Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104793 articles
Browse latest View live

Wabunge Waliosimamishwa Kuhudhuria Bunge Waapa Kuendeleza Moto wa Kuichachafya Serikali Watakapo Rudi..!!

$
0
0

Wabunge wanane waliokuwa wamesimamishwa kuhudhuria vikao vya Bunge kwa muda na makosa tofauti wanatarajiwa kurejea kwenye chombo hicho cha kutunga sheria mwisho wa mwezi huu baada ya kumaliza kutumikia adhabu zao huku baadhi yao wakiahidi kuendeleza moto wa bajeti.

Wabunge watano kati ya hao waliopigiwa simu wamesisitiza kwamba wataendelea kubainisha jinsi bajeti iliyotengwa na Serikali wakati wanasimamishwa ilivyo na changamoto za utekelezwaji wake.

Mei, 2016 Bunge kupitia Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge ilipitisha azimio la kuwasimamisha kuhudhuria vikao vya Bunge baadhi ya wabunge wa Kambi ya Upinzani waliodaiwa kufanya vitendo vya vurugu ndani ya ukumbi na kudharau mamlaka ya Spika Januari, 27, 2016.

Wabunge hao ni Zitto Kabwe (Kigoma Mjini), John Heche (Tarime), Halima Mdee (Kawe), Tundu Lissu (Singida Mashariki), Pauline Gekul (Babati), Godbless Lema (Arusha Mjini) na Ester Bulaya (Bunda) ambao adhabu yao ilitokana na kitendo chao cha kupinga msimamo wa Spika kuhusu Bunge kuonyeshwa ‘live’.

Alichosema Anne Kilango Malecela Baada ya Kuteuliwa Tena Kuwa Mbunge...!!

$
0
0

MBUNGE mteule Anne Kilango Malecela amesema ameupokea uteuzi wa ubunge wa Rais John Magufuli juzi, na kusema kuwa Mungu ana sababu za kumrejesha tena katika nafasi hiyo, ambayo ameifanyia kazi kwa muda wa miaka 15.

Uteuzi wa Kilango unazidi kuongeza joto kuwa huenda kukafanyika mabadiliko katika Baraza la Mawaziri, ukizingatia uteuzi uliofanywa na Dk Magufuli wiki iliyopita wa kumteua aliyekuwa Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu (Wenye Ulemavu), Dk Abdallah Possi kuwa Balozi; pamoja na uteuzi wa wabunge wengine wawili.

Kabla ya Anne Kilango, Dk Magufuli pia alifanya uteuzi wa wabunge wengine wawili, Profesa Palamagamba Kabudi na Abdallah Bulembo kuwa wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, katika nafasi zake 10 alizonazo kwa mujibu wa Katiba.

Juzi usiku, Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, Ikulu ilitangaza kuwa Rais Magufuli amemteua Anne Kilango Malecela kuwa Mbunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, na kwamba ataapishwa kwa mujibu wa taratibu za Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Akizungumza na gazeti hili jana, Kilango alisema anamshukuru Mungu pamoja na Rais Magufuli kwa kuwa na imani naye na kuamua kumteua tena katika nafasi hiyo.

“Kwa kweli sina maneno mengi, namshukuru Mungu na pia ninamshukuru Rais wangu kwa kuwa na imani tena kwangu na kuamua kunipa nafasi hii. Nimekuwa mbunge kwa miaka 15, ni kazi ninayoielewa na ninamuomba Mwenyezi Mungu aniwezeshe ili nifanye kazi itakayowaridhisha,” alisema mbunge huyo wa zamani wa Same Mashariki mkoani Kilimanjaro, ambako alihudumu kwa miaka 15 hadi aliposhindwa katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015.

Mbunge huyo mteule alisema pia anakwenda bungeni kwa ajili ya serikali, wananchi pamoja na kwenda kukitetea chama chake (Chama Cha Mapinduzi) pamoja na kurekebisha pale panapostahili, lengo likiwa ni kuunga mkono Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Dk Magufuli.

“Mungu ana sababu ya kunirejesha tena bungeni. Nitakwenda kufanya kazi nitakitetea chama changu na kukikosoa pale panapostahili pamoja na kuwatetea wananchi wangu na serikali kwa ujumla,” alifafanua Kilango ambaye katika Bunge la Tisa, alijipambanua kuwa mmoja wa wabunge mahiri na kujikita katika kupambana na ufisadi.

Baada ya kushindwa Uchaguzi Mkuu kwa mgombea wa Chadema, mapema mwaka jana, Dk Magufuli alimteua kuwa Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, lakini alidumu katika nafasi hiyo kwa muda wa mwezi mmoja tu, baada ya Rais kutengua uteuzi wake Aprili 11, mwaka jana.

Alitenguliwa nafasi hiyo baada ya kutangaza kwenye vyombo vya habari kuwa mkoa wake hauna watumishi hewa, jambo ambalo lilisababisha Ikulu kufanya uchunguzi wake na kubaini kuwepo kwa watumishi hao, hivyo yeye na Katibu Tawala wake, Abdul Rashid Dachi wakaondolewa katika nyadhifa zao.

“Na wale wote wa Shinyanga ambao walisemekana ni zero, hakuna mtumishi hewa, walikuwa tayari wameshalipwa shilingi milioni 339.9, nimejiuliza sana, na nikajiuliza sana na kwa kweli nimejiuliza sana na kwa masikitiko makubwa, kwa nini Mkuu wa Mkoa alisema hakuna mtumishi hewa?” alisema Dk Magufuli wakati akitangaza kuwavua madaraka Kilango na Dachi.

Kilango ambaye ni mwanamke mpambanaji, mwishoni mwa utawala wa Serikali ya Awamu ya Nne ya Rais Jakaya Kikwete aliteuliwa kuwa Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi, wadhifa alioushikilia hadi wakati wa Uchaguzi Mkuu wa 2015.

Uteuzi wake huo pamoja na wa kina Profesa Kabudi na Bulembo, sanjari na kubadilishiwa kazi kwa Dk Possi, kunazidi kuongeza joto la mabadiliko katika Baraza la Mawaziri, kwani hadi sasa, katika wateule wote wa ubunge wa Dk Magufuli, wamepewa uwaziri ukiondoa mmoja, Naibu Spika Dk Tulia Ackson.

Wabunge wa Kuteuliwa na Dk Magufuli ambao baadaye aliwateua kuwa mawaziri ni Profesa Makame Mnyaa Mbarawa (Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano), Balozi Dk Augustine Mahiga (Mambo ya Nje ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki), Dk Philip Mpango (Fedha na Mipango), Profesa Joyce Ndalichako (Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi) na Dk Possi ambaye sasa amemteua kuwa Balozi.

Kwa uteuzi wa Kilango, Rais Magufuli amefikisha idadi ya wabunge wanane wa kuteuliwa na amebakiza nafasi mbili kwa mujibu wa Katiba. Anne Kilango ni nani?

Alikuwa Mbunge wa Same Mashariki kwa miaka kumi kuanzia 2005 hadi 2015 na alikuwa Mbunge wa Kuteuliwa na Rais kwa miaka mitano kuanzia mwaka 2000 hadi 2005.

Pitia Vichwa vya Magazeti ya Leo 23/1/2017..!!!

Lowassa Ashauriwa Kuachana na Siasa Ili Afaidi Uzee Wake Vizuri..!!!

