Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104795 articles
Browse latest View live

Zijue Tabia za Wanaume Wanaotumia Mitandao ya VODA/AIRTEL/TIGO na HALOTEL..!!!

$
0
0

Hii ni  maalum kwa akina dada kujua tabia za wanaume wanaotumia mitandao ifuatayo.

VODACOM

~Wanaume wa mkoa huu ndio mtandao wao mkuu. Yaani hapa huwaambii kitu kabisa
~Wanaume wengi wanaotumia voda ni bahili sana
~Unatumiwa na wanaume wengi wanaofanya biashara za kati na ndogo ndogo 
~Unapendwa sana na wanaume wa mikoa ya kaskazini

TIGO

~Ni mtandao unaotumiwa zaidi na vijana hasaa wanafunzi wa sekondari na wale wachuo
~Kama wewe ni mwanamke mchunaji mwenzangu hapa kupata vibuzi vya maana ni ngumu
~Ni mtandao unaopendwa na wanaume wa kipato cha chini 
~Wanaume wa tigo wengi ni vijana wapenda miteremko na ofa za bure

AIRTEL

~Ni mtandao unaopendwa na wanaume wa mkoa wachache hasaa wale wa mkoa wa mara na wale wanaotoka bukoba akina Rweyemamu
~Mtandao huu unapendwa sana na wanaume wasomi
~Ukipata buzi hapa umelamba dume kwani sifa ya wanaume wa mtandao huu sio bahili

HALOTEL

~Unapendwa na vijana wengi wapenda miteremko na ofa za bure
~wanaume wengi wanatumia mtandao huu huwa na macho mekundu kutokana na kukesha usiku sababu ya kupenda ofa za Data
~Ni ngumu kupata kibuzi cha maana humu

Tuandikie na Wewe Uzoefu Wako Juu ya Suala Hili...!!!

Mwanaume Epuka Kufanya Mapenzi Katika Hali na Mazingira Haya...!!!

$
0
0

Kumekuwa na wimbo wenye vilio kwa wanaume kuwa hawana nguvu za kiume huku wengne wakiishia kagoli kamoja.

Lazima ujue kuwa ngono ni kuwa na hapetaiti au ashki ikiwa apetaiti yako ipo juu basi ni rahisi kukinahiwa haraka hivyo uangalifu unahitajika.
Ashki humalizwa na mambo mbalimbali na ni vizuri kuyafahamu ili usije kumbwela juu ya kifua cha mwandani wako.

Mambo ya kuepuka wakati unataka kufanya ngono;

1. Mazingira ya joto
Pafomansi ya kufanyia kwenye chumba chenye joto huwa hairidhishi. Mwili huwahi kupata moto na kupoteza hamu haraka.

2. Usifanye mapenzi tumbo likiwa tupu.
Kama unanjaa au unamuda mrefu tokea ule labda masaa kuanzia manne kuendelea basi usijefanya mapenzi kwani ukijitahidi utapiga vibao viwili tuu vya uchovu.

Utafiti huo ni kwa hisani ya kiumeni, nikiwa yamenikuta hayo kwa zaidi ya wanawake saba tofauti tofauti nikajikuta nikiambulia fedheha.

ZIMEBAKI SIKU 4 MSHINDI KUTANGAZWA, JISAJILI SASA NAFASI NI YAKO USIFE MOYO

$
0
0
Umeshawahi Kufikiria Kupata Gari la Bure bila Kulipa Chochote, Basi hii Kampuni ya Cars From Japan Wanakupa Nafasi Hiyo na ww miliki Gari bure.

Chakufanya ni Kubofya Link hapo chini na Ufate Maelekezo ya Jinsi ya Kuweza Kuwa Mshindi wa Gari hilo, Nirahisi sana wala usihofu

Kisha Jisajili kwa Kuweka Jina na Email Yako... USIWE NA WASIWASI HUDUMA HII NI SALAMA KABISA..

Jinsi ya kujiunga:
Bofya hayo maandishi ya rangi ya blue kisha itafunguka kurasa ambayo itakuwa iko hivi.

Kisha Bofya neno APPLY NOW kisha itafunguka hivi.

Kisha utajaza Form hii kisha utaBofya neno NEXT itafunguka kurasa ingine nayo ufate maelezo yake..

Mwisho wa Kujisajili ni 20 / 3 / 2017

Diamond Platnumz na Alikiba Ndani ya Wimbo Mmoja....

$
0
0


KUELEKEA fainali ya kombe la Mataifa Afrika kwa vijana chini ya miaka 17 nchini Gabon, kamati ya hamasa kwa Serengeti Boys inayoongozwa na Mwenyekiti Charles Hilal imeandaa wimbo wa pamoja utakaoimbwa na wasanii maarufu wa muziki wa Bongo Fleva, Naseebb Abdul ‘Diamond’ na Ali  Saleh ‘King Kiba' pamoja na wasanii wengine.

