Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104809 articles
Browse latest View live

Raha ya Kufanya Mapenzi Sehemu Hatarishi zisizo Sahihi..

$
0
0
Wimbi la Watu Kufanya Mapenzi kwenye Magari hapa Mjini mchana kweupe limeongezeka kwa kasi...Hapa namaanisha kufanya mapenzi katika maeneo hatarishi na siyo mapenzi hatarishi,yan kufanyia mapenzi maeneo ambayo hayakupi utulivu wa asilimia mia,na maeneo hayo ni kama vile kufanyia mapenzi ofisini au choo cha ofisi, Beach disco,kwenye siti ya nyuma ya bus la public,vichochoroni, Kwenye Gari  nk,hivi wapendwa huwa ujasili unatoka wapi?

Na je kufanya mapenzi sehemu hizi kuna raha zaidi ya kufanya kwenye chumba? 

MWIMBAJI Rosa Ree Kutoka The Industry Aachia Video ya Wimbo wake Mpya..Icheki Hapa

$
0
0
Mwanadada ROSA REE ambaye ndio mkali wa Hip Hop hapa nchini kwa sasa ameachia kichupa kipya kinachokwenda kwa jina la UP IN THE AIR.. 


Bonyeza Play:

Atimuliwa Uchungaji Kwa Kuwapa Mimba Waumini

$
0
0
Geita. Mchungaji wa Kanisa la Ufufuo na Uzima lililopo katika Kijiji cha Bukondo, Peter Msopela amefukuzwa kazi hiyo baada ya kukiri kuwapa mimba waumini wake wawili katika kipindi cha mwaka mmoja.

Akizungumza na mwandishi wetu baada ya kikao cha ngazi za juu za kanisa hilo kilichofanyika juzi, Askofu mkuu wa kanisa hilo, Herryabwana Majebele alisema amemsimamisha kazi mchungaji huyo kwa kuwa amechafua kanisa la bwana.

Mchungaji Msopela amekiri kufanya kosa hilo na amejitetea kwamba alipitiwa na shetani, hivyo kuwataka waumini wamsamehe. Pia amemsihi Askofu Majebele asimfukuze kanisani.

Hata hivyo, Askofu Majebele alisema mchungaji huyo licha ya kulitumikia kanisa kwa kipindi cha miaka sita, kitendo alichokifanya ni kuvunja Amri 10 za Mungu.

“Kumekuwa na malalamiko mengi kutoka kwa waumini wakimtuhumu Msopela kuwabebesha mimba wanawake wawili wa kanisa lake na kuwaahidi kuwaoa. Ushahidi upo kutoka kwa waliotendewa vitendo hivyo, nimemfukuza kazi ya uchungaji ili akaendelee na starehe zake huko kwingine,” alisema Majebele.

Baada ya kumvua wadhifa huo, Askofu Majebele alisema kanisa hilo sasa litakuwa chini ya uangalizi wa Mwinjilisti Malisafi Damasi hadi pale atakapoletwa mchungaji mwingine.

Mmoja wa waumini waliopewa mimba na mchungaji huyo, Sarah Muhayiwa alisema alianza uhusiano wa kimapenzi naye tangu mwaka jana na kwamba baada ya kubeba ujauzito, alianza kumshauri asiseme jambo hilo kanisani akiahidi atamuoa.

“Baada ya hapo alinipangishia chumba mjini Katoro tangu Januari 3 lakini akanitelekeza, muda mfupi nikasikia ametangaza kumchumbia mwanamke mwingine ambaye naye alikuwa na ujauzito wake,” alisema Sarah.

Mzee wa kanisa hilo, Penina Thomas alisema mchungaji huyo amekuwa akifumaniwa mara kwa mara na hivyo anapaswa kuondolewa kwenye nafasi hiyo.

Mwinjilisti Damasi alisema kutokana na tabia hizo, waumini wengi wamekata tamaa ya kuendelea kuhudhuria ibada.

Rais Amelisikiliza Bunge Kumteua Kamishna wa Madawa ya Kulevya

$
0
0
Dar es Salaam. Mbunge wa Iringa Mjini (Chadema), Mchungaji Peter Msigwa amesema mshikamano wa wabunge ulioweka pembeni tofauti za kiitikadi unaonyesha Bunge linaweza kurejesha nguvu zake iwapo halitaingiliwa katika utendaji.

Mchungaji huyo wa Kanisa la Vineyard amesema hata uamuzi wa Rais John Magufuli kumteua Rogers Sianga kuwa Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Kupambana na Kuzuia Dawa za Kulevya umedhihirisha nguvu hiyo ya Bunge.

Msigwa alikuwa akizungumza na Mwananchi katika mahojiano maalumu jijini Dar es Salaam wiki iliyopita.

Mbunge huyo wa Iringa Mjini alisema Rais Magufuli alifanyia kazi hoja za wabunge baada ya kitendo cha Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda kutangaza majina ya watu akiwahusisha na dawa za kulevya, kulalamikiwa na wabunge.

Makonda alitangaza majina ya wasanii, wanasiasa, wafanyabiashara na viongozi wa dini akiwataka kuripoti Kituo Kikuu cha Polisi cha Dar es Salaam kwa ajili ya mahojiano kuhusu matumizi na biashara ya dawa za kulevya, jambo lililopingwa na watu wengi, na hasa wabunge.

Wakizungumza katika mkutano uliopita, wabunge walisema wanaunga mkono vita hiyo, lakini hawakubaliani na kitendo cha kutangaza watuhumiwa na wengine wakasema chombo kinachostahili kuendesha vita hiyo ni mamlaka ambayo tangu iundwe kisheria haikuwa imepata watendaji wake.

Siku chache baadaye, Rais Magufuli alimteua Sianga na watendaji wengine, ambao mara moja wakaanza utekelezaji wa majukumu yao.

Uteuzi huo umemfanya Msigwa kuamini kuwa Bunge linaweza kuwa na sauti moja lisipoingiliwa kiutendaji.

