Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104795 articles
Browse latest View live

Imevuja..Kipigo Chamtoa Mbio Gigy Money kwa Mwanaume Huyu..!!!

$
0
0

UHUSIANO wa kimapenzi uliotawaliwa na sarakasi nyingi, kati ya muuza nyago machachari Bongo, Gift Stanford ‘Gigy Money’ na mtangazaji mwenzake wa kituo kimoja cha redio nchini, Moulad Alpha ‘Moj’ hatimaye umevunjika baada ya mwanadada huyo kusalenda kutokana na madai kwamba mchizi alikuwa akimshushia sana kichapo mwanadada huyo.

Kwa mujibu wa chanzo chetu kilichopo karibu na wawili hao, licha ya Gigy kuonekana machachari kwenye jamii, tangu aanzane na Moj aliamua kutulia mno, tatizo ni kwamba jamaa hajatulia na kila anapomuhoji kwa nini anamsaliti anampa mkong’oto.

“Habari ndo hiyo, wale wameshaachana maana mara kwa mara Gigy alikuwa anapigwa kwa kosa ambalo si lake, amevumilia sasa uzalendo umemshinda,” alisema sosi.

Kwa upande wake Gigy alipotafutwa, alisema alikuwa anampenda sana Moj kwani alimuona ni mstaarabu lakini ghafla amebadilika sana.

“Kweli kupenda utumwa, mateso niliyoyapata kwa huyu mwanaume nimesalenda, kwa nini haniheshimu na ananipiga?” alisema Gigy

Sekeseke la Madawa Masogange Kufikishwa Kortini Kesho...!!!

$
0
0

KAMANDA wa Polisi wa Kanda Maalumu Dar es Salaam, Simon Sirro amesema mtuhumiwa, Agnes Gerald maarufu Masogange na wenzake 15 wamepelekwa kwa Mkemia Mkuu wa Serikali kwa ajili ya kuchukuliwa vipimo vya damu ili kubaini kama wanatumia dawa za kulevya.

Staa huyo wa video za wasanii wa Bongo Fleva anayetajwa kama ni miongoni mwa mastaa wanaochukua fedha nyingi kama ujira wa kucheza katika nyimbo mbalimbali za wasanii kama video queen, anahushishwa na madawa ya kulevya kwa mambo matatu ambayo atachukuliwa vipimo. ni pamoja na kama anauza , anatumia au anasafirisha dawa za kulevya.

Masogange alikamatwa na polisi juzi na alifikishwa kituoni kwa mtindo tofauti na wasanii wengine kwani yeye hakutangazwa kama ilivyokuwa kwa Wema, T.I.D, Nyandu Tozi na wengine wakiwemo wafanyabaishara wakubwa Dar es Salaam.

Kamishna Sirro amewaambia wanahabari leo kuwa Masogange amepelekwa kwa Mkemia Mkuu wa Serikali na majibu yakipatikana kesho atafikishwa mahakamani kama itakuwa itakuwa ni tofauti anaweza kufikishwa kortini jumatatu.

“Tunamchunguza Masogange katika mambo matatu ili kujua kama anauza , anatumia au anasafirisha dawa za kulevya, “ amesema Kamishna Sirro.


Waliokamatwa kwa Dawa za Kulevya Wafikia 349..!!!

$
0
0

Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limetoa taarifa ya kukamatwa kwa jumla watuhumiwa 349 akiwemo 'video queen' Agnes Gerald maarufu kwa jina la 'Masogange', katika oparesheni ya kuwasaka watu wanaohusika na dawa za kulevya.

Akizungumza leo Jijini Dar es Salaam, Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Kamishna Simon Sirro amesema kati ya watuhumiwa hao, wamo wauzaji, wasafirishaji na watumiaji wa dawa za kulevya, na kwamba wataanza kufikishwa mahakamani siku ya kesho, huku mmoja akipandishwa kizimbani leo.

Pia ametoa taarifa ya kijana mmoja anayedaiwa kusambaza taarifa za uongo, ambapo amesema kuwa jeshi hilo linamshikilia kijana huyo ambaye ni mwanafunzi mwenye umri wa miaka 23, anayedaiwa kutaja majina ya viongozi na kuwatuhumu kuwa wanahusika na dawa na dawa za kulevya.

Kuhusu askari 9 waliotuhumiwa kuhusika na dawa hizo, Kamanda Sirro amesema askari hao wamekabidhiwa kwa Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya kuzuia na Kupambana na Dawa za Kulevya kwa ajili ya kuchukuliwa hatua za kisheria.

Kamanda Sirro amesema hadi sasa jumla ya kete 612 pamoja na bangi vimekamatwa na kwamba kuna watu wengine 17 ambao bado jeshi hilo linawafuatilia na watakuwa mbaroni wakati wowote.

Hizi Ndizo klabu Tajiri Zaidi Afrika,Simba ,Yanga na Azam Hazisomeki....!!!

$
0
0

KATIKA miaka ya hivi karibuni mchezo wa soka umekuwa chanzo kikubwa cha mapato kwa nchi zilizopiga hatua zikiwamo zile za barani Ulaya.

Kwa Afrika ambako nchi nyingi ni masikini, soka limekuwa kimbilio la vijana wengi ambao kwao ndicho chanzo kikubwa cha ajira.

Wachezaji, makocha, wauguzi na wafanyakazi wengine wa klabu wamekuwa wakifaidika na utajiri mkubwa unaozalishwa kupitia mchezo huo.

Lakini pia, Serikali kupitia mamlaka za mapato, imekuwa ikinufaika na fedha za kodi zitokanazo na mchezo wa soka.

Pia, klabu zimekuwa zikiingiza fedha nyingi kutokana na mapato ya uwanjani, mauzo ya wachezaji wakiwamo makinda wanaozalishwa katika ‘academy’ zao na hata dili za matangazo.