Wimbo huo wa pamoja ni maalum kwa ajili ya kuhamasisha kampeni za kuchangia timu ya taifa ya vijana chini ya umri wa miaka 17, Serengeti Boys itakayofanyika mwezi wa tano nchini Gabon ambapo zitapatikana nchi nne zitakazokwenda kombe dunia la vijana nchini India.

Mwenyekiti wa kamati hiyo, Charles Hilal amesema kuwa kwa pamoja wimbo utakaowahusisha wasanii wengine mbalimbali utakuwa na lengo kuu la kuhamasisha wananchi, wadau na wapenda michezo kuichangia timu hiyo ya vijana kwa lengo la kuisaidia malengo waliyokuwa wameyafikia ya kuipeleka timu hiyo kwenye fainali za kombe la Dunia nchini India.

Hilal amesema kuwa hatua hii ya kusaidia Serengeti Boys kutawajenga vijana hawa kufanya vizuri katika michuano ya mataifa Afrika kwa vijana ikiw ani pamoja na kupata kambi nje ya nchi na kuchgeza mechi kadhaa za kirafiki kutoka nchini jirani lakini hata hivyo bado wanafikria kutafuta mechi ya kirafiki itakayochezwa hapa hapa Jijini Dar es salaam ikiwa ni kwa ajili ya kuwaaga kuelekea nchini Gabon.

Mjumbe wa Kamati ya Serengeti Boys, Maulid Kitenge amesema kwamba tayari ala za wimbo huo zimekwishatengenezwa na wasanii hao wote wametumiwa kwa ajili ya kuingiza sauti, ili mara moja wimbo huo ukamilishwe na kuanza rasmi kusaidia kampeni ya kuhamasisha Serengeti Boys.

“Tayari wasanii Ali kiba na Diamond wameshakubali kurekodi nyimo hiyona wameahidi kufanya haraka kuingiza sauti kwenye ala ambazo tumeshawatumia na baadae wasanii wengine kama Mwasiti Almasi, Darasa na Vanesa Mdee nao wataweka sauti zao,"amesema Kitenge.

Kiba na Diamond wote wapo kwenye Kamati iliyoundwa na Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Nape Nnauye ya kuhamasisha na kuwaunganisha Watanzania kwa pamoja ili kuichangia Serengeti Boys iliyofuzu Fainali za Afrika nchini Gabon Mei mwaka huu.

Katibu wa Kamati hiyo ni Mwesigwa Selestine ambaye pia ni Katibu Mkuu wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) wakati wajumbe ni Kitenge wa EFM Radio na TV, Mkurugenzi wa Mahusiano wa kampuni ya Airtel Tanzania, Beatrice Singano na Mrembo wa Tanzania wa mwaka 1999, Hoyce Temu, yumo Mkurugenzi wa Habari katika Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Hassan Abbas, Mkurugenzi wa Global Publishers Limited, Eric Shigongo na Mkurugenzi wa Radio Clouds, Ruge Mutahaba.

Pia, Serikali iliridhia kuwa mshiriki wa karibu kwa kila hatua kuanzia Bodi ya Mfuko wa Maendeleo ya timu za taifa, Kamati ya Hamasa kwa lengo la kupanga pamoja na kushirikiana kwa pamoja.

 Mwenyekiti wa kamati ya hamasa kwa Serengeti Boys , Charles Hilal akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na maendeleo ya Serengeti Boys kueleka kwnye kombe la Mataifa Afrika chini ya miaka 17 yatakayofanyika nchini Gabon. Kushoto ni Mkurugenzi wa Habari katika Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Hassan Abbas na Mkurugenzi wa Mahusiano wa kampuni ya Airtel Tanzania, Beatrice Singano

Mwenyekiti wa kamati ya hamasa kwa Serengeti Boys , Charles Hilal akiwa pamoja na Mjumbe wa Kamati ya Serengeti Boys, Maulid Kitenge wakiwasikilizisha waandishi ala za wimbo unaotarajiwa kutumika kwa ajili ya kuhamasisha kuichangia Serengeti Boys

Ni Povu tu Mtandaoni Baada ya Willy Paul Kumtembelea Diamond Ofisini Kwake...!!!

$
0
0

Changamoto kubwa aliyonayo msanii wa gospel wa Kenya, Willy Paul Msafi ni kujichanganya na wasanii wanaoimba muziki wa kidunia (secular artist).

Hata hivyo, hicho siku kitu kinachomnyima usingizi msanii huyo mwenye nguvu nchini Kenya. Na ndio maana aliamua kufanya wimbo na Mjamaica, Alaine uitwao ‘I Do’ unaotamba ile mbaya kwa sasa.

Mkali huyo ametua Tanzania wiki hii kwaajili ya ziara ya vyombo vya habari kupromote wimbo huo. Na kwakuwa yupo kwenye ardhi ya role model wake, Diamond, hakuchelewa kutua kwenye makao makuu ya WCB kusaliamiana naye.

“Now you know!!! Fruitful meeting!!! No stopping!!! @diamondplatnumz
@wasafirecords,” ameandika Willy kwenye picha akiwa na Chibu aliyoiweka kwenye Instagram.

Post hiyo imezua mjadala mzito kwenye ukurasa wake na kila shabiki ana lake, ilimradi ni tafrani tu.