“Hakuna asiyeunga mkono vita hii lakini approach (mbinu) ya Makonda haikuwa na mamlaka kisheria na ndiyo maana Rais ametusikiliza (wabunge) na kumteua mtu atakayesimamia jambo hilo kisheria,” alisema Mchungaji Msigwa.

“Vita hii inatuhitaji wote; kuanzia kamishna, vyombo vingine vya usalama, viongozi na wananchi wote na si kwa kuitana kwa kutumia redio na televisheni, huko hatutafika zaidi ya kuishia kudhalilishana na kuchafuana,” alisema mbunge huyo machachari.

Aidha, Msigwa ambaye aliingia bungeni kwa mara ya kwanza 2010, alifananisha hatua ya Makonda na baadhi ya wakuu wa wilaya na mikoa nchini kujitwisha mamlaka ya kuwaweka mbaroni wananchi na waandishi wa habari, akisema wengi wanaendeleza chuki baada ya kuangushwa kwenye kura za maoni ndani ya CCM.

“Wengi wao ni wale walioshindwa kwenye kura za maoni ndiyo wanawaharibia sifa wabunge waliochaguliwa majimboni,” alisema

Chaguzi ndani ya Chadema
Mchungaji Msigwa pia alizungumzia chaguzi za ndani ya Chadema kwa ajili ya kusimika viongozi wa kanda, ukiwamo wa Desemba mwaka jana uliompa mbunge huyo uenyekiti wa Kanda ya Nyasa inayojumuisha mikoa ya Mbeya, Iringa, Rukwa na Songwe.

Uchaguzi huo nusura uingie dosari baada ya kamati kuu kuondoa jina la Makamu Mwenyekiti wa Baraza la Vijana wa Chadema (Bavicha), Patrick Ole Sosospi.

“Uchaguzi ulikuwa na kashikashi kwa kuwa kuna watu wako nje ya Chadema na hawakutaka nichaguliwe,” alisema Msigwa akidai kuwa hoja ya waliokuwa wakitaka asigombee ni kutokana na kuwa mbunge.

“Mbona (John) Heche ni mbunge na Mwenyekiti wa Kanda ya Serengeti? (Cecil) Mwambe ni mbunge na Mwenyekiti wa Kanda ya Kusini na (Kasuku) Bilago ni mbunge na Mwenyekiti wa Kanda ya Magharibi?.

“Katiba yetu iko wazi, Kamati Kuu ndiyo yenye mamlaka ya mwisho ya kuteua wagombea. Hata kwenye uchaguzi mkuu kuna wagombea walishinda katika kura za maoni, lakini Kamati Kuu iliwaengua.”

Msigwa alidai kuwa kuna watu hawakutaka awe mwenyekiti ili wakimalize chama Kanda ya Nyasa, lakini akasema “wana bahati mbaya”.

Msigwa alisema kuchaguliwa kwake kuongoza Kanda ya Nyasa kunalenga kuhakikisha Chadema inavuna ushindi mnono katika Uchaguzi Mkuu wa 2020.

“Tumedhamiria kuhakikisha Kanda ya Nyasa inashinda kata na majimbo mengi kuliko kanda yoyote ili kurahisha ushindi wa kiti cha urais. Hizi ni salamu kwa wote wenye nia mbaya na chama hiki,” alisema.

Utawala wa Awamu ya Tano
Kuhusu utawala wa Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais Magufuli, mbunge huyo alisema umewafanya watu kuwa na hofu, huku akidai kuwa mkuu huyo wa nchi haiamini CCM.

Msigwa alisema Serikali ya Awamu ya Tano haikubali kukosolewa.

“Mwalimu Nyerere hakujenga majengo, lakini fikra zake zinadumu mioyoni mwa watu. Utawala huu ni wa watu waoga,” alisema Msigwa. “Haujiamini na hauko tayari kukosolewa. Wamevuruga Bunge kwelikweli.”

Alikuwa akizungumzia uamuzi wa Serikali wa kutoruhusu baadhi ya shughuli za Bunge kurushwa moja kwa moja na vituo vya televisheni, kupiga marufuku mikutano ya hadhara ya kisiasa na kukamatwa mara kwa mara kwa viongozi wa upinzani.

Pia alisema Rais Magufuli haiamini CCM na ndiyo maana amefanya mabadiliko ya katiba ya chama hicho yaliyopunguza idadi ya wajumbe wa vikao vikuu na kuondoa baadhi ya nafasi za utendaji.

“Rais Magufuli haamini CCM inapigania nini na inataka nini,” alisema.

“Anafanya vitu vinavyotofautiana na Chama cha Mapinduzi. Watendaji wa chama hawaheshimiwi. Haya mabadiliko yaliyofanywa yanalalamikiwa na watendaji wa chini ambao wanatumia muda mwingi kufanya kazi za chama.

“Chama ni chambo tu, Magufuli anaamini kuna vyombo vilivyojificha chini ya CCM kuwa ndivyo vinaendesha nchi.”

Hata hivyo, Mabadiliko anayozungumzia Msigwa, yalipendekezwa na Kamati Kuu ya CCM na baadaye kupitishwa na kikao cha Halmashauri Kuu kilichofanyika Desemba 13, 2016 na sasa yanasubiri baraka za Mkutano Mkuu.

Miongoni mwa mabadiliko hayo ni kupunguza wajumbe wa Halmashauri Kuu kutoka 388 hadi 158, na wajumbe wa Kamati Kuu kutoka 34 hadi 24.

Utumishi kwa wananchi wa Iringa Mjini
Akizungumzia kipindi chake cha kuwatumikia wananchi wa Iringa Mjini, Mchungaji Msigwa alisema kazi yake ni kuhakikisha anakuwa daraja bora kati yao na Serikali.

“Ninajivunia wananchi wangu wa Iringa. Kazi kubwa tunayofanya ni kuhamasisha wananchi kutambua wajibu na haki zao. Nimelia nao na nimecheka nao katika vipindi vyote. Nimekamatwa na kuwekwa ndani lakini sijaacha kuwatumikia,” alisema Msigwa.

