Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104809 articles
Browse latest View live

Lissu Azidi Kumcharukia Magufuli, Akerwa Mtuhumiwa wa Range Rover Zilizofichwa Kwenye Makontena ya Mitumba Kusota Mahabusu Siku 23..!!!

$
0
0

RAIS wa Chama cha Wanasheria Tanganyika, Tundu Lissu, ambaye pia ni Mbunge wa Singida Mashariki, amesikitishwa na hatua ya Jeshi la Polisi – kitengo cha Bandari kuendelea kumshikilia Ramadhani Mussa Hamisi Ukwaju, bila kumfikisha mahakamani ama kumwachia kwa dhamana.

Ramadhani ndiye anayehusishwa na tukio la kusafirisha magari matatu ya kifahari aina ya Range Rover katika makontena ambayo taarifa zake zilionyesha mzigo huo ni nguo za mitumba, tukio lililofichuliwa na Rais Dk. John Magufuli alipofanya ziara ya kushtukiza katika Bandari ya Dar e s Salaam takriban wiki moja iliyopita.

Lissu ambaye pia ni Mwanasheria Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) na pia Mnadhimu Mkuu wa Kambi ya Upinzani Bungeni, aliweka bayana hayo jana, Machi 27, 2017. Kwa mujibu wa taarifa ya Lissu ambayo ‘tovuti’ hii imeinasa, Ramadhani amekuwa mahabusu kwa wiki kadhaa sasa.

“Nimetoka Polisi Bandari muda huu. Nilikwenda kumwona mtu aitwaye Ramadhani Mussa Hamisi Ukwaju ambaye yuko mahabusu ya Polisi Bandari tangu tarehe 4 ya mwezi huu. Ukwaju anatuhumiwa kuhusika na mzigo wa magari ya kifahari yaliyokamatwa na Bwana Mkubwa Rais siku chache zilizopita. Leo ni siku ya 23 yuko mahabusu. Hajapelekwa kwenye mahakama yoyote na hajashtakiwa kwa kosa lolote lile,” anaeleza Lissu

Anaendelea; “Suala lake limeshafika kwa DPP (Mwendesha Mashitaka) na kwa RPC Simon Sirro tangu siku kadhaa zilizopita lakini kila mkubwa anayehusika anaogopa kutoa maamuzi ya kumpeleka mahakamani au hata kumwachia kwa dhamana ya polisi.”

Kwa mujibu wa Lissu, hayo ndiyo madhara ya rais kuingilia majukumu ya kisheria yasiyomhusu. Anasisitiza; “Rais wetu anaweza kuwa Amiri Jeshi Mkuu lakini yeye sio askari polisi mwenye jukumu la kukamata wahalifu au kupeleleza makosa wanayotuhumiwa nayo.”

Anasema japokuwa ni Rais ndiye anayemteua DPP, lakini yeye si DPP na hana mamlaka ya kuamua nani apelekwe mahakamani na nani asipelekwe.

“Sasa inapotokea Rais anakwenda kwenye matukio ya uhalifu, kama ilivyokuwa kwenye suala la Ukwaju, anawafanya watendaji wanaohusika nayo washindwe kufanya kazi zao kwa mujibu wa sheria.

“Katika mazingira ya sasa ya 'utumbuaji majipu', watumishi wa umma wanaogopa kufanya maamuzi kwa hofu ya kutumbuliwa majipu, hasa kwa masuala ambayo yameshafikishwa kwa Rais kwa njia extra-legal kama hili la Ukwaju. Matokeo yake haki za wananchi za kuwa huru zinakiukwa bila sababu za msingi.”

“Haya ni masuala ambayo TLS chini ya uongozi wangu inatakiwa kuyashughulikia. Hii ni sehemu ya agenda tutakayompelekea Rais na IGP (Mkuu wa Jeshi la Polisi) na AG (Mwanasheria Mkuu wa Serikali) pamoja na Waziri mpya wa Katiba na Sheria, Profesa Palamagamba Kabudi tutakapoenda kuonana nao kama tulivyokwishawaomba. Kila mmoja wetu, mawakili na wasiokuwa mawakili tuyapigie kelele matumizi mabaya ya mamlaka ya kiupelelezi na ya kipolisi yanayopelekea haki za wananchi wetu kuvunjwa namna hii,” anasema Lissu na kuongeza kuwa kelele zitasaidia, ukimya ni sawa na kuyaunga mkono matendo hayo aliyoyaita mabaya.



Ukweli Mchungu...Rais Magufuli Kaitia Aibu Basata...!!!

$
0
0

MSANII Emanuel Elibariki ‘Nay Wa Mitego’ ameibua gumzo kubwa kufuatia kukamatwa kwake na kusafirishwa kutoka Turiani mkoani Morogoro hadi Kituo Kikuu cha Polisi Dar es Salaam, kwa kile kinachodaiwa kuwa maelekezo ‘kutoka juu’ kuhusiana na wimbo wake mpya, Wapo.

Jana asubuhi, Baraza la Sanaa la Taifa (Basata) chini ya Katibu wake Mkuu, Godfrey Mngereza, limetoa taarifa ya kuufungia wimbo huo, wakiukataza kutumika kwa namna yoyote hadi hapo maelezo mengine yatakapotolewa.

Basata ilitoa vifungu kadhaa vinavyoipa mamlaka ya kuchukua uamuzi huo, wakisema wimbo huo ulikosa maadili.

Mchana wa jana, Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk. Harrison Mwakyembe akizungumza na waandishi wa habari mjini Dodoma, amesema Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli ameliagiza Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam kumuachia huru Rapa Emmanue Elibariki ‘Nay wa Mitego’!

