Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104809 articles
Browse latest View live

WEMA Sepetu Acharuka..Amshukia Vikali Aliedai Amepata Bwana Mpya Arusha

$
0
0
Mrembo Wema Sepetu amemfungukia mtu anae eneza maneno kwenye mitandao kuwa amepata bwana mpya mkoani Arusha ambapo yupo hivi sasa

Maneno hayo yamemkuna Wema Sepetu na kuamua Kumshukia mtu aliyesema hayo maneno, Soma hapa chini:


‘Soooooooo, Rumor has it That huyu mkaka ndo New Baby…. Maskini ya Mungu…! First & Foremost, Nimeongea nae kwa simu akaniomba niweze kuwa MC and special appearance at his birthday party… I got my paycheck and did my work… Sasa sielewi Mipuuzi na Mi***** inayotokwa mapovu kuuutwaaaaa kunifatilia na maisha yangu…. Nd mimi nasemaje lets jus assume it was True, Ni maisha yangu ryt…. So i dont know where all These Bia**** with LowLives wanakuja na kuanza kufatilia wats goin on in my Life…. God…!!! Nimewakosea nini Mungu wangu…. Maisha yangu yamekuwa ni deal kwenu…. Naongea na wewe unaeuza Nchi za waarabu…. Leave me and my Life alone… I keep saying this jamani, Sijawahi bother na maisha ya mtu… I do my shit…. Huyu kaka simjui na nimemjua on da nyt of his Birthday…. Hata kumuwish sijamuwish…. Nimewish mtu mwingine Birthday ila mijitu mifala inatokwa mapovu….. Sasa labda niseme hivi, Wema ana maisha yake nd anaishi atakavyo yeye… Maisha ya Wema hayamuhusu mtu yoyote mwingine….. And again, My heart belongs to someone else…. Nd I love my baby tooo much…. So mkiwa mnaandika vitu vyenu vya kipuuzi…. Again Im talking to you, Stupid Bi-polar Biatch…. Uwe una uhakika….. Kwani unachotaka kwangu ni nini Mbwa wewe… Wallahy never have I done this in my Life, But this has just pushed my buttons to da extent that I cannot take it anymore…. Nimekaa kimya muda mrefu sana and I aint a person dat talks too much… Ila napigiwa simu nyingi mpaka za demu wake na huyu Ally akilalamika and I had to do this…. I keep telling you unatia huruma, You need a Hug… But nat from me honey… Waarabu siku hizi hawalipi nini…? Usiharibie watu bwaana… Afu ni sababu nilikukataa kuwa karibu na mimi ndo maana umenikaa rohoni au…. Maana nakuskia tu unaongeeaaa utasema u r my Mom…. Leave me the Fuck alone…!!! una bahati sana nina wisdom ila leo ningekutukana mbwa wewe… But naaaaaah I got my siblings tena wadogo goin thru my page so I wouldnt want them to see things they shudnt…. But wewe Nyau… Kuna kitu unachokitafuta kwangu and utakipata soon…. If it wasnt for my baby nisingefanya huu upuuzi But My baby comes first…. I had to do this’. -Wema Sepetu

Kuelekea Siku ya Harusi yake Shamsa Ford Aamua Kuwaomba Msamaha Wote Aliowakosea

$
0
0
Shamsa Ford
Zikiwa zimepita siku chache tu toka habari za Shamsa Ford kutarajia kuolewa na mfanyabiashara Chid Mapenzi kuzagaa mitandaoni , Leo asubuhi kaamua kuwaomba msamaha wale wote aliyowakosea ili aweze kuanza ukurasa mpya bila kinyongo..

Soma hapa alichosema:

SIKU zote tunamuomba Mwenyezi Mungu atusamehe dhambi zetu lakini sisi binadamu tunashindwa kusameana hali ya kwamba hakuna mwanadamu aliyekamilika kama MALAIKA. .Naomba nitumie nafasi hii kumuomba msamaha kila niliyemkosea katika maisha yangu iwe makusudi au kwa bahati mbaya .Naomba utafute nafasi ndani ya moyo wako kunisamehe kwasababu nahitaji kuanza ukrasa mpya wa maisha yangu bila kinyongo na mtu yeyote. .NA ww pia uliyenikosea kwa chochote nataka ujue nimekusamehe kutoka ndani ya moyo wangu. .Mungu atufanyie wepesi wa kila jambo na inshaaallah atupe nafsi za kusameana pale tunapokoseana kwasababu duniani tunapita. ...NAWAPENDA WOTE

Umeneja wa Muziki: Fursa Muhimu Isiyochangamkiwa na Wasomi wa Bongo

$
0
0
Muziki wetu una changamoto nyingi sana zinazoikabili. Mara nyingi tumekuwa tukiangazia yanayofanyika katika muziki wenyewe ambayo ni rahisi kuonekana, mfano aina ya muziki kwa kuigiliziana/mkumbo, au njia wanazotumia wasanii wetu katika Kufikisha kazi zao.

