Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live

Video:Riyama Ally Afunga Ndoa na Leo Mysterio

$
0
0
Msanii wa filamu Riyama Ally Alhamisi hii amefunga ndoa na mpenzi wake wa muda mrefu Leo Mysterio.

Muigizaji huyo mahiri wa filamu ambaye ni mama wa mtoto mmoja aliyezaa mume ambaye aliaacha naye, ameingia katika list ya wasanii wachache wa filamu waliofunga ndoa.

Leo Mysterio ambaye ni msanii chipukizi wa muziki, aliwahi kusema kuwa mahusiano yake na staa hiyo wa filamu, yalianza mwaka mmoja uliyopita.

Ndoa hiyo ilihudhuriwa na mastaa mbalimbali wa filamu.

PPFT : Gwajima Afutiwe usajili kwa kutoa kauli za uchochezi.

$
0
0

Ushirika wa wachungaji wa Kanisa la Kipentekoste Tanzania (PPFT)umeiomba serikali ifute usajili wa Kanisa la Ufufuo wa uzima la Askofu Josephat Gwajima kwa kukiuka maadili ya kanisa kwa kutoa kauli za uchochezi na kuzisambaza kwenye mitandao ya kijamii.

Mwenyekiti wa ushirika wa wachungaji hao Askofu Pius Ikongo mwenye makao yake katika Halmashauri ya wilaya ya Mwanga amesema,kauli hizo zinaweza kubadili fikra za wananchi na kuzaa chuki dhidi ya serikali yao na kusababisha vurugu na uvunjifu wa amani.

Askofu Ikongo ametoa tamko hilo katika taarifa yake kwa vyombo vya habari na kueleza kuwa kitendo kilichofanywa na Askofu Gwajima kinapaswa kulaaniwa na wapenda amani wote waliopo ndani na nje ya nchi.

Mwenyekiti huyo wa ppft amesema, kosa kubwa ambalo limewaumiza wachungaji wa Kipentekoste ni kitendo cha Askofu Gwajima kutumia Kanisa kama jukwaa la kisiasa kwa kuleta uchonganishi kati ya serikali ya awamu ya nne na iliyopo madarakani.

CUF Yamtega Lipumba, Yamtaka Achukue Upya Fomu za Kugombea Uenyekiti wa CUF

$
0
0

CHAMA cha wananchi CUF kimesema mkutano mkuu wa taifa ambao unategemewa kumpata Mwenyekiti wa chama hicho, upo pale pale, na kuweka msimamo kuhusu Ibrahimu Lipuma kuwa kama anataka kurejea katika nafasi yake achukue fomu.

Tamko hilo ni kufuatia sintofahamu kwa wanachama wa chama hicho kuwa huenda mkutano mkuu usiwepo kutokana na ujio wa ghafla wa Prof. Ibrahim Lipumba aliyekua Mwenyekiti wa chama ambaye alijihudhuru cheo hicho.

Shaweji Mketo, Mkurugenzi wa uchaguzi wa chama hicho amesema tayari fomu za ugombea zimeshapelekwa katika ofisi ya wilaya tayari kwa kujazwa.

“kuanzia 1 Julai washiriki katika ngazi ya Mbali mbali ikiwemo Mwenyekiti wa chama pamoja na Makamu mwenyekiti wachama hicho na wataanza kuchukua fomu hadi Julai 20,” amesema.

Amesema, 21 Agosti baada ya zoezi la ujazaji fomu kukamilika, wajumbe wa Mkutano Mkuu wa chama hicho Kitaifa watakaa kuchagua viongozi hao katika ukumbi wa Land Mark Ubungo Jijini Dar es Salaam.

Lipumba alijihudhuru katika kipindi cha uchaguzi Mkuu 25 Oktoba kutokana na sababu aliyoitoa kuwa ni uwepo wa aliyekua Mgombea urais, Edward Lowassa kuwa alihamia kwenye chama kwa kutofuata utaratibu.

Taarifa kutoka ndani ya chama hicho zinasema kutokana na katiba ya chama, Lipumba hatakiwi kurudi katika nafasi hiyo kwa kutengua kujiuzulu kwake isipokuwa kama anahitaji nafasi hiyo achukue fomu upya kugombea nafasi hiyo katika Mkutano Mkuu wa Taifa

Barua ya wazi kwa Freeman Mbowe na UKAWA wote

$
0
0
Na Thadei Ole Mushi.

Kama ni mfuatiliaji wa siasa za Tanzania mbinu ya wapinzania kutoka njee ya bunge kwa sababu mbali mbali haikuanza leo. Na tangu wameaanza kuitumia mbinu hii haijawahi kuwasaidia au hata kueleweka kwa wananchi badala yake sisi wananchi ndio huwa tunapata hasara.

Kwa mara ya Kwanza wapinzani walitoka njee ya Bunge wakati raisi Kikwete alipoingia madarakani kwa mara ya pili kwa kile walichokidai kuwa ni kutomtambua. Walitoka njee wakati wa kuhutubia bunge na kulifungua bunge.

