Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live

Muonekano wa Shilole Red Capet ya MTV Awards Wazua Gumzo Mitandaoni...

$
0
0
Mrembo Shilole aka Shishi Baby amezua gumzo mitandaoni kwa vazi alilovaa kwenye red kapeti ya MTV Mama Awards zilizofanyika jumamosi iliyopita...

Baada ya kutupia hiyo picha kwenye page yake hivi ndivyo watu walivyofunguka...

suzan.ndama
Kikwell mim huyu dada toka kaanzakufahamika sana cjawah kupendezewa na mavaz yake

sofia_omary78 
Kajifanya mjuaji kaharibu sasa ivyo ndo nini seemu yenye heshima Zake watu na misuti yao wewe unatuvalia kibkita kama uko kwenye singeli anawezekana hii safari ya kushitukiza hajajipanga igweeeeeee


Ukweli Unauma, Hizi Ndio Sababu Zilizotufanya Watanzania Tukakosa Tuzo MTV Awards

$
0
0
Ngoja Niongee Leo Hii.
Watu Wengi Wamekuwa Wakijiuliza Why Tumeshindwa Huku Wakipeleka Lawama Zote Kwa Teams Bila Hata Kuchambua KwA Kina.

KwA Upande Wangu Na Akili Zangu Hizi Hizi Za Insta Ni Wengi Mno AmbaO Wanaingia Katika Kusababisha Hili KwA Namna Moja Ama Nyingine.

1. Watu Wa Kwanza Kabisa Kuchangia Kukosa KwA Tuzo Ni Wasanii Wenyewe. Wasanii Wamekuwa Wanafiki Sana Sana. Naomba Nihakikishie Direct Hii, Hivi Bongo Kuna Wasanii Wawili Tu? Au Ndio Ile Hawana Management Nzuri?? Ifike Time Muache Ubinafsi, If Unaamini Mungu Anampa Kila Mtu Ridhiki Yake Then Acheni Uchoyo WA Kuwaambia NA Wenzenu Process Za Kuwafikisha Katika Mashindano, Tell Them What They Suppose To Do, Wingi Wenu Katika Categories Utasaidia Pia Kuwanyanyua, Usiniambie Bongo Kiba Na Mondi Tu Ndio Very Best Artist, Narudia Kama Unajiamini Ridhiki Yako Ipo Just Tell Na Wengine Nini Wanatakiwa Kufanya Wafike Hapo. Rayvanny Kama Asingekuwa WCB Am Not Sure Kama Angekuwa Katika Kipengele Chochote, Too Bad Namshangaa Kiba Why Abdu Kiba Bado Yupo Nyuma Tu Hafiki Popote. Hebu Mjifunze Kubebana Sana.

2. Teams ,This Is The Worse Part Dah!! Sitaki Hata Kufikiria Mara Mbili, But Mmeshawahi Hata Kujiuliza Wanapata Wapi Nguvu Zote Hizo?? KamA Utajiuliza Hili Swali KwA Kina Utajua Kuwa Wasanii Wenyewe Hapa Wanarudi Tena Humu Humu Katika Teams, Wao Ndio Vichocheo Vikubwa Vya Jeuri KwA Hizi Teams, We Know Kila Mtu Ana Njia Yake Ya Kutafuta Ugali Mezani, Ila Ifike Muda Kama Kweli Mnataka Uzalendo Make Sure Mnavunja Team Za Kibaguzi, Unajua Hata Wasanii Wakubwa Nje Wana Teams Zao (Tena Kuna Tuzo Wana Mpaka Category Team Ya Nani Ni Strong Team) Rihanna Navy Ya Rihanna, Beyhive Ya Beyonce, Swifties Ya Taylor Swift, Arianators For Ariana Grande, Selenators Hawa WA Selena Gomez, Dah Guys Wako Wengi Tu, Ila Hawa Wanaongoza Kununua Kazi Zao, KutoA Support Za Shows, Bidhaa Zao NA Kadhalika, Sisi Ni Mitusi Tu Mwanzo Mwisho, Mitusi Tu.

3. Media Hawa Unaweza Kuwaona Hawamo Ila Trust Me Hawa Watu Nao Kwa Namna Moja Ama Nyingine Wanachangia, Wanachangia Sana, Ifike Time Na Wasanii Wengine Wapewe Support,

Pamoja Na Kulalamika Kooote Wabongo Turudi Kwenye Ukweli Hivi Kweli Diamond Angemshinda Wizkid?Vanessa Amzidi Yemi Alade Na Rayvan Ampite Tecno. Nah Hapana Tuwe Wakweli At Once.

Tunajiliwaza Lakini Ukweli Ni Kwamba This Time Tulibanwa Mno, Vanessa Ana Ngoma Gani Ya Kumpita Yemi?? Nyimbo Mbili Za Rayvanny Ampite Techno Na Ma Wash Yake Sijui Maduro?? Diamond Tuzo Zilizopita My #1 iliweza Kumbeba, Mwaka Huu Alikuwa Na Kipi Cha Kumpita Wizkid?? Pamoja Na Kura Zote Na Yote Tunatakiwa Kukubali Mwaka Huu Tulibanwa. Who Knows YaMoto Band?? Where In Africa Wamefanya Hata Show, Kiukweli This Time Hatukuwa Na Lolote. (Najua Tutakataa Kuukubali Huu Ukweli)
Tatizo Wabongo Tunajiona Sisi Ni Wakubwa, Kiukweli Bado Tuna Safari Ndefu, Wizkid Sio Mwenzetu, Kiba Na Diamond Hawamgusi Hata Robo Ana Mashabiki Africa Nzima Na Nje Ya Africa.

