Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104808 articles
Browse latest View live

Wakati Watu Wakilia Hali Ngumu,Wabunge Washauri Bei ya Petroli na Dizeli Ziongezeke Mara Dufu..!!!

$
0
0

KAMATI ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji imelishauri Bunge wakati wa utungaji Sheria ya Fedha ya Mwaka 2017 kuongeza tozo kwa kila lita ya mafuta ya dizeli na petroli.

Nia ni kupatikana fedha kwa ajili ya Mfuko wa Taifa wa Maji, ili kugharimia miradi ya maji nchini.

Ilisema tozo hiyo iwe Sh 100 badala ya Sh 50 kwa sababu Mfuko huo umeonesha mafanikio makubwa katika kuwezesha upatikanaji fedha licha ya kiasi kinachopatikana kutokidhi mahitaji ya maji yaliyopo.

Akiwasilisha taarifa ya shughuli zilizotekelezwa na Kamati hiyo mwaka 2016 hadi 2017, Mwenyekiti wake Dk Christine Ishengoma alisema: “Kamati inashauri kuongeza tozo kutoka Sh 50 hadi Sh 100 kwa kila lita ya mafuta ya dizeli na petroli.”

Alibainisha kuwa hatua hiyo inalenga kupatikana fedha za kutosha kugharimia miradi ya maji.

Alibainisha kuwa Kamati hiyo ilibaini kuwa katika Bajeti ya Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi ya mwaka 2016/17, katika fungu la fedha za maendeleo, Serikali ilitenga kiasi kikubwa cha fedha za ndani ikilinganishwa na fedha za nje, ambazo hazikutolewa.

“Hazitolewi kama zilivyoidhinishwa na Bunge, hivyo kuchangia kutofikiwa kwa malengo yaliyopangwa,” alisema Dk Ishengoma.

“Hili si jambo dogo katika utekelezaji wa mipango ya Serikali, linahitaji ufumbuzi, la sivyo bajeti ya Serikali katika miradi ya maendeleo itaendelea kuwa kiini macho,” alisema.

Alibainisha kuwa upatikanaji wa fedha za ndani za miradi ya maendeleo kwa kipindi cha nusu mwaka zilizokuwa zimetolewa; kilimo kilipangiwa Sh bilioni 22 lakini mpaka wakati huo kilikuwa hakijatolewa kiasi chochote.

Kwenye Mifugo na Uvuvi, ilipangwa Sh. bilioni 8, lakini zilitolewa Sh milioni 280 huku Tume ya Taifa ya Umwagiliaji ikipewa Sh milioni 767 kati ya Sh bilioni 6.

Wakati akiwasilisha taarifa ya Kamati ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii, Mwenyekiti wake, Atashasta Nditiye alisema Kamati hiyo ilibaini changamoto ndani ya Mamlaka ya Wanyamapori nchini, ikiwa ni pamoja na mbinu mpya ya ujangili.

“Kuna mbinu mpya ya ujangili ambapo majangili wanatumia sumu kuua wanyamapori. Mbinu hii ni hatari, kwani wanaua wanyamapori wa aina mbalimbali, hata wasiokusudiwa,” alisema Nditiye.

Kamati hiyo ilishauri Serikali kuajiri watumishi wa kutosha wenye ujuzi na utaalamu wa kisasa hasa askari wa wanyamapori.

“Pia kutatua migogoro ya mipaka ya hifadhi na vijiji vinavyopakana na hifadhi kwa kushirikiana na wananchi. Serikali iondoe wafugaji kwenye hifadhi zetu ili kunusuru hifadhi na mazingira,” alisema.

Lusinde Amshukia Mbunge Mwenzake CCM

$
0
0

Mbunge wa Mtera (CCM), Livingstone Lusinde amesema kitendo alichofanya mwenzake wa Bunda kupitia chama hicho, Boniface Getere kugawana muda na mbunge wa Serengeti (Chadema), Marwa Ryoba ni utovu mkubwa wa nidhamu.

“Wapinzani hawajawahi hata siku moja kutoa dakika zao kwa CCM. Unampa dakika zako tano mtu ambaye kazi ya chama anachokiwakilisha ni kuikosoa Serikali tu hata katika mazuri si sahihi?” amehoji Lusinde.

