Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104809 articles
Browse latest View live

Install Application ya Blog Hii ya Udaku Special Kwenye Simu yako Kutoka Google Play Kusoma Habari Kirahisi

$
0
0

Download  Application ya Udaku Special Blog Kwenye Simu yako Kutoka Play Store Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi

Bonyeza Hapa CLICK HERE 




Vikongwe wawili wauawa kwa tuhuma za uchawi

$
0
0
Vikongwe wawili mke na mumewe wa Kitongoji cha Nyag’holongo, Wilaya ya Bukombe mkoani Geita, wameuawa kwa kutumia silaha za jadi na watu wasiojulikana wakituhumiwa kuwa ni wachawi.

Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Geita, Isack Msengi alisema tukio hilo lilitokea Julai 22 saa tatu usiku nyumbani kwao.

Aliwataja wanandoa hao kuwa ni Machene Magina (80) na Mkewe Genke Bundara (75) ambao waliuawa na wananchi wakiwatuhumu kwa uchawi.

Msengi alisema watu watano wanashikiliwa na polisi na upelelezi wa tukio hilo bado unaendelea. Diwani wa Kata ya Nanda, Jumamosi Mathias alisema kundi la watu ambalo halijulikani lilivamia nyumbani kwa familia hiyo wakati wakijiandaa kulala na kufanya ukatili huo.

Mathias alisema akiwa nyumbani kwake, alisikia kelele za watu wakisema; “Tumechoshwa na hawa wachawi. Kwa kuwa hawa wazee ni majirani zangu, nilianza kuhangaika ili kuona jinsi ya kudhibiti maafa hayo,” alisema Mathias.

 Hata hivyo, alisema kabla ya kutoa taarifa polisi, watu hao waliivamia nyumba hiyo na kufanya mauaji hayo ya kinyama kwa vikongwe hao.

Alilaani kitendo kilichofanywa na watu hao kuwa ni cha kikatili dhidi ya wazee kwani tangu aishi nao kijijini hapo hakuwahi kusikia tuhuma za uchawi dhidi yao.

Mathias alitoa wito kwa wananchi kuacha tabia ya kuwahisi wazee kuwa ni wachawi na kujichukulia sheria mkononi, badala yake wawathamini na kuwalinda kwani wazee ni hazina ya Taifa.

MASKINI Babu Seya Hali yake Kiafya Yawa Mbaya..Apelekwa Muhimbili...

$
0
0
Mwanamuziki nguli nchini anayetumikia kifungo cha maisha jela, Nguza Viking ‘Babu Seya’ anadaiwa yu taaban ambapo amekimbizwa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) kwa matibabu.

Mwandishi wetu alimshuhudia Babu Seya akiwa Muhimbili chini ya ulinzi wa askari magereza watatu na wafungwa wengine watano katika Jengo la Taasisi ya Mifupa na Mishipa ya Fahamu (MOI) huku akiwa amedhoofu.

Haikuweza kujulikana mara moja ugonjwa uliosababisha Babu Seya ahamishiwe Muhimbili kwa matibabu kwa sababu Jeshi la Magereza lina hospitali yake na mwandishi alipoomba kwa mmoja wa askari magereza ili aweze kumsalimia mwanamuziki huyo, hakupewa ruhusa.

Baadhi ya wananchi waliomshuhudia mwanamuziki huyo akiwa Muhimbili na kuingizwa katika chumba cha daktari namba 112 walisema, anavyoonekana ni dhahiri ni mgonjwa kwa sababu hakuwa mchangamfu kama ilivyo kawaida yake.

“Nguza (Babu Seya) mara nyingi huwa mchangamfu lakini leo amekuwa mnyonge, mwili umepungua na hata ngozi yake siyo ang’avu, bila shaka anaumwa sana,” alisema mwananchi mmoja hospitalini hapo.

Hata hivyo, mara baada ya matibabu, Babu Seya aliingizwa katika gari la magereza na kurudishwa Gereza la Ukonga kuendelea kutumikia kifungo chake.

Dodosadodosa ya mwandishi hospitalini hapo ili kujua kinachomsumbua Babu Seya, haikuambulia chochote kwani daktari mmoja alisema ni mwiko kwao kutaja ugonjwa wa mgonjwa bila ridhaa yake na ni kinyume cha maadili ya kidaktari.

“Umeniuliza anaumwa nini, kwanza mimi siye niliyemtibu lakini hata kama ningejua ugonjwa wa Babu Seya, siwezi kukuambia ni unethical (kinyume cha maadili). Lakini kweli ni mgonjwa na ndiyo maana ameletwa hapa kutibiwa,” alisema daktari huyo aliyekuwa nje ya jengo moja akizungumza na mwanamuziki huyo.

Juni 25, 2004, Hakimu Mkuu Mkazi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar, Eddy Lyamuya aliwatia hatiani Babu Seya na wanaye Papii Kocha kwa kupatikana na hatia ya kubaka na kulawiti watoto wa Shule ya Msingi Sinza-Mapambano, Dar na kuwafunga kifungo cha maisha jela huku rufaa ya kesi yao ikiwekwa kiporo kwenye Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu iliyopo jijini Arusha.

‎Kaka‬ wa Rais ‪Obama‬, Malik Obama Atoa Sbabu Sita za Kumuunga Mkono ‪Donald‬ Trump

$
0
0
Malik Obama is disappointed with his brother President Barack Obama so much that he has opted to support Donald Trump whom he will vote for come November 8th.
President Obama’s Kenyan half-brother Malik Obama has bought into Trump’s ideology “Make America Great Again”

Malik has caused a storm after he publicly declared his support for Republican presidential nominee, Donald Trump. In an interview with the Post from his home in Kogelo, Siaya County, Malik said that his brother President Obama had disappointed him and that he would vote for Trump. (Malik has a dual citizenship for Kenya and US.)