Hizi ni baadhi ya comments:

Veedeevirgy: I wonder how it is fruitful! No offense but I would advice some soul searching if you have the time to, God bless

princess_mwangi: Am eagerly waiting for the day Willy will say he has shifted to secular music, you really fit in secular music, gospel is a no for me… And there is nothing like gospel love song… Also we need new ideas not duplicated from someone… Anyways I wish you all the best in your music journey.. #You are awesome when you become you

shiqouhliz: @willy.paul.msafi am just weeping for you😢😢😢. Whoever sees this is right then u belong to the world @willy.paul.msafi am not righteous ata sina right yakukujudge but brother you are losing it #truth you should convert them n not the other way round but again I understand ninyakati za mwisho n it’s written in the bible ata nikachukua microphone and shout it in your ear hutaskia only God can change your mind n heart.

suzanne_awino: Kwa Yesu hakuna warm its either ua 🔥or ❄ so its either ua in gospel or secular na hizo signs zako!!!Enwe whos me to judge but am alert!! #uafulfillingthescriptures

davispicer: Dude!..😏jst stop with ur shitty gospel songs uimbe secular mara moja😬…coz whoever ein’t seeing the signs displayed by ur hands mkiwa na Diamond must be a blinded fool..😕

museti2: This boy is not of gospel at all, it was just a matter of him hiding ndo arudi kwa vyia dunia! Get tu kwa secular

sethlunanijr: You’ve actually transfered like a footballer(one team to another)FROM gospel to secular,!

Kimenukaa..Rais Magufuli Atumbua Agizo la Waziri Mwakyembe,Adai Halitekelezeki...!!!

$
0
0

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amelifuta agizo lililotolewa jana tarehe 16 Machi, 2017 na Waziri wa Katiba na Sheria Dkt. Harrison Mwakyembe linalotoa sharti la kuwa na cheti cha kuzaliwa kwa watu wote watakaofunga ndoa kuanzia tarehe 01 Mei, 2017.

Rais Magufuli amefuta agizo hilo leo wakati akizungumza na Waandishi wa Habari muda mfupi kabla ya kuondoka katika Ikulu ya Chamwino Mkoani Dodoma na kurejea Jijini Dar es Salaam.

Dkt. Magufuli amesema Serikali haiwezi kuruhusu sharti hilo kutumika kwa kuwa litawanyima haki ya kuoa na kuolewa Watanzania wengi ambao hawana vyeti vya kuzaliwa, huku utaratibu wa kupata vyeti hivyo ukiwa bado unakabiliwa na changamoto nyingi kwa wanaohitaji.

Amesema mpaka sasa idadi ya Watanzania walio na vyeti vya kuzaliwa ni chini ya asilimia 20 huku wengi wao wakiwa ni wananchi waishio vijijini ambako ni vigumu kupata vyeti hivyo, na wengine wakiwa ni waliozaliwa kabla ya kuanza kutolewa kwa vyeti vya kuzaliwa nchini mwaka 1961.

“Kwa hiyo ndugu zangu Watanzania msiwe na wasiwasi wowote, endeleeni na utaratibu wenu wa kuoa na kuolewa kama kawaida na kama kuna kifungu chochote cha sheria kinachomlazimisha mtu awe na cheti cha kuzaliwa ndipo aoe ama aolewe nitamuelekeza Waziri wa Katiba na Sheria Harrison Mwakyembe apeleke Bungeni kikarekebishwe”-Rais Magufuli.

Rais Magufuli ametoa wito kwa wanasheria kuziangalia vizuri sheria zinazohusiana na kuzaliwa na kifo na kuoa na kuolewa ili zisilete mkanganyiko kwa wananchi. Hata hivyo Mhe. Rais Magufuli ametoa wito kwa Watanzania kuendelea kupata vyeti vyao vya kuzaliwa kama kawaida na amewataka viongozi wote kuwahamasisha wananchi kuwa na vyeti hivyo.

Lowassa Ampa 'Makavu Live' Rais Magufuli,Amataka Afute Kauli Lasivyo...!!!!

$
0
0

WAZIRI Mkuu ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema, Edward Lowassa, amemwomba Rais Dk. John Magufuli kufuta kauli yake ya kuwazuia wabunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM),  kushirikiana na wabunge wa upinzani.

Akizungumza jana katika ziara viongozi wa Chadema katika mikoa ya Pwani na Dar es Salaam, Lowassa alisema kauli hiyo Rais Dk. Magufuli inabomoa misingi ya amani iliyojengwa na waasisi wa taifa letu.

'”Namuomba Rais (Magufuli)  aondoe kauli ile aisahihishekauli hiyo na nawaomba watanzaniatukatae kugawanywa…tusikubali nchi hii ni yetu sote hakuna mtu mwenye haki miliki hapa ikienda vibaya tunaangamia wote ikienda vizuri tunafaidi wote kwahiyo tukatae,” alisema

Alisema Watanzania wamekuwa wakiishi bila ya kubaguana kwa misingi ya dini, rangi au ukabila na kukumbushia kauli iliyowahi kutolewa na baba wa taifa kuwa ubaguzi ni sawa sawa na kula nyama ya mtu, ukishakula hutotaka kuiacha.