Lakini mimi leo nimeona niangalie upande mwingine kidogo ambao ni fursa kwa wasanii na vijana wengi ambao wanaangalia muziki kama wasanii tu, waandaji, na waongozaji video kama ndio sehemu pekee za kuweza kuingia.

Muziki ni tasnia/sekta kama sekta zingine ambazo hazijajitosheleza ili kujisimamia moja kwa moja kama wenzetu walioendelea, bado pesa zinavuja mahala ambapo kunahitaji usimamizi, bado mambo hayaendi kwa uweledi au kwa mfumo unaotambulika na kuweza kuwafanya vijana (wasanii, waandaaji, waongozaji) wawe matajiri na kuweza kusaidia makundi mengine na
kuongeza pato kwa taifa, ili tujivunie vipaji na uwepo wao.

Hapa naangalia sehemu ya uongozi ambayo inahitajika kuwaongoza wasanii wetu na kuwafanya wawe bidhaa bora ambazo zitaweza kuwasogeza kutoka hapa walipo na kupiga hatua zinazotakiwa mbele, wasanii wamekua wakiipigia kelele serikali irasimishe sanaa lakini bado wanasuasua, sasa inabidi wasanii waamke na kuamua kujinyanyua wenyewe mpaka hapo serikali itakapo amka na kuwaunga mkono, maana ni lazima watakuja tu wakiona mmesogea.

Fursa ipo kwenye umeneja, ni wakati sasa wasomi wetu ambao wana shahada mbalimbali kama masoko, uhasibu, au hata utawala wenye hamasa na sanaa wakatizamia upande huu wa muziki ambao una uhaba wa mameneja katika kuwaongoza wasanii wetu waweze kua na mipango iliyoandaliwa kitaalamu na mikakati mizuri kuanzia kujitengeneza kama bidhaa na muziki kwa
ujumla.

Inaweza kuwa labda nawaza kitu ambacho kinahitaji sijui utaalamu wa kisanaa lakini nachoona wasanii wetu wanahitaji kwa ukubwa ni watu wa kuwasimamia ili wawalipe sio mameneja ndio wawalipie vitu vyote wasanii wetu. Tunahitaji watu ambao watalipwa na wasanii, watakua chini ya wasanii.

Au ni wakati sasa wasanii wetu waanze kuangalia umuhimu wa kupata uongozi ambao utaweza kuwasimamia kila kitu kuweza kufikia malengo yao, uongozi ambao utaweza kuwatafutia matamasha ya kutumbuiza, masoko ya kuuza miziki yao, mpaka makampuni ya kuweza kuingia nayo ubia au kutangaza bidhaa zao au kua mabalozi, pamoja na kuwaongoza katika mstari ulio nyooka.

Maswali huwa najiuliza: Ni wasanii wetu wamekosa uweledi wa kuona umuhimu wa kuwa na watu watakao wasimamia kwa kuwachagua wao? Au ni kumekosekana watu mahiri wa kuweza kuonekana na wasanii ili wapewe hio kazi? Au ni watu wenyewe hawajafunguka na kuona kama kuna fursa ya kwenye muziki?

Au niseme umefika muda wa kutotafuta nani mchawi na kuanza kwa kila mmoja wao (wasanii na wenye uwezo wa kuwaongoza) kwa upande wake aone anaweza vipi kusimama na kuongeza thamani kwa mwenzake na kupeleka hili gurudumu mbele.

Ifike muda sasa wasanii waache kulalamika kuwa kuna wanaowabania, au muziki hauchezwi au serikali haisaidii kutatua matatizo yao na kuanza kuchukua hatua wenyewe kwasababu kwanza ni maisha yao na pili ni faida kwao, kwani ni wao wenyewe ndio walisababisha kusikilizwa, michango ya wengine ilikuwepo
ila ni wao walijianza ndipo wengine wakatokea.

Kuna vitu ambavyo serikali haviwezi kutusaidia mpaka tupige hatua wenyewe, cha kwanza ni hii tasnia, na ili hii tasnia ipige hatua kwa kasi inayostahili, wasanii na wadau waamue kusimama pamoja na kuanza kufanya mambo kitaalamu, kila mmoja awajibike kwa upande wake.

Wenye uwezo wa kuwaongoza wasanii wajitokeze, wasanii waamue kutafuta wenye uwezo wa kuwasimamia. Kila upande ufanye kazi kwa lengo la kuimarisha tasnia hii. Kuna vitu wasanii wetu wanakosa ambavyo vinahitaji maamuzi mazuri ili kusonga mbele.

Kwa pamoja tutafika pale tunapotakiwa kuwepo, kwa pamoja tujenge nyumba moja ambayo kila mtu anahisi anaweza kuijenga bila mchango wa mwingine.

