufanya mambo makubwa kwani amepata uongozi mzuri ambao unajua kuongoza wasanii na kuwaunganisha na televisheni za kimataifa.
“Kiba kwa sasa ngoma yake inachezwa kimataifa, juzikati kupitia televisheni ya Sound City Africa ambayo makao makuu yapo Nigeria, walitoa saa 12 kwa ajili ya Kiba, wakaiita Ali KibaDay, hapo zilichezwa nyimbo zake tu, ni nafasi kubwa sana ya kujitangaza, imempa connection nyingi za kimataifa,” kilisema chanzo hicho.

DIAMOND ATASUBIRI SANA
Chanzo hicho kilizidi kummwagia sifa Kiba kuwa kutokana na uwezo, uongozi na mkatapa huo mpya, sasa hivi  Diamond atasubiri sana kwani levo zake zitakuwa za mbali.
“Aaah! Diamond atasubiri sana. Kiba anabebwa na vingi kwa sasa, uongozi mzuri na anajua kuimba kuliko huyo Diamond. Ataisoma namba kama unavyosikia wimbo wa Aje ndani ya muda mfupi tu, tayari umekamata,” kilisema chanzo hicho.

MENEJA AFUNGUKA
Baada ya kushibishwa ubuyu huo, mwanahabari wetu alimvutia waya mmoja wa mameneja wa msanii huyo ambaye hapendi jina lake lichorwe gazetini kwa kile alichodai si mambo ya muziki aliyoulizwa, lakini akaweka bayana kuwa kweli Kiba hayupo tayari kurudiana na Jokate kwani ana mtu wake mpya.
“Hawezi kumrudia, sijui hata amemchukia nini yule mrembo (Jokate). Jamaa kwa sasa ana kifaa kipya lakini hapendi kukiweka wazi. Si unajua naye alivyo mtu wa sirisiri,” alisema meneja huyo.

KIBA ANASEMAJE?
Risasi Jumamosi lilimtafuta Kiba ili kuweza kumsikia anazungumziaje juu ya mrembo huyo na kama kweli hana mpango wa kurudi nyuma hadi kufikia hatua ya kutamka kuwa asutwe kuliko kurudina na mrembo huyo, Kiba alijibu kwa kifupi:
“Haya ni mambo yangu binafsi. Sipendi sana kuyazungumzia. Kifupi wewe elewa kwa sasa siwezi kurudi nyuma, nipo kwenye hatua nyingine za kimaendeleo na namshukuru Mungu nakubalika.”

YA AWALI
Miaka miwili iliyopita, Kiba na Jokate wamekuwa habari kwenye vyombo vya habari wakidaiwa kuwa wapenzi licha ya kwamba, mara nyingie alikuwa akikanusha huku mwenzake akiwema wazi.
Hata hivyo, maisha yao ya kimapenzi yamekuwa yakitawaliwa na mlolongo wa kumwagana na kurudiana.
Kuna wakati ilidaiwa Jokate alinasa mimba ya Kiba lakini baadaye ikasemekana kuchoropoka.
Maneno mengi yalisemwa kuwa,  hakuna tumaini la mbele katika uhusiano wao kwa vile, Jokate ni Mkristo, Kiba Muislam huku familia ya mrembo huyo ikitajwa kutokuwa tayari binti yao kuingia kwenye ndoa na mwanaume wa imani tofauti.
Kumwagana kwa safari hii na Kiba kupata kifaa kingine kunahitimisha ‘kapo’ yao iliyodumu kwa miaka mitatu sasa.

Ndalichako: Wanaodaiwa na HESLB tutaweka majina yao magazetini kuwashikiza kulipa

$
0
0
Waziri wa elimu Joyce Ndalichako amesema wana mpango wa kuweka majina ya wadaiwa na bodi ya mikopo kwenye magazeti ili kuwashinikiza walipe, amewaasa wadaiwa wakiwapo wabunge walipe ili majina yao yasiwekwe.

VIDEO: Mtumbwi Kigamboni Dar es salaam Wasababisha Vifo

$
0
0
Habari za ajali ya kuzama kwa mtumbwi ambao ulikuwa unatumika kuwavusha watu kutoka upande wa soko kuu feri na kuelekea Kigamboni zilianza kuenea May 27 2016 ambapo Mtumbwi huo unasadikika kubeba watu zaidi ya 16 ambao baadhi yao wametoka wazima na watano wameripotiwa  kufa.