Alisema hivi sasa huduma ya majisafi na salama inapatikana kwa zaidi ya asilimia 90 ya wananchi wa jimbo lake.

“Tumegusa maeneo yote, huduma za afya na elimu pia zimeimarika kwa ushirikiano wa viongozi na wananchi. Bado kuna muda mrefu kutekeleza mambo mengine,” alisema Msigwa.

Kocha Msaidizi Amtaja Aliyeiangusha Yanga

$
0
0
Mara baada ya Yanga kuchezea kipigo cha mabao 2- kutoka kwa mahasimu wao Simb, Kocha Msaidizi wa Yanga Juma Mwambusi amefunguka sababu za timu yake kupoteza mchezo mojawapo ikiwa ni kuumia kwa kiungo wake Thaban Kamusoko.

Mwambusi amesema kuumia kwa Kamusoko kuliwafanya Simba waje zaidi katika eneo la katikati, jambo ambalo liliwasaidia kupitisha mipira kirahisi na hatimaye kuweza kupata mabao mawili na kuibuka na ushindi.

Amesema licha ya kumuigiza Said Makapu kuchukua nafasi ya Kamusoko, lakini hakufanya kazi ipasavyo, na pia anapungukiwa baadhi ya vitu alivyonavyo Kamusoko ikiwa ni pamoja na kuwa na maono pamoja na kuunganisha safu ya nyuma na mbele.

Sababu nyingine aliyoitaja Mwambusi ni umakini wa wachezaji wote kwenye timu yake kupungua na kushindwa kukaba, jambo lililofanya wawe wanakaba kwa macho.

"Wao Simba waliongeza namba katikati, sasa na sisi vijana wetu tuliowaingiza baada ya kamusoko kuumia walipaswa walitakiwa kuongeza namba katikati lakini wakashindwa,.... Pia umakini wa ukabaji kwa wachezaji wetu haukuwa mzuri, Simba walikuwa wanakuja wanapita watu wanawasindikiza kwa macho" - Amesema Juma Mwambusi.

Hata hivyo amesema matokeo hayo inagawa yanawaumiza, hayajawapotezea lengo lao la kutwaa ubingwa wa ligi kuu Tanzania na kwamba atakaa na walimu wenzake kurekebisha makosa ambayo yamejitokeza ili yasijirudie tena.

Katika mchezo huo, mabao ya Simba yalifungwa na Mavugo na Kichuya kipindi cha pili, huku la Yanga likifungwa na Msuva kwa njia ya penati, katika dakika ya 5

Kocha Julio Aiponda Yanga..Adai ni Kama Gari la Kubeba Maiti

$
0
0


Kocha mwenye maneno mengi ambaye hivi karibuni Jamhuri Kihwelo 'Julio' alitangaza kustaafu kufundisha mpira nchini ameibuka na kuiponda Yanga kuwa haikuwa na uwezo wa kuifunga Simba, huku akiifananisha na gari ya maiti

Julio ambaye amewahi kuichezea Simba na baadaye kuifundisha kwa nyakati tofauti, ametoa kauli hiyo mara baada ya Simba kuishushia kipigo Yanga cha mabao 2-1 katika mchezo wa ligi kuu uliopigwa katika dimba la Taifa Dar es Salaam.

Kocha huyo ambaye alitangaza kustaafu akiwa na timu ya Mwadui FC kwa madai ya kuchoshwa na waamuzi wa Tanzania, amesema ameamua kuunganisha nguvu kutoka kwa baadhi ya wachezaji wa zamani wa Simba akiwemo Zamoyoni Mogella, kuunda kundi la hamasa kwa wachezaji wa Simba ili kuhakikiksha Simba inaifunga Yanga na kuchukukua ubingwa msimu huu.

Amesema kabla na wakati wa mchezo wa jana, yeye na wenzake wamefanya kazi kubwa ya kuwatia hamasa wachezaji na hata wakati wa mapumziko, waliingia vyumbani na kuwatia hamasa wachezaji ya kupambana na ndiyo maana timu kipindi cha pili ilibadilika na kucheza kwa ari kubwa.

"Sisi kazi yetu ni kuwahamasisha wachezaji, hatumuingilii mwalimu, mwalimu anafanya kazi yake, lakini sisi tunawaambia wachezaji wanapaswa kupambana, ndiyo kazi tuliyoamua kuifanya kuelekea mchezo huu hata wakati wa mapumziko, kwa kazi tuliyofanya Yanga wasingeweza kutufunga, na mimi tangu nimeanza kufundisha mpira sijawahi kufungwa na Yanga, .. Yanga ni kama gari ya maiti, ya kwanza kuondoka, ya mwisho kurudi, ndiyo maana nasema hawa ni kama mwembe wetu wa uwani, wakati wowote tunautikisa unadodosha maembe" Amesema Julio.

Pia Julio amewapongeza makocha wa Simba kwa kazi kubwa waliyoifanya ya kuusoma mchezo na kufanya mabadiliko yenye tija, pamoja na kuwajenga wachezaji kisaikolojia, ambapo licha ya kuwa nyuma, pamoja na mchezaji wao mmoja kutolewa, walionesha kutokata tamaa

Wachawi wa Nchini Marekani Waapa Kumroga Donald Trump Atoke Madarakani

$
0
0


Wapinzani wengi wa rais wa Marekani Donald Trump, wanaamini kuwa itawabidi wasubiri kwa miaka minne ili aweze kuondoka madarakani.

Lakini wachawi nchini Marekani hawakubaliani na hilo.

Usiku wa manane siku ya Ijumaa, wale wanaoamini uchawi kote nchini Marekani, waliandaa matambiko yenye nia ya kumuondoa Trump uongozini.

Hadi sasa ukurasa wa Facebook wa matambiko huyo umepata wafuasi 10,500.