$
0
0

MWENYEKITI wa Taifa wa Jumuiya ya Wazazi ya CCM, Abdallah Bulembo amemshangaa aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa kwa kuendelea kung’ang’ania siasa hadi sasa hivi, badala yake anastahili kukaa kimya kula maisha ili afaidi uzee wake vizuri.

Bulembo aliyasema hayo wakati akifunga kampeni za udiwani Kata ya Mateves iliyopo Wilaya ya Arusha juzi, ambako walitarajiwa kumchagua diwani wao katika uchaguzi mdogo. Mbunge huyo mteule wa kuteuliwa, alisema anashangaa Lowassa kung’ang’ania madaraka, badala yake anastahili kula maisha ili kufaidi uzee wake vizuri.

Alisema wapinzani wataruhusiwa kutumia barabara, maji, shule na vinginevyo, lakini kwenda Ikulu haiwezekani. Aidha, Bulembo alilaani kitendo cha wafuasi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kuingilia msafara wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) uliokuwa ukielekea Uwanja wa Ngorbob Sokoni kwa ajili ya kufunga kampeni za chama hicho.

Alisema wafuasi wa CCM ni wastaarabu na wavumilivu, hawakufanya fujo, bali waliwapita kwa mbele na kuelekea kwenye mkutano wa kufunga kampeni.

Mgombea Udiwani wa Kata ya Mateves, Julius Saing’ore maarufu kwa jina la Sovoyo na mgombea uenyekiti wa serikali ya kijiji, Mohamed Nassoro maarufu kwa jina la Arsenal, waliomba kura kwa wananchi hao ili walete maendeleo.

Mgombea udiwani Saing’ore aliwasihi wananchi wa kata hiyo, kumpa kura ili waliokwenda mahakamani kudai uchaguzi uliokuwa na kasoro wajue kuwa CCM ndio yenyewe.

Awali, Katibu wa Siasa na Uenezi wa CCM Mkoa wa Arusha, Shabani Mdoe alisema wananchi wana imani kubwa na chama hicho na hawataki porojo, bali wanataka maendeleo.

Alisisitiza kuwa awali alipokuwa madarakani aliyekuwa diwani wa CCM kabla ya kutenguliwa na mahakama mwaka jana, Saing’ore maarufu kwa jina la Sovoyo, alifanya kazi mbalimbali za maendeleo ikiwemo kuhakikisha wananchi wanapata maji safi na salama.

Alisema diwani huyo ambaye sasa anagombea tena, alikaa madarakani kwa siku 63 kama Diwani wa Kata ya Mateves kwenye Halmashauri ya Wilaya ya Arusha Vijiji (Arusha DC) hivyo kurudi kwake kama diwani kutawezesha wananchi kupata maendeleo

PICHAZZ..!! Hivi Ndivyo Rais wa Uturuki Alivyopokelewa Kwa Shangwe Kubwa na Waziri Mkuu Majaliwa..!!!

$
0
0

RAIS wa Uturuki Mheshimiwa Recep Erdogan amewasili nchini jana jioni (Jumapili, Januari 22, 2017) kwa ziara ya kikazi ya siku mbili na kupokelewa katika Uwanja wa Nde
ge wa Kimataifa wa Julius Nyerere  na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa na niaba ya Mheshimiwa Rais. Dkt. John Magufuli.

Rais huyo ameambatana na mkewe Mama Emine Erdogan pamoja na Mawaziri watatu ambao ni Waziri wa Mambo ya Nje Mheshimiwa Mevlüt Çavuşoğlu, Waziri wa Uchumi Mheshimiwa Nihat  Zeybekekci na Waziri wa Nishati na Maliasili Mheshimiwa Berat Albayrak

Pia Rais huyo ameambatana na wafanyabiashara wapatao 85 wa nchi hiyo.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU

Mchawi Akutwa Amekufa Akiwa na Kuku Mweupe..!!!

$
0
0

BIBI mwenye umri wa miaka 60 amekutwa amekufa mkoani Tabora huku amevaa nguo nyeusi aina ya kaniki, akiwa na vibuyu vitano na kuku mweupe, katika mazingira yanayoashiria kushiriki vitendo vya kishirikina.

Aidha, mwili wa mtu mwingine umekutwa pembeni ya mti aliokuwa akichimba dawa.

Taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tabora, Hamis Selemani iliwataja waliokutwa wamekufa kuwa ni Nsoma Dotto (60) mkazi wa Kijiji cha Zugimlole Wilaya ya Kaliua na Mayara Marashi (50) ambaye ni mkazi wa Igunga.

Kamanda Selemani alisema Nsoma alikutwa akiwa amekufa umbali wa mita 200 kutoka nyumbani kwake juzi.

Alisema bibi huyo alikutwa amevaa nguo nyeusi aina ya kaniki akiwa na vibuyu vitano huku pembeni yake kukiwa na kuku mweupe. Uchunguzi wa awali wa jeshi hilo, unaonesha kuwa huenda ni imani za kishirikina.

Aidha, alisema Marashi ambaye ni mkazi wa Kijiji cha Mwakapinga, Kata ya Nanga, aliyekuwa mganga wa kienyeji, mwili wake uliokotwa Januari 16, mwaka huu ukiwa umeanza kuharibika.

Kwa mujibu wa Kamanda Selemani, mganga huyo wa kienyeji aliondoka nyumbani kwake Januari 8, mwaka huu kwenda porini kuchimba dawa, lakini hakurudi kijijini hadi maiti yake ilipookotwa akiwa amekufa.

Alisema Polisi wanaendelea na uchunguzi wa kifo hicho. Aliwaomba wananchi wanaoenda porini kwa ajili ya shughuli zozote zile, wawe wanatoa taarifa kwa ndugu zao ili iwe rahisi tatizo linapotokea.

Mashabiki Wamgomea Darassa Kuachia Ngoma Mpya

$
0
0

Mziki imekuwa ni ngoma ya kihistoria katika maisha ya Darassa pamoja na Bongo Flava kwa ujumla kwa sasa. Naweza kusema ni ngoma ambayo imeishi muda mrefu na bado inazidi kufanya vizuri.

Haikuwa mategemeo yangu kuona watu watagoma kupokea kazi nyingine kutoka kwa mbabe huyo wa ‘Muziki’ ambaye ametumia ukurasa wake wa Instagram kuuliza kama mashabiki wake wapo tayari kupokea kazi mpya.

“Any new about #muziki before to drop another bullet please?” Darassa ameandika kwenye Instagram.

Hizi ni baadhi ya comments za mashabiki wake kuhusu post hiyo:

luganoh: Class Kwa maana ya soko miezi hii sio mizuri pia MUZIKI bado inafanya vizuri sana subili, endelea kula hela uliyo tengeneza mwaka 2016

runih_ Wahurumiee kidogo hta wapumue pumueee

galasagangijr: Utauwa @darassacmg

mwasandendetaimu: Subiria kidogo mpaka March
benritykev Utaua clax ckilizia kidogo

wema_la_diva: Hatareee we leta tyu

maeza_dam: Acha maneno letee muziki

alikibatz_fans: Noma

djmvungy: Vunga kidogo coz bado muziki ni Wimbo wa Taifa drop new kwny mwez6 hv @darasacmg

samuelnkangala: Usidondoshe kwanza mpaka muziki iishe utamu mwakan

adelicious58: Don’t drop yet muziki is still the talk in two n

tammylians: Hapana subiri tupoe kwanza siavicen Subir baba uwiiiiii muziki bado ni shidaah siuzoei aisee @darassacmg

umbeatz_ Afu wabongo bwana kwaiyo mnataka Darassa atulie adi wimbo wa muziki uchuje? Wimbo wa muziki auchuji leo wala kesho. Darassa angusha lingine

27minjesha: Muziki is still on..subiri kidogo bro..endelea kupiga show kidogo

top_barbie12: Tuleteee mamboooooo

kingkibamusics: @darassacmg vunga kwanz mana #muzik bado inasumbua dunia

Kwa upande wangu nasubiri kwa hamu sana ujio wa ngoma inayofuta baada ya Muziki ambayo mpaka sasa imetazamwa mara 3.6m kwenye mtandao wa Youtube

By Gami Dee
@gamideetz IG

Kubwa Kuliko..!!! Shilole Awatolea Uvivu Wanaolia Njaa na Kumlalamikia Magufuli..!!!