Diamond Asubiri Mwakani Wimbo Wake Na P Square Una Nafasi Kubwa Sana YA Kumpa Tuzo, My #1 Na Nana Zilimbeba Sana, Ila Baada Ya Hapo Kiukweli Alikuwa Na Nyimbo Za Kawaida Za Wabongo Na Sio Nyimbo Za Tuzo Kubwa.

Kiba Japo Hakuwepo Direct Katika Nominee, Ila Kajitahidi As An Artist Kwa Show Yake, Amefanya Poa Performance Japo NAe Pia Anabezwa. For Now Sasa Ndio Tuonyeshe Huo Uzalendo, Kumuombea NA Kupiga Kura Ile Tuzo Ile MtvEMA Ije Home.

NINI KIFANYIKE
Wasanii Wetu Needs To Go Outside, Wanatakiwa Waanze Kupiga Shows Across Africa Countries, Isiwe Tu Shows Wanazoalikwa Ulaya. Leo Hii Wizkid Anakuja Tz Kupiga Show Coz Hapa Tz Ana Mashabiki, Plus Nchi Mbalimbali Za Africa Anazokwenda. Nina Hakika Katika Hizo Tuzo Wapo WaTz Kibao Waliompigia Kura, Tukiacha Hizo Mateam But As Fans Wake From Tz.
Mziki Wetu Unakuwa Yes, Lakini Tutoke Pia, Tupige Shows Africa Na Itasaidia Kukuza Jina, Soko Na Kujitangaza.

Hayo Yoooote Yakishafanyika Sasa Ndio Tuje Katika Kura, Na Narudia Teams Sio Shida Kama Tutajua Jinsi Ya Kuzitumia NA Sio Kusambaza Chuki, Hata Ulaya Wana Teams (As Mentioned Mwanzo) Team Zetu Zinakosa Uzalendo, ZinaendekezA Chuki Hata Katika Mambo Ya Msingi.
Tunashukuru 5 nominations, Ni Jambo La Khery, Hata Appearance Ya Idris NA Navy Kenzo. Tupo Pazuri, Next Year Tuwe Na 10 Nominations

Kutana na Mwanamke Mnene Kuliko Wote Duniani… Ana Uzito wa Kilo 500

$
0
0
Kwa mujibu wa jarida la Daily Mail, inaelezwa kuwa mwanamke huyo aitwaye Iman Ahmad Abdulati mwenye miaka 36 hajawahi kutoka ndani kwa miaka 25 na amekua akiongezeka uzito wake kwa haraka mpaka kufikia kilo 500 zinazompa shida ya kujifanyia usafi na hata kula. Ripoti ya madaktari inaonesha kuwa mwanamke huyu anasumbuliwa na maambukizi ya bakteria wanaoshambulia ukuaji wa mwili.

Akiwa na miaka 11 alianza kusumbuliwa na tatizo hilo ingawa wazazi wake wanakiri kuwa hawakudhani kuwa ni tatizo lakini siku zilivyozidi kwenda ndipo wakabaini kuwa halikua jambo la kawaida hivyo wakaamua kutafuta wataalamu ambao walitoa ripoti kuwa ana matatizo ya mwili wake kukaa na maji mengi bila kuyatoa nje kitu ambacho sio cha kawaida kwa binadamu.


Huyu Hapa Mpenzi Mpya wa Idriss Sultan....Wagandana Kama Ruba Huko MTV Awards

Lipumba aitaka Chadema Kutoingilia Mgogoro CUF......Aifananisha Opareshi UKUTA na Biskuti

$
0
0
Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahim Lipumba,  amewataka viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kutoingilia mgogoro uliopo ndani ya chama hicho kwa sababu hauwahusu.

Kauli hiyo aliitoa jana jijini Dar es Salaam alipokuwa akizungumza na wanachama wa chama hicho katika kikao cha ndani, kilichofanyika Wilaya ya Kinondoni ambapo alisema Chadema kushindwa kutekeleza Operesheni Ukuta ni dhahiri chama hicho kimeshindwa kutekeleza kile wanachoahidi kwa Watanzania.

Alisema mpaka sasa kumekua na vikao mbalimbali vinavyofanywa na viongozi wa Chadema kwa ajili ya kuivuruga CUF, jambo ambalo alisema haliwekezani.

“Chadema wanajitahidi kutuvuruga kwa kutuma waasi wa chama hiki, lakini naomba niwaambie hawawezi, CUF ni ngangari hata serikali inajua na  wanachokifanya ni kupoteza muda bure.

“Unajenga Ukuta wa biskuti, ukiumwagia juisi unamong’onyoka, Ukuta gani huo, huu muziki wa CUF ni ngangari hawauwezi,” alisema Lipumba.