Hatua hizo zimezua ghadhabu kotoka kwa wakirsto ambao wamewalaumu wachawi hao wa kutangaza vita vya kiroho.

Wachawi hao wanapanga kurudia tambuko hilo hadi pale Trump atakapoondoka ofisini. Tambiko lingine litafanyika machi 26.

Chama cha wakiristo nacho kilitangaza tarehe 24 mwezi Februari kama siku ya maombi ya kuukabili uchawi huo.

Hata hivyo Trump hajazungumzia lolote kuhusu vita hivyo kati ya kanisa na uchawi.

Paul Makonda Adai Kuna Watu 12 Walikuwa Wamepanga Njama za Kumtupia Majini...

$
0
0

Mkuu wa mkoa wa Dar, Paul Makonda amesema katika vita ya watu wanaojihusisha na dawa za kulevya, kuna waumini 12 walikuwa wamepanga njama za kutaka kumtupia majini lakini hawajafanikiwa kutokana na maombi ya viongozi wa dini.

Amedai waumini hao waliandaa mbuzi mweupe ili kumtoa kafara na aliwatambua kupitia mtandao wake.

Makonda amesema haamini kama waliofanya hivyo walikuwa ni Waislamu, bali kundi la watu waliokuwa wamevaa kanzu kwa utambulisho huo na kwamba huenda walitumika kuwalia watu fedha zao.

Mbunge Paulina Gekul Anusurika Kifo......Alazwa ICU, Ziara Yaahirishwa

$
0
0
Mbunge wa jimbo la Babati mjini Paulina Gekul amenusurika kifo baada ya gari lake lenye namba za usajili T 189 BHQ kuacha njia na kupinduka vibaya ambapo mbunge huyo alikuwa katika msafara wa naibu waziri wa Mazingira Luhaga Mpina wilayani Babati mkoa wa Manyara.

Baada ya ajali hii kutokea mmbunge Paulina Gekul ambaye ni mmbunge wa babati mjini akakimbizwa hospitali ya mkoa wa manyara na kulazwa katika chumba cha wagonjwa mahututi I.C.U huku wanahabari wakikatazwa kuingia katika chumba hiki na madakatari ambao wanamuhudumia mbunge huyo

Hata hivyo baada ya ajali kutokea naibu waziri wa mazingira amelazimika kuahirisha ziara yake ya kutembelea maeneo mbalimbali ndani ya mji wa babati huku mpina akiipongeza halmasahauri ya mji wa babati kwa kutambua umuhimu wa kutunza mazingira katika hali ya usafi baada ya kununua gari kwaajili ya kubebea taka lenye thamani ya zaidi ya milioni 200.

Vigogo Shirika la Posta Watenguliwa Nafasi zao.....Wengine Wasimamishwa Kazi

$
0
0
Taarifa kamili ya bodi hiyo kama ilivyowasilishwa na Mwenyekiti wake, Dk. Haruni Kondo jijini Dar es Salaam jana.

  ***
Kwa kuzingatia maendeleo ya mageuzi makubwa yanayojitokeza katika sekta ya mawasiliano, Shirika la Posta Tanzania kama mtoa huduma kwa umma (Public Postal Operator), linawajibika kuhakikisha kuwa huduma za kisasa zinazozingatia vigezo vya ubora, usalama, uadilifu katika utendaji na uwajibikaji zinawafikia watu wengi zaidi katika maeneo yote ya nchi.

Kwa hivi sasa Bodi ya Wakurugenzi pamoja na Menejimenti imechukua hatua katika maeneo yafuatayo:-

1) KUPAMBANA NA UHALIFU WA MADAWA YA KULEVYA.
Shirika la Posta Tanzania limechukua hatua kadhaa ili kuhakikisha linashiriki na kuchangia kikamilifu jitihada za Serikali ya Awamu ya Tano za kupambana na uhalifu, ikiwa ni pamoja na usafirishaji, uuzaji na utumiaji wa madawa ya kulevya, usafirishaji na utakatishaji wa fedha haramu, ugaidi, udanganyifu katika utambulisho pamoja na uhalifu mwingine wa kimtandao wa Kitaifa na Kimataifa.

Bodi ya Wakurugenzi ya Shirika imedhamiria kuongeza msukumo na kasi ya usimamizi ili kupambana na uhalifu huu ambao una madhara makubwa kwa jamii.

Hatua mojawapo zilizochukuliwa na Shirika ni kusimika mfumo wa kisasa wa kudhibiti usalama na kurahisisha utambuzi wa vitu na matukio hatarishi na haramu yanayopitishwa au kujitokeza kupitia mtandao wa Shirika.

Mfumo huu uliogharimu zaidi ya shilingi milioni mia mbili (200) ambao unajumuisha ufungaji wa kamera za kiusalama (CCTV) katika Posta Kuu ya Dar es Salaam, tayari mzabuni aliyeusimika ameshakamilisha kazi yake na ataukabidhi kwa Shirika wiki ijayo na utazinduliwa rasmi wakati wowote kuanzia hapo.

Aidha, tumesimika mifumo ya kisasa ya kiusalama ikiwa ni pamoja na mashini za ukaguzi wa mizigo (baggage scanners) katika Ofisi zenye uwezekano wa kuwa uchochoro wa uhalifu wa aina hii ikiwa ni pamoja na Ofisi za Zanzibar, Kigoma, Dar es Salaam na Arusha.

Hatua hii imechukuliwa kwa kuzingatia kuwa matukio ya uhalifu uliopangwa (organized crimes) yamekuwa ni changamoto kubwa kwa Mashirika ya Posta Duniani na hivyo tumedhamiria kuhakikisha kuwa, mtandao wa Shirika wa Kitaifa sio uchochoro wa uhalifu huu.

Vitu visivyoruhusiwa kusafirishwa katika mtandao wa Posta kwa mujibu wa sheria ni pamoja na madawa ya kulevya, bidhaa za kemikali zenye sumu, silaha za moto na milipuko, wanyama hai, nyara za Serikali, vifaa vya mionzi, vyakula vinavyooza, betri za aina mbalimbali, vimiminika, fedha haramu, utakatishaji wa fedha na vitu vyovyote hatarishi.

