Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104809 articles
Browse latest View live

Producer Nahreel na Kundi la Weusi Kuna Tatizo? Jibu Liko Hapa

$
0
0
Hivi karibuni kumeibuka taarifa kuwa ule ukaribu uliokuwepo mwanzo kati ya kundi la Navy Kenzo na Weusi umepotea tangu yalipofanyika mabadiliko ya studio ya The Industry. Nahreel amesema hilo siyo kweli bado ni washkaji kama zamani tofauti watu wanavyowachukulia.

Navy Kenzo na Weusi wamekuwa watu wa karibu sana hali iliyopelekea watu kuona wivu kwa kusema kuwa Nahreel anawapendelea wasanii hao kwa kuwatengenezea beat nzuri zaidi ya wasanii wengine.

Akiongea na Bongo5, Nahreel amesema kuwa wao na Weusi bado ni washkaji na bado wana kazi zao kwenye studio yake hazijatoka.

“Ni kweli utaratibu umebadilika na mimi kama mfanyabiashara mwingine lazima kila siku niendelee kuweka utaratibu fulani,” alisema Nahreel.

“Hapa kati nimekuwa busy na ratiba zangu na focus na Navy Kenzo tumekuwa tuna move hapa na pale kwahiyo unajua Weusi na wao wana mipango yao kama wana muziki siwezi nikawa mimi tu nawacheleweshea time zao, na hapa wana nyimbo nyingi zipo bado hazijatoka,” aliongeza.

Hata hivyo Mei 6 mwaka huu Navy Kenzo walifanya sherehe za kuzindua studio yao ‘The Industry lakini hakuna hata msanii mmoja wa kundi la Weusi aliyehudhuria sherehe hizo.

Chanzo:Bongo5

Breaking News: Jeshi la Polisi Lawatawanya Wanafunzi wa Vyuo Vikuu Dodoma Ambao ni Wafuasi wa Chadema Kwa Kufanya Mahafali Bila Kibali

$
0
0
Jeshi la Polisi mkoa wa Dodoma  limewasambaratisha wanafunzi  wa vyuo vikuu  wanachama wa Chadema ( Chadema Students Organization -CHASO ) waliokuwa wakishiriki hafla ya mahafali katika  Ukumbi wa African Dreams  ulipo Area D mjini Dodoma.

Katika hafla hiyo mgeni rasmi alitarajiwa kuwa Waziri Mkuu Mstaafu, Frederick Sumaye ambapo baadhi ya wanafunzi wamekamatwa baada ya kuwambiwa watawanyike na kurudi majumbani kwao.

Polisi wamesema mikusanyiko  yote ya kisiasa ilishapigwa marufuku, hivyo hata mahafali hiyo ilikuwa batili

Mkurungenzi Sober House Akanusha Ray C Kupelekwa Kituoni Hapo

$
0
0
MKURUGENZI wa Kituo cha Kusaidia Waathilika wa Dawa Za Kulevya, Sober House, kilichopo Bagamoyo, Pwani, Karim Banji amekanusha taarifa zinazosambaa kuwa mwanamuziki mkongwe wa Bongo Fleva, Rehema Chalamila ‘Ray C’ amepelekwa katika kituo hicho.

Akizungumza na mtandao huu uliofunga safari mpaka kituoni hapo, Karim alisema kuwa ni kweli siku ya jana (Ijumaa) alipokea taarifa kutoka kwa watu wa karibu wa mwanamuziki huyo kuwa wangempeleka kituoni hapo leo (Jumamosi), lakini hadi majira ya saa tisa leo mchana hakuwa amepelekwa.

“Jana nilipokea taarifa kwa njia ya simu kutoka kwa mtu aliyejitambulisha kuwa ni mtu wa karibu wa Ray C (hakumtaja jina) kuwa watamleta leo, hapa unaponiona nimefunga safari kutoka Dar kwa ajili ya suala hilo lakini mpaka sasa hajafika, kama ni kweli watamleta, basi nitawajulisha,” alisema Karim.

Baada ya kupokea maelezo hayo kutoka kwa mkurugenzi huyo, mtandao huu uliacha mawasiliano yake kituoni hapo  na kung’oa nanga kusubiri taarifa zaidi.

Naumia Sana Pale Mwanangu Sasha Anapouliza Kuhusu Baba yake – Faiza Ally

$
0
0
Aliyekuwa mke wa Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ ambaye pia ni msanii wa filamu, Faiza Ally amefunguka na kueleza kitu ambacho kinamnyima furaha maishani mwake.
Faiza na mtoto wake Sasha

Muigizaji huyo ambaye aliachana na mume wake ambaye ni mbunge Mbeya mjini, Joseph Mbilinyi aka Sugu, amekuwa akilalamika mara kadhaa kuhusu mume wake huyo ambaye alifanikiwa kuzaa naye mtoto mmoja aitwae Sasha.

“Jambo linalonipa huzuni mara kwa mara ni pale mwanangu Sasha anaponiuliza habari za baba yake, huwa naumia mno. Ila tukio la furaha ambalo siwezi kulisahau ni pale nilipopata uchungu wa dakika kadhaa lakini nilikuja kupata furaha ya maisha yangu yote siku nilipo jifungua, Sasha,” Faiza aliliambia gazeti la Mtanzania.

