Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104799 articles
Browse latest View live

Mamelod Sundowns Yashangazwa na Azam Fc,Kocha Wao Haamini Kilichotokea Uwanjani Jana Usiku..!!!

$
0
0

Mabingwa wa Ligi ya Mabingwa Afrika, Mamelodi Sundowns ya Afrika Kusini  wameshindwa kufurukuta mbele ya Mabingwa wa Kombe la Mapinduzi, Azam FC baada ya kutoka sare ya bila kufungana kwenye uwanja wa Taifa usiku huu.

Mamelodi ambao wapo nchini kwa ziara ya maandalizi kwa ajili ya ligi kuu nchini Afrika Kusini na mchezo wa Super Cup dhidi ya TP Mazembe itakayochezwa mwezi huu, licha ya kutawala muda mwingi wa mchezo walishindwa kupenya ngome imara ya Azam iliyoongozwa na nahodha Himid Mao.

Akizungumza baada ya mchezo huo, kocha mkuu wa Sundowns, Pitso Mosimane alisema kuwa Azam FC walikuwa kipimo bora kwao kutokana na kiwango walichoonyesha.

“Nawapongeza vijana wangu kwa kucheza vizuri na nimeridhika na kiwango chetu ingawa sijafurahi kwa sababu hatukufunga bao. Pia niwapongeze Azam kwa kucheza vizuri na walionyesha kiwango bora uwanjani,” alisema Mosimane.

Wabunge Wacharuka Bungeni Kuhusu Suala la Maslahi ya Zanzibar,Hoja za Lissu Zazidi Kuichachafya Serikali..!!!

$
0
0

SERIKALI imetoa ufafanuzi juu ya marekebisho ya Sheria ya Mikopo, Misaada na Dhamana na kubainisha kuwa masharti ya mikopo ya nje, yaliyowekwa dhidi ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ), yanatokana na masharti ya wadau wanaotoa mikopo hiyo.

Aidha, imebainisha kuwa kupitia marekebisho hayo ya Sheria ya Mikopo, Misaada na Dhamana yanayopendekeza Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (SMT) kufaulisha mkopo kwa SMZ, yana nia njema na yamelenga kuwahakikishia wahisani hao kuwa masharti yao yanafuatwa.

Ufafanuzi huo wa serikali umekuja baada ya kuibuka mjadala mkali bungeni kutoka kwa baadhi ya wabunge, wanaotaka marekebisho ya sheria hiyo yabadilishwe kwa kuwa yanainyima uhuru Zanzibar kukopa yenyewe kadri ya uwezo wake.

Hoja hizo ziliibuka baada ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, George Masaju kuwasilisha Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria Mbalimbali Namba 4 wa Mwaka 2016 bungeni mjini Dodoma jana.

Akitoa ufafanuzi huo, Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Philip Mpango alitaja baadhi ya wadau wanaoikopesha SMT ambao ni Benki ya Dunia, Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB), Saudi Fund, kuwa katika moja ya sehemu ya makubaliano ya primary loans wanahitaji kuona kuna utaratibu wa wanaonufaika kuwajibika katika malipo.

“Haya si masharti ya SMT ni masharti ya wanaotukopesha, mkiyafungia mtaweka vikwazo kwa hawa wanaotukopesha kwa masharti nafuu,” alisisitiza Dk Mpango.

Alisema lengo la muswada huo, ni kuweka kisheria sasa kwamba fedha zinazokopeshwa na SMT kwa SMZ zinawasilishwa kwa masharti yaliyopo na zinalipwa kama ilivyopangwa lakini pia kuhakikishia wahisani hao kuwa masharti waliyoweka ya ukopeshaji yanafuatwa.

Alisema madai kwamba SMZ imekuwa ikikandamizwa na kunyimwa fursa ya kujipatia mkopo si ya kweli, kwani hata katika sheria hiyo ya Mikopo, Misaada na Dhamana vipo vifungu vinavyotoa mamlaka ya serikali hiyo kupokea fedha bila kupitia mgongo wa SMT.

“Leo nimeangalia deni la nje kuanzia mwaka 1993 mpaka mwaka jana, fedha zilizokopwa na SMT kwa ajili ya SMZ zilifikia dola milioni 772.39 sawa na asilimia 2.59 ya deni lote la taifa letu,” alieleza Dk Mpango.

Masaju wakati akihitimisha mjadala huo, alimuunga mkono Dk Mpango kuhusu suala hilo la kufaulisha mkopo kwa SMZ na kubainisha hata pale itakapotokea tatizo lolote katika mikopo hiyo inayokopeshwa tena kwa Zanzibar atakayewajibika si Zanzibar bali ni Serikali ya Tanzania.

Mbunge wa Bariadi Magharibi, Andrew Chenge (CCM) aliwataka wale wote wanaopinga marekebisho ya sheria hiyo ya mikopo, misaada na dhamana, kuwasilisha hoja za nini kifanyike na si kubakia kulalamika hali ambayo hailisaidii Bunge wala serikali.

Alisema kwa upande wake kutokana na uzoefu wake, haoni tatizo lolote katika marekebisho ya sheria hiyo kutokana na ukweli kuwa yamefanyika kwa sababu ya matakwa ya wakopeshaji na wala hayana nia yoyote ovu kama inavyodhaniwa na baadhi ya wabunge.

“Muswada huu ni muswada mzuri, uzuri wa sheria yoyote ni pale unapoanza kuitumia ndio utaona. Kazi ya bunge ni kutunga sheria, tunapaswa tuwe watulivu na kujenga hoja ili kutengeneza sheria nzuri,” alisisitiza Chenge aliyewahi kuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali.

Aliongeza kuwa, “Namheshimu sana Lissu (Waziri Kivuli wa Kambi ya Upinzani Bungeni Tundu Lissu) amesema mengine mazuri, lakini kwa hili angesaidia sasa nini tufanye, kulalamika hakusaidii Bunge wala mtu”.

Alisema sheria hiyo imetungwa kulingana na matakwa ya Katiba kwani kwa mujibu wa katiba hiyo mikopo ya nje na dhamana inayotolewa na serikali sheria zake haziwezi kutungwa nje ya Katiba hiyo.

“Kupitia muswada huu inapendekezwa angalau ifanyike utaratibu utakaowezesha SMZ kupata mikopo ya nje kupitia mgongo wa SMT. Huu ni utaratibu wa watoa mikopo, haya yanayozungumzwa hapa hayaendani na wanachokitaka watoa mikopo hiyo,” alisema.

Katika muswada huo, ambao una sheria sita zilizofanyiwa marekebisho, kwenye marekebisho ya sheria ya Mikopo, Misaada na Dhamana Sura ya 134, inapendekeza masharti mapya ya mikopo kuhusu serikali ya Muungano na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ).

Marekebisho hayo yamependekeza serikali hizo kuingia katika utaratibu wa on-lending (serikali ya muungano ndiyo inayokopa na baadaye kuikopesha SMZ baada ya serikali hiyo kukidhi mahitaji na masharti ya kupewa mkopo).

Kwa mujibu wa Masaju, marekebisho ya sheria hiyo yanapendekeza kabla ya SMT haijakopa kwa niaba ya SMZ, lazima ijiridhishe kuwa mkopo huo unaweza kulipwa.