Lusinde ni mmoja wa wabunge wa CCM waliomshukia Getere kumpa dakika tano Ryomba ili aweze kuchangia taarifa za kamati za Bunge; Kamati ya Ardhi, Maliasili na Utalii na ya Kilimo, Mifugo na Maji baada ya mwenyekiti wa Bunge, Mussa Hassan Zungu kumruhusu azungumze kwa dakika kumi.

“Duniani kote kazi ya upinzani ni kuipinga Serikali iliyopo madarakani na kazi ya wabunge wa chama tawala ni kuishauri Serikali na kuipongeza pale inapofanya vizuri. Hizi ni kambi mbili tofauti,” amesema Lusinde.

Hata hivyo, mbunge wa Ubungo (Chadema), Saed Kubenea amesema haoni ubaya kwa mbunge wa CCM kumpa muda mbunge wa upinzani, bali anachokiona CCM wanahamishia kampeni bungeni.

Katibu wa wabunge wa CCM, Jason Rweikiza amesema ni makosa makubwa kwa mbunge wa CCM kutoa muda wake kwa upinzani.

“Si sawa kabisa. Wabunge wengi wa CCM walitamani kuchangia, lakini muda hauruhusu. Tutalijadili hilo kwenye vikao vya chama,” amesema Rweikiza.

Hata hivyo, alipoulizwa Getere iwapo haoni kama amefanya makosa kumgawia mbunge wa upinzani, ametaka kufahamu ni wabunge gani wanaomlalamikia, akisema hajaona madhara yoyote kwa kitendo chake hicho.

Gigy Money-Wengi Walikuwa Wananishangaa Navyopiga Picha za Nusu Utupu..Ila Leo Nimekuwa Staa

$
0
0

Niwakumbushe kitu mlisemaga sitokua star kipindi kile naaanzaaa hustle zangu yes am not a star but am morethan a star am 👑ueen of queens ......nawengine walikua wananishangaa why napiga picha half nude kikubwaaa sasa sikuiz nawao wanapiga wengine ndio mnawaita mastar wenu gigy ndio star wewe wana ni copy 😂 wana copy copy wana ni copy .....#mimindiorolemodelwao😂 SIMKUBALI TU HATERS COZ U GUYS MAKE ME FAMOUS

Alichokisema Kamanda Siiro Juu ya Watuhumiwa wa Dawa za Kulevya Wanaolala Selo..!!!

$
0
0
eshi la Polisi Mkoa wa Dar es Salaam limesema siyo lazima kila mtu aliyemo kwenye orodha ya Mkuu wa mkoa huo, Paul Makonda anayefika Kituo Kikuu cha Polisi kuhojiwa alale mahabusu.


Kamanda wa Kanda ya Dar es Salaam, Simon Siro amesema wanalazimika kuwashikilia watu wenye viashiria ili kutafuta ukweli wa kuthibitisha yale yaliyofikiriwa kuona kama wanaweza kubaini lolote.

Siro amesema juzi walikwenda watu wa mahotelini (wamiliki), lakini baada ya kuhojiwa walionekana hawana jambo zito na la msingi, hivyo waliachiwa huru.

Kamanda huyo amesema kuna watu waliotajwa wanapiga simu kuulizia kuna nini na wengine wanawatuma ndugu zao.

“Hakuna sababu ya kuwa na woga mpaka kumtuma ndugu kwa Kamishna Siro, bali unapoitwa njoo uripoti kwa timu iliyoundwa na mkuu wa mkoa, watapeleleza mambo yote ukionekana huhusiki utaachiwa,” amesema.

“Kwa wale ambao hawajaripoti, ikifika kesho hawajafika hakuna shida, kikubwa ni kututaarifu juu ya udhuru wake. Unaweza ukasema mtu aje kumbe siku hiyo yupo kitandani, hakuna shida kwa kuwa lengo la upelelezi huu si kukomoa watu, bali ni kupata ukweli kuhusu hao watu.”

Pia, Siro amezungumzia kauli ya Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe akisema, “Kama Mbowe hawezi kuja sisi tutamfuata, wala hakuna shida katika hilo kwa sababu kama umeitwa na wewe hutaki kuja na sisi tunataka kukuhoji kujua ukweli kuhusiana na wewe, tutamfuata tu.”