Hata hivyo, Faiza aliwahi kukaririwa akisema kuwa yupo tayari kuzaa mtoto mwingine na Sugu lakini sio kurudiana naye.

Makamo wa Rais: Wanafunzi wa Vyuo Wanaongoza Kwa Kujiuza Miili yao

$
0
0
Akiongea katika harambee ya kuchangia ujenzi wa bweni la wasichana chuo kikuu cha Mzumbe amesema wanafunzi wa kike wanaosoma vyuo vikuu wanaongoza kwa tabia ya kujiuza miili yao, na kujipanga foleni kwenye hoteli na madanguro, na kuleta aibu kwa jamii
amesema zamani wao wkiwa wanasoma walikuwa wanaishi kwa 'bum' hilo hilo lakini walikuwa hawajiuzi na ameshangaa kwa nini sasa hivi wanafanya hivyo:

Video:

Jionee Mawaziri wa Sudan Kusini Wanavyovyaa

$
0
0
Kulia ni Waziri wa Kilimo na Umwagiliaji huko Sudan Kusini bwana MABIOR GARANG (aliyevaa viatu vyeupe).

Katikati ni Waziri wa Ulinzi aliyevaa kandambili na utepe mwekundu begani,

Kushoto ni Waziri wa Mambo ya ndani ya Nchi, aliyeshika kirungu nje ya ukumbi wa Bunge mjini Juba Sudan Kusini.

SUMAYE: Magufuli Anapandikiza Chuki na Hasira Katika Jamii

$
0
0
Waziri mkuu mstaafu Fredrick Sumayeleo, katika ukumbi wa hoteli ya African Dream mjini Dodoma, amesema ameshangazwa na kitendo cha utawala wa rais Magufuli kutumia nguvu nyingingi kukandamiza uhuru wa maoni kwa kuwa yeye ni mtu aliyechaguliwa kwa njia ya demokrasia ambapo maoni tofauti yanakuwepo na yanaruhusiwa kusemwa
Amesema vitendo hivyo badala ya kuleta amani na utulivu katika jamii ndio vinazidi kuleta hasira na chuki.

Ameongezea kusema kama rais hataki kusemwa basi atangaze rasmi kuwa yeye ni dikteta na atakaye mkosoa atakatwa kichwa au kutupwa gerezani

Video:

Lowassa Atoboa Siri Ya Ujio wa TB Joshua Nchini, Asema Aliitwa na CCM Kumshawishi Akubali Matokeo ya Uchaguzi Mkuu

$
0
0
Aliyekuwa mgombea urais wa Chadema, Edward Lowassa amesema hakuridhika na matokeo ya uchaguzi wa Oktoba 25, na kwa kulijua hilo, ‘watawala’ walimleta rafiki yake kutoka Nigeria, TB Joshua ili amshawishi akubali matokeo.

Lowassa alisema baada ya TB Joshua, muhubiri na kiongozi wa Synagogie Church of All Nations, kukaa naye pamoja na viongozi wengine wa Chadema na kumueleza jinsi ‘walivyoporwa’ ushindi, kiongozi huyo wa kidini alichukia na kusitisha azma yake ya kuhudhuria sherehe za kumuapisha Rais John Magufuli.

TB Joshua aliwasili nchini Novemba 3, siku mbili kabla ya kuapishwa kwa Magufuli kuwa Rais, na alienda Ikulu na baadaye nyumbani kwa Lowassa ambaye alitumia muda mwingi wa ziara yake pamoja naye.

“Walimuita rafiki yangu TB Joshua, wakaenda wakampokea. Alipokelewa na Rais Magufuli, akapelekwa Ikulu akazungumza na Kikwete,” alisema Lowassa.

“Baadaye akawaambia wamlete kwangu. Kweli akaja nyumbani kwangu, tukazungumza naye. Sitaki kusema mengi sana niliyomwambia, lakini moja, nilimwambia ukikubali yale matokeo ndugu yangu, heshima yako itashuka hapa nchini na duniani kwa ujumla,” alisema.

Lowassa alisema hayo jana alipokuwa akizungumza katika mahafali ya Shirikisho la Wanafunzi wa Vyuo Vikuu Wafuasi wa Chadema (Chaso) katika Ukumbi wa Karimjee jijini Dar es Salaam.

Alisema ni kutokana na msimamo na mazungumzo waliyofanya na TB Joshua ndio yaliyosababisha kiongozi huyo wa kidini maarufu barani Afrika kutohudhuria sherehe hizo za kuapishwa zilizofanyika Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Katika hotuba yake, Lowassa alimpongeza Rais Magufuli kwa jitihada anazozichukua za kujaribu kufufua uchumi wa nchi, lakini akasema hakubaliani na mbinu anazotumia.

Alisema anafurahia kumsikia Rais Magufuli akiihubiri nchi ya viwanda, lakini hana imani na lugha anazotumia.

“Rafiki zangu nawasikia na nafurahi sana wanasema wanataka kujenga nchi ya viwanda. Natamani nchi hiyo, lakini lugha hiyo sina imani nayo sana,” alisema.

Alisema haziamini lugha hizo kwa kuwa ni vitu visivyowezekana kutokana na ukweli kuwa viwanda vilivyopo haviwezi kufufuka na kuondoa tatizo la ajira lililopo nchini.