$
0
0

Msanii wa muziki wa bongo fleva Zuhena Mohammed alimaarufu kama Shilole amefunguka na kuwapa neno baadhi ya vijana ambao wamekuwa wakilalamika juu ya hali ngumu ya maisha huku wengi wao wakiitupia lawama Serikali ya awamu ya tano.

Shilole kupitia mtandao wake wa Instgram amesema amewachana baadhi ya vijana hao na kusema wamekuwa wakilalamika kuwa kuna hali ngumu ya maisha au pesa haipatikani ikiwa wao wenyewe hawahitaji kujishughulisha wamebaki kukaa vijiweni pasipo kuhangaika kutafuta mishe za hapa na pale za kuingiza kipato.

“Unalalamika hali ngumu huku umekaa” aliandika Shilole  ambae yupo mikoa ya kanda ya ziwa akifanya shows.

Baadhi ya mashabiki wa Shilole wamemuunga mkono kutokana na kauli yake hiyo huku wengine pia wakionyesha kutokubaliana naye wakiendelea kusema kweli maisha ya sasa ni magumu na mishe hakuna.

Hatariii!! ..Zitto Asakwa na Polisi kwa Uchochezi, Dereva Wake na Katibu wa Chama Wakamatwa ..!!

$
0
0

Naibu Katibu Mkuu wa ACT Wazalendo ndugu Msafiri A Mtemelwa ametoa taarifa kuwa kiongozi wa Chama cha ACT Wazalendo Mh Zitto Kabwe hajakamatwa na polisi na kusema yupo salama hapa hapa nchini.

Akitumia mtandao wa twitter wa Chama cha ACT Wazalendo Msafiri Mtemelwa anadai kuwa kiongozi huyo wa chama yupo salama lakini dereva wake ndg Patrick Muhidin pamoja na katibu wa Chama wa Jimbo la Kahama ndg. Vincent Ikerenge ndio walikamatwa na walipelekwa kituo cha polisi Kahama na kuandikishwa maelezo.

“Tunawajulisha kuwa kiongozi wa Chama cha ACT Wazalendo ndg. Zitto Kabwe, Mb hajakamatwa na polisi na yupo salama hapa hapa nchini. Tarehe 21/1/2017 Polisi wilayani Kahama wakiwa na magari 7 kati yao manne ya FFU walivamia mkutano wa Kampeni wa Chama katika kata ya Isagehe, Halmashauri ya Mji wa Kahama. Kiongozi wa Chama alikuwa jukwaani wakati polisi wanafika na aliendelea na hotuba yake mpaka mwisho na kumnadi Mgombea ndg Ibrahim Masele. Baada ya kushuka jukwaani, Kama kawaida 
yake alipeana mikono na wananchi na baadaye alipotea katika eneo Hilo” alisema Msafiri Mtemelwa

Kwa mujibu wa Naibu Katibu Mkuu wa ACT Wazalendo ndugu Msafiri Mtemelwa anadai wamefuatilia polisi kutaka kujua kwanini kiongozi wa Chama chao anatafutwa na polisi na kusema wamejulishwa kuwa ana mashatka ya kutoa lugha ya uchochezi katika hotuba zake za kampeni.

“Tumejulishwa na polisi kwamba Kiongozi wa Chama  ana mashtaka ya kutoa lugha ya uchochezi katika hotuba zake za kampeni katika kata ya Isagehe Jimbo la Kahama Mjini. Polisi wanasema Zitto Kabwe amemchonganisha Rais na wananchi kwa kusema kuwa Rais anakula bure na kulala bure ndio maana hajali hali ngumu ya maisha ya wananchi wakati huu wa balaa la njaa” ameandika Mtemelwa

Hata hivyo mbunge huyo wa Kigoma mjini na kiongozi wa Chama cha ACT Wazalendo kupitia viongozi wa chama cha ACT Wazalendo amesema polisi wataweza kumkamata iwapo yeye atataka kukamatwa na siyo kwa kuvamiwa bali kwa kuitwa rasmi na polisi na kuelezwa makosa yake.

“Chama kinalitaka jeshi la polisi kufuata taratibu za kukamata raia kwa mujibu wa sheria na pia protokali za kuwaita polisi viongozi wa Kitaifa Kama ilivyo kwa ndg Zitto. Chama kinajiandaa na wanasheria wake ili kwenda na KC kituo chochote cha polisi nchini Mara watakapopata wito wa kwenda polisi.”. Amesema Msafiri Mtemelwa

Prof Lipumba Anusurika Kipigo Kutoka kwa Vijana wa Ukawa, Akimbilia Msikitini Kujinusuru..!!!

$
0
0

MWENYEKITI wa Chama Cha Wananchi (CUF) anayetambuliwa na Msajili wa Vyama vya Siasa, Profesa Ibrahim Lipumba amenusurika kupigwa na vijana wanaoaminika kuwa ni wa Ukawa wakati akitoka kwenye mkutano wa kampeni mjini Morogoro.

Katika vurugu zilizotokea juzi jioni wakati vijana wa Ukawa na kikundi cha ulinzi cha CUF (blue guard) cha Dar es Salaam wakiwa na Profesa Lipumba walikuwa wakitoka kwenye mikutano ya kampeni maeneo tofauti walipokutana barabarani na kuanza kurushiana maneno na hatimaye kupigana.

Katika vurugu hizo, vijana wa Ukawa waliwazidi wenzao wa blue guard na Profesa Lipumba kulazimika kukimbilia kwenye Msikiti wa Mungu Mmoja Dini Moja ili kujinusuru.

Ghasia hizo zilizodumu kwa takribani saa moja na nusu ambapo baada ya Profesa Lipumba kukimbilia msikitini hapo, wafuasi wa Ukawa walibaki nje mpaka polisi walipofika na kuwatawanya.

Akizungumzia tukio hilo, Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, Leonce Rwegasira alikiri kutokea kwa vurugu hizo ambapo alisema wafuasi watatu wa CUF walijeruhiwa.

Alisema kuwa polisi wanaendelea na uchunguzi ili kuwabaini walioanzisha vurugu hizo ikiwa ni pamoja na kuweka doria kali katika mikutano ya vyama vya siasa.

Profesa Lipumba hakupatikana jana kuzungumzia suala hilo, baada ya simu yake kutokuwa hewani jana.

Alichokisema Tundu Lissu Baada ya Ukawa Kushindwa Kufurukuta Katika Uchaguzi wa Marudio..!!!

$
0
0

Anaandika Mwanasheria wa Chadema Tundu Lissu.