Katazo la vitu hivi kusafirishwa katika mtandao wa Posta limezingatiwa katika sheria na taratibu mbalimbali za Kitaifa ikiwa ni pamoja na sheria ya Mawasiliano ya Elektroniki na Posta (EPOCA) ya mwaka 2010, Umoja wa Posta Duniani (UPU), Shirika la Kimataifa la Usafiri wa Anga (ICAO) na Shirika la Forodha Duniani (WCO).

Kwahiyo, Shirika la Posta Tanzania kwa kushirikiana na vyombo vingine vya usimamizi wa sheria, kwa hivi sasa limeimarisha uhakiki wa mifumo yake na pia ukaguzi wa barua, vifurushi, vipeto na mizigo ili kujiridhisha juu ya usalama na uzingatiaji wa sheria.

2)   UANZISHWAJI WA JAMII CENTRE
Hatua nyingine iliyochukuliwa ni uanzishwaji wa kituo cha kisasa cha huduma ya Jamii Centre katika Posta Kuu ya Dar es Salaam iliyoko mtaa wa Azikiwe.

Maandalizi ya Ofisi ikiwa ni kaunta za kutolea huduma, mifumo ya mawasiliano, samani kwa wateja, mafunzo ya wahudumu na vifaa vya kazi tayari vimefungwa ili vitumike na kituo kiko tayari kwa uzinduzi, wakati wowote kuanzia sasa.

Kituo kinatoa huduma jumuishi za kimtandao katika sehemu moja (One Stop Community Centre) ili kuwapunguzia wananchi usumbufu wa kufuata huduma hizo maeneo mbalimbali tofauti.

Huduma zinazotolewa kwa njia ya mtandao kwa sasa ni pamoja na:-
Malipo ya wastaafu (NSSF)
Malipo ya gawio (dividends) za makampuni mbalimbali
Malipo ya usajili wa Baraza la Mitihani
Huduma za kibenki- CRDB
Moneygram
Maxmalipo (Road lincense), Luku, Ving’amuzi n.k
Huduma mbalimbali za Posta.
Bodi imeelekeza Menejimenti kuendelea na ushawishi kwa makampuni na taasisi nyingine kama RITA, NHIF, NIDA, Mabenki n.k ili kujiunga na mfumo huu wa kisasa.  Hapo baadae zichukuliwe hatua za kufungua vituo vingine katika miji/mikoa ya Zanzibar, Dodoma, Mbeya, Mwanza, Arusha na Morogoro kabla kufikia mwisho wa 2017.

3)   USIMAMIZI WA KADA ZA UONGOZI NA RASILIMALI WATU
Baada ya Bodi kufanya tathmini yake juu ya utendaji wa Wafanyakazi wa Shirika, imeelekeza Menejimenti ichukue hatua stahiki kwa kada zote za Wafanyakazi kuanzia hapa Makao Makuu, Zanzibar, Mikoani, Wilayani hadi Vijijini.

Bodi inatambua kuwa ufanisi wa Shirika hili utatokana na utendaji wa Rasilimali watu iliyopo. Kwa hivi sasa Shirika lina Wafanyakazi wenye ajira ya kudumu wapatao 1,082 hadi kufikia Disemba 2016 lakini, baadhi yao wanafanya kazi kwa mazoea na lazima sasa wabadilike.

Menejimenti iendelee kusimamia uwajibikaji wa Viongozi na Watumishi wa kada zote ndani ya Shirika ili kujenga nidhamu ya kazi, kujituma, kuheshimu kanuni na taratibu, kuongeza ubunifu na kufanya kazi kwa ufanisi wenye tija kwa Shirika.

Bodi inatambua jitihada za Menejimenti za kuwa na mkakati wa kuimarisha usimamizi na udhibiti wa nidhamu za Wafanyakazi hususani katika kuwaongezea uwezo, kutokana na mafunzo wanayopewa kulingana na uhitaji wa soko, utii, uaminifu na hamasa katika utendaji wa kazi.

Ili kuthibitisha hilo, Wafanyakazi wanapoajiriwa wanakula viapo vya utii na kutunza siri katika utendaji kazi wao na tunapenda kuendelea kuajiri Wafanyakazi wenye uwezo na fuzu sahihi ili kuendana na mabadiliko ya soko na Wafanyakazi waendelee kupewa mafunzo ya mara kwa mara ili kuongeza ufanisi na dhana ya kumjali mteja.

Aidha, kwa wakati huu kuna mwelekeo mzuri kwani Shirika limeanza kuwapima Wafanyakazi kwa kutumia mfumo wazi wa kazi (OPRAS) kwa kuanzia mwaka huu wa fedha 2016/2017, na itakapobainika kuwa wapo Wafanyakazi ambao hawakufikia viwango vya utendaji lazima wawajibishwe.

Kwa kuzingatia yote hayo, katika kikao chake cha jana  tarehe 24/2/2017 Bodi ilipitia kwa makini utendaji, uwajibikaji na nidhamu na uwezo wa watendaji wakuu katika Shirika hilo ambao wanatakiwa kuwa mfano bora wa uongozi wa utendaji mzuri .

Imebainika na kujiridhisha kuwa baadhi ya watendaji wakuu Makao  Makuu ya Posta wamekuwa kikwazo katika dhana ya uwajibikaji, weledi, na kujituma katika kutekeleza wajibu na majukumu yao ili kulifanya Shirika la Posta kuwa mfano bora wa Mashirika yenye ubora katika kutoa huduma.

Aidha, kuna baadhi ya vitendo kwa baadhi ya watendaji vinadhihirisha tabia ya umangimeza, urasimu, kufanya kazi kwa mazoea ubadhirifu na wizi.