“Wanasema watafufua viwanda, lakini viwanda vilivyopo vili kuwa analojia sasa hivi mambo yote ni ‘digital’. Hicho kiwanda kitafufuliwaje maana hata madukani spea zake hazipo labda zitengenezwe upya,” alisema.

Alisema tatizo lililopo kwa sasa nchini ni la ajira na kwamba hata kaulimbiu yao kwenye kampeni ilikuwa ajira kwa kutambua kuwa wapo vijana wengi waliomaliza vyuo, hawana ajira na kwamba eneo kubwa litakaloweza kuwaajiri ni sekta ya kilimo.

Lowassa, ambaye pia ni mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chadema, alisema anakubaliana na kauli iliyotolewa na Jenerali Ulimwengu aliyoitoa hivi karibuni kuwa Rais Magufuli ameturudisha nyuma miaka 50, akiponda uamuzi wa Serikali kuzuia matangazo ya Bunge kurushwa moja kwa moja.

“Uamuzi ule si mzuri na una matatizo makubwa kwa kuwa ni kuwanyima wananchi haki yao muhimu ya kuwasikiliza wawakilishi wao,” alisema.

Akizungumzia elimu, Lowassa alisema wakati Chadema na Ukawa waliposema watatoa elimu bure kuanzia chekechea mpaka chuo kikuu walikuwa wamejipanga, lakini Serikali imebeba sera hiyo bila kujiandaa.

Aliwapongeza vijana kwa kuwa kiini cha mabadiliko na kusema mpaka sasa akikutana na watoto wadogo wanamsalimia kwa kumwambia “Mabadiliko Lowassa”.

Alisema vijana walifanya kampeni nzuri na kumwezesha kupata kura nyingi zilizowapa ushindi, lakini wakanyimwa ushindi.

“Tulishinda vizuri sana lakini hata hizo walizotupa, zinatosha kuwaambia kuwa tuliwapa kazi ya kutosha. Nyie mnajua, wao wanajua na mimi najua,” alisema.

Lubuva aondolewe
Alisema licha ya kumuheshimu mwenyekiti wa NEC, Jaji Damian Lubuva, anapaswa kutimuliwa kwa kushindwa kuisimamia vyema tume hiyo.

“Tume ya Uchaguzi inapaswa iondoke. It must go na ndio maana nasema iko haja ya kuanza upya kudai Katiba mpya haraka iwezekanavyo,” alisema Lowassa.

“Kama yupo mtu yeyote anayechukia matokeo ya uchaguzi uliopita, suluhisho lake ni kuwa na tume huru ya Uchaguzi itakayotokana na Katiba mpya. Tusipohangaika na Katiba mpya tutarudi palepale.”

Alirudia kauli yake kuwa baada ya uchaguzi kulikuwa na waliomtaka atangaze “kuingia barabarani”, lakini aliwakatalia.

“Tutakuwa tunakwenda Ikulu kwa kufagia barabarani kwa damu za watu. No, tutakwenda Ikulu bila damu za watu wakati wowote na Mungu atatusaidia. Nawaambia wale wote ambao hawakuridhika, mnajua nguvu ya umma lakini msiitumie kuwaumiza watu,” alisema.

Aliwataka viongozi wote wa Chadema kujali maslahi ya wanyonge kwa kuepuka kufanya kazi kwa mazoea.

Meya wa Jiji la Dar es Salaam ambaye ni diwani wa Chadema, Charles Mwita aliwataka wanafunzi kufanya kazi ya kukijenga chama kwani mabadiliko ya kweli yataletwa na vijana.

Muasisi wa Chaso, Pamela Maasaio aliwataka vijana wa Chadema kuachana na siasa za kwenye mitandao na badala yake waende mitaani kupiga kelele na kuweka mikakati ya pamoja.

Rama D Afunguka Kuhusu Yeye na Lady Jay Dee

$
0
0
Mwanamuziki wa R&B nchini Tanzania Rama D, amekanusha vikali habari zilizotapakaa mtandaoni kwamba kwa sasa anatoka kimapenzi na mwanadada Lady Jay Dee, amesema wanaheshimiana sana na haiwezi kutokea kitu kama hicho daima .

Hata hvyo Rama D ameendelea kusema kwamba yeye anamfaham mpaka mpenzi wa mwanadada Lady Jay Dee na kusema hata siku ya show ya ‘Naamka Tena Concert’ alipanda jukwaani kuonesha jinsi anavyomkubali mwana dada huyo.

Rama D anasema anawashangaa sana watu wanaoenda kufanya video zao nje na kusema kwamba haoni sababu ya kufanya video hizo nje kwani hapa nyumbani kuna mazingira ya kutosha kufanya video nzuri zitakazoitangaza nchi.

Video ya Aibu ya Wema Sepetu Yavuja!

$
0
0
 Video ya aibu inayomuonesha msanii maarufu wa filamu Bongo, Wema Sepetu ‘Madam’ akicheza kihasara mbele ya mwanaume imevuja, Risasi Jumamosi linayo kibindoni.

‘Klipu’ hiyo ambayo Wema anaonekana akikata mauno huku suruali aliyokuwa amevaa ikimvuka na kuacha wazi sehemu ya makalio yake, ilivujishwa hivi karibuni na mdau mmoja wa burudani ambaye hakupenda jina lake liandikwe gazetini.