He cited six reasons why he will be voting Trump on November 8th.

1. Malik admires Donald Trump
Malik told the Post Donald Trump speaks from his heart adding that he was deeply disappointed by Democrats.
He particularly singled out his brother’s administration as the reason why he switched allegiance to Republican.

2. President Obama failed to prosecute Clinton over leaked mails
Democrat Presidential nominee Hillary Clinton was involved in email scandal back then when she was the Secretary of State.
Hillary emails were leaked when she used private e-mail servers instead of secured ones provided by the US government.
Even though FBI have recommended not prosecuting Hillary for the breach of security for using private e-mail servers, Malik Obama thinks his brother Barack should have pushed for the prosecution of Clinton.
“She should have known better as the custodian of classified information,” Malik told the Post.

3. President Obama and Clinton ‘killed’ Muammar Gaddafi
US was part of NATO-led coalition airstrikes in Libya that saw the death of Muammar Gaddafi and downfall of his administration in 2011.
Malik Obama is annoyed President Obama and Clinton killed the Libyan leader whom he called one of his best friends. (Fact: Gaddafi's convoy was hit by a French airstrike and then rebels killed him afterwards).
Malik dedicated his 2012 biography of his late father Barack Obama Sr. to Gaddafi for making the world a better place.

4. President Obama and Democrats are pro same-$ex marriage
A polygamous Malik Obama (has three known wives though there are claims he has 12) is opposed to same-$ex relationships which his brother President Obama and Democrats at large, have been advocating for.
Malik told the Post he felt like a Republican because they don’t stand for same-sex marriage.

5. President Obama wanted to shut Barack H. Obama Foundation
Malik Obama is director of Barack H. Obama Foundation, a controversial Virginia charity organization named after his father.
Malik started the foundation in 2008 with the aim of bringing development in K’ogelo village, Siaya County.
The charity came under fire when The Post revealed in 2011 that it was an off-the-books operation that hadn’t registered with the state of Virginia and didn’t have tax-exempt status from the Internal Revenue Service (IRS).
IRS later gave Barack H. Obama Foundation a clean bill of health sparking speculations President Barack Obama had intervened.
Even so, Malik claims President Obama hasn’t provided any assistance to Barack H. Obama Foundation and instead he (Barack) wanted to shut it down.
“My brother didn’t help me at all. He wanted me to shut it down when I set it up. He hasn’t supported me at all.” Malik was quoted by the Post.

6. President Obama didn’t support his bid for Siaya gubernatorial race in 2013
Malik Obama failed with honors when he vied for Siaya gubernatorial seat in 2013 after spending close to Kes 2 million in campaign. And he’s blaming President Barack Obama for failing to endorse him as Siaya governor.

Malik expected President Obama to be by his side in his bid to be Siaya governor having been the President’s best man in his wedding, besides being his brother.
But surely, politics in Siaya and the greater Luo nation are determined by who Raila Odinga says ‘Tosha’, There is no way President Obama would have helped Malik won the Siaya gubernatorial seat.
Malik plans to travel to US in November to vote for Trump.

Mashabiki wazishtukia picha za Temba zinazomuonyesha amefunga ndoa

$
0
0

Mashabiki wa muziki katika mitandao ya kijamii wazipokea kiutofauti picha zinazomuonyesha msanii wa muziki kutoka TKM Wanaume Family, Temba akiwa amefunga ndoa.

Huwenda ikawa sio kweli kama mashabiki katika mitandao ya kijamii wanavyozungumza kutokana na rapper huyo kuonekana hivi karibuni akiwa na director Justin Campos wa Afrika Kusini.

Wiki moja iliyopita, Mkurugenzi wa TMK Wanaume Family, Mkubwa Fella alitoa taarifa kwa mashabiki wa muziki kwamba staa huyo anaelekea nchini Africa Kusini kuandaa kazi mpya.


Kupitia ukurasa wa instagram, msani wa kundi la TMK Wanaume Family Chege aliandika:

Naomba sana nisaidieni kumpa hongera amani james kwa jambo hili la kheri
HONGERA sana bro Temba.
Baada ya kauli hiyo, mashabiki katika mitandao ya kijamii wamekuwa na maoni tofauti juu wa picha hiyo.

Mwigane
_Jamani eeh? Uyu jamaa. Si” arishaoa? Au hiyo ni video ya wimbo?

Salehenemganga579

Kweli jamani alioaga uyu.duh nas anakipaji.tena alioaga kiti kama st joseph au st alban dah

Allie_kb

Hii ni nyimbo bila shaka maana @mhtemba alishaowa kipind cha nyuma

tathriba_

mmhhh watu hawataki kutoa kiki wameshtuka

Noti na Sarafu za Shillingi 500 zatoweka

$
0
0

NOTI na sarafu ya Sh 500 zimeadimika kwenye mzunguko wa fedha kwa zaidi ya mwezi sasa, hali inayosababisha adha kubwa kwa wafanyabiashara,imefahamika.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti   mwishoni mwa wiki, baadhi ya wafanyabiashara na makondakta wa mabasi ya daladala, Dar es Salaam, walieleza kuwa kukosekana kwa noti na sarafu ya Sh 500 kunasababisha usumbufu na kuongeza ugumu   katika kurudisha chenji kwa wateja.

