Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104795 articles
Browse latest View live

Makardinali Wapanga Kumshinikiza Papa Ajiuzulu..!!!

$
0
0

Jopo la Makardinali waliompa ushirikiano mkubwa Papa Francis wa 16 wakati wa uteuzi wake, wamepanga kumshinikiza ajiuzulu kutokana na ukiukwaji wa maadili ya kanisa.

Gazeti la The Times na Libero la Italia, yameandika kuwa Makardinali hao zaidi ya dazeni, wamepanga kushinikiza Papa Francis ajiuzulu lakini bila kujitenga naye kwa namna yoyote ile. Hata hivyo haijafafanuliwa ni maadili gani aliyoyavunja Papa huyo.

Makardinali hao ndiyo waliofanya jitihada kubwa za kuteuliwa kwa Papa Francis katika uteuzi wa nafasi hiyo mwaka 2013.

Mwandishi  Antonio Socci ameandika katika gazeti la Libero na kueleza kuwa kwa sasa  Makardinali wanajadili iwapo Papa akijiuzulu nani atashika nafasi yake.

Mtaji wa Godbless Lema ni Dola...

$
0
0

Hapa Lema wala sitaki kukupamba kinafiki. Siamini hata kidogo kuwa wewe ndiye hasa unatakiwa kuwa mbunge maarufu zaidi, nikipima michango yako ndani na nje ya Bunge.

Kama ingekuwa unapimwa kwa hoja zako za ndani ya Bunge au hata nje, ungebaki kuwa mbunge wa kawaida, japo sisemi wewe huna athari bungeni. Athari unayo, tena kubwa, ila wapo ambao wanakuzidi bungeni lakini unawameza nje ya Bunge.

Lema, wewe mtaji wako ni dola. Kadiri dola inavyotumia nguvu kukudhibiti ndivyo na wewe unavyopaa kwa umaarufu. Utaendelea kuitesa na utazidi kuitumia kama ngazi ya kupaa kwako kisiasa kama haitajishitukia na kujirekebisha.

Nguvu haijawahi kuwa nyenzo bora ya mapambano kama akili haipewi ushiriki wa kutosha. Mabavu bila kushirikisha ubongo matokeo yake ni kuua mende kwa shoka kwenye marumaru. Mwisho muuaji kugeuka kichekesho.

Yapo mambo ambayo kweli hayakuwa na maana yoyote wewe kuyatamka, lakini jinsi ambavyo nguvu kubwa imetumika kukushughulikia, ndiyo inayowafanya watu kusahau makosa yako na kuishia kukuhurumia, huku wakiwafikiria watumia nguvu kwa pupa bila kupata majibu.

Kama wangekuwa wanatumia kiasi cha nguvu sawasawa na kosa husika, pengine hali isingekuwa kama ilivyo sasa. Tatizo wanaamini mno mamlaka. Hawajui kuwa mamlaka yameelekezwa kufuata sheria. Tanzania ni nchi ya utawala wa sheria.

Kufikia sasa, jina lako halizungumzwi Tanzania tu, bali ulimwengu umeambiwa mengi kuhusu msoto wako wa dhamana. Utaona kuwa jina lako linakua zaidi. Maana yake nguvu za dola zimekuwa daraja la kupaisha jina lako mpaka anga nyingine.

Ndimi Luqman MALOTO

CCM Yawaonywa Wanaochafua Wenzao Mitandaoni

$
0
0

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) visiwani Zanzibar, imetishia kuwachukulia hatua za kinidhamu viongozi na wanachama wake wanaowachafua wenzao mitandaoni.

Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho Zanzibar, Vuai Ali Vuai, alionya wakati akizungumza na viogozi, watendaji na wafuasi wa CCM wa jimbo la Malindi alipokuwa katika ziara ya kuimarisha chama.

Alisema CCM kwa sasa inaandaa utaratibu kupitia vikao vyake vya kikanuni kuwaita baadhi ya viongozi wanaotuhumiwa kuhusika na tabia hizo ili kuwahoji na kuwapa nafasi ya kujitetea.

Aidha, vikao vinavyosimamia maadili baada ya hatua hiyo vitaweza kuchukua hatua za kinidhamu kwa watakaokutwa na hatia.
Vuai alisema kuwa ndani ya chama hicho kuna tatizo kwa baadhi ya viongozi kutokuwa wa kweli na waaminifu.

Aliongeza kuwa wapo baadhi ya viongozi wamekuwa wakiwachafua viongozi wenzao kwa lengo la kuwawaharibia ili wasiweze kuendelea na nyadhifa zao.

Aidha, alionya kuwa chama kimekuwa na mwongozo katika mambo mbalimbali na kama kuna tatizo kanuni zinaelekeza kuwa linatakiwa kutatuliwa kupitia vikao.

Alieleza kuwa chama hicho kimekuwa kikitoa onyo na tahadhari za mara kwa mara ili watu wenye tabia hizo waache, lakini baadhi yao wamekuwa hawataki kubadilika, hali ambayo haiwezi kuvumiliwa.

Alikemea pia kitendo cha baadhi ya watu kutumia mitandao ya kijamii vibaya kwa kuupotosha umma.

Aliwatuhumu CUF kuwa ndiyo wanaotumia mitandao hiyo kuupotosha umma kwa lengo la kukiangusha chama na serikali iliyopo madarakani.