Dkt. Mwakyembe amesema kuwa Rais Magufuli ametaka Nay aachiwe huru na wimbo wake uendelee kupigwa kama ulivyo katika vyombo vyote vya habari, lakini kuna baadhi ya maneno ametaka yaongezwe endapo atataka, kama wauza madawa ya kulevya na wakwepa kodi.

Rais Magufuli ameusikiliza wimbo ule kama walivyousikiliza maofisa wa Basata na mamlaka zingine. Ameona jinsi Nay wa Mitego alivyojitosa kufikisha ujumbe wake kwa namna alivyofanya.

Kuagiza kuwa wimbo huo uendelee kupigwa na kujaribu kushauri kuongeza baadhi ya mada, ni wazi Rais Magufuli hakuona popote penye ukosefu wa maadili.

Katika hali ya kawaida, hili si jambo zuri hata kidogo, hasa kwa mamlaka kama Basata, ambao wanapaswa kuona kilichoonwa na rais tokea awali.

Ukilitazama jambo hili kwa macho mawili, unabaini kuwa mamlaka zetu hazifanyi kazi zao kwa weledi, isipokuwa kwa hisia, tena za uoga. Na huenda kuna mtu anatumia ukali wa Rais Magufuli kupenyeza ajenda kwa masilahi yake, huku akiwajengea wenzake hofu.

Jeshi la Polisi lilimkamata Ney juzi saa nane usiku na baada ya kulala ‘sentro’ kwa siku moja, Basata likaupiga marufuku wimbo wake asubuhi ya Jumatatu.

Kinachotokea ni watu, hawa walio katika mamlaka, kutekeleza majukumu yao kwa uoga na kujaribu kumtafsiri kiongozi mkuu wa nchi, badala ya kuangalia sheria walizoapa kuzisimamia zinasema nini.

Hii ni hatari, Nay amefanikiwa kutoka mikononi mwa dola kwa sababu habari zake zimemfikia rais kupitia mitandao, vipi kuhusu makumi kwa mamia ya watu wasio na umaarufu wanaotupwa selo kwa staili hii Tanzania nzima?

Iyobo ..Siachi Kunengua Ng'oo..!!!

$
0
0

MNENGUAJI wa kundi la Wasafi Classic (WCB), Moses Iyobo, amesema hajawahi kufikiria kuwa mwimbaji kwakuwa ni kazi inayohitaji kutumia akili nyingi tofauti na unenguaji.

Iyobo ambaye amejizolea umaarufu mkubwa kutokana na aina yake ya uchezaji, amesema ataendelea kubaki kuwa mnenguaji katika maisha yake yote sambamba na kuwa mwalimu kwa wenzake.

Alisema kazi ya kuimba inahitaji akili nyingi ili kufikia malengo hivyo ataendelea kubaki na kazi yake ya unenguaji.

“Nitabaki kuwa dansa maisha yangu yote, labda nitakachoongeza hapo ni kuwa mwalimu na kuwafundisha wengine, unajua kuimba kunahitaji akili nyingi ili ufanikiwe. Sasa kwa upande wangu sitaweza ni bora nibaki huku huku ndio pananifaa zaidi,” alisema Iyobo ambaye ni mpenzi wa msanii Aunt Ezekiel.

Rasmi..Okwi Athibitiha Kuwa Anatua Simba Msimu Ujao,Atoa Kauli Hii kwa Yanga..!!!

$
0
0

AMA kweli Emmanuel Okwi amenogewa na Simba, kwani licha ya uongozi wa Wekundu hao wa Msimbazi kuweka wazi kuwa atarejea msimu ujao, taarifa kutoka Uganda zinadai kuwa, hata yeye mwenyewe ameonyesha mapenzi ya kurejea kwenye timu yake hiyo ya zamani.

Okwi, ambaye alikuwa akikipiga nchini Denmark katika Klabu ya SonderjyskE, kwa sasa anaichezea SC Villa ya nchini kwao Uganda na anafanya mambo makubwa, hali iliyomfanya kuitwa kwa mara nyingine katika kikosi cha timu ya Taifa ya nchi hiyo.

Miongoni mwa marafiki wa Okwi kutoka nchini Uganda, amesema kuwa, mchezaji huyo anasubiri tu kumalizika msimu huu arejee Tanzania kujiunga na Simba, baada ya viongozi wa timu hiyo kuonyesha nia ya kumhitaji.

“Hata yeye mwenyewe anaipenda Simba, kwa sasa baada ya kusikia kuwa viongozi pamoja na mashabiki wanataka arejee, anajiandaa kumalizia msimu huu na kuna kila dalili wakamalizana mapema,” alisema rafiki huyo wa karibu.

Kwa upande wake, Kocha wa zamani wa Simba, ambaye kwa sasa ni kocha msaidizi wa timu ya Taifa ya Uganda, Mosses Basena, alisema kuwa, Okwi amekuwa akionyesha kiwango kizuri kila siku, hivyo kama Simba atamrejesha watakuwa wamelamba dume.

Mapema Makamu wa Rais wa Simba, Geofrey Nyange ‘Kaburu’, aliliambia gazeti hili kuwa, suala la Okwi wala halina mjadala mkubwa, kwani yeye kwa klabu hiyo ni kama nyumbani, hivyo anakaribishwa muda wowote.