Majidi Seifu ambaye ni kondakta wa daladala linalofanya kazi kati ya Kariakoo na Temeke, alisema mbali na kuadimika, noti za 500 zilizopo kwenye mzunguko zimechakaa kwa kiasi kikubwa.

“Noti na sarafu ya Sh 500 imekuwa ngumu kupatikana na kusababisha usumbufu mkubwa kwetu na abiria hususan wakati wa asubuhi.

“Hutulazimu kununua chenji kwa gharama kubwa na kutusababishia hasara  na uchelewaji vituoni,” alisema Seifu na kuongeza:

“Kama ukibahatika kupata noti hiyo inakuwa imechakaa sana na hata ukimpa abiria anaikataa huku  wauza chenji wakipandisha kiwango kutoka  Sh 4,500 hadi  Sh 4,700 kwa noti ya Sh 5000,” alisema Seif.

Mfanyabiashara wa kuuza chenji katika eneo la  Kariakoo, Orimpora Hussein, alisema  upatikanaji wa fedha hizo kwa kwa sasa ni mgumu tofauti na awali kwa vile  inaweza kupita siku siku nzima bila kushika noti wala sarafu ya Sh 500.

“Kawaida kuuza chenji ndogo kama 100 au 200 kwa  Sh 1,000 unauza kwa Sh 800 na chenji ya  50 au 100 ni Sh 700  ikiwa ni bei ya kawaida.

“Kutokana kuadimika kwa noti na sarafu hizo ni fursa kwetu maana chenji ya Sh 5,000 tunauza kwa Sh 4,500 na fedha hizo naona zinazidi kupotea katika mzunguko wa kila siku,” alisema Orimpora.

Alipoulizwa kuhusu hali hiyo, Mkurugenzi wa Huduma za Benki kutoka Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Marcian Kibello, alisema noti za Sh 500 hazitakuwapo katika mzunguko wa fedha kwa vile hazitatengenezwa tena.

“Tangu tulipoitambulisha sarafu ya Sh 500 Oktoba 2014 hatujatengeneza noti tena kwa sababu  zinachakaa na kuharibika mapema ingawa wananchi wanazikataa sarafu.

“Ila sarafu zinapunguza gharama kwa vile zinadumu tofauti na   noti.

“Nashauri taasisi za fedha kuhakikisha zinasambaza sarafu hizo katika mzunguko wa fedha na pia wananchi wazizoee kwa matumizi na  wazichukue sarafu hizo katika benki mbalimbali  kuhakikisha zinakuwapo katika mzunguko,”alisema Mkurugenzi huyo.

Kibello aliwakumbusha wananchi kuwa BoT inatoa huduma ya chenji za sarafu ya Sh 500 kila siku za Jumanne na Alhamisi hivyo wananchi na wafanyabiashara watumie fursa hiyo kuzipata.

Shilole alalamika kufanyiwa udhalilishaji kwenye kivuko cha Kigamboni

$
0
0
Msanii wa Bongo Flava, Shilole amelalamika kupitia akaunti yake ya Instagram kuwa amefanyiwa vitendo vya udhalilishaji katika kivuko cha Kigamboni, jijini Dar es Salaam.



Muimbaji huyo ameishia kulalamika tu na hakutaja hasa kitu gani amefanyiwa.

“Uzalendo maana yake nini??
Je kuna thamani yoyote kuwa mtanzania??
Je jitihada zozote zinazofanywa na wasanii kuitambulisha nchi yao zinathaminiwa??
Jana nimetendewa kitendo cha ajabu katika kivuko cha kigamboni na kutendewa udhalili bila kujali kuwa mimi ni mwanajamii nayegusa maisha ya watu.
Muziki ni biashara, lakini pia tuna nafasi yetu katika kuisaidia jamii na kupeleka ujumbe muhimu.
Tusiheshimiwe tunapohitajika na kudharaulika tunapohitaji tuheshimiwe.
Nimeguswa…. Nimeumia.
Someone should act. @paulmakonda @paulmakonda”

ameandika Msanii huyo

Zitto Kabwe aiunga mkono kauli ya Rais Magufuli

$
0
0
Mwenyekiti wa Chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe ameunga mkono kauli ya rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, John Magufuli kuwataka mawaziri wote wahamie Dodoma.


Akihutubia kwenye maadhimisho ya Siku ya Mashujaa yaliyofanyika kitaifa mkoani Dodoma mapema leo Jumatatu, Rais Magufuli alisema, “Makao makuu yapo Dodoma, Dodoma ndiyo penyewe, haiwezekani wabunge zaidi ya mia saba wanakaa Dodoma na makao makuu ya chama changu ninachokiongoza yapo Dodoma.”

Kauli hiyo inaonekana kupokelewa kwa mikono miwili na Mhe, Zitto Kabwe ambaye ni Mbunge wa jimbo la Kigoma Mjini kwa kusema kuwa uamuzi huo wa rais unapaswa kuungwa mkono na kila Mtanzania.

“Dodoma Kutekelezwa kwa Uamuzi wa kuhamia Dodoma ni sahihi unapaswa kuungwa mkono na Wazalendo wote wa Tanzania,” ameandika Zitto kupitia akaunti yake ya Twitter.

Rais Magufuli anaonekana kukerwa zaidi na viongozi hao wakubwa wa serikali kung’ang’ania Dar es Salaam wakati makao makuu yapo Dodoma na kwa kuonyesha mfano Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa ametangaza kuhamia mkoani humo mapema mwezi Septemba mwaka huu.

