Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104795 articles
Browse latest View live

Mkubwa Fella Atolea Ufafanuzi Tetesi za Chid Benz Kujiunga na Lebo ya Wasafi...Asema Haya

$
0
0
MKURUGENZI wa kundi la Wanaume Family na Yamoto bendi, Saidi Fella maarufu Mkubwa Fella, amesema yeye na meneja wa msanii, Diamond Platnumz, Babu Tale, wameamua kumsaidia mkali wa rapu, Rashid Makwiro ‘Chid Benz’, arudi katika sanaa yake na si kujiunga na kundi lolote.

Fella alisema msanii huyo kwa sasa wamemwanzishia mazoezi maalumu ya kumwezesha kurudisha mwili wake na pumzi ili aweze kurudisha makali yake katika uimbaji bila kuchoka.

Chid Benzi hawezi kujiunga na Wasafi kwa sasa mimi na Babu Tale tumekubaliana tumsaidie yeye kama yeye na si kujiunga na kundi lolote lakini kama anataka kujiunga na lebo yoyote hilo litakuwa la kwake,” alifafanua Mkubwa Fella.

Breaking News: Polisi Waizingira Nyumba ya Askofu Gwajima

$
0
0

Taarifa zilizotufikia muda huu zinasema Polisi 6 wakiwa ndani ya Landcruiser wamezingira nyumbani kwa Askofu Josephat Gwajima. 


Sababu za kufanya hivyo bado hazijafahamika, tutaendelea kuwajuza kadri tunavyoendelea kupata taarifa.

Taarifa ya CCM kukanusha Tuhuma Zilizotolewa na Askofu Gwajima

$
0
0

Bila ya shaka mmepata habari kupitia mitandao ya kijamii na vyombo vya habari kuwa siku ya Jumapili ya tarehe 11/06/2016 akiwa kanisani kwake, Mchungaji Josephat Gwajima wa Kanisa la Ufufuo na Uzima alitoa kauli za uongo, uchochezi na uchonganishi dhidi ya Chama cha Mapinduzi, Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Dkt Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano Dkt John Pombe Magufuli, Viongozi wa CCM, Watendaji wa CCM na Serikali ya Awamu ya nne.


Mchungaji Gwajima amedai ati kwamba lipo kundi la wanaCCM wanaozunguka sehemu mbalimbali za nchi wakishawishi wanachama na wakimshawishi Mwenyekiti wa sasa Dkt Jakaya Mrisho Kikwete ili aendelee na Uenyekiti na kuleta hoja ya kutenganisha kofia ya Uenyekiti wa CCM na Urais wa nchi.


Napenda kuwafahamisha wana CCM, wapenzi wa CCM na wananchi kwa jumla kuwa madai hayo ya Mchungaji Gwajima ni uongo mtupu na hayana hata chembe ya ukweli. Ni mambo ya uzushi na hadithi ya kufikirika. 

Watu hao hawapo kwani kama wangekuwepo habari hizo zingekwishajulikana Chamani kupitia mfumo mahiri wa usalama na maadili wa ndani ya Chama cha Mapinduzi. Chama chenyewe kingekwishawatambua watu hao na kuwachukulia hatua zipasazo za udhibiti na nidhamu.


Kama mambo hayo yangekuwepo viongozi wa Chama wa Mikoa, Wilaya na Matawi waliofuatwa wangekuwa ndiyo wa kwanza kuwafichua. 

Habari za namna hiyo hazijapokelewa kutoka popote na kutoka kwa kiongozi yeyote wa Chama. Kama kweli Mchungaji Gwajima anawajua watu hao awataje hadharani na aseme walikwenda kumuona nani, wapi na lini kufikisha ujumbe wao huo hasi dhidi ya CCM.


Napenda kusisitiza kuwa habari za namna hiyo hazipo katika Chama cha Mapinduzi. Kwa hakika kinachoendelea sasa Mikoani na Wilayani ni maandalizi ya Mkutano Mkuu Maalum ambapo Mwenyekiti wa CCM wa sasa Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete atastaafu na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt John Pombe Joseph Magufuli atachaguliwa kuwa Mwenyekiti mpya. Hakuna jambo lingine.


Nafurahi kuwafahamisha Viongozi na Wanachama wa Chama cha Mapinduzi kwamba kazi ya maandalizi ya Mkutano Mkuu Maalum inakwenda vizuri kabisa.

Shughuli hiyo inasimamiwa na Naibu Katibu Mkuu Bara Ndugu Rajabu Luhwavi kwa niaba ya Sekretarieti ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM. 

Kwa mujibu wa hatua iliyofikiwa sasa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa inaweza kukutana siku yoyote kupanga tarehe ya kufanyika kwa Mkutano Mkuu Maalum wa CCM kwa uhakika.


Sisi katika Chama cha Mapinduzi hatushangazwi ingawaje tunasikitishwa na kauli za uongo, uchochezi na uchonganishi za Mchungaji Gwajima dhidi ya Chama cha Mapinduzi. 

Ana chuki iliyopitiliza dhidi ya CCM na Mwenyekiti wake. Yeye ni mtu ambae hajawahi kuitakia mema CCM. Hata yeye mwenyewe amekiri kwenye mahubiri yake ya tarehe 11 Juni, 2016 kuwa “alitaka CCM ishindwe katika chaguzi zilizopita na ndivyo anavyotaka iwe hivyo hata sasa, ili Chama chake cha upinzani kishinde.


Mchungaji Gwajima pia hana mapenzi na wala hamtakii mema Rais Dkt John Pombe Magufuli. Kwanza, hakutaka ashinde uchaguzi kwani alimpigania kwa hali na mali mgombea wa UKAWA. Pili, hataki adumu na kufanikiwa katika kazi yake ya Urais, ndiyo maana anatoa ushauri usiokuwa na mashiko na wakihasidi dhidi ya Mheshimiwa Rais. 