Kwa mujibu wa ripoti ya mwaka jana ya Jarida la Forbes la Marekani, zifuatazo ni klabu ambazo mpaka sasa zimeshavuna fedha nyingi kutokana na biashara ya soka.

Al Ahly (Misri)

Ndiyo timu tajiri zaidi barani Afrika kwa sasa ikiwa na thamani ya euro milioni 19,25. Klabu hiyo ndiyo inayoongoza kwa kuwa na mataji mengi barani Afrika (132).

Lakini pia, inaongoza kwa kutwaa mara nyingi lile Kombe la Klabu Bingwa Afrika ikiwa imefanya hivyo mara nane.

Miaka miwili iliyopita, thamani ya Al Ahly ilikuwa mara mbili ya ile ya Orlando Pirates ya Afrika Kusini.

Esperance (Tunisia)

Utajiri wao unafikia euro milioni 12,75 na wanamiliki mataji mawili ya Ligi ya Mabingwa Afrika.

Timu hiyo iliyoanzishwa miaka 98 iliyopita, ina heshima kubwa Tunisia ambapo imeshinda makombe 26 ya ligi kuu nchini humo.

Club Africain (Tunisia)

Huenda si mara nyingi umekuwa ukiisikia kwenye mazungumzo ya kila siku, lakini ni moja ya klabu zenye heshima kubwa Tunisia na barani Afrika kwa ujumla.

Wakali hao wanamiliki mataji 13 ya Ligi Kuu Tunisia na utajiri wao unatajwa kuwa ni euro milioni 11, 80.

Mbali na soka, ‘vibopa’ hao wa jijini Tunis, wanamiliki timu za michezo mbalimbali ikiwamo ya mpira wa kikapu.

Uwanja wao wa nyumbani unaoitwa Stade Olympique de Rades, una uwezo wa kuchukua mashabiki 60,000.

Mamelodi Sundowns (Afrika Kusini)

Mamelodi ndiyo mabingwa watetezi wa mbio za kufukuzia taji la ya Mabingwa Afrika mwaka huu.

Walipochukua mwaka jana, ulikuwa ubingwa wao wa kwanza katika historia ya klabu na michuano hiyo.

Mwaka 2001 walikaribia kulitoa mkononi lakini walipochapwa mabao 4–1 na Al Ahly katika mchezo wa fainali. Mamelodi inaongoza kwa kuwa na makombe mengi katika historia ya soka la Afrika Kusini.

Forbes linaitambua klabu hiyo kuwa na utajiri wa euro milioni 10.35.

Kaizer Chiefs (Afrika Kusini)

Kama ilivyo Mamelodi, Chiefs nayo ni miongoni mwa klabu zinazoogelea kwenye dimbwi la utajiri kutokana na biashara ya soka.

Takwimu za kiuchumi za Forbes linaitaja timu hiyo kumiliki utajiri wa euro milioni 10, 48.

Ujenzi wa Uwanja wa Amakhosi unaoingiza mashabiki 55,000 unaomilikiwa na klabu hiyo uligharimu pauni milioni 105.

Mchezo ambao Chiefs huutolea macho zaidi ni ule unaowakutanisha na mahasimu wao wakubwa Orlando Pirates.

Zamalek SC (Misri)

Ilipoanzishwa mwaka 1911, ilifahamika kwa jina la Qasr El-Neel na haikuwa na utajiri iliyonao leo wa euro milioni 10,30.

Mbali na mataji mengine, imeshinda mara tano lile la Ligi ya Mabingwa Afrika.

Miongoni mwa mastaa wakubwa waliowahi kutamba na timu hiyo ni pamoja na Hassan Shehata, Hossam Hassan, Junior Agogo na Amr Zaki.

Klabu nyingine tajiri

USM Alger (euro milioni 9.65), E.S Setif (euro milioni 8.6), Raja Casablanca (euro milioni 8.13), na T.P. Mazembe (euro milioni 7.70).

Taarifa za Mchekesha Kansime Kukamatwa na Madawa ya Kulevya London..Ukweli Huu Hapa

$
0
0
Kuna picha inasambaa kwenye mitandao kuanzia ikionyesha sehemu ya habari iliyoandikwa na mtandao uitwao METRO na inasema Mwigizaji/Mchekeshaji wa Uganda Anne Kansiime amekamatwa na Polisi kwenye uwanja wa ndege London akiwa na dawa za kulevya kilo mbili.

Ni habari zilizowashtua wengi lakini ukweli tumeupata, Anne hajakamatwa na yeye ni mzima wa Afya nyumbani kwao Kampala Uganda na usiku wa leo anatarajia kufanya show inayohusiana na sanaa yake.


Baadhi ya mitandao imekanusha na kusema kuwa sio kweli lakini pia baada ya hili nikapita kwenye ukurasa wa Instagram wa Anne kansime na kwenye picha ya mwisho kupost alicomment kusema yuko salama baada ya mwimbaji Irene Namubiru kumuuliza.


Kupitia ukurasa wake wa Twitter @Kansiime256 Anne aliandika pia kwamba kuwa yuko uwanja wa taifa Uganda tayari kwa show yake usiku wa leo.


"At the National Theatre Kampala, Uganda ready for tonight's show with my family @funfactory ......."

Orodha Waliofunguliwa Kesi Chadema Inatisha

$
0
0

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimesema wanachama na viongozi wake 215 wamefunguliwa kesi katika mahakama mbalimbali nchini tangu kufanyika kwa Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015.

Chadema imesema wanachama hao wamepandishwa kizimbani katika jumla ya kesi 78 huku wengi wao wakinyimwa dhamana na wale waliopatikana na hatia, walipewa adhabu za vifungo bila ya kupewa fursa ya faini.

Kutokana na hali hiyo Chadema inatarajia kuandaa orodha itakayoainisha kesi zote za jinai ambazo bado zipo mahakamani pamoja na kuonyesha aina ya mashtaka na vifungo vilivyotolewa, kwa vyombo vya habari na taasisi za ndani na nje ya nchi.