Mjumbe wa huyo wa Kamati Kuu alisema hali ya maisha imezidi kuwa ngumu, huku bei ya bidhaa ikizidi kupanda kila siku.

Kutokana na hali hiyo alisema CCM kiliiba sera ya Chadema, ikiwemo elimu bure, lakini imeshindwa kuitekeleza.

“'waliiba sera na ilani yetu ya uchaguzi, lakini kwa kuwa hawakujiandaa wamefanya hali kuwa ngumu sana,” alisema

Katika kikao hicho cha ndani cha kuimarisha chama, Lowassa ameeleza tatizo la ajira linavyozidi kuwa kubwa na kuongeza kuwa mipango mibovu imesababisha sekta binafsi kuyumba, huku makampuni kadhaa na shughuili nyingine za kutoa ajira zikifungwa na kusababisha ongezeko kubwa la wasiyo na ajira.

Kuhusu ushirikiano miongoni mwa vyama vya upinzani, Lowassa alisema Ukawa ni muhimu kuliko wanavyoweza kudhani kwani muunganiko wa vyama vya siasa katika karne hii ni jambo la muhimu.

“Kikubwa cha kuzingatia ni umoja na mshikamano. Watanzania wana imani kubwa sana na chadema kwa sasa na kama kuna mtu anatafuta chama mbadala cha kuhamia basi ni Chadema,” alisema 

Lulu Atoa Povu Uchumba’ake Kuvunjika..!!!

$
0
0

JUZIKATI yaliibuka madai kwamba, uchumba wa staa wa filamu Bongo, Elizabeth Michael ‘Lulu’ na yule bosi wa redio Bongo umevunjika huku kila moja akiongea lake. Madai hayo yalienea kwenye mitandao ya kijamii na wapo waliokwenda mbali zaidi kudai kuwa, sasa Lulu karejea kwao na ana mpango wa kuanzisha maisha yake mengine.

“Wamemwagana, uchumba haupo tena, ila kusema ukweli inauma kuachwa na umpendaye,” aliandika mdau mmoja kwenye Mtandao wa Instagram kisha akasindikiza maneno hayo kwa picha ya Lulu na baby wake huyo.

Kufuatia madai hayo kusambaa mithili ya moto wa kifuu huku mashabiki wengi wa mastaa hao wakipiga simu kwenye chumba chetu cha habari na kutaka ufafanuzi wa habari hizo, Ijumaa lilifanya jitihada za kumtafuta Lulu kupitia simu yake lakini alipoulizwa, badala ya kutoa ufafanuzi alitoa povu kuashiria kuwa hataki habari zake ziandikwe.

“Sitaki kuongelea chochote…sitaki kuongelea chochote, pliz…unajua mimi siyo mtu wa magazeti kabisa na unanijua vizuri…” alisema Lulu na kumuacha mwandishi ameduwaa hasa kwa ile  sentensi kwamba eti yeye si mtu wa magazeti.

Ohhoo Simba Hali Si Hali..Ajibu, Mkude, Banda Waipasua Simba..!!!

$
0
0

WAKATI Simba ikiwa imesaliwa na mechi sita kabla ya kumaliza msimu wa Ligi Kuu Bara, klabu hiyo imeanza kuumiza vichwa kufuatia majembe yake matatu kugoma kusaini mkataba mpya. Majembe hayo ambayo yanategemewa katika kikosi cha kwanza, mikataba yao inafikia tamati mwishoni mwa msimu huu

ambapo kwa sasa viongozi wanahaha kuhakikisha wanawabakisha kikosini hapo kwa misimu mingine ijayo. Wachezaji hao ni Ibrahim Ajibu, Jonas Mkude na Abdi Banda ambapo imeelezwa kuwa viongozi wamepata ahueni kidogo kwa Banda ambaye kwa sasa ndiye wapo naye kwenye mazungumzo ya kumpa mkataba.

Akizungumza Ijumaa, bosi mmoja kutoka ndani ya Simba ambaye hakutaka kuweka wazi jina lake, alisema wachezaji hao pekee ndiyo mikataba yao inafikia tamati mwishoni mwa msimu huu lakini bado hawajaonyesha dalili za kuongeza. “Hadi sasa wachezaji ambao wanatarajia kumaliza mikataba yao hapa Simba ni watatu tu ambao ni Banda, Mkude na Ajibu, lakini wote waliobakia wapo vizuri kwa kuwa mikataba yao ni ya muda mrefu.

“Kwa upande wa Mkude na Ajibu wenyewe tayari walishagoma kuongeza mkataba kuendelea kubaki Simba licha ya uongozi kuwafuatilia, hivyo tumeamua kuwaacha hadi hapo mikataba yao itakapoisha na kujua nini cha kufanya, lakini Banda mazungumzo yanaendelea na huenda akaongeza mkataba mwingine,” alisema bosi huyo.