Bodi imeamua kufanya mabadiliko ya uongozi wa juu wa Shirika la Posta kwa kutengua nafasi za watendaji wakuu:
1)   Meneja Mkuu Menejimenti ya ya Rasilimali za Shirika Ndg. James M. Sando na kumteua Ndugu Macrice Mbodo kukaimu nafasi hiyo.
2)   Meneja Mkuu uendeshaji wa Biashara Bi. Janeth Msofe na kumteua aliyekuwa Meneja Mkoa Shinyanga Ndugu. Hassan Mwang’ombe.
3)   Imemsimamisha kazi Ndugu. Jasson Kalile aliyekuwa Meneja Msaidizi Mail and Logistic.
4)   Imemsimamisha Kazi Ndugu Ambrose John aliyekuwa Senior Motor Transport Officer.

IMETOLEWA NA:-
MWENYEKITI
BODI YA WAKURUGENZI
SHIRIKA LA POSTA TANZANIA
DAR ES SALAAM

Paul Makonda Aeleza Kilichomfanya Kutaja Majina ya Watuhumiwa wa Madawa ya Kulevya

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda amesema kuwa uamuzi wa kuwataja hadharani majina ya watuhumiwa wa biashara ya dawa za kulevya ni kutokana na maombi ya Watanzania waliyayotoa wakati wa serikali ya awamu ya nne.

Makonda alisema kuwa licha ya watu wengi kupaza sauti zao wakitaka watuhumiwa wa dawa za kulevya watajwe hadharani, lakini Rais Mstaafu, Dkt Jakaya Kikwete yeye hakuwataja huku akiacha vyombo husika vifanyekazi zao kwa usiri.

Lakini kwa upande wa serikali ya awamu ya tano, waliamua kuwataja watuhumiwa hao ikiwa ni kujibu maombi ya kile watanzania walichokitaka tangu kipindi cha nyuma, alisema Makonda jana akiwa kwenye semina ya Walimu Wanaosomesha Quran Tanzania (JUWAQUTA).

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda akizungumza katika unafunguzi semina ya Walimu wanaosomesha Qur-an Tanzania (JUWAQUTA) leo jijini Dar es Salaam.

“Mzee Jakaya mlimpigia kelele taja, taja, taja, taja, sasa tulipoingia sisi tukaona wacha tufanye kama alivyokuwa mnataka” alisema RC Makonda.

Aidha, RC Makonda amewakosoa wote walioibuka na kumdhihaki sababu alitaja majina hayo akisema kuwa giza haliwezi kuondolewa kwa giza bali ni kuwaleta waliopo gizani kwenye nuru.

“Uliona wapi giza linaondolewa kwa kutumia giza? Aliyefanya mafichoni anawekwa hadharani na harudii tena,” alisema Makonda.

Katika awamu ya tatu ya vita dhidi ya dawa za kulevya, RC Makonda hakutangaza majina hadharani kama alivyofanya katika awamu mbili zilizopita ambapo alimkabidhi majina 97, Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Kuzuia na Kupambana na Dawa za Kulevya Rogers Sianga ili ayashughulikie.

Rais Magufuli Awagomea Wazungu..Adai Wanataka Kurudisha Ukoloni

$
0
0
Na: Lilian Lundo – MAELEZO

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli na Rais wa Jamhuri ya Uganda Yoweri Museveni kwa pamoja wamekubaliana kutosaini mkataba wa mahusiano ya kiuchumi na kibiashara kati ya nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki na Ulaya (EPA).

Makubaliano hayo yamefanyika jana Ikulu, Jijini Dar es Salaam ambapo  Rais Yoweri Museveni yuko nchini Tanzania kwa ziara ya kikazi ya siku mbili kuanzia tarehe 25 – 26 Februari, 2017.

Akiongea na waandishi wa habari Rais Magufuli amesema kuwa mkataba wa EPA hauna faida bali ni aina nyingine ya ukoloni ambao unataka kurejeshwa kwa nchi za Afrika.

“Nimeongea na Rais Yoweri Museveni amekubali kutosaini mkataba wa EPA, nitawaagiza wataalamu waliosaidia kutupa maelezo juu ya madhara ya mkataba huo kwenda pia Uganda kuwapa maelezo ambao waliyatoa kwa Tanzania,” alifafanua Dkt. Magufuli.

Kwa upande wake, Rais Yoweri Museveni amesema kuwa ameongea na Rais Magufuli na wamekubaliana kutosaini mkataba huo na kuongeza kuwa suala la EPA ni lazima lijadiliwe na nchi zote za Afrika Mashariki ili kuwepo na msimamo wa pamoja kwa nchi zote za Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Aidha Rais Museveni amempongeza Rais Magufuli kwa kulifufua Shirika la Ndege Tanzania (ATCL) kwa kununua ndege mpya Sita, hivyo amekaribisha shirika hilo kutoa huduma za usafiri wa anga nchini Uganda kutokana na nchi hiyo kuwa na uhitaji wa huduma hiyo.

Vilevile amempongeza Rais Magufuli kwa ujenzi wa Reli ya Kiwango cha Kimataifa (Standard Gauge Railway) kutoka Dar es Salaa mpaka Mwanza na Isaka mpaka Rwanda ambapo itapelekea ujenzi wa bandari kavu katika mkoa wa Mwanza hivyo wafanyabiashara wa Uganda kunufaika na bandari hiyo ambayo itakuwa karibu zaidi kuliko ilivyo kwa Dar es Salaam.

Wakati huohuo Mawaziri wa Nje kutoka Tanzania na Uganda Balozi Dkt. Augustine Mahiga na Oryem Henry Okello wamesaini makubaliano ya uhusiano katika mambo ya Diplomasia baina ya nchi hizo mbili.

Museveni yupo nchini kwa ziara ya kikazi ya siku mbili ambapo atatembelea baadhi ya maeneo kadhaa ikiwemo kiwanda cha Juice cha mfanyabiashara Mtanzania Said Bakhressa ambaye pia amewekeza nchini Uganda.