Kamanda huyo amesema operesheni ya dawa ya kulevya bado inaendelea ambapo Jumatano walikamatwa watu 11 na kete 38 za dawa ya kulevya na magunia sita ya bangi.

 “Waliokwishakamatwa wanaweza wakafikishwa mahakamani au wasifikishwe na kwamba utaratibu unaotumika sasa wa kuwatangaza watuhumiwa badala ya kuwakamata kuwafisha kituoni unawapa raha sana na unawarahisishia kazi polisi,” amesema.


Kutana na Maalim Hussein Mtabibu wa Nyota za Binadamu Africa na Dunia Nzima,

$
0
0

Kutana na Maalim Hussein Mtabibu wa nyota za binadamu Africa na dunia nzima,
Anatoa TIBA MAENEO YOTE NCHINI, KWA WALE WENYE KUHITAJI TIBA ANATIBU YAFUATAYO,
Husafisha nyota na kutoa Pete za bahati na kwa wale walia sumbuka kwaajili ya matiba na hawakufanikiwa njoo ujionee muujiza wa papo kwa papo-humpa mtu jini la mali kwa yule anaetaka kumiliki mali bila masharti yoyote,
Anatibu magonjwa yalio shindikana-Mpenzi/MUME/MKE Aliekukimbia Anakurudishia Ndani ya saa 72 tu, Pia tunatoa dawa za Nguvu za KIUME na Kurefusha kwa saizi unayo Taka-Anatoa Dawa za BIASHARA NA MVUTO-Tunatoa Dawa za Uzazi kwa kina Mama kwa wale wenye Tatizo Sugu-Anatoa Zindiko ya Nyumba,Mwili, na Mvuto kazini- Tunamaliza kesi zilizo kaa muda Mrefu bila kumalizika, Tung'arisha Nyota na Cheo kazini. Tunarudisha Mali zilizopotea au Kuibiwa na Mengine Mengi ya Siri tuwasiliane kwa Simu-Whatsapp +255674835107
+255 629254849

Bunge Laonya Ubabe wa Kutaja Watu Majina,Habari Katika Vichwa vya Magazeti ya Leo..!!!

Serikali Kujenga Kiwanda cha Kutengeneza Simu..!!!

$
0
0

 Serikali imesema inalenga kuanzisha kiwanda cha kutengeneza simu hapa nchini ili kuwalinda watumiaji.

Akijibu bungeni, Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage amesema kwa sasa wanawashukuru watendaji wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) kugundua simu feki kwa sababu zina madhara kwa binadamu.

Mwijage alikuwa akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalumu (Chadema), Aida Khenani aliyeitaka Serikali kuwalipa fidia wananchi walioathirika na kufungwa kwa simu feki kwa sababu watendaji wake hawakuwa makini wakaruhusu ziingizwe nchini na kulipiwa kodi.

“Serikali ina mpango gani wa kuwalipa watu walioathirika na kuzimwa kwa simu feki uliotokana na uzembe wa watendaji?” amehoji.

Akijibu swali hilo, Mwijage amesema Serikali inadhibiti uingizwaji wa bidhaa hizo kwa kuimarisha ukaguzi, kuendelea kuajiri wataalamu zaidi na kufungua vituo vya ukaguzi wa ubora wa bidhaa katika mipaka zinakopitishwa kutoka nchi nyingine.

Pia, amesema Serikali hufanya ukaguzi wa mara kwa mara kwenye njia za kuingizia bidhaa ikiwamo Bandari ya Dar es Salaam, Tanga na Mtwara, viwanja vya ndege vya Julius Nyerere na Kilimanjaro na mipaka inayopitishiwa bidhaa kutoka nje ya nchi.

“Serikali itaendelea kuwachukulia hatua wale wote watakaohusika na uingizaji wa bidhaa bandia ikiwa ni pamoja na kuziteketeza  au kuzirejesha zilikotoka,” amesema Mwijage.

Simba Kuifanyia Umafia Yanga Leo...!!!

$
0
0

Wakati Yanga ikikwea pipa kesho kwenda Comoro kuikabili timu ya Ngaya Club de Mbe katika mchezo wa awali wa Ligi ya Mabingwa Afrika, watani zao Simba watakuwa kwenye dimba la Taifa jijini hapa kusaka poiti tatu.