Makamu Mwenyekiti wa Chadema, Profesa Abdallah Safari aliyasema hayo jana wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu mrejesho wa kikao cha kamati ndogo ya Kamati Kuu ya Chadema kilichokaa Jumanne.

Katika uchaguzi huo uliofanyika Oktoba 25, 2015 Rais John Magufuli wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) aliibuka mshindi kwa kupata kura 8,882,935 sawa na asilimia 58.46 ya kura zote halali.

Nafasi ya pili ilishikwa na mgombea wa Chadema aliyeungwa mkono na mwamvuli wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), Edward Lowassa aliyepata kura 6,728,480 sawa na asilimia 39.97.

Prof. Safari alisema mara baada ya Uchaguzi Mkuu huo kumalizika, viongozi wa Chadema wamekuwa wakikamatwa na kushtakiwa kwa makosa ya kubambikizwa; kwa kisingizio cha uchochezi.

“Hivi sasa umekuwa ni mtindo kwa mahakama kuwakatalia dhamana wanachama wa Chadema bila ya sababu za msingi," alisema Prof. Safari.

"Pia imekuwa ni mtindo kuwahukumu vifungo bila kuwapa fursa ya kulipa faini.”

Prof. Safari alisema katika kikao hicho cha kamati kimetoa wito kwa mhimili wa Mahakama kutekeleza wajibu wake kwa weledi uliotukuka; kuhakikisha kuwa haki inatendeka bila kuwapo kwa vitisho kutoka kwa mtu yeyote.

“Majaji wanapaswa kuiga mfano wa uhuru wa Mahakama na weledi wa majaji wa Afrika Kusini, Zimbabwe na Marekani ambao waliweza kutengua amri batili zilizotolewa na marais wa nchi zao,” alisema Prof. Safari.

Aidha, Profesa Safari alisema Kamati Kuu imetoa wito kwa mawakili kuchukua wajibu mkubwa kuisaidia mahakama kutekeleza majukumu yake kwa weledi kwa kuhakikisha haki inatendeka bila woga, vitisho au vishawishi, pamoja na kutokukubali kutishwa na mtu au asasi yoyote katika kuitetea, kuilinda Katiba na sheria za nchi.

Kimenukaaa..Baada ya Madawa ya Kulevya..Kibano kwa Wavutaji Sigara Chaja.

$
0
0

SERIKALI ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) inakusudia kutunga sheria ya kuzuia uvutaji wa sigara hadharani katika visiwa vya Unguja na Pemba.

Hatua hiyo ilitangazwa jana na Waziri wa Afya, Mahmoud Thabit Kombo, wakati akijibu swali la Mwakilishi wa Mpendae kwenye Baraza la Wawakilishi.

Mwakilishi huyo, Mohammed Said Dimwa, alitaka kujua athari kubwa inayopatikana kutokana na utumiaji wa sigara pamoja na mikakati ya wizara katika kukabiliana na hali hiyo.

Waziri huyo alisema serikali imeamua kuchukua hatua hiyo kutokana na uwapo wa idadi kubwa ya wagonjwa wa maradhi yasiyoambukiza na kwamba uvutaji wa sigara umebainika kuwa chanzo chake.

Kombo alisema katika kukabiliana na hali hiyo, Serikali itatenga maeneo maalum ya uvutaji wa sigara.

Picha 8:Benzi Watengeneza Gari la Kifahari Litakalouzwa Kwa Watu 9 tu Duniani

$
0
0
Kampuni ya Mercedes Benz imetangaza toleo lao jipya ya gari za kifahari aina ya Maybach — ambalo ni gari la kifahari lenye muonekano wa gari linaloweza kuhimili barabara mbovu.

Gari hili linaitwa Mercedes G650 Landaulet, lina nafasi kubwa kuliko tulivyozoea gari nyingi zilivyo na viti vyake vimetengenezwa kukufanya ustarehe zaidi ya unapolala kwenye kitanda chako!

Tazama hapa baadhi ya picha za gari hili:

Landaulet ni gari ya kwanza kutoka kampuni ya Maybach kutengenezwa na Benz. Gari hii ilitengenezwa na kuwekwa kwenye kundi la ‘S –Class’, katika jitihada za Benz kuinusuru kampuni ya Maybach.


Gari hii ambayo baada ya kuboreshwa ikaitwa S600 lina vioo visivyoruhusu risasi kupenya na jenereta linalotoa moshi nje ya gari endapo mtakuwa kwenye hatari
Mercedes wakatengeneza gari hili toleo la  S650 Cabriolet ambayo ilikuwa mara ya pili kwao kuboresha gari la kampuni ya Maybach.


Lina viti vine na paa linalofunguka (comvertible)
Gari hili toleo la sasa lina nafasi ya kutosha mtu kukaa na kujiachia. Kuna nafasi ya futi 2 kati ya miguu ya mtu aliyekaa na kiti kingine!


Wanaokaa mbele wanakuwa kwenye paa lililofunikwa wakati wale wa viti vya nyuma wanakuwa kwenye paa linaloweza kufunguka.



Ni kawaida kuwekewa starehe kenye magari aina hii. Kila abiria aliyekaa viti vya nyuma amewekewa televisheni yenye ukubwa wa inchi 10

Limetengenezwa kukupa utulivu wa hali ya juu kabisa uwapo ndani gari. Viti vyake vinaweza kukanda mwili wako (massage) kwa kubonyeza kitufe tu.



Pia kunakioo kinachotenganisha watu walio kwenye viti vya mbele na wale waliokaa viti vya nyuma.



Benz hawajatangaza bado gari hili litauzwa kwa gharama gani lakini endapo itakuwa kama gari nyengine mbili za kampuni ya Maybach ambazo washazitengeneza awali, lazima litauzwa zaidi ya dola laki tatu za Marekani. Itatengeneza magari 99 tu na kuuzwa kwa mwaka huu.