Aliwataka wana CCM na wananchi kutobabaika na taarifa za uongo zinazosambazwa katika mitandao ya kijamii dhidi ya CCM na Rais wa Zanzibar Dk. Ali Mohammed Shein.

“Serikali ya Zanzibar inaendelea kuongozwa na Rais wake Dk. Shein hadi mwaka 2020 utakapofanyika uchaguzi mwingine.”

Kada Chadema Mjini Moshi Alivyouawa Kinyama..!!!

$
0
0

MFANYABIASHARA wa Jiji la Dar es Salaam na kada wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) aliyewania ubunge wa viti maalumu wilayani Hai bila mafanikio katika uchaguzi mkuu uliopita, Anitha Kimario (44), ameuawa kinyama na maiti yake kukutwa kwenye shamba la miwa.

Awali, ilidaiwa kuwa Anitha alipotea katika mazingira ya kutatanisha kuanzia Jumatatu ya Februari 27 mwaka huu baada ya kuondoka nyumbani kwake Tarakea, Wilaya ya Rombo na kuaga kuwa anaelekea jijini Arusha kudai madeni yake yatokanayo na shughuli za kibiashara.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Wilbrod Mutafungwa, alithibitisha kupokea taarifa za kuokotwa kwa mwili wa mfanyabiashara huyo ukiwa umevuliwa nguo zote na kutupwa katika matuta ya kuoteshea miwa karibu na Kiwanda cha Sukari cha TPC, Wilaya ya Moshi.

“Jana (juzi) saa 11:30 jioni, tulipokea taarifa kutoka uongozi wa Kiwanda cha TPC kwamba kuna mwili wa mwanamke umekutwa kwenye matuta ya kupandia miwa. Polisi walikwenda eneo la tukio na kuukuta mwili wake ukiwa umevuliwa nguo zote na kisha kufunikwa pembeni na udongo,” Alisema.

Kwa mujibu wa Mutafungwa, mwili wa mfanyabiashara huyo na kada wa Chadema, ambaye amegunduliwa kuwa ni mkazi wa Mbezi Beach Jijini Dar es Salaam na Tarakea-Rombo mkoani, ulipatikana Machi 2 (juzi) ukiwa hauna majeraha yoyote kwa nje.

Alisema uchunguzi wa kina wa kitabibu utafanywa na madaktari wa Hospitali ya Rufaa ya KCMC kwa kushirikiana na Polisi ili kujua kiundani juu ya kile kilichotokea.

ILIVYOKUWA
Machi Mosi mwaka huu, makachero wa Polisi walilikuta gari la marehemu huyo aina ya Toyota RAV 4, lenye namba za usajili T 728 CEW, rangi nyekundu, likiwa imetelekezwa eneo la Bomambuzi, Manispaa ya Moshi, huku milango yake ikiwa imefunguliwa na funguo za gari zikiwa kwenye swichi.

Kamanda Mutafungwa alisema katika eneo la tukio, Polisi waliokota pochi ya mfanyabiashara huyo ikiwa na kadi yake ya uanachama wa Chadema, leseni ya gari, cheti cha uraia na kadi ya mpiga kura -- vyote vikimtambulisha kwa kina marehemu Anitha.

Alisema hadi sasa, mwili wa Anitha umehifadhiwa katika Hospitali ya Rufani ya KCMC na Polisi inawashikilia watu wawili kwa tuhuma za mauaji hayo. Wanahojiwa katika Kituo Kikuu cha Polisi Moshi Mjini.

Akizungumzia msiba huo, Katibu wa Chadema Mkoa wa Kilimanjaro, Basil Lema, alisema amesikitishwa mno na mauaji ya mfanyabiashara huyo ambaye ni mwanachama wao na akaliomba jeshi la Polisi kufanya uchunguzi wa kina kubaini watu waliohusika na mauaji hayo ili sheria itwae mkondo wake.

Mashoga Zanziba Wakiona cha Moto,Haya Ndiyo Yaliyowakuta Baada ya Kukamatwa..!!!

$
0
0

POLISI visiwani Zanzibar imewakamata wanaume 16 wanaodaiwa kufanya mapenzi ya jinsia moja, katika operesheni maalum inayoendelea kwenye mkoa wa Mjini Magharibi.

Akizungumza na waandishi wa habari Mkuu wa mkoa huo, Ayoub Mohammed, alisema mashoga hao waliokamatwa walipelekwa hospitali kwa ajili ya kufanyiwa uchunguzi wa kiafya na kubaini iwapo wanafanyiwa vitendo hivyo.

Alisema kati yao 11 walibainika wanajihusisha na mapenzi ya jinsi moja na tayari majalada yao yameshafikishwa kwa Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP), kwa ajili ya kushitakiwa.

Alisema kuwa watuhumiwa wengine wanaendelea kuchunguzwa na uchunguzi utakapokamilika majalada yao ripoti itaamua hatua za kuwachukulia iwapo wanapelekwa kwa DPP au wanaachiwa.

“Kazi ya kuwasaka mashoga inaendelea na tutahakikisha tunawakamata ili kutokomeza vitendo hivyo ambavyo havikubaliki kisheria, kimaadili wala kijamii,”alisema.

Aidha, alisema operesheni hiyo itawahusu pia wale wanaojifanya waume na kuwafanyia vitendo hivyo wenzao ili wakamatwe.

Aliwataka mashoga kuwataja wale wote wanaowafanyia vitendo hivyo ili wachukuliwe hatua za kisheria kwani ushoga umekuwa ukiidhalilisha jamii.