Simba ina pointi 48 ikiwa nyuma ya Yanga kwa pointi moja na Yanga na ushindi wowote itakaoupata kwenye dimba hilo dhidi ya Prisons ya Mbeya itakuwa na maana kwamba inarejea kwenye usukani wa ligi.

Rekodi zinaonyesha kuwa katika michezo mitano ya karibuni baina ya Simba na Prisons, Wekundu wa Msimbazi wameshinda miwili wakati maafande hao wakishinda miwili huku mchezo mmoja timu hizo zikitoka sare.

Utamu wa mechi hiyo ni ushindani uliopo baina ya mabeki wa Simba chini ya mkongwe Method Mwanjali na Novaty Lufunga dhidi ya washambuliaji Prisons, Victor Hangay na Lambart Subiyanka.

Kocha wa msaidizi wa Simba, Jackson Mayanja ametambia ushindi walioupata dhidi ya Majimaji ya Songea katika mchezo uliopita wa mabao 3-0 kuwa umewaongezea ari ya kuiua Prisons.

Naye Kocha wa Prisons, Abdallah Mohammed amesisitiza kwamba licha ya mchezo kuwa mgumu, lakini ushindi ndiyo matarajio yao.

Alichokisema Baba Diamond Kuhusu Nani Mkali Kati ya Mwanae Diamond na Darasa..!!!

$
0
0

BABA wa staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’, Abdul Jumaa amefunguka kuwa Mwanamuziki, Shariff Thabeet ‘Darassa’ licha ya watu kusema yupo juu lakini hawezi kumshinda au kufikia levo alizopo mwanaye.

Akichezesha taya na Mikito Nusunusu, baba Diamond alisema licha ya watu wengi kuvutiwa na Wimbo wa Muziki wa Darassa lakini hawezi kumshinda mwanaye huyo kwa sababu ni wimbo huo mmoja tu ndiyo uko kwenye chati kitu ambacho ni tofauti na Diamond ambaye anazo nyingi zinazofanya vizuri.

“Diamond ni mpiganaji sana na ana mbinu nyingi kwenye suala zima la muziki wake ndiyo maana kila siku anazidi kuwa juu na kujulikana mataifa mbalimbali, wanaosema Darassa atampita au kumfikia Diamond alipo wanajidanganya, hawezi hata kwa nusu yake,” alisema baba Diamond

MWANZA: Anaswa na Shehena ya Dawa za Kulevya Chumbani, RPC Asimulia Sakata Zima

$
0
0

Mtu mmoja anashikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoani Mwanza kwa kosa la kupatikana na dawa za kulevya yanayodhaniwa kuwa heroine kiasi cha pinchi 240 na ndonga mbili.

Taarifa ya jeshi hilo iliyotolewa leo, imedai kuwa mtu huyo aliyejulikana kwa jina la Kassim Hemed Kesi mwenye umri wa miaka 43,  amekamatwa majira ya saa 6 usiku wa kuamkia leo katika mtaa wa Kanyerere kata ya Butimba wilaya ya Nyamagana Jijini Mwanza

Taarifa hiyo imedai kuwa mtu huyo ni  mfanyabiashara wa spear za magari katika mtaa huo.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza DCP Ahmed Msangi amesema kuwa awali polisi walipata taarifa za mtuhumiwa huyo kuwa anajihusisha na biashara ya madawa ya kulevya, hivyo askari walikuwa wakiendelea na upelelezi pamoja na uchunguzi kuhusiana na  tuhuma hizo.

Aidha wakati askari wakiendelea na upelelezi dhidi ya tuhuma za mfanyabiashara huyo, jana tarehe 09.02.2017, polisi walipokea taarifa kutoka kwa raia wema kwamba mtuhumiwa huyo ameingiza mzigo mkubwa wa madawa ya kulevya kutoka Dar es Salaam na ameanza kuusambaza mtaani.

Tukio lilivyokuwa

Askari walianza kufanya ufuatiliaji wa haraka kuhusiana na taarifa hizo, ndipo ilipofika majira ya saa sita usiku askari walifika hadi nyumbani anapoishi mtuhumiwa na kuizingira nyumba yake yote na kumuona kupitia dirisha akiendelea kufunga madawa hayo kwenye vikete vidogovidogo maarufu kama pichi.