Waheshimiwa na makamanda poleni kwa mapambano na hongereni kwa kazi kubwa mliyoifanya kwenye chaguzi hizi. Naona kila mmoja wetu anasikitika jinsi matokeo ambavyo yamekuwa tofauti na matarajio yetu na kazi tuliyoifanya.

Ni rahisi, katika mazingira haya ya kushindwa na kabla vumbi halijaisha, kuanza kulalamika, kunyoosheana vidole na kukatishana tamaa. Hii haitusaidii sana. Badala yake, tunachohitaji zaidi ni 'brainstorming' kuliko 'blamestorming.' Naomba nifanye ya kwanza. Chaguzi ndogo za ubunge au udiwani ni ngumu sana kushinda katika mazingira halisi ya nchi yetu.

Mifano michache inathibitisha ukweli huu. Katika election cycle ya '05-'10, tulishinda Jimbo la Tarime lakini tukapigwa Biharamulo Magharibi na Busanda. Tarime lilikuwa Jimbo letu tangu Uchaguzi Mkuu wa '05, Busanda lilikuwa la maCCM na Biharamulo Magharibi lilikuwa la TLP. Sikumbuki vizuri kama tulishinda Kata hata moja katika mzunguko wa uchaguzi wa kipindi hicho.

Katika election cycle ya '10-'15, tulipigwa Igunga licha ya kazi kubwa tuliyofanya, lakini tukashinda Arumeru Mashariki iliyokuwa chini ya maCCM. Vile vile tulishindwa Kalenga, Chalinze na Ulanga Magharibi yaliyokuwa ya maCCM tangu Uchaguzi Mkuu wa '10.

Kwenye chaguzi za Kata za '12 kama mnakumbuka, licha ya kazi kubwa na rasilimali nyingi, tulipata Kata tatu tu kati ya 26 zilizokuwa zinagombaniwa. Ukiachia Ifakara Mjini ya Mh. Juakali, Kata nyingine mbili - Kiboriloni na Iseke - zilikuwa zetu tangu Uchaguzi Mkuu wa '10.

Kwa mantiki hii, matokeo ya jana sio ya kushangaza sana. Kata ya Duru ilikuwa ya kwetu na tumeitetea, nyingine zote tulikopigwa zilikuwa za maCCM. Hatujanyang'anywa iliyokuwa yetu, hatujanyakua zilizokuwa zao. Hata hivyo, funzo kubwa zaidi la historia ya chaguzi hizi ni hili hapa: licha ya kupigwa kwenye chaguzi ndogo hizi, tumeendelea kufanya vizuri zaidi katika kila Uchaguzi Mkuu uliofuatia kipigo cha chaguzi ndogo.

Mwaka '10 tulifanya vizuri zaidi licha ya kupigwa Busanda na Biharamulo Magharibi katika mzunguko wa '05-'10. In fact, tulichukua Jimbo la Biharamulo Magharibi mwaka huo. Na tulipata Kata nyingi zaidi '10 kuliko ilivyokuwa '05. Mwaka '15 tulipata ushindi mkubwa zaidi katika Kata na majimbo licha ya kupigwa kwenye chaguzi ndogo za mzunguko wa '10-'15.

Hoja yangu hapa ni kwamba uchaguzi wa marudio hauna direct and negative bearing kwenye matokeo yetu ya Uchaguzi Mkuu unaofuatia. On the contrary, uchaguzi wa marudio unatupa fursa ya kupanda mbegu ambayo, ikitunzwa vizuri, inakuwa na mazao bora kwenye chaguzi zinazofuatia.

Kwa upande mwingine, chaguzi za marudio - kwa sababu ya udogo au uchache wa maeneo yanayogombaniwa - yanawapa maCCM fursa ya kutumia nguvu kubwa za rasilimali na za kidola ukilinganisha na tunazotumia sisi. Kwenye Uchaguzi Mkuu unaofuatia, nguvu hizo zinasambazwa nchi nzima na kwa hiyo effectiveness yake inapungua.

Ndio maana tumefanya vizuri zaidi kwenye Uchaguzi Mkuu kuliko kwenye chaguzi ndogo za marudio. Hili, kwa maoni yangu, ndilo fundisho kuu la chaguzi hizi za marudio. Hatuna sababu kubwa ya kushangilia kutokana na matokeo ya jana. Hata hivyo, hatuna sababu yoyote ya kuomboleza pia. Obviously, maCCM na wapambe wao wataandika 'wasifu wa marehemu' wa CHADEMA/UKAWA na kuutangaza dunia nzima na kwa sauti kubwa. Hilo lisitupofushe macho yetu, hata kama linakera sana.

Tutathmini kazi tuliyoifanya na matokeo tuliyoyapata. Tupate mafundisho sahihi ya kazi hiyo na matokeo yake. Tutumie mafundisho hayo kwa kujipanga vizuri zaidi kwa ajili ya 'the real prize': 2020.

Mtatiro - Kilichotuangusha Ukawa Katika Marudio ya Uchaguzi ni Kutokuwa na Umoja na Mshikamano..!!

$
0
0


Na. Julius S. Mtatiro (23 Jan 2017).

Goodmorning. Katika uchaguzi huu mdogo CUF ilikuwa inatetea kata 1 ya Kimwani Muleba na CHADEMA ilikuwa inatetea kata 1 ya Duru, Babati. Kata zingine zote zilikuwa za CCM na zilikuwa zinatetewa na CCM.

Matokeo yanaonesha CCM imetetea viti vyake vyote vya udiwani (takribani 20), CUF imenyang'anywa kiti chake kimoja (Kimwani) na CHADEMA imelinda kiti chake kimoja (Duru).

Kwa vyovyote vile vyama mbadala haviwezi kujivunia matokeo haya kwani havikuweza kuishinda CCM, na CCM haina cha kutambia kwani imeongeza kata moja tu. Kwa saa nina mambo kadha ya kuzungumza;

1. Hali halisi inaonesha kuwa kama vyama mbadala vingeshirikiana vingelishinda kata si zaidi ya 7 hivi. Bahati mbaya mashirikiano haya yalikosekana tangu mwanzo baada ya upande wa "CUF ya Msajili na Bwana Yule" kusisitiza kuwa wataweka wagombea nchi nzima na hakuna UKAWA.

2. Lakini pia, hata shajihisho la ushirikiano mkubwa zaidi lililokuja kuzuliwa na kaka yangu Prof. Kitila Mkumbo lilifanywa TOO LATE kwa lengo la kutafuta sababu ya kujificha baada ya matokeo. Niliwahi kusema, kiuzoefu vyama haviwezi kuachiana maeneo wiki moja kabla ya siku ya uchaguzi na kushauri hivyo si kwa nia njema.

3. Baada ya CUF ya Msajili na Bwana Yule kujipanga kuvuruga uchaguzi huu na kushusha spirit ya UKAWA, vyama vya NCCR na CHADEMA pia vilionelea kila kimoja kijipiganie jambo ambalo ni kosa kubwa. Na madhara ya migawanyiko yote yalijulikana.

4. Uzoefu unaonesha kuwa, kuishinda CCM kwenye chaguzi ndogo ni nadra mno. Kuliwahi kuwa na mfululizo wa chaguzi ndogo, Tarime, Busanda, Tunduru, Mbeya Vijijini n.k. na kote huko CCM ilishinda isipokuwa Tarime na baadaye Arumeru. Katika chaguzi ndogo CCM hutawanya rasilimali zake nyingi zikajaa kwenye majimbo au kata hadi POMONI.