Hii tasnia tamu, hata kwa asiyependa.
Yapasa kushika hatamu, ila mazuri kutenda.
Tena akili timamu, ni nyumba moja twajenga.
Wa karibu yumtamu, na wa mbali hato song

Makala imeandika na
Baraka Jereko

Nafasi za Kazi CVPeople, Bonyeza Hapa

VIDEO: Alichokiongea RC Makonda Kuhusu September 1

$
0
0
August 30 2016 Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda amewataka wananchi kuungana na Jeshi la Wananchi Tanzania katika maadhimisho ya miaka 52 ambayo yatafanyika September 1 2016.
Katika maadhimisho hayo Jeshi la Wananchi pamoja na wananchi wenyewe wataitumia siku hiyo kuchangia damu salama pamoja na kufanya usafi wa jiji.
Lakini RC Makonda amewataka wana Dar es salaam wote pamoja na watanzania kwa ujumla kuondoa hofu ya kuwepo kwa maandamano yanayoitwa ‘UKUTA’

Unaweza kuendelea kumsikiliza RC Makonda kwenye hii video hapa chini…

SERIKALI Yapiga Marufuku Mashindano ya Wanawake Wenye Makalio Makubwa

$
0
0
Serikali ya Burkina Faso imepiga marufu shindano ya kila mwaka kwa wanawake wene makalio makubwa kwa maelezo kuwa shindano hilo halina maadili na linaleta ubaguzi katika jamii.

Tangazo la shindano hilo maarufu kama “Miss Bim-Bim” lililoonyesha wanawake wawili wenye makalio makubwa sana, lilizungua maswali mengi kwenye mitandao ya kijamii nchini humo.

Baada ya watu kukosoa tamasha hilo, Waziri mwenye dhamana, Laure Zongo alisema kazi ya serikali ni kuhakikisha kuwa mwanamke hanyanyaswi na kuwa maoni ya watu kwenye mitandao ya kijamii imemsukuma kuzungumzia tukio hilo.

Mtayarishaji wa mashindani hayo, Hamado Doambahe alisema kuwa walikuwa na lengo la kusifia umbo zuri la mwanamke wa ki-Afrika na wala sio kulenga kufanya jambo lolote baya.

Mashindano ya namna hii yamekuwa yakifanyika katika nchi nyingine Magharibi mwa Afrika na kuwa wanawake wamekuwa na mitazamo tofauti juu ya mashindano haya.

Lowassa, Mbowe Watakiwa Kuripoti Polisi Keshoi Septemba 1

$
0
0
Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama hicho, Edward Lowassa na viongozi wengine waandamizi wameitwa na Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam kwenda kuripoti kesho Septemba Mosi.

Hatua hiyo inatokana na viongozi hao kukamatwa juzi, baada ya kufanya mkutano maalumu wa ndani wa Kamati Kuu, na walipelekwa Kituo Kikuu cha Polisi cha Kanda hiyo na kuhojiwa kabla ya kuachiwa.

Mbali na Mbowe na Lowassa, viongozi wengine wa Chadema waliokamatwa na kutakiwa kwenda Polisi kesho ni Katibu Mkuu, Vincent Mashinji, Naibu wake, John Mnyika na Makamu Mwenyekiti wa Chama hicho, Said Issa Mohammed.

“Wameitwa Polisi waende Septemba mosi kuripoti baada ya jana kukamatwa na kuhojiwa wakituhumiwa kukiuka maagizo ya Polisi,” alisema Msemaji wa Chadema, Tumaini Makene na kufafanua:

“Lakini wanaweza kwenda au wakaanzia kwenye maandamano kisha wakaenda Polisi kuripoti.”

Alisema maandamano hayo yatakuwapo kama yalivyopangwa kwani maandalizi yake yamekamilika.

Habari zaidi zilieleza, kwamba jana mchana viongozi hao walikuwa wakifanya kikao Makao Makuu ya chama hicho Kinondoni Dar es Salaam, ambapo pia walikutana na wabunge wote wa chama hicho kwa makundi tofauti.

Kwa mujibu wa mtoa habari ndani ya Chadema makao makuu katika kikao hicho walijadili mambo mengi ikiwa ni pamoja na suala la utekelezaji wa Ukuta kesho.

Mmoja wa wabunge wa Chadema alisemai kwamba walikuwa wakiwekana sawa kuhusu maandamano yao.

Alibainisha kwamba katika mkutano huo ambao Mbowe hakuwepo pia walijadili maombi ya viongozi wa dini kuwataka kusitisha maandamano hayo Septemba mosi.

“Viongozi wa dini wamekuwa wakituomba tusitishe maandamano ya Ukuta Septemba mosi, tusubiri hadi baada ya mkutano wa vyama vya siasa Septemba tatu,” alisema Mbunge huyo wa Kanda ya Ziwa.

Aliongeza: Katika mkutano huo, Lowassa na viongozi wengine walijadili hayo na ikikubalika kwa heshima ya viongozi wa dini maandamano ya Ukuta yafanyike baada ya Septemba tatu.”

Hata hivyo, mwandishi alishuhudia wabunge wengi wa chama hicho wakitoka katika mkutano huo kimya kimya bila kutaka kuzungumza na kabla muda uliopangwa kwisha, huku taarifa zikieleza kwamba mkutano huo uliahirishwa baada ya kuwepo taarifa za kutaka kuvamiwa na Polisi.