“Idadi ya matukio ya udhalilishaji hasa kwa watoto yamekuwa yakiongezeka na hivi sasa vitendo hivyo vimeshamiri kwa watoto wa kiume kulawitiwa,” alionya.

Aliitaka jamii kutoa ushirikiano na kuunga mkono juhudi hizo za kuwasaka na kuwakamata wanaojihusisha na vitendo hivyo ili kuinusuru Zanzibar na wimbi la udhalilishaji na maradhi.

Alisema kitendo hicho kimekuwa kikipoteza nguvu kazi ya taifa kutokana na vijana wengi wa kiume kujihusisha na vitendo hivyo ambayo athari zake ni magonjwa na vifo.

“Vijana ndiyo nguvu kazi ya taifa hili tukisema vitendo hivi tunavifumbia macho tutakosa nguvu kazi ya taifa,”alisema.

Aunt Ezekieli Alilia Watoto ...!!!!

$
0
0

MSANII wa filamu za Bongo, Aunt Ezekiel, amedai kwamba anatamani kupata watoto zaidi kwa kuwa huu ndio wakati wake wa kufanya hivyo na hajui atapata watoto wangapi katika maisha yake.

Aunt Ezekiel ambaye yupo kwenye uhusiano na dansa wa msanii Diamond Platnumz, Mose Iyobo, amesema kwa kuwa ndio wakati wake wa kufanya maamuzi sahihi na haoni idadi kamili ya watoto atakaokuwa nao katika familia yake na Iyobo.

“Nilitamani kuitwa mama sasa naitwa mama, naomba Mungu anisaidie nikuze familia yangu na anibariki nipate watoto wengine kwa kuwa watoto ndiyo furaha yangu zaidi,” alisema Aunt Ezekiel mwenye mtoto anayeitwa Cookie.

“Mtoto wangu wa pili natamani awe wa kiume na wengine zaidi ambao hata sijui watakua wangapi watakaokuwa na jinsia yoyote nitafurahi kwa kuwa tamaa yangu ni kuwa na watoto wengi,” alisisitiza.

Hatariii..Wolper Amvaa Kininja Harmorapa,'Amchamba' kwa Maneno Haya Mazito...!!!

$
0
0

STAA wa fi lamu za Kibongo, Jacqueline Wolper ameeleza  kukerwa na mwanamuziki chipukizi, Athuman Omary ‘Harmorapa’ aliyesema amewahi kutoka naye kimapenzi jambo ambalo siyo kweli.

Akichonga na Mikito Nusunusu Wolper alisema mwanamuziki huyo ambaye ameimba kwenye wimbo wake wa Kiboko ya Mabishoo kuwa ameshatoka naye kimapenzi amemkosea heshima  na hata alivyousikia wimbo huo umemshangaza kwa sababu hata Harmorapa mwenyewe anamuona kwenye mitandao ya kijamii na magazetini tu hajawahi kumuona ‘live’.

“Jamani huku ni kukoseana heshima maana huyo Harmorapa hata simfahamu huwa namuona kwenye mitandao na magazetini tu, sasa alivyoimba ametoka na mimi kimapenzi naona kama ni kituko kikubwa sana,” alisema Wolper.

Baada ya Kuachiwa Huru, Hii ni Sentensi ya Lema kwa Rais Magufuli...!!!

$
0
0

MBUNGE wa Arusha Mjini kwa Tiketi ya Chadema, Godbless Lema jana Machi 3, 2017 ameachiwa huru na Mahakama Kuu Kanda ya Arusha kwa dhamana ya milioni 1 huku akipewa masharti ya kuwa na wadhamini wawili wanaokidhi vigezo kwa mujibu wa sheria.

Mbunge Lema aliyesota mahabusu kwa takribani miezi minne akikabiliwa na kesi ya uchochezi, katika Gereza Kuu la Arusha lililopo Kisongo, hatimaye amepata dhamani na kupokewa kwa mbwembe na washabiki wake waliomtandikia kanga ili apite wakati akitoka mahakamani hapo.

Mara tu baada ya kuachiwa huru, Lema amesema kuwa ameandaa Walaka Maalum kwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli kuhusu mateso wanayoyapata watu waliyoko mahabusu na kwamba atautoa siku za hivi karibuni.

Baada ya Wema Sepetu Kuhamia Chadema… Hii ni Kauli ya Lulu Kujiunga na Siasa

$
0
0

ELIZABETH Michael ‘Lulu’ amefunguka kuwa anajivunia uamuzi wake wa kutojihusisha na siasa maana amepata amani ya moyo kuliko wasanii wenzake ambao kwa sasa  wapo kwenye malumbano ya kisiasa.

Mrembo huyo ambaye ni mkali wa sinema za Kibongo, alisema, wakati wa Kampeni za Uchaguzi Mkuu Mwaka 2015, watu wengi walikuwa walikuwa hawamuelewi lakini ukweli ni kwamba aliliona hili ambalo linatokea kwa sasa ambapo wasanii wanaumbuana, wanasemana na kuwagawa mashabiki.

“Unajua watu wengi walikuwa hawanielewi kwa nini sipendi siasa na ninajua wazi wengi waliniona labda mimi naringa sitaki kujumuika na wezangu lakini siyo hivyo nilijua nini kinaweza kutokea mbeleni kama ilivyo sasa,” alisema Lulu kufafanua anazungumzia malumbano yapi hasa.