5. Mkakati wa DOLA na CCM kuvitumia baadhi ya vyama au baadhi ya viongozi kwenye vyama (mamluki) unaelekea kufanikiwa sana. Lakini, sera za "Self Protectionism" ndani ya vyama mbadala hata kwenye mambo yanayohitaji ushirikiano wa kitaifa zitaendelea kuvigharimu vyama vyetu.

6. Good News kwa ACT Wazalendo kwamba huenda ndicho chama kilichofanikiwa kwenye uchaguzi huu kuliko vyama vyote (CCM inclusive) kwani pamoja na uchanga wake kimevishinda baadhi ya vyama vikongwe kwenye kata chache (kwa idadi ya kura na si ushindi wa jumla). Na hiyo ni alert call kwamba ACT is needed in the UKAWA basket na kwa hiyo ianze ku BEHAVE like a true party wakati UKAWA pia ikiiandalia mazingira kisaikolojia.

7. Bado CCM inashinda chaguzi kwa kutumia mifumo ilele; rushwa, mabavu, hila, wawakilishi wa NEC na NEC yenyewe, uwezo wa uelewa wa wapiga kura (Mfano. CCM imepeleka uandikishaji wa Bima ya Afya kwa wananchi kata ya Nkome, wakati wa uchaguzi = Rushwa).

8. Vyama vya upinzani vinashindwa chaguzi hizi kwa sababu ya kukosa ushirikiano wa kweli baina ya vyama hivyo, maelezo namba 7 hapo juu na sentensi ya kwanza ya maelezo yaliyo namba 5 hapo juu.

9. Kwa hakika, matokeo haya hayana athari zozote za kufaulu kwa Magufuli katika sera zake au kushindwa kwa Magufuli katika sera zake. Yaani, CCM ya Magufuli haijawa na ushawishi wa ziada kwa wapiga kura ili kupata ushindi huu kwenye ngome zake. CCM bado inashinda chaguzi kibabe na kwa mkakati dola zaidi bila kujali nani yuko madarakani.

10. Sijaona connection yoyote kati ya matokeo haya na siasa za 2020. Vyama vyote vinayo fursa ya kuendelea kujipanga na kama tutafanikiwa kuuvunja mfumo dola unaoathiri vyombo vya uchaguzi na uhuru wake, unaoondoa mazingira sawa kwa vyama kufanya siasa n.k, mabadiliko ya kikatiba kwenye NEC na sheria za uchaguzi na mengine mengi, siasa za 2020 zitakuwa mbichi sana.

Nimechokoza mada, tujadiliane.

#Note; Haya ni maoni yangu binafsi, si ya CUF wala UKAWA.

#JSM@Jan2017.

Soma Hapa Hotuba ya Kusisimua ya Rais Donald Trump,Imetafsiriwa kwa Kiswahili..!!!

$
0
0

TRUMP: Jaji Mkuu Roberts, Rais Carter, Rais Clinton, Rais Bush, Rais Obama, Wamarekani wenzangu na watu wote duniani, asanteni sana. (MAKOFI)

Sisi, Wananchi wa Marekani, tunaungana katika juhudi za pamoja kitaifa kujenga nchi yetu na kutunza ahadi zake kwa watu wetu wote. (MAKOFI)

Pamoja, tutaamua hatima ya Marekani na dunia kwa ajili ya watu wote (na tutafanya hivyo) kwa miaka mingi ijayo. Tutakutana na changamoto, tutakutana na vikwazo, lakini tutahakikisha kazi inafanyika.

Kila miaka minne, tunakusanyika hapa kubadilishana madaraka kwa njia ya amani, na tunamshukuru sana Rais Obama na mke wa Rais Bi. Michele Obama kwa msaada wao mkubwa muda wote tulipokuwa tunafanya mchakato huo. Wamekuwa watu muhimu. Asanteni sana. (MAKOFI)

Pamoja na hayo, sherehe ya leo, ina maana kubwa, hatuko hapa kwa ajili tu ya kuhamisha madaraka kutoka utawala mmoja kwenda mwingine au kutoka chama kimoja kwenda chama kingine, lakini tuko hapa kuhamisha madaraka kutoka Washington D.C na kuyakabidhi kwenu, watu. (MAKOFI).

Kwa muda mrefu, kikundi kidogo kwenye mji mkuu wa nchi yetu kimekuwa kikivuna matunda ya serikali wakati watu wakibeba gharama. Washington iliendelea kuneemeka lakini watu hawakupata mgao wa utajiri wake. Wanasiasa walifaidika lakini kazi ziliondoka na viwanda vikafungwa. Mfumo wa Waanzilishi (The Establishments) ulijilinda na siyo kuwalinda wananchi wa nchi yetu. Ushindi (wa Waanzilishi) haukuwa ushindi wenu. Mafanikio yao hayakuwahi kuwa mafanikio yenu. Na wakati walikuwa wakisheherekea kwenye mji mkuu wa nchi yetu, familia zinazohangaika nchi nzima hazikuwa na cha kusheherekea. (MAKOFI)

Mabadiliko yote hayo yanaanzia hapa na yanaanza sasa hivi kwa sababu wakati huu ni wakati wenu na ni wakati unaomilikiwa na nyinyi. (MAKOFI)

TRUMP: Wakati huu unamilikiwa na kila mmoja aliyekusanyika hapa leo na kila mmoja anayetufuatilia akiwa sehemu yoyote hapa Marekani. Hii ni siku yenu. Hii ni sherehe yenu. Na hii, Marekani, ni nchi yenu. (MAKOFI).

Cha msingi siyo chama gani kinaongoza serikali yetu, cha msingi ni ikiwa serikali yetu inadhibitiwa na nyinyi, watu. (MAKOFI).

Tarehe 20 Januari 2017 itakumbukwa kama siku ambayo watu (Wa Marekani) walikuwa watawala wa taifa hili tena. (MAKOFI).

Wanaume na Wanawake wa nchi yetu hawatasahaulika tena. (MAKOFI).

Kila mmoja anawasikiliza hivi sasa. Mmekuja kwa wingi mno kwa makumi na mamilioni kuwa sehemu ya vuguvugu, mfano ambao dunia haikuwahi kuuona kabla. (MAKOFI).

Katikati ya vuguvugu hili kuna ahadi muhimu, kwamba taifa lipo kwa ajili ya kuwatumikia raia wake. Wamarekani wanahitaji shule bora kwa ajili ya watoto wao, majirani salama kwa ajili ya familia zao, kazi nzuri kwa ajili yao. Haya ni mahitaji halali na ya msingi ya watu sahihi na jamii sahihi.

Lakini sehemu kubwa ya watu wetu, wanakumbana na halisia tofauti: akina mama na watoto wameshikiliwa na umasikini ndani ya miji yetu; viwanda vilivyochakaa vimetapakaa kama makaburi kila kona ya nchi yetu; elimu yetu inatolewa kwa wenye pesa, jambo linaloacha wanafunzi wetu wadogo na wazuri wakinyimwa maarifa; na uhalifu na makundi ya kihalifu na madawa ya kulevya ambavyo vimeshachukua maisha ya watu wengi na kuiondolea nchi yetu nguvu kazi muhimu. Mabalaa hayo kwa Wamarekani yanasimamishwa mahali hapa na yanasimama sasa hivi. (MAKOFI)

Sisi ni taifa moja na maumivu yao ni maumivu yetu. Ndoto zao ni ndoto zetu. Na mafanikio yao yatakuwa mafanikio yetu. Tunashirikishana moyo mmoja, nyumba moja na matarajio ya aina moja. Kiapo cha Urais nilichokula leo ni kiapo cha utii kwa Wamarekani wote. (MAKOFI).