Anamshauri ati kwamba atoke Chama cha Mapinduzi na kuanzisha Chama chake. Kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Rais lazima awe mwanachama wa Chama fulani cha siasa. Hivyo basi, Rais John Pombe Magufuli akitoka CCM anapoteza Urais na Makamu wa Rais anakuwa Rais na CCM inaendelea kuongoza. Yeye atakuwa hana chake. 

Hivyo Rais wetu atakuwa amepata au atakuwa ameharibikiwa? Huo kweli ni ushauri wa mtu anayedai kuwa na mapenzi mema na Mheshimiwa John Magufuli? La hasha! Huo ni ushauri wa adui yake na wala siyo wa mtu rafiki na mwenye huruma na mapenzi na Rais wetu.


Mchungaji Gwajima anataka kufanya “danganya toto”. Napenda kumhakikishia yeye na genge lake kuwa “CCM hatudanganyiki na Rais Magufuli ndiyo kabisa “hadanganyiki na wala hababaiki”. 

Mheshimiwa John Pombe Magufuli siyo kama Bwana fulani aliyekubali kudanganywa na Gwajima na kudanganyika. Alitoka CCM akiamini kuwa angeshinda. Aliyomtabiria hayakuwa na sasa yeye na wenzake wanajuta na wengi wameanza kukimbia. 

Rais wetu mpendwa na Mwenyekiti wetu mtarajiwa hawezi kudanganyika kiurahisi namna hiyo. Mheshimiwa John Pombe Magufuli ni mtu makini na mahiri.


Shabaha ya Mchungaji Gwajima ni kutaka kuleta mfarakano ndani ya Chama cha Mapinduzi kwa kumchonganisha Rais na Mwenyekiti wa CCM. 

Anachotaka ni kukidhoofisha Chama cha Mapinduzi na kumdhoofisha Rais John Magufuli ili kupalilia Chama chake na mgombea wake washinde uchaguzi ujao.


Napenda kusema kwa kujiamini kuwa hilo halitatokea kamwe. Mwenyekiti Kikwete ni kada aliyelelewa na kupikika vyema na viongozi waasisi wa Chama na Taifa. 

Anaelewa na kuheshimu mila na desturi nzuri ya CCM kuunganisha kofia ya Urais na Uenyekiti. Hawezi kwenda kinyume. Hakung’ang’ania Urais, hawezi kung’ang’ania Uenyekiti na wala hana mpango huo.


Hali kadhalika, hata ushauri wake wa kutaka Marais Wastaafu waondolewe kinga ili washitakiwe, shabaha yake ni ile ile ya kutaka kuleta mfarakano baina ya Rais John Pombe Magufuli na Marais wastaafu kwa lengo lile lile la kutaka kuleta mfarakano ndani ya CCM na nchini. Matumaini yake ni yale yale ya kudhoofisha CCM na Rais wake ili kunufaisha upinzani. Kamwe Rais wetu hatanasa katika mtego huo.


Kwa kweli inasikitisha kuona Kiongozi wa dini akitumia madhabahu takatifu kusema uongo na kupanga fitina na kupandikiza chuki katika jamii. Hatutegemei Kiongozi wa dini kuwa hivyo. 

Hatukupenda kujibizana na Kiongozi wa dini lakini kwa vile ameacha ya dini na kuingilia ya upande wetu tumelazimika kusema. Wahenga wamesema “lisilobudi hutendwa”


Nawaomba wanaCCM na Wananchi kupuuza uongo, uzushi na ushauri hasi wa Mchungaji Josephat Gwajima.


Christopher Ole Sendeka.

Msemaji wa Chama Cha Mapinduzi.

Dewji alivyojipanga kufanikisha mikakati ya JPM kuingiza Tanzania uchumi wa kati

$
0
0
Miongoni mwa mambo yanayoifanya Tanzania kuwa masikini ni watu wengi kutokuwa na kipato cha uhakika na cha kutosheleza mahitaji muhimu kwa maisha.

Takwimu za Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) zinaonyesha kuwa utafiti uliofanyika mwaka 2014 umebaini nguvu kazi ya Taifa ni watu milioni 22.3 kati ya idadi ya Watanzania wanaokadiriwa kufikia milioni 45.

Kati ya nguvu kazi hiyo ya watu milioni 22.3, wenye ajira ni 20 milioni na wasio na shughuli yoyote ya kuingiza kipato ni milioni 2.2.

NBS inasema kuwa kwa kadri uchumi wa Tanzania unavyokua ndivyo na idadi ya watu wasio na ajira inavyopungua.

Takwimu nyingine zinaonyesha kuwa kila mwaka vijana 850,000 wanamaliza masomo na kuingia katika soko la ajira na miongoni mwao asilimia tano ndio wanaofanikiwa kupata ajira kwenye sekta rasmi. Wengi wao hubakia wakizurura mijini kutafuta ajira miaka kadhaa na miongoni mwao pia hujiunga katika sekta isiyo rasmi, wakijihusisha na shughuli za ujasiriamali.

Rais John Magufuli amekuwa akihimiza shughuli za kiuchumi ili kuisukuma Tanzania katika uchumi wa kati, ambao Watanzania wengi watakuwa na ajira na vipato vizuri.

Miongoni mwa mikakati hiyo ni kuhimiza uwekezaji, kufufua viwanda na kuhamasisha ukuaji wa viwanda vya ndani kwa kudhibiti uingiaji wa bidhaa kutoka nje.

Rais Magufuli anaona wazi kuwa sekta ya uzalishaji nchini inasuasua. Lengo lake ni kuona sekta ya uzalishaji viwandani inachangia zaidi ya asilimia 15 ya pato la Taifa na kuongeza asilimia 40 ya ajira nchini. Katika mkutano na wafanyabiashara wakubwa nchini, Dk Magufuli aliwahakikishia kuwa Serikali yake itakuwa bega kwa bega nao katika kuhakikisha uchumi wa nchi unakua.