Nafasi za Kazi Halotel, Air Tanzania na Zingine Nyingi Kutoka Kwenye Makampuni Mengine

Lissu kizimbani, asomewa mashtaka matano

$
0
0


Dar es Salaam. Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu (Chadema) amesomewa mashtaka matano na Wakili wa Serikali, Faraja Nchimbi  likiwamo ya kutoa maneno  yenye nia ya kuhimiza hisia za kidini ambayo yangeweza kupelekea uhasama baina ya jamii za Watanzania.

Lissu amekana mashtaka yote na upande wa mashtaka umedai upelelezi umekamilika na wameomba wamsomee maelezo ya awali leo (Ijumaa).

Lissu  ambaye anajiwakilisha yeye mwenyewe mahakamani hapo aliomba maelezo hayo ya awali yasomwe Jumatatu, ili aweze kuhudhuria uchaguzi wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) unaotarajia kufanyika kesho.

Ameomba apewe dhamana kwa masharti nafuu.

Riyama Ally Amuwashia Moto Mwizi wa Akaunti za Mastaa Huko Instagram..!!!

$
0
0

Staa wa filamu Nchini Riyama Ally, amewafungukia na kuwashambulia wezi wa mtandaoni wanaofanya hivyo kwa kutumia akaunti za watu maarufu.

Riyama amedai wezi hao wameichukua akaunti  ya mumewe na kufuta picha zote kisha kutangaza kuiuza kwa Sh. 70,000.


Aidha Riyama ameeleza kuwa mwizi huyo ameshapatikana na watamchukulia hatua za kisheria ili liwe fundisho kwa wezi na matapeli wengine wa mtandaoni.

Muigizaji huyo mahiri wa filamu ambaye ni mama wa mtoto mmoja, yupo katika list ya wasanii wachache wa filamu waliofunga ndoa.

Sakata la Kupotea kwa Msaidizi wa Mbowe Lafikia Hatua Hii,Mapya Yaibuliwa...!!!

$
0
0

MKURUGENZI wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI), Kamishna Robert Boaz, amesema mpaka sasa ofisi yake haijafanikiwa kupata taarifa za kuisaidia kujua kilichompata Ben Saanane, Msaidizi wa Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe.

Aidha, Kamishna Boaz amesema ofisi yake imetoa taarifa kwa kutumia mfumo wa kiuchunguzi kwa Jeshi la Polisi la Kimataifa (Interpol) kumsaka mwanachama huyo wa Chadema, lakini bado halijapata mrejesho wowote.

Saanane anadaiwa kupotea katika mazingira ya kutatanisha na hajawahi kuonekana tangu Novemba mwaka jana, takribani miezi mitano sasa.

Akizungumza na Nipashe mwishoni mwa wiki kuhusu suala hilo, Kamishna Boaz alisema licha ya taarifa nyingi walizozipata kutoka kwa watu mbalimbali juu ya kupotea kwa mwanachama huyo wa Chadema, hakuna hata moja iliyotoa mwanga wa kupatikana kwake.

Alisema mpaka sasa wameshawahoji watu wote ambao kwa namna moja ama nyingine walionekana kuwa karibu na Saanane.

Kamishna Boaz alisema wamewahoji pia watu wote waliokuwa wanazungumzia suala hilo katika vyombo vya habari na majukwaa mbalimbali, lakini hakuna mafanikio yoyote waliyoyapata kwenye msako wa mwanachama huyo wa Chadema.

"Uchunguzi wa Saanane bado unaendelea, na tunachunguza taarifa zote tunazopatiwa, lakini mpaka dakika hii hatujaweza kupata taarifa nzuri ambazo zinaweza kutusaidia yuko wapi au kuna nini kimemkuta mpaka asionekane," Kamishna Boaz alisema.
"Tunaendelea kukaribisha taarifa kwa mtu yeyote ambaye anaweza kusaidia katika uchunguzi huu."

UCHUNGUZI KIMATAIFA
Kamishna Boaz alisema mbali na kuhoji vyanzo mbalimbali vya ndani ya mipaka, ofisi yake pia imeshatoa taarifa kwa kutumia mfumo wa kiuchunguzi kwa Jeshi la Polisi la Kimataifa (Interpol), lakini bado hawajapata mrejesho wowote.

"Kama mtu amepotea na taratibu zote tumeshazifanya hakuna mafanikio, tunaendelea kuwaomba watu watupe taarifa," alisema.

"Kwa mfano, tunapomtafuta mtu huwa kuna fomu maalumu tunajaza ambayo inaonyesha huyo mtu alikuwa anafananaje, anavaaje, tunaweka picha yake, anapenda kutembelea wapi, na huwa tunazisambaza katika maeneo tofauti, yote hayo tumefanya.

"Na hata Interpol huwa tunatangaza na ambacho huwa kinafanyika ni kuweka taarifa za mtu kwamba tunamtafuta ni ‘missing person’ (mtu aliyepotea).

"Kwa hiyo, inaweza kutokea kwa mfano kama ni mtu amekwenda nchi za nje kwa njia moja ama nyingine kutokana na utaalamu uliopo anaweza akapatikana.

