Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104795 articles
Browse latest View live

Tazama Video ya Rais Magufuli Akihutubia Kwa Kiswahili Kwenye Mkutano wa Viongozi wa Afrika..!!!


Gazeti la MwanaHalisi Lapewa Saa 24 Kuomba Radhi Kwa Kumchafua Rais Magufuli

$
0
0
Gazeti la MwanaHalisi Lapewa Saa 24 Kuomba Radhi Kwa Kumchafua Rais Magufuli

Simu Yaweza Kumuingiza Matatizoni Paul Pogba

$
0
0

 Kiungo wa bei kubwa wa Manchester United, Paul Pogba anaweza kuingia matatani baada ya kuonekana akiendesha gari huku akitumia simu kitu ambacho ni kinyume na sheria za uendeshaji gari nchini England.

Pogba ameonekana akiendesha gari lake aina ya ua Audi RS6-R lenye thamani ya pauni 85,000 alipokuwa akiwasili mazoezini kwenye Uwanja wa Carrington, Ijumaa iliyopita.

Picha zimemuonyesha akiwa ameishika simu yake hiyo huku akiendesha gari na kama mamlaka husika za usalama barabarani zitaamua kutumia picha hiyo zinaweza kumuingiza matatizoni.

Wanachama 200 Waikimbia CHADEMA na Kujiunga CCM

$
0
0
Chama   cha  Demokrasia  na Maendeleo (Chadema), kimeendelea  kupata  pigo  baada  ya  wanachama  200, wakiwamo  viongozi  wa Kitongoji  cha Kwemghogho Mahezangulu kujitoa  na  kujiunga  na  Chama Cha Mapinduzi (CCM) .

Akizungumza  baaada ya  kupokea  wanachama  hao, Mbunge wa  Bumbuli, January Makamba (CCM),  alisema  wananchama  hao  wameamua  kurudi  wenyewe nyumbani   kutokana  na   kuona  ahadi  nyingi  za maendeleo zimetekelezwa  kwa  kiasi kikubwa.

Alisema  chama  chake kimefanya mambo mengi  hivyo  haoni  ajabu  ya  kupokea  wanachama kutoka  vyama  vingine  vya  upinzani.

January, ambaye pia ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais anayeshughulikia Muungano na Mazingira, alisema  hivi sasa kuna kazi kubwa ya kuendelea kuleta maendeleo ambayo yanahitaji umoja  na mshikamano.

Alisema migogoro, majungu na fitina inatokana na kambi  zilizokuwapo huku akiwasisitiza wana CCM watambue ni hema kubwa na linavumilia tofauti za watu.

Aliyekuwa  Mwenyekiti wa  Chadema  Kitongoji cha Kwemghogho, Shabani Kahema,  aliwataka   vijana  na  wanachama  wengine  kubadilika kwa kuwa CCM ndiyo chama chenye ilani inayotekelezeka.

Afariki kwa Kipigo Baada ya Kufumaniwa Akila Raha na Mke wa Mtu,Stori Kamili Hii Hapa..!!!!

$
0
0

WATU watatu wilayani Igunga mkoani Tabora wamekufa akiwemo mwanaume aliyeuawa na kundi la wananchi baada ya kufumaniwa akifanya mapenzi na mke wa mtu. Watoto wawili wa familia moja wamepoteza maisha kwa kuzama kwenye shimo la maji.

Akizungumza jana mjini Tabora, Kamanda wa Polisi wa Mkoa, Kamishna Msaidizi Hamisi Selemani amesema katika tukio la Januari 28, mwaka huu katika Mtaa wa Stoo, Kata ya Igunga Mjini, mkazi wa Mtaa wa Masanga, Khalid Kassim (50) aliuawa na kundi la wananchi zaidi ya 100 ikidaiwa alifumaniwa akifanya mapenzi na mke wa mtu.

Kamanda Selemani amefafanua kuwa Kassim alifumaniwa na mwenye mke, Muungano Isaack (44) mkazi wa Mtaa wa Stoo.

Amesema baada ya kumfumania, Isaack alipiga kelele kuomba msaada, ndipo wananchi walitoka kwa wingi na kumshambulia kwa kipigo Kassim.