“Tumeambiwa tusambaratike, tutajulishwa wapi tutakutana tena, kama hapa au wapi,” alidokeza mmoja wa wabunge hao.

Baada ya mkutano huo kuahirishwa, Lowassa alitoka eneo hilo huku taarifa zikieleza alikuwa akielekea kwenye moja ya hoteli jijini humo kuungana na Mbowe ambapo walikuwa na mazungumzo na baadhi ya viongozi wa dini.

FAIZA Ally 'Napenda Kuvaa Nusu Utupu, Najipenda Nilivyo Bomba Najua Wengi Mnatamani'

$
0
0
Mrembo Faiza Ally Ameamua Kufunguka haya Hapa Chini:

"Napenda kuvaa half naked - Na najipenda kujiangalia nilivyo bomba Na kuangalia watu wanavyo niponda.... najue wengi mnatamani lkn Ndio hivyo tumeumbwa tofaut....
Msinifananishe na mtu mwenye mzigo nyuma#hakunaga star mnene duniani hlf pia msinifananishe na wenye vijuso Kama katuni - mi niko Na class beauty 😉 I AM DIFFERENT" Faiza Ally

Weka Picha za Utupu Mtandaoni Uende Miaka 20 jela – TCRA

$
0
0
Unataka kwenda jela? Ni rahisi, weka picha za ngono mtandaoni, na utakuwa mkazi wa huko kwa kipindi cha miaka 20.

Kwa mara nyingine tena, mamlaka ya mawasiliano Tanzania, TCRA imewakumbusha watanzania kutozichezea sharubu za sheria ya makosa ya mtandaoni, lasivyo wataishia pabaya.

“Ni vyema wananchi wakatambua kwamba uchochezi kwenye mitandao kwa kusambaza ujumbe wenye viashiria vya uvunjifu wa amani au kuweka picha zisizofaa kwenye mitandao sheria ipo wazi na watu watajikuta wanaishia pabaya, hivyo ni vyema kuchukua tahadhari mapema,” alisema Mhandisi wa Mawasiliano wa Victoria Rulakara wakati akizungumza kwenye kipindi cha Hotmix cha EATV.

Wakati huo huo, mamlaka hiyo imeendelea kutoa elimu kwa wananchi kuhusu matumizi sahihi ya mitandao ikiwa ni pamoja na kuwaonya watu wanaonzisha blog zenye majina ya uongo kutukana watu wengine.

Sheria ya Makosa ya Mtandaoni ilipitishwa mwaka jana na rais mstaafu, Jakaya Mrisho Kikwete.

Afande Sele Mikononi Mwa Polisi Morogoro

$
0
0
Msanii mkongwe wa muziki kutoka Morogoro, Afande Sele amedai anashikiliwa na jeshi la polisi mkoani Morogoro kwa madai anagawa pesa kwa watu ili kuwashawishi wajitokeze katika maandamano ya UKUTA ambayo yamepigwa marufuku.
Afande

Rapper huyo ambaye ni mwanasiasa na aligombea ubunge kupitia cha ACT Wazalendo katika uchaguzi uliyopita, amedai yupo mikononi mwa polisi toka jana.

“Huku ni kushindwa kama sio kufeli, toka jana nipo mikononi mwa polisi eti naambiwa nimeratibu mkutano wa UKUTA , nimechapisha T-shirt na kugawa fedha ili kesho watu waandamane, pia kuaandaa mkutano maeneo ya Msamvu.,” aliandika Afande Sele kupitia facebook yake.

Aliongeza, “Nina zaidi ya mwezi sijakaa maeeneo ya Msamvu zaidi ya kupita nikiwa naelekea mikoani tena nikiwa kwenye gari yangu. Ila hii aibu na fedheha kwa jeshi la polisi, maamuzi ya kukurupuka . Tusubiri,”

Breaking News: Chadema Yatangaza Kuhairisha Operesheni UKUTA...

$
0
0
CHADEMA yatangaza kuhairisha 'Operesheni UKUTA' hadi Oktoba Mosi kutoa nafasi ya mazungumzo kati ya Rais na viongozi wa Dini.

Freeman Mbowe asema wamekutana mara nyingi kwenye vikao na Viongozi wa Dini lakini CCM imekuwa ikigoma kudhuria vikao hivyo Msikilize Hapa:

Diamond Platnumz Anunua Rolls Royce ya $400,000 na zaidi?

$
0
0
Huenda Diamond Platnumz akawa ameitimiza ndoto aliyokuwa nayo kwa miaka mingi – kumiliki gari alipendalo zaidi, Rolls Royce.

Kwa muda mrefu, staa huyo amekuwa akisema kuwa hilo ndilo gari analotaka kulimiki kiasi cha kujipa jina ‘The Rolls Royce Musician From East Africa.’

Diamond ambaye yupo jijini Los Angeles, Marekani alikoenda kushoot video ya wimbo aliomshirikisha Ne-Yo, ameshare kipande cha video kwenye Instagram cha gari hilo na kuashiria kuwa huenda akawa amelinunua tayari.