Hivi karibuni, Muigizaji Wema Sepetu alitangaza kujitoa CCM na kujiunga na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) ambapo alitupa dongo  kwa CCM kwa kusema anawadai hela za kampeni hali ambayo iliwaibua wasanii wenzake, kumpinga vikali kwa maelezo kuwa walilipwa.

Za Moto Moto... Mama Wema Akamatwa na Polisi kwa Tuhuma za Utapeli...!!!!

$
0
0
\
 Msala tena! Baada ya mwanaye kukamatwa na kushtakiwa kwa tuhuma za kutumia madawa ya kulevya, kuhama chama na juzikati nyumba yake kupigwa mawe kwa muda mrefu na watu wasiojulikana, Miriam Sepetu, mama mzazi wa muigizaji Wema Sepetu, amejikuta mikononi mwa polisi, Risasi Jumamosi linakupa mchapo kamili.

Chanzo cha uhakika kimelidokeza gazeti hili kuwa mama huyo amejikuta mikononi mwa polisi baada ya kufikishwa Kituo cha Polisi Oysterbay, akidaiwa kumtapeli mfanyabiashara Alex Msama, kiasi cha fedha kinachotajwa kufikia shilingi milioni 16.

“Mama Wema alipatwa na matatizo, akataka kuuza nyumba yake ile ya Sinza Lion, sasa katika kutafuta wateja akakutana na Msama, lakini Msama akamwambia kwa wakati ule alikuwa hana hela, lakini kuna mkopo wake katika benki moja ulikuwa umeiva, hivyo avute subira kidogo angeinunua nyumba hiyo (bei haijatajwa).

“Wakakubaliana, sasa mama akamwambia Msama hata hivyo ana shida kidogo ya hela, basi jamaa akawa anampa mara leo milioni mbili, mara tatu hadi zikafika hizo 16, lakini ghafla Msama akaja kusikia ile nyumba imeshauzwa kwa mtu mwingine, alipofuatilia akakuta ni kweli, kumuuliza mama akawa haeleweki hadi jamaa akaamua kwenda polisi,” kilisema chanzo hicho.

Ili kuweka sawa mambo hayo, Risasi Jumamosi lilifika nyumbani kwa mama Wema, Sinza Mori Jumanne iliyopita, lakini lilizuiwa kuingia ndani kwa maelezo kutoka kwa mlinzi kuwa mama hakuhitaji kuonana na mtu yeyote siku hiyo. Kesho yake, alipigiwa simu yake ya mkononi na akaipokea, lakini mwandishi alipojitambulisha na kuanza kumsomea tuhuma hizo, alisema hana muda wa kuzungumzia jambo hilo kabla ya kukata simu.

Kwa upande mwingine, Risasi Jumamosi lilifika ofisini kwa Alex Msama, iliyopo Kinondoni Block 41, lakini mfanyabiashara huyo hakuwepo. Mmoja wa maofisa wa ofisi hiyo, ambaye alikataa utambulisho wake kwa kuwa siyo msemaji wa Kampuni ya Msama Promotions, alikiri kuwahi kumsainisha mama Wema kiasi cha shilingi milioni tatu. Hata hivyo, gazeti hili lilimfikia Msama kwa njia ya simu yake ya mkononi na alipoulizwa kuhusu madai hayo, alisema;

“Ni kweli nimetapeliwa na mama Wema, lakini kwa kuwa jambo hili nimeshalifikisha polisi, nadhani mkondo wa sheria utafuatwa,” alisema na kuomba asilizungumzie zaidi suala hilo. Jalada la shauri hilo limefunguliwa katika kituo cha Polisi Oysterbay kwa namba OB/RB/3358/2017.

Jitihada za RC Makonda Zimeuleta Uwanja Huu wa Soka ..!!!

$
0
0

Bila shaka kila mmoja wetu anakumbuka ahadi ya RC Makonda aliyoitoa mwaka jana ya kujenga viwanja vitatu (3) vya mpira kwa ajili ya maendeleo ya mashindano mbalimbali ya michezo ikiwemo Ndondo Cup kwani mashindano haya kwa ujumla wake yanalenga kuboresha mazingira ya michezo na kuzalisha vipaji vingi zaidi ambavyo vinabeba ajira nyingi za vijana ndani yake.

Kimsingi RC Makonda hakuishia tu kuahidi bali alikwenda mbali zaidi na kumualika Balozi wa China nchini Tanzania, Dr. Lu Youqing kushuhudia hali halisi ya viwanja vinavyotumika kwa sasa kama sehemu ushahidi wa kile alichokuwa amemueleza wakati akimshawishi.

Ikiwa imepita miezi kadhaa tangu Balozi kukubaliana na ombi la Mkuu wa Mkoa, jana Machi 3, 2017 Balozi huyo wa China akiwa na RC Makonda wameweka historia mpya baada ya kuweka jiwe la msingi la kuanza ujenzi wa viwanja hivyo, huku wakianza na kiwanja cha Bandari ambacho kitagharimu Dola za Kimarekani 450,000, huku kikijengwa kwa viwango vya kimataifa na kampuni iliyojenga uwanja wetu wa taifa.