Amebainisha kuwa polisi walipata taarifa na kufika katika mtaa huo na kukuta wananchi wakiwa wamekimbia, hivyo askari walimchukua mtuhumiwa na kumpeleka Hospitali ya Wilaya ya Igunga ambako aliaga dunia wakati akipatiwa matibabu.

Kamanda Selemani amesema katika tukio la pili lilitokea siku hiyo, katika Kijiji cha Mwazizi Kata ya Bukoko, watoto wawili wa familia moja, Gumba Ngasa (2) na Kija Ngasa (1) wote wa kike, walizama maji na kufariki dunia wakati wakivuka maji.

Kamanda amesema watu wawili, Muungano Isaack na Maria Joseph wanashikiliwa na Polisi huku wengine walioshiriki mauaji ya Kassim wanaendelea kutafutwa na jeshi hilo.

Ametoa mwito kwa wazazi kuwa makini na kipindi cha masika kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha.

Kaimu Mganga Mkuu wa Wilaya ya Igunga, Dk Godfrey Mgongo amesema uchunguzi wa awali unaonesha kifo cha Kassim kilisababishwa na kuvuja damu nyingi kichwani kutokana na majeraha aliyokuwa nayo.

Aidha, Dk Mgongo alibainisha kuwa vifo vya watoto wawili Gumba na Kija vilisababishwa na maji mengi waliyomeza baada ya kuzama.

Mwili wa Mwanafunzi Waopolewa Ziwani

$
0
0

Mwili wa mwanafunzi wa kidato cha tatu katika Sekondari ya Chato mkoani Geita, Shilinde Nicolaus (18) umeopolewa Ziwa Victoria baada ya kuzama Januari 28 saa tisa alasiri alipokuwa akivua na wenzake.

Kamanda wa Polisi mkoani Geita, Mponjoli Mwabulambo alisema  mwili huo ulipatikana juzi baada ya jitihada za wavuvi wa eneo hilo kwa kushirikiana na wananchi.

Mwenyekiti wa Serikali ya Kijiji cha Muungano lilipotokea tukio hilo, Kapembe Charles alisema kijana huyo na wenzake ambao walinusurika, walipata ajali hiyo  baada ya mtumbwi wao kupigwa na dhoruba kisha kuzama.

Charles alisema katika tukio hilo wenzake wawili, Daud Deus na Mgonyolo Hamis wote wakazi wa Kijiji cha Kitela walinusurika  baada ya kuogelea hadi nchi kavu.

Mmoja wa wanafunzi hao, Daud Deus alisema wakati wakiendelea  kuvua, kulikuwa na upepo mkali uliosababisha mtumbwi wao kuzama.

“Mimi na Hamis tulifanikiwa kuogelea kwenye majani yaliyoota ndani ya maji, kisha tukaokolewa na wavuvi,” alisema Deus.

TRA Kutoongeza Muda wa Usajili wa TIN namba Baada ya Leo..!!!

$
0
0

Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imesema haitaongeza siku za kufanya uhakiki wa namba ya utambulisho wa mlipakodi (TIN) hapa jijini baada ya muda kumalizika leo, hivyo wote watakaokuwa hawajahakikiwa watafutiwa namba zao na watatakiwa kuomba upya.

Kwa mara ya kwanza TRA imepanga kufanya uhakiki wa TIN kwa siku 60 kati ya Agosti na Oktoba lakini baada ya kujitokeza watu wengi tarehe ya mwisho iliongezwa hadi Novemba na mara ya tatu ilisogezwa hadi Januari 31. Lengo la uhakiki huo ni kuondokana na mfumo wa kizamani wa usajili wa namba hiyo.

Kayombo alisema kutokana na idadi kubwa ya watu waliokuwa wanahitaji kuhakikiwa namba, mamlaka iliamua kusogeza mbele muda wa kutoa huduma hiyo pamoja na kufungua vituo vya kutoa huduma ambako watumishi walifanya kazi hiyo hadi Jumamosi na Jumapili kuwapa nafasi wafanyakazi.

Alisema madhara kwa watakaofutiwa TIN ni makubwa kwani wafanyabiashara na madereva wa magari leseni zao zitakuwa batili na watachukuliwa hatua kwa kosa la kufanya biashara bila kuwa na namba ya utambulisho.