Ayo TV imezungumza na  Mratibu msaidizi wa Jeshi la Zimamoto, Bashir Mazehebi ambaye amezungumza haya …………….’>>>’chombo kilichopata ajali ni Boti za fiber ambazo zinatumika mara kwa mara pale Kigamboni kunapokuwa na msongamano wa watu kuna biashara ya kuvusha watu huwa inafanyiaka, jana kulikuwa na msongamano wa watu pale hatimaye baadhi ya watu waliamua kupanda chombo hicho ambacho sio rasmi’

UNAWEZA KUANGALIA VIDEO HII:

SOMA Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumapili ya May 29, Ikiwemo ya Magufuli Kutokuwa na Rafiki

$
0
0
SOMA Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumapili ya May 29, Ikiwemo ya Magufuli Kutokuwa na Rafiki

Zitto Kabwe Avunja Jungu: Nusu ya Walimu Wanalipwa Mishahara ya Bure, Hawafundishi

$
0
0
Baada ya Hussein Bashe kusema ni watu waliofeli, Zitto Kabwe nae amesema nusu ya walimu hawafanyi kazi na ndio 'watumishi hewa haswa'

Ameongezea pia utafiti uliofanyika na Benki ya Dunia na REPOA ukitembelea ghafla kwenye shule za umma utakuta walimu hawapo shuleni

Mtazame Hapa:

KIMENUKA Wanafunzi 7,000 Watimuliwa UDOM

$
0
0
Chuo Kikuu cha Dodoma (Udom) kimewasimamisha masomo zaidi ya wanafunzi 7,000 wa kozi maalumu ya ualimu wa sayansi kwa ngazi ya stashahada na kuwataka waondoke chuoni hapo mara moja.

Jana, lilitolewa tangazo chuoni hapo likiwataka wanafunzi hao kuondoka kati ya jana hadi leo saa 12 jioni. Tangazo hilo lilieleza kuwa kutokana na matatizo yaliyopo katika ufundishaji wa stashahada hiyo, Serikali kupitia Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi imeamua wanafunzi hao kurejea majumbani na wataelezwa mustakabali wao “mapema iwezekanavyo”.

Makamu Mkuu wa chuo hicho, Profesa Idrisa Kikula alipotakiwa kufafanua suala hilo, alisema kwa ufupi kuwa suala hilo lipo lakini akaelekeza apigiwe simu Ofisa Uhusiano wa chuo hicho, Beatrice Baltazal kwa maelezo zaidi.

Baltazal alipotafutwa alisema kusimamishwa kwa wanafunzi hao kulitokana na agizo la Serikali na wametakiwa kulitekeleza.

Kuhusu lini na nini hatima ya wanafunzi hao, alisema bado hawajui hadi hapo watakapoelekezwa vinginevyo.

Hata hivyo, kulikuwa na malalamiko kwa wanafunzi hao juu ya namna walivyopewa taarifa za kusimamishwa masomo yao kwa ghafla na kutakiwa kuondoka.

Kozi ya stashahada ya ualimu wa sayansi, ilianzishwa maalumu kwa agizo la Rais Jakaya Kikwete kwa lengo la kuziba pengo la walimu wa sayansi na ilikuwa inatolewa UDOM pekee.

Waliokuwa na sifa za kujiunga na kupewa mikopo ni wanafunzi waliomaliza kidato cha nne na kufaulu vizuri masomo ya sayansi.

Wanafunzi hao waliokuwa wamekopeshwa na Serikali wamesimamishwa siku mbili baada ya wenzao zaidi ya 480 wa Chuo Kikuu cha St. Joseph kusimamishwa baada ya kubainika hawakuwa na sifa za kudahiliwa.

Maalim Seif Atikisa Zanzibar, Mabomu Yarindima Kuwatawanya Wafuasi Wake

$
0
0
Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad jana aliitikisa Zanzibar pale alipoanza ziara yake ya siku sita katika Wilaya ya Kaskazini A na kusababisha polisi kuwatawanya wafuasi wake kwa mabomu na risasi huku baadhi wakijeruhiwa.

Wakati wa ziara hiyo, shughuli za biashara zilisimama kwa muda ili kupisha ziara ya Maalim Seif na mamia ya wananchi wake kwa waume walimpokea na kumfuata kila alipoelekea.

Ulinzi uliimarishwa katika maeneo yote ya Mkoa wa Kaskazini Unguja, wakati wote wa ziara hiyo na vikosi vya ulinzi na usalama vilionekana vikipiga doria kila mahali.

Akiwa Kinyasini, Jimbo la Chaani ambako alifanya kikao cha ndani, wakazi wa eneo la Kivunge kwa mamia walianza kujikusanya katika maeneo ambako Maalim Seif alitarajiwa kutembelea huku wakijipanga barabarani kumsubiri kiongozi huyo. Hata hivyo, askari wenye silaha waliwatawanya.

Katika kuwatawanya, polisi walitumia mabomu ya machozi na risasi hali iliyosababisha kizaazaa kwa takriban dakika 30 katika eneo la Kivunge kabla ya kurudi hali ya kawaida.

Baada ya hapo baadhi ya askari waliokuwa na silaha waliwazuia waandishi kusogelea eneo hilo wala kuwapiga picha majeruhi.