Katika kuhakikisha kuwa Watanzania wanafaidika na kukua kwa uchumi, amekuwa akiisafisha Serikali yake juu ya vitendo vya rushwa, ufisadi na uzembe katika uwajibikaji.

Wakati wafanyabiashara wakihimizwa kushirikiana bega kwa bega na mikakati ya Serikali ya kuinua uchumi na kupambana na umaskini, Mfanyabiashara Mtanzania, bilionea mdogo Zaidi Afrika, Mohammed Dewji ameahidi neema kwa Watanzania.

Mtandao wa Forbes; unaoandika taarifa za watu bilionea duniani, unamnukuu Dewji akisema kuwa anatarajia kuzalisha ajira 100,000 kabla ya kufikia 2020.

Katika mpango huo wa ajira, anasema nafasi nyingi zitachukuliwa na Watanzania. Mpaka sasa Dewji kupitia kampuni zake ameajiri Watanzania 28,000.

Mfanyabiashara huyo ambaye amefanikiwa kutunukiwa zawadi mbalimbali kutokana na umahiri wake kibiashara, akifanikisha mpango huo atatoa ajira 100,000.

“Ninatarajia kuwekeza Dola 500 milioni (sawa na Sh1.1 trilioni) katika kipindi cha miaka minne ijayo. Mkakati huo utawezesha ajira zaidi ya 500,000 katika bara la Afrika katika kipindi kinachoishia 2021 na wengi wao watakuwa ni Watanzania,” Dewji ananukuliwa na mtandao huo.

Dewji ambaye sasa ana umri wa miaka 41, ni mmoja wa wafanyabiashara wanaomiliki kampuni binafsi zinazokuwa kwa kasi nchini na eneo la Afrika Mashariki na Kati.

Mfanyabiashara huyu chini ya kampuni zake zilizo chini ya MeTL anamiliki viwanda 35 vinavyojishughulisha na uzalishaji wa bidhaa mbalimbali katika sekta ya kilimo, nishati, mafuta, huduma za fedha, simu za mikononi, miundombinu, mashamba makubwa, usafirishaji na usambazaji.

Mpaka sasa Kampuni za MeTL zinatoa ajira inayofikia asilimia mbili katika sekta binafsi, hali inayomfanya Dewji kushika nafasi ya pili ya chombo kilichoajiri Watanzania wengi baada ya Serikali.

Ili kuhakikisha MeTL inatoa nafasi nyingi za ajira nchini, Dewji anasema tayari amechukua hatua mbalimbali za kufanikisha mpango huo.

Miongoni mwa mipango hiyo anaitaja kuwa ni kupanua na kuongeza wigo wa miradi kwenye kampuni zake kama vile kuongeza mitaji, kupanua maeneo ya kazi, kuchochea ufanisi na thamani.

Mwaka jana, Mtandao wa Forbes ulimtangaza Dewji kuwa mfanyabiashara wa mwaka kutokana na umahiri wake kibiashara ambao uliomfanya kuwa bilionea mdogo kuliko wote Afrika.

Umahiri wake pia kwenye biashara barani Afrika ulimfanya apate pia tuzo mwaka 2012 na kumfanya ang’ae zaidi mbele ya mabilionea wakongwe Afrika.

Miongoni mwa mabilionea wakongwe Afrika ni James Mwangi ambaye ni Mkurugenzi wa Benki ya Equity Kenya, Akinwumi Adesina (Rais wa Benki ya Maendeleo Afrika) na Aliko Dangote (mfanyabiashara tajiri zaidi Afrika anayejishughulisha na uzalishaji wa saruji).

Utafiti: Zoezi la uzimaji simu feki limeongeza furaha kwa taifa

$
0
0
Shamra shamra zilizolipamba taifa kwa wiki kadhaa sasa juu ya uzimaji wa simu feki hazina tofauti na zile za kuukaribisha mwaka mpya. Huki vijineno na vijimifano vya kiutani vikitembea kwenye social medias, zoezi hili limeonekana kuleta hamasa ya pekeee na kuliunganisha taifa. Watu wa familia wamekua wakipigiana simu kutaniana na kukumbushana kuchukua taadhari juu ya kuzimwa simu, vijimisemo kama vile, 'Hii kazi wangepewa TANESCO ingekuwa imekwisha kitambo, na vijimisemo kama 'ukiona sipatikani ujue niko nje ya nchi', ni baadhi tu ya vikorombwezo ambavyo vimekuwa vikiendelea kwenye social media.

Kiuhalisia ingawa inaonekana ni asilimia chache ya wananchi watakao athirika na zoezi hili, woga flani uemwashika watu wengi wakihofia kupotea hewani, jambo ambalo linaonesha jinsi mawasiliano kwa njia ya simu yalivyokuwa muhimu kwa taifa la sasa.

Wakati tunangojea zoezi hili kukamilika, nawatakia shamra shamra njema.

Waziri Mkuu: Tutakuwa Tunatumia Kiswahili Kwenye Mikutano ya Kimataifa, Tutaajiri wa Kututafsiria

$
0
0
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa amesema Serikali inaanda mikakati ya kuanza kutumia lugha ya Kiswahili kwenye mikutano mikubwa ya kimataifa. Ameyasema hayo alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa viti maalum Zainabu Vulu Bungeni mjini Dodoma.

Amesema Kiswahili imekuwa sasa na ni lugha ya sita au ya nane kwa matumizi duniani, na watakuwa wanaenda na watafsiri wakienda safari za nje na kuwapa vijana ajira. Video:

Rais Magufuli Aanza Kubanwa

$
0
0
RAIS John Magufuli ametakiwa kutangaza rasmi tarehe na namna ya kurejea kwenye mchakato wa kuandika Katiba Mpya ili kukamilisha hatua zilizobaki, anaandika Pendo Omary.