Picha: Shilole awatoa udenda mashabiki wake baada ya kuwapa nafasi ya kushika kiuno chake

$
0
0
Msanii wa muziki Zuwena Mohammed ‘Shilole’ amewatoa udenda wakutosha mashabiki wa muziki wake hivi karibuni baada ya kuwapa nafasi ya kushika kiono chake.
prima

Muimbaji huyo ambaye kwa sasa anafanya vizuri na wimbo wake ‘Say My Name’ amefanya tukio hilo katika show yake iliyofanyika Jumamosi iliyopita katika hotel ya Kijiji Beach Kigamboni.

Katika picha mbalimbali ambazo zimesambaa katika mitandao ya kijamii zinamuonyesha muimbaji huyo akishikwashikwa kiuno na mashabiki hao huku wakionyesha kufurahiwa na kitendo hicho.

Pia katika show hiyo muimbaji huyo aliambatana na msanii wake ‘Gaucho’.

Hata hivyo kitendo hicho kimewakasirisha baadhi ya mashabiki wake katika mitandao ya kijamii huku kila mmoja akiongea lake.

Waziri Mkuu kuhamia Dodoma Septemba mwaka huu......Asema akishahamia, Mawaziri na Naibu Mawaziri wote wafuatie mara moja

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema atahamia Dodoma ifikapo Septemba, mwaka huu kuonyesha kuwa Serikali imedhamiria kutekeleza ahadi ilizotoa kwa wananchi.

Ametoa kauli hiyo leo asubuhi (Jumatatu, Julai 25, 2016) wakati akizungumza na mamia ya wakazi wa mkoa wa Dodoma na kuwashukuru kwa ushiriki wao kwenye maadhimisho ya Siku ya Kumbukumbu ya Mashujaa zilizofanyika kwenye uwanja wa Mashujaa, mjini Dodoma.

“Jana nilimwita Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu na kumwambia akamilishe matengenezo kwenye nyumba yangu kwa sababu ninataka kuhamia Dodoma ifikapo Septemba,” amesema na kushangiliwa na mamia ya wakazi wa mji wa Dodoma waliohudhuria maadhimisho hayo.

Amesema tangu Serikali ya awamu ya tano iingie madarakani, kazi nyingi zimefanyika na wananchi wameziona na kwamba sasa hivi kazi iliyobakia ni utekelezaji wa ahadi alizotoa Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. John Magufuli.

“Wananchi kazi mmeziona na sasa tunaenda kwenye utekelezaji. Ninatoa agizo kuwa mawaziri na manaibu wote wahame mara moja kutoka Dar es Salaam na kuja Dodoma. Wana ofisi ndogo Dodoma na kwa kuwa wamekuwa wakiishi wakati wote wa Bunge, wahamie mara moja. Mimi nahamia Septemba, na utekelezaji wake nitausimamia kwa juhudi zote,” alisisitiza.

Amewataka wakazi wa Dodoma watumie fursa hiyo kutunza amani ya nchi na kudumisha umoja uliopo na pia akataka watumie fursa hiyo kujenga nyumba za kuishi za kutosha, nyumba za kulala wageni na hoteli za kitalii ili watu watumishi na wageni wanapokuja wasipate taabu mahali pa kuishi.

Wakati huo huo, mgeni rasmi kwenye maadhimisho hayo, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. John Magufuli katika muda wa siku tatu amerudia kusisitiza nia ya Serikali kuhamia  Dodoma katika kipindi chake cha uongozi ili kutekeleza ndoto ya hayati Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere ya kutaka makao makuu ya nchi yawe Dodoma.

Akizungumza na mamia ya wakazi wa mji wa Dodoma kwenye uwanja wa mashujaa huku akishangiliwa, Rais Magufuli amesema atahakikisha Dodoma inakuwa makao makuu ndani ya miaka minne na miezi minne iliyobakia kwenye awamu ya kwnza ya uongozi wake.

“Kama wabunge karibu 300 na mawaziri na manaibu wao ambao hawafiki 30 wanakaa hapa kwa miezi mitatu na maisha yanakwenda, kama makao makuu ya chama kinachotawala nchi yako hapa sioni sababu ni kwa nini Serikali ninayoiongoza iendelee kubakia Dar es Salaam,” amesema.

Mara kwanza kutoa kauli hiyo, ilikuwa ni Jumamosi iliyopita, Julai 23, 2016 wakati akitoa hotuba yake ya kwanza mara baada ya kuchaguliwa kuwa Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) na Mkutano Mkuu maalum wa chama hicho.

Rais Magufuli amesisitiza wananchi na wanasiasa kutunza amani na kudumisha amani iliyokuwepo nchini. Pia amewataka Watanzania wote kuendelea kuwaenzi mashujaa walioipigania nchi hii.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
S. L. P. 980,  
DODOMA.

JUMATATU, JULAI 25, 2016.