“Lengo la marekebisho haya ni kuweka utaratibu wa kisheria utakaowezesha serikali ya Tanzania kukidhi masharti ya baadhi ya wakopeshaji wanaohitaji masharti hayo na pia kuhakikisha mikopo inalipwa kwa mujibu wa makubaliano ya mkopo,” alisema.

Hata hivyo, wakati akiwasilisha mapendekezo ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria kuhusu muswada huo, Mwenyekiti wa kamati hiyo, Mohammed Mchengerwa, alisema kamati hiyo inaishauri serikali katika suala hilo la ukopaji itoe uhuru mkubwa wa kukopa kwa Zanzibar kadri ya uwezo wake.

Naye Lissu wakati akiwasilisha maoni ya Kambi ya Upinzani kuhusu muswada huo, alisema ni wakati sasa wa serikali ya Tanzania kuipatia uhuru Zanzibar ili nayo iwe na uwezo wa kukopa yenyewe kwa maslahi ya wananchi wa Zanzibar.

Pamoja na yao, baadhi ya wabunge wa CUF na CCM walirushiana maneno makali walipokuwa wakichangia muswada huo, hatua iliyompa wakati mgumu Mwenyekiti wa Bunge hilo, Najma Murtaza Giga.

Mwenyekiti huyo alilazimika kuwatuliza wabunge hao na kuwaomba waheshimiane na kuvumiliana wakati mjadala huo ukiendelea, kwani wakati mmoja wao akiwasilisha hoja inayopinga upande mwingine, walikuwa wakirushiana maneno bila kuheshimu kiti.

Wakati akichangia mjadala huo, mbunge wa Wingwi, Juma Kombo Hamadi (CUF), aliitaka serikali kuangalia kwa makini marekebisho ya sheria hiyo kwani badala ya kutoa unafuu kwa upande wa Zanzibar, yanazidi kuinyima haki serikali hiyo ya SMZ.

Mbunge wa Vwawa, Japhet Hasunga (CCM) alisema marekebisho ya sheria hiyo, hajalenga kukandamiza upande wowote, isipokuwa imeweka kinga na kuongeza masharti kwa wakopaji ili kudhibiti taasisi zinazokopa kiholela bila kuwa na uwezo wa kulipa.

Masaju alisema marekebisho hayo ya sheria ya mikopo ya elimu ya juu, yanapendekeza bodi ya mikopo kutoa mikopo kwa wanafunzi wanaosomea kozi za Stashahada (Diploma) na sifa za kupata mkopo huo zitachapishwa kwenye gazeti la serikali.

Pitia Vichwa vya Magazeti ya Leo 2/2/2017..!!!

Rasmi...Kiini cha Kufeli Kidato cha 4 Dar Chaanikwa

$
0
0

KUPELEKWA wanafunzi waliopata alama za chini katika mtihani wa darasa la saba na hivyo kushindwa kumudu masomo ya sekondari, kumetajwa kuwa ni moja ya sababu za kufanya vibaya kwa shule sita za Mkoa wa Dar es Salaam katika matokeo ya Kidato cha Nne mwaka jana.

Mbali ya hilo, imebainika kuwa viashiria vya matokeo mabaya kwa shule hizo vilianza kuonekana katika matokeo ya mtihani wa majaribio, jambo ambalo liliwafanya wakurugenzi kuwaandikia barua wakuu wa shule hizo kuongeza juhudi katika masomo ili kuepuka matokeo mabaya katika mtihani wa mwisho.

Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA) juzi lilitangaza matokeo ya mtihani wa kidato cha nne kwa mwaka 2016 na kubainisha ufaulu wa jumla kwa watahiniwa wa shule kuongezeka kwa asilimia 2.44, idadi ya watahiniwa waliopata alama za kuwawezesha kuendelea kidato cha tano kuwa chini kwa miaka mitatu mfululizo.

Hata hivyo, katika matokeo hayo, shule sita za mkoa wa Dar es Salaam zimekuwa miongoni mwa shule 10 za mwisho kitaifa. Shule hizo ni Kitonga, Nyeburu, Kidete, Mbopo, Mbondole na Somangila Day, ambazo katika kundi hilo zimo pamoja na Masaki (Pwani), Dahani (Kilimanjaro), Ruponda (Lindi) na Makiba (Arusha).

Wanafunzi wasio na uwezo

Gazeti hili jana na juzi lilitembelea baadhi ya shule hizo na kuzungumza na walimu, watendaji wa elimu na watendaji wa serikali wa kata pamoja na wanafunzi, na katika mazungumzo hayo, zimetajwa sababu mbalimbali zikiwamo za kuchukuliwa kwa wanafunzi wanaopata alama za chini darasa la saba, na suala la umbali kwa wanafunzi kutoka wanakoishi hadi shule walizopangiwa kusoma.

Shule zilizotembelewa ni Kitonga, Mbondole zilizopo katika Kata ya Msongola na Sekondari ya Nyeburu iliyopo katika Kata ya Chanika, zote katika Manispaa ya Ilala.

Mmoja wa walimu katika shule hizo, alisema kumekuwa na tabia ya kupeleka wanafunzi wenye ufaulu wa chini ya alama zinazotakiwa za ufaulu wa darasa la saba ambazo ni 250, hivyo kusababisha kuchukua wanafunzi wasio na uwezo darasani.

“Sababu zinaweza kuwa nyingi, lakini hili la kuchukua wanafunzi ambao walifeli darasa la saba kiasi cha kushindwa kumudu masomo ya sekondari lipo. Mwanafunzi anatakiwa kupata alama 250, lakini wapo wanafunzi ambao wamepata hata alama sabini wamechukuliwa,” alisema mmoja wa mkuu wa shule msaidizi wa shule mojawapo ambaye alikataa kutaja jina lake.

Kama ilivyokuwa kwa mwalimu huyo, mmoja wa wenyeviti wa kata hizo naye alikataa kutaja jina, lakini alieleza kuwa kumekuwapo na wanafunzi wanaopelekwa katika shule hizo wakiwa wamepata alama za chini sana katika mitihani ya kumaliza darasa la sababu.

Umbali watajwa

Suala la umbali pia lilitajwa kama sehemu ya changamoto zilizosababisha matokeo hayo mabaya kwa wanafunzi wa shule hizo za Dar es Salaam. Katika Sekondari ya Kitonga, walimu walikutwa wakiwa kwenye kikao na viongozi wa kata kujadili changamoto zilizofanya shule hiyo kushika nafasi ya mwisho.

Akizungumza baada ya kumaliza kikao, Mratibu wa Elimu katika Kata ya Msongola, Venance Mwakilembe alisema bado anafanya utafiti katika shule za kata hiyo zilizofanya vibaya kufahamu sababu ya kwa nini wamepata alama hizo na akipata majibu atapeleka sehemu husika.

Lakini alidai kwa ujumla changamoto kubwa ni watoto kukaa mbali na shule na hakuna mabweni hivyo kutumia muda mrefu kufika shule na kurudi nyumbani.

“Kutokana na usimamizi mbovu wa wazazi ambao wamekuwa wagumu kushirikiana na walimu haijulikani watoto wanafanya nini njiani, lakini wamekuwa watoro na kuibuka kujisajili kufanya mtihani wa mwisho wa kidato cha nne,” alisema Mwakilembe.