Je waliposusia bunge mwisho wa siku hawakuja kumtambua raisi Kikwete?? jibu ni NDIO wakikuja kumtambua na walivunja rekodi kupiga hodi ikulu kuomba busara za raisi kuliko vipindi vingine vyote.Tuliwashuhudia wakiburudika na juice mara nyingi tu Ikulu wakipata picha ya pamoja nk.

Mara ya pili tunawaona upinzani ukitoka njee kususia bunge la katiba. Mwisho wa siku bunge liliendelea na katiba pendekezwa ikapitishwa bila kuwa na mawazo mbadala ya wapinzani ndani ya katiba ile inayosubiria kupigiwa kura.

Mara ya tatu upinzani unatoka njee kupinga matokeo ya uraisi yaliyompa raisi Magufuli ushindi. Wanatoka siku ya raisi kulifungua bunge kama walivyotoka kipindi cha Kikwete. Raisi analifungua bunge na baada ya hapo bunge lilelile lililopewa uhalali na rais Magufuli baada ya kulifungua wapinzani wanarudi na kulitumia. Na hata sasa wapinzani wameshamtambua raisi Magufuli kuwa ni raisi halali na aliyechaguliwa kihalali.

Mara ya nne ni hili la kumkimbia Dr Tulia. Katika hali ya kawaida nilifikiri wangelifanya hivi kwa siku moja tu. Mpango wa kususia kila siku kumetuathiri sana sisi wananchi kuliko kulivyomuathiri Dr Tulia. Tena wapinzani wanatoka njee kipindi muhimu kabisa ambacho walipaswa kuombea majimbo yao miradi ya kimaendeleo toka kwenye bajeti ambayo itapitishwa muda mfupi ujao.

Upinzani umetoka kwenye mstari wa kujenga hoja hadi kususia kususia mambo ya ajabu ajabu.Nakiri kabisa kuwa kilichoijenga kambi ya upinzani nchini ni hoja zao nzito miaka ya 2005-2015.

Sote tunakumbuka jinsi upinzani ulivyopata umaarufu kwa kujenga hoja za kukataa ufisadi, kudai katiba mpya, swala la Buzwagi, na hata juzi juzi swala la ESCROW. Kafulila pamoja na kutukanwa tumbili alisisimama kidete hadi akafanikiwa kuwangoa kina Warema bungeni na wengineo. Nataka nikuonyeshe nguvu ya hoja ilivyo na mantiki kuliko hii zomea zomea na kutoka nje ya bunge.

Katika nchi zote za jumuiya ya Madola Tanzania upinzani ndio unaongoza kwa kuthaminiwa kuliko nchi zote. Thamani hii upinzani umeshindwa kuutambua na kuutumia kujijenga badala yake wamekimbia na kinachowakimbiza ni kanuni walizojiwekea wenyewe.

Ni Tanzania tu katika ukanda huu Kambi rasmi ya upinzani inatambulika bungeni, kuwa na baraza la mawaziri kivuli, na baadhi ya kamati nyeti zinazogusa maslahi ya Taifa kuwekewa kanuni lazma ziongozwe na upinzani kama PAC nk.

Hii ni fursa ambayo upinzani walipaswa kuitumia kujitangaza kuliko kuzurura njee ya viwanja vya bunge. Inauma sana kuona wanakosea na hawataki kujirekebisha.

Naamini si wabunge wote wa upinzani wanataka kutoka njee ya Bunge lah hasha. Prof Elton Mayo aliwahi kutoa nadharia ya Hawthorne Effect, nadharia ya kisaikolojia ambapo mtu hufanya jambo kwa kuwa tu kuna mtu anayemsimamia kufanya hivyo au anafanya tu kwa kuwa anajua anaonekana anachokifanya. Hivyo unafanya jambo si kwa kuwa unapenda kulifanya ila unafanya kwa kuwa kuna sababu zinakufanya ufanye.Nikiangalia huu utoto anaoufanya Mbatia pamoja na uelewa wake wote naona madhara ya mob psychology.

MBOWE nakuomba usitumie tena mbinu hii haiwajengi inawabomoa.

Ole Mushi.

MwanaCCM mwenye kujali maslah mapana ya nchi.

Wabunge Wengine Wawili Wasimamishwa Kuhudhuria Vikao

$
0
0
Leo June 17 2016 idadi ya wabunge kusimamishwa imeongezeka baada ya Naibu Sika, Tulia Ackson kutangaza kusimamishwa kwa wabunge wawili ambao ni Mbunge wa viti Maalum CHADEMA Suzan Lyimo na Anatropia Theonest.

Mbune Suzan Lyimo amesimamishwa na Bunge kuhudhuria vikao vitano vya Bunge baada ya kubainika kusema uongo kwamba Jeshi la polisi nchini limenunua magari 777 ya washawasha wakati ukweli ni kwamba hiyo ni idadi ya magari inayopangwa kuingizwa na jeshi hilo kwa ajili ya matumizi mbalimbali.

Licha ya Mbunge kuonesha ushirikiano kwa kamati ya maadili, haki na madaraka ya bunge, kamati imemwona Mbunge ni mzoefu wa shughuli za bunge hivyo anapaswa kusimamishwa vikao hivyo kuanzia June 17 hadi 24 mwaka huu.