Kuonyesha kutambua utendaji na msukumo mkubwa wa RC Makonda katika kutimiza azma ya Rais John Pombe Magufuli ya kutatua changamoto za wanyonge, Balozi pia amemuahidi Mkuu wa Mkoa kufanya yafuatayo:

1. Kuwapatia kipaumbele cha ajira vijana wote watakaoshiriki mashindano ya Ndondo Cup kwenye kampuni mbili za nchi hiyo ambazo zinatarajia kuanza shughuli zake hivi karibuni huku wakitarajia kuajiri zaidi ya vijana 24,000

2. Kuipeleka nchini China timu itakayoshinda michuano hiyo ili ikacheze mechi za kirafiki kama sehemu ya kuwaongezea ujuzi wa soka.

3. Kama haitoshi, timu ya pili na ya tatu kwenye mashindano zitapewa mualiko rasmi kwenye ubalozi wa nchi hiyo.

Kwa namna ya kipekee RC Makonda amemshukuru Balozi huyo kwa kuwa sehemu ya watu ambao wamechangia maendeleo ya jiji la Dar es Salaam na hivyo shughuli za maendeleo ambazo hazikuwepo kwenye bajeti ya serikali kuweza kufanyika pia.

Video za Taarab Zampeleka Khadija Kopa Kambini..!!!

$
0
0

Malkia wa taarabu nchini Tanzania Khadija Kopa amesema kwa sasa anajipanga ili aweze kufanya video tofauti na video za kawaida za muziki huo.

Akiongea kupitia eNewz ya EATV, Khadija amesema "Video tunazotaka kuzitengeneza ni zile za kiwango cha juu ambazo kuna wadhamini ambao watakaotudhamini ili tuweze kukaa kambini kwa siku mbili hadi tatu ili kutengeneza video zenye kiwango cha juu na zakimataifa" Amesema Khadija

Khadija Kopa pia amesema bado yuko fiti katika fani hiyo huku akitumia kauli ya "Ng'ombe hazeeki maini" na amelithibitisha hilo kwa mashabiki zake kupitia show kali aliyoipiga siku ya jana katika ukumbi wa Hisaje Park, Boko Magengeni DSM, akishirikiana na Young Killer.

Dogo Janja Amlilia Paul Makonda..!!!

$
0
0

Rapa Dogo Janja ambaye anafanya vyema na wimbo wake 'Kidebe' amefunguka na kumuomba Mkuu wa Mkoa Dar es Salaam, Paul Makonda kuanzisha kampeni nyingine ya wezi wa vipuli vya gari.

Dogo Janja anasema kutokana na namna Mkuu wa Mkoa alivyoweza kusimamia vyema suala la madawa ya kulevya anaamini kuwa kiongozi huyo anaweza kuanzisha kampeni nyingine ya wezi wa vipuli vya magari ambao wanazidi kuongezeka mjini na kuwaliza.

Dogo Janja amesema hayo baada ya wezi hao kumliza kwa kuiba vitu kwenye gari yake. 

"Mheshimiwa Makonda tunashukuru umelisimamia vizuri suala la madawa ya kulevya na tumeona matunda yake. Lakini bado kuna hili la hawa wezi wa vipuli vya magari kama taa, radio, power window, naona kama alijaongelewa hivi. Hawa jamaa wapo wengi sana mjini na wanajulikana wanakuibia halafu wanakupigia simu wapi pakuvipata vitu vyako. Mheshimiwa tuanzishe na kampeni hii tupunguze kutiana hasara..ki-gari changu chenyewe ndiyo hiki natafutia riziki jana usiku wamekuja wameiba kila kitu radio, taa za mbele na nyuma, nitatokaje kujitafutia riziki? Alihoji Dogo Janja

Hiki Hapa Kisa cha Man Fongo Kumpa Makavu Live Msaga Sumu...!!!

$
0
0

Msanii wa muziki wa singeli Bongo, Man Fongo amemjia juu msanii mwenzake wa muziki huo, Msaga Sumu na kuikosoa kauli yake ya kujiita 'Mfalme wa Kisingeli' kwamba siyo kweli, na kwamba Msaga Sumu hana sifa za kujiita 'mfalme wa singeli'

Hivi karibuni Msaga Sumu alizungumza na eNewz na kubainisha kuwa wasanii wengi wa singeli hawana ubunifu, na ndiyo sababu muziki huo unaelekea kuwa kwa kuwa wanashindwa kutoa kazi zenye utofauti, huku akijiita kuwa yeye ndiye mfalme wa singeli Tanzania.

Akionge kupitia kipindi cha eNewz cha EATV, Man Fongo amesema "Kama anasema kwamba sisi hatuna uwezo siyo kweli na kama kweli yeye ni mfalme mbona hajaachia nyimbo tangu mwaka huu uanze? Mimi nitaachia nyimbo tuone kama haita sikika. Namuona Msaga Sumu kwangu bado kabisa kwa kuwa tunaimba aina tofauti ya muziki"

Hii ni ishara kuwa huenda Man Fongo akawa anakerwa zaidi na Msaga Sumu kujiita Mfalme wa Singeli
Hata hivyo Man Fongo amewasihi wasanii wa nyimbo za singeli kupendana ili kuweza kufanya mapinduzi makubwa katika muziki na kuweza kwenda sawa na muziki wa bongo fleva

Dawa za Kulevya: Watuhumiwa 11,503 Watiwa Mbaroni..!!!