“Wale wote ambao watakuwa hawajahakikiwa watafutiwa namba zao za TIN, itawalazimu kuomba upya ingawa kuomba kwao upya hakutafuta madeni yao ya nyuma,” alisisitiza Kayombo.

Mmoja wa watu waliokwenda kuhakiki namba zao kituo cha Mwenge, Abdul Namwelesi alikosoa utaratibu huo akipendekeza uhakiki ungekuwa endelevu badala ya kuweka muda maalumu kutokana na ugumu wa watu wote kuhakikiwa kwa wakati mmoja.

Pata Bidhaa za Kiafya Kutoka Kwa Markson Beauty...Kungarisha Ngozi, Kukuza Makalio na Vingine

$
0
0


MWAKA MPYA NA
MAMBO MAPYA

Katika kusherehekea miaka kumi na saba (17) MARKSON BEAUTY tumezindua bidhaa mpya za mwaka 2017 kwa mafanikio makibwa.
Bidhaa mpya zimeboreshwa mara 3 zaidi hivyo zina matokeo ya haraka sana. Bidhaa zetu zimetengenezwa kwa mimea na matunda na kuthibitishwa ktk mamlaka husika. (NO SIDE EFFECTS).j

BIDHAA MPYA NA BEI:-
1.Kerefusha nywele na kuzuia kukatika ovyo @120,000/=
2.Kuongeza shepu (hips na makalio) kwa (a)Dawa ya kunywa au kupaka @150,000/=
(b)Vidonge @170,000/=
3.Kuwa mweupe na softi mwili mzima kwa :- (a)mafuta @120,000/=
(b)Vidonge @150,000/=
4. Kupunguza unene na manyama uzembe @150,000/=
5. Kuongeza uume pamoja na nguvu za kiume kwa :-
(a)Gely ya kupaka @120,000/=
(b)Vidonge @120,000/=
(c)Mashine original ya HANDSOME UP @180,000/
6.Kuondoa mvi milele zisiludi tena @120,000/=
7.Kuongeza hamu ya kula, unene na uzito wa mwili mzima @120,000/=
8.Kupunguza tumbo (kitambi) na nyama za pembeni kwa :-
(a)Dawa ya kunywa au kupaka @ 120,000/=
(b)Mkanda (corset) 150,000/=.
9.Kubust maziwa na kuyasimamisha @100,000/=
10.Kushepu miguu na kuwa minene @120,000/=
11. Kuondoa mipasuko mwilini (michirizi) @100,000/=.
12.Kurudisha usichana (bikra) @120,000/=
NB. HAKIKISHA UNAPATA RISITI YENYE MUHURI HALISI WA MARKSON CO PAMOJA NA GARANTII ILI KUKUHAKIKISHIA KUFANIKIWA KWAKO.

Popote ulipo duniani
Wasiliana nasi kwa (+255) 0767447444 au 0714335378. Utapata huduma zetu.
(Google seach MARKSON BEAUTY)

CCM - Chadema Wanasababisha Migogoro ya Ardhi..!!!

$
0
0

MWENYEKITI wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wa Wilaya ya Monduli mkoani Arusha, Loota Sanare amesema halmashauri ya wilaya hiyo inayoongozwa na Chadema, inachochea migogoro ya ardhi na chama hakitakaa kimya kwa hilo.

Sanare alisema hayo juzi katika mkutano wa hadhara wa kijiji cha Lendikinya, uliohudhuriwa na vijana wa jamii ya Kimasai (morani) na wazee wa mila (Laigwanani) zaidi ya 300, kueleza ardhi ya kijiji hicho inayotaka kunyang’anywa na halmashauri hiyo.

Alisema vijana wa kimorani, Laigwanani na watu wengine akiwemo yeye mwenyewe Sanare, wanamiliki ardhi iliyopo katika kijiji hicho kwa kufuata michakato yote ya kisheria na hatimaye kupata hati ya kumiliki ardhi.

Alisema amesikitishwa na kauli ya Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Monduli, Isack Joseph kutangaza baadhi ya watu kuwa wanamiliki ardhi katika msitu huo kinyume cha sheria.

Alisema CCM haitavumilia uchochezi unaofanywa na baadhi ya viongozi wa halmashauri kwa maslahi binafsi.