"Taratibu zote hizo tumeshafanya, lakini mpaka sasa hatujapata mrejesho wowote."

Kwa mujibu wa Mwanasheria Mkuu wa Chadema na Mjumbe wa Kamati Kuu ya chama hicho cha siasa, Tundu Lissu, Saanane aliwasiliana kwa mara ya mwisho na Mbowe Novemba 14, mwaka jana na tangu siku hiyo, hawajawahi kupata mawasiliano yake ya simu na hajulikani aliko.

Matukio ya wanasiasa kupotea nchini ni nadra, ingawa Juni 12 mwaka jana, chama cha ACT-Wazalendo kilidai kiongozi wake mkuu, Zitto Kabwe alikuwa hajulikani alipo kwa zaidi ya saa 12.

Msafiri Mtemelwa, Kaimu Katibu Mkuu wa ACT, alidai Zitto alikuwa akitafutwa na Polisi tangu usiku wa kuamkia siku hiyo na kwamba "mpaka sasa hatujui kiongozi wetu yupo wapi na yupo kwenye hali gani. "Askari kanzu wanalinda nyumbani kwake na kwa watu wake wa karibu. Sisi kama chama tunaliambia Jeshi la Polisi kuwa lolote litakalotokea kwa kiongozi wetu wao watajibu kwa umma."

Zitto aliibuka siku mbili baadaye, hata hivyo, na kusema yuko salama wa afya huku akilaani mbinu za Jeshi la Polisi kutaka kumkamata kwa siri bila kufuata utaratibu unaotakiwa.

"Ilikuwa Jumamosi, walikuja nyumbani kwangu wakiwa na magari matatu ila hawakufanikiwa, siwezi kukamatwa kwa 'terms' (matakwa) zao," alisema Zitto, "ila nitakuwa tayari kukamatwa kwa 'terms' zetu na wala siyo kuviziana.

Kama Ningelikuwa Makonda....!!!!!

$
0
0

INAKARIBIA mwezi sasa suala la vyeti vya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam linaendelea kuzungumzwa kila kona ya nchi, kwa watoto wa mjini wanasema hivi sasa Bashite ndio habari ya mjini. Naingia kwenye mtandao wa kijamii kuangalia hili na lile nakutana na maneno yasomekayo kama “acha maneno weka vyeti acha kulialia weka vyeti” yakiambatanishwa na alama ya reli ili kuyakoleza na kuweka msisitizo.

Ama kweli Bashite ndio habari ya mjini, maana kila kona habari ni Bashite, lakini ikabidi nijiulize nini hasa kinachofanya mjadala huu uendelee kuwa gumzo kiasi hiki? Hivi mtuhumiwa mwenyewe hili halimkeri? Baada ya kulitafakari vyema nikagundua kuwa anayefanya mjadala huu uwe mrefu ni Makonda mwenyewe na si mtu mwingine yeyote. Kwa nini nasema yeye mwenyewe ndiye sababu? Hebu tuangalie mambo yafuatayo tuone nini kingefanyika kama ningelikuwa Makonda.

Kwanza kabisa isingenihitaji mimi kulia ningekuwa nacheka muda wote, kwa nini kicheko? Kwa sababu ningekuwa na vyeti visivyo na utata wowote, ingetoka wapi sababu ya mimi kulia kanisani, kwa nini nilie wakati nina uhakika kuwa mimi ni Paul Makonda  na si Daudi Bashite kama wasemavyo, yaani nilie wakati nasoma kwa kuwa nilisoma kwa shida halafu walimwengu nao waje kuniliza tena na wakati  pa kusemea nnapo na nina uhakika wa kutosha halafu nitafute sehemu niende kulia wananchi wanionee huruma kwa nini? Ningelikuwa Makonda ningekuwa nacheka tu.

Pili, ningeita vyombo vya habari huku nikiwa nina ushahidi wa kutosha, ningeanza kwa kuwaonesha cheti cha kuzaliwa, cheti cha ubatizo kama kipo, vyeti vyangu vinavyoonesha ngazi tofauti za elimu niliyopitia huku pakiwepo na walimu wangu kama ningefanikiwa kuwapata ili waje watoe ushuhuda kama mimi ndie Paul Makonda au ni Daudi Bashite na wakati wananifundisha nilikuwa natumia jina gani. Natumai baada ya kufanya hili suala ningekuwa nimekata mzizi wa fitina na ndio ungekuwa mwisho wa kuitwa  Daudi Bashite, utata ungetokea wapi kama ningemuita Mwalimu wangu Kawiche aliyenifundisha darasa la tatu pale Shule ya Msingi Minazi Mirefu au Mwalimu Mruma aliyenifundisha darasa la saba pale Shule ya Msingi Bryceson, wa sekondari je, nafikiri nisingebakisha hata wale walionifundisha chuo nao ningewaita waje kuthibitishia ulimwengu kwamba mimi si Daudi Bashite.