Aliweka wazi kuwa katika kikao cha wazazi cha mwisho kwa watoto 200 waliopo shuleni, walifika wazazi 20 pekee huku kuna wakati wazazi waliwapangia wanafunzi vyumba bila kuwa na uangalizi kwa sababu ya umri wao waliishia katika matendo machafu, jambo ambalo shule ililazimika kupiga marufuku.

Katika shule hiyo yenye ikama nzuri ya walimu 26, wana maabara na masuala mengine ya kitaaluma yakiwa vizuri, lakini changamoto ni ya umbali wanaosafiri watoto. Jirani wa shule hiyo, Hassan Waziri anasema serikali inatakiwa kuhakikisha wanafunzi wanaosoma hapo wawe wanakaa karibu au vinginevyo wajenge mabweni.

Wanafunzi waishia njiani

Katika Shule ya Sekondari ya Ndombole, mmoja wa walimu aliyekataa kutaja jina alisema wanafunzi hadi kufika maeneo hayo ambayo yako karibu na shule ya Kitonga, wanatoka maeneo mbalimbali ya jiji, lakini anaeleza kuwa kuanzia watakaomaliza kidato cha nne mwaka huu walianza kupangiwa wanaoishi karibu na shule.

Inaweka bayana kuwa mwanafunzi hadi kufika shuleni anapanda daladala nne kwa anayetokea Buguruni mpaka Gongo la Mboto, Chanika, Mvuti na mwisho anapanda yanayoenda Mbagala na kushuka shuleni anapolazimika kutembea kilometa tatu au kuchukua bodaboda kwa Sh 1,000.

Anaeleza kuwa umbali huo wa shule umesababisha wanafunzi wengi kuwa watoro na kuishia vichakani huku wengine wa kike wakidanganywa na waendesha bodaboda.

Alisema kutokana na changamoto hiyo, walilazimika kutafuta basi la shule lililokuwa likibeba wanafunzi kutoka Buguruni mpaka shuleni na kulipa Sh 2,000 kwa siku, lakini baadhi ya wazazi walikuwa wagumu kulipa kwa kusema ni nyingi hivyo kuacha huduma hiyo.

Alieleza kuwa wanafunzi waliofaulu kwa alama 240 hadi 245 darasa la saba ndiyo wamepata daraja la tatu huku wengine wakifeli kutokana na kuvutwa na waliofeli ambao ni wengi; kama ilivyokuwa kwa shule nyingine zilizovurunda kwa kuchukua wenye alama za chini sana.

Mmoja wa watendaji wa kata hiyo ambaye hakutaka jina lake kuandikwa kwa madai ya kuwa siyo msemaji wa shule hizo, aliweka bayana kuwa alitembelea moja ya shule na kubaini kuwepo mwanafunzi wa kidato cha tatu asiyeweza kuandika kwa ufasaha sentensi ya Kiswahili.

Alisema changamoto ya umbali na kupelekewa wanafunzi waliofanya vibaya mtihani wa darasa la saba nayo ni changamoto kwani wapo waliofaulu mtihani huo kwa wastani mzuri wamepata daraja la tatu.

Katika Sekondari ya Kidete iliyopo kilometa 10 kutoka daraja la Mwalimu Julius Nyerere katika Wilaya ya Kigamboni, inaeleza kuwa ufaulu mdogo wa wanafunzi wanaojiunga kidato cha kwanza shuleni hapo na umbali wa shule kwa wanafunzi ni changamoto shuleni hapo.

Mwalimu wa shule hiyo aliyekataa kutaja jina, alisema kutokana na umbali wanafunzi wengi hufika kwa kuchelewa muda wa masomo kwani wengi wanatokea Yombo Buza na maeneo mengine ya wilaya ya Temeke kwani wanatoka nyumbani saa 10 au 11 alfajiri na kuondoka shuleni saa 8:30 mchana.

Mzazi, mwanafunzi wasifu walimu Katika Sekondari ya Nyeburu, mwanafunzi wa kidato cha pili, Roneco Nziku alisema walimu wanao na wamekuwa wakifundisha vizuri isipokuwa tatizo lipo kwa wanafunzi.

Alisema licha ya kuwa matokeo hayo yanakatisha tamaa, lakini anaamini akijitahidi kusoma kwa bidii hasa masomo ya sayansi anayoyapenda atafanya vizuri kwani shule hiyo ina maabara tatu za masomo ya Kemia, Baolojia na Fizikia isipokuwa tatizo lipo kwa wanafunzi kutozingatia kile wanachofundishwa.

Nziku alisema umbali wa shule kwa wanafunzi ni changamoto kwani wanafunzi wengi hutoka Buguruni na maeneo mengine ya mbali.

Mwananchi anayeishi jirani na shule hiyo, Severino Wami alisema wanafunzi wenyewe wanaonekana hawana nidhamu, lakini pia hawaonekani kama ni watu wanaopenda kusoma kwani huwa hawafiki shule wanakwenda kukaa kwenye mabanda ya mtaani.

“Tunasikia kuna banda moja lipo mtaani ambapo wanafunzi baadhi huishia huko, kitu kingine tunasikia wengi wanatoka maeneo ya mbali kama Buguruni, atatoka saa ngapi arudi ajisomee na kesho awahi, mazingira magumu,” alisema Wami.

Pia alisema hata wazazi wanaweza wakawa ni sababu ya wanafunzi kufeli kwa sababu hawana muda wa kufuatilia viwango au maendeleo ya watoto wao darasani au kama anasoma anaporudi nyumbani.

Naye mzazi wa mtoto Michael Kitumbo anayesoma kidato cha tatu kwenye shule hiyo, Subira Kitumbo, alisema haoni kama walimu wana matatizo kwenye shule hiyo kwani siku zote wamekuwa wakisisitiza umuhimu wa wazazi kushirikiana nao katika kuhakikisha mtoto anafanya vizuri.

Viashiria vilionekana mapema Akizungumza na waandishi wa habari jana, Kaimu Ofisa Elimu wa Mkoa, Janeth Nsunza alisema wakuu wa shule hizo zilizofanya vibaya wametakiwa kujieleza na walianza kutoa maelezo, ikiwa ni sehemu ya hatua walizoanza kuzichukua.

“Mkoa umepokea matokeo hayo kwa masikitiko kwani umekuwa ni kinyume cha matarajio yetu na serikali kwa ujumla kwa kuwa serikali imekuwa ikisisitiza utoaji wa elimu msingi bora kwa wote,” alisema Nsunza.

Alisema viashiria vya matokeo mabaya kwa shule hizo yalianza kuonekana katika matokeo ya mtihani wa majaribio (Mock), jambo ambalo liliwafanya wakurugenzi kuwaandikia barua wakuu wa shule hizo kuongeza juhudi katika masomo ili kuepuka matokeo mabaya katika mtihani wa mwisho.

“Wakati wa mtihani wa Mock, shule hizi zilionesha viashiria vya matokeo mabaya na wakurugenzi waliwaandikia barua wakuu wa shule na kuwataka kuhakikisha wanafanya jitihada ili kuhakikisha shule zao zinakuwa na matokeo mazuri. Lakini tumeona bado hali imekuwa tofauti hawa wanatoa maelezo na mkoa utatangaza hatua za kuchukua baada ya kukamilisha,” aliongeza ofisa huyo.