Aidha Mbunge Anatropia Theonest amesimamishwa kuhudhuria vikao vitatu vya bunge kwa kosa la kulidanganya Bunge kuwa waziri wa ardhi na nyumba William Lukuvi alichukua ardhi ya wananchi akiwa mkuu wa mkoa wa Dar es salaam.

Kalala Ammbwaga Muna Love Rasmi, Apata Kifaa Kingine Kikali

$
0
0
Habari ‘hot’ iliyotua kwenye meza ya gazeti hili inadai kuwa lile penzi lililokuwa gumzo mjini kati ya Mwanamuziki Kalala Hamza ‘Junior’ na msanii wa filamu za Kibongo, Rose Alphonce ‘Muna Love’ limevunjika na sasa jamaa huyo amehamishia majeshi kwa mwigizaji aitwaye Mamy Mushi.

Inaelezwa kuwa, sasa hivi Kalala na Mamy wamekuwa ni kama kumbikumbi kwani wamekuwa wakionekana pamoja sehemu mbalimbali za kujiachia.Akizungumzia kumwagana na Kalala, Muna alisema kwa kifupi: “Ni kweli nimeachana na Kalala. Sasa kila mmoja ana maisha yake.”


Kalala ambaye kwa sasa anapiga mzigo kwenye Bendi ya The African Stars ‘Twanga Pepeta International’ hakupatikana kuzungumzia penzi lake jipya ila Mamy alipozungumza na Ijumaa alikiri kumrithi Muna: “Penzi letu wala siyo la kificho, Muna na Kalala ilikuwa zamani, sasa ni zamu yangu.”

Barua ya wazi kwa Freeman Mbowe na UKAWA wote

$
0
0
Na Thadei Ole Mushi.

Kama ni mfuatiliaji wa siasa za Tanzania mbinu ya wapinzania kutoka njee ya bunge kwa sababu mbali mbali haikuanza leo. Na tangu wameaanza kuitumia mbinu hii haijawahi kuwasaidia au hata kueleweka kwa wananchi badala yake sisi wananchi ndio huwa tunapata hasara.

Kwa mara ya Kwanza wapinzani walitoka njee ya Bunge wakati raisi Kikwete alipoingia madarakani kwa mara ya pili kwa kile walichokidai kuwa ni kutomtambua. Walitoka njee wakati wa kuhutubia bunge na kulifungua bunge.

Je waliposusia bunge mwisho wa siku hawakuja kumtambua raisi Kikwete?? jibu ni NDIO wakikuja kumtambua na walivunja rekodi kupiga hodi ikulu kuomba busara za raisi kuliko vipindi vingine vyote.Tuliwashuhudia wakiburudika na juice mara nyingi tu Ikulu wakipata picha ya pamoja nk.

Mara ya pili tunawaona upinzani ukitoka njee kususia bunge la katiba. Mwisho wa siku bunge liliendelea na katiba pendekezwa ikapitishwa bila kuwa na mawazo mbadala ya wapinzani ndani ya katiba ile inayosubiria kupigiwa kura.

Mara ya tatu upinzani unatoka njee kupinga matokeo ya uraisi yaliyompa raisi Magufuli ushindi. Wanatoka siku ya raisi kulifungua bunge kama walivyotoka kipindi cha Kikwete. Raisi analifungua bunge na baada ya hapo bunge lilelile lililopewa uhalali na rais Magufuli baada ya kulifungua wapinzani wanarudi na kulitumia. Na hata sasa wapinzani wameshamtambua raisi Magufuli kuwa ni raisi halali na aliyechaguliwa kihalali.

Mara ya nne ni hili la kumkimbia Dr Tulia. Katika hali ya kawaida nilifikiri wangelifanya hivi kwa siku moja tu. Mpango wa kususia kila siku kumetuathiri sana sisi wananchi kuliko kulivyomuathiri Dr Tulia. Tena wapinzani wanatoka njee kipindi muhimu kabisa ambacho walipaswa kuombea majimbo yao miradi ya kimaendeleo toka kwenye bajeti ambayo itapitishwa muda mfupi ujao.

Upinzani umetoka kwenye mstari wa kujenga hoja hadi kususia kususia mambo ya ajabu ajabu.Nakiri kabisa kuwa kilichoijenga kambi ya upinzani nchini ni hoja zao nzito miaka ya 2005-2015.

Sote tunakumbuka jinsi upinzani ulivyopata umaarufu kwa kujenga hoja za kukataa ufisadi, kudai katiba mpya, swala la Buzwagi, na hata juzi juzi swala la ESCROW. Kafulila pamoja na kutukanwa tumbili alisisimama kidete hadi akafanikiwa kuwangoa kina Warema bungeni na wengineo. Nataka nikuonyeshe nguvu ya hoja ilivyo na mantiki kuliko hii zomea zomea na kutoka nje ya bunge.

Katika nchi zote za jumuiya ya Madola Tanzania upinzani ndio unaongoza kwa kuthaminiwa kuliko nchi zote. Thamani hii upinzani umeshindwa kuutambua na kuutumia kujijenga badala yake wamekimbia na kinachowakimbiza ni kanuni walizojiwekea wenyewe.