Ridhiwani Kikwete Ameizungumzia Hii Picha yake na Mbowe

$
0
0
Mechi ya Yanga na Simba jana February 25 2017 ilikutanisha watu mbalimbali na hata wenye Nyadhifa za kisiasa kama Edward Lowassa, Mbunge wa Chalinze Ridhiwani Kikwete na Mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe ambao walikutana wakasalimiana.

Leo Ridhiwani Kikwete amepost picha ikimuonyesha uwanja wa taifa akionekana kumgusa Freeman Mbowe ili amsalimie ambapo kwenye caption ameandika
Kaka tusalimiane kidogo kwa afya ya Yanga”

The Industry’s Rosa Ree Tearing Up The Streets

$
0
0
The Industry’s femcee Rosa Ree is really tearing up the hip hop scene in Tanzanian rap game right now. Rosa Ree was one of the first Tanzanian artistes signed to newly-opened The Industry label run by super producer Nahreel and Aika of Navy Kenzo.

You can’t deny Rosa the credit, as in every single rap she delivers with swag and quality content, just as memorable as the likes of Nicki Minaj and Lil Kim. Rosa just released the video to her latest song “Up in the air”. Too fresh!

Her previous video and song “One Time” introduced her to the industry, establishing her as a fierce rapper and artiste, standing up for the females.

Rosa Ree has what it takes to take over East Africa and Africa as a whole. She is set for the league of G.O.A.Ts femcees . Watch closely…

Source: notjustok website

Kamanda Sirro: Nasumbuliwa Sana na Wanawake Usiku

$
0
0

Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam Kamishna Simon Sirro, amesema miongoni mwa changamoto anazokutana nazo ni pamoja kupigiwa simu za vishawishi na wanawake hasa usiku wa manane, wakidhani anapata pesa nyingi kwenye kazi yake.


Kamishna Sirro afichua siri hiyo hivi karibuni akiwa kwenye kipindi cha East Africa Breakfast, ambapo amesema pamoja na changamoto hizo, anajitahidi kukabiliana nazo kwa kuwa tayari amekwishawazoea.


Amesema kuna wanawake wengine wakiona amependeza kwenye tukio fulani, wanajua lazima atakuwa na pesa za kuwasaidia katika maisha yao hivyo wakati mwingine humpigia usiku, na yeye akidhani kuwa ni taarifa za uhalifu, lakini hukutana na vishawishi vikiambatana na sifa kedekede.


"Mwigine anaweza kukupigia simu tu usiku, kama unavyojua hawa wadada wa mjini, wakiniona wanajua niko vizuri, mwingine anakupigia anakuambia mzee tulikuona umevaa kofia vizuri, mjini kuna namna nyingi ya kuishi". Amesema Kamanda Sirro


Sirro ametaja changamoto nyingine ambazo hukutana nazo kuwa ni pamoja na suala la askari wake kulalamikiwa jambo linaloonesha dhahiri kama kiongozi ameshindwa kuwasimamia vijana anaowaongoza  na mara nyingi huwa anachukua hatua.


Lingine ni uhalifu kuzidi katika eneo fulani na hufanya wananchi kuwa na uoga, na kupoteza imani kwa jeshi la polisi jambo ambalo linamfanya yeye ajisikie vibaya zaidi kuliko hata wananchi, huku nyingine ikiwa ni viongozi wa mitaa kutowajibika katika kudhibiti uhalifu pamoja na kuletewa

Uwoya: Sikutemwa na CCM ila Kura za Rais Zilikuwa Chache

$
0
0

Msanii wa filamu nchini Irene Uwoya amefafanua sababu za kutopitishwa na chama chake cha CCM kuwa mbunge wa Viti Maalum vya wanawake, na kusema kuwa kilichomuangusha ilikuwa ni kura za Rais kuwa chache.

Uwoya alikuwa akijibu maswali ya wapenzi na mashabiki zake LIVE kupitia ukurasa wa Facebook wa EATV, ambapo swali la kwanza kabisa kuulizwa, lilihoji sababu za yeye kutemwa kwenye ubunge ndani ya CCM na kama bado ana ndoto za kuwa mbunge.


Katika majibu yake, Uwoya alisema bado ana ndoto za kuwa mbunge huku akiweka wazi kuwa yeye hakutemwa na wala hakushindwa katika kinyang'anyiro hicho isipokuwa nafasi yake kuwa mbunge ilikuwa inategemea idadi ya kura ambazo angepata aliyekuwa mgombea urais


"Niligombea kupitia upande wa vijana na nilishinda, sikushindwa wala sikutemwa, kwanza kwa mkoa wa wangu wa Tabora nilipata kura za kutosha tena nilikuwa namba moja kabisa, kwenye taifa pia nilifanikiwa kuwa kwenye majina 10 ambayo yalikuwa yanategea kura Rais, kama Rais angepata kura nyingi basi tungechukuliwa wote, lakini kwa kura alizopata Rais ilibidi wachukuliwe 6, kwahiyo mimi sikushindwa, mimi nilishinda lakini asilimia za kura za Rais ndiyo hazikutosha". Alisema Uwoya


Kuhusu nafasi ambayo angependa kuteuliwa kwa sasa katika serikali ya awamu ya tano, Uwoya amesema Mungu ndiye anayejua, na wakati ukifika anaweza kupata nafasi yoyote kwahiyo hawezi kujipangia. 

Mawaziri 13 Kikaangoni...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatatu ya February 27

$
0
0

Mawaziri 13 Kikaangoni...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatatu ya February 27

Sauti: Askofu Gwajima Aelezea Sakata Zima la Makonda Kutumia Vyeti Vya Mtu Mwingine

$
0
0

Siku moja baada ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda kusema kuwa hawezi kujibu madai ya mitandao ya kijamii kuwa alitumia vyeti vya mtu cha kidato cha nne, Askofu Gwajima wa Kanisa la Ufufuo na Uzima ameibuka na kusema kuwa ni kweli alitumia vyeti hivyo.