Nsunza alisema wanafunzi waliofeli ni 619 ambao ni sawa na asilimia 1.1 kati ya wananfunzi 55,980 waliosajiliwa kufanya mtihani mwaka 2016. Aliongeza kuwa shule hizo sita zilizoshika nafasi ya mwisho ni miongoni mwa shule 128 zilizojengwa kwa nguvu za wananchi katika manispaa za jiji hilo.

Wizara yatoa neno

Akizungumzia kufanya vibaya kwa shule hizo, Kaimu Kamishna wa Elimu kutoka Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi, Nicolas Buretta alisema ipo haja ya kukaa pamoja na mamlaka za Mkoa wa Dar es Salaam ili kufanya uchambuzi wenye kutafuta sababu.

Buretta alisema suala hilo linahitaji utulivu, sio la kuzipata sababu za kufeli kwa shule hizo kwa haraka, bali inahitajika kuwatafuta wadau mbalimbali wa elimu ili kuchambua na kupata kiini cha suala hilo.

“Suala la kuanguka kwa shule hizo sio la kulipatia jibu kwa haraka, ni jambo linalotaka utulivu ili kuweza kuwashirikisha wadau wote na kutafuta sababu za kufeli kwa shule hizo,” alifafanua Kaimu Kamishna wa Elimu.

Kibaha yaibeba serikali Kwa upande mwingine, shule kongwe ya Kibaha mkoani Pwani ni miongoni mwa shule 20 bora, ambayo imeshika nafasi ya 16 kati ya shule 3,280 za sekondari nchini.

Kwa mujibu wa takwimu za viwango vya ufaulu zilizowekwa kwenye tovuti ya Baraza la Mitihani Tanzania (Necta), Kibaha iliyoko Mkoa wa Pwani wanafunzi wamepata daraja la kwanza hadi la nne, na hakuna mwanafunzi aliyefeli.

Kibaha imepanda kwani mwaka 2015 ilishika nafasi ya 69 na mwaka 2014 ilikuwa ya 87. Wakati Kibaha ikiwa ya kwanza kwa ufaulu bora kwa shule za serikali, imefuatiwa na shule ya wanafunzi wenye vipaji ya Mzumbe ya Morogoro iliyoshika nafasi ya 27, na haina mwanafunzi aliyefeli.

Mwaka 2015, Mzumbe ilikuwa nafasi ya 71 na mwaka 2014 ilikuwa ya 56. Shule ya wasichana ya Kilakala imeshika nafasi ya 28 na hakuna mwanafunzi aliyefeli. Mwaka 2015 ilishika nafasi ya 94 na mwaka 2014 ilikuwa ya 96.

Tabora Boys ikishika nafasi ya 41 na kufuatiwa na Ilboru ya Arusha iliyo nafasi ya 42. Shule zingine na nafasi zao kwenye mabano ni shule ya wasichana Tabora (114), Msalato (129), Songea Boys (201), Bwiru (214) na Moshi Sekondari (226).

Kwa upande ya 20 za mwisho, bado inaonekana shule za serikali ndizo zilizoko kwenye eneo hilo kwa kuwa na wastani hafifu. Shule zingine 10 zinazofuatiwa zile zilizotangazwa na Necta ni Mtombozi (Morogoro), Mkikira (Mara), Ndangalimbo na Mnero (Lindi), Ngiresi (Arusha), Piki (Kaskazini Pemba), Kazamoyo (Pwani), Zingiziwa na Sangara (Dar es Salaam), Mugango (Mara) na Mkera (Dar es Salaam).

Kudadeki..Obama Amuibukia Trump,Amshambulia Kwa Kauli Hizi Juu ya Agizo Lake la Kuwazuia Waislamu Wasiingie Marekani

$
0
0

RAIS mstaafu Barack Obama ameibuka na kuzungumzia siasa ikiwa ni mara ya kwanza tangu astaafu urais – akiunga mkono maandamano yanayosambaa nchini kote kupinga agizo la Rais Donald Trump kuhusu uhamiaji.

“Rais Obama amesikitishwa na kiwango cha matukio yanayotokea hivi sasa kwenye jamii mbalimbali nchini,” kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na ofisi yake ya rais mstaafu.

“Wananchi kutekeleza haki yao ya kikatiba ya kukusanyika, kuandaa na kufanya sauti zao zisikike na maofisa waliochaguliwa, ndicho hasa tunachotarajia kukiona pale maadili ya Marekani yanapokuwa matatizoni,” alisema Obama.

Hata hivyo, Rais huyo mstaafu hakuingia ndani zaidi kuhusu matamko ya Trump – yakiwamo ya kuzuia ruhusa ya wakimbizi kuingia nchini na kusimamisha uhamiaji wa watu kutoka nchi saba duniani zikiwamo Iraq na Syria.

Badala yake, Obama ambaye ana haki ya kuingilia kati pale mambo ya kisiasa na hasa ‘masuala nyeti’ yanapokuwa hatarini, aliomba “kulinganishwa kwa uamuzi wa sera zake za nje na za Trump.”

“Kwa kuzingatia mlinganisho na uamuzi wa sera za nje za Rais Obama, kama tulivyosikia kabla, kimsingi rais hakubaliani na suala la ubaguzi dhidi ya watu kwa sababu ya imani yao au dini,” kwa mujibu wa taarifa.

Katika mkutano wake wa mwisho na waandishi wa habari, Obama alisema anaweza kuingilia “nyakati fulani wakati anapokuwa anadhani kwamba maadili yetu ya msingi yamo hatarini.

Obama kwa kiasi kikubwa alishambulia moja kwa moja kauli ya Rais Trump: kwamba “Sera yangu ni sawa na alichokifanya Rais Obama mwaka 2011 alipopiga marufuku viza kwa wakimbizi kutoka Iraq kwa miezi sita.”

Gazeti la Washington Post lilielezea kauli hiyo kama madai yasiyo na kichwa wala miguu, “kwa sababu utawala wa Obama haukupata kuzuia Wairaqi kuingia nchini. Utawala huo ulibana uingiaji wa Wairaqi nchini mwaka 2011 wakati ilitangaza majina yaliyokuwa kwenye kanzidata ya nchi, baada ya Mwiraqi ambaye alikuiwa na hifadhi nchini, kubainika kuwa alipata kutega mabomu barabarani nchini mwake”.

Hata hivyo, msaidizi wa Obama hakujibu swali la alikokuwa Rais huyo mstaafu wakati akitoa taarifa yake hiyo.

Ridhiwani Kikwete Afafanua Kwanini ilikuwa ni Aibu Kwa TFF na Waziri, Diamond Kukabidhiwa Bendera Kwenda Gabon

$
0
0

Ridhiwani Kikwete aliingia kwenye headlines mwanzoni mwa mwezi uliopita pale alipoandika post Instagram akisikitishwa na kitendo cha Diamond kukabidhiwa bendera na Waziri wa michezo, Nape Nnauye kwenda kutumbuiza kwenye ufunguzi wa kombe la mataifa ya Afrika, nchini Gabon.



Mbunge huyo wa Chalinze, amedai kuwa, post yake haikumlenga Diamond, bali aliwapa ujumbe shirikisho la soka Tanzania, TFF na Waziri Nape.


“Kilichonifanya niandike ile meseji ni baada ya kuona kwamba mashindano yanayoenda kufanyika ni ya mpira wa miguu, sisi tunayo timu ya taifa ya mpira wa miguu, lakini to our surprise, badala ya kutoa bendera kwa timu ya mpira wa miguu, tunawapa waburudishaji kwa maana ya wanamuziki kama Diamond,”
Ridhiwani alisema kwenye mahojiano na The Beauty TV.