Wakati askari wanataka kuingia ndani ya nyumba mtuhumiwa alishtuka na kukimbiza mzigo huo wa madawa ya kulevya chooni ili kupoteza ushahidi.

Aidha askari waliona kitendo kile kupitia dirishani na baadhi YA askari waliingia ndani na kufanikiwa kukuta pinchi 240 zikiwa chooni lakini bado hazikuwa zimetumbukia shimoni na kufanikiwa kuzitoa kwenye tundu la choo.
Msangi amesema wakati huohuo askari wengine waliokuwa nje walikwenda kuvunja bomba linalopitisha uchafu/choo linalokwenda kwenye shimo na kuweka kizuizi hapo na kufanikiwa kupata ndonga 2 za dawa za kulevya huku nyingine zikibebwa na maji .
 Polisi wanaendelea na mahojiano na mtuhumiwa ili kuweza kubaini mtandao wa watu aliokuwa akijihusisha nao katika biashara hiyo ya madawa ya kulevya.

Video..Spika Ndugai Awapiga Mkwara Mzito Polisi kwa Kukamatakamata Wabunge Ovyo..

$
0
0

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Job Ndugai amekemea tabia ya ukamatwaji wa wabunge wanapokuwa kwenye vikao vya Bunge na kusema kuwa jambo hilo ni kinyume cha sheria na utaratibu.


Video..Askofu Gwajima Akimfufua Mtu Kanisani Kwake..!!

Mwanasheria wa Wema Sepetu Alberto Msando Adai Wapo Waliochukia Yeye Kumtetea Wema

$
0
0

Mwanasheria wa #WemaSepetu, #AlbertMsando amefunguka kwa kudai kuwa kuna watu hawakupenda yeye kumsaidia kisheria muigizaji huyo wa filamu ambaye hivi karibuni alishikiliwa na jeshi la polisi kwa tuhuma za kukutwa na msokoto wa bangi nyumbani kwake pamoja na makosa mengine.

Mwanasheria huyo aliamua kumsaidia kisheria muigizaji huyo pamoja na wenzake na February 9 malkia huyo wa filamu alipata dhamana.

Baada ya tukio hilo mwanasheria huyo amedai kuna watu hawakupenda yeye kumsaidia malkia huyo wa filamu.

#AlbertMsando👉 “Have you ever had a sister who is the opposite of you? A friend who you can not explain why he or she is your friend? I have. Having a one-on-one with Wemasepetu. Kuna watu wameongea walichoongea. Wamekasirika kumsaidia Wema,” aliandika mwanasheria huyo Instagram.

Aliongeza👉“Ila ukweli unabaki kwamba Wemasepetu has her following. I must say yeye kama ilivyo mimi na wewe sio mkamilifu. She has her share of mistakes. And failures. But she is not a bad person. She has a special heart. Her charge is “to be found in possession of small amount of narcotics drugs commonly known as bhangi. 1.85gms” nothing serious. Kweli au si kweli ni kazi ya Mahakama. Kwa hiyo kwa wale ambao wameamua kupigana vita kwa kuniattack I am leaving it to them. For me all I have to do is, guide her to being better and realising her full potential. Thats not law. Thats friendship.

Za Hivi Punde..Makonda Awajibu Viongozi wa Vyama na Serikali Wanaomkosoa Juu ya Hatua Anazochukua..!!!

$
0
0

Mkuu wa Mkoa Dar es salaam kupitia Account yake ya Instagram Ameandika Ujumbe unaotafsiriwa ni kama kuwajibu wakosowaji wote ambao wanabeza na kudharua kile anachokifanya.