Mkazi wa Kivunge ambaye alidai ni miongoni mwa watu waliopatwa na mkasa huo, Omari Makame (32) alisema, “Sisi tumejipanga kwa heshima zote kumsubiri kiongozi wetu kipenzi cha Wazanzibari, tukiimba kwa furaha lakini ghafla tumepata kipigo na mabomu ya machozi, nini hiki kama siyo chuki na choyo kibaya.”

Mkazi mwingine, Haji Omar (27) alisema hata baada ya kuwajeruhi wenzao, polisi wali wakatalia kuwapa fomu za kwenda kupata matibabu na hata walipopelekwa hospitali ya Kivunge, polisi walifika na kuwachukua kwa nguvu.

“Wamekataa ushauri wa madaktari wa hapa kwamba wawapeleke Hospitali ya Rufaa ya Mnazi mmoja, lakini wamewachukua kwa nguvu wamekwenda nao Kituo cha Polisi Mkokotoni,” alisema Omar.

Naibu Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai Zanzibar, Salum Msangi alikiri kuwapo kwa tukio hilo akibainisha kuwa yote hayo yanatokea kwa sababu kuna watu hawataki kufuata sheria, lakini akasema Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kaskazini Unguja, Hassina Tawfik ndiye mwenye nafasi ya kufafanua zaidi.

Juhudi za kumpata Tawfik hazikufanikiwa ikielezwa na baadhi ya watendaji wa ofisi yake kuwa bosi wao hapatikani na hawakuwa na mawasiliano na yeye.

Mkurugenzi wa Haki za Binaadamu wa CUF, Pavu Juma Abdalla alifika katika Makao Makuu ya Polisi Mkoa wa Kaskazini Unguja na kushuhudia majeruhi hao wakiwa mikononi mwa polisi.

Waliojeruhiwa ni Makame Abdalla Makame (28), mkazi wa Kivunge Bondeni na Shaame Juma Haji (45) mkazi wa Tumbatu Chwaka.

“Tunapigwa kwa sababu ya umma kuonyesha mapenzi kwa Maalim Seif, wangelikuja watu wa vyama vingine wasingelipigwa lakini ipo siku hawa jamaa wataheshimu haki zetu,” alisema mtu aliyejitambulisha kwa jina moja la Haji akisema baadhi ya majeruhi ni ndugu zake.

Mkurugenzi wa Habari wa CUF, Salim Bimani ambaye alifika hospitali kuwaona majeruhi alisema:“Wenye mabomu na risasi wamewahujumu watu bure kwa sababu za chuki lakini yote hayo yana mwisho.”.

Bimani alisema Chama chake kinalaani kwa nguvu zote uonevu na hujuma hizo walizo tendewa wananchi wasiokuwa na hatia.

“Tunatumia pia kumbukumbu za hujuma hizi za leo kuongeza ushahidi wa kesi yetu tutakaouwasilisha ICC,” alisema Bimani.

Ziara yenyewe
Maalim Seif alianza ziara hiyo ya kwanza Unguja tangu kumalizika kwa uchaguzi wa marudio aliosusa kushiriki katika eneo la Kinyasini, Chaani na kupokewa na mamia ya wafuasi wake ambao walikuwa wakiimba “rais! rais! rais!

Aliambatana na viongozi na watendaji wa CUF, akiwamo Naibu Katibu Mkuu, Nassor Ahmed Mazrui; Bimani; Pavu Abdalla na Mkurugenzi wa Mipango na Chaguzi, Omar Ali Shehe.

Aliondoka Kinyansini kuelekea Gamba, Mkwajuni ambako mamia ya wananchi waliokuwa wakimshangilia walijipanga barabarani na walionekana kuongezeka kadri alivyoelekea Kaskazini na kukaribia Jimbo la Mkwajuni.

Baadaye Maalim Seif aliwahutubia wajumbe wa kamati mbalimbali za wilaya na majimbo akieleza kile alichosema ni mwelekeo wa kisiasa wa chama chake, Zanzibar na Tanzania kwa jumla.

Alisema dunia ilishuhudia ukiukwaji mkubwa wa haki na demokrasia visiwani humo, akidai kwamba pamoja na maonyo ya jamii mbalimbali za kitaifa na kimataifa, watawala waliamua kupora uamuzi wa mamlaka halali ya wananchi kupitia masanduku ya kura ya Oktoba 25, 2015.

“Angalieni watu hawa walivyokosa aibu, umma uliwakataa, mataifa yaliwakataa hata kuwanyima misaada lakini bado hawakuonyesha dalili za kujali kutokana na dhulma waliyotenda.

“Nasema hali hii haitupeleki pema sisi na Taifa kwa ujumla maana iliyoporwa ni haki ya umma na haiwezekani kuisamehe dhambi hii, hivyo mwishowe si mwema na dhuluma haiwezi kudumu kwa muda mrefu asilani, sasa kusema hivyo kuna ubaya gani?”