KUTANA na Mtabibu Ostadhi Khamisi Kutoka Mombasa Kenya Kwasasa Yupo Tanzania Kwa Ajili yako

$
0
0



Kutana na ostadhi khamisi kutoka mombasa Kenya kwa sasa yupo Tanzania ni mtabibu na mtafiti Wadawa za asili anatibia kama vile:
Miguu kuuma
Miguu kufagazi
Miguu kuwakamoto
Chango lauzazi kwakina mama
Dawa ya uzazi wakina mama inapatikana
Kusafisha nyota ili uwe namuonekano kwa kila mtu
Kumrudisha mpenzi wako na liekukimbia ndani yasiku 3 bila yapingamizi yoyote
Kumshika mume au mke asitoke nnje ya ndoa
Pata pete ya Bahati inayo endana na nyota yako
Kurudisha mali ilipotea au kudhurumiwa ndani yasiku 3
Pata utajili usiokuwa namashaliti yoyote
Dawa za nguvu za kiume
Dawa ya biashara inapatikana
Dawa ya kuzuia chuma ulete kwenye biashara inapatikana
 Zindiko la nyumba au shamba
 Anatuliza familia zinazogombana DUWA pamoja navisomo vya ufunguzi wa mwili wako njoo ufunguliwe vifungo ulivyo fungwa kutana na ostadhi khamisi utimiziwe ahadi ulizo hadiwa acha kuteseka acha kuhangaika ostadh khamisi yupupo tanzania kwajili yako...

Call +255718746825 +255754765246 kwa what'sapp +255783708487

Jipatie WATER DISPENSER Kwa Bei Nafuu Kabisa

$
0
0

*OFA KABAMBE..DONT MISS IT..*

Sasa Kwa bei Nafuu Kabisa unajipatia *WATER DISPENSER*,Kwa matumizi ya OFISINI NA NYUMBANI, Upate Maji BARIDI na MOTO.

Tunakuletea Oda yako kwa Wakati na Mikoani tunatuma Oda zenu pia.

Tunatoa DHAMANA ya Mwaka 1.

BEI 195000/= TU HAINA FRIJI.

BEI 290000/= INA FRIJI CHINI

CALL/WHAT'SUP. 0743757575

BIDHA ZINGINE TUFATE INSTAGRAM PAGE YETU.

👇🏽👇🏽👇🏽

@beinafuu_shop
@beinafuu_shop
@beinafuu_shop
@beinafuu_shop

BREAKING: Maalim Avuliwa Ukatibu Mkuu CUF

$
0
0


Baraza Kuu la Uongozi Taifa la Chama cha Wananchi(CUF) leo limemvua Maalim Seif nafasi ya Ukatibu Mkuu na kumpa Magdalena Sakaya.

Taarifa ya hatua hiyo imetangazwa Mapema leo na Prof Ibrahim Lipumba


Habari zaidi itakujia hivi punde...

Asasi 30 Afrika zalaani uvamizi Clouds

$
0
0

Dar es Salaam. Asasi za kiraia 33 barani Afrika zimelaani kitendo cha kuvamiwa kwa studio za televisheni ya Clouds na kulazimisha maudhui yasiyostahili yarushwe hewani.

Tamko la asasi hizo limetolewa ikiwa ni siku chache baada ya Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora, (THBUB), Jukwaa la Wahariri (TEF) na Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) kulaani kitendo hicho kinachodaiwa kukandamiza uhuru wa vyombo vya habari.

Asasi hizo zinazohusika na utawala bora, demokrasia, haki za binadamu na uhuru wa habari zilikutana hivi karibuni mjini Kampala nchini Uganda katika mkutano uliokuwa ukizungumzia uhuru wa kujieleza na kupata habari.

Tanzania kwenye mkutano huo iliwakilishwa na Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu (THRDC) , miongoni mwa mijadala iliyotawala ni kukemea vitisho na vitendo vya kunyanyasa waandishi.

Pia, wajumbe katika mkutano huo waligusia mabadiliko madogo ya baraza la mawaziri yaliyofanywa na Rais John Magufuli kwa kumtoa Nape Nnauye kwenye nafasi ya Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo.

Asasi hizo zilimpongeza Nape ambaye kabla ya kuondolewa kwenye nafasi hiyo aliunda kamati iliyochunguza tukio la uvamizi wa studio za Clouds, wakisema uamuzi huo ulionyesha ujasiri wa kusimamia uhuru wa vyombo vya habari na uhuru wa kujieleza.

Taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa na asasi hizo, ilidai kwa siku za karibuni Tanzania imekuwa na matukio zaidi ya 40 yanayolenga kukandamiza uhuru wa vyombo vya habari.

“Waandishi wamekuwa wakizuiwa au wakati mwingine kubughudhiwa ili wasifanye kazi yao. Vitendo hivyo vimekuwa vikifanywa hasa na wakuu wa wilaya na polisi,” ilibainisha taarifa hiyo.

Wajumbe walikumbusha kifungu cha pili cha Azimio la kanuni za uhuru wa kujieleza Afrika la mwaka 2002, kinachoelekeza Serikali ihakikishe inachukua hatua stahiki kuzuia uvamizi kwenye vyombo vya habari.

Kifungu hicho kinaelezea endapo uvamizi huo utatokea, Serikali ina wajibu wa kuchunguza na kuwaadhibu wahusika kwa mujibu wa kosa lao.

Kimenukaa..Rais wa Malawi Atangaza Vita na Tanzania Kuhusu Ziwa Malawi,Kumbe Alimdanganya Rais Magufuli Walipokutana Ethiopia..!!!

$
0
0

Rais wa Malawi, Peter Mutharika ameanza tena chokochoko baada ya kutangaza kuwa hakuna nchi ambayo inamiliki kwa pamoja Ziwa Nyasa na kwamba haijafikia makubaliano na nchi yoyote, hivyo ameahidi kulinda umiliki na masilahi yake.