Katika Ukarasa wake wa Instagram Paul Makonda Ameanza kwa kuandika "Usiogope Mbwa Mwitu, unapoanza kuchipuka katika wazo lako…. na ndio maana kuna wimbo wa mwimbaji anaitwa Ephraim kutoka Zambia naupenda sana“

Pia akaenda mbali zaidi na Kusema kuwa Mungu hajalala kama watu wanavodhani hii ikiwa na Maana kuwa kila akifanyacho yu Pamoja na Mungu na Mungu anamsimamlia kwa kile anachokifanya

“Wimbo unasema wewe ni Mungu usielala…………. Mungu wetu hajalala, mantiki ya Mungu kutokulala hachoki na kuna mahala nimekupa katika hii mistari anasema utataka jambo nawe litakua, imani utakayokua nayo itakusukuma kutaka jambo litakua“

“Mbwa Mwitu ni wale watu ambao wanabweka tu… unaanza jambo wanakubwekea kiasi kwamba wanakufanya mpaka unakata tamaa”

Ningekuwa bado natumia Madawa ya kulevya jina langu lingetajwa na Makonda – Q Chief

$
0
0

Msanii wa muziki Q Chief amedai kuwa jina lake halikutajwa katika list ya RC Makonda kwa kuwa yeye tayari alishaachana na matumizi ya Madawa ya kulevya.

Muimbaji huyo amedai kutembea au kukaa na watu ambao wanatumia Madawa ya kulevya haimaanishi kwamba na yeye bado anaendelea kutumia.

“Mimi siko kwenye hiyo list na nilishaacha hizo mambo,” Q Chief alikiambia kipindi NLF cha EATV. “Ningekuwa natumia ungekuta jina langu kwenye list ya Makonda lakini mimi siko,”

Aliongeza, “Mimi ni mtoto wa uswahilini, nimekuwa huko kwa hiyo kutembea au kuonekana maeneo ambayo wanakaa wahumi ni maeneo yangu kwa sababu ndiko waliko washkaji zangu,”

Q Chief alidai yeye aliweza kuacha mwenyewe matumizi ya Madawa ya kulevya baaada ya kuona yanampotezea mwelekeo katika maisha yake.

Video.Mbwana Samatta Azidi Kuwakuna Wazungu kwa Kiwango kikubwa cha Kufumania Nyavu..!!

$
0
0

Nahodha wa timu a taifa ya Tanzania , Mbwana Samatta amezidi kuwasha moto katika ligi kuu ya Ubelgiji maarufu kama Jupiler Pro League baada ya kuifungia timu yake ya KRC Genk bao moja katika ushindi wa mabao 3-0 walioupata wakiwa ugenini usiku wa Ijumaa hii dhidi ya Sint-Truiden.

Mabao ya Genk yalifungwa na Alejandro Pozuelo Melero dakika ya 37, Mbwana Ally Samatta dakika ya 39 na Ruslan Malinovskiy dakika ya 45.

Kwa sasa Genk wanashika nafasi ya tano katika ligi hiyo wakiwa na pointi 41 huku klabu ya Club Brugge ndio wanaongoza ligi hiyo wakiwa na pointi 52.

Picha: TID Aanza Maisha Mapya Baada ya Siku 5 za Lupango, Amtambulisha Mpenzi Wake Mpya..!!!

$
0
0

Msanii mkongwe wa muziki TID ameamua kusahau yaliyopita na kuanza maisha mapya ikiwa ni siku chache toka aachiwe na mahakama kwa sharti la dhamana ya shilingi milioni 10 na kutakiwa kuripoti polisi kwa mwezi mara mbili baada ya kukiri kutumia Madawa ya kulevya pamoja na wenzake 12.

Muimbaji huyo ambaye alikaa lupango kwa siku tano kabla ya kuachiwa, amemtangaza mpenzi wake mpya ambaye jina lake halikutambulika mara moja.

“The Smile i needed to see after all the trouble i have been through. Million Dollar Smile, am i in Love again!,”aliandika TID Instagram huku akaiwa ameweka picha ya mrembo huyo hapo juu.

Aliongeza, “Watasema sana na kisha watalala kama kunipenda najua unanipenda sana ooohyeahhh,”.

Mhubiri Awapa Waumini Dawa ya Kuua Panya..!!!

$
0
0

Mhubiri mmoja nchini Afrika Kusini amekuwa akiwapa waumia sumu ya kuua panya kama moja ya njia ya kujaribu imani yao.

Light Monyeki, ambaye anaongoza kanisa la Grace Living Hope Ministries mjini Pretorria, anasema kuwa kwa kunywa sumu hiyo, inaonyesha kuwa kifo hakina nguvu kwa waumini.

Picha kwenye ukurasa wake wa Facebook, zinamuonyesha akichanganya dawa inayotumiwa kuua panya wa chupa na kuinywa na kisha kuwapa waumini.