$
0
0

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa amesema jumla ya watuhumiwa 11,503 wa uzalishaji, usambazaji, uuzaji na utumiaji wa dawa za kulevya wamekamatwa kwa kipindi cha Julai mwaka jana hadi Januari mwaka huu nchini.

Akizungumza Ijumaa hii katika kikao cha Baraza la Mawaziri cha kwanza tangu Serikali kuhamia mjini Dodoma, Majaliwa amesema katika kipindi hicho kesi za kujibu zilikuwa ni 9,811 ambapo watuhumiwa 941 walikutwa na kesi za kujibu huku 238 wakiachiwa huru na kesi 478 bado zinaendelea mahakamani.

Mapema, akizungumza na waandishi wa habari wakati akifungua kikao hicho, Waziri Mkuu alisema kati ya Julai 2016 na Januari 2017, Tume ya Kudhibiti Dawa za Kulevya iliwakamata watu 11,503 ambao wanatuhumiwa kujihusisha na uzalishaji, usambazaji, uuzaji na matumizi ya dawa za kulevya.

Aidha Waziri Mkuu alisema “Wengi kati ya hao, wameshikwa na vithibitisho, ingawa uchunguzi wa kesi zao bado unaendelea. Na hawa ni wale waliokamatwa na dawa za viwandani kama heroine na cocaine. Hatujawaingiza wale waliokamatwa na mirungi au bangi. Bado mikoa inaendelea na kazi, na hii operesheni ni ya nchi nzima.”

Sakata la Askofu Gwajima na Polisi Lachukua Sura Mpya, Hiki Ndicho Kimetokea...!!!

$
0
0

Wakili Peter Kibatala amesema polisi wamepiga picha nyumbani kwa Askofu wa Kanisa la Mchungaji wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Askofu Josephat Gwajima.

Kibatala ambaye ni wakili wa Askofu Gwajima amesema jana kuwa mbali na kupekuwa na kupiga picha kila kona walikwenda katika kanisa lake lililopo Ubungo.

“Waache wafanye yao na sisi tutafanya yetu kisheria. Kwani hatuwezi kuwazuia Polisi kufanya shughuli yao na baada ya kumaliza na sisi tutajua nini cha kufanya,”amesema Kibatala.

Aidha Msemaji wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, David Mngongolwa amesema “Gwajima alikwenda jana kuripoti kama alivyoamriwa kufanya hivyo, baada ya kuripoti askari walimchukua na kwenda naye nyumbani kwake wakakaa kwa dakika zisizozidi sita na kuondoka naye.”

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi Kinondoni, Suzan Kaganda amesema hana taarifa za kukamatwa kwa Gwajima kwa maelezo kuwa alikuwa katika kikao.

Johari, Chuchu Kimenuka Tena,,,!!!!

$
0
0

Warembo wa Bongo Movies, Blandina Chagula ‘Johari’ na Chuchu Hans wamedaiwa kuwa wametibuana vibaya kufuatia Chuchu kumchokonoa Johari mitandaoni kuhusu jina la Kampuni ya RJ, Risasi Jumamosi  linakupa ubuyu kamili.

Chanzo makini kilicho karibu na wawili hao, kimeeleza kuwa, Chuchu amemchokonoa Johari kwa kutupia picha mtandaoni na kuitangaza muvi ambayo  imezalishwa na Kampuni ya RJ inayomilikiwa na mpenzi wa sasa wa Chuchu, muigizaji Vincent Kigosi ‘Ray’ na mpenzi wa zamani wa Ray, Johari kuwa Johari, Chuchu kimenuka tena! imezalishwa na kampuni mpya ya Ray na mwanaye aliyoiita Rjaden (akimaanisha Ray na mwanaye aliyezaa na Chuchu aitwaye Jaden).

“Johari alimaindi kweli baada ya kusikia Chuchu amebadilisha jina la kampuni na kuita kampuni hiyo jina la mtoto wake. Hakupendezwa na hivi ninavyokwambia wakikutana ni ama za Johari ama za Chuchu. “Johari ameanza kuona kuna mipango ya kutaka kumuondoa jina lake katika kampuni na kubadilisha kisanii jambo ambalo hawezi kukubaliana nalo maana si unajua wamechuma Ray na Johari kwa muda mrefu sana, wamepitia mambo mengi,” kilisema chanzo hicho na kuongeza:

“Huwezi amini Johari wa watu yupo nyumbani akitafakari cha kufanya maana anaona kuna mchezo anataka kuchezewa.” Hata hivyo, baada ya Chuchu kuweka posti hiyo, chanzo hicho kilieleza kuwa alishambuliwa vibaya na wafuasi wa Johari ambao hawakupendezwa na jambo hilo. “Walimtukana kweli. Waliona ana mipango mibaya. Si unajua tena mihemko ya mashabiki, ilikuwa ni kazi kwelikweli,” kilisema chanzo.

Baada ya kutonywa na chanzo ubuyu huo, Risasi Jumamosi lilimvutia waya Chuchu na kumuuliza kulikoni hadi awe chanzo cha ugomvi huo kutokana na kauli yake aliyoandika mitandaoni na kama kweli ana mpango wa kumzunguka Johari, Chuchu alijibu kwa kifupi na kukata simu. “Hamna kitu kama hicho,” alisema Chuchu.

Kwa upande wake Johari, alipoulizwa na mwanahabari wetu na kuelezwa kuwa ameingia kwenye vita mpya na Chuchu ambaye amefuta jina lake katika utambulisho wa kampuni, Johari alikiri kuiona posti hiyo. 