Alisema katika kipindi hiki ambacho wana kesi mahakamani, wanachama wa chama hicho wataendelea na shughuli za kukijenga chama hicho pamoja na kuwasisitiza  kuwa na msimamo wa kutetea chama na katiba yake, jambo ambalo linaweza kuwasaidia kufikia malengo waliyokusudia ya kushika dola kafika Uchaguzi wa mwaka 2020.

Alisema kutokana na hali hiyo, rasilimali za chama hicho zinasimamiwa kwa umakini chini ya walinzi wa chama hicho, Blue Guard ambao Katibu Mkuu wa chama hicho, Maalim Seif Sharif Hamad alisema ni wavamizi hawatambui.

“Ninamshangaa Maalim Seif sasa hivi anaibuka na kusema hawatambui walinzi wa chama Blue Guard ambao miaka yote walikua wanamlinda pamoja na rasilimali za chama, lakini hayo yamekwisha nitazidi kumwomba aje tujenge chama hata kama kesi inaendelea mahakamani,” alisema.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Habari na Mawasiliano anayemunga mkono Profesa Lipumba, Abdallah Kambaya alisema kupoteza nafasi ya umeya na naibu wake katika Manispaa ya Kinondoni ni matokeo ya mgogoro wa CUF na kutokuwepo ushirikiano ndani ya Ukawa.

“Maalim Seif anaunga mkono Ukawa, mbona wanachama wa Ukawa wameshindwa kutusaidia ili kupata meya na naibu wake kwenye uchaguzi wa leo? (jana),” alihoji.


Serikali Kuwabana Wanafunzi Wanaopewa Mikopo Kwa Kipaumbele

$
0
0
Serikali ipo katika mkakati wa kuwabana wanafunzi wanaopewa mikopo katika fani za kipaumbele, kutumikia katika utumishi wa umma nchini kwa muda fulani ili kuhakikisha dhamira ya serikali ya inatimia.

Fani hizo ni sayansi za tiba na afya, ualimu wa sayansi na hisabati, uhandisi wa viwanda, kilimo, mifugo, mafuta, gesi asilia, sayansi asilia, mabadiliko ya tabia nchi, sayansi za ardhi, usanifu majengo na miundombinu.

Serikali inachukua uamuzi huo, baada ya kubaini kuwapo wanafunzi wanaosomea fani hizo ili kupata mikopo, lakini baada ya kumaliza hukimbilia kufanya kazi nyingine au nje ya nchi na hivyo kuendelea kuwepo upungufu wa wataalamu waliowakusudia kubaki.

Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na mafunzo ya ufundi, Stella Manyanya aliyasema hayo hivi karibuni, alipozungumzia utoaji wa mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu. Alieleza kuwa serikali inafikiria kuwe na utaratibu kwa wanaonufaika na mikopo ya kipaumbele kuingia makubaliano na serikali.

Alisema suala hilo halitakuwa jipya kwani hapo nyuma walikuwa wakibanwa kuwa lazima kufanya kazi angalau kwa miaka mitano serikalini na baadaye ni ruhusa kwenda popote, lakini kwa sasa hawawezi kuwabana wote, lakini lazima kufanya hivyo kwa hao wa kipaumbele.

Aidha Manyanya alizungumzia ulipaji mikopo hiyo na kudai wanaboresha sheria ya kukusanya madeni kwa kushirikiana na waajiri.

“Serikali itakusanya madeni hata kwa wakopaji ambao wamejiajiri kwa sababu wengi wakimaliza masomo hawafikirii kulipa,” alisema.”Sasa lazima walipe, wakopaji watambue fedha hizo ni mikopo na lazima kulipa.”

Alisema kwa wakopaji watakaoajiriwa, wizara inataka mkopo huo kuwa wa kwanza kukatwa kabla ya mingine ili kuepuka kuingiliana na sheria za kazi, zinazotaka mkopaji kuachiwa fedha fulani katika mshahara wake.

Vyakula Vinavyoongeza Hamu na Nguvu ya Kufanya Tendo la Ndoa

$
0
0
Tatizo la uwezo wa kufanya tendo la ndoa linazidi kukua miongoni wa wanandoa na wapenzi wengi. Takwimu za kitafiti zinaonyesha kuwa karibu ndoa 4 kati ya 10 zenye umri wa miaka 3 na kuendelea zinakabiliana na tatizo hili. Aidha wanaume 6 kati ya 10 wanatajwa kulalamikia upungufu wa nguvu za kiume.

Pamoja na matatizo mengine kutajwa kuchangia upungufu wa nguvu za kiume na kushuka kwa msisimko wa tendo miongoni mwa wanandoa, uchunguzi umeonesha kuwa utumiaji holela wa vyakula hasa vyenye mafuta ni moja kati ya sababu zinazochangia kwa kasi tatizo hili.