Kauli hiyo ni tofauti na mazungumzo ya Mutharika na Rais John Magufuli yaliyofanyika Januari 30 jijini Addis Ababa, Ethiopia wakati walipokuwa wakihudhuria kikao cha Umoja wa Afrika (AU).

Katika taarifa iliyotolewa na Idara ya Mawasiliano ya Rais baada ya kikao hicho, ilisema marais wote wameridhishwa na jitihada zinazofanywa na jopo la usuluhishi lililoteuliwa na Umoja wa Maendeleo wa Nchi za Kusini mwa Afrika (Sadc).

Jopo hilo linaongozwa na rais wa zamani wa Msumbiji, Joachim Chisano.

Mwananchi ilimtafuta Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dk Augustine Mahiga ili kujua msimamo wa Tanzania lakini hakupatikana na simu ya Naibu Waziri Dk Susan Kolimba iliita bila majibu.

Mkuu wa kitengo cha mawasiliano katika wizara hiyo Mindi Kasiga alikiri kuiona taarifa hiyo ila alisema anayeweza kulizungumzia suala hilo ni Naibu Waziri.

“Tumeiona hiyo taarifa ila jaribu kumtafuta Naibu Waziri maana Waziri atakuwa nje ya nchi. Ninachofahamu baraza la usuluhishi bado linaendelea na vikao vyake. Ukimpata naibu waziri atakuwa na maelezo ya kina.”alisema Mindi.

Lakini, akihudhuria Siku ya Maji Duniani Jumatano iliyopita mjini Mangoshi, Rais Mutharika alisisitiza msimamo wa Malawi kulinda umiliki wa ziwa hilo dhidi ya watu aliowaita wavamizi.

Mutharika alisema Malawi ndiye mmiliki pekee wa Ziwa Malawi, ambalo huku linajulikana kama Ziwa Nyasa, na kuonya kuwa utawala wake hautavumilia watu watakaokuwa na nia ya kuyumbisha taarifa za umiliki.

“Hebu tulilinde ziwa letu. Hili ni ziwa letu na ninaposema ziwa letu namaanisha ziwa lote. Mtu yeyote asifanye kosa la kubadili umiliki ambao umekuwepo kwa miaka 124 iliyopita,” alisema Mutharika akikaririwa na tovuti ya Nyasa Times la Malawi juzi wakati wa mkutano huo uliofanyika ukumbi wa Kituo cha Mikutano cha Nkopola Lakeshore mjini Mangochi.

“Tunathamini ziwa letu na tutahakikisha tunachukua hatua za kulilinda kwa gharama zozote,” alisema.

Mutharika aliwataka wananchi kupunguza matumizi mabaya ya maji ili yapatikane kwa ajili ya kilimo na viwandani wakati wa msimu wa ukame.

Hivi karibuni, Malawi na Tanzania zimejikuta katika mzozo wa umiliki wa Ziwa Nyasa lililo kusini mwa Tanzania, mzozo ambao umesababisha kuanza kwa mazungumzo ya usuluhishi kumaliza kutokubaliana huko baada ya nchi hizo mbili kushindwa kufikia muafaka. Mzozo wa mpaka kwenye Ziwa Nyasa umekuwepo tangu mwaka 1967.

Lakini, mzozo wa hivi karibuni umeibuka baada ya Malawi kuanza utafiti wa mafuta na gesi kwenye ziwa hilo.

Hata hivyo, Mutharika alisema uchimbaji mafuta utaendelea katika ziwa hilo licha ya wanaharakati wa mazingira kuitaka Malawi iache mpango huo.

“Wale wanaohofia kuhusu mipango yetu ya kutafuta na kuchimba mafuta hawana sababu ya kuhofia. Kama tutaamua kuchimba mafuta katika ziwa, tutahakikisha tunatumia teknolojia safi,” alisema akikaririwa na Nyasa Times.

CREDIT - MWANANCHI

Ameibuka Upya..Baada ya Kimya Kirefu Rc Makonda Aibuka na Kudai Mkoa Wake si Salama Tena,Awanyooshea Kidole Polisi..!!

$
0
0

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda amesema mkoa wake hauko salama kama watu wanavyodhani kwa sababu silaha nyingi zinamilikiwa kiholela na mafunzo ya matumizi ya silaha hizo hutolewa hata kwa watoto.

Makonda alisema hayo jana wakati wa ibada ya Pasaka iliyofanyika katika Kanisa la Anglikana la Mtakatifu Albano na kuwataka wakazi wa Dar es Salaam kujitokeza kuhakiki silaha zao na kusalimisha zile zinazomilikiwa kinyume cha sheria.

Alisisitiza kwamba ifikapo Julai Mosi, operesheni maalumu ya kukamata silaha zinazomilikiwa kinyume cha sheria itaanza na yeye mwenyewe ndiye atakayeiongoza.

“Tumegundua kwamba kwenye bonde la mto unaotenganisha Mkoa wa Dar es Salaam na Pwani, kuna mafunzo yanatolewa kwa watoto. Wazazi wanadhani watoto wao wamekwenda shule kumbe wamechukuliwa huko. Hatuwezi kukubali hali hiyo iendelee,” alisema.

Mkuu huyo wa mkoa aliwataka waumini waendelee kumwombea ili aifanye kazi yake vizuri kwa kutenda haki na aliwataka pia kumwombea pia Rais John Magufuli kwa sababu kazi anayoifanya ni kubwa.