Kauli hiyo imetolewa leo jijini Dar es Salaam na Jukwaa la Katiba Tanzania (JUKATA) katika mkutano maalum na waandishi wa habari.

Deusi Kibamba, Mwenyekiti wa JUKATA amesema, tathimini jumala ya taasisi hiyo mebaini kwamba, mchakato umeshidwa kujenga muafaka wa kitaifa unaohitajika kama za la mchakato wa katiba na hivyo kupelekea katiba inayopendfekezwa kuwa na kiwango duni cha maridhiano ya kitaifa.

“Kwa hapa tulipo, mchakato wa Katiba unahitaji nguvu ya ziada ili uanze mapema katika mwaka wa fedha unaoanza wiki mbili zijazo kwa sababu mchakato haukuahirishwa kisheria kwa mtindo wa tangazo la serikali kabala ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2015.

“Pia, zaidi ya kugusiwa na Rais Magufuli wakati wa uzinduzi wa Bunge mwishoni mwa mwaka 2015, haijaonekana nia wala dalili za serikali kutaka kurejesha mchakato wa katiba mpya. Ndio maana JUKATA tunaungana na Rais Mstaafu Benjamini Mkapa katika hoja kuwa mjadala wa kitaifa unahitajika sasa,” amesema Kibamba na kuongeza;

“Bila Katiba Mpya yenye misingi imara ya utawala bora utumbuaji majipu na ‘hapa kazi tu’ inaweza kuwa kauli mbiu zisizoeleweka kwa Watanzania kwa kukosekana misingi imara ya kikatiba na sheria wa utekelezaji wake.

Kibamba amesema, namna utumbuaji majipu unavyofanyika wakati mwingine unaonekana kuvunja heshima, utu na faragha ya binadamu pamoja na misingi mikuu ya haki za binadamu kwa mujibu wa Katiba.

Aidha, JUKATA limeitaka serikali kupitia Wizara ya Katiba na Sheria kupeleka bungeni miswada ya kurekebisha sheria zinazosimamia mchakato wa wa katiba kwa ajili ya kuzihuisha katika tarehe zake zote zilizopitwa na wakati.

Hatua hiyo inatokana na Sheria ya Mabadiliko ya Katiba ya mwaka 2011 na ile ya Kura ya Maoni ya mwaka 2013 kupitwa na wakati na haziwezi kutumika tena bila marekebisho, bunge la bajeti kuelekea kumalizika bila miswada wa marekebisho ya sheria hizo kupelekwa bungeni na hakuna bajeti iliyotengwa katika suala la katiba kwa mwaka wa fedha 2016/2017

Dokta Aoboa Siri 8 Mimba za Wema Sepetu Kuyeyuka!

$
0
0


Imevuja! Kuyeyuka au kuharibika kwa ule ujauzito wa Miss Tanzania 2006, Wema Sepetu ‘Madam’ hivi karibuni kumetajwa na daktari kuwa ni matokeo ya tabia yake ya kukaidi ushauri wa kitaalam, Amani lina cha kuwapa wasomaji wake.

Hayo yalisemwa na mtu wa karibu we Wema (jina lipo) akizungumzia  masharti ambayo daktari aliyepata kumtibu mrembo huyo aliyasema. Lakini pia, daktari mwingine wa jijini Dar, Dk. Fadhili Emily naye ameibuka na kuliambia Amani kuwa, Wema ana sababu 8 za mimba zake kuyeyuka akiwa anajua au hajui.

DAKTARI WA KWANZA
Mtu huyo wa karibu na Wema alisema mimba ambayo staa huyo aliifanyia shoo kwenye mitandao mbalimbali ya kijamii na kuyeyuka Februari, mwaka huu, ilitokana na sababu ya kugoma kutii masharti ya kitabibu.

SABABU YA KWANZA
“Vipimo vya kitabibu vilisema kuwa Wema alitakiwa kupumzika kwa muda mrefu ili kuilinda mimba hiyo kwani ilikuwa katika hatihati ya kutoka kama mhusika atakuwa ni mzururaji. Sasa Wema akiwa mjamzito alikuwa hakosi viwanja.”

USHAHIDI
Februari, mwaka huu, akiwa mjamzito, Wema alihudhuria tukio la uzinduzi wa Video ya Lupela iliyozinduliwa na Alikiba Salehe kwenye Hoteli ya Slipway, Oysterbay jijini Dar.

SABABU YA PILI
“Ilifika wakati, Wema alitakiwa kupewa bed rest (mapumziko ya kitandani) ili kulinda mimba yake. Hilo nalo likawa gumu kwake kukubaliana nalo. Ndiyo ikawa sababu ya mimba kutoka.”

SABABU YA TATU
“Sababu ya tatu, aliambiwa na daktari wake asifanye kazi ngumu, jambo ambalo lilikuwa likimshinda. Yeye si mtu wa kukubali kukaa tu muda wote. Hilo nalo lilichangia.”
Wema SepetuWema akiwa na mama yake mzazi

SABABU NYINGINE 5
Naye Dk. Fadhili, akizungumza na gazeti hili Jumatatu iliyopita, alisema sababu tatu ambazo zinadaiwa zilichangia mimba ya Wema kuyeyuka ni za kweli, lakini akasema Wema bila kujijua au akijua, mimba zake kadhaa zimeshatoka kwa vile wanawake wengi wenye matatizo ya kutoshika mimba, hushika na kutoka bila wenyewe  kujijua na pia akaanika sababu za hali hiyo kumtokea mwanamke.

Lakini akasisitiza kuwa kuharibika kwa mimba ni tatizo ambalo linaweza kumkumba mwanamke yeyote, si Wema tu.

SABABU ZA KIMAUMBILE
“Sababu za mimba kutoka zenyewe zinatajwa kwamba ni tabia ya kurithi, yaani vinasaba ambavyo si vya kawaida. Kwa hiyo, kiumbe kinakuwa katika hali ambayo kwa asili mimba haiwezi kukua.  Kama mtoto akizaliwa basi atakuwa na matatizo ya kimaumbile na kiakili.”