Kwa kuzingatia hilo, watafiti wa masuala ya uhusiano wa kimapenzi wamebaini aina mbalimbali ya vyakula ambavyo vina uwezo wa kumuongezea mtu nguvu ya kufanya tendo la ndoa.  Vyakula hivyo ni hivi vifuatavyo:

1. PILIPILI
Kama tunavyojua wote mara nyingi chakula ambacho kimeungwa pilipili hufanya hata mapigo ya moyo kuwa tofauti na wakati mwingine hata jasho au kamasi hutoka. Ndani ya pilipili kuna kitu kinaitwa capsaicin ambacho hufanya pilipili iwe na hali ya ukali. Capsaicin huwezesha ubongo kutoa homoni ya endorphins ambayo huleta mgusu wa hisia za raha wakati wa kufanya tendo la ndoa.
Pia pilipili husisimua mfumo wa fahamu (nerves) wa ubongo na katika kufanya hivyo huwezesha kuamshwa haraka kimapenzi (kunyegeka) wakati wa tendo la ndoa na pia ukiguswa au kubusiwa au kunyonywa au kupapaswa unapata hisia kila sehemu ya mwili.

2. MATUNDA NA MBOGA ZA MAJANI
Ulaji wa matunda na mboga za majani una matokeo makubwa sana katika hamu ya tendo la ndoa kwa njia nyingi. Kwanza matunda na mboga za majani hupunguza kiwango cha mafuta na unene (cholesterol).  Kuongezeka kwa mafuta mwilini huzuia mzunguko wa damu kwa kubana mishipa ya damu.

Pia kula matunda na mboga za majani huhakikisha balance ya uzito kwani unene (obesity) kwa wanaume kuna matokeo mabaya katika kuzalisha homeni za testoeterone na hatimaye jogoo kushindwa kuwika na kuwa na pia mwanaume anakuwa na hisia za mapenzi (libido) kidogo.
Na pia wanandoa wanapozidi kunenepeana ndipo na hali ya kufurahia au kuwa na hamu ya tendo la ndoa huzidi kupungua. Kitalaam inashauriwa kula milo (potions) 3-5 za matunda kwa siku.

3. NAFAKA ZISIZOKOBOLEWA
Nafaka hasa zisizokobolewa kama mahindi, ngano, uwele, nk zina nyuzinyuzi (fibre) na sukari ngumu (complex sugar) ambazo kusaidia kutunza uzito wa mwili. Nafaka husaidia katika kuzalisha homoni za testosterone kwenye damu. Na pia nafaka huwezesha mtu kuwa na nguvu hatimaye kwenda masafa marefu wakati wa tendo.

Kula nafaka nzima kama vile brown bread badala ya white bread, pia kula nafaka halisi badala ya cornflakes ni jambo zuri linalokuhakikisha afya nejama na mahusiano mazuri ya ndoa yako.

4. TANGAWIZI
Tangawizi ni kiungo cha mboga ambacho husisimua sana na kusaidia mfumo wa mzunguko wa damu mwilini. Tangawizi zinajulikana sana kwa kusukuma damu kwenda sehemu za viungo vya uzazi yaani uke na uume hivyo kuwa na umuhimu sana katika kuboresha ufanyaji wa tendo la ndoa. Inaweza kuliwa mbichi, au kuliwa ikiwa imeungwa kwenye chakula au kusagwa na kuwa kama unga na kutumiwa kama chai.

5. ASALI
Asali ina madini yanayoitwa boron, ambayo husaidia mwili kutumia homoni ya estrogen ambayo ni homoni inayohusika na viungo ya uzazi na mapenzi kwa mwanamke.
Pia kuna utafiti unaoonesha kwamba asali huongeza nguvu, kitendo ambacho kitapelekea mwanamke kuwa uwezo na hamu ya tendo la ndoa au libido.

6. KARANGA
Karanga huhusika katika kuchochea mfumo wa mzunguko wa damu (vascular system). Mzunguko wa damu ulio sawasawa katika uke na uume huwezesha mwanaume na mwanamke kupata msisimko wa mapenzi haraka hatimaye tendo la ndoa kuwa murua. Pia karanga zina madini muhimu kama vile magnesium, asidi ya folic na zinc ambayo ni muhimu sana katika usalishaji wa mbegu za mwanaume.

7. CHAZA (OYSTERS) NA PWEZA
Hawa ni aina ya samaki ambao hupatikana katika maji chumvi. Huwa na kiasi kikubwa sana cha madini ya zinc na haya madini ndiyo huhusika zaidi na uzalishaji wa homoni ya testosterone kwa wanaume.
Pia imethibitika kwamba wanaume wenye ukosefu wa madini ya zinc huwa na matatizo ya nguvu za kiume.  Pia madini mengi ya zinc mwilini huongeza kiwango cha shahawa kwa wanaume.

8. SOYA
Pamoja na kuwa na kiwango kidogo sana cha mafuta (fat) na pia kuwa na kiwango kizuri cha protein, soya zina phytoestrogens ambayo husaidia sana wanawake ambao wamefikia menopause kutengeneza homoni estrogen ya ziada.
Husaidia uke kuwa laini (wet, lubricated) mwanamke akisisimuliwa wakati wa tendo la ndoa.

9. CHOKOLETI
Chocolate ina phenylethylamine, kemikali ambayo husababisha hisia (feelings) za furaha wakati wa mwanamke au mwanaume kufika kileleni (orgasm). Inasaidia sana kula chocolate masaa machache kabla ya kuanza kufanya tendo la ndoa.