“Nimeiona posti hiyo mtandaoni na nikwambie tu kuhusu la kuchezewa mchezo, siwezi kukubali kufanyiwa mchezo wowote mbaya… mimi kwa sasa nipo nyumbani namuuguza mama yangu lakini nikienda ofisini na kukuta kitu cha tofauti, nitajua cha kufanya,” alisema Johari.

Wawili hao, awali waliwahi kuingia kwenye malumbano kutokana na kitendo cha Ray kutembea na Chuchu na kumuacha Johari ambaye walitoka naye mbali. Hata hivyo wawili hao wameendelea kufanya kazi pamoja kupitia kampuni yao ya RJ ambayo ipo nyumbani anapoishi Ray na mama’ke,  Sinza-Mori jijini Dar.

Kutana na Miujiza ya Shekh Sharifu Rashid Kutoka Bagamoyo..Una shida ya Mahusiano, Hela Hazikai Basi Mcheki

$
0
0

MIUJIZA YA SHEKH SHARIFU RASHID KUTOKA BAGAMOYO PWANI. (RUDISHA MAHUSIANO YAKO NDANI YA MASAA 72 TU) ASANTE KWA KUENDELEA KUMPIGIA SIMU SHEKH SHARIFU RASHID KWA WALE WENYE MATATIZO NA WALE WANAOTOA SHUKRANI: SHEKH SHARIFU RASHID ni mtaalamu wa tiba mbalimbali za asili, anatumia kitabu cha quran dawa za asili dawa za kiarabu, na njiwa, Anakuvutia mpenzi alie kuacha au alie mbali, anazo dawa za mapenzi, nguvu za kiume, chango kwa kina mama, ngiri maji na n.k, anakuvutia mali zilizo potea au kudhulumiwa, pia anatoa Pete za bahati zilizoambatanishwa na jini mali, Wenye matatizo ya uzazi, jini mahaba, mapepo ya kichawi, vifungo vya kimaisha, ndoto mbaya za usiku, uelewa mdogo wa ufahamu shuleni kwa watoto wote, pia anauwezo mkubwa wa kumaliza kazi zilizoachwa na wataalamu wengine ndani ya masaa 48 tu, Pia anatibu kwa njia ya simu popote ulipo. WASILIANA NAE KWA WhatsApp na SIMU NO: +255 718-668347 na +255 767-204308 +255 685-224047 Email shekhsharifurashidi@gmail.com.

USHAURI: ni vyema kupiga simu kuliko kutuma sms ili upate huduma kwa haraka.

Kutana na Mtoto wa Ajabu Mwenye Miaka Minne Aanyezungumza Lugha Saba za Kimataifa kwa Kiwango ch Juu

$
0
0

MTOTO mwenye umri wa miaka minne amewashangaza wengi baada ya kuzungumza kwa lugha saba kwa ufasaha katika kipindi cha televisheni nchini Urusi.

Video inamwonesha msichana huyo,  Bella Devyatkina akionesha umahiri wake kwa sasa inavuta watu kote duniani baada ya msichana huyo kuzizungumza kiufasaha lugha hizo moja baada ya nyingine.

Msichana huyo mweye kipaji alishiriki katika kipindi hicho cha televisheni cha Urusi cha 'Udivitelniye Lyudi' yaani ‘Watu wa Ajabu’ akiwashangaza majaji mjini Moscow kwa ujuzi wake huo wa lugha.

Mbali ya kufahamu vyema Kirusi, Bella pia anazungumza Kiingereza, Kijerumani, Kihispania, Kifaransa, Kichina na Kiarabu kwa ufasaha; zote hizo ni lugha zinazotambulika rasmi kwa matumizi katika Umoja wa Mataifa.

Sehemu inayoshangaza zaidi ni kwamba Bella anaweza kuzungumza kwa ufasaha katika lugha hizo, huku ujuzi wake ukizidi ule wa msamiati wa mazungumzo rahisi ya kawaida.

Wakati wa kipindi aliweza kujibu maswali yaliyohusu mtaala wa shule kwa kutumia lugha hizo zote na hata kuimba nyimbo zao.

Mama wa Bella, Yulia anaeleza kuwa alianza kumfundisha bintiye huyo lugha hizo wakati alipokuwa na umri wa miaka miwili.

Walianza kwa somo la Kiingereza, lakini baadaye aliona kuwa Bella alikuwa akifurahia somo na hivyo akaanza kuongeza lugha nyingine za kumfundisha.

Bella alifanyia kazi lugha ya Kiingereza na mama yake huku lugha nyingine akifundishwa na wazungumzaji wa asili wa lugha hizo.

Kama ilivyotarajiwa wataalamu wa lugha wameshangazwa na uwezo wa Bella kama ilivyokuwa kwa watazamanaji walioshuhudia kwa macho, kupitia televisheni au kuiona video mtandaoni.

Mtaalamu mmoja wa lugha alikaririwa akisema: “kesi kama hizi ni nadra mno lakini zimewahi kutokea huko nyuma. Lugha hujikita katika ubongo wa mwanadamu na kuendelea katika hatua tofauti za maendeleo.”

Anaamini kuwa Bella hatapoteza ujuzi wake lakini alionya kwamba wakati fulani unaweza kupotea iwapo hautafanyiwa kazi mara kwa mara kimazoezi.