Pia, alisema CCM haitavumilia kuona mwananchi yeyote anaonewa.

Sanare alisema yeye alipata shamba hilo kama mwananchi wa kijiji hicho na hakuchukua shamba hilo kama kiongozi wa CCM. Alisema kitendo cha kuingiza chama katika mambo yake binafsi kimemsikitisha, hivyo na yeye hatavumilia hayo.

Alisema si yeye tu anayemiliki ardhi katika kijiji hicho, kwani hata Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema, Edward Lowassa (Waziri Mkuu mstaafu) ana ekari za kutosha katika eneo hilo pamoja na diwani wa Monduli Juu na wengine walioko ndani ya Chadema.

Lakini, alisema hao wote hawakuguswa, kwa sababu ni wana Chadema.

Alidai huo ni ubaguzi na uchochezi na unapaswa kupigwa vita. Mjumbe wa Kamati ya Siasa ya Wilaya ya Monduli, Amani Ole Silanga, aliwataka wanakijiji kuwa na subira, kwani huo ni upepo mchafu unaovuma kupitia baadhi ya viongozi wa halmashauri na baraza la madiwani.

Alisisitiza kuwa upepo huo mchafu utapita. Laigwanani, Oleleku Ndeese aliitaka CCM kusimamia hilo kwani Chadema iko Monduli kutaka kupora haki za watu na hilo halitavumilika kamwe na ameomba wasaidie damu isimwagike.

Morani, Songoro Matata alihamasisha wanakijiji walioko kwenye vyama vya siasa kupima na kuona ni chama gani kipo kutetea maslahi ya wananchi na kukifuata chama hicho.

Hivi karibuni Baraza la madiwani la Halmashauri ya wilaya ya Monduli, lilipitisha azimio la kuchukua ardhi ya kijiji hicho kwa madai kuwa waliochukua ardhi hiyo hawakufuata sheria, akiwemo mwenyekiti wa CCM wa wilaya hiyo.

Pitia Vichwa vya Magazeti ya Leo 31/1/2017..!!!

Serikali Kutoa Majibu Juu ya Hali ya Chakula Nchini Leo Bungeni..!!!

$
0
0

MKUTANO wa Sita wa Bunge la 11 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania unaanza leo mjini Dodoma. Serikali inatarajiwa kutoa kauli mbili kuhusu hali cha chakula nchini na deni la Taifa linaloenda sanjali na hali uchumi nchini.

Akizungumza na vyombo vya habari mjini Dodoma jana, Mkurugenzi wa Kitengo cha Habari, Elimu na Mawasiliano, Owen Mwandumbya alisema pamoja na kauli hizo za serikali, kabla yake kutakuwa na kauli ya Spika wa Bunge, Job Ndugai ambazo zitatolewa kabla ya kipindi cha maswali na majibu.

Katika kikao cha leo, kutakuwa na kiapo cha uaminifu wabunge watatu wa Kuteuliwa na mmoja wa kuchaguliwa ambao ni Abdallah Bulembo, Profesa Palamagamba Kabudi na Anne Kilango Malecela (wote wa Kuteuliwa) na mbunge wa kuchaguliwa kutoka Jimbo la Dimani Zanzibar, Ali Juma Ali (Dimani-CCM).

Katika mkutano huo, Kamati 14 za kisekta zitawasilisha taarifa mbalimbali ambazo zitajadiliwa na wabunge kadiri ratiba itakavyokuwa inaelekeza siku hiyo. Aidha, katika mkutano huo, itawasilishwa misaada mitatu.

Katika Mkutano wa Tano, miswada hiyo mitatu iliwasilishwa na ikasomwa kwa mara ya kwanza na baadaye ikapelekwa kwenye kamati sasa inaletwa bungeni kujadiliwa.

Miswada hiyo ni wa Muswada wa Sheria ya Madaktari, Madaktari wa Meno na Watalaamu wa Afya Wasaidizi wa Mwaka 2006, Muswada wa Huduma za Msaada wa Kisheria wa Mwaka 2016 na Muswada wa Marekebisho Mbalimbali ya Sheria Namba 4 wa Mwaka 2016.