“Hii video niliichukua siku ya ile eventi ya Christian Bella ya kutimiza miaka 10 pale Escape One. Wakati akicheza na msanii wa Kundi la Pah One aitwaye Igwe, Wema alionekana kama alikuwa amelewa, alikuwa akikata mauno lakini aibu zaidi ilikuwa pale ambapo ile suruali yake ilipomvuka na sehemu ya makalio yake kubaki wazi.

“Sidhani kama alikuwa kavaa kufuli, baadhi ya watu waliokuwa wakimkodolea macho walishindwa kuamini kama ni Wema yule wanayemjua,” alisema mnyetishaji huyo.
Baada ya mwandishi wetu kupata nafasi ya kuiangalia mwanzo mpaka mwisho, alijiridhisha kuwa aliyekuwa akionekana kwenye video hiyo ni Wema na kweli alichokuwa akifanya ni aibu tupu.

Aibu yake ni pale ambapo suruali inamvuka na kuacha sehemu zake za siri wazi lakini pia staili ya kumkatikia msanii aliyekuwa akicheza naye kwani jamaa alikuwa ‘akikamatia chini’ huku naye akionekana kutokwa na udenda.

Paparazi wetu alijaribu kumtafuta Wema ili kuizungumzia ‘klipu’ hiyo lakini simu yake kila ilipopigwa ilikuwa haipokelewi.

Chanzo:GPL

Download Application ya Udaku Special Blog Kwenye Simu yako Kutoka Play Store Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi

$
0
0

Download  Application ya Udaku Special Blog Kwenye Simu yako Kutoka Play Store Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi

Bonyeza Hapa CLICK HERE 

Au Bonyeza hii picha hapa chini

Madiwani Misungwi Wakanusha Kumtetea Kitwanga

$
0
0
Baraza la madiwani Halmashauri ya Misungwi limesema halijawahi kutoa kauli ambazo zimesambaa kwenye mitandao ya kijamii kwamba hawakuunga mkono uamuzi wa Rais Dkt. John Magufuli kumfuta kazi aliyekuwa Waziri wa mambo ya ndani Charles Kitwanga.

Taarifa ya baraza hilo baada ya kikao imesema kwamba ''Sii kweli kwamba kuna tamko lolote tulitoa kuhusu kufukuzwa Waziri Kitwanga na wala hatuna uwezo huo, taarifa hizo zibezwe na kupuuzwa.''
Madiwani hao wamesema wanaungana mkono na kauli ya Rais Dkt. John Magufuli kuhusu hapa kazi tu hivyo uamuzi wake alioufanya hawawezi kupingana nao.

Aidha baraza hilo limesema kama kuna mtu alitoa kauli kwa niaba ya baraza hilo siyo sahihi kwani baraza hilo hutoa taarifa zinazohusu mambo yao kwa kutumia vikao maalumu.

Baada ya TCRA Kuzima Simu Feki, Wafanyabiashara Wamepata Soko Jipya la Simu Hizo

$
0
0

Moja ya habari iliyoripotiwa ni hii kutoka gazeti la Mwananchi, yenye kichwa cha habari ‘simu bandia zapata soko Msumbiji, Congo’.

Gazeti hilo limeripoti kuwa Siku mbili baada ya mamlaka ya mawasiliano Tanzania (TCRA) kuzima simu feki, wafanyabiashara wa simu hizo wamepata soko jipya katika nchi za Msumbiji na Congo.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti na gazeti hilo, baadhi ya vijana waliokutwa wakizunguka madukani kuzikusanya, walisema wanazinunua na kuzisafirisha kwenda huko kwa ajili ya kuziuza kwa watumiaji. Walisema katika nchi hizo kuna soko kwa sababu zinakamata mawasiliano kama kawaida.

Gazeti hilo limemnukuu Lawrence Kyondo ambapo amesema wanazinunua kwa bei ya makubaliano na kwenda kuziuza katika soko la nje……….>>>’hatujaanza hii biashara leo, siku nyingi isipokuwa wenye maduka walikuwa bado wagumu kuziuza wakidhani hazitazimwa’

Utameza Mate Kama Fisi! See What This Naughty Swahili LADY was Doing in Private (VIDEO)

$
0
0
Forget about Wadada wa Mjini and their fake dancing styles, Swahili ladies are the real deal.
They have mastered the skills of teasing men with seductive dance moves that leave little to one’s imagination.

See what this hot Swahili lady was doing in her house.

Dakika 90 za Mchezo wa Mpira Zinanichosha - Wema Sepetu

$
0
0
Muigizaji Wema Sepetu, amesema mchezo wa soka unamchosha kuangalia kwa kuwa unatumia muda mrefu wa dakika 90 huku wachezaji wake wakihangaika mno kutafuta mabao tofauti na mpira wa kikapu (Basketball).

Wema anasema mara nyingi akiwa nyumbani kwake hupenda kuangalia mpira wa kikapu kwani hauchoshi na wachezaji huwa wanatumia muda mfupi kupachia mabao.
Ili aangalie soka na kumaliza muda wote wa mchezo ni lazima awe na kampani yake na mara nyingi iwe laivu uwanjani

Kinachomtesa Raisi Magufuli ni Woga

$
0
0
NCHI inatikisika. Kilicho nyuma ya mtikisiko huo ni woga wa mkuu wa nchi, Rais John Magufuli, tena woga usio na mchungaji, anaandika Faki Sosi.
Mambo mengi yanayoonekana kumpoteza Rais Magufuli kwenye nyoyo za Watanzania ni yale anayoweza kuyatibu.