Wakati akiendelea kujifunza lugha, dogo Bella anasema ndoto yake ni kuwa nguva jike kama alivyo kipenzi chake Ariel wa picha ya vibonzo za Disney– ambaye pengine ni moja ya sababu ya Bella kuwa na uwezo wa kuzungumzia kiufasaha wanyama wa baharini.

Fahamu Maajabu ya Ndizi Ambayo Huyajui..!!!

$
0
0

Ndizi ni miongoni mwa tunda lenye ladha nzuri na hupendwa na watu wengi katika nchi mbalimbali hapa ulimwenguni ikiwemo Tanzania, ndizi ina aina tatu za kipekee za sukari zinazojulikana kitaalam kama ‘sucrose’, ‘fructose’ na ‘glucose’ na vile vile ina kiasi kingi cha nyuzi yaani 'fiber' ambazo husaidia sana katika usagaji wa chakula tumboni. 

Pia tunda hili linaelezwa kuwa na uwezo mkubwa wa kuongeza na kuimarisha nishati ya mwili, ambapo pindi ulapo tunda hili unaweza kupata nishati ya kufanya kazi ya muda wa dakika 90 endapo utakuwa umekula ndizi mbili tu na kwa sifa hiyo tunaweza kusema ndizi huenda likawa tunda muhimu sana pia kwa wanamichezo. 

Hata hivyo, nishati siyo faida pekee unayoweza kuipata katika ndizi kwani pia ni tunda lenye uwezo wa kuponya na kuzuia matatizo mengine ya kiafya likiwemo suala la mfadhaiko wa akili (depression) 
Kwa mujibu wa utafiti uliofanywa na Chama cha Afya ya Akili cha Taifa (MINDI) cha nchini Uingereza kwa watu wanaosumbuliwa na tatizo la mfadhaiko wa akili, watu wengi waliondokana na tatizo hilo na kujisikia vizuri baada ya kula ndizi mbivu. Hali hii inatokana na ukweli kwamba ndizi huwa na kirutubisho kinachojulikana kama ‘tryptophan,’ ambacho ni aina fulani ya protini inayotumika mwilini kumfanya mtu kuwa mtulivu na mwenye furaha. 

Hali kadhalika, ndizi pia huwasaidia wanawake wanaopata matatizo wakati wa hedhi, hivyo endapo wewe ni miongoni mwa wale akina mama wanaopatwa na matatizo mbalimbali ya kiafya wakati wa hedhi, unashauriwa kula ndizi mbivu na unaweza kuponywa. 

Mbali na kusaidia wakina mama katika matatizo ya hedhi pia ndizi huweza kuwasaidia watu ambao husumbuliwa na tatizo la upungufu wa damu (anemia), hii ni kwasababu ndizi imekuwa ni chanzo kizuri cha madini ya aina ya chuma (iron), hivyo inaweza kuwa ni dawa ya kuzuia na kuponya tatizo la upungufu wa damu kwasababu madini ya chuma huamsha uzalishaji wa chembechembe za damu mwilini. 

Ama hakika tunda hili ni la kipekee kwani pia huweza kusaidia kukabiliana na tatizo la shinikizo la damu kwani lina kiwango kikubwa cha madini ya ‘potassium’ na wakati huo huo pia tunda hili lina kiasi kidogo cha chumvi ‘sodium’ na hivyo kulifanya kuwa tunda bora katika kupambana na tatizo la kupanda na kushuka kwa shinikizo la damu na katika kuonesha uwezo wa tunda hili juu ya kusaidia kukabilina na shinikizo la damu ni pale ambapo miaka ya hivi karibuni Mamlaka ya Dawa na Chakula ya nchini Marekani iliamua kuwaruhusu wazalishaji na wauzaji wakubwa wa ndizi nchini humo, kutangaza rasmi uwezo wa ndizi katika kupambana na hatari ya shinikizo la damu na kupatwa na kiharusi (stroke) kwa binadamu. 

Lakini mbali na hayo pia hivi karibuni wanafunzi wapatao 200 katika shule ya Twickenham nchini Uingereza, waliweza kufaulu mitihani yao kwa kula chakula cha mchana, ambapo inaelezwa kuwa ndizi ziliongeza uwezo wao wa kufikiri. Hii ni kwasababu utafiti unaonesha kuwa 'potassium' inayopatikana kwa wingi katika ndizi inaaminika kuwa na uwezo wa kumsaidia mwanafunzi kuamsha uwezo wake wa kufikiri zaidi. 

Sambamba na faida hizo za tunda hili pia inaelezwa huweza kusaidia kupunguza Kasumba yaani 'hangovers' ndizi ni moja ya dawa ya haraka ya kuondoa uchovu unaotokana na ulevi wa jana yake (hangovers) , hivyo unaweza kunywa ‘milk shake’ iliyotengenezwa kwa ndizi na kutiwa asali. Ndizi hutuliza tumbo ikisaidiwa na asali, inayorejesha kiwango cha sukari kilichopungua kwenye damu wakati maziwa nayo hutuliza na kurejesha maji kwenye mfumo wake. 

Pamoja na hayo ndizi pia husaidia katika matatizo mengi na kutuliza mishipa ya fahamu, kuondoa wasi wasi, kutuliza vidonda vya tumbo, tindikali na kushusha joto mwilini pamoja na kurekebisha mapigo ya moyo. n.k.
Viewing all 104795 articles
Browse latest View live




Latest Images