Kwa miongo mingi, tumekuwa tukitajirisha viwanda vya nje ya Marekani kwa gharama za viwanda vya Marekani; tumekuwa tukitoa ruzuku na kuyapa majeshi ya nchi nyingine, wakati tukiruhusu hali mbaya na ya kusikitisha kwa majeshi yetu. Tumekuwa tukilinda mipaka ya nchi nyingine na tukikataa kulinda mipaka yetu wenyewe. (MAKOFI).

Tumekuwa tukitumia trilioni na trilioni za dola za Marekani nje ya nchi yetu wakati miundombinu ya Marekani ikiwa imeanguka, kuharibika na kuoza. Tumekuwa tukizifanya nchi nyingine kuwa tajiri, wakati utajiri, uimara na kujiamini kwa nchi yetu kukipungua kwa kila namna.

Kimoja baada ya kingine, viwanda vikafungwa na vikaiacha ardhi yetu, bila hata kufikiria kuhusu mamilioni na mamilioni ya Wamarekani ambao walikuwa wanapotezewa kazi. Utajiri wa watu wa kati umeondolewa kutoka kwenye familia zao na kisha ukagawanywa katika nchi zote duniani. Lakini hayo yamepita. Na sasa, tunaangalia mbele tu. (MAKOFI).

TRUMP: Tumekusanyika hapa leo kutoa AMRI MPYA itakayosikika katika kila mji, katika kila mji mkuu wa nchi za Dunia yote, na katika kila sehemu yenye madaraka. Kuanzia leo kwenda mbele, dira mpya ndiyo itaongoza taifa letu. Kuanzia leo kwenda mbele, itakuwa ni Marekani kwanza, Marekani kwanza. (MAKOFI).

Kila maamuzi kuhusu biashara, kuhusu kodi, kuhusu uhamiaji, kuhusu mambo ya nje yatafanywa kuwanufaisha wafanyakazi wa Marekani na familia za Marekani. Lazima tulinde mipaka yetu dhidi ya mipango ya nchi nyingine kutengeneza bidhaa zetu, kuiba makampuni yetu na kuharibu kazi zetu. (MAKOFI).

Kujilinda kutapelekea tupate uimara na mafanikio makubwa. Nitawapigania kwa kila pumzi iliyomo kwenye mwili wangu. Na kamwe sitaawangusha. (MAKOFI).

Marekani itaanza kushinda tena, kushinda kuliko ilivyowahi kutokea. (MAKOFI).

Tutarudisha kazi zetu. Tutarudisha mipaka yetu. Tutarudisha utajiri wetu. Tutarudisha ndoto zetu. (MAKOFI).

Tutajenga njia mpya, na njia kuu na madaraja na viwanja vya ndege na mitaro na reli kila mahali katika nchi yetu kuu. Tutawatoa watu wetu kwenye matatizo na kuwarudisha wafanye kazi, kuijenga upya nchi yetu kwa mikono ya Wamarekani na Wafanyakazi wa Marekani. (MAKOFI).

Tutafuata kanuni mbili za kawaida; nunua Mmarekani na ajiri Mmarekani (Nunua bidhaa ya Marekani na toa ajira kwa Raia wa Marekani). (MAKOFI).

Tutatafuta marafiki na kuonesha nia njema kwa mataifa ya dunia, lakini tutafanya hivyo kwa kuelewa kwamba ni haki ya kila taifa kuweka mbele maslahi yake.

Hatutatafuta kuanzisha aina yetu ya maisha kwa taifa lolote, lakini badala yake kufanya maisha yetu yangare na kuwa mfano. Tutangara ili kila taifa lifuate mfano wetu. (MAKOFI).

Tutarejesha marafiki wa zamani na kukaribisha wapya na kuunganisha dunia iliyostaarabika dhidi ya Ugaidi wa Uislamu wa siasa kali, ambao tutauondoa katika uso wa dunia. (MAKOFI).

Katika kitovu cha siasa zetu kutakuwa na utii mkubwa kwa Marekani, na kupitia heshima kwa nchi yetu tutavumbua heshima kwa kila mmoja. Unapofungua moyo wako kwa ajili ya uzalendo, hakutakuwa na nafasi ya kuhujumiwa. (MAKOFI).

Biblia inatueleza namna ilivyo jambo jema pale watu wa Mungu wanapoishi pamoja katika muunganiko/muungano. Lazima tuseme yaliyomo katika fikra zetu kwa uwazi, tujadiliane mambo ambayo hatukubaliani kwa uaminifu, lakini muda wote tukilinda umoja wetu. Wakati Marekani inapoungana, hakuna awezaye kuisimamisha. (MAKOFI).

Hakupaswi kuwa na woga. Tunalindwa na siku zote tutalindwa. Tutalindwa na wanaume na wanawake wasio na mfano ambao wako kwenye majeshi yetu na vyombo vya dola. Na muhimu kuliko yote, tutalindwa na Mungu. (MAKOFI).

TRUMP: Mwisho, lazima tufikiri mbali na kuota ndoto kubwa zaidi. Marekani, tunafahamu kwamba taifa linaishi ikiwa tu linapambana kupata matokeo bora. Hatutaendelea kukubali wanasiasa ambao wanaongea bila vitendo, muda wote wanalalamika, lakini hawajawahi kufanya chochote ili kubadilisha kile wanachokilalamikia. (MAKOFI)

Muda wa mazungumzo hewa umekwisha. Sasa imefika saa ya vitendo. (MAKOFI).

Usiruhusu mtu yeyote akwambie kwamba haiwezi kufanyika. Hakuna changamoto inayoweza kuendana na jitihada na ari ya Marekani. Hatutashindwa. Nchi yetu itavuka na kushamiri tena.

Tunasimama wakati wa kuzaliwa kwa milennia mpya, tukiwa tayari kufungua majaribu ya anga, kuifanya dunia kuwa huru dhidi ya majanga ya magonjwa, na kujenga nishati, viwanda na teknolojia kwa ajili ya kesho. Tunu mpya za taifa zitakuwa ndani yetu, zitainua maono yetu na kuponya migawanyiko yetu.

Ni muda wa kukumbuka busara za zamani ambazo wanajeshi wetu hawawezi kusahau, kwamba hata kama sisi ni weusi au kijivu au weupe, sote tunavuja damu moja nyekundu ya wazalendo. (MAKOFI).

Sote tunafurahia uhuru wa kipekee na sote tunaipiga saluti, bendera moja kuu ya Marekani. (MAKOFI).

Na ikiwa mtoto amezaliwa katika eneo la Mjini la Detroit au maeneo yenye upepo mwingi huko Nebraska, wote wanaangalia anga moja ya usiku, wote wana ndoto moja, na wote wamepewa pumzi ya maisha na Muumbaji mmoja. (MAKOFI).

Kwa hiyo, kwa Wamarekani wote katika kila mji karibu na mbali, mdogo na mkubwa, mlima kwa mlima, bahari kwa bahari, sikilizeni maneno haya. Hamtadharauliwa tena. (MAKOFI).