Hata hivyo, Mwangalizi Mkuu wa Ujumbe wa Waangalizi wa Uchaguzi wa Umoja wa Ulaya (EU – EOM) kwa Tanzania, Judith Sargentini amesema atawasilisha ripoti kamili na mapendekezo ya umoja huo, kuhusu Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 25, mwaka jana Alhamisi ijayo.

Maalim Seif aliwataka wananchi wote, kama walivyoikataa CCM kabla ya uchaguzi, wakati na baada ya kupiga kura Oktoba mwaka jana, kuunga mkono juhudi na mikakati ya CUF, ili kuhakikisha haki inapatikana, uamuzi wao unaheshimiwa, kwa masilahi ya nchi na Taifa kwa jumla.

Viongozi wa chama hicho Wilaya ya Kaskazini A, walimhakikishia Maalim Seif; “sisi tuko tayari kwa lolote, na naona siyo sisi pekee, kwa sasa kila mtu anaisoma namba, tutakuwa bega kwa bega mpaka haki yetu ipatikane,” alisema Makame Bakari, mmoja wa makatibu wa CUF.

Nape Nhauye: Namheshimu Sana Edward Lowassa

$
0
0
Waziri wa Habari mheshimiwa Nape amesema anamheshimu sana aliyekuwa mgombea wa uraisi kupitia Chadema, Edward Lowasa kwani kuna mambo mengi ameyajifunza kwake!

Source: Vichwa habari Magazetini.

We should learn that, politics is not flexible. Leo unasema hivi, kesho unakana ama kugeuza kile ulichosema jana!

Mambo Matatu yanayoipa Nguvu Lebo ya Wasafi Kufika Mbali

$
0
0
Hutakiwi kushangaa siku ukisikia lebo ya WCB inayomilikiwa na Diamond kuwa ipo juu zaidi ya Mavin Records inayomilikiwa na Don Jazzy, hiyo ni kutokada na mikakati pamoja na jitihada zinazozidi kuwekwa na uongozi wa lebo hiyo.

Mpaka sasa lebo ya WCB inawamiliki wasanii wanne akiwemo Diamond, Harmonize, Raymond na Q Boy Msafi huku kukiwa na taarifa za chini chini kuwa tayari Rich Mavoko ameshamwaga wino wa kuwa chini ya lebo hiyo huku bajeti yake ikiwa tayari imeshawekwa pembeni na tayari amesharekodi wimbo pamoja na video iliyofanyika huko Afrika Kusini. Lakini pia nje ya kutafuta vipaji kwenye hili analolifanya Diamond ni biashara kubwa ambayo itafanya akaunti zake za benki kujaa kila siku.

Hiki ndicho kitaweza kuipaisha lebo ya WCB kuwa kubwa zaidi.

Ukubwa wa jina la Diamond

Hili halina ubishi kwa sasa Diamond amekuwa ni miongoni mwa wasanii wenye majina makubwa kwenye tasnia ya muziki kwa Afrika kwa sasa. Hicho ni kitu ambacho kimemfanya kujitengenezea fan base kubwa kutokana na kazi zake anazofanya, lakini pia ana uwezo wa kuwatengenezea connection wasanii wa lebo yake [WCB] kufanya kazi na msanii yeyote wa Afrika endapo muda utaruhusu kutokana na jina lake huku yeye mwenyewe akizidi kujitafutia connection za Marekani na Ulaya kama walivyoanza kwa Harmonize kufanya kazi na Korede Bello kutoka Mavin Records lakini pia Harmonize aliwahi kusema ana kazi na Kiss Daniel wa Nigeria.

Mashabiki wanaomsupport Diamond

Diamond ni msanii mwenye washabiki wengi wanaomsupport ambao wapo tayari kupambana na lolote endapo wataona msanii wao anaandamwa na na maneno kutoka upande mwingine. Kutokana na hilo uongozi wa WCB unaweza kutumia pointi hiyo kuifanya lebo yao kuwa juu zaidi kama wanavyofanya sasa kwa Harmonize na Raymond kutembelea nyota ya Dangote.

Menejimenti ya WCB

Uongozi wa WCB ukiongozwa na Salaam pamoja na Babu Tale umefanikiwa kufaulu kwenye suala la mipango na kujiamini kwenye kila wanalolifanya na hawashindwi kujaribu. Kutokana na uwezo wao walionao wanaweza wakaifanya lebo ya WCB kufika mbali zaidi lakini itachukua muda mpaka kufika huko.

Source:Bongo5

Wema aweka wazi kuhusu mimba, alivyojigundua mpaka ilivyoharibika ‘nikaona donge la damu likidondoka’

$
0
0
Mashabiki wa malkia wa filamu, Wema Sepetu pamoja na wadau wa burudani walikuwa bado wanamaswali mengi kuhusu mimba ya Wema Sepetu huku wengine wakihisi labda zilikuwa ni kiki, lakini Jumamosi hii staa huyo amefunguka kinagaubaga kuhusu sakata hilo.