“Matarajio yetu sisi ni kumuona kapteni wa taifa ndiye anayepokea bendera na sio wanamuziki,” ameongeza. “Pia watu wa TFF, kwamba nao wanashangilia yale anayoyafanya waziri?” Hivi vitu lazima tuwe serious.”

“Diamond yeye nampongeza sana, kwa hatua aliyofika, anafanya kazi nzuri, na ndio maana watu wamemuona, wamempa nafasi ya kwenda kutumbuiza ambayo sisi kama watanzania we feel proud. Lakini the bottom line ni kwamba, nini agenda kubwa inayomfanya Diamond aende Gabon? Ni mpira wa miguu, Diamond si mchezaji wa mpira wa miguu, hata kama labda anashabikia mpira wa miguu, lakini yeye ni mshabiki tu, wanaoenda kushiriki pale ni wachezaji.”

Ridhiwani amekiri kuwa kitendo hicho kilimsikitisha na ndio maana hakupenda kukaa kimya.

“Si kwamba sikupenda kwasababu amepewa Diamond, hapana, sikupenda kwa sababu, matarajio ya mimi mpenzi wa mpira ni kumuona kapteni wangu wa timu ya taifa anapokea bendera kwa niaba ya watanzania wote, anakwenda kutuwakilisha kule, hata kama tutashindwa, hata kama tutafanikiwa lakini anayetakiwa kwenda kule ni kapteni wa timu ya mpira wa miguu kwenda kutuwakilisha kama taifa na si vingine.”

Kutana na Maalim Hussein Mtabibu wa Nyota za Binadamu Africa na Dunia Nzima,

$
0
0

Kutana na Maalim Hussein Mtabibu wa nyota za binadamu Africa na dunia nzima,
Anatoa TIBA MAENEO YOTE NCHINI, KWA WALE WENYE KUHITAJI TIBA ANATIBU YAFUATAYO,
Husafisha nyota na kutoa Pete za bahati na kwa wale walia sumbuka kwaajili ya matiba na hawakufanikiwa njoo ujionee muujiza wa papo kwa papo-humpa mtu jini la mali kwa yule anaetaka kumiliki mali bila masharti yoyote,
Anatibu magonjwa yalio shindikana-Mpenzi/MUME/MKE Aliekukimbia Anakurudishia Ndani ya saa 72 tu, Pia tunatoa dawa za Nguvu za KIUME na Kurefusha kwa saizi unayo Taka-Anatoa Dawa za BIASHARA NA MVUTO-Tunatoa Dawa za Uzazi kwa kina Mama kwa wale wenye Tatizo Sugu-Anatoa Zindiko ya Nyumba,Mwili, na Mvuto kazini- Tunamaliza kesi zilizo kaa muda Mrefu bila kumalizika, Tung'arisha Nyota na Cheo kazini. Tunarudisha Mali zilizopotea au Kuibiwa na Mengine Mengi ya Siri tuwasiliane kwa Simu-Whatsapp +255674835107
+255 629254849

Utata Mtupu ‘Dili’ Minofu ya Punda,Kasi Uchinjaji Yafika 100 kwa Siku,...!!!

$
0
0

UTATA umeibuka kuhusiana na biashara ya minofu ya punda nchini baada ya watetezi wa haki za wanyama kudai kuwa viumbe hao watatoweka nchini ndani ya miaka michache ijayo ikiwa kasi ya kuchinjwa kila uchao itaendelea kama ilivyo sasa.

Aidha, imeelezwa kuwa endapo jitihada hazitafanywa katika kusimamia biashara ya minofu ya wanyama hao, kuna uwezekano mkubwa wa kuongezeka kwa umaskini katika kaya za maeneo yanayotumia wanyama hao kama chombo chao cha usafiri.

Mkurugenzi wa shirika lisilo la kiserikali la Ustawi wa Wanyama Tanzania (Taweso), Dk. Thomas Kahema, ndiye aliyeeleza kuhusu dalili za kutoweka kwa punda nchini wakati akizungumza katika uzinduzi wa ripoti ya biashara ya punda wilayani Mpwapwa, mkoa wa Dodoma, jana.

Mkurugenzi Msaidizi Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi, Dk. Joram Mghwira, ambaye anashughulikia wanyama, alikiri kuwapo kwa hatari ya kutoweka kwa punda na jambo hilo kuwaathiri wananchi wanaowatumia wanyama hao kama chombo cha kazi na usafiri, chanzo cha tishio hilo kikiwa ni pamoja na kuwapo kwa wizi na uchinjaji holela wa wanyama hao kwenye viwanda vilivyopo Dodoma na Shinyanga.

UTATA WENYEWE
Akifafanua juu ya kuwapo kwa hofu ya kutoweka kwa punda nchini, Dk. Kahema alisema kuwa hadi sasa, utafiti uliofanywa na shirika lake unaonyesha kuwa nchi nzima ina punda takribani 500,000 huku kasi ya uchinjwaji wa wanyama hao ikifikia wastani wa punda 100 kila uchao.

Alisema takwimu hizo ndizo zinazoongeza hofu ya kutoweka kwa punda na hivyo akazitaka mamlaka husika kuchukua hatua ya kusimamia sheria kwa umakini ili kuwaokoa viumbe hao.

Dk. Kahema alisema kushamiri kwa biashara hiyo kila siku, kutasababisha pia kupungua kwa nguvu kazi ya jamii zenye punda ambao huwasaidia katika shughuli zao zikiwamo za ubebaji wa mizigo na kazi nyingine mbalimbali.

Alisema mbali na biashara ya kitoweo, pia ngozi za punda zaidi ya 100 wanaochinjwa kila uchao huuzwa katika viwanda vya Wachina vilivyopo Dodoma na Shinyanga.

Aliongeza kuwa iwapo jitihada za makusudi hazitachukuliwa sasa, taifa litakuwa halina mnyama huyo kutokana na ukweli kuwa biashara ya ngozi yake pia ingali ikishika kasi kubwa China na kwingineko barani Asia.

Alisema hatari zaidi ya kutoweka kwa punda nchini inaongezwa pia na ukweli kuwa hakuna uwiano mzuri kati ya idadi ya wale wanaochinjwa kila uchao na kuzaliana kwao.

Kuhusiana na athari za kiuchumi, Dk. Kahema alisema wastani wa bei ya punda mmoja kwa sasa ni Sh. 200,000, lakini utafiti unaonyesha kuwa thamani yake kwa ujumla kutokana na mchango wake kwa kaya zenye wanyama hao ni takribani Sh. milioni 5 kwa mwaka.

“Kwa sasa punda mmoja anauzwa Sh. 200,000 wakati kwa mwaka mnyama huyo hufanya kazi ya zaidi ya Sh. milioni 5 kwa mkulima iwapo atatumika kusaidia shughuli za kulima, kuchota maji, kubeba mizigo na kazi nyingine za kila siku,” alisema Dk. Kahema.

Akizungumzia utata kuhusiana na hatima ya punda nchini, Dk. Mgwira wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, alisema pamoja na serikali kuwapa vibali wawekezaji kufungua viwanda vya nyama za punda, lakini sheria zinawataka wawekezaji hao kuwa na mikakati ya inayoonyesha jinsi watakavyoongeza kuzaliana kwa wanyama hao nchini.