Sauti zenu, matumaini yenu na ndoto zenu, zitaeleza ukuu wa Marekani yetu. Na ujasiri wenu na uzuri wenu na mapenzi yenu vitatuongoza siku zote katika njia tunayopita. (MAKOFI).

Pamoja, tutaifanya Marekani kuwa imara tena. Tutaifanya Marekani kuwa tajiri tena. Tutaifanya Amerika kujivuna tena. Tutaifanya Marekani kuwa salama tena. Na ndiyo, pamoja tutaifanya Marekani kuwa Kuu tena. (MAKOFI).

Asanteni sana. Mungu awabariki. Na Mungu aibariki Marekani. (MAKOFI).

#Note: Nimeifasiri baada ya maombi mengi. Nawatakia mjadala mwema.

Na. Mtatiro J (Imefasiriwa na JSM).

Baruapepe: juliusmtatiro@yahoo.com, Whatsup: +255 787 536759.

@#JSM2017.

Trump Awashukia Waandishi wa Habari,Adai Hakuna Watu Waongo Duniani Kama Wanahabari..!!!

$
0
0

SIKU moja baada ya Rais wa Marekani Donald Trump kuchukua 
hatamu ya uongozi wa taifa hilo amewashutumu waandishi wa habari akiwaita watu waongo zaidi dunuiani.

Trump ametoa kauli hiyo akionekanwa kukerwa na taarifa juu ya idadi ya watu waliohudhuria sherehe za kuapishwa kwake.

Wakati vyombo vya habari vikisema idadi ya watu waliohudhuria ni 250,000 kinyume na 900,000 waliokadiria awali, Trump anadai watu milioni 1.5 walihudhuria sherehe hiyo.

Idadi hiyo ni ndogo kulinganisha na watu milionin 1.9 waliohudhuria sherehe za kuapishwa kwa Rais aliyemaliza muda wake Barack Obama mwkaa 2008.

Msemaji wa White House, Sean Spicer, amesema vyombo vya habari vinaendesha kampeini ya kugawa watu kwa kuangazia habari ambazo hazina msingi wowote.

Hata hivyo, kanda za video za matangazo ya moja kwa moja wakati wa hafla hiyo hazikunasa umati mkubwa wa watu kama anaodai Trump.

Picha zinaonekana zikionyesha watu wengi zaidi waliohudhuria shereha ya kupishwa kwa Rais Barack Obama mwaka 2009.

Trump hakuzungumzia maandamano ya watu wanaompinga wakati akitembelea Makao Makuu ya Shirika la Ujasusi Marekani (CIA) katika Jimbo la Virginia juzi, badala yake alivishambulia vyombo vya habari.

Trump alisema kuwa video na picha wakati wa kuapishwa kwake zilionyesha taarifa ziziso za ukweli.

“Walionekana watu kama milioni 1.5 siku ya Ijumaa, alisema Trump, akipinga ripoti za vyombo vya habari kuwa walikuwa watu chini ya 250,000.

“Ndio maana nasisitiza kwamba waandishi wa habari ni watu waongo zaidi duniani.”

INATISHAAH..!!!,Njemba Yavamia Watu na Kuwachoama Visu Ovyo..!!!

$
0
0
 
Inatisha! Njemba mmoja, Shadra Maninje ‘Idd’, anashikiliwa na polisi kwa tuhuma za kuwaua watu wawili na kujeruhi wengine wanne kwa kuwachoma visu sehemu tofauti za miili yao akiwemo mtoto wa kike, Fatuma Hamis mwenye umri wa miaka miwili.


Wakizungumza na Wikienda lililofika eneo la tukio, kila shuhuda alikuwa na lake la kusema kutokana na mshangao walioupata.

“Hatujui nini kilimpata Idd kwani alionekana amelewa na alipokuwa anakutana na mtu anamchomachoma visu. Alimchoma Miraji Kondoa kisu cha kifuani na kufariki dunia.

“Pia inasemekana kuna mwanachuo wa NIT wa kike alimchoma kisu na yeye alifariki dunia.

“Mbali na hao alimchoma kisu mfanyabiashara aliyefahamika kwa jina la Jackson Mushi ‘Rasta’ sehemu ya tumboni na utumbo kuonekana. Baadaye wasamaria walimpeleka Hospitali ya Mwananyamala.

“Baada ya kufanya matukio hayo, watu walianza kumkimbiza huku wakiwa wameshika mawe. Alipoona hivyo alikimbia na kupotelea uchochoroni lakini cha ajabu alipofika huko nako alimchoma kisu mwanafunzi wa NIT,” alisema mmoja wa mashuhuda huyo akiungwa mkono na mwingine:

“Mbali na huyo kuna mama mwingine ambaye hajafahamika naye alichomwa kisu cha tumboni na kutokezea mgongoni na inasemekana hali yake ni mbaya sana.”

Katika tukio hilo, wanahabari wetu walizungumza na mmoja wa majeruhi ambaye ni mwanafunzi wa NIT, Maiko Erasto (26) ambapo alisimulia:

“Nilikuwa ndani na mwenzangu, ghafla tulisikia kishindo cha kitu kuanguka nje, nikatoka ili kufahamu kilichotokea, nilipofungua mlango nikamuona jamaa ambaye sikuwa namfahamu, akanyanyua kisu kunichoma kichwani nikakwepa lakini kikanipata begani.

“Baada ya kuona vile, mwenzangu alinivuta chumbani na kuufunga mlango, kumbe pale nje kulikuwa na mtoto wa kike (Fatuma Hamis) ambaye naye alichomwa kisu shingoni na ameshonwa nyuzi 8.”

Naye Mwenyekiti wa Mtaa wa Jitegemee,  Kilema alikiri kutokea kwa tukio hilo la kusikitisha na kusema kuwa kuna watu walipoteza maisha na wengine kujeruhiwa na mtuhumiwa huyo ambaye alikamatwa na kufikishwa katika Kituo cha Polisi cha Urafiki jijini Dar.20170122_0819380
Wakazi na wafanyabiashara wa Mabibo jijini Dar es Salaam wakiwa wameizunguka ofisi ya soko la Mabibo-Mwisho alimohifadhiwa mtu anayetuhumiwa kuua na kujeruhi watu kadhaa katika soko hilo kabla polisi hawajafika.

Haya Ndio Majibu ya Mrithi wa Kanumba Kuhusu Lulu ...!!!

$
0
0

KUTOKANA na hivi karibuni mama wa aliyekuwa staa mkubwa wa filamu, Steven Kanumba, Flora Mtegoa kumwanika kijana Fredy Swai kuwa ndiye mrithi wa mwanaye, msanii wa filamu nchini, Michael Sangu ‘Mike’, alibadilika muonekano usoni baada ya mmoja wa wafanyakazi wa Global publisher alipomuhoji maswali na kumtaka ajibu ndio au hapana.

Mike aliulizwa kama anamawasiliano na muigizaji wa kike Elizabeth Michael ‘Lulu’, alikosa jibu la moja kwa moja na alijibutofuti na maswali aliohojiwa mwanzo, kwa hali ya kujilazimisha alijibu kuwa hana namba ya Lulu huku akionesha hali ya kukosa amani.