Hata hivyo hajasema iwapo gari hilo limeshakuwa mali yake ama alikuwa tu showroom kuosha macho!

Rolls Royce, ni magari yanayozalishwa na kampuni ya Uingereza na yalianzishwa na Charles Stewart Rolls na Sir Frederick Henry Royce, March 1906. Bei yake huanzia $300,000 – $500,000.

“Nataka nibadilishe aina ya gari sababu imekuwa ni muda mrefu, nafikiri ni muda wa kuwa na gari nililokuwa nalitamani siku zote, gari la ndoto yangu ni Rolls royce na ndio ninalotaka kulinunua mwaka huu wa 2016 na litakuwa na jina la PLATNUMZ na sio namba za kawaida,” aliiambia tovuti ya Millard Ayo miezi kadhaa iliyopita.

Alidai kuwa kwa alipofikia ni muhimu kwa na gari la hadhi yake ili kujiongezea thamani zaidi.

“Ndio maana nikipata Rolls Royce inatengeneza heshima,” alisema.

Video:Ndege za Kivita za Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Zikivinjari Anga la Jiji la Dar es Salaam Leo Hii

$
0
0
Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) kesho Septemba Mosi litaadhimisha miaka 52 tangu kuanzishwa kwa jeshi hilo. Katika maadhimisho hayo, jeshi hilo limeeleza kuwa litaadhimisha miaka 52 kwa kufanya usafi maeneo mbalimbali nchini.

Leo asubuhi zimeonekana ndege za JWTZ zikafanya mazoezi kati angala la jiji la Dar es Salaam ikiwa ni maandalizi ya maadhimisho ya miaka 52.

Tazama video hapa chini kuonda ndege hizo.


 VIDEO: NDEGE ZA KIVITA ZA JESHI LA WANANCHI WA TANZANIA (JWTZ) ZIKIVINJARI ANGA LA JIJI LA DAR ES SALAAM HII LEO.

Mwanafunzi wa Kidato cha nne Amteka Nyara Mtoto wa Miaka 3

$
0
0
Mwanafunzi  wa kidato cha nne alimteka nyara mtoto wa miaka mitatu baada ya kumpa dawa za kulevya.

Mwanafunzi wa kidato cha nne kutoka shule ya upili ya Maralal kaunti ya Samburu alisemekana kumteka nyara mtoto wa miaka mitatu baada ya kumpa madawa ya kulevya.

Mwanafunzi huyo alienda mafichoni na mtoto huyo, huku akimtaka mamake mtoto  kutoa  Ksh 170,000 huku akidai kumuua mtoto huyo iwapo hangepewa pesa hizo.

Joy Lekimain, mamake mtoto alihofia maisha ya mwanawe, jambo lililomfanya kutuma Ksh 2,500.

“Inaonekana alimpa mtoto dawa za kulevya kabla ya kuenda mafichoni katika kaunti ya Nyahururu,umbali wa kilomita 226 kutoka Maralal. Alipiga simu akitishia kwamba atamdhuru mtoto iwapo hatapewa fidia ya Ksh 170,000 kwa muda wa siku tano,” alisema kamanda wa polisi kaunti ya Samburu,Francis Kumut.

Hata hivyo ilisemekana kuwa mtekaji nyara huyo alikuwa wa jamii moja na mtoto huyo .

Alipatikana siku sita baadae akiwa amejificha kwenye nyumba moja katika mtaa wa Chang’aa kaunti ya Nyahururu.

Katibu wa Chadema Mwanza Akihama Chama, Ahamia CCM

$
0
0
Aliyekuwa Katibu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema mkoani Mwanza, John Nzwalile (kulia), akirejesha kadi ya chama hicho kwa Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM mkoani Mwanza, Dkt.Anthony Diallo katika ofisi za CCM hii leo.

Nzwalile ambaye pia alikuwa Mjumbe wa Mkutano Mkuu Chadema Taifa, Mjumbe Baraza Kuu Chadema Taifa, Mwenyekiti wa Baraza la Mashauriano Chadema Mkoa wa Mwanza, amefikia uamuzi huo baada ya jana kujivua vyeo hivyo.

Amesema amefikia hatua hiyo kutokana na kwamba Chadema imepoteza mwelekeo kwani kimekuwa kikiibuka na oparesheni za kuichonganisha serikali na wananchi huku pia demokrasia ikikosekana ndani ya chama hicho.

"Kama ni udikiteta basi mimi niseme Chadema ndiko kuna udikiteta kwani zaidi ya mara tatu nimemsikia Lowasa (Edward Lowasa, aliyekuwa mgombea urais 2015) akisema yeye ndiye mgombea urais mwaka 2020, kwa kikao gani". Amesema Nzwalile na kuongeza kwamba yale mambo yote mabaya yaliyokuwa yakifanyika ndani ya CCM yamenyooshwa hivyo hakuna haja ya yeye kuendelea kukaa Chadema.

Amesema atazunguka Wilaya zote ili kuhakikisha anawarejesha wengine ndani ya CCM huku akiwa na jukumu moja la kuubomoa Ukuta unaoelezwa kujengwa na Chadema kwani ni ukuta wa tope hivyo atatumia tu maji kuubomoa.