Maswali 125 ya kawaida yataulizwa katika mkutano huo, ambao utamaliza shughuli zake Februari 10, mwaka huu. Pia katika mkutano huo, maswali ya Papo kwa Papo 16 yataulizwa kwa Waziri Mkuu.

Hii ni zaidi ya Laana,Diamond na Ali Kiba Wakimbia Mwaliko wa Kuhudhuria Maulidi ya Kuzaliwa Mtume Muhammad(S.A.W),Shehe Mkuu Dar Atoa Kauli Hii..!!!

$
0
0

Ama kweli imeshangaza wengi! Kitendo cha nyota wa muziki wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’ na Ally Saleh Kiba  kushindwa kutokeza kwenye sherehe za kumbukumbu ya kuzaliwa Mtume Muhammad (S.A.W), yaani Maulidi iliyofanyika wilayani Temeke jijini hapa ambapo walialikwa na Shehe Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhad Mussa Salum na kumuahidi kuwa wangefika.

Katika Maulidi hiyo ambayo ilifanyika Mtaa wa Liganga wilayani hapo na mwenyeji wa shughuli hiyo kuwa Shehe Alhad, ilihudhuriwa na waheshimiwa mbalimbali wakiwemo Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Idd, Makamu wa Rais Mstaafu wa Tanzania, Dk. Mohammed Gharib Bilal, Mufti wa Tanzania, Shehe Abubakar Zubeir na wengineo.

KAULI YA SHEHE MKUU JUKWANI

Wakati Maulidi hiyo ikiendelea, Shehe Alhad aliutangazia umati uliojaa kuwa, katika hafla hiyo aliwaalika wasanii mbalimbali na kuwataka watu kuwachukulia wasanii hao kama wenzao. Akiendelea kuweka mambo sawa, alisema mpaka muda huo msanii ambaye alishafika ni Ahmed Olotu ‘Mzee Chilo’ na pia akaongeza kuwa, msanii wa nyimbo za kughani, Mrisho Mpoto ‘Mjomba’ alikuwa njiani kufika eneo la tukio ingawa mpaka wageni waalikwa wanaondoka, Mpoto alikuwa hajafika.

Baadhi ya watu walifurika kwenye eneo hilo na kujua kuwa, Diamond na Kiba wangekuwepo, walishangaa kuona muda unakwenda bila wapendwa hao kuonekana licha ya kusubiriwa kwa hamu kubwa.

KAMA WANGEFIKA

Baadhi yao walisema kuwa, kama Diamond na Kiba wangejitokeza kwenye Maulidi hiyo, wanaamini Shehe Alhad angewaunganisha na kuwashikanisha mikono ya wengine wakiwa hawezi hata kuongea.

WAGENI WAALIKWA WAONDOKA

Baada ya Shehe Alhad kuwasindikiza wageni waalikwa, Wikienda lilimuweka chemba na kuanza kumuhoji kuhusiana na kutofika kwa Diamond na Kiba ambao ilisemekana aliwaalika. “Aaah! Ni kweli Diamond na Kiba niliwaalika na wote waliniahidi kufika lakini nashangaa mpaka muda huu hawajatokea, sijui ni kwa nini lakini hilo siwezi kulizungumzia zaidi isipokuwa hata mimi nashangaa,” alisema Alhad na kuomba aachwe aendelee na majukumu yaliyombana, ikiwemo

kuagana na wageni wengine. Wikienda liliwapigia simu Diamond na Kiba ili kutaka kujua kilichowasibu mpaka kushindwa kutokea kwenye mwaliko huo.

DIAMOND:“Ni kweli nilialikwa, lakini nilipata dharura ya kifamilia, niko Afrika Kusini.”

Kiba simu yake haikuwa hewani.

Mbeya: Mwenyekiti wa CCM Wilaya Apigwa Risasi Mgongoni Akiwa Usingizini..!!!

$
0
0

Habari kutoka Jijini Mbeya, zimeeleza sema kuwa Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Mbeya Mjini, Ndugu Ephrahim Mwaitenda mwenye umri wa miaka (60) amenusurika kifo baada ya kupigwa risasi mgongoni na mtu au watu wasiofahamika.

Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Emmanuel Lukula amesema tukio hilo limetokea mnamo tarehe 29. 01. 2017 majira ya saa 05. 45 usiku katika kitongoji cha Ilopa, Kijiji cha Mahenge, Kata ya Makwele, Tarafa ya Ntebela, wilayani Kyela Mkoa wa Mbeya.