Akizungumza na gazeti la Mwanaspoti, Wema alikiri kwamba ni kweli alikuwa ni mjamzito.

“Nilikuwa na ujamzito kweli,” alisema Wema. “Mwezi wa 12 mwaka jana, nilikuwa najihisi kuongezeka uzito, hivyo nikaenda kwa daktari kwa lengo la kusafisha kizazi. Nilipofika kwa dokta nilimwambia hata hivyo nimemisi period, akaniambia ya Mungu mengi pengine nime-concive, nilimkatalia katakata.”

Wema anaendelea kwamba daktari alimshauri akanunue kipimo cha ujauzito ajipime haja ndogo atakapoamka asubuhi na asile kitu chochote kwa ajili ya zoezi la kusafisha kizazi.

“Nilipokuwa narudi nyumbani nilipitia dukani na kununua kipimo hicho na asubuhi nikafanya hivyo, nilishtuka sana, nilikuwa kama nimewehuka nilipoona mistari miwili katika kipimo, siku zote nilizoea kuona mstari mmoja. Nikawauliza rafiki zangu nikiwa katika hali ya furaha baadaye nikampigia daktari nikamwambia nimepima lakini sielewi ninachokiona maana kuna mistari miwili, aliniambia niende na kipimo hicho na akanihakikishia kwamba nilikuwa na ujauzito, sikutaka kumwamini, nikamtaka anipime, hapo ndipo nilipothibitisha, nilisema sasa watanikoma,” anasema.

Baada ya fuhara ya muda mchache akisubiria kupata mtoto, aliona dalili mbaya katika mwili wake.

“Siku ambayo sipendi kuikumbuka ni ile niliyokwenda msalani kwa ajili ya kujisaidia haja ndogo kisha nikaona donge la damu likidondoka, nilichanganyikiwa kwa kuwa daktari aliniambia sikutakiwa kuona damu. Nilipompigia mama yangu naye alinilaumu sana badala ya kunipa pole aliniambia, ‘Wema nilikuambia mimba haitangazwi!, unaona sasa kilichotokea, niliyajua madhara ya kufanya hivyo!”

Wema alisema alikwenda kwa daktari akiwa na Idris kuthibitisha ni kweli ujauzito ulikuwa umetoka na ulikuwa na wiki 13.

Wema anasema, daktari alimwambia ndugu yake mwingine aliyeambatana naye kwamba ujauzito huo ulikuwa ni wa watoto wawili, yaani pacha.

Source: Mwanaspoti

Benki ya Dunia yaionya Tanzania Kuhusu Kuitegemea China Kimisaada

$
0
0
Taarifa za hivi karibuni kutoka katika serikali ya China kuwa Tanzania itapewa kiasi kikubwa cha fedha cha dola bilioni 20 ambazo China imezitenga kwa ajili ya kuzisaidia nchi za Afrika kufanya mapinduzi ya kiuchumi, inaonyesha ushirikiano mkubwa uliopo kati ya nchi hizi mbili.

Benki ya Dunia imeonya kuwa, kuongezeka kwa ushirikiano wa kiuchumi baina ya Tanzania na China kunaweza kuathiriwa na kushindwa kukua kwa Beijing.

China ni moja kati ya wabia wakubwa wa biashara na Tanzania na hutoa fedha kwa ajili ya miradi ya maendeleo na pia imewekeza nchini. Mwaka 2014 inakaririwa kuwa thamani biashara ya Sino-Tanzania iliongezeka thamani hadi kufikia dola bilioni 2.6 kutoka kiwango kidogo kilichokuwepo mwaka 2000.

Katibu Mkuu katika Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji Adelhelm Meru, alisema Tanzania inatumia nafasi ya mapinduzi ya viwanda China kwa kuhakikisha uwekezaji unafanyika kwenye vitu vitakavyoisaidia nchi.

Aidha aliendelea kueleza kuwa ifikapo mwaka 2020 sekta ya viwanda itakuwa inachangia asilimia 15 ya pato la taifa.



Katika ripoti ya uchumi nchini Tanzania yenye jina, The Road Less Travelled: Unleashing Public-Private Partnerships in Tanzania, Benki ya Dunia ilibaini kuwa kwa miaka ya hivi karibuni uchumi wa China umekuwa ukikua kwa kasi ndogo. Hili ni onyo kwa Tanzania ambayo ushirika wake na Beijing umekuwa ukizidi kila iitwapo leo.