10. PARACHICHI
Aina nyingine ya chakula ambacho husaidia kuongeza uwezo wa mtu kufanya tendo la ndoa ni Parachichi. Tunda hili linauwezo mkubwa wa kuzalisha vitamini E ambayo husaidia katika uzalishaji wa homoni. Inatajwa kuwa watu wanaotumia tunda hili kwa wingi huwana msisimko mkali wa kimapenzi na kwa upande wa wanawake husaidia kuongeza majimaji yenye utelezi sehemu za siri na hivyo kuzuia uwezekano wa kuchubuka wakati wa kujamiiana.

Thomas Ulimwengu Aondoka TP Mazembe, Afuata Ndoto zake Kucheza Ulaya

$
0
0
Baada ya kucheza misimu mitano kwenye klabu ya TP Mazembe, mchezaji wa Taifa Stars, Thomas Ulimwengu ameondoka kufuata ndoto zake kucheza Ulaya.

Mchezaji huyo aliyekuwa akivaa jezi namba 28 na aliyepewa jina la utani ‘Rambo’ alichukuliwa na klabu hiyo akiwa na umri 18 kutoka AFC Academy ya Stockholm, Sweden. Akiwa na TP Mazembe, Ulimwengu amecheza mechi 130 na kufunga mabao 35.

Wakati anachezea klabu hiyo klabu nyingi zilitaka kumchukua lakini aliamua kumaliza kwanza mkataba wake na Mazembe. Aliamua kutoongeza tena mkataba na TPM. Na sasa Ulimwengu anataka kufuata nyayo za Mtanzania mwenzake Mbwana Samatta wa Genk ya Ubelgiji.

Kabla ya kuondoka Lubumbashi, Ulimwengu alisema kupitia taarifa kwenye tovuti ya klabu hiyo, “Kwa miaka mitano Mazembe imeniruhusu kuendelea kukua kisoka na nataka kuwashukuru wote walioniunga mkono na kusaidia kushinda vikombe wakiongozwa na Rais Katumbi na Mrs Carine, viongozi na makocha.”

Mrithi wa Pluijm Asaini Miaka Miwili Yanga

$
0
0
Taarifa inayosambaa kwa kasi kwenye mitandao ya kijamii ni ujio wa kocha mpya George Lwandamina anayetajwa kuchukua nafasi ya Babu Hans van der Pluijm kwenye kikosi cha Yanga SC.

Jana iliripotiwa kocha huyo ameshatua jijini Dar kwa ajili ya kumaliza taratibu za kukabidhiwa mikoba kutoka kwa Mholanzi Van Pluijm, lakini taarifa iliyopo sasa ni kwamba, Lwandamina tayari amesaini mkataba wa miaka miwili kuifundisha klabu ya Yanga.

Awali ilielezwa kuwa, baada ya kocha huyo mzambia kupewa majukumu ya kukinoa kikosi cha Yanga, Pluijm atakuwa Mkurugenzi wa ufundi wa mabingwa hao watetezi wa taji la VPL. Taarifa zilizopo ni kwamba klabu ya Yanga itamleta Mkurugenzi wa ufundi kutoka nchini Ureno.

Unasoma Hadi PHD Hujawahi Kufanya Kazi, Una Matatizo – Mwijage

$
0
0
Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage amewachana vijana wanaotumia miaka mingi kuwa chuoni wakisoma hadi kufika kiwango cha PHD bila kupitia ujuzi wa kazi yoyote.

Ameyasema hayo Jumatatu hii katika kipindi cha Clouds 360 kinachorushwa na Clouds TV akidai kuwa vijana wengi wanapenda elimu aliyooita ya ‘mseleleko’ akimaanisha elimu ya moja moja kwa moja bila ya kujaribu kufanya kazi yoyote au bila kupitia ujuzi mbalimbali wa kazi.

“Tatizo moja tulilonalo tunapenda elimu mseleleko,” alisema. “Sipendi kuizungumzia elimu lakini nataka niseme tunapenda elimu mseleleko, yaani unaanza leo miaka 6 unaanza darasa la kwanza, unakwenda moja kwa moja mpaka unamaliza PHD,hujawahi kufanya kazi. Mimi sikusoma elimu mseleleko na ndiyo maana mimi watu wengine kama ntalisema hili wengine litawaudhi shauri yao,” alisisitiza.

“Watu wengine wanapenda kujua mimi nimesoma shule gani, kimsingi mimi elimu ya darasani ni ndogo, niliyonayo ni elimu ya mtaani nimefanya kazi nyingi, mi nimevua samaki, nimefanya kazi gereji, ukiniuliza naweza nikakuuliza ukasema na hili Mwijage unalijua. Mimi nilikuwa hata Dj nilikuwa MC, nimefanya kazi nyingi sana kwenye field,nimepiga debe mimi, kwahiyo mimi vitabu vya darasani sina,” alieleza.