Amesema tukio hilo limetokea wakati akiwa amelala Kitandani nyumbani kwake Ntebela, ambapo mbinu iliyotumika ilikuwa ni kukata wavu wa dirisha na kumjeruhi kwa kutumia silaha za kienyeji zinazotumia risasi za goroli.

Taarifa zaidi zimeeleza kuwa, Mwenyekiti huyo amefikishwa Hospitali ya Rufaa Mbeya na hali yake inaendelea vizuri.

Kamanda Lukula, amewaambia waandishi wa habari kuwa nia ya shambulizi hilo ilikuwa ni kutaka kumuua na kwamba juhudi za kuwatafuta na kuwakamata wahusika zinaendelea Kulia ni Kaimu Katibu wa CCM Mkoa wa Mbeya ndugu Lobe Zongo akimpokea Mwaitenda katika hospitali ya rufaa Mbeya wakati alipofikishwa hospitalini hapo CCM wilaya ya Mbeya mjini ndugu Ephrahim Mwaitenda akifikishwa hospitalini hapo

Katibu Mkuu Umoja wa Matifa Amwakikishia Rais Magufuli Ushirikiano ..!!

$
0
0

KATIBU Mkuu wa Umoja wa Mataifa (UN), Antonio Guterres amemhakikishia Rais John Magufuli kuwa UN itaimarisha ushirikiano wake na Tanzania katika kutekeleza majukumu mbalimbali, hususan tatizo la wakimbizi.

Kwa mujibu wa taarifa ya Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Gerson Msigwa, Guterres alisema hayo jana, alipokutana na Rais Magufuli kando ya Mkutano wa 28 wa Wakuu wa Nchi Wanachama wa Umoja wa Afrika (AU), unaoendelea mjini Addis Ababa nchini Ethiopia.

Guterres aliahidi kuwa UN itaongeza ushirikiano na Tanzania na kwamba itatia msisitizo zaidi katika kukuza wadau mbalimbali wa maendeleo ndani ya jumuiya ya kimataifa, kuchangia juhudi zinazofanywa na Tanzania katika kuwapa hifadhi wakimbizi wa nchi mbalimbali tangu mwaka 1971.

Kwa upande wake, Rais Magufuli alimpongeza Guterres kwa kuchaguliwa kwake hivi karibuni kushika wadhifa huo.

Alisema Tanzania itaendelea kushirikiana kwa karibu na Umoja wa Mataifa. Rais Magufuli pia alimweleza Katibu Mkuu huyo wa UN juhudi mbalimbali, zinazofanywa na Tanzania na Jumuiya ya Afrika Mashariki, kushughulikia mgogoro wa Burundi chini ya Mpatanishi wa mgogoro huo, Rais mstaafu Benjamin Mkapa na alimhakikishia kuwa juhudi hizo zinakwenda vizuri.

Breaking News..Kocha wa Simba Afunguka Mazito Juu ya Hali ya Timu Yake,Awatolea Povu Mashabiki ..!!!

$
0
0

KOCHA Mkuu wa Simba, Joseph Omog ameshusha presha ya mashabiki wa timu hiyo kwa kuwataka kuwa watulivu kwa kuwa bado wana nafasi ya kurekebisha makosa yao na kutimiza lengo ambalo ni ubingwa.

Simba inashika nafasi ya pili nyuma ya mahasimu wao Yanga, baada ya Jumamosi kufungwa bao 1-0, na Azam FC katika mchezo wa Ligi Kuu, ya Tanzania Bara, uliopigwa Uwanja wa Taifa Dar es Salaam.

Yanga imekamata usukani baada ya kuifunga Mwadui ya Shinyanga juzi kwa mabao 2-0 na kufikisha pointi 46 na kuiondoa Simba kileleni ambayo ina pointi 45 baada ya kipigo cha Jumamosi.

Akizungumza  Omog, ambaye amekuwa katika wakati mgumu kufuatia kipigo hicho alisema hata yeye pamoja na wachezaji wameumizwa na matokeo hayo, lakini mpira ni mchezo wa makosa na kilichobaki kwa sasa ni kujipanga upya ili kuhakikisha wanafikia malengo waliyokusudia mwishoni mwa msimu huu.