Nzwalile amekaribishwa ndani ya CCM na Mwenyekiti wa Chama hicho mkoani Mwanza, Dkt.Antony Diallo, ambaye pia amewakaribisha makada wengine wa upinzani kuhamia CCM akisema kwamba chama hicho kinaendesha mambo yake kidemokrasia.

Serikali Yashikilia Msimamo Kupinga ndoa za Jinsia Moja

$
0
0
Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imeendelea kushikilia msimamo wake wa kupinga ndoa za jinsia moja,kuongeza uwigo wa uhalalishaji wa utoaji mimba,adhabu ya kifo,kuweka sera ya kutonyonga wanaokutwa na adhabu ya kifo na uridhiwaji wa mikataba ya Kimataifa inayozuia masuala ya utesaji kwa kuwa masuala hayo yanaonekana kutoendana na Katiba na Sheria za nchi, Sera,mila desturi na tamaduni za watanzania ikiwa ni sehemu ya mapendekezo 72 yaliyokataliwa na Serikali wakati wa mapitio ya taarifa ya nchi ya ukuzaji na usimamizi wa haki za binadamu.

Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali Ndugu Gerson Mdemu ameyasema hayoleo jijini Dar es Salaam alipokuwa akifunga kikao maalumu cha siku mbili cha wadau mbalimbali wa masuala ya haki za binadamu ambapo ameeleza kuwa Serikali ilipokea jumla ya mapendekezo 227 yaliyotolewa na Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa mwezi Mei 2016 chini ya mfumo wa mapitio kwa kipindi maalum (The Universal Periodic Review).

Mdemu ameongeza kuwa mapendekezo hayo kwa ujumla yalijikita katika majukumu ya Tanzania kwenye mikataba ya kimataifa ,Mifumo ya kikatiba na kisheria,miundombinu ya kitaasisi ya haki za binadamu ,masula ya kisera,ushirikiano na vyombo vya kikanda na kimataifa,utawala wa sheria,uendeshaji haki,masuala ya kulinda haki za msingi za binadamu kama vile haki ya kuishi,haki ya afya,haki za walemavu,watoto,haki ya habari na kujieleza,afya elimu mazingira haki za watu asilia na wakimbizi.

Hata hivyo, Tanzania ilikubali kutekeleza mapendekezo 130 tu kati ya 227 yaliyokuwa yanahusu mchakato wa Katiba,kuijengea uwezo Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora, kuhuisha Sera za nchi ili ziendane na malengo endelevu ya Dunia ,kuandaa taarifa za nchi za utekelezaji wa masuala ya haki za binadamu na kuziwasilisha kwenye vyombo vya vya umoja wa mataifa kwa wakati.

Vilevile Serikali iliahirisha jumla ya mapendekezo 25 ambayo yalijikita katika marekebisho ya sheria ya Takwimu, 2015, Sheria ya makosa ya mtandao, 2015,ukamilishaji wa Sheria ya Habari, Sheria ya vyombo vya Habari,uandaaji wa mikakati na mipangokazi ya utekelezaji wa msuala ya kuzuia ndoa za utotoni na za kulazimishwa ,upitishaji wa sera mpya mbalimbali ikiwemo ya kutoa vyeti vya kuzaliwa na usajili wake kuwa bure na masuala ya uchaguzi Zanzibar, kwa lengo la kuyapitia tena kwa kina na kushirikisha zaidi wadau ili hatimaye kuweka msimamo stahiki kabla mapendekezo hayo hayajawasilishwa tena Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa kwa hatua za mwisho za kupitisha rasmi taarifa ya nchi katika kukuza na kulinda haki za Binadamu.

Aidha, Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali ametumia fursa hiyo kusisitiza kuwa Serikali itaendelea kulinda na kukuza haki za bindamu ikiwa ni pamoja na kupokea hoja na maoni ya wadau ili kuboresha taarifa ya nchi itakayowasilishwa katika Baraza la Haki za Binadamu la umoja wa mataifa kabla au ifikapo tarehe 9 Septemba, 2016 na kuwataka watanzania wote kushiriki ipasavyo katika dhana nzima ya kukuza na kulinda haki za bindamu nchini.

Utaratibu wa Mapitio kwa kipindi maalum (The Universal Periodic Review) wa masuala ya haki za binadamu ulianzishwa na Umoja wa Mataifa mnamo mwaka 2006 kwa lengo la kuzifanyia mapitio nchi 192 ambazo ni wanachama wa Umoja wa Mataifa, Tanzania ikiwa miongoni, kwa lengo la kuangalia utekelezaji wa masuala ya kulinda na kukuza haki za binadamu nchini mwao.