Alisema Rais anapotumbua jipu moja, ndani yake kuna kundi la watu wanaoathirika na hatua aliyoichukua hivyo, alisema watu wa aina hiyo hawawezi kumpenda kwa sababu amevunja mtandao wa masilahi yao.

“Ninaomba kanisa pamoja na viongozi wote wa dini mnisaidie katika kuhimiza suala la ulinzi na usalama ili amani yetu iendelee kudumu. Ninaomba tushirikiane katika hilo, Dar es Salaam haiko salama kama mnavyodhani, mengine siwezi kusema kwa sababu sijaruhusiwa na Rais,” alisema.

Migogoro kanisani

Akizungumzia migogoro makanisani, Makonda alisema hataki kusikia kiongozi yeyote wa dini anakimbilia polisi au mahakamani kutaka suluhisho la matatizo yao ya ndani na kuwa atamweka ndani atakayejaribu kufanya hivyo.

Alisema ni aibu kubwa kwa kanisa kukimbilia kwenye vyombo vya dola badala ya polisi na Serikali kukimbilia kanisani kuomba ushauri. Alisema kanisa ndicho chombo cha usuluhishi wa matatizo mbalimbali ya jamii.

“Serikali inahitaji msaada wa kanisa na viongozi wa dini ili iweze kufanya kazi vizuri. Sitaki kusikia polisi wanakwenda kanisani (kukamata watu) katika mkoa wangu na wale wanaotoa taarifa kutaka polisi nitawaweka ndani,” alisema Makonda ambaye kabla ya kuwa mkuu wa mkoa, alikuwa mkuu wa Wilaya ya Kinondoni.

Askofu Mokiwa

Awali, Askofu Mkuu wa Kanisa la Anglikana, Dayosisi ya Dar es Salaam, Valentino Mokiwa alibainisha mambo mbalimbali aliyoyaita majipu ambayo yanafanya kanisa hilo lisiendelee katika kufundisha waumini wake yaliyo mema.

Mokiwa alitaja mambo hayo kuwa ni pamoja na mashindano ya kimadhehebu. Alisema madhehebu mbalimbali yanashindanishwa kupima kanisa lipi ni kubwa, lina waumini wangapi, linamilikiwa na nani na nguvu yake ni ipi.

Jambo jingine alisema ni maaskofu wenyewe kupigana vita. Alisema sasa ni kawaida kwa askofu mmoja kumchimba mwingine, askofu mmoja kupanga mapinduzi dhidi ya mwingine na baadhi ya maaskofu kutukanana waziwazi.

“Maaskofu wanasemana na kusingiziana mambo ya uongo, injili haiwezi kwenda mbele. Wengine wanatumia fedha na vyombo vya habari ili kutukana wengine. Kanisani pia kuna walaghai na wezi ambao wanavaa kanzu,” alisema Askofu Mokiwa.

Alisisitiza kwamba waumini wanapaswa kuogopana wao kwa wao kwa sababu ndiyo vikwazo vya wao kwenda mbinguni.

Rasmi..Manji Anyoosha Mikono Juu,Kesi Yake Mahakamani Yafikia Hatua Hii...!!!!

$
0
0

Idara ya Uhamiaji imemwachia kwa dhamana mfanyabiashara, Yusuf Manji ikiwa ni siku chache baada ya kufungua maombi Mahakama Kuu akiomba amri ya kutaka idara hiyo iitwe mahakamani kueleza uhalali wa kumshikilia.

Jana, mawakili wake, Alex Mgongolwa, Hudson Ndusyepo na Jeremiah Mtobyesa walidai mahakamani kuwa Manji alikuwa akishikiliwa.

Hata hivyo, baada ya kupatiwa dhamana, Manji aliomba kuondoa maombi hayo aliyofungua dhidi ya Kamishna Mkuu wa Uhamiaji, Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), Ofisa Uhamiaji Mkoa wa Dar es Salaam na Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu.

Jaji Ama-Isario Munisi aliyekuwa akisikiliza maombi hayo aliamuru kuondolewa mahakamani maombi hayo baada ya Wakili wa Serikali Mkuu, ambaye pia ni Naibu Mkurugenzi wa Mashtaka, Oswald Tibabyekoma kueleza kuwa hakuwa na pingamizi dhidi ya maombi hayo.

Nje ya Mahakama, Mgongolwa alilieleza gazeti hili kuwa, Machi 21 mteja wake alimpigia simu akimweleza alipigiwa simu na ofisa uhamiaji akimtaka kufika ofisini kwake kwa ajili ya utaratibu wa dhamana.

Alisema alikwenda naye ofisi za uhamiaji Machi 22 na alipewa dhamana na kutakiwa kuripoti ofisini hapo Jumatatu.

Kabla ya kufungua maombi hayo, Manji ambaye pia ni Diwani wa Mbagala (CCM), alikuwa amelazwa katika Hospitali ya Aga Khan akiwa chini ya ulinzi wa maofisa wa uhamiaji.

Machi 20 wakati maombi hayo yalipotajwa na Mwanasheria Mkuu wa Serikali kuwasilisha hati ya kiapo kinzani, alikana kumshikilia mfanyabiashara huyo.

Hata hivyo, mawakili wake walisisitiza kuwa mteja wao alikuwa chini ya ulinzi wa maofisa wa uhamiaji na polisi waliokuwa wakimlinda akiwa hospitalini usiku na mchana.

Mawakili hao waliomba kuwasilisha mahakamani ushahidi wa viapo vya maofisa wa Hospitali ya Aga Khan kuhusu madai ya mteja wao.

Manji alipelekwa ofisi za uhamiaji mkoa Februari 20 na kuhojiwa kwa tuhuma za kuingia nchini kinyume na sheria, akidaiwa siyo raia wa Tanzania.