“Hakuna anayependa kufungwa au kutolewa kwenye nafasi nzuri , lakini mashabiki wanapaswa kujua Simba siyo lazima kila siku ishinde ingawa malengo yetu ni ushindi, hivyo inapotokea tumepoteza mchezo kama ilivyotokea Jumamosi tunatakiwa tukubaliane na matokeo alafu tujipange kwa mechi nyingine,” alisema Omog.

Mcameroon huyo alisema, kipindi hiki walichokuwa nacho siyo cha kutupiana lawama bali ni muda wa kuongeza mshikamano na kuisapoti timu yao kwa kuja kwa wingi uwanjani ili kuweza kushinda mechi zao na kuitoa

Huyu Ndiye Trump Bana.. Amtimua Kazi Mwanasheria Mkuu wa Serikali Baada ya Kupinga Mpango Wake wa Kuwazuia Waislamu Wasiingie Marekani..!!!

$
0
0

Rais wa Marekani Donald Trump amemfuta kazi kaimu mwanasheria mkuu Sally Yates saa chache tu baada ya kuwaagiza mawakili wa idara ya haki nchini humo kutotetea uamuzi wa kuwawekea vikwazo raia wanaotoka katika baadhi ya mataifa ya kiislamu.

Taarifa ya Ikulu ya Whitehouse imemshtumu kwa usaliti.

Sally Yates ambaye aliteuliwa na Obama alisema kuwa hafikirii kwamba marufuku hiyo ya muda kwa raia wa mataifa saba ya Kiislamu ni halali.

Wadhfa wake umechukuliwa na kiongozi wa mashtaka katika mahakama ya kijimbo huko Virginia Dana Boente.

Agizo hilo la rais lililotiwa saini Ijumaa iliopita limesababisha maandamano nchini Marekani na ughaibuni.

Awali kundi moja la wanadiplomasia liliandika barua likikosoa agizo hilo wakisema litazidi kuhatarisha usalama wa taifa hilo.

Breaking News..Necta Watangaa Matokeo ya Kidato cha Nne Mwaka 2016,Tazama Matokeo Hapa..!!!

$
0
0

 Baraza la Taifa la Mitihani (NECTA) limetangaza matokeo ya mitihani ya kidato cha nne (CSEE) na QT kwa mwaka 2016. Jumla ya watahiniwa 277,283 ambao ni sawa na asilimia 70.09 ya watahiniwa waliofanya mitihani kidato cha nne 2016 wamefaulu.

Wasichana waliofaulu ni 135,859 ambao ni swa na asilimia 67.06 wakati wavulana waliofaulu ni 142,424 sawa na asilimia 73.36.

Kwa mwaka 2015, watahiniwa waliofaulu walikuwa 272,947 sawa na asilimia 67.53. Ukilinganisha na matokeo ya mwaka huu, ufaulu umeongezeka kwa asilimia 2.56. Idadi hii ni ya watainiwa wote, yaani watahiniwa wa shule na watahiniwa wa kujitegemea.

Bonyeza hapa kuweza kuona matokeo ya kidato cha nne mwaka 2016 –>CSEE 2016

Bonyeza hapa kuweza kuona matokeo ya QT mwaka 2016  –>(QT) 2016

Wanafunzi 10 Bora Kitaifa


  1.      Alfred Shauri (Feza Boys)
  2.     Cynthia Nehemiah Mchechu (St. Francis Girls)
  3.     Erick Mamuya (Marian Boys)
  4.     Jigna Chavda (St. Mary Goreth)
  5.     Naomi Tundui (Maria Girls)
  6.     Victoria Chang’a (St. Francis Girls)
  7.     Brian Johnson (Marian Boys)
  8.     Esther Mndeme (St. Mary’s Mazinde Juu)
  9.     Ally Hassan Koti (ALCP Kilasara)
  10.     Emmanuel M. Kajege (Marian Boys)