SABABU YA MUUNGANO
“Sababu nyingine ni kukosekana kwa yai lililorutubishwa.  Katika kuumba, yai la mwanamke hukutana na mbegu ya mwanaume na zoezi la kiumbe kukua huanzia hapo kwa yai kujitenga mara mbili.  Upande mmoja hutengeneza kondo la nyuma na kifuko cha kutunza maji na sehemu ya pili hutengeneza kiumbe au mtoto.

“Huwa inatokea sehemu ya kondo la nyuma inaendelea kukua wakati sehemu ya mtoto haikui. Katika hali kama hii, kama mama hajafanya vipimo kujua maendeleo ya mtoto, uwezekano wa mimba kutoka kabla ya kufikisha wiki 24 ni mkubwa.
“Lakini hili la muunganiko nasema pia kwamba, kwa mwanamke ambaye mimba yake inahofiwa kutoka, ni hatari kuendelea kukutana kimwili na mwanaume wake kwani uwezekano wa kutoka ni mkubwa.”

KUHUSU IDRIS
Hakuna ushahidi wa moja kwa moja kwamba walikuwa wakiendelea ‘kukutana’, lakini kipindi cha ujauzito wake, Wema na Mbig Brother, Idris Sultan uhusiano wao ulikuwa umekolea.

SABABU YA POMBE
“Sababu nyingine inayochangia kuharibika kwa mimba ni unywaji wa pombe kupita kiasi kwa mama mjamzito au kuvuta sana sigara,” alisema dokta huyo.

SABABU YA MAGONJWA
Sababu nyingine alizitaja kuwa ni magonjwa yanayoshambulia mwili wa mama na kiumbe wake tumboni kama vile malaria na kaswende.

SABABU YA KUTOA MIMBA
Daktari huyo alisema kuwa, mwanamke kutoa mimba mara kwa mara kunachangia kuharibika au kushindwa kunasa mimba baadaye.
“Lakini si lazima awe anatoa mimba mara kwa mara, mwanamke anaweza kutoa mimba mara moja tu ikiwa katika mazingira ya ukuaji salama. Hilo linaweza kuwa tatizo kubwa la mimba kutoka siku za usoni,” alisema.

USHAHIDI
Katika mahojiano na gazeti damu moja na hili, Risasi Jumatano mwaka jana, Wema alikiri kuwahi kutoa mimba moja tu ya aliyekuwa staa wa filamu za Bongo, marehemu Steven Kanumba.

WEMA ASAKWA
Mpaka juzi Jumanne, gazeti hili lilikuwa limetimiza siku saba za kumsaka Wema kwa ajili ya kupata vielelezo vyake kufuatia madai au maelekezo hayo ya daktari lakini bila mafanikio kwani hapokei simu na hata alipotumiwa ujumbe mfupi, nao hakuujibu

Chanzo:GPL

Freeman Mbowe: Watu Kuwa na Uhuru wa Kusema ni Afya kwa Taifa

$
0
0
Watu kuwa na uhuru wa kusema ni afya kwa taifa. Waache watu waseme. Wakosoe kwa nia ya kujenga nchi. Watu wote wawe wa CHADEMA, wawe wa CCM hata wasio na vyama ni haki yao kusema.

Ukiwazuia watu kusema ni hatari sana. Katika maeneo mengine duniani ambako ugaidi umekuwa tishio, ni kwa sababu watu walizuiliwa na kunyimwa haki ya kusema na ukajengwa utawala wa mtu mmoja kusikika peke yake.

Tusifike huko. Tuwapatie watu uhuru wa kusema, kukosoa na kutoa mawazo mbadala. Hii ndiyo haki tunaipigania mahakamani.

SOMA Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya June 17, Ikiwemo ya Majanga Kwa Askofu Gwajima

$
0
0

SOMA Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya June 17, Ikiwemo ya Majanga Kwa Askofu Gwajima

Namkubali Sana Mr. Blue". - Belle 9

$
0
0
Msanii Belle nine amesema amkubali sana rapper Mr. Blue, kwani ni msanii ambaye amaeonyesha njia kwa vijana wengi kwa kitendo chake zha kuanza muziki akiwa mdogo.

Akiongea kwenye Planet Bongo ya East Africa Radio, Belle 9 amesema Mr. Blue ni rapper mzuri si kwa kuanza muziki akiwa mdogo, bali pia alishawahi kufanya naye kazi na kufanya vizuri.

“Mr. Blue ni rapper ninayemkubali alianza muziki akiwa na umri mdogo na kutuhamasisha wengi, hata nilipofanya naye kazi ya we ni wangu alifanya poa ni ikawa kazi nzuri”, alisema Belle 9.

Belle 9 ambaye ameachia remix ya wimbo wa 'burger, movie, selfie' amesema kuamua kushirikisha wasanii watano kwenye wimbo huo, ni idea aliyoipata baada ya watu wengi kumpigia simu kutaka remix au refix, na kaumua kuifanyia kazi mwenyewe kwa kuchanganya ladha tofauti tofauti.

“Unajua baada ya kuitoa burger, movie selfie, watu wengi walinipigia wanataka kufanya remix, cover, refix, nikaona niifanyie remx, na kuamua kuwashirikisha wasanii tofauti tofauti”, alisema Belle 9.

Mayweather Atumia $37m Kununua Ndege Binafsi ya Pili

$
0
0
Aliyekuwa bingwa wa ngumi kwa uzito wa kati Floyd Myweather amenunua ndege binafsi nyingine iliyomgharimu zaidi ya dola milioni 37.

Mtu wa karibu wa Mayweather ameiambia TMZ, “It’s a 12 passenger Gulfstream III with gold cup holders, gold sink, gold accents throughout. It has all white leather seats and a fully stocked kitchen. He now has two jets.