Bado haijafahamika kwanini alitahamaki vile kiasi cha kushindwa kufuata sheria za maswali ya ndio ua hapana yeye alitoa maelezo.Akizungumza na Global Tv Online, Mike alisema hana namba ya Lulu na hajawahi kukutana na Lulu na endapo atakutana nae ataongelea kazi tu kwani amekuwa akizifuatilia sana kazi zake na si vinginevyo.

GEITA : Wachina Wafanya Unyama Tena, Wapiga Mtu Hadi Kulazwa Hospitalini Huku Hajitambui..!!!

$
0
0

Mkazi wa Kijiji cha Nyarugusu Mkoani Geita, Elisha Sylvester (26) amelazwa katika wodi nane katika Hospitali teule ya Mkoa wa Geita huku akiwa hajitambui baada ya kudaiwa kupigwa na raia wawili wa China

Hili ni tukio la pili kutokea mkoani hapa baada ya Julai 6 mwaka jana mkazi wa Kijiji cha Nyamitondo tarafa Butundwe, Masanja Shilomero (25) kushambuliwa na mwajiri wake ambaye ni raia wa China Myo baada ya kuomba kupandishiwa mshahara

Hata hivyo Sylvester anadaiwa kufanyiwa unyama huo Januari 19 mwaka huu ndani ya mgodi unaomilikiwa na wachina hao uliopo katika kijiji cha Mawemeru, Kata ya Nyarugusu wilayani Geita

Mashuhuda wa tukio hilo walidai kuwa wachina hao ambao majina yao hayakupatikana walimshambulia kijana huyo ambaye ni Mfanyakazi wa mgodi huo kwa fimbo, ngumi na mateke baada ya kumtuhumu kuiba mawe mawili ya dhahabu

"Baada ya kijana huyo kupigwa, alifikishwa katika kituo kidogo cha polisi Nyarugusu na kuchukuliwa maelezo kisha kupewa PF3 na kulazwa kwenye zahanati ya Nyarugusu akipatiwa matibabu". alidai shuhuda huyo.

Kudadeki..!! Tazama Hapa Alichosema Ommy Dimpoz Juu ya Mjengo Wake Anaoporomosha Huko Mbezi..!!!

$
0
0

Msanii wa muziki wa bongo fleva Ommy Dimpoz ambaye bado anafanya vyema na wimbo wake 'Kajiandae' amefunguka na kusema hajapangishiwa nyumba Mbezi na jimama kama ambavyo inadaiwa na kudai kuwa kwa sasa yeye anaishi Mikocheni. 

Ommy Dimpozi akiongea na EATV alisema hana nyumba ambayo amepangisha wala hajapangishiwa nyumba ila kwa sasa anafanya ujenzi katika viwanja vyake viwili Mbezi pamoja na Kigamboni.

"Unajua binadamu wanaweza kuongea hiki na hiki lakini ukweli ni kwamba mimi naishi Mikocheni kwenye apartment hivyo siishi Mbezi, ila Mbezi kuna sehemu nina site yangu ambayo najenga na site nyingine ipo Kigamboni. 

Kwa hiyo sina nyumba ambayo nimepangisha au nimepangishiwa kwa hiyo hizo stori sijui bimkubwa sijui nini siyo kweli, mimi mambo yatakapokuwa tayari nitamuweka wazi mtu wangu ila demu wangu si Mzungu ni Mchina" alisema Ommy Dimpoz.

Tobaah..!! Nay wa Mitego Afunguka Juu ya Bifu na Mama Yake Mzazi,Adai Kuwa Hajaongea Naye kwa Miaka Mitano..!!!

$
0
0

Rapa Nay wa Mitego ambaye anafanya vyema na wimbo wake 'Sijiwezi' amefunguka na kusema kuwa ni kweli alikuwa amezinguana na mama yake mzazi na walikaa miaka mitano bila kupiga stori yoyote ile. 

Nay wa Mitego alisema haya kupitia kipindi cha Planet bongo na kusema kwa sasa wameshamaliza tofauti zao na anaishi na mama yake mzazi ingawa anakiri kuwa ni kweli ameishi zaidi ya miaka mitano bila kuongea na mama yake mzazi.

"Mimi na mama mzazi tuko poa sana na nina kaa naye this time, ni kweli kabisa tumekaa miaka mitano bila kuzungumza jambo lolote lile ila ni mazingira ya maisha ya mtaa niliyokuwa naishi lakini mpka muda huu tunaongea mimi naishi na mama yangu nyumbani kwangu, hivyo niko naye nyumbani" alisema Nay wa Mitego 

Mbali na hilo Nay wa Mitego anasema yeye haamini katika dini kwani anaona dini nyingi saizi zimekuwa biashara, hivyo yeye anamini Mungu na anajua Mungu yuko kila sehemu si lazima iwe kanisani.

Live Bila Chenga..!!Mtoto wa Mbunge Anaswa Usiku na Golikipa wa Timu ya Mtibwa Sugar Wakipeana Mahaba Mazito+Pichazz

$
0
0

Binti wa aliyekuwa Mbunge wa Mafia, Abdulkarim Shaa (CCM), Naima Shaa amezua balaa kwa mara nyingine baada ya kunaswa akijiachia kwa mapozi ‘tata’ na golikipa namba moja wa Timu ya Mtibwa Sugar, Saidi Mohamed ‘Nduda’.
naimaTukio hilo lililoacha gumzo kwa muda lilijiri katika Ukumbi wa Maisha Basement, Kijitonyama, Dar ambapo wawili hao walikuwa wamekwenda kustarehe.

Kwa kamera ya shushushu wetu, Nduda alifika ukumbini hapo akiwa na washkaji zake na Naima naye alikuwa kivyake lakini walipokutana hali ilibadilika na kuanza kufanya yao.naima-na-manyika-jr-3-001Naima Shaa akiwa na Manyika JR
“Walionesha kama watu waliomisiana kitambo. Nduda alipomuona Naima tu, alimfuata harakaharaka na kuanza kupiga naye mapicha tata kabla ya kukumbatiana na kuzungumza kwa muda huku wengine wakisema kuwa ni mrithi wa aliyekuwa mpenzi wa mwanadada huyo ambaye ni kipa wa Simba, Peter Manyika Jr,”naima-na-manyika-jr-2“Baada ya kujiachia kwa mapichapicha, wawili hao walipoulizwa kama kwa sasa ni wapenzi hawakuwa tayari kufunguka.naima-2 alifunguka shushushu wetu na kuongeza:“Zaidi sana waliendelea kuburudika kwa muda kabla ya mwishoni kabisa kutokana na wingi wa watu waliokuwemo ukumbini hapo, haikujulikana mara moja kama waliondoka pamoja.”
naima-1naima-na-manyika-jr-1Naima ambaye aliwahi kuwa mke wa mfanyabiashara wa jijini Dar, Mwanamboka, aliwahi kuripotiwa kumzidi kete aliyekuwa shosti wake, Wema Isaac Sepetu na kudaiwa kumpora kigogo wake aliyekuwa maarufu kwa jina la CK.Mbali na hilo, pia aliwahi kuripotiwa kuwa na uhusiano wa kimapenzi na msanii wa Bongo Fleva, Aslay Isihaka ‘Dogo Aslay’ hadi kujichora tatuu ya msanii huyo. Baada ya kuachana na Dogo Aslay, Naima alitumbukia kwenye penzi la Peter Manyika Jr kabla ya uhusiano wao kukata kamba miezi kadhaa iliyopita.
Viewing all 104793 articles
Browse latest View live




Latest Images