Ingawa ndani lina muonekano wa gari la starehe, gari hili limetengenezwa kumudu barabara mbovu. Limeinuliwa juu kwa futi 1.7 kutoka ardhini na lina injini yenye nguvu aina ya V12 Biturbo.

Spika Ndugai: Makonda ni Mtani Wangu, Hivyo Msijali Maneno yake

$
0
0
Bila shaka hili ni dongo zuri kwa Makonda, na ni sawa na kusema watu wayapuuze maneno anayoyaongea kwa kuwa ni utani tu

Siku moja baada ya Spika wa Bunge, Job Ndugai, kutakiwa kutimiza ahadi yake ya kuweka vifaa vya kupima wabunge kama wametumia kilevi ama dawa za kulevya kabla ya kuingia Ukumbi wa Bunge, amesema Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda ni mtani wake, hivyo watu wasijali maneno yake. Aidha, katika Mkutano wake uliofanyika juzi, Makonda alimuomba Spika Ndugai kuweka kipimo hicho ili kabla wabunge hawajasimama kuchangia hoja wabainike kama wanatumia dawa za kulevya au la.

Chanzo: Dar24

Maneno ya Wema Sepetu Baada ya Kuona Yusuph Manji Kaachiwa Kwa Dhamana

$
0
0

Mwigizaji Wema Sepetu ameyaandika haya baada ya kuona taarifa za Mfanyabiashara maarufu na Mwenyekiti wa Yanga kuachiwa kwa dhamana leo Mahakamani Kisutu Dar es salaam baada ya kushikiliwa kwenye sakata la dawa za kulevya.

Eric Omondi: Namshukuru Sana Diamond, Ndiye Aliyenifungulia Mlango Kwenye Soko la Tanzania

$
0
0
Mchekeshaji maarufu kutoka nchini Kenya, Erick Omondi ijumaa iliyopita ya tarehe 10 alifunguka jinsi Diamond alivyomsaidia kupenya kwenye soko la Tanzania.

Omondi anasema kwa mara ya kwanza alikutana na Diamond Mombasa nchini Kenya akiwa kwenye harakati za kurekodi wimbo wa Diamond unaoitwa Nabeba Mawe.

Katika mazungumzo yao Diamond alimualika Omondi kwenye show kubwa maarufu kama "Zari All White Part" na kumuomba awe MC wa show.

Katika show hiyo ambayo ilikuwa na zaidi ya wahudhuriaji 10,000 , redio na TV nyingi za Tanzania Omondi hakufanya kosa kama MC, alitumia kudhihirisha kipaji chake cha uchekeshaji na ikawa ndio mwanzo wa kujulikana Tanzania.

Omondi anasema bila Diamond kumwalika Tanzania huenda asingeweza kupenya katika soko la Tanzania, soko lenye mashabiki wengi sana wa kazi zake.

Mpaka sasa Erick Omondi ana mpango katika kipindi cha miezi miwili ijayo, kuanzisha Comedy TV show nchini Tanzania kwenye moja ya Runinga maarufu hapa nchini.
Japo hakuweka wazi kipindi hicho kitarushwa hewani kupitia kituo cha habari cha shirika lipi.

Source: NTV ya nchini Kenya.

Ali Kiba Ametoa Video ya Wimbo Remix ya Aje...Itazame Hapa

$
0
0
Msanii Alikiba baada ya kufanya vizuri na wimbo wa “Aje”, ameachia rasmi Video mpya ya wimbo wa “Aje Remix”, akiwa amemshirikisha msanii M.I kutoka Nigeria. Tazama hapa chini alafu toa komenti yako.

Mfanyabiashara Mbaroni Kwa Dawa Za Kulevya

$
0
0

MFANYABIASHARA maarufu jijini Mbeya, Steven Samweli maarufu kwa jina la Maranatha, ametiwa nguvuni akituhumiwa kujihusisha na biashara ya dawa za kulevya.

Kutiwa nguvuni kwa mfanyabiashara huyo ni mwendelezo wa nia ya Serikali ya kupambana na biashara ya dawa hizo nchini.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Dhahiri Kidavashari, aliwaambia waandishi juzi kwamba, Maranatha alikamatwa juzi usiku akiwa katika moja ya maduka yake ya dawa baridi.

“Baada ya polisi kupata taarifa za mfanyabiashara huyo kuhusishwa na biashara ya dawa za kulevya, tuliweka mtego na hatimaye kufanikiwa kumtia nguvuni.

“Kwa sasa tunamshikilia kwa mahojiano na baada ya uchunguzi kukamilika, atafikishwa mahakamani,” alisema Kamanda Kidavashari.

Pamoja na hayo, kamanda huyo wa polisi alisema kukamatwa kwa mfanyabiashara huyo kunafikisha idadi ya watu wanane waliokamatwa kwa tuhuma za kujihusisha na uingizaji, usambazaji na utumiaji wa dawa za kulevya mkoani Mbeya.

“Miongoni mwa hawa tunaowashikilia, baadhi yao walikutwa na vielelezo, hivyo watafikishwa mahakamani wakati wowote wakati uchunguzi zaidi ukiendelea.

“Kwa hiyo, nawaomba wananchi mkoani hapa, waachane kabisa na biashara ya dawa hizo kwa sababu wakikutwa nazo, watakamatwa na kufikishwa katika vyombo vya dola,” alisema Kamanda Kidavashari.

Hivi Ndivyo Arosto inavyowatesa Watumiaji Dawa za Kulevya

$
0
0

Dar es Salaam. Daktari bingwa mwandamizi wa Tiba na Afya ya Akili katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH), Frank Masao amesema mtumiaji aliyeacha ghafla matumizi ya dawa za kulevya hupata tatizo la arosto linalowasumbua sana.

Alisema mtumiaji anapokosa kilevi, arosto huwa kali zaidi siku tatu za kwanza, hupungua kati ya wiki moja hadi mbili na ili hamu ya matumizi ya dawa za kulevya imalizike kabisa huweza kuchukua hadi miaka miwili.