Manji alikwenda kuhojiwa akitokea hospitalini, baada ya kutoa maelezo alirejea hospitali.

Hivi Ndivyo Nape Nnauye Alivyomkabidhi Ofisi Mwakyembe Leo..!!!

$
0
0

Aliyekuwa Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Nape Nnauye leo amekabidhi ofisi kwa Waziri Mpya wa Wizara hiyo, Dk Harrison Mwakyembe.

 Makabidhiano hayo yalifanyika katika Ofisi za Wizara Mjini Dodoma na kushuhudiwa na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo  Profesa Elisante Ole Gabriel.

Wengine walioshuhudia makabidhiano hayo ni Naibu Waziri Anastazia Wambura , Naibu Katibu Mkuu Nuru Millao na watendaji wa Wizara.

Ohhh..Sakata la Kuvamia Clouds Lavuka Mipaka ya Tanzania,Kila Kona Afrika Wamtuhumu Makonda..!!!!

$
0
0

Asasi za kiraia 33 barani Afrika zimelaani kitendo cha kuvamiwa kwa studio za televisheni ya Clouds na kulazimisha maudhui yasiyostahili yarushwe hewani.

Tamko la asasi hizo limetolewa ikiwa ni siku chache baada ya Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora, (THBUB), Jukwaa la Wahariri (TEF) na Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) kulaani kitendo hicho kinachodaiwa kukandamiza uhuru wa vyombo vya habari.

Asasi hizo zinazohusika na utawala bora, demokrasia, haki za binadamu na uhuru wa habari zilikutana hivi karibuni mjini Kampala nchini Uganda katika mkutano uliokuwa ukizungumzia uhuru wa kujieleza na kupata habari.

Tanzania kwenye mkutano huo iliwakilishwa na Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu (THRDC) , miongoni mwa mijadala iliyotawala ni kukemea vitisho na vitendo vya kunyanyasa waandishi.

Pia, wajumbe katika mkutano huo waligusia mabadiliko madogo ya baraza la mawaziri yaliyofanywa na Rais John Magufuli kwa kumtoa Nape Nnauye kwenye nafasi ya Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo.

Asasi hizo zilimpongeza Nape ambaye kabla ya kuondolewa kwenye nafasi hiyo aliunda kamati iliyochunguza tukio la uvamizi wa studio za Clouds, wakisema uamuzi huo ulionyesha ujasiri wa kusimamia uhuru wa vyombo vya habari na uhuru wa kujieleza.

Taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa na asasi hizo, ilidai kwa siku za karibuni Tanzania imekuwa na matukio zaidi ya 40 yanayolenga kukandamiza uhuru wa vyombo vya habari.

“Waandishi wamekuwa wakizuiwa au wakati mwingine kubughudhiwa ili wasifanye kazi yao. Vitendo hivyo vimekuwa vikifanywa hasa na wakuu wa wilaya na polisi,” ilibainisha taarifa hiyo.

Wajumbe walikumbusha kifungu cha pili cha Azimio la kanuni za uhuru wa kujieleza Afrika la mwaka 2002, kinachoelekeza Serikali ihakikishe inachukua hatua stahiki kuzuia uvamizi kwenye vyombo vya habari.

Kifungu hicho kinaelezea endapo uvamizi huo utatokea, Serikali ina wajibu wa kuchunguza na kuwaadhibu wahusika kwa mujibu wa kosa lao.

Baada ya Rais Magufuli Kuamuru Wimbo wa Wapo wa Nay wa Mitego Uchezwe Redioni,Basata Wameibuka na Haya Mapya...!!!

$
0
0

Baraza la Sanaa Taifa ‘BATASA’ limerudi tena na kuufungilia wimbo ‘Wapo’ wa Nay wa Mitego kwa madai waliufungia ili kupisha uchunguzi wa kipolisi upite baada ya jeshi hilo kumshikilia rapa huyo kwa siku mbili kutokana na wimbo huyo.

Awali baraza hilo lilitangaza kuufungia wimbo huo kwa madai hauna maadili kabla ya Rais Magufuli kutoa tamko la wimbo huo kuendelea kupigwa kwa kuwa hauna tatizo lolote.

Baraza hilo limedai kuwa msanii kama ilivyo kwa raia yeyote anaweza kukamatwa na kushtakiwa kwa mujibu wa sheria kama kazi yake ikibainika kuwa na kosa la jinai.

“Tulifanya mazungumzo na wenzetu jeshi la polisi waliokua wanamhoji msanii Nay wa Mitego na kuchunguza jinai katika wimbo wake wa Wapo,” Basata walitweet.

Aliongeza, “Baada ya ushauri kutoka kwa Waziri Mwakyembe na baadaye taarifa ya jeshi la polisi na mazungumzo na msanii Nay kituo cha kati cha polisi.Tunaruhusu wimbo wa ‘Wapo’ wa msanii Nay kuchezwa katika vyombo vya habari. Kama taarifa yetu ilivyoeleza, ulisitishwa kupisha taratibu za kipolisi,”

Rapa huyo aliachiwa jana jioni na jeshi la polisi kwa kauli ya Rais Magufuli baada ya kushikiliwa kwa siku mbili.

Baada ya Harmorapa Kulalamika Kuwa Nature Amemtoza Pesa Nyingi kwa Kolabo,Juma Nature Amefunguka Haya Kuhusu Madai Hayo..!!!

$
0
0

Msanii mkongwe wa muziki nchini, Juma Nature amevunja ukimya baada ya Harmorapa kumtuhumu kumdai pesa ya mavazi kwa ajili ya video ya wimbo wake mpya ‘Kiboko Ya Mabishoo’.