Tatu, kama baba na mama yangu  wako hai basi nafikiri wao ndio wangekuwa wasemaji wa mwisho, hata kama niliwahi kubadilisha jina nafikiri wao ndio wangekuwa na sababu za kutosha kwa nini nilibadilisha jina, sidhani kama wazazi wanaweza kuja kuzungumza kwenye vyombo vya habari wakaongopa hata kwenye kipindi kama hichi ambacho vyombo vya habari vinausaka ukweli wa jabo nyeti kama hili kwa gharama yeyote.

Nne, baada ya kufanya hayo yote hapo juu jambo la nne ambalo ningelifanya ni kuwaruhusu wale wote wenye ushahidi juu yangu ya kuwa nimeghushi vyeti vyangu basi waweke ushahidi hadharani na yeyote atakayenituhumu na ikabainika hana ushahidi wa kutosha basi ningemfikisha mbele ya mahakama ili anisafishe jina langu na iwe fundisho kwa wengine.

Haya ni baadhi ya mambo ambayo yangetokea kama ningelikuwa Paul Makonda lakini ikumbukwe tu kuwa haya yangetokea kama sijaghushi vyeti vipi kama ningekuwa nimeghushi je, ningekaa kimya kama alivyo kimya Mheshimiwa? Ama kweli ukitaka kuzijua shuruba za safari vaa viatu vya msafiri.

Noma Sana..Baada ya Taarifa za Kuisaidia CCM Kusambaa,Lowassa Aibuka na Jibu Hili Zito..!!!

$
0
0

Waziri Mkuu Mstaafu ambaye ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Edward Lowassa amejibu madai ya Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi, Abdallah Bulembo kuwa aliwahi kumsaidia shilingi milioni 40 za kampeni.

Bulembo ambaye pia ni Mbunge wa kuteuliwa wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, jana aliliambia gazeti la Mwananchi kuwa aliwahi kuiomba kambi ya Lowassa kiasi cha shilingi milioni 40 ili zimsaidie katika kampeni za uchaguzi wa Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi ya CCM, mwaka 2014, kiasi ambacho anadai alipewa na kambi hiyo.

“Unajua kipindi kile nagombea uenyekiti nilimfuata Lowassa nikaomba anichangie katika kampeni zangu, naye alinipa shilingi milioni 40,” Bulembo anakaririwa.

Alidai kuwa kambi hiyo iliutumia msaada huo kama fimbo wakati wa mchakato wa kumpata mgombea urais, baada ya kuona kuwa hamuungi mkono Lowassa kwani alikuwa akimuunga mkono Waziri Mkuu Mstaafu, Mizengo Pinda. Alisisitiza kuwa hakuwahi kuwa kambi ya Lowassa na kwamba baada ya kuona wanamzonga kwa kumuita msaliti, aliahidi kuuza gari zake mbili ili awarudishie kiasi hicho cha fedha alichopewa kama msaada. Lakini hakufanya hivyo.

Hata hivyo, Lowassa alikanusha vikali madai hayo ya Bulembo akiyaita upuuzi usio na ukweli wowote.

“Sio kweli,” alisema Lowassa. “Huo ni upuuzi, upuuzi mtupu,” alisisitiza katika mahojiano yake na gazeti hilo kuhusu madai ya Bulembo.

Katika hatua nyingine, Bulembo alikiri kuwa kuondoka kwa Lowassa ndani ya CCM kulizua mpasuko mkubwa katika kipindi cha uchaguzi, na kwamba kwa mara ya kwanza Wajumbe wa Halmashauri Kuu walisimama na kuimba wana imani na ‘Lowassa’ mbele ya Mwenyekiti wa chama hicho, Dkt. Jakaya Kikwete.

Bulembo alidai kuwa endapo Lowassa asingeingia Chadema na kupewa nafasi ya kugombea urais, leo hakuna ambaye angekuwa anamzungumzia na jina lake lingefutika kwenye vichwa vya watu.

Mwanasiasa huyo ambaye tayari ameshatangaza kutogombea tena nafasi ya Uenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi alimshauri Lowassa kupumzika na kuachana na siasa kwani hatakuja kufanikiwa kuwa rais.

Matokeo ya Droo ya UEFA Champions League Hatua ya Robo Fainali

$
0
0

Leicester City itakutana na klabu ya Uhispania Atletico Madrid katika robo fainali ya kombe la vilabu bingwa Ulaya.

Mabingwa hao wa ligi ya Uingereza walisonga na kuingia katika robo fainali ya mchuano huo baada ya kuishangaza miamba wa Uhispania Sevilla 3-2 kwa jumla.

Leicester itacheza awamu ya kwanza ya mechi hizo nchini Uhispania mnamo tarehe 11 ama 12 ya Aprili huku mechi ya marudiano ikichezwa kati ya tarehe 18 na 19 ya Aprili.

Mabingwa watetezi Real Madrid watakutana na Bayern huku Barcelona wakimenyana na Juventus.

Borussia Dortmund kutoka Uingereza itacheza dhidi ya Monaco.