Hata hivyo, ameshauri kuwa watumiaji wanaoshikiliwa polisi wanapaswa kupewa matibabu kwa sababu dawa za kulevya zina madhara mwilini japo hawafi isipokuwa kuteseka.

Akizungumza na gazeti hili katika mahojiano maalumu jana, Dk Masao alisema arosto ni kitendo cha mtumiaji wa kilevi kutamani au kuwa na kiu zaidi ya kukitumia kilevi hicho wakati anapokosa.

Dk Masao alisema arosto ya kila dawa hutofautiana na kwamba mtumiaji wa heroine anapokosa kilevi hicho, huanza kupiga miayo, kutoa machozi, kamasi, maumivu makali ya viungo, tumbo na kuharisha.

“Pia, huwa anakosa hamu ya kula, hapati usingizi, hofu isiyo na ulazima, hatulii sehemu moja, anakosa amani na huwa na hamu ya kilevi hicho kupindukia,” alisema.

Dk Masao alisema kawaida katika kichwa cha binadamu kuna sehemu inayoitwa ‘Mesolimbiq System’ au ‘Reward System’ ambayo ndiyo huwa inasababisha mtu kuendelea au kuiacha tabia fulani.

Alidai kuwa sehemu hiyo huwa inatoa kemikali inayoitwa Dopamine, hivyo ikiwa utatumia dawa za kulevya zozote zile huwa zinasababisha kemikali hiyo kutoka na kumfanya mtumiaji ajisikie raha zaidi.

“Kile kitendo cha kujisikia raha maana yake ni kwamba Dopamine imeachiliwa na isipoachiliwa utajisikia kinyume chake. Pia, huwa zinaacha kumbukumbu kwenye ubongo na baada ya muda raha hiyo ikiisha, mtu anatamani kuipata tena, hivyo ni lazima Dopamine itoke tena,” alisema.

“Ndiyo maana mtu anayetumia ulevu baada ya muda fulani anakuwa hana ujanja ni lazima atumie tena kilevi kwa sababu ‘Dopamine’ zinakuwa wazi. Ile hamu kupindukia ndiyo ambayo tunaita ‘arosto’ na hapo hulazimika kufanya kila kinachowezekana kupata kilevi,” alisema.

Aliongeza watumiaji wa dawa za kulevya wanapokuwa na arosto, hujikuta wakifanya vitendo vya uhalifu ilimradi wapate fedha za kununua dawa za kulevya kumaliza hamu waliyonayo.

“Ile hamu ya kuvuta kwenye ubongo wake huwa inakaa hadi miaka miwili na ndiyo maana sisi wataalamu, yule tunamuona ni mgonjwa. Kwa wataalamu mtu huyu kumfunga ni kuendelea kumtesa, anatakiwa kutibiwa kwa sababu hamu haiishi,” alisema.

Alisema kwa sababu hamu hiyo huwa inakaa muda mrefu na mtu huyo akitoka ‘soba house’ baada ya muda mfupi na ikiwa hajapata mafunzo stahili, ataanza tena matumizi ya dawa za kulevya.

“Kuna baadhi ya soba house huwa zinatoa mafunzo stahili, kama namna ya kukwepa matumizi ya dawa hizo, kukwepa marafiki wabaya, kufanya kazi halali,” alisema.

Dk Masao alisisitiza kuwa kikawaida arosto haiuwi na kwamba, kibinadamu huwa wanateseka na kuhitaji kupata tiba.

MSUMBIJI: Mwanamke wa Kitanzania Abakwa Mpaka Kufa. Serikali Imefungwa Pasta?

$
0
0

Jamani, Hii inasikitisha sana tangu kuanza kusikika kwa sakata la watanzania kufurushwa uko msumbiji mengi yametokea lakini serikali yetu inaonesha kuwakandamiza watanzania kuwaonesha hawakuwa wakiish kihalali kabisa.

Okay Yote sawa mtu kwao lakini serikali ya msumbiji inafata utaratbu kuwarudsha watanzania?

Je, sisi huwa tunavunja sheria kuwarudsha kistarabu??

Maofisa wa msumbiji wamekuwa wakifanya vitendo vya kikatili ikiwemo kuwapora mali zao, pesa, na hati za kusafiria.

Sikuridhika nliamua kufunga safari kwenda mtwara kuonana na wahanga.

Katika yote kilichoniumiza nlipofanya mahojiano na mwanamke ambaye rafiki yake kutoka Morogoro alokuwa akiishi Msumbiji kubakwa na maofisa wa Msumbiji mpaka kufa akiwa anawahishwa hospital huko Msumbiji.

Tukio hilo liltokea usiku maofisa hao walivamia nyumba ya huyo mdada kisha kumbaka kwa zamu hatimaye akawa na hali mbaya hadi anakuja kupata msaada kupelekwa hospitali hali yake ilikuwa mbaya sana na kufariki dunia

Je, serikali hawajui haya? Mbona hawazungumzii lolote?
Kwanini wanaishia kuwakandamiza watanzania na kuwaonesha dunia watanzania wale hawakufata sheria?

Nimeweza kuona vibali vya wengine walofankiwa kurudi navyo vibali vya kuishi na kufanyia kazi lakini bado wamewafurusha.

Kama sheria hao wote wamevunja sheria za ukaazi?

Yupo mwingine ambaye alikuwa akiishi na mkewe na mtoto na mkewe ni mjamzito lakini alipohitaji kurudi na mkewe Tanzania maofisa wa Msumbiji walimkatalia.Je, sheria ipi inayoruhusu hayo??

Mbona wao wanarudishwa na familia zao ikiwa wamekuja nazo?

Serikali ya Tz inawaogopa Msumbiji kutetea Raia wao?

Rais wa Msumbiji, Filipe Nyusi alizaliwa Tanzania na kusoma Tunduru na kupata mafunzo ya kijeshi hapa Tanzania.