Askofu Gwajima amesema kuwa anamfahamu sana Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam na kuwa jina lake halisi ni Daudi Bashite na kwamba hilo la Paul Makonda ni la mwenye vyeti hivyo.

Aidha, Askofu Gwajima amedai kuwa anavyovyeti vya Daudi Bashite vinavyoonyesha kuwa hakufaulu na kwamba atashangaa kama Waziri wa Elimu, Prof. Ndalichako atalifumbia macho jambo hili. Pia ametishia kuwa, kama mamlaka husika hazitachukua hatua haraka basi yeye atatoka hadharani na vyeti hivyo.

Hapa chini ni sauti ya Askofu Gwajima akihubiri kanisani kwake.

Diamond Platnumz Apata Dili Jingine la Mamilioni

$
0
0
Mwanamuziki Diamond Platnumz amezidi kufanya vizuri katika tasnia ya muziki barani Afrika na nje ya Afrika ikiwa ni pamoja na kushirikiana na wasanii wengi wakubwa wanaozidi kumuongezea mashabiki katika mataifa mbalimbali.

Hivi karibuni Diamond alipotoa video ya wimbo wa Marry You alimshirikisha mwanamuziki Ne-Yo kutoka nchini Marekani aliuweka katika akaunti yake mpya ya Youtube ambayo ipo chini VEVO.

Diamond ni miongoni mwa wasanii wachache wa Tanzania wenye akauti ya VEVO ambapo wanalipwa kutokana na matangazo yanayowekwa wakati wa kutazama video na pia kulingana na idadi ya watazamaji.

Diamond Platnumz ameeleza kwanini alichelewa kujiunga na huduma VEVO na kwanini sasa hivi amejiunga nayo. Kupitia ukurasa wake ameandika;

Kuna siku niliulizwa kwanini we haupo Vevo… Nikawambia: “uwepo wa msanii @VEVO anatakiwa msanii alipwe zaidi ya alivyokuwa analipwa kwenye Youtube channel ya kawaida.. Vevo wenyewe pia wamtambue kuwa kuna msanii anaitwa Nasibu Abdul aka Diamond toka Tandale, na pia anacholipwa msanii wa Marekani kwa view moja ama tangazo lolote liekwalo mwanzo ama lipitalo katikati pindi ya utazamaji wa video hyo basi nae anapaswa kulipwa hivyohivyo…na mbali tu ya kumlipa VEVO yapaswa kwa namna moja au nyingine kusaidia kupromote maana ni biashara yao wote na kila msanii ana shabiki zake na ukubwa na nafasi yake atokapo”…..hivyo nikawambia: “siku mkiniona nipo vevo basi jua nimeyakamilisha haya, vinginevyo wacha niendee kuokota senti mbili tatu, kwenye chanel yangu ya Youtube kawaida….

SABABU YA KUYASEMA HAYA:
Ni kutaka kuwafahamisha ama kuwaamsha baadhi ya wasanii wenzangu watambue kuwa
Mziki wetu hata kama hauko mkubwa saaaana ulimwenguni, ila Mwenyez Mungu kausaidia kuufikisha sehem flani, hivo wasanii lazma tujitambue na Tuwe na Misimamo na kazi zetu, vilevike umakini kwenye maamuzi ama hatua yoyote tutayoichkua juu ya sanaa zetu kwa sasa, maana tuliamualo leo linaweza kutujenga ama kutubomoa baadae… nafaham wasanii wengi hawakuwa wakilifaham hilo na badala yake kuingia @VEVO kupitia watu kati ama madalali na kuambulia status mtaani kuwa wako @VEVO ilhali nyuma kuna watu wanawadhurumu mamilioni ya pesa zitokanazo na jasho lao…” kwa uchungu wa kufaham namna gani inauma msanii ukinyonywa kazi yake ndio umenifanya nilizungumze hili leo, ila ukiona kwa namna moja au nyingine nimekosea Tafadhali mnisameh…🙏 -SIMBA #MALENGO

Hussein Machozi Afunguka Mazito...Adai Watu Wake wa Karibu Wanataka Kumpora Mke Baada ya Kushuka Kisanii

$
0
0
Kwa msanii au mtu maarufu, kinga pekee inayomsaidia kuendelea kuwa na heshima yake, ni kuwa na wimbo unaofanya vizuri ama kuwa na fedha.



Anapokosa hivyo, mambo hubadilika na hapo ndipo ule usemi wa Fid Q kuwa usupastaa ni mzigo wa miiba huwa na maana. Hussein Machozi anaijua hali hiyo na kupitia mitihani aliyopitia miaka miwili iliyopita, amejifunza mengi.

“Nimejifunza kuna watu wa kweli na kuna watu feki,” Machozi ameiambia Bongo5.
“Kuna watu wa kweli ambao wamekaa na mimi kwa shida mpaka sasa hivi wapo na mimi, marafiki wa kweli. Na kuna watu baadhi ambao walikuwa wapo karibu sana na mimi kipindi nipo juu, lakini kipindi ambacho nilikuwa kimya kwa muda mrefu, wameniacha mbali wamenitupa,” anasema.

“Wamenisahau,wameninyanyasa, imefikia kipindi wengine wanatongoza mpaka mke wangu. Ni kitu ambacho kinauma sana na sio kwamba mtu anamtongoza mtu hamjui, anamtongoza anajua kabisa huyu ndio future ya Hussein Machozi, yaani ndio mtu anayemtegemea. Siwasemi wengine ni mabosi walikuwa wanajifanya mabosi na vitu kama hivyo. Lakini yote tupilia mbali, ni kwamba mimi nasonga mbele na maisha naendelea na maisha yangu, nimesahau mabaya yote, nimefungua ukurasa mpya.”

Machozi ambaye kwa sasa anaishi nchini Italia amesema amenyanyuka tena na sasa yupo tayari kurudi kwenye muziki. Anatarajia kuachia kazi yake mpya iitwayo Nipe Sikuachi.

Viewing all 104809 articles
Browse latest View live




Latest Images