Fedha za China katika miradi ya maendeleo ya Tanzania zimezidi kuongozeka kila baada ya mwaka ikiwa ni pamoja na dola bilioni 1.2, 2013/14-2014/15 kwa ajili ya ujenzi wa bomba la gesi toka Mtwara hadi Dar es Salaam. Ripoti ya iwekezaji wa China nchini Tanzania imeongezeka maradufu, unakadiriwa kuwa na thamani ya dola milioni 60 kwa mwaka 2013

Kuyumba kwa uchumi wa China kuna weka katika mashaka uchumi wa Tanzania ambapo unategemea sana uwekezaji toka China. Benki ya Dunia ilieleza kuwa kuyumba kidogo kwa uchumi wa China kunaweza kutaiathiri tanzania moja kwa moja au vingine kupitia uwekezaji.

China imechaangia asilimia 10 ya bidhaa zote zinazotolewa nje ya nchi na ni nchi ya tatu kwa kuchukua bidhaa baada ya India na Afrika Kusini.

Chabzo: Swahili times

Wema Sepetu Achukua Pointi Tatu Kwa Kumuombea Kura za BET Awards Diamond

$
0
0
Inaonekana somo la uzalendo limewaingia vyema mastaa wetu licha ya tofauti zao. Baada ya hivi karibuni Alikiba kuwaomba watanzania wampigie kura Diamond anayewania tuzo za BET, Wema Sepetu naye amefanya hivyo.

Wema ametumia Instagram kuwaambia mashabiki wake wampigie kura ex wake huyo aliyetajwa kuwania kipengele cha Best International Act: Africa.

“Uzalendo ndo unaotakiwa… Tanzania Kwanza Vingine Baadae… Ama nene…? Vote Vote Vote….,” ameandika Wema kwenye picha ya BET Awards aliyoiweka Instagram.

Mashabiki wengi wamempongeza kwa uzalendo huo aliounesha licha ya yeye na Diamond kuwa mbali kwa sasa kutokana na kila mmoja kuwa na maisha yake. Wema na mpenzi wa sasa wa Diamond ni paka na panya.

Diamond anachuana na mastaa wengine wa Afrika wakiwemo Wizkid, Yemi Alade, AKA, Cassper Nyovest na wengine wawili.

Hii ni mara ya pili kwa muimbaji huyo wa Make Me Sing kutajwa kuwania tuzo hizo kubwa duniani.

Takriban 17 Wafariki Kwenye Ajali ya Moto Ukrain

$
0
0
Takriban watu 17 wanahofiwa kufariki baada ya moto mkubwa kutokea katika jumba moja la makaazi ya kuwahudumia wakongwe, karibu na mji mkuu wa Ukraine, Kiev.

Wakuu wanasema kuwa idara ya huduma za kuwaokoa watu ilifaulu kuwaokoa watu wengine 17, watano kati yao wamekimbizwa Hospitalini, wakiwa na majeraha mabaya ya moto.

Taarifa kutoka huduma ya zima moto mjini humo, zinasema kuwa moto huo ulitokea mapema leo Jumapili, katika jumba moja la kibinafsi lililoko karibu na makao hayo, ambayo yalikuwa yakiwahudumia kwa muda watu 35, kutoka katika kijiji kimoja kilichoko hapo karibu.

Basi Jingine la Mwendo kasi Lapata ajali Eneo la Magomeni Usalama

$
0
0
Basi jingine la mwendo kasi limepata ajali mabaya eneo la Magomeni Usalama. Ni baada ya gari dogo kukatisha kwenye barabara ya magari ya mwendo kasi.


Advertisement

Muhongo Aitumbua Kampuni Iliyoingiza Mafuta FEKI Nchini

$
0
0
SERIKALI imemsimamisha msambazaji wa mafuta Kampuni ya Sahara Energy Resourses Limited ya Nigeria aliyeingiza mafuta ya ndege (JET A1) yaliyochafuka na kumtaka kusafisha matangi pamoja na mabomba ya mafuta ya kampuni zilizopokea mafuta hayo.

Aidha, imeelezwa pamoja na kutokea kwa tatizo hilo la kuchafuka kwa mafuta hayo nchi haitaingia katika ukosefu wa nishati hiyo muhimu kwa kuwa kuna akiba ya kutosha kwa siku 14 na tayari kampuni ya Puma imeagiza mafuta ambayo yataingia nchini Juni 7, mwaka huu.

Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo alitoa kauli hiyo jana wakati alipotembea kampuni za mafuta zilizopokea mafuta yaliyochafuka kwa kuchanganyika na petroli jijini Dar es Salaam ili kubaini ukweli wa uhaba wa mafuta ya ndege.

Profesa Muhongo aliiagiza kampuni hiyo ya Sahara Energy Resources Limited ya Nigeria kuhakikisha inasafisha matangi pamoja na mabomba ya mafuta kuanzia leo na kama haitatekeleza hilo itakuwa ni mwisho kufanya kazi nchini.