Lakini watu hawa ambao wamesaidiwa na Tanzania wameshindwa kuagiza vikosi vyao wawarudishe kistarabu na kufata utaratbu bila kuvunja sheria?

Vipi wawafukuze kama Mbwa? Wamewafunga mahabusu bila kuwapa chakula siku tatu.

Wakawapakiza kwenye malori bila ya chakula wala mali zao.

Inasikitisha Mtanzania mwenzetu anabakwa mpaka kufa serikali haina inalosema?


Sisi mbona hawathamini watanzania na kuwaonesha dunai raia wa Kitanzania wana makosa?

Hakuna ofisa wa Msumbiji alochukuliwa sheria mpaka sasa kwa mujibu wa chanzo cha uhakika ndani ya Msumbiji.

Ofisa mmoja ambaye mama yake ni mtanzania na baba yake ni Msumbiji ameambia chanzo chetu kawaida na maofisa wa Msumbiji hufanya vitendo vya kikatili kwa wageni.

Ameongeza na kusema kuwa tatizo mabalozi wa Tanzania pia sio wakali kutetea raia wao bali kuwakandamiza.

Anazidi kusema kuwa anaumia sana kuona watanzania wenzake kwa wanayofanyiwa lakini hana mamlaka ya kuweza kuzuia.

Amethibitisha pia kuwa ni kweli mwanamke huyo wa kitanzania alibakwa na maofisa wa Msumbiji wapatao sita hadi saba kwa uchunguzi wake.

Jamani tuungane tusaidie wenzetu lazima tujifunze kupendana serikali inahisi hawa watu sijui manyani sijui sio raia wao nashindwa kuelewa.

Taarifa ya Kikao cha Kamati Ndogo ya Kamati Kuu cha Dharura cha CHADEMA...!!!

$
0
0

CHAMA CHA DEMOKRASIA NA MAENDELEO (CHADEMA)

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI JUU YA MAAZIMIO YA KIKAO CHA KAMATI NDOGO YA KAMATI KUU

1.0 UTANGULIZI

Kikao cha Kamati Ndogo ya Kamati Kuu cha dharura kilichoketi tarehe 14 Februari, 2017 Jijini Dar es Salaam katika Hoteli ya Bahari Beach kilipata nafasi ya kujadiliana kwa kina kuhusu matukio mbalimbali yanayoeendelea hapa nchini ikiwa ni pamoja na kutolewa kwa kauli mbalimbali na viongozi wa kiserikali na ambazo zimeendelea kuuthibitishia umma wa watanzania kuwa nchi yetu haiendeshwi kwa misingi ya kuzingatia Katiba, Sheria na Kanuni tulizojiwekea kama Taifa .

Aidha Kamati hiyo ilipata muda wa kutafakari kwa kina zaidi juu ya Operesheni UKUTA ambayo tumeendelea kufanikiwa katika kuitekeleza kwa vitendo na pia watanzania wengi zaidi sasa wameona umuhimu wa kuendelea na Operesheni UKUTA kwani Taifa linaelekea kwenye kutumbukia kwenye utawala wa kutokufuata Katiba na Sheria za Nchi (Udikteta kamili).

Mwalimu Nyerere Julai 19, 1967 alisema hivi kuhusu udikteta “Udikteta ni serikali ya mtu mmoja au kikundi cha watu wachache na wao ndiyo huwa sheria.Anayepinga watakayo,basi huonyeshwa cha mtema kuni”

Kamati hiyo imejiridhisha bila shaka kuwa sasa Chama chetu kinawindwa na watawala pamoja na Rais Mwenyewe na hii ni katika kuelekea kufikia lengo la Rais alilolitangaza alipokuwa Singida mwezi Juni ,2016 ya kuhakikisha kuwa upinzani unakufa ,ifikapo au kabla ya mwaka 2020.

Aidha Kamati hiyo imejiridhisha bila shaka ya kuwa sasa zinatengenezwa chuki za makusudi baina ya vyombo vya dola na wananchi . Hii inatokana na ukweli kuwa Amiri Jeshi Mkuu alisikika akiagiza Polisi wawe na utaratibu unaofanana na Jeshi la Wananchi. Hii ina maana kwamba Polisi lisiwe tena ni jeshi la kulinda wananchi na mali zao bali ni jeshi la kuilinda serikali .

Tumeshaona tayari Polisi wamepiga marufuku (Tamko la Advera –msemaji wa jeshi la Polisi) wananchi kwenda kuwatembelea ndugu , jamaa na marafiki wanapokuwa katika vituo vya polisi bila hata kutaja kifungu cha sheria kinachowapa mamlaka hayo.

2.0 KAMATAKAMATA NA FUNGAFUNGA YA WAPINZANI

Mara baada ya Uchaguzi Mkuu wa 2015 viongozi na wanachama wa CHADEMA wamekuwa wakikamatwa na kushtakiwa kwa makosa ya kubambikiziwa kwa kisingizio cha uchochezi na mpaka sasa kuna jumla ya wanachama na viongozi 215 ambao wamefunguliwa kesi zaidi ya 78 katika nchi nzima .Wengi wao wamenyimwa dhamana bila sababu za msingi . Na wale ambao walipatikana na hatia walipewa adhabu za vifungo bila ya kupewa fursa ya faini.

Hivi sasa umekuwa ni mtindo kwa mahakama kuwakatalia dhamana wanachama wa CHADEMA bila ya sababu za msingi.Pia imekuwa ni mtindo kuwahukumu vifungo bila kuwapa fursa ya kulipa faini.

Tumeamua na tunandaa orodha kamili itakayoainisha kesi zote za jinai ambazo ziko mahakamani na kuonyesha aina ya mashtaka na vifungo vilivyotolewa ambayo itawekwa wazi kwa vyombo vya habari na taasisi za ndani na nje ya nchi kuthibitisha kuwa kuna mpango wa kuwafunga viongozi wa upinzani kwa kusudi ili kuudhoofisha upinzani.