Akiongea na kipindi cha E News cha EATV Jumatatu hii, muimbaji huyo amesema rapper huyo chipukizi hana pesa ya kumlipa.

“Nikisema nimemlipisha Harmorapa pesa kwa ajili ya kolabo nitakuwa nakosea. Mimi ni mtu mzima nilikubali kufanya wimbo na msanii yule kwa sababu ni mkali na anajua muziki pia na imani atafika mbali. Hawezi kunilipa mimi, ana hela gani?,” amesema Nature.

Wiki chache zilizopita, Harmo alimlalamika msanii huyo mkongwe kupitia kipindi hicho kwa kusema, “Haipo sawa kwa wasanii wakubwa kutudai sisi ‘underground’ pesa ya kufanyia collabo wakati wanajua bado hata hatuanza kufaidika na muziki wenyewe.”

Kudadeki..Wachina Noma Sana Aisee..Tazama Wamejenga Reli Inayopita Ndani ya Maghorofa ya Watu..!!!

$
0
0

Kwa wakazi wa mji mmoja huko China, usafiri wa treni unapatikana barazani kwao, tena ghorofani.

Katika mji wa Chongqing nchini humo, reli ya treni imejengwa kukatiza juu ya nyumba wanamoishi wapangaji.


Chongqing, mji uliopo kusini mashariki mwa China, umefurika wakazi takriban milioni 49, kitu kilichowafanya watu wanaohusika na mipango miji kuwa wabunifu.

Kutokanana hilo walianzisha mradi uliozalisha kile kilichoitwa, Mountain City.

Ehe,,Kumbe Aliyemtishia Nape Bastola Siyo Polisi Wala Nini,,Mwigulu Afunguka Jinsi Walivyomkamata..!!!

$
0
0

Waziri wa Mambo ya Ndani, Mwigulu Nchemba amesema mtu aliyemtishia kwa bastola aliyekuwa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye si askari wa Jeshi la Polisi, lakini ameshapatikana na atashughulikiwa kwa mujibu wa utaratibu wa ulinzi na usalama.

Mwigulu alisema hayo baada ya kufungua mkutano wa kazi wa mwaka wa maofisa waandamizi wa polisi, makamanda wa mikoa na wakuu wa vikosi wa Jeshi la Polisi ambao unafanyika mjini hapa. “Ameshapatikana (aliyemtishia Nape) na atashughulikiwa kwa mujibu wa taratibu za ulinzi na usalama ambazo zimekuwa zikifanyika ndani, lakini hazitangazwi,”alisema.

Hata hivyo, Mwigulu alikataa kuelezea kwa undani kuhusu mtu huyo kwa kubainisha anatoka taasisi gani wala jina la mtuhumiwa kwa madai kuwa ni kwa sababu ya usalama wake. Mtu huyo alifanya kitendo hicho wakati Nape, ambaye alikuwa Waziri wa Habari, alipokuwa anaelekea Hoteli ya Protea alikopanga kuzungumza na waandishi wa habari baada ya mbunge huyo wa Mtama kuachwa katika mabadiliko madogo ya Baraza la Mawaziri.

Mtu huyo alikuwa pamoja na wenzake wawili ambao kwa pamoja walikuwa wakimlazimisha arudi kwenye gari lake na kuondoka, lakini Nape alibisha na ndipo mtu huyo aliporudi nyuma, kuchomoa bastola kutoka kiunoni na kisha kumtishia kabla ya kutulizwa na mwenzake.

Watu hao walitoweka eneo hilo muda mfupi baadaye. Siku moja baada ya tukio hilo Mwigulu alimwagiza Mkuu wa Jeshi la Polisi, Ernest Mangu kumtafuta mtu huyo.

Imefichuka..Hii Ndio Sababu Kubwa ya Prof Lipumba Kumtumbua Jipu Maalim Seif Cuf..!!!

$
0
0

Baraza Kuu la Uongozi Taifa la Chama cha Wananchi (CUF) leo limemvua, Maalim Seif nafasi ya Ukatibu Mkuu wa Chama hicho na nafasi hiyo kukaimiwa Bi. Magdalena Hamis Sakaya.

Akizungumza na wanahabari jijini Dar es Salaam leo, Mwenyekiti wa CUF Taifa, anayetambulika na Msajili wa Vyama vya Siasa, Prof. Ibrahim Lipumba amesema kuwa Baraza hilo limefiki uamuzi huo kutokana na sababu mbalimbali ambapo moja wapo ni Maalim Seif kutofika ofisini na kutohudhuria kwenye vikao vya chama vinavyotambulia kwa mujibu wa katiba ya chama hicho.

“Miongoni mwa ajenda tulizo zijadili ni kuthibitisha wakurugenzi na manaibu wakurugenzi, kupitisha jina la wagombea Ubunge wa Bunge la Jumuiya ya Afrika Mashariki, kujaza nafasi za wajumbe wa Baraza Kuu zilizokuwa wazi, kuunda Bodi ya wadhamini, kuunda kamati ya maadili, taarifa ya fedha, taarifa ya kesi na taarifa ya hali ya kisiasa,”.

Pia Prof. Lipumba ametangaza majina matatu ya Wagombea Ubunge Bunge la Afrika Mashariki kupitia majina yaliyoteuliwa na kikao cha Baraza Kuu la Uongozi la Taifa kilichokaa Machi 25 na 26 mwaka huu.

Majina matatu yaliyoteuliwa na Baraza kuu la uongozi la Uongozi ni, Sonia Magogo, Mohammed Habib Mnyaa na Thomas Malima mmoja kati yao akitoa serikali ya Mapinduzi Zanzibar.