“Air Mayweather 1 and 2,” aliongeza.

Mayweather amekuwa akitumia fedha nyingi kununua vitu vya gharama tangu alipotangaza kustaafu ngumi mwaka jana.

Uenyekiti wa Rais Magufuli CCM Waiva, Kamati Kuu ya Chama Hicho Kukutana Dar es Salaam Kesho

$
0
0
Maandalizi ya CCM kumkabidhi Rais John Magufuli uenyekiti wa chama hicho ili ashike kofia zote mbili, yataanza kesho katika kikao cha Kamati Kuu kilichopangwa kufanyika jijini Dar es Salaam.

Taarifa kuhusu kikao hicho iliyotiwa saini na msemaji wa chama hicho, Christopher ole Sendeka ilisema: “Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM itafanya  kikao cha kawaida siku ya Jumamosi jijini Dar es Salaam. Kikao hicho kitafanyika chini ya Mwenyekiti wa CCM, Rais mstaafu Jakaya Kikwete.”

Japokuwa taarifa hiyo haikueleza ajenda za kikao, habari kutoka ndani ya chama zinasema kikao hicho cha siku moja kinatarajiwa kujadili masuala mbalimbali, ukiwamo mchakato wa makabidhiano ya kiti hicho katika mkutano mkuu wa chama hicho utakaofanyika mwezi ujao.

Kipindi cha uongozi wa chama kwa Kikwete kitamalizika mwakani, lakini imekuwapo desturi kwa rais mpya kuachiwa kofia hiyo mapema, hivyo Rais Magufuli anatarajiwa kurithi mikoba ya uenyekiti mwezi ujao.

Vilevile, kikao hicho kinatarajiwa kuhitimisha hoja zinazodaiwa kuibuka katika vikao vya ndani vya chama hicho kwamba CCM inataka kuvuruga utaratibu uliodumu kwa muda mrefu wa mwenyekiti kumwachia kijiti Rais aliyeko madarakani.

Madai kuhusu mkakati huo wa ndani yalisambazwa katika mitandao ya kijamii yakimnukuu Mchungaji wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima, lakini Ole Sendeka alisema hana sababu yoyote ya kumjibu kiongozi wa dini.

Februari 5, mwaka huu Kikwete alipokuwa anazungumza na wazee wa Manispaa ya Singida alisema sherehe za mwaka huu za maadhimisho ya miaka 39 tangu chama hicho kuanzishwa zilikuwa za mwisho kwake akiwa mwenyekiti, kauli ambayo iliashiria ataachia mapema uenyekiti.

Kwa desturi, wenyeviti wa CCM huwa wanaachia madaraka yao kabla ya muda wa uongozi wao kumalizika.

Rais wa Awamu ya Tatu, Benjamin Mkapa alikabidhiwa chama na Alhaji Ali Hassan Mwinyi mwaka 1996 badala ya 1997 na Mkapa alimkabidhi Kikwete kiti hicho mwaka 2006 badala ya 2007.

Kulingana na kalenda ya chama hicho, Mkutano Mkuu wa CCM kumchagua mwenyekiti unapaswa kufanyika mwaka 2017, lakini utafanyika mwaka huu kuendeleza utamaduni wa kung’atuka mapema.

Habari kutoka ndani ya chama hicho zinaeleza kuwa kinachoendelea sasa mikoani na wilayani ni maandalizi ya mkutano huo mkuu yanayosimamiwa na Naibu Katibu Mkuu wa Bara, Rajabu Luhwavi kwa niaba ya Sekretarieti.

“Kikao hicho cha Kamati Kuu ndicho kitakachojadili ajenda za mkutano huo sambamba na kupanga tarehe ya kufanyika kwa mkutano mkuu,” zilieleza taarifa hizo.

Dk Magufuli anatajwa kuwa uongozi wake ndani ya CCM utakuwa wa kasi ya aina yake kutokana na hatua mbalimbali za ‘utumbuaji majipu’ anazozifanya ndani ya Serikali tangu Novemba 5, alipoapishwa kuwa Rais.

Wabunge UKAWA Wasusa Futari ya Waziri Mkuu

$
0
0
Wabunge wa vyama vinavyounda Ukawa jana walisusia futari iliyoandaliwa na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa ikiwa ni mwendelezo wa hatua za kususia shughuli zote zinazoongozwa na Naibu Spika, Dk Tulia Ackson.

Naibu Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni, Riziki Ng’wale, alisema wamechukua hatua hiyo kutokana na Dk Tulia kuwa mgeni rasmi wa shughuli hiyo.

“Dk Tulia ndiye mgeni rasmi katika shughuli hiyo ya kufuturisha na sisi tumeamua kuwa hatutashiriki shughuli yoyote inayoongozwa naye,” alisema muda mfupi baada ya kutoka katika kikao cha wabunge wa kambi hiyo kilichofanyika katika ukumbi wa Pius Msekwa.

Mbunge wa Ubungo (Chadema), Saed Kubenea alisema wamekubaliana wabunge wote wa kambi ya upinzani waliofunga watakwenda kufuturu majumbani kwao.

“Tumekubaliana hatutakwenda kufuturu bungeni na kila mbunge atakwenda kufuturu nyumbani kwake,” alisema.

Uamuzi huo ulifikiwa katika kikao cha wapinzani kilichoketi chini ya uenyekiti wa Mwenyekiti Mwenza wa Ukawa, James Mbatia.

Futari hiyo ilitangazwa na Dk Tulia tangu juzi na kusisitizwa jana baada ya kikao cha Bunge kuahirishwa mchana kuwa ingefanyika kwenye viwanja vya Bunge ambako wabunge wote walialikwa.

Kwa siku zaidi ya 10 sasa, wabunge hao wamekuwa wakisusa vikao vya Bunge vinavyoongozwa na Dk Tulia kwa sababu hawana  imani naye.