3.0 VITUKO VYA MKUU WA MKOA WA DAR ES SALAAM KUTANGAZA MAJINA YA WATU HADHARANI KUWA WANAHUSIKA NA DAWA ZA KULEVYA

Chama kinaunga mkono jitihada za dhati za kupambana na madawa ya kulevya nchini, kama sheria na taratibu tulizojiwekea zitafuatwa kikamilifu wakati wa mapambano hayo.

Kamati kuu inalaani kwa nguvu zote kitendo cha Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam (Paul Makonda) kutangaza majina ya watu mbele ya vyombo vya habari na kuwatuhumu kuwa ama wanahusika katika kusambaza, kuuza au kutumia madawa ya kulevya kwa lengo la kuwachafulia majina, kuwadhalilisha,kuwafedhehesha na kuwaondolea heshima yao kwa umma .Tunalaani kitendo hiki kwa sababu zifuatazo:

i. Mkuu wa Mkoa amekiuka masharti ya Katiba ibara ya 13(6) (b) na (e) ambavyo vinaweka bayana kuwa mtu hatachukuliwa kuwa ametenda kosa la jinai mpaka itakapothibitika kuwa anayo hatia ya kosa hilo na kuwa ni marufuku kwa mtu kuteswa ,kuathibiwa kinyama au kupewa adhabu zinazomtweza au kumdhalilisha

ii. Mkuu wa Mkoa amekiuka kifungu cha 54 cha Sheria ya Mwenendo wa Mashtaka ya Jinai

iii. Mkuu wa Mkoa hana mamlaka kwa mujibu wa sheria iliyotungwa na Bunge inayompa kazi na majukumu yake yaani ‘sheria ya Tawala za Mikoa ya 1997’ kuwa ana wajibu wa kutaja majina ya watu anaowatuhumu kuhusika na madawa ya kulevya .

iv. Mkuu wa Mkoa alikiuka ‘sheria ya Kuthibiti na kupambana na dawa za Kulevya,2015’ ambayo haimpi mamlaka ya kutangaza na au kuwataka watu ambao yeye anawatuhumu kujihusisha na usambazaji, uuzaji na au utumiaji wa dawa za kulevya kufika katika vituo vya Polisi .

v. Mkuu wa Mkoa alienda kinyume kabisa na mila na desturi za Kitanzania ,kuwachafulia watu majina na kuwadhalilisha mbele ya jamii huku akijua kuwa hawezi kuwasafisha na wengine ni viongozi wa dini ambao wanaaminiwa na waumini wao .

4.0 HATUA 

a. Kamati hiyo inaunga mkono hatua ya Mwenyekiti wetu Taifa Mhe.Freeman Mbowe (MB) ya kumfungulia kesi ya Kikatiba na ya Madai Paulo Makonda katika Mahakama Kuu ya Tanzania na itaungana naye katika kesi hiyo kwa kumpatia mawakili wa Chama .

b. Aidha inatoa wito kwa wale wengine wote ambao walitajwa na wanaamini kuwa walionewa,kuchafuliwa majina na au kudhalilishwa wafungue mashauri mahakamani , kwani hii ndio njia pekee ya kuzuia wengine wasifanyiwe uonevu kama huu siku zijazo.

c. Kamati hiyo inawapongeza kwa dhati kabisa wabunge wote wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kukubaliana, kuungana na kuweka itikadi za vyama vyao pembeni wakati wa mjadala wa kulinda hadhi na madaraka ya Bunge. Inatoa rai kuwa waendeleze moyo huohuo kwa siku zijazo kwa maslahi mapana ya Taifa letu.

5.0 HITIMISHO.

Kamati hiyo inatoa wito ufuatao kwa viongozi, asasi za Serikali, wananchi wazalendo na wanachama wa CHADEMA, kufanya mambo yafuatayo;

1. Viongozi wana wajibu wa kuitetea , kuilinda na kuitekeleza Katiba ya Jamhuri ya Muungano na Sheria za Nchi. Mwalimu Nyerere aliwahi kutuasa kuwa Rais asiyeweza kuilinda,kuitetea na kuihifadhi Katiba hatufai.

2. Mahakama Itekeleze wajibu wake kwa weledi uliotukuka kuhakikisha kuwa haki sio tu inatendeka bali inaonekana kutendeka bila ya vitisho kwake kutoka kwa mtu yeyote.Iige mfano wa uhuru wa mahakama na weledi wa Majaji wa Afrika ya Kusini, Zimbabwe na Marekani ambao waliweza kutengua amri batili zilizotolewa na Marais wa nchi zao.

3. Polisi na Jeshi la Wananchi wa Tanzania watekeleze majukumu yao kwa weledi kwa mujibu wa sheria na taratibu zilizowekwa.Wasikubali kuwaonea watu kwa misingi ya Vyama ,Itikadi au misimamo yao.Polisi Wajibu wao Kisheria ni kulinda usalama wa raia na mali zao , Jeshi la Wananchi wa Tanzania wajibu wao Kikatiba ni kulinda mipaka ya Nchi.

4. Mawakili wana wajibu mkubwa kuisaidia mahakama kutekeleza majukumu yake kwa weledi kuhakikisha haki inatendeka bila woga ,vitisho au vishawishi .Wasikubali kutishwa na mtu au asasi yeyote katika kuitetea ,kuilinda na kuitekeleza Katiba na Sheria za Nchi.

5. Wasomi na wanataaluma wana wajibu wa kutambua na kuitikia mwito wao wa kutetea ukweli na kulinda haki za jamii hata kama kwa kufanya hivyo kutaathiri maslahi yao binafsi

6. Wanachama tuendelee kudai demokrasia kwa nguvu zote bila woga kwa mujibu wa Katiba na sheria za Nchi.Tushikamane kukikuza Chama kuanzia ngazi ya Misingi hadi Taifa kuendelea na Operesheni UKUTA .