Bila shaka, kama angekaa na wasaidizi wake na wasaidizi hao wakaondoa woga, Rais Magufuli angeendelea kutawala nyoyo za wananchi.
Rais Magufuli hapendi kukosolewa, anapotokea mtu na kumkosoa, huumia na kuhemuka, hili ndio tatizo kuu.

Katika hili, amepishana kwa asilimia kubwa na mtangulizi wake, Rais Mstaafu, Jakaya Kikwete. Mkwere huyu (Kikwete) kwake maneno hayakuwa tija.

Na kama yalikuwa yakimuumiza basi aliwezi kuhimili mihemuko yake ingawa kwenye utawala wake waandishi waliathirika kwa kuvamiwa na wengine kuuawa.
Kwenye utawala wa Rais Kikwete, watu walikuwa huru kusema, kujadili na hata kugongana mawazo hadharani na kisha mjadala kuhitimishwa bila kutoana ngeu.

Hulka hii haipo kwa Rais Magufuli, anapoguswa hutaka kujitutumua kwa haraka na pale anapojitutumua mara nyingi hukosea. Hana subira.
Lakini pia wapinzani wanaposema jambo hata kama lina ukweli kiasi gani, yeye huliingia kwa pupa hatimaye hujikuta akizama ‘chaka.’

Kinachomtesa zaidi Rais Magufuli ni kutaka kupendwa, kuaminiwa na hata kushangiliwa na kila Mtanzania. Bila shaka atofanikiwa.

Jambo hili ndio linamtia doa kwa kuwa, anaamini kwamba ametawala nyoyo za Watanzania. Anaamini kuwa afanyalo ni lulu kwa Watanzania hivyo anayetokea kumkosoa, anakuwa adui yake.
Haamini kwamba, wapo walio na mawazo mbadala dhidi ya uamuzi wake, mawazo hayo kwake hataki kuyasikia. Anayempigia makofi na kumsifu, huyo ndiye rafiki yake, anayemkosoa anajenga uadui naye.

Naamini maisha kama haya ndiyo yanayomliwaza Rais Magufuli, lakini bila shaka hakuna taifa linaweza kuongozwa na kiongozi mwenye fikra za namna hii, asiyependa kukosolewa.
Rais Magufuli hatofurahia kuwa rais kama ataendelea kuwa na tabia hii. Taifa hili limeondoka kwenye mtazamo wa ‘zidumu fikra za mwenyekiti’ anapaswa kunong’onezwa hivyo.
Walio karibu naye wanapaswa kumweleza kuwa, dunia imehama na Tanzania imehama. Anapaswa kuishi kulingana na wakati na kwamba, sasa si zama za giza.

Anapaswa kuelezwa kuwa siku zinasonga mbele, waliomuona shujaa wanaanza kujutia, uamuzi wa kulipuka umewagusa na kuwaumiza.

Mashabiki wake wanaanza kupukutika. Waliomuona jasiri wanamuondoa kwenye fikra hizo, anaonesha kushindwa mapema.
Makundi yanayoonekana kutoridhika na utawala wake licha ya kumpamba wakati na baada ya uchaguzi yanadhihiri.

Wapo waliodhani Rais Magufuli ni shujaa katika utumbuaji majipu, lakini kumbe sivyo. Sakata la Kampuni ya Lugumu limemshusha, halizungumzi na wala hajihusishi. Watanzania wanajiuliza kulikoni? Kaishiwa nyembe ama sindano za kutumbulia?

Wapo wanaojadili ukanda kwamba, uteuzi wake unazingatia hivyo, hawa wanaoneshwa kutoridhishwa na hatua hii. Kundi hili tayari linamtazama tofauti.

Wapo wanaojadili ubaguzi. Ni kwa kuwa Baraza la Mawaziri aliloliunda limetelekeza Wazanzibari. Kwake Wazanzibari huenda si lolote si chochote.

Hii maana yake hata ile idadi ndogo ya Wazanzibari waliompa kura kwenye Uchaguzi Mkuu wa 2015, watazidi kupungua. Hawa si wapumbavu, wanampa muda tu, hisabu yao ipo wazi.
Kundi lingine ni la Waislam, hawa wanaamini kwamba Rais Magufuli amewatelekeza. Wanaibua maswalia kwamba, wao hawajasoma? hawana nafasi kwenye utawala wake? ama hawakumpigia kura?

Wanajiuliza maswali hayo kutokana na uteuzi wake, ni kwa kuwa wanahesabu wanaotemwa na wanaosajiliwa kwenye serikali yake, ni katika ngazi zote.
Bila shaka kuongoza taifa lenye dini mbili na moja ikaonekana kulalamika kuelemewa, yapo madhara lakini tuombe yasitokee. Wapo waliomshangilia kwenye kundi hili na sasa wamemjengea chuki.

Kundi la waliopenda kuangalia matangazo ya moja kwa moja ya Bunge, nalo linamtazama kwa jicho la chuki. Kwa kuwa amezuia kupata huduma hiyo.