Hali hiyo imefanya bajeti kuu kwa ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2016/17 kuchangiwa na wabunge wa CCM tu baada ya Dk Tulia kuongoza vikao kila siku, akiingia asubuhi na jioni.

Mwimbaji Ray C Katika Hali Mbaya Tena..Adhalilika Kinondoni Polisi Wamchukua..Video

$
0
0
Hali ya Kiafya ya Ray C imeleta Sinto fahamu baada ya Video inayozunguka mitandaoni ikionyesha akichukuliwa na Polisi huku akisema kuwa wanamteka....

Shuhuda wa tukio hilo ameandika haya hapa chini:

Esha Buheti
"Nashindwa hata niongee nini jamani, rayc Leo kinondoni umenitoa machozi, jamani tufanye kitu tumsaidie rayc, I mean it jamani siku zote nlikua najua anaonewa ila nlichokishuhudia leoo nimeumiaa kutoka moyoni amedhalilika mwanamke mwenzetu, jamani tufanyeje? Nlikua na @kabulaflavour kino kwa wapemba tumefata chips mara tukaskia mtu anasema me rayc nataka kuvua nguoo, nikajua utani kushuka ni rayc anasema nishikenj kuna watu wanataka kuniteka, alikua na nguvu sana watu kamshika akaanza kuongea vitu havieleweki, akaanza kutafta kisu ajichome, watu walimzuia sana walishindwa akaaanza kugaragara kwenye matope akipiga KELELE kiukweli nilijikuta nalia mara ikaja gari YA polisi ikambeba ila kwa tabu sanaa alikua akipiga kelele jamani nisaidieni msiniache kiukweli mpk rayc anaondoka na ile gari yapolisi sikujua anapelekwa wapi alikua kama mtu alopata kichaa, YARRAB TUNAMSAIDIAJE RAYC?"

Tazama Video:

A video posted by Udaku Special (@udaku_special) on

Baraka da Prince Afunguka Kuhusu Yeye na Linah Baada ya Picha ya Utata Kuzagaa Mtandaoni

$
0
0
Msanii Baraka da Prince amekanusha vikali kumshika msanii wa kike wa bongo fleva sehemu za kifuani, na kusema aliyepiga picha hiyo aliikuza.

Akiongea kwenye eNews ya East Africa TV, Baraka amesema hajwahi kufanya kitendo kama hicho kwani walikuwa sehemu yenye watu wengi, na pia hajawahi kuwaza kuwa na uhusiano wa kimapenzi na Linah.

“Siwezi kufanya kitu kama hicho kwa sababu pale pana watu wengi, ile picha ilikuwa ya kawaida, yule aliyeipiga na kuipost amekuwa kama kaikuza, sijawahi kufikiria hata kutoka naye”, alisema Baraka.

Pia Baraka amesema siku ya tukio ambayo ilikuwa ni siku ya kuadhimisha miaka 10 ya muziki wa Christian Bella, aliondoka mapema na hakufanya tukio lolote baya.

“Nimetoka kuperfom nikaondoka zangu, sikukaa hata nusu saa, nimemaliza nikaondoka, wasiwe wanaamini mambo ya hivyo”, alisema Baraka.

Polisi Wamuwinda Askofu Gwajima Kwa Masaa 7 Bila Mafanikio, Ni Baada ya Kusambaa kwa Video Akimsema Vibaya Rais Mstaafu Jakaya Kikwete

$
0
0
Polisi jana walipiga kambi kwa saa saba kwenye geti la nyumba ya Askofu Josephat Gwajima wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, wakitaka kumkamata bila ya mafanikio.

Polisi hao walikuwa kama wageni wa askofu huyo wakisubiri wafunguliwe geti, kuanzia saa 3:00 asubuhi hadi saa 10:10 jioni walipoamua kuondoka wakitumia gari aina ya Toyota Landcruser lenye namba za kiraia, ambalo kwa muda wote huo lilikuwa limeegeshwa pembeni mwa geti hilo.

Hii ni mara ya pili katika kipindi cha takriban miezi 16, kwa askari wa jeshi hilo kwenda nyumbani kwa askofu huyo na kushinda mbele ya nyumba yake kwa saa kadhaa, kabla ya kuondoka bila ya kumtia nguvuni.

Tukio hilo pia linatokea wakati kukiwa kumesambaa mkanda unaotoa sauti ya Askofu Gwajima, ikizungumzia kitendo chake cha kuamua kumuunga mkono Rais John Magufuli na kumshutumu Rais wa Serikali ya Awamu ya Nne, Jakaya Kikwete ikiitaka afikishwe mahakamani kwa yote yaliyofanyika wakati wa utawala wake ambayo Rais wa sasa anayashughulikia.

Jana, mbele na nyuma ya gari hilo kulikuwa na askari waliokuwa wamevalia kiraia, kila mmoja akionekana kama anafanya shughuli tofauti, lakini wote wakionekana kuwa na lengo moja; kusubiri kufunguliwa lango la nyumba ya Askofu Gwajima.

Mbele ya nyumba walikuwapo askari watatu na raia wawili, mmoja mwanamke na mwingine mwanamume ambao baadaye ilibainika kuwa walikuwa wamezuiwa na askari hao baada ya kuonekana wakitokea mlango wa nyuma wa nyumba hiyo.

Mwandishi  alishuhudia mwanamke huyo akiitwa na askari aliyekuwa ndani ya gari na kuonywa kuepuka kutumika, kisha akarudishiwa simu yake ambayo walikuwa wakiishikilia.

Raia hao walisema, walifika kwenye nyumba hiyo kwa ajili ya kufanya tathmini ya matengenezo na baada ya kumaliza walipokuwa wanatoka wakakutana na askari hao na kukamatwa.