7. Wananchi nchi hii ni yetu sote ni lazima tufaidike nayo kwa mujibu wa Katiba na Sheria za nchi bila vitisho .Tuungane kudai demokrasia na uhuru wa kweli wa kisiasa na kiuchumi. Wasikubali kuyumbishwa na mbinu ovu kama hizi ambazo zimelenga kutupotezea lengo la kuhoji masuala ya msingi kama ufaulu hafifu wa matokeo ya Kidato cha nne Mkoa wa Dar Es Salaam, hali ya chakula nchini (njaa),zilipo milioni 50 za kila kijiji zilizoahidiwa , upatikanaji wa Tume huru ya Uchaguzi,Katiba Mpya na hali mbaya ya kiuchumi kwa wananchi .


Mwisho Kamati Ndogo ya Kamati Kuu inawashukuru watanzania wote kwa kuendelea kuunga mkono jitihada za kupambana na udikteta nchini na inawaomba waendelee kuwakumbuka kwa sala/dua viongozi mbalimbali wa Chama waliopo kwenye mateso ya kesi, mahabusu na wengine wanatumikia vifungo kutokana na kuonewa na watawala.​




……………………

Prof. Abdalah Jumbe Safari

Makamu Mwenyekiti Taifa –Bara

16 Februari, 2017

Message Sent...Hii ni Kwenu Wasichana...!!!!

$
0
0

Napata malalamiko kutoka kwenu kwamba kuna muda Boyfriend zenu hawapokei simu wala kujibu message...Mnachukua strange numbers mnabeep, wanapiga simu...mnahoji kwanini Wanafanya hivyo na
kwanini hawapokei simu zenu. Ningependa niwaambie siri...

Sometimes, Wanaume wanahitaji space..Si kila Muda ni wa mahaba tu, Baby Baby this and that 24hours zinatuboa.. Wanaume wameumbwa tofauti, they need to be alone sometimes kufanya other issues, si kwamba wewe sio muhimu, ila kuna ya muhimu zaidi...They also need time with friends...

Sasa wewe unakazana kutext,asipojibu unakazana kupiga...Utabaki kuwaza hakupendi, anakupenda sana ila humpi muda wa kupumua..Mahaba yamezidi! Too much of anything is harmful, kuwa na kiasi....Mjue mpenzi wako, Ongea nae, utajua haya ninayosema...

Otherwise utabakia kulalamika, Girls do your Homework, usiishi na mpenzi kama mfuga kuku, kuku hawaongei,wewe una mdomo...Know Your Lover(KYL), maana hata Benki wana KYC-
Know Your Customers! Ukielewa itakusaidia! Stop Complaining!

Waziri Nape Afanya Ziara ya Kushitukiza Kariakoo, Akamata Kazi Feki za Sanaa....!!!

$
0
0

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mh Nape Nnauye aongoza timu yake katika operesheni maalumu ya kufanya msako mkali wa wauzaji wa kazi za wasanii bila vibali vya Bodi ya filamu ya Tanzania.

Waziri huyo amevamia maduka yanayouza CD FEKI pamoja na ofisi ambayo inajihusisha na kurudufu kazi za wasanii kutoka ndani na nje ya nchini.

Hii ni ziara ya Pili kuifanya Kariakoo. Ziara ya kwanza ya kushitukiza aliifanya July 15, 2016 ambapo aliwataka wauzaji wa CD kote nchini kufuata sheria ya kuuza CD zenye stika huku akisema mtu yoyote ambaye atakutwa na CD ambayo haina stika mnunuaji na muuzaji wote watakamatwa. 

Operesheni hizi zinafanywa kwa lengo la kutokomeza uharamia wa bidhaa za filamu na muziki kwa kuokoa pato la TAIFA.

Amesema Seikali itawachukulia hatua za kisheria ikiweemo kuwafutia leseni wauzaji na wasambazaji wa filamu nchini ambao wamekuwa wakiuza bidhaa hizo bila vibali kutoka kutoka mamlaka husika jambo ambalo likiikosesha serikali mapato pamoja na kuchangia momonyoko wa maadili katika jamii.

Tanzia..Mchezaji Kiungo wa Yanga Godfrey Bonny Afariki Dunia...!!!

$
0
0

Kiungo wa zamani wa klabu ya Yanga na timu ya taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ Godfrey Boniface amefariki dunia alhamisi hii huko nyumbani kwao Mbeya.

Mchezaji huyo alikuwa amelazwa kwa muda mrefu hospitali ya Rungwe-Tukuyu Mbeya alikokuwa akipatiwa matibabu.

Wakati akicheza soka, Bonny aliwahi kuvitumikia vilabu vya Tanzania Prisons na Yanga kwa vipindi tofauti pamoja na timu ya taifa ya taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’.

Nay wa Mitego: Nina List ya Wasanii Wanaobebwa, Nitaitoa Muda Wowote..!!!

$
0
0

Imekua desturi ya Nay wa Mitego kuandika mistari ya utata kwenye baadhi ya ngoma zake,kitu ambacho kimejitokeza tena pia kwenye wimbo wake mpya, Muda Wetu.

Kwenye ngoma hiyo, Nay amedai kuwa kuna wasanii ambao wanabebwa kwa kupewa promo kubwa lakini promo ikikata wanabaki hawana lolote. Kwenye mahojiano na kipindi cha Supermega kupitia Kings Fm kinachoongozwa na Prince Ramalove, Nay ameweka wazi kuwa anafahamu wasanii hao na yupo tayari kuwaweka hadharani.

““Nafikiri hiyo tuwape kazi wananchi watuorodheshee ni msanii gani kwa kipindi hichi anaishi kwa upepo wa promotion na upepo ukikata tutaona reaction zake,” amesema Nay.

Amedai kuwa yeye baada ya kupata matokeo makubwa ya ngoma hiyo,ataweka wazi list ya wasanii ambao anaamini kwa asilimia zote kuwa wanabebwa na washkaji zao ambao wapo kwenye vyombo vya habari.

Viewing all 104795 articles
Browse latest View live




Latest Images