Naibu Mwanasheria mkuu wa Serikali Mhe. Gerson Mdemu akiongea na wajumbe kutoka Serikalini na Asasi za Kiraia wakati wa ufungaji wa kikao kuhusu mapendekezo yaliyotolewa kwa serikali wakati wa majadiliano ya taarifa ya nchi ya utekelezaji wa masuala ya haki za binadamu chini ya mfumo wa mapitio kwa kipindi maalum na baraza la haki za binadamu la umoja wa mataifa, Leo Jijini Dar es Salaam. Kulia ni Mkurugenzi Masuala ya Katiba na Haki za Binadamu Kutoka Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali Bi. Sarah Mwaipopo.

AG2-Wajumbe kutoka Serikalini na Asasi za Kiraia wakimsikiliza Naibu Mwanasheria mkuu wa Serikali Mhe. Gerson Mdemu wakati wa ufungaji wa kikao kikao kuhusu mapendekezo yaliyotolewa kwa serikali wakati wa majadiliano ya taarifa ya nchi ya utekelezaji wa masuala ya haki za binadamu chini ya mfumo wa mapitio kwa kipindi maalum na baraza la haki za binadamu la umoja wa mataifa, Leo Jijini Dar es Salaam.

Umati wa Watu Wakesha Wakisubiri Kupatwa Kwa Jua...

$
0
0
Umati wa watu umepiga kambi eneo la Rujewa, wakisubiri tukio la kupatwa kwa jua kipete linalotokea baadaye leo.

Katika eneo hili ambalo awali halikuonekana kuwavutia wapita njia hata kufaa kutumika kama sehemu ya kujiburudisha kutokana na shughuli ya uchimbaji mawe na upasuaji kokoto, usiku huu watu wamejaa huku watu wakijiburudisha.

Mwandishi wa habari hizi ameshuhudia watu wakiingia na kutoka eneo hilo, ambalo wataalam wa anga wameweka mitambo yao kwa ajili ya kuratibu tukio hilo la kihistoria.

Mama lishe, wachoma nyama na wauzaji wa vinywaji vikali wapo kazini kuwahudumia watu waliofika kushuhudia tukio hilo.

“Kwa kweli tukio hili ni kukumbukwa, muda kama huu ninakuwa nyumbani lakini hawa watu  lazima wahudumiwe,” mamalishe Christina Mgaya.

Hata hivyo, uhaba wa nyumba za kulala wageni katika mji mdogo wa Rujewa umesababisha baadhi ya wageni kukosa sehemu ya kulala na kukesha eneo hilo.

Deni Analodaiwe mh Mbowe na NHC Madalali Wavamia Ofisi za Tanzania Daima na Kuanza Kutoa Vitu nje

$
0
0

Taarifa zilizonifikia hivi punde ni kuwa Tanzania Daima wako kwenye crisis kubwa kwasababu watu wanaodaiwa kuwa ni Madalali wa shirika la nyumba la Taifa la NHC wamefika ofisini kwao asubuhi hii na kuanza kutoa vifaa vyao vyote nje ofisini.

Madalali wa NHC sasa wanatoa vitu nje kwenye ofisi za Mmiliki wa Tanzania Daima gazeti ambalo inahisiwa linamilikiwa na mh Mbowe.

Nadhani mtakumbuka siku kadhaa zilizopita mkurugenzi wa NHC ndugu Nehemia Mchechu alimtaja Mbowe kama miongoni mwa wadaiwa sugu wa shirika hilo na kudai alishamuandikia notisi yakulipa deni notisi ambayo imeisha jana.



Raia Mwema: Benki zakumbwa na Ukata

$
0
0
Wakopaji kutoka sekta mbalimbali za uchumi huenda wakakabiliwa na changamoto za ukosefu wa fedha au kukumbana na viwango vikubwa vya riba sasa na baadaye, kutokana sekta ya benki kukabiliwa na uhaba wa fedhaa benki
Hii ni habari katika ukurasa wa mbele wa gazeti la Raia Mwema la siku ya leo huku habari hiyo ikiwa ndio habari kuu.

Hali hii pia itasababisha wakopaji wengi kupewa kupewa na masharti magumu ya kupata mikopo kwenye benki za biashara hasa kipindi hiki ambacho adadi ya mikopo kichefuchefu (mikopo ambayo imeshindikana kulipa) imekuwa chngamoto kubwa.

Kwa mujibu wa ripoti za Benki Kuu BoT kiwango cha mikopo kichefuchefu ni zaidi ya asilimia tano, ambacho ndicho kiwango cha wastani.
Hadi kufikia mwezi Juni mwaka huu, Mikopo kichefuchefu iliongezeka hadi kafikia asilimia 8.3 kutokaasilimia 6.7 mwezi Machi mwaka jana.

Kuongezeka kwa mikopo kichefuchefu ni ishara mbaya kwani huashiria kupungua kwa imani ya wateja dhidi ya benki. Ukata huo ambao tayari umeonekana kwenye soko, umesababisha kuongezeka cha riba ambacho benki hutumia kuikopesha benki nyingine kwani mahitaji ya fedha kwa ajili ya benki kuyafanyia biashara yamekua kwa kwasi.