“Msafishe haya matenki pamoja na mabomba yote kwa gharama zenu. Haya ni maagizo sisi hatuwezi kuendelea kusubiri, hamuwezi mkasababisha nchi ikawa na uhaba wa mafuta kwa majadiliano yenu ambayo hayana mwisho.

“Usafishaji unatakiwa kuanza kesho, kama hautafanyika kuanzia hiyo kesho, basi Sahara isahau kufanya biashara katika nchi hii. Na sio hilo tu hata tenda (zabuni) alizokuwa amepata nazo tutazifuta,” alisema Profesa Muhongo.

Alisema kuwa kampuni hiyo haitakiwi kupewa zabuni nyingine hadi hapo uchunguzi utakapokamilika wa kubaini ukweli wa mafuta hayo kuchafuka kwa kuchanganyika na petroli.

Profesa Muhongo alisema hatua walizochukua ya kwanza ni kumsimamisha kujihusisha na zabuni yoyote itakayotangazwa kuanzia sasa lakini pia kutakiwa kusafisha matangi na mabomba hayo.

Aliongeza kuwa hii ni mara ya pili kwa kampuni hiyo mafuta yake kuwa na tatizo kwani mara ya kwanza mafuta yake yalibainika kuwa machafu akarudishwa nayo.

Awali mwakilishi wa kampuni hiyo ambaye yuko hapa nchini alisema, hawana sehemu ya kuhifadhi mafuta hayo ambayo yamechafuka hivyo wanasubiri meli yao irudi ili waweze kuyaondoa mafuta.

Hata hivyo, kampuni ya kuhifadhi mafuta nchini ya Tanzania International Petroleum Reserves Limited (TIPER) ilimhakikishia Profesa Muhongo kuwa wana nafasi ya kuhifadhi mafuta yote yaliyochafuka, hatua ambayo waziri huyo aliiagiza kampuni hiyo kuhifadhi mafuta hayo katika matangi ya TIPER badala ya kusubiri meli.

“Hilo linatuchelewesha TIPER wameshakubali wana nafasi ya kuhifadhi hayo mafuta, kwa hiyo yahifadhi hapa ili msafishe hayo matenki, ili mafuta yatakayokuja yakute matenki ni masafi,” alisema.

Aidha, alisisitiza kuwa taifa haliwezi kuingia kwenye uhaba wa mafuta ya ndege na yapo ya kutosha siku 14 kwani kampuni ya Puma tayari imeshaomba mafuta kutoka katika kampuni za Total na SP ya Rwanda.

Pia meli ya Puma itaingia nchini Juni 7 na meli nyingine itaingia Juni 13.

Awali akizungumzia hali hiyo, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Wakala wa Uagizaji Mafuta kwa Pamoja, Michael Mjinja alisema, meli hiyo iliingia nchini Mei 5, mwaka huu na mafuta hayo yalithibitishwa kuwa na ubora na Shirika la Viwango nchini (TBS).

Alisema baada ya mafuta hayo kushushwa ilibainika kuwa yamechafuliwa hatua iliyowafanya kumuagiza aliyeleta mafuta hayo kuyaondoa.

Naye Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) Felix Ngamlagosi alisema, kwa sasa kuna mafuta ya kutosha kwa siku 14 lakini kuna hatua nyingine zinazochukuliwa ili kuhakikisha hakuna uhaba wa mafuta utakaotokea.

 “Hayo yaliyochanganyika kuna hatua zinazochukuliwa ikiwa ni pamoja na kuchukua sampuli za pamoja na sisi ni wasimamizi ili kuhakikisha zinapelekwa maabara na kujua kitu gani kilitokea,” alisema.

Profesa Muhongo alizitembelea kampuni hizo ambazo ni Puma Energy, Gapco Tanzania Ltd, Oilcom, ORXY Energies na TIPER. Meneja wa Huduma za Usafiri wa Anga wa Oilcom, Haruna Magota alimwambia Waziri Muhongo kuwa, mafuta waliyopokea yalikuwa ni lita milioni 8.8 na wao walikuwa na lita milioni 2.6, ambapo mafuta hayo yote yameharibika.

Alisema ukosefu wa mafuta hayo umekuwa ni tatizo kwa wateja wao ambao ni mashirika ya ndege kwani jumla ya lita milioni 10.8 yote yamechafuka.

Aidha aliongeza kuwa wakaguzi wa meli walishawahi kutoa onyo kwa kampuni hiyo kuwa meli zake hazina viwango vinavyotakiwa vya kubeba nishati hiyo.

Aidha kampuni za kuagiza mafuta nchini zilitaka kampuni ya Sahara Energy Resources Ltd ya nchini Nigeria kuweka hadharani uthibitisho wa kuhujumiwa kuhusiana na kashfa ya uingizaji mafuta ya ndege machafu hapa nchini inayolikabili shirika hilo.