Ni Tanzania tu katika ukanda huu Kambi rasmi ya upinzani inatambulika bungeni, kuwa na baraza la mawaziri kivuli, na baadhi ya kamati nyeti zinazogusa maslahi ya Taifa kuwekewa kanuni lazma ziongozwe na upinzani kama PAC nk.

Hii ni fursa ambayo upinzani walipaswa kuitumia kujitangaza kuliko kuzurura njee ya viwanja vya bunge. Inauma sana kuona wanakosea na hawataki kujirekebisha.

Naamini si wabunge wote wa upinzani wanataka kutoka njee ya Bunge lah hasha. Prof Elton Mayo aliwahi kutoa nadharia ya Hawthorne Effect, nadharia ya kisaikolojia ambapo mtu hufanya jambo kwa kuwa tu kuna mtu anayemsimamia kufanya hivyo au anafanya tu kwa kuwa anajua anaonekana anachokifanya. Hivyo unafanya jambo si kwa kuwa unapenda kulifanya ila unafanya kwa kuwa kuna sababu zinakufanya ufanye.Nikiangalia huu utoto anaoufanya Mbatia pamoja na uelewa wake wote naona madhara ya mob psychology.

MBOWE nakuomba usitumie tena mbinu hii haiwajengi inawabomoa.

Ole Mushi.

MwanaCCM mwenye kujali maslah mapana ya nchi.

Diamond asema 90% ya bifu za wasanii wa bongo zinazozungumzwa sio bifu kweli

$
0
0
Mkali wa muziki na CEO wa label ya WCB, Diamond Platnumz amesema 90% ya bifu ambazo zinazungumzwa na waandishi wa habari na kukuzwa sio bifu za kweli.
Simba

Akiongea na waandishi wa habari hivi karibuni, Diamond amesema kuna bifu nyingi zinakuzwa na waandishi wa habari lakini kiundani unakuta sio bifu kweli.

“Mimi nikiangalia karibu 90% ya wasanii wa Tanzania ambao watu wanadhani wanamatatizo, sio kweli wanamatatizo,” alisema. Diamond. “Kuna baadhi ya vyombo vya habari vinatumia hiyo nyenzo ili kutengeneza maslahi binafsi, mimi nakwambia ukweli kabisa, kwa sababu watu wengi ambao wanasema wanamatatizo hawana matatizo, wangekuwa wana matatizo tungesikia mtu akisema mimi nikikutana na flani nitamtia ngumi ya meno,”

Aliongeza, “Ukitaka kuamini kama ni uongo, juzi tukilisikia kuna bifu kati ya Shilole na Vanessa lakini kesho yake wakafanya show, hamna ugomvi,”

Pia muimbaji huyo amevitaka vyombo vya habari kuandika habari ambazo zina tija kwa wasanii na taifa kwa ujumla.

“So kama tulivyowaomba mwanzo, tunaviomba vyombo vyetu, na tunawaomba sana sana mtutengenezee umoja kwa wasanii ili tuweze kusaidia familia zetu. Watu wanapogombana tunatia vita katika sanaa, familia, watu kulogana, tuwapumzishe nao waganga wanachoka, tunapeleka hela za bure,” alisema Diamond.


TCRA na uzimaji wa simu: Ni sanaa, propaganda, utani au ufinyu wa teknolojia?

$
0
0
Kwa Karibu mwezi mzima kumekuwa na Habari ya Kitaifa kuhusu Kuzimwa kwa simu feki.

Tukapewa na namna ya kuzitambua hizo simu feki kupitia mfumo wa namba za IMEI (International Mobile Station Equipment Identity).

Huu utaratibu ulikuwa unatambua IMEI ambazo ni "null" yaani hazipo kabisa na nyingine ambazo ni "duplicates" yaani zinashabihiana na simu nyingine ambayo ni halali. Tukaambiwa kutakuwa na uzimaji wa hizo kupitia mtambo au mfumo maalum na wa kisasa kuzinyima fursa ya kupata mtandao (Network Access).

Lakini kinachotokea baada ya muda huo kufika ni simu nyingi kuendelea kuwa hewani mojawapo nimeshuhudia mimi ambayo ina IMEI ya "duplicate" na jina la Darago lakini simu inaonekana ni "Nokia" zikiwa na model tofauti ,na kadhalika kutoka kwa watu wengine ambao walithibitisha kuwa simu zao zitazimwa.

Maswali yangu kadhaa ili kujua hili zoezi ni Sanaa,Propaganda, utani au Ufinyu wa Teknolojia mahususi ni kama ifuatavyo:-

1.Je Elimu haikutolewa vyema kiasi ambacho simu tulizojua zinazimwa hazikuzimwa?

2.Je Teknolojia ya mfumo wa kuzimia ina mapungufu ambayo yameufanya kushindwa kuzizima hizo simu?

3.Zoezi la uzimaji simu:TCRA hawakujiandaa au kufanya majaribio kabla ya kuchukua hatua?