Mikutano ya hadhara amezuia, wapo wanaotaka kujua nini kianendela kutoka kwa viongozi wao na katika mkusanyiko ya hadhara. Hawa wamenyimwa uhuru huo, bila shaka amewachukiza.
Mteule wake ndani ya Bunge, Dk. Tulia Ackson, Naibu Spika naye anakwenda kwa filimbi ya bosi wake (Rais Magufuli), yote haya yanaonekana wazi na kuchukiza wengi.

Idadi ya watu wengi waliokuwa wakimshabikia Rais Magufuli inapungua kila kukicha. Rais Magufuli anajitengenezea uadui mwenyewe hivyo anapaswa kujipima.
Katika yote hayo, anapotokea mtu na kukosoa, Rais Magufuli anaingia woga kwamba, wananchi wataelewa na wanaweza kumwona hafai. Hili ndio tatizo kuu.

Fikra hizi ndizo zinazomlazimu kuhakikisha anaminya sauti za wengi. Anachopaswa kuelezwa ni kuwa, woga huu ndio unammaliza na njia rahisi ni kuacha watu waseme na yeye asikilize.
Rais Magufuli anapaswa kujua kwamba, asitegemee kukosolewa na wabunge wa CCM, njia ya kujua wapi anapoteleza ni kuruhusu sauti huru kuvuma.

Chanzo:Mwanahalisionline

Irene Uwoya na Skendo ya Kubakwa!

$
0
0
Untold story! Skendo ambayo haijawahi kuandikwa wala kusimuliwa popote inayomhusu mwigizaji ‘hot’ wa sinema za Kibongo, Irene Pancras Uwoya ‘Mama Krish’ ni juu ya madai ya kubakwa na mfanyabiashara maarufu wa Kihindi jijini Dar (jina linahifadhiwa kwa sasa), alipokuwa na umri wa miaka 18 ambapo kwa sasa ana umri wa miaka 28, Ijumaa limefukunyua na kuinyaka.

Chanzo chetu makini ambacho ni mtu wa karibu wa Uwoya kilichoomba hifadhi ya jina gazetini kilidai kuwa, tukio hilo limekuwa likimtesa Uwoya kwenye maisha yake kiasi kwamba kila akilikumbuka huwa anakosa amani.

KISIKIE CHANZO
“Irene (Uwoya) ana kitu ambacho kinamtesa sana na mara kadhaa amekuwa akiniambia kuwa, ipo siku atakitengenezea filamu, anazungukazunguka sana ila alimdokeza mtu kuwa aliwahi kunusurika kubakwa, labda mkijaribu kumdodosa anaweza kuwapa ukweli,” kilifunguka chanzo hicho na kuongeza:

“Chondechonde asijue tu kwamba mimi ndiye nimewaambia maana alisema skendo hiyo ikiandikwa magazetini na dunia ikajua kilichompata, anaweza akajifungia ndani mwaka mzima kwa aibu.”

UWOYA ANASEMAJE?
Baada ya kuinasa habari hiyo, Ijumaa lilifanya jitihada za makusudi za kumsaka mlimbwende huyo aliyeshiriki Shindano la Miss Tanzania 2006/07 na kushika nafasi ya tano ambapo baada ya kubanwa ipasavyo kwa kuwa alikuwa hataki kusikia habari hiyo, alikiri kunusa skendo hiyo ila akafafanua kuwa, si kweli kwamba alibakwa bali ilibaki ‘kiduchu’ kitendo hicho kikamilike.

“Nikiri tu kwamba ni tukio ambalo sijawahi kulisimulia popote lakini kwa kuwa umenibana, ngoja niseme kilichotokea ili iwe fundisho kwa wengine,” alisema Uwoya na kuendelea:

“Sikumbuki ilikuwa mwaka gani ila ni kweli nilikuwa na kama miaka 18. Nilikuwa na tabia ya kwenda na wenzangu kwenye nyumba ya mfanyabiashara mmoja ambaye alikuwa jirani yetu, Mbezi- Beach (naomba nisimtaje) kuangalia muvi.

“Siku moja, tukiwa kwenye sebule ya tajiri huyo ambaye ana asili ya Kihindi aliyekuwa akiishi peke yake, aliniita chumbani kwake.

“Kwa kuwa tulikuwa tumezoeana sana, sikuwa na wasiwasi wala kudhani angeweza kunifanyia jambo baya. Hee! Ile kuingia ndani si akafunga mlango, wenzangu kule sebuleni hawakujua chochote. Alichokifanya ni kunilazimisha kufanya naye mapenzi kwa nguvu, akaanza kunivua nguo, nikaona hapa nimekwisha.

“Nilichokifanya nilipiga kelele huku nikipiga ule mlango ndipo wale wenzangu walipokuja na kutaka mlango ufunguliwe, jamaa alipoona kimenuka alifungua mlango akatoka nduki na kutokomea nje.”

TAARIFA YAFIKA KWA WAZAZI
Kufuatia tukio hilo, Uwoya alifikisha taarifa kwa wazazi wake ambapo baba yake, Mzee Pancras Uwoya alilivalia njuga na kumfungulia kesi mfanyabiashara huyo, kesi ambayo ilinguruma kwa muda mrefu.