Ofisa mmojawapo wa Kiwanda cha Nyama ya Punda cha Huwa Cheng Company Limited kilichopo mjini Dodoma, Mohamed Hamis, alisema baada ya kufungiwa na Baraza la Taifa la Usimamizi wa Mazingira (NEMC) na kutozwa faini kutokana na kasoro za kimazingira, sasa kiwanda hicho kimefunguliwa na kinaendelea na uzalishaji.

“Hivi sasa kwa siku tunaingiza punda 40 kulingana na kibali tulichopewa… lakini uwezo wetu ni kuchukua punda 600,”alisema Hamis, na kuongeza kuwa jana serikali iliwapatia kibali kingine cha kuingiza punda 80 kwa siku kutokana na wingi wa punda mnadani.

Kuhusu mkakati wa kuufanya uzalishaji uwe endelevu ili punda wasipotee, Hamisi alisema kuna shamba la punda mkoani Singida na hadi sasa wapo punda zaidi ya 200 wanaofugwa kukidhi sharti hilo.

Mmoja wa wafanyabiashara wa punda katika Manispaa ya Dodoma, Mussa Charles, alisema wamekuwa wakiuza punda mmoja kwa Sh. 190,000.

VIDEO:Hii ni Kali Aisee..Baada ya Kuimba 'Wacha Waisome Namba'Khadija Kopa Naye Aanza Kuisoma Namba,Alia Hali Ngumu,...!!!

$
0
0

Msanii wa taarab Bongo, Khadija Kopa ni kama naye sasa 'anaisoma namba' baada ya kutoa kilio chake juu ya kupungukiwa na mapato yatokanayo na muziki na kutaja sababu mojawapo kuwa ni uamuzi wa serikali kuzuia matamasha ya muziki baada ya saa 6 usiku.

Amesema hivi sasa yeye na wenzake wapo katika mpango wa kuongea na mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam ili aangalie upya sheria iliyowekwa ya kufunga sehemu za starehe saa sita usiku kwa kuwa inawaumiza wasanii wa taarabu.

Amesisitiza kuwa kwa sasa biashara ya bendi za taarabu imekuwa ngumu na wanakosa mashabiki kwa kuwa muda wa kutumbuiza umekuwa mchache hivyo wanajipanga kuomba kwa mkuu wa mkoa ili siku za Ijumaa na Jumamosi ziongezewe  muda hadi saa tisa usiku.

Khadija Kopa aliyekuwa akizungumza kupitia eNewz ya EATV, amesema sababu nyingine ni utapeli unaofanywa na baadhi ya watu wanaotumia majina ya wasanii wakubwa wa taarab kufanya show na kujiingizia kipato kisicho halali.

Hii ni ishara kuwa Khadija Kopa ambaye pia ni muimbaji wa wimbo wa 'Wataisoma namba' kupitia bendi ya TOT, naye sasa 'anaisoma namba'.

Mtazame hapa mbele ya kamera ya eNewz:- 

Miujiza ya Shekh Sharifu Rashid Kutoka Bagamoyo , Anarudisha Mapenzi na Kusafisha Nyota

$
0
0

MIUJIZA YA SHEKH SHARIFU RASHID KUTOKA BAGAMOYO PWANI, (RUDISHA MAHUSIANO YAKO NDANI YA MASAA 48 TU) ASANTE KWA KUENDELEA KUMPIGIA SIMU SHEKH SHARIFU RASHID KWA WALE WENYE MATATIZO NA WALE WANAOTOA SHUKRANI:

SHEKH SHARIFU RASHIDI ni mtaalamu wa tiba mbalimbali za asili, anatumia kitabu cha quran, dawa za asili, dawa za kiarabu na majini, anazo dawa za mapenzi, nguvu za kiume, chango, ngiri maji na n.k, anakuvutia mpenzi alie kuacha au alie mbali, pia anatoa pete za bahati zilizoambatanishwa na jini mali kulingana na nyota yako, anaouwezo mkubwa wa kutumia jina la muhusika kwa kutatua tatizo lako, anaouwezo wa kumrudisha mtu aliepotea kimiujiza, pia anatibu kwa njia ya simu popote ulipo,

WASILIANA NAE KWA SIMU NA WHATSAPP NO: 0718-668347. 0685-224047, 0767-204308 au follow@shekh_sharifu_rashid, Email:shekhsharifurashid@gmail.com

VIDEO..Hivi Ndivyo Mbowe na Naibu Spika Leo Walivyoozana Bungeni Kisa Swali la Lema Kufungwa Gerezani kwa Waziri Mkuu..!!

$
0
0

Mbowe aliuliza kuwa kutokana na viongozi wa chadema ikiwamo wabunge 2 Lema kunyimwa dhamana na Lijuakali kufungwa kwa sababu za kisiasa, wabunge 6 wa Chadema kufungwa, kiongozi wa Chadema Lindi nae kufungwa na viongozi wengine takribani 216 kufungwa au kuwa na kesi mahakamani ni utekelezaji wa kauli ya Magufuli kufuta upinzani kabala ya 2020?

Waziri mkuu anasema masuala ya mahakamani hawezi kuyazungumzia na nchi inaongozwa kwa katiba na sheria

Mbowe anasema ushahidi upo wa kauli za rais kuanagamiza upinzani kabla ya 2020 na hafuati katiba na sheria kama alivyodai ila waziri na wakithibitisha hilo waziri mkuu atakuwa tayari kujiuzulu, ndipo naibu spika akazuia maswali hayo na kukawepo kelele kutoka kwa wabunge wa upinzani

Usipunjwe Tena Nyama Buchani..!!!

$
0
0

Ukienda kununua nyama buchani utaona kuna kajiwe kadogo karobo ambako mudawote kapo kwenye mizani.

Kajiwe hako kanawekwa makusudi ili kukufanya usijue kama mizani imeelemea katika upande inapowekwa nyama.

Mwambie akatoe kabla hajaweka nyama kwenye mzani iliuone kama mzani upolevo.

Ukituliatuu ujue umepunjwa nusu ya robo, kwasababu baadhi ya wauzaji wanatabia ya kuchezea mizani.

Njia ya Pili

Ule upande wa sahai huwa wameweka kitu (mfano sumaku ambayo imenasishwa upande wa chini)
Hilo jambo huwa wanalificha kwa kuweka jiwe la kilo kadhaa upande wa pili wa mzani..!


Sasa wakati anakuuzia nyama au hata bidhaa nyingine kama sukari au mchele, anaweka kabisa hiyo bidhaa kabla ya kuondoa yale mawe uliyoyakuta, akishaweka hiyo bidhaa yako (kwa makadirio) hapo ndio utaona anatoa yale mawe uliyoyakuta kisha anaweka jiwe lenye kilo unazohitaji wewe (mfano kama unataka mchele wa kilo 1 basi hapo ndipo ataweka jiwe la kilo 1), halafu ataanza kubalance kwa kupunguza huo mchele au kuongezea hadi mzani ubalance.

Tafsiri
Hapo maana yake ni kwamba lile jiwe la kilo moja limebalance na uzito wa mchele wako + sumaku aliyoinasisha chini ya sahani.
Let say sumaku ilikuwa ni robo kilo, basi mchele wako ni robo tatu ya kilo.