4.Je hakuna siasa katika suala zima linaloendelea kuhusu uzimaji wa simu "Standardization" ?

5.Nini hatima ya wale ambao hawajazimiwa,Je simu zao ni halali kisheria au waendelee kukaa na wasiwasi? (Hapa naweka angalizo Isije kukawa na kesi nyingi za kuflash simu)

6.Maswali mengine Ongeza wewe!!!!!

---------------------------
Nesto E Monduli
Chanika,Dsm

Ndege ya Precision Air Yanusurika Kuwaka Moto Uwanja wa Ndege Zanzibar

$
0
0
Ndege ya Precision Air ikitokea Kilimanjaro kuelekea Dar es salam kupitia Zanzibar usiku wa Alhamisi ili pata hitilafu ya injini yake moja kushika moto wakati ikitaka kuruka Uwanja wa Kimataifa wa Karume wa Zanzibar na kupelekea abiria  kushuka haraka na kurejea sehemu ya mapokezi. Hakuna madhara ambayo yameripotiwa na abiria wote walishuka salama,

Kwa mujibu wa shuhuda wa tukio hilo, mojawapo ya injini ilishika moto  na kulazimisha marubani  kusimamisha ndege na kuirudisha sehemu ya kupakia abiria, baada ya kuchukua hatua za dharura za kuuzima moto huo kabla ya kuleta madhara.

Kampuni ya Precision imethibitisha tukio  hilo na hii hapa tarifa yake rasmi:

 FIRE INCIDENT IN ZANZIBAR
’S KARUME
 INTERNATIONAL AIRPORT
This is an official statement from Precision Air Services PLC with regards to the fire incident that
took place in Zanzibar’s Karume
 International Airport on the 16 th
 of June 2016. Precision Air Services operating its equipment with registration number 5HPWB between Zanzibar and Dar es Salaam registered a fire alarm, on noticing the alarm the pilot immediately initiated standard operating procedures to extinguish the fire and taxied the aircraft back to the apron. This aircraft had operated Dar es Salaam

 Kilimanjaro as PW432 and Kilimanjaro

 Zanzibar as PW2433 with no incidences. No one was harmed during this incidence; all 34 passengers and 4 crew members were safely evacuated and given accommodation for the night. We wish to inform all our passengers and the general public that due to our strict adherence to safety, immediate measures were taken to send another engine from Dar es Salaam. We have also sent a rescue flight to take TCAA officials together with our engineers to conduct required standard investigations for such an event. The same equipment will also airlift the passengers back to Dar es Salaam to continue on their journeys. Precision Air is an IOSA certified airline therefore the safety of our passengers, crew and aircraft is always a priority. We hereby sincerely apologize to all our passengers for any inconveniences caused and would like to assure them that all our other operations will continue as scheduled. We will notify them of any changes or updates.
For more information please Contact: Azda Nkullo

 Head-Marketing & Corporate Communications Email; ankullo@precisionairtz.com Tel: +255 222

Shilole Alia Wasanii Wenzake Kumdhalilisha

$
0
0
Msanii wa filamu na muziki Bongo, Zuwena Mohammed ‘Shilole’ ameonesha masikitiko yake kufuatia madai ya kudhalilishwa na baadhi ya wasanii wenzake kwa kuipa promo video ya wimbo mpya wa zilipendwa wake, Naftal Mlawa ‘Nuh Mziwanda’ wa Jike Shupa.

Kwa mujibu wa Shilole, video ya wimbo huo inaonesha matukio ya kumdhalilisha ambayo inaonekana yeye alikuwa akimfanyia Nuh enzi za uhusiano wao kama vile kumpiga na kumzodoa, mambo ambayo hakuwahi kuyafanya.

“Nimesikitishwa sana na kitendo cha baadhi ya wasanii wenzangu kuiposti video hiyo kwenye mitandao mbalimbali, huko ni kunidhalilisha kwa sababu jamii ikiangalia inaweza kunitafsiri tofauti,” alisema Shilole.

Katika video hiyo, msichana anayefanana na Shilole aitwaye Zuwena aliyetumika kama video queen anaonekana akimfanyia vitimbi Nuh huku akitafsiriwa kuwa, ndivyo Shilole alivyokuwa akimfanyia jamaa huyo.

Hatma ya Kesi ya Chadema Dhidi ya Polisi Kuzuia Mikutano ya Kisiasa Kujulikana Jumatatu June 21

$
0
0
Hatima ya shauri lililofunguliwa na Chadema dhidi ya Polisi kupinga amri ya kupiga marufuku maandamano na mikutano ya kisiasa itajulikana Juni 21, Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza itakapotoa uamuzi kuhusu pingamizi lililowasilishwa na upande wa utetezi kuomba litupiliwe mbali.

Jaji Mohamed Gwae anayesikiliza shauri hilo, alifikia uamuzi huo baada ya kusikiliza hoja za mawakili wa pande zote za utetezi na mleta maombi.

Awali, Mawakili wa utetezi, Robert Kidando na Obadia Kajungu waliomba Mahakama kutupilia mbali maombi ya Chadema kuruhusiwa kufungua kesi yaliyowasilishwa na Mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe, kwa madai kuwa hayajakidhi mahitaji ya kisheria.