“Ni tukio ambalo liliwashangaza wengi na sikumbuki hasa kilichoendelea ila ninachojua yule mfanyabiashara alitoa fedha nyingi kwa kitendo kile cha kunidhalilisha,” alifunguka Uwoya.

ANAFICHA KUBAKWA?
Alipobanwa juu ya madai kuwa alibakwa ila hataki watu wajue kuwa alifanyiwa kitendo hicho, Uwoya alisema: “Kwa kweli hakufanikisha azma yake, alilazimisha kunivua nguo kweli lakini hakufanikiwa baada ya mimi kupiga kelele.

KWA NINI AMEFUNGUKA LEO?
“Nimeamua kuliweka wazi kwa kuwa umenibana juu ya ishu hiyo na ili watu wajue kwamba sijawahi kukwaa skendo ya kubakwa ‘pasee’ ila nilinusurika kubakwa. Lakini pia nimefanya hivi ili kuwapa fundisho wasichana wengine kutomuamini kila mtu, kwani aliyetaka kunifanyia kitendo hicho ni mtu ambaye sikumdhania.”

Hizi ni Aina Kumi za Dawa Ambazo Hazipatani Kabisa na Pombe

$
0
0
Kumekua na kesi mbalimbali za vifo sababu ya watu kumeza dawa kisha kujisahau na kunywa pombe.hii ni changamoto kubwa sana kwenye sekta ya afya..kawaida dawa yeyote anayopewa binadamu kutibu kitu fulani ni sumu na ikichanganywa na baadhi ya kemikali kama pombe huweza kudhuru na kuua kabisa hivyo leo naenda kuzungumzia dawa kadhaa amabazo ukiona umezimeza usiguse pombe kabisa.

Dawa za kutibu bacteria[antibiotics]; 
hizi ni dawa ambazo hutumika mara kwa mara kwenye jamii kutibu magonjwa mbalimbali kama vidonda, kikohozi, kifua kikuu, madonda ya tumbo na kadhalika.matumizi ya dawa hizi na pombe huweza kuua. mfano fragile. isoniazid,grisiofulvin. lakini pia  na baadhi ya dawa za malaria kama quinine na dawa za ya mseto ya malaria ni hatari zikitumika na pombe.

Dawa za kuzuia damu kuganda[ant cougulant]; 
kuna dawa amabazo hupewa kwa wajawazito mara nyingi kulainisha damu ili isigande....sasa matumizi ya pombe hufanya dawa hizi kushindwa kufanya kazi na kusabisha damu kuganda hivyo kuziba mishipa ya damu ana kuleta kifo..mfano warfin

dawa ya kupunguza mgandamizo wa mawazo[ant depressant];
pombe huingilia kazi ya dawa izi na kufanya dawa hizo ziongezeke kwenye damu kwa kiasi kikubwa kuliko ilivyopangwa. hii humfanya mgonjwa alegee sana mfano amitriptyline.

Dawa za kutibu kisukari[ant diabetic]; 
dawa za kisukari hutengenezwa kwa ajili ya kushusha kiasi kikubwa cha sukari mwilini, sasa matumizi ya dawa hizi na pombe husababisha hali moja kitaalamu kama lactic acidosis... dalili ya hali hii ni maumivu ya misuli,tumbo kuuma na kusikia usingizi.hali hii isipodhibitiwa hospitali huua.mfano metformin vidonge.

Dawa za mafua na aleji;[ant histamine]
hizi dawa hutolewa kutibu mafua, miwasho ya ngozi na kikohozi lakini dawa hizi pia husababisha usingizi na uchovu kila zikitumika.pombe huongeza uzingizi huu na uchovu mara duvu na kufanya mtu ashindwe kazi. mfano promethazine maarufu kama fenigani  na chlropherinamine maleate maarufu kama piriton.

Dawa za magonjwa ya akili;
dawa za akili kama chlopromazine hutolewa kwa wagonjwa wa akili kupunguza dalili a magonjwa haya kwa kuwapa usingizi...sasa matumizi ya pombe huongeza usingizi huu maradufu na kuwafanya washindwe kupumua hivyo huweza kuleta kifo.

Dawa za kutibu madonda ya tumbo; 
mara nyingi madonda hutibiwi na mchahnganyiko wa dawa tatu kitaalamu kama triple therapy, sasa moja ya mchanganyiko huo kama cimetidine, metronidazole,scenidazole au tinidazole hazitakiwi kuchanganywa na pombe kabisa sababu ya madhara ambayo zimeonyesha.

Dawa za moyo;
hichi ni kikundi kikubwa cha dawa ambacho hutumika kutibu matatizo ya moyo. matumizi ya dawa hizi wakati mwingine huingilia mfumo wa kazi wa mwili na kusababisha kizunguzungu na kuanguka wakati wa kusimama mfano methyldopa, hydralazine na isosorbine mononitrate na dinitrate lakini pia matumizi ya pombe hupunguza uwezo wa dawa ya presha kitaalamu kama propanalol na kuzuia uwezo wake wa kufanya kazi.

Dawa za maumivu makali;
kuna dawa za maumivu kali sana ambazo hutolewa kwa wagonjwa wenye maumivu makali kama ya kansa, uzazi na maumivu ya ajali. pombe huongeza wingi wa dawa hizi kwenye mfumo wa damu na kusababisha overdose yaani dawa kua nyingi mwilini pale inapomezwa na pombe hata kama ulimeza dozo sahihi.mfano morphine,pethidine, codeine,meperidine...hali hii huleta kifo mara nyingi kwani wasanii wakubwa kama michael jackson na prince waliuawa na hali hizi.