Kwa mujibu wa taarifa ya Chama cha Waagizaji Wakubwa wa Mafuta ya Petroli nchini (TAOMAC) iliyosambazwa kwenye vyombo vya habari jijini Dar es Salaam juzi, waagizaji hao waliitaka kampuni hiyo kutaja jina la kampuni au mhusika yeyote anayeaminika kuihujumu kampuni hiyo kama ambavyo imenukuliwa na vyombo vya habari nchini ikijitetea kupinga kashfa hiyo.

“Tunawaomba wenzetu hawa wahakikishe wanakabidhi jina la kampuni au mtu yeyote wanayemshuku kuwa anahusika na kashfa inayowakabili kwa Jeshi la Polisi au chombo chochote cha usalama nchini vinginevyo sisi tutaamini kuwa utetezi wao ni uwongo na unalenga kutafuta njia ya kutokea,’’ alisema Mkurugenzi Mtendaji wa TAOMAC, Salum Bisarara kupitia taarifa hiyo.

Sakata la kuingizwa kwa mafuta machafu ya ndege aina ya Jet A1 na hofu ya kukosekana kwa mafuta hayo nchini liliibuliwa na Mbunge wa Kigoma Mjini (ACT-Wazalendo), Zitto Kabwe wakati akichangia hotuba ya bajeti ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017, alisema mafuta hayo yatakosekana kutokana na kampuni moja ya kigeni iliyopewa zabuni kuagiza mafuta hayo, kuingiza mafuta ambayo hayawezi kutumiwa na ndege.

Waziri Mkuu Mstaafu Fredrick Sumaye Akerwa na Ving'ang'anizi wa Madaraka

$
0
0
WAZIRI Mkuu Mstaafu, Fredrick Sumaye amezitaka nchi za Afrika kuhakikisha zinakubali kubadilishana madaraka pale chama kimoja kinaposhindwa kuongoza ili kuepusha nchi kuingia kwenye machafuko.

Aidha, Sumaye alisema ni vyema wataalam wakaongoza nchi kwa kubuni mbinu mbalimbali za kujikwamua kiuchumi.

Sumaye aliyasema hayo jana Jijini hapa wakati akizungumza kwenye kongamano la Nafasi ya Wasomi na Wafanyabiashara Katika Kujenga na Kukuza Uchumi wa Nchi, lililoshorikisha viongozi wa vyama, wafanyabiashara na wasomi wa kada mbalimbali wa Arusha.

Sumaye alisema uongozi ni kubadilishana nafasi na katika nchi za Ulaya kwa mfano, chama kikishindwa kutawala kinakubali lakini kwa nchi za Afrika kuna uroho wa madaraka au ubinafsi.

"Tunataka kuwajengea uwezo wasomi wetu kwa kujiamini na kujipatia fursa za kujikwamua kiuchumi," alisema Sumaye ambaye alikuwa Waziri Mkuu kwa miaka 10 mfululizo kati ya 1995-2005, kwa mara ya kwanza katika historia ya nchi.

"Ubinafsi tuache, tukishindwa uchaguzi achia ngazi.Mimi niliyasema haya nikiwa CCM na leo hii nipo Chadema nasema unapoang'angania madaraka, aidha unaogopa ukiachia utasababisha machafuko au ubinafsi."

Naye Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema, Dk. Vincent Mashinji akifungua kongamano hilo, alisema chama chake kinataka kutengeneza mabepari wa kitanzania ambao watajiongeza wenyewe katika kujiinua kiuchumi.

Alisema Arusha ni mji wa kitalii hivyo ni vyema wafanyabiashara wakatumia fursa zilizopo kwa ajili ya kujikwamua kiuchumi, na inawezekana Jiji hilo kuwa na fursa nyingine za kibiashara badala ya kutegemea madini ya Tanzanite pekee.

Wema Sepetu Akubali Ndoa na Idris, Asema haya Kuhusu Ndoa yao itavyokua

$
0
0
Penzi la Wema na Idriss kwa sasa linazidi kupamba moto, mpaka kupelekea Wema Sepetu kuanza kuwaza kufunga ndoa na Idriss. Wema alifunguka hayo katika video alipoulizwa na shabiki yake ni lini atafunga ndoa na Idriss. Na Wema

Video:Diamond Platnumz Aliwahi Kufikiria Kujiua Kisa Huyu Demu

$
0
0
Diamond ni mmojakati ya mastar wakubwa wanaojulikana Afrika wakitokea hapa hapa kwetu Bongo. Ukiacha mziki ambao umemfungulia milango na kumpa mkwanja alionao, Diamond Platnumz anafahamika kwa kula madem wengi tu hapa Bongo huku asilimia kubwa wakiwa ni maarufu.

Lakini wanasema kila mjanja ana mjanja wake, je wajua kua Diamond alishawahi kutaka kujiua kisa katoswa na demu??? Basi bana jibu ni ndio na Diamond kafunguka kupitia video hii hapa chini, mskilize.....
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live




Latest Images