Akifafanua, Wakili Kidando alidai mleta maombi hajataja baadhi ya vifungu muhimu ikiwamo kifungu cha 5(1)(2), vinavyoipa Mahakama mamlaka ya kisheria kusikiliza na kuamua maombi hayo.

Madai hayo yalipingwa na mawakili wa Chadema; Gasper Mwanaliela na John Mallya waliodai hoja za wajibu maombi hazina uhalali kisheria kwa sababu hati ya maombi yaliyopo mbele ya Mahakama yamekidhi mahitaji ya kisheria.

Wakili Mallya alidai kisheria, hati ya maombi inapaswa kuwa na vitu vitatu muhimu; hati ya kiapo, maelezo ya mleta maombi na ombi la shauri kusikilizwa kama inavyoelekezwa na kifungu cha 5(3).

Wakili Mallya aliomba Mahakama kutupilia mbali pingamizi la upande wa utetezi na kumpa nafuu mleta maombi, kesi yake kusikilizwa na kuamuliwa.

Baada ya kusikiliza hoja za pande zote, Jaji Gwae aliahirisha shauri hilo hadi Juni 21, Mahakama itakapotoa uamuzi huku akiuagiza upande wa utetezi kuwasilisha hati kinzani kujibu hoja za mleta maombi.

Katika maombi ya msingi, Chadema inaomba Mahakama kutamka kuwa amri ya polisi na utekelezaji wake ni batili, kwa sababu ni kinyume cha katiba na sheria ya vyama vya siasa ya mwaka 1992.

Gwajima Atoweka, Polisi Waendelea Kumsaka Usiku na Mchana

$
0
0
Baada ya kuweka kambi kwa zaidi ya saa saba nyumbani kwa Askofu Josephat Gwajima wa kanisa la Ufufuo na Uzima, Jeshi la Polisi limesema bado linamsaka kiongozi huyo wa kiroho usiku na mchana.

Juzi askari wa jeshi hilo, Kanda Maalumu ya Dar es Salaam walishinda mbele ya geti la nyumba ya askofu huyo kwa zaidi ya muda huo bila kufunguliwa na kuondoka bila kumkamata, hiyo ikiwa ni mara ya pili kwa chombo hicho cha dola kufanya hivyo katika kipindi cha miezi 16.

Baada ya kushindwa kumtia nguvuni mapema mwaka jana, Askofu Gwajima alijisalimisha kituoni siku iliyofuata.

Lakini jana, Gwajima hakufanya hivyo,  na haijulikani alipo. Kamanda wa Kanda ya Dar es Salaam, Simon Sirro amesema wanaendelea kumtafuta askofu huyo na kuwataka wenye taarifa za mahali aliko, waisaidie polisi.

Akieleza sababu za kwenda nyumbani kwake bila ya kumtaarifu askofu huyo, Kamanda Sirro alisema hawalazimiki.

“Si lazima apelekewe taarifa, askari walikwenda kwa nia njema ya kuonana naye ndiyo maana hawakutoa taarifa,” alisema Sirro na kuongeza: “Kama amejificha, tukimbaini alipo tutamkamata na atambue bado tunamtafuta.”

Askofu Gwajima anatafutwa na polisi katika kipindi ambacho mkanda unaodhaniwa una sauti yake, umezagaa kwenye mitandao ya jamii.

Sauti kwenye mkanda huo inasema Rais wa Serikali ya Awamu ya Nne, Jakaya Kikwete afikishwe mahakamani kwa yote yaliyofanyika wakati wa utawala wake ambayo rais wa sasa, John Magufuli anayashughulikia.

Pia, sauti hiyo inadai kuwa baadhi ya viongozi wa CCM wametuma watu mikoani kupiga kampeni ya kutaka Magufuli asipewe uongozi wa chama hicho kwa sasa kama ilivyo utaratibu wa chama hicho.

Wakizungumza  kwa sharti la kutotajwa majina yao kwa kile walichodai si wasemaji wa familia wala kanisa, watu wa karibu na askofu huyo walisema wanashangaa kuona polisi wanamtafuta bila kufuata taratibu kama kumuandikia barua.

Mmoja wa watu hao alisema hadi sasa wanashindwa kufahamu kama waliokuja kwa askofu ni askari kama inavyoelezwa au majambazi kwa sababu hawakuwa na sare wala vitambulisho.

Alisema sababu anayotafutiwa Gwajima ni kukinanga chama, wanaomtafuta ni wana usalama ambao hawatakiwi kuwa na chama kitu ambacho kinatia shaka.

Makachero Watumwa Mwanza na Arusha Kuchunguza Mauaji ya dada wa bilionea Msuya

$
0
0
Jeshi la Polisi Kanda Maalumu Dar es Salaam limetuma timu ya maofisa wake kwenda mikoa ya Arusha na Mwanza kufanya upelelezi wa mauaji ya dada wa bilionea Erasto Msuya, Aneth Msuya.