Dawa za usingizi;
dawa za usingizi kama valium hutumika kwa wagonjwa wenye kushindwa kupata usingizi na wakati mwingine kwenye chumba cha upasuaji. dawa hizi huleta usingizi mkali...matumizi ya dawa hizi na pombe huongeza usingizi huu, hupunguza mapigo ya moyo, hupunguza uwezo wa kupumua, kupoteza fahamu na kifo lakini pia dawa za kifafa kama phenytoin  hupunguzwa uwezo wake na pombe na kushindwa kuzuia uwezo wake wa kuzuia degedege za kifafa.

Mwisho;
kutaja dawa hizi haimaanishi kwamba dawa zote ambazo sijataja hapa zinafaa kunywa na pombe, hapana..kuna dawa bado zinafanyiwa utafiti kama zina madhara zikitumika na pombe lakini pia ni vizuri kujenga tabia ya kutokunywa pombe kabisa kama uko kwenye dozi ya ugonjwa wowote na hata kama una ugonjwa ambao unataka kumeza vidonge maisha yote kama kisukari, presha, ukimwi, kifafa na kadhalika basi ni vizuri ukaacha pombe kabisa.

UDART Wazindua Kadi ya Mabasi Yaendayo Haraka

$
0
0
Kampuni ya UdaRT imeanzisha mfumo mpya wa kadi za kielekroniki kwa ajili ya malipo ya nauli kwa watumiaji wa usafiri wa mabasi yaendayo haraka.

Mkurugenzi mtendaji wa UdaRT, David Mgwassa amesema kadi hizo zitaanza kuuzwa kesho katika vituo vikuu vya mabasi vya Kimara, Ubungo, Morocco, Gerezani na Kivukoni.

Kwa upande wake mkurugenzi wa kampuni ya Maxcom Afrika ambao ndiyo watengenezaji wa kadi hizo, Juma Rajab amesema bei ya kadi hiyo ni Sh 5,000 na itakuwa na Sh 4,500 ndani yake ambazo abiria anaweza kuzitumia kama nauli kwa safari nane.

Ameaema kadi hizo hazitakuwa na namba ya siri na kuwa kiwango cha juu kitakachowekwa katika kadi hiyo ni Sh30,000.

Tanzania Inawahitaji Watu Aina ya Mch. Gwajima Walau Kumi Hivi....

$
0
0
Spin Doctoring ni taaluma ya juu sana katika Ujasusi na ili mtu ujifunze ni lazima uwe na kipaji cha hali ya juu cha maswala hayo, ambacho kimsingi mtu huzaliwa nacho.

Nchini Marekani kuna mtu anaitwa Bob Bekwen, huyu ni jasusi wa CIA, hutumiwa kwenye maswala mengi ya ku spin mambo mengi ndani na nje ya USA hasa kubadili hali ya upepo wa kisiasa,

Nchini Urusi kuna mtu pia anaitwa Lavrov kwa sasa ni waziri wa Mashauri ya nje, huyu ni jasusi wa shirika la ujasusi la FSB, huyu anatumika zaidi kwenye mashauri ya kidiplomasia

Uingereza ina mtu anaitwa Tony Blair, huyu amewahi kuwa Waziri Mkuu wa Nchi hiyo, lakini kwa sasa anatumika kama special spinning doctor ndani ya shirika la Ujasusi la nchi hiyo la M16, na vilevile anatumika kwenye misheni iitwayo "IC" ya nchi hiyo ndani ya G8, katika hilo ameweza kusaidia taifa hilo kwa kiwango kikubwa.

Tanzania pia imekuwa na spinning Doctor wazuri wengi japo sio "majasusi", mathalani Dr Slaa, Tundu Lissu, Zitto Kabwe, John Mnyika, Godbless Lema, Salumu Mwalimu nk. Pia yupo bingwa wa wote Tanzania, huyo sio mwingine ni Abdulahman Kinana, huyu ni mstaafu wa Jeshi la Wananchi Tanzania, ametumia kwa ufanisi mkubwa kipawa chake katika siasa za kijana kwa nyakati zote ndani ya chama hicho, lakini kipawa chake hakikuwahi kuwa na mafaa kwa nchi ya Tanzania zaidi ya angamizo tu.

Ingizo jipya katika medani hizi ni Mchungaji Gwajima huyu ni mmoja ya watu wachache duniani ambao ni special Spinning Doctors ambao taifa limebahatika kuwa nao..... Haimaanishi yeye ni jasusi, lakini tendo alilolitenda lina sura na haiba ya kijasusi.

Kwa uwezo wake wa ku spin mambo, Gwajima ameweza kubadili upepo wa kisiasa ndani ya ccm, na sasa wamebaki kuhaha kumzima, lakini kundi lililonufaika na spinning hizo ambalo kimsingi ndio la wafanya maamuzi ndani ya chama wala halina presha, yaani limeshinda na 23/07/2016 litafunga kitabu cha nyakati za siasa za ubwa.

By Yericko Nyerere
Viewing all 104809 articles
Browse latest View live




Latest Images