Kwa mujibu wa ripoti za fedha za BoT, kiwango cha riba ya mikopo baina ya benki kiliongezeka hadi kufikia wastani wa asilimia 18 hadi Jumatatu wiki hii.
Ripoti hiyo inaonyesha kwamba viwango vya riba ya jumla kwa mikopo baina ya benki kiliongezeka na kufikia asilimia12.31 kutoka asilimia 11.17 huku riba ya ya mikopo ya siku moja kiongezeka hadi asilimia 12.25 kutoka asilimia 11.6

Kwa mujibu wa mapitio ya ripoti ya uchumi mwezi Juni mwaka huu, benki zilikopeshana kiasi cha shilingi trilion 1.28 kutoka shilingi 1.12 mwezi Aprili mwaka huu. Ukubwa wa kiwango hiki cha mikopo baina ya benki huakisi pia viwango vya mikopo ambayo benki hizo hutoa kwenye sekta za uzalishaji mali pamoja na mikopo ya biashara.

Chanzo: Kutoka magazetini.

Kauli 10 Nzito Alizotoa Mbowe, Akiahirisha Ukuta

$
0
0
Mbowe
LEO mchana, Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) taifa, ametangaza uamuzi wa kuahirishwa kwa maandamano na mikutano ya chama hicho nchi nzima iliyopangwa kuanza kesho, anaandika Charles William.

Zifuatazo ni kauli kumi zilizotolewa na mwenyekiti huyo wa Chadema, wakati akitangaza kuahirishwa kwa operesheni hiyo maarufu kama Ukuta, iliyotawala vyombo vya habari vya ndani na nje pamoja na mitandao ya kijamii kwa zaidi ya mwezi mmoja.

1.“Tunajua uamuzi huu utawaumiza sana wafuasi wetu, na uamuzi huu umeniumiza sana hata mimi mwenyewe, lakini ni nani miongoni mwa viongozi wetu na wanachama wetu ambaye anaweza kuombwa kuahirisha jambo na viongozi wa madhebu na dini zote hapa nchini na akawakatalia?”

2.“Polisi na Serikali wajue kuwa, hatuahirishi maandamano na mikutano yetu kwa sababu ya mazoezi, risasi au mabomu ya polisi. Hatuahirishi kwasababu ya usafi wao, wanaofanya kesho na wala hatuahirishi kwasababu ya ndege za kijeshi zinazoruka, ila tumeamua kuwaheshimu viongozi wetu dini.”

3.“Tunawaomba wanachama wetu, wapenzi wetu na wapenda demokrasia kote nchini watusamehe na wakubali kuwapa viongozi wa dini hizi wiki tatu, watafute suluhu kwa kuonana na Rais na ikishindikana, hatutarudi nyuma. Tutaingia barabarani.”

4.“Tangu tulipotangaza operesheni Ukuta, jumla ya wanachama na viongozi wetu 230 katika maeneo mbalimbali wamekamatwa na kushitakiwa kwa tuhuma mbalimbali ikiwemo uchochezi na jumla ya viongozi na wanachama wetu 28 wapo rumande mpaka sasa pasipo sababu za msingi.”

5.“Haikuwa rahisi sisi kufikia uamuzi huu, hatukuwa tayari kurudi nyuma. Lakini viongozi wa dini na taasisi zinazoheshimika hapa nchini wametusihi. Mpaka Mama Maria Nyerere ameongea na Mheshimiwa Lowassa na kutuomba tuahirishe ili watafute suluhu ya suala hili.”

6.“Hatuogopi mabomu wala risasi za polisi, tuna uwezo wa kuandamana kwasababu tunazo mbinu za kufanikisha mipango yetu. Juzi polisi walitukamata na kuzuia kikao cha Kamati Kuu ila jana tumekifanya na wala hawajui tumefanyia wapi na saa ngapi.”

7.“Wakati tukifanya harakati hizi, tunaendelea pia kufungua kesi sehemu mbalimbali. Tundu Lissu na jopo lake tayari wameandaa mashitaka 15 ili tuweze kuyafungua katika mahakama zetu hapa nchini. Tutadai haki mahakamani na tutaidai barabarani.”

8.“Inasikitisha sana kuona taifa lina rais anayeomba watu wamuombee kila siku, ‘Niombeeni jamani’, lakini amekuwa akijaribu kuwakwepa viongozi wa dini kila wanapotaka kumuona ili kuzungumza naye kuhusu amri haramu ya kuzuia mikutano ya hadhara.”

9.“Viongozi wa dini walituomba wiki mbili au tatu ili wafanye mazungumzo na Rais Magufuli, sisi tumewapa mwezi mzima kabisa, ili wasake suluhu ili sisi kama vyama vya siasa tupewe haki yetu ya kisheria na kikatiba. Ikishindikana hakika sisi hatutarudi nyuma.

10.“Salum Mwalimu bado yupo rumande kwasababu za hovyo, Polisi wamekataa kumpeleka mahakamani leo wanadai wapo ‘busy’ eti wanazuia maandamano ya UVCCM, yalipangwa kufanyika leo. Sisi wote ni wafungwa watarajiwa lakini hatutarudi nyuma.
Viewing all 104809 articles
Browse latest View live




Latest Images