Mbali na hayo, Lipumba amemtangaza rasmi Bw. Abdul Kambaya kuwa Mkurugenzi wa Habari, Uenezi na Mahusiano ya Umma ambapo hapo awali alikuwa Mkurugenzi wa Habari, Uenezi na Mahusiano ya Umma.

NEVER GIVE UP:.Kwa Waliowahi Kuumizwa Katika Mapenz,Yajue Haya..!!!

$
0
0

kuvunjika moyo ni moja ya jambo zito na ambalo mtu hupitia na inahitaji sana moyo kwasababu ya kupitia wakati mgumu,fikra,mawazo,maumivu,kujiona huna thamani,jamani mtu kaamua kukuacha wa nini kumganda,let him or her go kama alivotaka,duniani hayuko pekeyake, mbona wamejaa kama yy ,na unaweza kupata mzuri zaid yake ,na ufurahie sana na kumshukur mungu mana mpaka anakuacha manake kajionesha ngozi yake asili kua not your type and he/she does not deserve to be wid u.kwaiyo never give up maisha yenyew mafupi,wacha aende utapata bora kuliko yeye.

jaribu kukaa na familia,marafiki na watu wako wa karibu ,cheka, furahia existence yako,io ni moja ya kuanza kumsahau na kutoa mawazo taratibu.

kua makini kwa kutokua muwazi,namaanisha kua sio kisa umeumizwa uko nyuma ,ndo usiwaamini ke/me wote ,binadamu hatufanani,unahis umependa for the second time achilia toa la moyoni kuliko kukaa nalo,kua free kufanya lolote unaloona its good for you.

baada ya kuumizwa sio unaenda na ww kufanya vitu vya kipuuzi.fanya vitu ambavo vitakavokufanya utoe mawazo na kukupungizia stress ,unafanya ili uwe na furaha na sio depression ukaja kufa bure siku sio zako ndugu.

jikite katika mazoez mfano kukimbia au jiweke busy na kazi yoyote ili kukuweka busy na kupoteza attention ktk kichwa ya yule aliekuumiza,usijiumize kabisa,unajiona maumiv yanazid ,zidisha kujiweka busy na jiweke kama hujawah kuumizwa na jipe moyo be u as u, kua duniani hayuko pekeake.

ukijiweka karibu sana na watu,kua na furaha cheka nao,nao watafurahia uwepo wako,nakuhakikishia unaweza kujipatia apoapo mwngn hahaha,just be u.

badala ya kuangalia mabaya ya kuvunjika uhusiano ,wewe tizama yale mazuri tu uloyafanya,usiseme labda nlifanya baya flani ndo mana nkatendwa,mana skuizi unaweza kutendwa kweupee na huna kosa ulilolifanya,unajishangaa unakaushiwa tu,usijitie mnyororo wa roho buree ukasema hata nkitongoza naweza nsikae nae sana kama wa mwanzo ,no no no,hamna kitu kama iko,ndo mana tukaambiwa binadamu tunatofautiana,just move one,kua huru na nafsi yako,fanya roho yako kitu kinachojiskia ipate faraja for the second time.

toka mitoko ya hapa na pale,tafuta marafiki zako wa karibu,kua na ile tabia ya kutoka out kuspend kuenjoy ,pia itakusaidia kutoa mawazo.

unajua ni bora kua single kuliko kua katika uhusiano m,baya.unaweza pia kupost story yako ktk jukwaa husika ili kupata msaada zaid wa kimawazo ,it ll help too.

Wanaume wameumbiwa wanawake,na wanawake wameumbiwa wanaume,so hata ukiumizwa haifai kusema sitopenda tena,ohh sjui stokuja kutafuta mwenza tena,inamaana utaweza kukaa ivo pekeako mpk uzeeni mpk kufa,mara ohh stopenda tena bali ntawachezea tu na kuwaacha kama nlivoachwa mm,jamani jamani jamani,we chezeaaa mwisho wake uchezewe,chezea wee mwisho wake unajikuta umekondeana kwenda kupima ngoma unayo,utamlaumu aliekuacha au utajilaumu na nafsi yako.

Nmemaliza.love u ol.

Naomba Ushauri..Mwanafunzi Wangu wa Kike Ananitaka Kimapenzi,Kila Siku Hukaa Viti Mbele Kihasara,Aliwahi Kuniletea Zawadi ya Boxer..!!!

$
0
0

Mimi  ni mwalimu wa shule moja  ambayo sitaitaja. mwezi uliopita mwanafunzi wangu wa kike ambaye  yuko  kidato  cha  tatu alinifuata na kuniambia anataka kunipa zawadi...

Sikuwa na hili wala lile, hivyo nilimwambia ni poa tu kama ameamua  kunikumbuka mwalimu wake..

Zawadi aloniletea ilinifanya  nishike  kichwa maana  sikutegemea.Yule mwanafunzi  aliniletea chupi aina ya boxer 3  na  tangu siku hiyo kila akiniona ananifanyia vituko mpaka ananikalia nusu  uchi  darasana nikiwa nafundisha  kwa vile anakaa viti vya Mbele....

Nikiwa  kama  mwalimu, nimejaribu  kutumia  viboko  ili  kumuonesha  kwamba  sina  mpango  naye lakini  bado  imeshindikana..

Nifanyaje  ndugu  zangu?  Maadili  ya  kazi  yananibana.Hata  hivyo, mwanao  ni  mwanetu  sote.
Viewing all 104809 articles
Browse latest View live




Latest Images