“Lakini hii elimu mseleleko hii hujawahi kufanya kazi yoyote unakuwa injinia hujawahi kusimamia hata jengo moja ina matatizo. Kwahiyo vijana mkikwama tafuta namna ya unavyoweza kuanza. Mi nawafahamu watu ambao waliokwenda kusoma kutokana na vipato walivyojitafutia,mi nawafahamu watu waliofanya vibarua kujilipia karo.”

“Sasa mtu anasoma kuanzia darasa kwanza moja kwa moja mpaka PHD bila kufanya kazi yoyote, hata vijana wa Ulaya mbona wanafanya kazi wanajilipia karo, so we have problem kwasababu ni maskini tunapenda kwasababu ya kupenda haya ya mseleleko. Mtu akianza wenzake wakimtangulia aliokuwa anasoma nao anajisikia vibaya. Mi mbona kuna watu tulimaliza nao form six wakaenda chuo kikuu na mimi sikuenda nilikuwa nafanya mambo mengine!

VIDEO:Majambazi Wenye Pikipiki Wapora $40,000 Ofisini Kwa Mohamed Ishaq (Scandinavia)

$
0
0
Jamaa katika Nissan kaibiwa usd 40,000 na majambazi ofisini kwa Mohamed Ishaq (scandinavia)

Majambazi walimfuatilia tokea benki.

Video ya pili inaonesha tukio lililochukuliwa na rekodi za cctv camera

MTV MAMA: Ushindi wa Kishindo wa Wizkid Utuamshe Kuhusu Tunavyozichukulia Tuzo

$
0
0
Ushindi wa kishindo wa Wizkid kwenye tuzo za MTV MAMA mwaka huu, unanikumbusha wale wanafunzi wa kiume ambao huwa hawana time kabisa na wasichana wa darasani, lakini bado watamnasa kila demu mkali.

Wanafunzi wa aina hii ni wale ambao huwa na akili sana darasani au kwao mambo safi (wana mkwanja) – vitu viwili muhimu vinavyowadatisha madenti wa kike! Warembo hujipeleka wenyewe!

Tangu kutangazwa kwa majina ya wasanii watakaowania tuzo hizo mwaka huu, Wizkid hakuwahi kusema chochote. Alikuwa kimya tu utadhani hakuna kinachoendelea licha ya kuwepo kwenye vipengele vingi.

Hakuwa na muda wa kusema ‘thanks for the nomation.’ Hakuwa na hata muda wa kusema ‘jama eeh, mwenzenu nimetajwa kwenye MTV MAMA hebu nipigieni kura.’ He didn’t give a damn! Si ajabu lakini kwasababu ni kawaida yake bwa’mdogo huyu. Yeye tuzo huziona kitu cha kawaida, mpe sawa, mnyime, fresh tu!

Ehh! Jumamosi kaibuka na tuzo nne, kawa ‘man of the night.’ Unadhani ni kura ndizo zimempa ushindi wa tuzo zote hizo? Napata tabu kuamini. Msanii mmoja mkubwa sana ameniambia, namnukuu: Sometimes KURA zinapotosha. Watu wamepiga kazi nzuri ila kura zinapick wengine.”

Anachomanisha kuwa, msimamo wa Wizkid kutojishughulisha na kusema lolote kuhusu tuzo, kunaweza kukawa kulimfanya asipate kura nyingi kihivyo, lakini ukweli ni kwamba, hakuna msanii Afrika aliyefanya makubwa kumzidi Wizkid mwaka huu.

Alishirikishwa kwenye wimbo ‘One Dance’ wa Drake ambao umeweka rekodi kibao ikiwemo ya kusikilizwa mara bilioni 1 kwenye mtandao wa Spotify na kuwa wa kwanza kuwahi kuvutia namba hizo. Wizkid amefanya kazi na Chris Brown, Trey Songz, French Montana na wasanii wengine wakubwa. Ndio msanii anayefanyia kazi Afrika anayefahamika zaidi kwa sasa Marekani. Hata kama hakuonesha kuzitilia maanani tuzo hizo, ilikuwa ngumu kumkwepa.

Fundisho hapa ni kwamba, wingi wa kura unaweza usiwe na maana yoyote katika kumpata mshindi. Haiko sawa kwa namna yake ndio maana Eddy Kenzo amelalamika. Kwamba kama waandaji wanasisitiza watu wapige kura, lakini waliopigiwa kura nyingi hawapewi ushindi, ya nini kuwaambia watu wapige kura? Ni sawa na kampuni kutangaza ajira na kuwafanyia usaili baadhi ya waombaji huku ikiwa na watu wengine itakaowapa kazi.

Hatuna ulazima wa kujilaumu au kuumia sana au kuushusha muziki wetu. Wasanii waliotuwakilisha wamefanya kazi kubwa na ngumu kuipeperusha bendera ya Tanzania. Tusiwabeze, tuwape moyo na kuwaunga mkono bila kuchoka. Katika kipindi wanachohitaji zaidi support yetu, basi ni hiki.

Bongo5

Hans van Pluijm amejiuzulu Yanga Baada ya Kusikia Ujio wa Kocha Mpya

$
0
0
Kocha Mkuu wa klabu ya Yanga Hans van der Pluijm ameandika barua ya kujiuzulu kuifundisha klabu hiyo ya Jangwani.