Atletico Madrid (Spain) v Leicester City (Eng)

Borussia Dortmund (Germany) v Monaco (France)

Bayern Munich (Germany) v Real Madrid (Spain)

Juventus (Italy) v Barcelona (Spain)

Mwanamitindo afariki dunia kwa kugongwa na treni

$
0
0

Mrembo wa miaka 19 aliyefahamika kwa jina la Fredzania Thompson amegongwa na treni wakati akipiga picha.

Fredzania alikuwa ni mwanafunzi wa chuo cha Blinn na alikuwa na ndoto za kuwa mwanamitindo mkubwa duniani. Mzazi wa mrembo huyo, Akamie Stevenson ameliambia shirika la habari la CNN, “Bila shaka hilo ndio jamba ambalo alilokuwa akilitaka kulifanya katika maisha yake. Ndiyo shughuli aliyoanza kuifanya siku aliyofariki dunia.”

Hata hivyo msemaji wa polisi wa Navasota, Justin Leeth amesema mpaka sasa hawajagundua tatizo lolote juu ya kifo hicho kama kilikuwa cha hila yoyote.

Lissu aachiwa kwa dhamana ya bondi ya Sh10m

$
0
0

Dar es Salaam. Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu leo (Ijumaa) imemuachia, Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu (Chadema)  kwa dhamana ya bondi ya Sh10 milioni.

Lissu amedhaminiwa na maelezo ya awali yatasomwa Aprili3, mwaka huu.

Leo asubuhi, Lissu alisomewa mashtaka matano na Wakili wa Serikali, Faraja Nchimbi  likiwamo ya kutoa maneno  yenye nia ya kuhimiza hisia za kidini ambayo yangeweza kupelekea uhasama baina ya jamii za Watanzania.

Lissu  ambaye anajiwakilisha yeye mwenyewe mahakamani hapo aliomba maelezo hayo ya awali yasomwe Jumatatu, ili aweze kuhudhuria uchaguzi wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) unaotarajia kufanyika kesho.

Baada ya Kutupiwa Virago Yanga, Pluijm Ahama Dar na Kuhamia Singida ...!!!

$
0
0

Kocha wa zamani wa klabu ya Young Africans, ambaye ni raia wa Uholanzi Hans van Der Pluijm leo March 17 2017 ametangazwa rasmi kujiunga na club ya Singida United ya Singida, Hans anajiunga na Singida United baada ya uvumi sasa hatimaye amejiunga na timu hiyo.

Hans van Pluijm anajiunga na Singida United kwa mkataba wa miaka miwili, hiyo ni baada ya kuachana na Yanga kama utakuwa unakumbuka vizuri Hans van Pluijm ndio kocha aliyeipa Yanga mataji ya FA na Ligi Kuu msimu uliyopita sambamba na kuifikisha hatua ya makundi ya Kombe la shirikisho barani Afrika.

Baada ya Video Inayodhaniwa ni ya Mwanae Kusambaa Ikimuonyesha Akifanya Mapenzi na Jibaba,Kajala Afunguka Haya Mapya..!!!1

$
0
0

Muigizaji wa Filamu Tanzania Kajala Masanja amewafungukia wanaomsema kwamba ameshindwa kumlea binti yake ' Paula' na kusema anatamani awaoneshe watu hao malezi anayompatia binti yake huyo.

Akipiga story na eNewz, Kajala amedai kuwa hawezi kushindwa kumlea mtoto wake na kwamba malezi anayompatia binti yake ni tofauti na yale watu wanayoyazungumzia katika mitandao ya kijamii na kuongeza kuwa binti huyo analelewa katika maadili, yanayotakiwa.

"Sijashindwa kumlea mtoto wangu, natamani wangekuwa wanaona malezi ninayompatia Paula kwani kila wanachokiona na kukisikia kwenye mitandao ni tofauti sana na ninavyomlea". Kajala alisema.

Kajala ameongeza kwamba katika jambo linalomuumiza ni watu kutumia jina la binti yake hyo na kujifanya ni  yeye na wakati mwingine kuweka vitu hasi ambavyo vinamfanya mtoto wake achukuliwe tofauti katika jamii.

Aidha  muigizaji huyo ameongeza kuwa serikali inapaswa kushughulikia matatizo yanayotolewa na watumiaji wa mitandao  kwa umakini wa hali ya juu  ikiwa ni pamoja na kuweka nguvu ya kutosha.

“Ile akaunti siyo ya Paula kwanza, kwani hajawai  kuwa na simu au kumiliki, nimeshawahi  kuwaambia wamiliki wa ukurasa huo wabadilishe jina au waandike ni ‘fanpage’ lakini naona wamegoma , Baba  yake naye amejaribu kuzifunga lakini bado zinaendelea kutumika mpaka sasa nimechoka ila bado hatujajua tuchukue hatua gani". Kajala aliongeza.

Paula ambaye ni mtoto wa muigizaji huyo pamoja na Producer P- Funky Majani aliwahi kukutwa na mkasa wa kufananishwa na binti aliyerekodiwa akiwa mtupu na kusambazwa mitandaoni.
Viewing all 104795 articles
Browse latest View live




Latest Images

<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>
<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596344.js" async> </script>