Hadi sasa jeshi hilo limewakamata watu wanne kwa tuhuma za mauaji hayo, akiwamo mumewe Aneth, mfanyakazi wao wa ndani na hawara wa mfanyakazi huyo.

Kamanda Sirro hakumtaja mtuhumiwa wa nne aliyekamatwa kwa tuhuma za mauaji hayo yaliyogusa hisia za watu.

Aneth aliuawa kwa kuchinjwa na watu wasiojuliana Mei 26 mwaka huu, nyumbani kwake Kibada Kigamboni jijini Dar es Salaam, ambao inadaiwa hawakuchukua kitu chochote ndani na kutoweka.

Sirro alisema alituma maofisa hao kwenda Mwanza na Arusha kufanya upelelezi wa mauaji ya Aneth ili kubaini chanzo chake.

Hata hivyo, hakutaka kufafanua zaidi sababu za kutuma timu hiyo kwenye mikoa hiyo wakati mauaji hayo yalifanyika jijini Dar es Salaam.

“Jeshi la polisi bado tunafuatilia, kwa sasa tumeshatuma maofisa wetu wameenda katika mkoa wa Mwanza na Arusha ili kufanya upelelezi zaidi,”alisema Sirro.

Alisema jeshi hilo linaendelea kuwahoji watuhumiwa wanaowashikilia ili kubaini chanzo cha mauaji hayo, hivyo upelelezi ukikamilika watafikishwa mahakamani.

Bilionea Msuya aliuawa kwa kupigwa risasi zaidi ya 12 na watu wanaosadikiwa kuwa majambazi kandokando ya barabara eneo la Mojohoroni wilayani Hai Mkoa wa Kilimanjaro.

Februari 10, mawakili wanaosimamia kesi ya bilionea huyo, Hudson Ndusyepo, Majura Magafu, Emmanuel Safari na John Lundu, waliiambia mahakama kuwa Serikali inakusudia kuita mashahidi 50 kuthibitisha mashtaka na kuwasilisha vielelezo 40, ikiwamo bunduki iliyotumika katika mauaji hayo.

Mawakili hao walidai mipango ya kumuua bilionea Msuya ilianza Julai 26, mwaka 2013 jijini Arusha, ikiwahusisha washtakiwa hao baada ya kuahidiwa wangelipwa Sh5 milioni kila mmoja.

Askofu Gwajima Atimka Nchini. Adaiwa Kuelekea Dubai

$
0
0
Maoni yangu

Watanzania tuwe makini na wachochezi wanaotumia vibaya uhuru wa maoni kama Askofu Gwajima, kwani hawana nia njema na watanzania masikini.

Ikiwa kina gwajima wanauwezo wa kupanda ndege na ndivyo itakavyokuwa pale uchochezi wao utakapoleta machafuko watakimbia nchi na watanzania masikini wasiokuwa na uwezo wa kuapanda ndege wataishia kuteseka wakati wao wakila bata uhaibun

By kalulukalunde

Marafiki wa Isaac, Aliyekuhumiwa Kwa Kumtukana Rais, Wamchangia Mil 4.5 ya Faini

$
0
0
Marafiki wa Isaac Habakuk pamoja na wadau ambao hawakupendezwa na hukumu dhidi yake ya kwenda gerezani miaka 3 au kulipa faini ya milioni 7 kwa kudaiwa kumtukana Rais Magufuli kupitia mtandao wa Facebook kwa kutumia neno bwege wamemkabidhi jumla ya shilingi milioni 4.5 kwa ajili ya kulipa faini kuepuka kifungo gerezani.

Akikabidhi fedha hizo Jijini Arusha mchana wa leo, mwakilishi wa marafiki hao, Ndg Ephata Nanyaro amesema fedha hizo zimekusanywa kutoka kwa marafiki mbalimbali ambao wametafutana kwa njia ya simu na kila mmoja kuchangia kuanzia sh 500 na kuendelea mpaka zikafika kiasi hicho.

Fedha hizo ni makusanyo ya michango ya makundi mawili, moja likiratibiwa na Ephata Nanyaro na lingine likiratibiwa na Malisa Godilistern, wote wanachama wa Chadema na ambao hutumia mitandao ya kijamii kueleza mawazo yao kuhusu mambo mbalimbali.

Nanyaro amesema wameamua kufanya harambee ya kumchangia kijana mwenzao aepukane na dhahama ya kutotumikia kifungo kwasababu kwa jinsi sheria ya makosa ya mtandao ilivyo, kila mwananchi yuko hatarini kupelekwa gerezani kwa sheria hiyo kwasababu inavifungu ambavyo vinakiuka msingi mkuu na uhuru wa binadamu kuwaza na kujieleza.

Madai ya Ndoa ya H Baba Kusambaratika...Flora Mvungi Arudi Kwao

$
0
0
Huku kukiwa na madai ya ndoa ya staa wa Bongo Fleva, Hamis Ramadhan ‘H. Baba’ na mwigizaji Flora Mvungi kusambaratika, mwana mama huyo amedaiwa kurudi nyumbani kwa mama yake mzazi, Kimara jijini Dar.