Uamuzi wa Pluijm umekuja baada ya tetesi kuzangaa kwamba uongozi wa klabu hiyo unampango wa kubadili benchi la ufundi la klabu hiyo huku yeye kama kocha wa sasa akiwa hana taarifa rasmi kutoka kwa klabu.

“Nimeandika barua ya kujiuzulu kutokana na jinsi mambo yanavyokwenda, sikufurahishwa nayo. Nimeamua kujiuzulu na tayari nimekabidhi barua kwa uongozi wa Yanga, kama watapitisha nahitaji wanikamilishie stahiki zangu,” Van Pluijm amenukuliwa na chanzo cha habari hii.

Wakati huohuo, mzambia George Lwandamina amesema hajasaini mkataba wowote na Yanga ingawa amekiri Yanga inamuhitaji.

Amesema kwamba, kama watakubaliana yupo tayari kuja na kuipa Yanga mafanikio zaidi.

Focus Yangu Sio Kufanya Collabom Kama Wafanyavyo Wengine – Alikiba

$
0
0
Alikiba amedai kuwa collabo si kitu kilichopo kwenye menu yake.
Akiongea na mtangazaji wa Times FM, Lil Ommmy kwenye red carpet za MTV MAMA jijini Johannesburg, Afrika Kusini Jumamosi iliyopita, aliyemuuliza iwapo ametumia fursa hiyo kuzungumza na wasanii mbalimbali wa Afrika kuhusu collabo, Kiba alidai kuwa mipango yake ni kufanya muziki mzuri.

“Hiyo sio focus yangu, focus yangu ni kufanya muziki mzuri,” alisema Alikiba.

Muimbaji huyo alikuwa ametajwa kuwania vipengele viwili akiwa na Sauti Sol kupitia wimbo wao Unconditionally Bae.

Matumaini Mapya Kwa Mchezaji Kutoka Tanzania Hasheem Thabit Kurudi Kucheza NBA Baada ya Kutemwa

$
0
0
Miaka kadhaa iliyopita, kwa mara ya kwanza Tanzania ilipata mwakilishi kwenye ligi bora ya kikapu duniani; NBA kupitia Hasheem Thabeet. Wapenda michezo na maendeleo kwa ujumla walifurahia uwakilishi huo kwa kile kilichoonekana kutafungua milango kwa wengine. Na kweli, kuingia kwa Hasheem NBA kuliongeza hamasa ya Watanzania kutaka ku-break to NBA Gates.

Ni bahati mbaya Hasheem hakufanya vizuri sana NBA na baada ya miaka michache akajikuta anapelekwa D-League!

Kwa sasa Hasheem ni kama amesahaulika lakini ifahamike tu hajalala! Kwa miaka takribani miwili sasa amekuwa aki-fight kurudi NBA. Rekodi zake za D-League msimu uliopita zilikuwa mzuri na zilitia matumaini kwamba huenda angerudi NBA. Hata hivyo bahati haikuwa upande wake.

Wakati namfuatilia mwaka jana nilipata hofu kwamba kukosa kwake kurudi NBA (mwenyewe alitarajia angerudi) kungemfanya awe disappointed kama ilivyo kwa Watanzania wengi. Hata hivyo, Hasheem ni kama aliongeza struggle za kutaka kurejea NBA ingawaje alikuwa na fursa ya kwenda kucheza ligi zingine nje ya US! Hakutaka… bila shaka anachotaka yeye ni kurudi NBA; period!

Katika kuhakikisha anafanikiwa katika hilo, Hasheem akajiunga na coaching ya Frank Matrisciano na Milt Newton. Hawa jamaa wawili si watu wa mchezo mchezo linapokuja suala la individual training. Lakini kubwa zaidi Hasheem anaonekana kujitambua zaidi na kuonesha ni nini hasa anataka.

Rumors zinazoendelea ni kwamba, timu kubwa tatu za NBA zilituma watu wake kumwangalia for workout kwenye training camp ya Hasheem. Haya yametokea miezi sita tu tangu Hasheem aanze kujifua kwa dozi za kila siku za Matrisciano’s program.

Mtu wa mwanzo kutoa taarifa hizo ni Alex Kennedy kupitia mtandao wa Twitter. Alex ni Managing Editor wa Basketball Insiders.

Kwa mujibu wa rumors hizo, timu ambazo zilijitokeza mwezi uliopita ni LA Leakers, Washington Wizards na New York Knicks.

Waswahili wanasema Kufa Kufaana! Wakati Hasheem alifanyiwa workout na Wizards katika mazingira ya kawaida tu (labda ya kutaka kuimarisha safu yao ya ulinzi) lakini hivi sasa beki tegemeo wa Wizards, Ian Mahinmi atakuwa nje ya uwanja kwa takribani wiki 4 hadi 6 kutokana na kuwa majeruhi!!!

Kwa upande mwingine, wakati Knicks na Wizards walipeleka watu wao kwenye kambi ya mazoezi ya Hasheem, LA Leakers walienda mbali zaidi kwa kumpeleka Hasheem kwenye facility yao (ya Lakers) kwa siku mbili for free agent workout.