Wolper awa kada rasmi wa CCM, mashabiki wamuita ‘Yuda Iskarioti’

$
0
0
Jacqueline Wolper, muigizaji aliyejipatia umaarufu mwaka jana kwa kuwa bega kwa bega na aliyekuwa mgombea urais kupitia tiketi ya Ukawa, Edward Lowassa, amejiunga rasmi na Chama cha Mapinduzi, CCM.
Wolper alitangaza kujiunga na chama hicho tawala Jumamosi iliyopita kwenye mkutano mkuu uliofanyika Dodoma ambapo pia Rais Dkt John Magufuli alichaguliwa kuwa mwenyekiti mpya.
Muigizaji huyo alishare kwenye Instagram picha ikimuonesha akimpa mkono Rais mstaafu, Dkt Jakaya Kikwete kwenye mkutano huo.
Picha hiyo hata hivyo imesababisha hasira nyingi kwa mashabiki wake ambao ni wapenzi wa upinzani huku wakimfananisha na Yuda Iskarioti kwa madai kuwa amewasaliti Ukawa.
Hizi ni baadhi ya comments:


Wabunge chadema kuhojiwa kwa kukiuka agizo la kutofanya mikutano

$
0
0
Arusha. Jeshi la polisi mkoani Arusha, limewaita kwa mahojiano, mbunge wa Karatu,Wilbroad Qambalo, mbunge wa viti maalumu Mkoa wa Arusha, Cecilia Paresso na Mwenyekiti wa halmashauri ya Karatu,Jubilate Mnyenye kutokana na kupuuza agizo la kutofanya mikutano ya hadhara katika jimbo hilo.

Mwingine ambaye ametakiwa kwenda kuripoti polisi ni Makamu mwenyekiti wa halmashauri ya Karatu, Lazaro Bajuta.

Wakizungumza jana baada ya kukabidhiwa barua za wito wa polisi, Qambalo na Paresso walisema wamestuka kutakiwa kuripoti ofisi ofisi ya Mkuu wa upelelezi mkoa wa Arusha jumatano.

Parreso alisema,walipokea barua jana saa sita mchana na kutakiwa kuripoti kwa RCO, saa nane  lakini wakampigia na kumweleza wana ratiba nyingine tayari waende jumatano na akakubali.

Kamanda wa polisi mkoa wa Arusha, Charles Mkombo alipotakiwa kuelezea agizo hilo alisema yupo likizo.

Simu za Nokia kuja kivingine na mfumo wa Android Nougat

$
0
0
Nokia imeripotiwa kuwa kwenye mipango ya kurejea kwenye soko la smartphone na simu mpya zinazotumia mfumo mpya wa Google, Android Nougat, version 7.0.

Simu hizo zinatarajiwa kuingia sokoni mwishoni mwa mwezi huu na zinatarajiwa kuzuia majina vumbi kama simu mpya za Samsung, Galaxy S7, S7 Edge na S7 Active.

Zitakuwa na screen yenye ukubwa inchi 5.2.

Jux afunguka asema "Kama hakuna wivu basi hakuna mapenzi"

$
0
0
Msanii Jux ambaye sasa ni mpenzi wa Vanessa Mdee amefunguka na kusema kuwa wimbo wake mpya 'Wivu' ambao unafanya vizuri kwa sasa hajaimba kwa ajili ya mpenzi wake Vanessa Mdee.

bali ameimba wimbo huo kutokana na hisia kwani jambo hilo linawakuta wengi ambao wanapendana kweli katika mahusiano yao ya kila siku.

Jux akizungumza kwenye kipindi cha ENEWZ ya EATV alidai kwenye mapenzi kama hakuna wivu kati ya wawili wapendanao hapo kunakuwa hakuna mapenzi ya kweli kati yao kwani wivu ndiyo ishara ya upendo wa kweli.

"Wimbo wa Wivu ni matukio ya kimapenzi ambayo yanatokea kwa watu wengi ila siyo kama nimejiimbia mimi, unajua kabla sijarekodi wimbo ule tukiwa studio niliwauliza wakina Bob Manecky na wengine jamanii mnadhani 'idea' hii inaweza kuwa sawa ndipo hapo wakaniambia ni wazo zuri kwani kwenye mapenzi bila uwepo wa wivu kuna kuwa hakuna mapenzi ya kweli, ndiyo hapo nikajua kumbe suala hili linawagusa watu wengi" alisema Jux.

Mbali na hilo Jux amesema kuwa hivi sasa muzuki unakuwa kama haupo kutokana na ukweli kwamba watu wanatanguliza life style mbele kuliko hata kazi zao na ndiyo maana wasanii wengi wakitaka kutoa kazi zao wanafanya mambo mbalimbali kutafuta kiki ili waweze kutambulisha kazi zao hizo.

"Sipendi sana kuulizwa maswali juu ya Vanessa napenda niulizwe maswali juu ya kazi zangu mimi kama msanii, ili nitangaze kazi zangu mimi ndiyo maana kuna vitu saizi sisi tunavikwepa kwa makusudi, tunataka kurudisha muziki hivyo mambo ya kiki, life style tunataka yakae pembeni" alisema Jux

Vanessa na Jux waenda vekesheni Serengeti, walipofikia kila kichwa hulipa shilingi mil 3.2 kwa usiku

$
0
0
Vanessa Mdee na mpenzi wake Jux wameamua kwenda kupumzika kwa muda kwenye mbuga ya wanyama ya Serengeti. Wawili hao wamelazimika kusimamisha ratiba zao ndefu za muziki na biashara kujionea maajabu kwenye mbuga hiyo maarufu duniani iliyopo wilayani Serengeti, mkoani Mara.

Wamefikia kwenye moja ya hoteli za mbugani bora zaidi duniani, Singita Serengeti Grumeti. Hoteli hizo zinazomilikiwa na wawekezaji wa Afrika Kusini, ni miongoni mwa hoteli zinazotoza gharama kubwa zaidi kwenye mbuga za wanyama barani Afrika.

Wawili hao wamefikia kwenye hoteli ya Faru Faru Lodge ambayo ni miongoni wa himaya za Singita zilizo katikati kabisa mwa mbuga hiyo kiasi ambacho wakati mwingine wageni huwezi kuwaona wanyama wakiwa wamejipumzisha kwenye vyumba vyao.