Askari hao wasikika wakisemezana kuwa kuna taarifa zinasambazwa kwenye simu kuwa nyumba ya kiongozi huyo wa kiroho, ambaye aliibuka kuwa maarufu mwishoni mwa mchakato wa Katiba Mpya, imezingirwa, wakati hakukuwa na kitu kama hicho.

Pia, askari hao walisikika wakieleza kushangazwa na kitendo cha wenyeji kutowafungulia geti hilo ili waingine.

“Mtu kama huna tatizo; ni raia mwema. Una sababu gani ya kukataa kufungua mlango? Afungue akutane na sisi wageni wake,” alisema mmoja wa askari hao wakati wakiongea baina yao.

“Tumekuja bila silaha, tunataka kuzungumza naye, hataki kufungua mlango, anataka nini sasa?” alihoji.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Christopher Fuime alipoulizwa alisema hajatuma askari yeyote nyumbani kwa Gwajima.

“Wapigie makamanda wengine kwa  sababu si kila anayeishi Kinondoni amefanya kosa Kinondoni,” alisema.

Alipoulizwa kuhusu suala hilo, Kamanda wa Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Simon Sirro alisema wanamuhitaji askofu huyo.

“Kama uko na Gwajima mwambie tunamuhitaji.” Alipoulizwa wanamuhitaji kwa sababu gani, Kamanda Sirro alisema: “Tumepata clip (mkanda) inayosemekama ni ya kwake. Tunamtaka athibitishe kama hayo maneno ni ya kwake. Na kama ni yeye ameyasema, anaelewa nini kuhusu kile alichokizungumza kwa sababu hayo maneno ni ya kichochezi. Tupo kwenye uchunguzi .”

Askofu Gwajima si mgeni wa matukio kama hayo dhidi ya mamlaka.

Mwaka 2012 aliingia kwenye mzozo na Jeshi la Polisi baada ya kijana mmoja kudai amejisalimisha kanisani kwake kutubu, baada ya kushiriki kwenye tukio la kumteka kiongozi wa madaktari, Dk Steven Ulimboka.

Hata hivyo, Askofu Gwajima aliekeza kuwa kijana huyo hakuwahi kufika kwenye kanisa hilo, wala kukutana naye na kwamba taarifa hizo zililenga kuchafua kanisa lake.

Mwaka 2015, Askofu Gwajima aliingia kwenye mgogoro mwingine na Jeshi la Polisi baada ya mkanda wa sauti ya mahubiri kanisani kwake kutoa maneno yaliyoonekana kukashifu msimamo wa Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Kanisa Katoliki Dar es Salaam, Kardinali Polycarp Pengo dhidi ya tamko la maaskofu wa Jukwaa la Wakristo la kuwataka waumini wao wasipige kura ya maoni kupitisha Katiba Inayopendekezwa.

Katika sakata hilo, Askofu Gwajima alifunguliwa shtaka la kutoa lugha ya matusi dhidi ya Kardinali Pengo, na kushindwa kuhifadhi silaha na risasi wakati akiwa hospitalini.

Kabla ya kufunguliwa mashtaka hayo, askari walizingira nyumba yake kwa takriban saa saba, lakini hawakufanikiwa na siku iliyofuata kiongozi huyo alijisalimisha Kituo Kikuu cha Polisi cha Dar es Salaam.

Akiwa huko aliugua na baadaye kulazwa. Polisi walitangaza kukamata watu 15 wakiwatuhumu kuwa walikuwa na mpango wa kumtorosha na kukamata silaha hiyo pamoja na risasi walizodai walizikuta kwenye gari.

UKAWA Kususia Futari za Viongozi wakuu Mfungo wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani ni Dhihaka kwa Waislam

$
0
0
Mwezi mtukufu wa Ramadhani kwa wasiojua ni nguzo mojawapo kubwa katika Nguzo kuu za dini ya waislam. Na mwezi huu kwa waislam ni mwezi wa kufututrishana kusamehehana na kuombeana mema. Ata kama mnaugomvi mkubwa wengi huwa wanausubiri kwa ajili ya kusameheana ni mwezi wa rehema kwa waislam, Lakini kwa nchi yetu hatujafikia hatua mbaya ya kususia ata chakula au maji .

Ukawa wanachofanya ni kutaka kutengeneza Chuki baina ya watanzania ifikie hatua hatuzikani kisa siasa, Najiuliza tu km kiongozi wanayeshindana nae hakifiwa na mtu wa karibu yake Je wapo tayari kumsaidia au kumfariji??

Kama wameweza kususia Futari kisa yupo Naibu Spika?
Watanzania je tumefikia hapo?

Nafasi za Ajira Zilizotangazwa Katika Magazeti na Mitandaoni leo 17 June 2016

$
0
0

Mimi ni mwanamuziki, Shilole ni mcheza shoo – Nuh Mziwanda

$
0
0
Msanii wa muziki, Nuh Mziwanda ameendelea kumponda aliyekuwa mpenzi wake, Zuwena Mohammed ‘Shilole’ kwa kudai sio mwanamuziki bali ni mcheza shoo.
nuhu

Muimbaji huyo wa wimbo ‘Jike Shupa’ amekuwa akitupiana maneno na Shilole kupitia mitandao ya kijamii toka wimbo huyo utoke.

Akiongea katika kipindi cha The Base kinachoruka katika runinga ya ITV, Nuh alisema hawezi shindana na Shilole kwa kuwa sio mwanamuziki.

“Mimi sitaki kiki, mimi mambo ya kiki nimeshayaacha, sasa hivi na fans base kwa ajili ya Jike Shupa,” alisema Nuh. “Ila yeye (Shilole) anajaribu kunichokonoa ili maisha yake yaende. Mimi ni mwanamuziki babu, siwezi kushindana naye, yule ni mcheza shoo,”

Shilole na Nuh hawakuachana vizuri, kila mmoja amekuwa akimtupia maneno machafu mwenzake.
Viewing all 104795 articles
Browse latest View live




Latest Images