Hapo atachukua mchele wako atakuwekea kwenye package, utaondoka na robo tatu zako ila ile robo (sumaku yake) utamuachia muuza duka

Breaking Newss..Mkuu wa Mkoa Dar Es Salaam,Paul Makonda Amtaja Wema Sepetu Katika Orodha ya Wauza Madawa ya Kulevya Nchini,Tazama List ya Wasanii Wote Aliowataja Hapa..!!!

$
0
0

Akitoa taarifa katika kipindi cha infomer cha clouds FM kufuatia msako wa kukamata wahusika wa madawa ya kulevya alichofanya mkuu wa mkoa Paul makonda.

Askari 9 wamekamatwa wakishirikia na wauza madawa ya kulevya
Huku wasanii watumiaji wa madawa hayo wakitajwa na kutakiwa kuripoti polisi wenyewe mapema ,

wasanii waliotajwa na kutakiwa kuripoti polisi ni
1. Wema sepetu
2. Petiman wakuache
3. TID
4. Mr. Blue
5.Recho(kizunguzungu)



SOURCE; Clouds FM (Informer)

Hii Hapa List Nyingine ya Vigogo wa polisi Waliotajwa na Makonda Kuhusika na Madawa ya Kulevya,Ampiga Biti Tena Kamanda Sirro

$
0
0

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda amewataja Askari 9 wanaotuhumiwa kuhusika na biashara ya dawa za kulevya.

1- Detective Koplo Noel (Kituo chake cha kazi ni Central Police Dar)

2- Dotto (Yuko Kituo cha Kijitonyama)

3- Mwingine anafahamika kama 'Makomeo' (Kituo cha Oyster-bay)

4- Glory (Yuko Kituo cha Kawe)

5- Inspector Fadhili (Yuko Kituo cha Kinondoni)

6- Steve (Kinondoni)

7- James (Kinondoni)

8- Ditective Koplo (Wille)

RC Makonda amewataja wanaotuhumiwa kutumiwa dawa za kulevya wakiwemo TID, Wema Sepetu, Chid Benz, Recho, amewataka kesho wakutane polisi

Kuna maeneo watu wanatuambia madawa ya kulevya wanayapata sehemu hizo, wamiliki wake kesho niwakute polisi, wasipokuja nitawafuata - RC Makonda

Kama unajua una eneo unafanya biashara za dawa za kulevya DSM natoa siku 7 biashara hii iishe, operesheni hii naiongoza mwenyewe - RC Makonda

Kama Kamishna Sirro na timu yake watashindwa kutokomeza dawa za kulevya DSM maana yake wamekosa sifa za kuendelea kuwa askari - RC Makonda

Watano tayari nimeshawakamata na wengine nimewakamata wakiwa na dawa za kulevya - RC Makonda

Duh..Umesikia Jipya Alilosema Rais Magufuli Leo?Amefunguka Juu ya Issue Hii ya Trilion 7.3..!!!

$
0
0

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa TANZANIA Dkt. John Pombe Magufuli ametoa wito kwa Mahakama kukusanya Shilingi Trillioni 7.3 ambazo ni matokeo ya serikali kushinda kesi mbalimbali za ukwepaji kodi.

Rais Magufuli ameyasema hayo leo jijini Dar es Salaam wakati wa maadhimisho ya siku ya Sheria na Mwaka mpya wa Mahakama iliyobeba kauli Mbiu isemayo Utoaji haki kwa wakati kuwezesha ukuaji wa uchumi.

Alisema  kuwa Takwimu zinaonesha kuwa kumekuwa na baadhi ya kesi za pingamizi za kodi ambapo  Serikali imeshinda kesi hizo japo  fedha hizo hazijakusanywa mpaka sasa.

“Kukwepa au kutolipa kodi ni kosa kubwa sana, kila mtu anawajibu wa kulipa kodi nchini kwa maendeleo ya nchi” nalifafanua Dkt Magufuli.

Aidha, Rais Magufuli alisema kuwa katika kuelekea ukuaji wa uchumi, Mahakama iwe sehemu ya chanzo cha pato la taifa kwa kwa kuhakikisha wale wanaotakiwa kulipa fidia baada ya kushindwa kesi wanafanya hivyo pamoja na kuwabana wakwepa kodi kwani kutimiza hilo kutaleta mabadiliko katika uchumi wa nchi.

Katika hatua nyingine Rais Magufuli alisema kuwa Maendeleo ya nchi hayaangalii chama chochote, hivyo amevitaka vyombo vya utoaji haki kutoa haki kwa usawa.

Kwa upande wake Kaimu Jaji Mkuu wa Tanzania Profesa Ibrahim Juma alisema kuwa Mahakama imeandaa Mpango mkakati uliolenga kufanya maboresho ndani ya Mahakama.

Alisema kuwa mpango mkakati huo umelenga masuala makuu matatu ikiwemo Utawala bora, uwajibikaji na usimamizi wa rasilimali, upatikanaji wa haki na kwa wakati, uimarishaji wa amani kwa wananchi na ushirikishwaji wa wadau katika shughuli za mahakama.

Aidha Kaimu Jaji Mkuu alisema kuwa Mahakama imefanikiwa kusikiliza mashauri ya kesi za uchaguzi kwa asilimia 100.

“kati ya mashauri ya kesi 249 ikiwemo 53 za ubunge na 196 za madiwani ya waliopinga uchaguzi kati ya kesi hizo, kesi 52 za ubunge zilikamilishwa na kesi zote za madiwani zilikamilishwa” alifafanua Kaimu Jaji Mkuu.

Naye Mwanasheria Mkuu wa Serikali George Masaju amesema kuwa Katiba imeanisha bayana Kanuni ambazo zinapaswa kuzingatiwa na Mahakama wakati ikitekeleza mamlaka yake ya utoaji haki.

“utoaji haki mapema ipasavyo ni moja ya Kanuni ambazo Mahakama inapaswa kuzingatia katika utekelezaji wa majukumu yake kama inavyoelekezwa katika Katiba” alifafanua Mwanasheria Mkuu.

Alisema kuwa Serikali imeendelea kuboresha mazingira ya uwekezaji na kufanya biashara katika nchi ya Tanzania hivyo kuchochea maendeleo ya kiuchumi.

Siku ya Sheria nchini ilioanzishwa mwaka 1996 ikiwa ni siku muhimu ya kuombea Majaji na Mahakimu ili kuweza kusikiliza kesi.

Ile Issue ya Manara Kumposa Wema Imeishia Wapi?Haya Hapa Majibu..!!!

$
0
0

Hatimaye Msemaji wa klabu ya Simba, Haji Sunday Manara atashindwa kumposa mnyange Wema Sepetu, baada ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kupangua tena ratiba ya ligi kuu, kwa kusogeza mbele mchezo wa Azam na Ndanda FC.

Mchezo huo uliokuwa umepanga kufanyika Jumamosi ya Februari 4, sasa utafanyika Jumapili Februari 5 ili kutoa nafasi kwa Azam FC kujiandaa vizuri kutokana na timu hiyo kucheza mechi ya kirafiki dhidi ya Mamelod Sundowns ya Afrika Kusini, siku ya Jumatano usiku.

Maamuzi haya yamefanyika ikiwa ni takriban siku 10 tangu Msemaji huyo wa Simba Haji Manara atangaze kumposa aliyewahi kuwa Miss Tanzania, ambaye pia ni nyota wa bongo movie Wema Sepetu, endapo ratiba isingepanguliwa tena.