Trainers wa Hasheem, Frank Matrisciano na Milt Newton wanaamini Hasheem anaweza kurudi NBA! Tatizo ambalo analiona Frank ni NBA Community kuwa na perception ya Old Hasheem wakati Frank, kwa kuangalia improvement ya Hasheem; yeye kama Trainer anamuona Hasheem wa sasa ni tofauti sana na Old Hasheem inayesemekana ni mvivu na mtu asiyependa kujituma.

Ni matumani yangu kadri atakavyoendelea kupata workout ndipo chance ya kurudi NBA inaongezeka. Na bila shaka wapenda michezo na burudani watamuombea our only boy ili aweze kurudi NBA. Nothing impossible under the sun. Hata hivyo, Waswahili husema, Kisicho Riziki Hakiliki... NBA ikigoma si vibaya kuangalia ligi zingine duniani kama vile Euroleague. Umri unaenda, na in fact, muda si mrefu atakuwa beyond the expiry date. Katika hali kama hiyo mtu anatakiwa kuangalia zaidi maisha kuliko career. Hata ligi ya Uchina nayo si haba!

Diamond: Wasanii Wengi wa Kimataifa Wametaka Kujiunga na WCB ila Nimewakatalia

$
0
0
Diamond amedai kuna wasanii wengi wa kimataifa Afrika na nje ya Afrika wametaka kujiunga na WCB lakini amewakatalia kwa kuwa anatka kukuza wa nyumbani kwanza 
Pia amesema sasa hivi hawachukui wasanii wengine wachanga mpaka Ray vanny na harmonize wakue vizuri
Msikilize Hapa:

Install APP ya Blog Hii ya UDAKU SPECIAL Kwenye Simu yako Kutoka Google Play Kusoma Habari Kirahisi

$
0
0

Download  Application ya Udaku Special Blog Kwenye Simu yako Kutoka Play Store Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi

Bonyeza Hapa CLICK HERE 



Kwanini Sauti ya Diamond Live ni Mbaya Lakini Nzuri Kwenye Nyimbo Tofauti?

$
0
0
Jamani mi ni shabiki mkubwa na mzuri wa mziki wa bongo fleva, ila ili jambo linanipa wakati mgumu kuamini, huyu mkali wa bongo fleva diamond ana nyimbo kali sana ila kumekuwa na tofauti kubwa sana katika uwasilishwaji wa nyimbo hizo katika live performance na nyimbo tunazozisikia kwenye radio.

Diamond katika nyimbo ana sauti nzuri yenye base kidogo. Ila huyu jamaa sielewi kwanini akiimba live sauti inakua ingine kabisa yaani mbaya, mbona kina ben paul, banana, kiba king, rayvanny harmonise bela etc wakiimba live sauti inakua ile ile. au kuna ka application kwenye playstore anachokitumia kufanya sauti iwe nzuri studio.

Pia nafikiri sasa diamond aachie kina iyobo kucheza awapo jukwaani yeye afanye kazi moja tu ya kuimba, asijifanye michael jackson, na hii sasa ndo imekuwa weakness ya diamond ambapo mpinzani wake kiba anamfunikia.

Namshauri atafute mwalimu wa sauti na mziki wa live, vinginevyo hatutamuelewa . sauti ya jukwaani cjui ndo yake maana huwa mbaya, na akishindwa kabisa basi bana hata pua bwana

Kwaheri

EFM Yamburuza Paul James Mahakamani Kwa Kuvunja Mkataba, Yadai Fidia ya Shilingi Milioni 200

$
0
0
Mtangazaji wa Clouds FM, Paul James aka PJ ameshtakiwa mahakamani na kituo cha redio cha EFM kwa kuvunja mkataba kinyemela
Mtangazaji huyo aliondoka EFM mwanzoni mwa mwezi huu na kurejea kwenye kituo chake cha zamani, Clouds FM, alichoondoka pamoja na mwenzake Gerald Hando. EFM imefungua mashtaka katika mahakama ya kazi jijini Dar es Salaam kwa madai ya kukiuka mkataba wa kazi wa kituo hicho.

Kufuatia mashtaka hayo, EFM inadai fidia ya shilingi milioni 200 kutoka kwa mtangazaji huyo.
Inadai PJ alikatisha mkataba kiholela na kurudi tena Clouds FM bila kufuata makubaliano pamoja na sheria alizokubaliana nazo katika mkataba wake pale alipojiunga nacho.

Kesi hiyo imepangwa kusikilizwa November 23, 2016 katika mahakama ya kazi jijini Dar es Salaam.


Baada ya Ali Kiba Kusemwa Kuwa Anaishi Kwa Mama yake Kariakoo...Aamua Kuonyesha Nyumba yake

$
0
0
Baada ya kusemwa sana kuwa hana nyumba na anaishi kwa mama yake kko, hatimaye Ali Kiba. king kiba, King wa bongo flavour kaamua leo kuachia picha za mjengo wke uliopo Tabata thamani ya jiko la ndani ni milioni 19 soon nitawapa updates gharama za nyumba hii ambayo ni ghorofa na naamini ni kwake maana namuonaga hapo 
Pongezi kwa king kiba yooooh 

Viewing all 104789 articles
Browse latest View live




Latest Images