Kwa mujibu wa gharama za mwaka 2016 za kulala Faru Faru Lodge, katika kipindi hiki kinachojulikana kwa lugha za mbugani kama ‘high season’ ambacho huanzia June 1 hadi Octoba 31, suite ya bei rahisi zaidi (double/twin) hutoza dola 1,500 (zaidi ya shilingi milioni 3.2) kwa mtu mzima, kwa usiki mmoja (per adult per night).

Hiyo ina maana kuwa Vanessa Mdee na Jux wanalipa shilingi milioni 6.4 kwa usiku mmoja kulala Faru Faru Lodge. Hata hivyo Jux alianza kwa kufikia Sasakwa Lodge ambayo ina gharama kubwa zaidi kuliko Faru Faru. Yenyewe bei ya chini kwa usiku mmoja kwenye high season ni dola 1995 ambazo ni takriban shilingi milioni 4.2 za Kitanzania.

Akipost picha ya Vanessa akiwa kwenye Jacuzzi, mbele kukiwa na glasi mbili za champagne, akifurahia mandhari ya mbuga hiyo, Jux ameandika: Day 1 at Sasakwa Lodge was nice but the queen arrived on day 2 so we had to upgrade for that better view Farufaru is almost as dreamy as her #Tanzania #Serengeti #Vacation.”

Naye Vee kwenye picha hiyo hiyo aliyoiweka Instagram, aliandika: Reboot in session #SheKing #OurSingita. Kwenye picha nyingine aliandika #Day 1 at Faru Faru. Much needed vacay. #Safari #Tanzania #Serengeti #Africa #UtaliiwaNdani #OurSingita.”

Tazama picha zaidi:

Makongoro Nyerere Anusurika Ajalini....

$
0
0
Mbunge wa Bunge la Afrika Mashariki, Makongoro Nyerere amenusurika katika ajali baada ya gari lake kuwagonga ng’ombe saba kwenye eneo la Makatanini, Babati mkoani Manyara.

Mtoto huyo wa Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere, alikuwa anatoka Dodoma kwenye mkutano mkuu maalumu wa CCM uliomchagua Rais John Magufuli kuwa mwenyekiti wa tano wa chama hicho kwenda Arusha.

Kamanda wa polisi wa mkoa wa Manyara, Francis Massawe amesema ajali hiyo ilitokea saa 1 usiku jana na kuwaua ng’ombe saba na kondoo mmoja.

Amesema chanzo cha ajali hiyo ambayo haikuwa na madhara ya binadamu, ni mifugo hiyo kuvushwa barabara sehemu isiyo na kivuko rasmi cha mifugo na katika tukio hilo. Mchungaji wa mifugo hiyo, William German alikimbia baada ya ajali hiyo.

SOMA Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumanne ya July 26

$
0
0


Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumanne ya July 26

Hatua iliyochukuliwa na Serikali Kuhusu Madereva 18 Waliogoma Bukoba

$
0
0
JESHI la Polisi Kikosi cha Usalama Barabarani nchini kwa kushirikiana na Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (SUMATRA) imesitisha leseni za madereva 18 kutokana na mgomo walioufanya kupinga wenzao kupelekwa mahakamani.

Wamiliki wa mabasi 12 ambayo madereva hao walikuwa wanaendesha kwenda sehemu mbalimbali nchini, wamepewa siku saba kujieleza ni kwa nini wasifutiwe leseni za kutolea huduma hizo pamoja na kutakiwa kusitisha ajira kwa madereva hao.

Akizungumza na waandishi wa habari jana Dar es Salaam, Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani, Mohamed Mpinga, alisema Julai 23 mwaka huu mkoani Kagera, madereva wa mabasi hayo walifanya mgomo kupinga kitendo cha madereva wenzao kupelekwa mahakamani, kukosa dhamana na kulala rumande kutokana na makosa mbalimbali ya usalama barabarani ikiwamo kuendesha kwa mwendo kasi.

Kamanda Mpinga alisema dereva yeyote atakayeendesha gari kwa kasi ya zaidi ya kilometa 90 kwa saa atafikishwa mahakamani na sio kutozwa faini kama awali ili kuhakikisha matukio ya ajali yanapungua nchini.

Alisema kutokana na hali hiyo madereva wanaoendesha mabasi yanayoanza safari zake kwenye Manispaa ya Bukoba, walisitisha huduma kwa kushinikiza Mahakama iwaachie wenzao waliokamatwa kwa makosa ya mwendo kasi.

‘’Serikali haitavumilia kuona madereva wasiofuata sheria za usalama barabarani na sheria za kazi na ajira. Jeshi la Polisi ndio tunawapa madereva mafunzo, tunasajili vituo vya mafunzo na kuwapa leseni. Hivyo tunasitisha leseni zao kwa mujibu wa sheria kwa kukiuka kanuni za leseni,’’ alisema Mpinga na kuongeza kuwa askari watakaoachia madereva na kampuni za mabasi kutembea kwa zaidi ya kilometa 90 kwa saa watachukuliwa hatua za kinidhamu.

Mkurugenzi wa Sumatra, Gilliard Ngewe, aliyataja mabasi pamoja na madereva waliositishiwa leseni kuwa ni Hussein Tegatega na Miraji Kondo wa Kampuni ya RS Express wanaoendesha basi lenye namba za usajili T 425 DDT aina ya Zongtong linalotoka Bukoba kwenda Dar es Salaam.