Manara alisema kuwa alikuwa na uhakika kuwa ni lazima ratiba ingepanguliwa tena, mara baada ya TFF pia kupangua tarehe ya mchezo kati ya Simba na Yanga uliosogezwa kutoka Februari 18 hadi Februari 25 huku akionesha kushangazwa na jinsi ambavyo TFF inashindwa kutengeneza ratiba ya uhakika.

Katika taarifa yake aliyoitoa usiku wa Januari 23 mwaka huu, manara alisema  "Iwapo Kama ratiba yao ya Ligi kuu na Kombe ila shirikisho haitabadilishwa kuanzia sasa hadi mwisho wa msimu, ntamposa mlimbwende Wema Sepetu, na akikubali ntamuoa, akikataa ntatembea na boxer toka Nyumbani kwangu hadi TFF" 

Kwa mabadiliko haya ambayo sasa TFF imeyatanga, ni dhahiri kuwa hakuna ndoa tena kati ya Manara na Wema Sepetu, isipokuwa tu kama atatangaza vinginevyo.

Kauli ya Serikali Kuhusu Upinzani Nchini Kufutwa...!!!

$
0
0

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema kuwa Rais, Dkt. John Magufuli hajawahi kutangaza ama kutoa kauli ya kufutwa kwa vyama vya siasa nchini.

Ametoa kauli hiyo leo Bungeni mjini Dodoma wakati akijibu swali la Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni, Mheshimiwa Freeman Mbowe  katika kipindi cha maswali kwa Waziri Mkuu.
Katika swali lake Mheshimiwa Mbowe alisema Rais Dkt.  Magufuli alinukuliwa akisema atahakikisha anafuta vyama vyama vya upinzani na ifikapo mwaka 2020 hakuna upinzani nchini.

Pia Mheshimiwa Mbowe alitaka kujua nini kauli ya Serikali kuhusu kunyimwa dhamana kwa Mbunge wa Arusha Mjini, Mheshimiwa Godbless Lema ambaye anashikiliwa kwa muda miezi mitatu.

Mbali na Mheshimiwa Lema, pia kiongozi huyo alitaka kujua kuhusiana na kufungwa kwa Mbunge wa Kilombelo, Mheshimiwa Peter Lijualikali pamoja na madiwani sita wa chama hicho ambao wamefungwa na viongozi wengine 215 wanakabiliwa na kesi mbalimbali.

“Kwanza nataka nikanushe kwamba Mheshimiwa Rais hajawahi kutangaza kuvifuta vyama vya upinzani. Pia Watanzania wote wanajua nchi hii inaongozwa kwa sheria, kanuni na taratibu i,” amesema Waziri Mkuu.

Waziri Mkuu ameongeza kuwa “tunajua katika kuendesha nchi tunaendesha kwa mihimili mitatu ipo Serikali, Mahakama na Bunge na hakuna mhimili unaoweza kuuingilia mhimili mwingine,”.

“Pia Watanzania wote wanajua kwamba jambo lolote ambalo lipo Mahakamani haliwezi kuzungumzwa mahali pengine popote, hivyo siwezi kutumia nafasi hii kuzungumzia mambo yote yanayoendelea chini ya sheria na yaliyo mahakamani,” amesema.

Video..Mzee wa Upako Ahubiri Kanisani Kwake Huku Akiimba Wimbo Mpya wa Darasa wa Muziki..!!!!

Serikali - Zaidi ya Walimu 5000 Wamekimbia Kazi..!!!!

$
0
0

Serikali imesema kuwa kati ya walimu zaidi ya 8,000 wa Sayansi na Hisabati waliotajwa kuhitaji ajira serikalini, ni walimu 2100 pekee waliotuma maombi, ikimaanisha kuwa kuna walimu zaidi ya 5,000 ambao hawajulikani waliko.

Takwimu hiyo imetajwa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Utumishi na Utawala Bora) Angela Kairuki wakati akizungumza na watumishi wa umma wanawake katika Manispaa ya Dodoma katika wiki ya maadhimisho ya miaka 40 ya Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Kairuki alikuwa akizungumzia suala la uhakiki wa vyeti kwa watumishi wa umma, na kusisitiza kuwa ifikapo mwezi Machi mwaka huu watumishi wote wa umma ambao watakuwa hawajawasilisha vyeti vyao vya kitaaluma watafukuzwa kazi.

Amebainisha kuwa katika zoezi lililofanywa na mamlaka ya vitambulisho vya Taifa (Nida) waligundua watumishi wengi hawana vyeti na baadhi yao wanatumia vyeti feki hasa wa kada ya ualimu kwa kuwa wana uhakika wa ajira pindi wanapomaliza vyuo.

"Kulikuwa na taarifa kuwa kuna zaidi ya walimu 8,000 waliokuwa wanatakiwa kuajiriwa lakini baada ya serikali kutangaza nafasi hiyo ni walimu 2,100 tuu ndiyo walioomba nafasi mpaka sasa. 

Sasa hapo suala la kujiuliza je hao wengine mpaka sasa wako wapi kama hawana vyeti feki!? Nataka niwaambie kuwa hakuna mwenye cheti feki atakayesalimika kwenye Utumishi wa umma," amesema Kairuki.

Amesema ni bora aonekane ni waziri anayechukiwa na jamii kuliko kulifumbia macho suala la vyeti feki kwa watumishi wa umma.

"Tumetoa muda wa kutosha kwa watumishi wa umma kuwasilisha vyeti vyao vya kitaaluma bila shaka walifika mpaka hapa kwenu lakini jambo la kusikitisha ni kwamba mpaka sasa kuna baadhi ya watumishi bado hawajawasilisha," alisema Kairuki.....Vyeti hawajaleta na hata namba ya utambulisho (index number) hawaleta sasa wanataka tuwafanyaje??? Nawamegemea tu siri na mkawaambie na wenzenu itakapofika Machi Mosi hawajawasilisha vyeti vyao tunawafukuza kazi."

Amesema kama serikali itaharakisha zoezi hilo watumishi wa umma wanaostahili watapandishwa vyeo na mishahara yao kwa kuwa zoezi hilo limesitishwa kutokana na uhakiki wa vyeti.

Unakumbuka Ile Issue ya Gigy Money Kutaka Kuokoka,Sasa Leo Ameibuka an Hili Jipya..!!!!

$
0
0

Mtangazaji wa kipindi cha Lavidavi cha Choice FM, Gigy Money amekanusha uvumi ambao ulizagaa kwenye mitandao ya kijamii kuwa anataka kuokoka.

Taaifa hizo zilidai kuwa video queen huyo anataka kuokoka ili kufuta mabaya aliyoyafanya katika kipindi cha nyuma.

Akiongea katika kipindi cha Star News cha Star TV wiki hii, mrembo huyo amedai hana mpango huo huku adai labda abadili dini kumfuata mpenzi wake wa sasa Mo J.

“Kusema kweli Gigy kama Gigy Gigy hana mpango wa kuokoka, niokoke kwanini labda nibadili dini kwa sababu ya mpenzi wangu wa sasa lakini sio kuokoka,” alisema Gigy.

Pia video queen huyo amedai kwa sasa anapata deal za matangazo mengi ya nguo kutokana mwonekano wake wa mwili.
Viewing all 104799 articles
Browse latest View live




Latest Images