Bwana Monyeki ni mhubiri wa hivi majuzi kuripotiwa kuhusika na visa vyenye utata kanisani.

Picha: Defoe Akubali Kulala na Bradley Lowery Kwenye Siku Yake ya Mwisho Duniani..!!

$
0
0

Jumamosi ya leo ndio siku ambayo ilidaiwa kuwa mtoto ambaye ni shabiki mkubwa wa klabu ya soka ya Sunderland, Bradley Lowery atafariki dunia kutokana na ripoti ya madaktari ambapo anasumbuliwa na maradhi ya kansa ambayo imedaiwa kufika mwisho hadi kushindikana kutibika.

Bradley amemuomba Jermain Defoe kulala naye kitanda kimoja hospitalini ambapo amelazwa katika siku yake hiyo ya mwisho duniani ambayo alidaiwa kuwa atafariki ambapo mshambuliaji huyo amelikubali ombi hilo.

Miezi kadhaa iliyopita ilidaiwa kuwa matibabu ya mtoto huyo yatagharimu kiasi kisichopungua bilioni mbili ambapo timu za Everton, Man City na Sunderland pamoja na wadau wengine walijitolea kumchangia lakini baadae jopo la madaktari lilitoa taarifa ya kushindikana kwa matibabu hayo.

Utajiri wa Makonda Wawa Gumzo Bungeni...Mbunge Ataja Mali Mpya za Paul Makonda

$
0
0

Dodoma. Sakata la mali zinazodaiwa za Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda limeendelea kulitikisa bunge baada ya Mbunge wa Rombo, Joseph Selasini (Chadema) kuongeza nyingine.

Akichangia taarifa za Kamati za Bunge za Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge na ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama, Selasini alisema Makonda amenunua jengo (apartment), lenye thamani ya Sh600 milioni.

“Makonda amenunua apartment pale Viva Towers kwa Sh600 milioni. Makonda amempa mke wake gari aina ya Mercedes Benz lenye thamani ya Dola 250,000 za Marekani (Sh550 milioni) kama zawadi ya ‘Birthday’,” alisema Selasini.

Suala la utajiri wa Makonda, liliibuliwa bungeni kwa mara ya kwanza Februari 6 na Mbunge wa Geita Vijijini (CCM), Joseph Msukuma akitaka mteule huyo wa Rais achunguzwe kwa kujilimbikizia mali.

Kiini cha mbunge huyo kumshukia Makonda ilitokana na hatua yake ya kutangaza majina ya watu aliodai wanajihusisha na biashara ya madawa ya kulevya, huku akidai utajiri wake una shaka.

Msukuma Februari 7, mwaka huu aliomba mwongozo kwa Spika, akitaka Bunge litoe mwongozo kuhusu utajiri huo wa Makonda ndani ya muda mfupi.

Msukuma alisema kuwa katika kipindi cha mwaka mmoja tu wa wadhifa wake kama mkuu wa mkoa, Makonda amejilimbikizia mali likiwamo gari aina ya Lexus, lenye thamani ya Sh400 milioni.

Mbali na mali hizo Msukuma alisema Makonda anamiliki magari mengine ya kifahari aina ya V8, anajenga maghorofa jijini Mwanza na amekarabati ofisi yake kwa Sh400 milioni bila kutumia utaratibu wa sheria ya manunuzi.

Mbali na hilo, Selasini alisema utaratibu unaotumiwa na Makonda kushughulikia tatizo la dawa za kulevya, umetoa mwanya kwa wafanyabiashara wakubwa wa dawa hizo kukimbilia nje ya nchi.

“Kama unawatangaza watu kwa utaratibu huu. Ni mfanyabiashara gani wa dawa za kulevya mjinga amebaki katika hii. Makonda amesaidia kuwakimbiza labda anashirikiana nao,” alisema.

Wakati huo huo Mbunge wa Ukonga, Mwita Waitara (Chadema), ameliomba Bunge kutoa mwongozo kwa kile alichodai ni hatua ya katibu wa Bunge, Dk Thomas Kashililah kupingana na maazimio ya Bunge.

Source: Mwananchi
Viewing all 104808 articles
Browse latest View live




Latest Images