Said Omary na Amos Danney wa basi la Kimotico lenye namba za usajili T 966 CDY aina ya Nissan linalotoka Bukoba kwenda Arusha na madereva wanne wa mabasi ya Princess Muro yenye namba za usajili T 166 DCA na T 923 DCT yanayosafiri kutoka Bukoba kwenda Dar es Salaam.

Madereva hao ni Ally Mshuza, Twalibu Ondossy, Costa Andrew na Witness Lema.

Madereva wengine ni Musa Tindwa na Gerald Beti wa Kampuni ya Osaka Raha wanaoendesha basi lenye namba za usajili T 968 CPC linalofanya safari zake Bukoba kwenda Dar es Salaam na Paul Ngussa wa basi lenye namba za usajili T 810 BDW aina ya Scania linalotoka Bukoba kwenda Musoma, mali ya Kampuni ya Bunda Express.

Mchungaji Anthony Lusekelo Adai Lowassa ni Tishio CCM......Asema Uchaguzi Umekwisha, si Busara Kuendelea Kumpiga V ijembe

$
0
0
Mchungaji wa Kanisa la Maombezi (GRC) la Ubungo jijini Dar es Salaam, Anthony Lusekelo maarufu ‘Mzee wa Upako’ amesema kitendo cha viongozi wa CCM kulitaja zaidi jina la Edward Lowassa katika Mkutano Mkuu Maalumu wa chama hicho ni ishara kuwa Waziri Mkuu huyo wa zamani ni tishio.

“Nani! Lowassa…. jina lake kutajwa sana katika vikao vya CCM. Hiyo inaashiria kuwa ni mtu tishio. Ndiyo ni tishio,” alisema Lusekelo jana katika mkutano wake na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.

Lusekelo ambaye hivi karibuni, Rais John Magufuli alishiriki ibada katika kanisa lake, alimzungumzia Lowassa baada ya kuulizwa swali juu ya mtazamo wake kuhusu Mkutano Maalumu wa CCM ambao jina la mgombea huyo wa urais kupitia Chadema na Ukawa lilitajwa na makada wengi wa chama hicho tawala.

Alisema hilo lilidhihirika hata katika mchakato wa CCM kupata mgombea wake wa urais, kutokana na Lowassa kuungwa mkono kwa kiasi kikubwa.

Alisema kitendo cha Waziri Mkuu huyo wa zamani kuzua mjadala katika Mkutano Mkuu wa chama hicho tawala sambamba na wimbi la makada wanaohama vyama vyao, si mambo yanayopaswa kuwa mjadala kwa sababu uchaguzi ulishapita.

Huku akisema: “Sizungumzi haya kwa ajili ya kujipendekeza, sihitaji ukuu wa wilaya,” Lusekelo aliwataka viongozi kukataa kuendeleza uhasama wa kisiasa na chuki kwa maelezo kuwa mwaka huu uwe maalumu kuzika tofauti hizo, kufanya kazi kulijenga Taifa na kuhubiri amani na umoja.

Katika mkutano huo, Lusekelo alipongeza kuimarika kwa vyama vya upinzani akaponda mvutano ulioibuka bungeni akisema kukosa uzoefu kwa Naibu Spika, Dk Tulia Ackson kulichangia huku akiunga mkono kauli ya Rais kuzuia shughuli za siasa na kubainisha jinsi Rasimu ya Katiba ya Tume ya Jaji Joseph Warioba, ilivyopendekeza kupunguzwa kwa madaraka ya Rais.

Jumamosi iliyopita, katika Mkutano Mkuu wa CCM mjini Dodoma, uliomalizika kwa Rais Magufuli kuchaguliwa kuwa mwenyekiti, mzimu wa Lowassa ulitawala kutokana na kila aliyepewa nafasi ya kuzungumza ama kumtaja kwa jina au kwa mafumbo.

Mwenyekiti wa CCM aliyemaliza muda wake, Jakaya Kikwete ndiye aliyeanza kuzungumzia hali ya mchakato wa chama hicho kupata mgombea wake wa urais, kuwa ulikuwa mgumu na majaribu makubwa na kwamba wazee walifanya kazi kunusuru hali hiyo.

Katika mchakato huo, CCM ilikata jina la Lowassa katika hatua za awali, jambo lililosababisha kiongozi huyo kuhama na kundi la wanaCCM na kujiunga na Chadema ambayo ilimteua kuwa mgombea wake wa urais.

Hata hivyo, katika mkutano wake wa jana, Lusekelo alisema katika mchakato wa chama hicho tawala kupata mgombea wake wa urais kulikuwa na watu wenye majina makubwa, akiwamo Lowassa na aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Nje, Bernard Membe.

“Niliwaambia CCM, Membe huwezi kumpuuza, Lowassa naye huwezi kumpuuza maana wanataka madaraka na kwa vyovyote lazima mtapata mtikisiko. Nikawaomba waahirishe suala la kupata Katiba Mpya maana wasingelimaliza na muda ulikuwa mfupi,” alisema na kuongeza: “Kama mwaka huu hautatumika kutibu majeraha yaliyotokea huko nyuma, tutaharibikiwa sana.”

Alisema mchakato wowote wa uchaguzi na kura ya maoni ndani ya vyama huacha mpasuko na watu hutumia dini na ukabila kubaguana, hivyo lazima baada ya uchaguzi mambo hayo yamalizwe.

“Tunapaswa kukumbuka kuwa wote ni Watanzania tusahau uchaguzi. Sasa ni wakati wa kuijenga nchi. Amani inatengenezwa, na Mungu huwapa hekima maana kujenga ni kazi na kubomoa ni rahisi, huu ni mwaka wa uponyaji na kurejesha Taifa pamoja,” alisema Lusekelo.