Wasichana 10 Bora Kitaifa


  1.     Cynthia Mchechu (St. Francis Girls)
  2.     Jigna Chavda (Mary Goreti)
  3.     Naomi Tundui (Maria Girls)
  4.     Victoria Chang’a (St. Francis Girls)
  5.     Esther Mndeme (St. Mary’s Mazinde Juu)
  6.     Christa Edward (St. Francis Girls)
  7.     Nelda John (Marian Girls)
  8.     Mariamu Shabani (Kifungilo Girls)
  9.     Beatrice Mwella (St. Mary’s Mazinde Juu)
  10.     Rachel Kisasa (Canossa)


Wavulana 10 Bora Kitaifa


  1.     Alfred Shauri (Feza Boys)
  2.     Erick Mamuya (Marian Boys)
  3.     Brian Johnson (Marian Boys)
  4.     Ally Koti (ALCP Kilasara)
  5.     Emmanuel Kajege (Marian Boys)
  6.     John Ng’hwaya (Nyegezi Seminary)
  7.     Clever Yohana (Living Stone Boys)
  8.     Desderius Rugabandana (Morning Star)
  9.     Kennedy Boniface (Feza Boys)
  10.     Assad Msangi (Feza Boys)


Shule 10 Bora Kitaifa


  1.     Feza Boys
  2.     St. Francis Girls
  3.     Kaizirege Junior
  4.     Marian Girls
  5.     Marian Boys
  6.     St. Aloysius Girls
  7.     Shamsiye Boys
  8.     Anwarite Girls
  9.     Kifungilo Girls
  10.     Thomas More Machrina


Shule 10 za Mwisho Kitaifa


  1.     Kitonga
  2.     Nyeburu
  3.     Masaki
  4.     Mbopo
  5.     Mbondole
  6.     Somangila Day
  7.     Dahani
  8.     Ruponda
  9.     Makiba
  10.     Kidete


Baada ya Kuachana na Stars,Mkwasa Atua Yanga na Kupewa Cheo Hiki Kikubwa Zaidi..!!!

$
0
0

Aliyekuwa Kocha Mkuu wa timu ya Taifa, Taifa Stars, Charles Boniface Mkwasa Jumanne hii ametangazwa rasmi kuwa Katibu Mkuu wa Yanga.


Mkwasa mwenye taaluma ya ukocha daraja la kwanza la CAF, amewahi kuzifundisha klabu mbalimbali ikiwemo Yanga kwa vipindi tofauti na timu za taifa za wanaume na wanawake.


Kabla ya hapo, Mkwasa alikuwa kocha wa timu ya Taifa Stars kwa kipindi cha miezi 17 kabla ya TFF kusitisha mkataba wake mapema Januari 2017.


Makamu mwenyekiti wa klabu ya Yanga, Clement Sanga amemtambulisha Mkwasa leo mbele ya waandishi wa habari na kusema kocha huyo ambaye pia ni mchezaji wa zamani wa klabu hiyo, ameingia mkataba wa miaka miwili.


Mkwasa anachukua nafasi ya Baraka Deusdedit aliyekaimu nafasi hiyo kwa kipindi cha mwaka mmoja, kufuatia kuondoka kwa Jonas Tiboroha mapema mwanzoni mwa mwaka jana.


“Kwa niaba ya uongozi mzima wa Yanga Sc namtangaza rasmi sasa Boniface Mkwasa mchezaji wetu na mwalimu wetu wazamani kuwa ndie katibu mkuu mpya wa klabu yetu ya Yanga Sc”

Picha Hizi 6 za Irene wa Video ya Kwetu ya Rayvanny , Lazima Zikutoe Mate..!!!!

$
0
0

Mrembo wa video ya wimbo wa ‘Kwetu’ wa Rayvanny, Irene maarufu kwa jina la Lyyn kwenye mtandao wa Instagram anazidi kuwa mtamu kila kukicha.

Japo mrembo huyo ameonekana kuwa kimya kwa kipindi kirefu lakini kupitia picha alizoziweka kwenye mtandao huo Lyyn ameonekana kuzidi kunoga na kuwatoa udenda kwa kumfanya kila kidume rijali kumtamani. 

Tazama picha za mrembo huyo hapa chini.



Kudadadeki..Hii Hapa Video ya Diamond Akishusha Matusi Mazito Kwa mashabiki Zake,Huku Akitaja Kiasi cha Pesa Alichonacho Benki(Video)

Viewing all 104795 articles
Browse latest View live




Latest Images