Awali, mtoa taarifa wetu ambaye ni mtu wa karibu na familia hiyo, amedokeza kuwa chanzo cha Flora kurudi kwao Kimara ni mzozo uliotokea katika hoteli moja iliyopo Magomeni Mwembechai (jina linahifadhiwa).

H.Baba-akiwa-na-mke-wake-Frora-MvungiH.Baba akiwa na mke wake Frora Mvungi
“Mzozo ulikuwa mkubwa siyo kitoto, mastaa wote wanajua, wanajitahidi kuwasuluhisha ili suala lisifike magazetini. Flora alitoa picha zote za mumewe, lakini mama (anatajwa jina mdau mkubwa wa filamu, ambaye hakupatikana) akamshauri arudishe picha hizo ili watu wasishtukie, ndo anaweka kwa shingo upande lakini kwa sasa Flora yupo nyumbani kwao Kimara na H. Baba ametimkia Mwanza,” kilisema chanzo hicho.

Alipotafutwa H. Baba kwa njia ya simu, alikiri kuwa yupo Mwanza na mkewe yupo kwao Kimara lakini hakuna mzozo wowote kati yao.

Alisema hashangazwi na habari hizo kwa sababu siku zote watu wamekuwa wakimuombea mabaya katika ndoa yake, kwanza walianza hivyo tangu walipooana wakidai wasingeweza kufikisha mwaka mmoja wakiwa pamoja.

“Kuna watu wanatuombea mabaya tangu zamani, sisi tupo imara na hakuna wa kututenganisha isipokuwa Mwenyezi Mungu,” alisema H. Baba na kuongeza kuwa;

“Mke wangu kweli yupo kwao kwa sababu kila nikisafiri yeye huenda huko ambapo hukaa wiki au zaidi na ninaporudi naye hurejea. Ameenda na watoto wote na kule nyumbani kwangu wapo wadogo zangu.”

Chanzo:Global Publishers

Petit Man: Sipo tena Endless Fame..lakini Sina Tatizo na Wema Sepetu.

$
0
0
Aliyekuwa meneja wa wasanii walikuwa kwenye kampuni ya Endless Fame chini ya Wema Sepetu,PetitMan amesema kuwa kwa sasa hayupo tena kwenye kampuni hiyo kutokana na matatizo ya kifamilia lakini hata tatizo na Wema Sepetu na kuwa wanaongea kama kawaida.

‘’Endless Fame nilikuwa kama ‘Coordinator’ na pia nilikuwa meneja wa wasanii, kwa sasa hivi nimesimama kufanya kazi Endless kutokana na matatizo yetu ya kifamilia na unajua ile kampuni ni kama familia yangu nimekaa nayo kwa miaka tisa, nimeishi na Wema Sepetu zaidi ya miaka tisa kwahiyo siwezi kusema kitu chochote kwenye media kwa sababu sina tatizo na Wema wala Martin Kadinda, matatizo yametokea upande mwingine, kuna tofauti ilitokea kati yangu mimi na Mirror lakini sasa hivi tuko poa’’ Alisema PetitMan akiwa kwenye kipindi cha Leo Tena.

Ray C Apelekwa Sober house Bagamoyo, Uongozi wa Sober Wazungumzia

$
0
0

Muimbaji mkongwe wa muziki nchini, Rehema Chalamila ‘Ray C’ Ijumaa hii amepelekwa Life and Hope & Rehabilitation Centre (Sober House) iliyopo Bagamoyo kwa ajili ya kusaidiwa kuanacha na matumizi ya Madawa ya kulevya, uongozi wa sober hiyo umethibitisha.


Hatua hiyo imekuja ikiwa ni siku moja toka aonekane katika video iliyosambaa katika mitandao ya kijamii ikionyesha jinsi anavyosaidiwa na jeshi la polisi baada ya kudaiwa kutaka kijichoma kisu.


Mmoja kati ya wasimamizi wa kituo cha Life and Hope & Rehabilitation Centre (Sober House) ambacho pia kilimsaidia Chidi Benz kuachana na matuzi ya Madawa ya kulevya, Karim Banji, amesema kuwa ni siku moja toka Ray C apelekwe katika kituo hicho.


“Kweli jana tumempokea Ray C, na kusema kweli kwa sasa siwezi zungumzia maendeleo yake kwa sababu ni siku ya kwanza, lakini leo mchana amekula vizuri na nimemuacha amepumzika,” alisema Karim.


Pia alisema bado hajajua Ray C atakaa kwa muda gani ndani ya sober house.


“Kusema kweli mgonjwa akiletwa hapa, atapimwa afya na baada ya hapo anawekwa katika chumba maalum kwa siku tatu ili aweze kukabiliana na hali ngumu, na baada ya hapo ataendelea na matibabu ya kawaida, kwa hiyo kikubwa ni kuombea tu,” alisema Karim.

Rais Magufuli Kukabidhiwa Uenyekiti wa CCM July 23 Mwaka Huu

$
0
0
Kitendawili cha Nani Atakuwa Mwenyekiti wa CCM baada ya Kikwete Kimepata Jibu , Sasa CCM wameamua Kumpa Rais wa Sasa John Magufuli Kuendeleza Kijiti
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live




Latest Images