Alisema kuanza kubagua watu kwa sababu walitoka CCM kwenda Chadema au kutoka Chadema kwenda chama tawala si jambo sahihi huku akitolea mfano mataifa yaliyovurugika kwa kuendekeza siasa za chuki na uhasama.

Yaliyotokea bungeni
Akizungumza yaliyotokea bungeni na kusababisha wabunge wa Ukawa kususia vikao vya Bunge vilivyoongozwa na Dk Tulia, Lusekelo alisema Mtanzania anayejua historia ya nchi yake hawezi kufumbia macho suala hilo.

“Binafsi nawalaumu waliotoka (wabunge wa upinzani) na waliobaki (wabunge wa CCM). Kushindana si kuzuri. Mbatia (James Mbunge wa Vunjo na Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi) na wenzake wanapaswa kujua kuwa naibu spika ni mchanga katika siasa waende naye taratibu maana kapewa ubunge tu na kuwa naibu spika,” alisema.

Huku akiponda uamuzi wa Serikali kufuta urushwaji wa matangazo ya moja kwa moja ya Bunge alisema: “Nashangaa wazee kama Salim (Ahmed Salim – Waziri Mkuu mstaafu), Pinda (Mizengo – Waziri Mkuu mstaafu) na Warioba. Sijui walishindwa nini kukaa na wabunge hawa ili kumaliza tofauti zao.”

Alisema si jambo jema kuongoza nchi kwa mabavu na kusisitiza kuwa hata uhuru ulipatikana kwa mazungumzo.

Mchungaji huyo aliusifu utawala wa Rais Magufuli kuwa una kasi kubwa na kwamba licha ya wananchi kulia ukata, watacheka baada ya mwaka mmoja huku akiwananga wanaomponda Kikwete kuwa hawajui mazuri aliyoyafanya.

Awapongeza wapinzani
Akizungumzia nguvu ya vyama vya upinzani, Lusekelo alisema ushindani wa kisiasa umekuwa mkubwa kutokana na kuimarika kwa upinzani: “Chadema ya sasa si ile ya miaka ya 1990. Wanaongoza miji mikubwa na ukiona chama kina wabunge 40 usikipuuze. Hata nguvu ya mfalme ni watu.”

Mikutano ya siasa
Kuhusu kauli ya Rais kusitisha shughuli za siasa hadi mwaka 2020, alisema jambo hilo linaweza kuonekana baya lakini lina unafuu mkubwa, kwamba Kenya wamelifanya na kufanikiwa kumaliza tofauti za kisiasa.

“Hivi watu 10,000 wakiandamana na kusema Magufuli aliiba kura itakuwaje? Tuna askari wa kuwazuia! Nadhani wanasiasa wafanye kazi ya utawala katika vyama vyao. Tutulie kwanza tutibu majeraha. Hakuna jambo baya kama kuwaongoza watu wenye njaa maana hawana la kupoteza,” alisema.

Hata hivyo, Lusekelo alisema Rasimu ya Katiba ilipendekeza Rais kupunguziwa madaraka na huenda madaraka makubwa aliyonayo Rais yakawa sababu ya nchi kuendelea kuwa na amani.

“Kenya kuzuia maandamano ni ngumu sana lakini hapa kwetu hadi Zitto (Kabwe-Kiongozi wa ACT-Wazalendo) alizuiwa kufanya mkutano wa ndani. Kwetu rais ana madaraka makubwa sana,” alisema huku akiwataka polisi kutekeleza wajibu wao vyema, wakikumbuka kuwa nao ni binadamu.

Zambia yakanusha kumzuia Koffi Olomide kufanya maonyesho

$
0
0
Baada ya kuzagaa kwa tetesi ya kuwa Koffi Olomide amekufutiwa maonyesho yake nchini Zambia kutokana na tukio la hivi karibuni la kumpiga dansa wake aitwaye Pamela, Taasisi ya Kilimo na Biashara ya Zambia ambayo ndio waandaaji wa onyesho hilo wamekanusha tetesi hizo.

Kwa mujibu wa mtandao wa Lusakatimes umeripoti kuwa Taasisi ya Kilimo na Biashara ya Zambia bado inaendelea na maandalizi ya show hiyo.

“Tungependa kuwajulisha wananchi kwa ujumla kuwa mipango maonyesho ya muziki na mfalme wa rhumba Koffi Olomide yaliyopangwa kufanyika tarehe 29, 31 Julai na Agosti 1 bado lipo pale pale. Taarifa ambazo zimezagaa katika vyombo vya habari kwamba Koffi amezuiwa na onyesho limefutwa sio kweli,” taarifa hiyo imesema.

Taarifa iliendelea “Tumesha saini mkataba na Koffi wa kuja na kufanya show katika ukumbi wa Mulungushi International Conference Centre tarehe 29 Julai na zitafuata show za tarehe 31 Julai na 1 Agosti.”

Ijumaa iliyopita akiwa Uwanja wa Ndege wa Jomo Kenyatta, (JKIA) Nairobi, Koffi alinaswa katika video akimpiga teke dansa huyo kwa kilichodaiwa kwamba dansa huyo alikorofishana na mwanamuziki wa kundi hilo aitwaye, Cindy Le Couer ambaye amekuwa na uhusiano wa kimapenzi na Koffi tangu mwaka 2012.
Viewing all 104809 articles
Browse latest View live


Latest Images