Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104795 articles
Browse latest View live

MATUKIO ya Watu Kutekwa Yamemfanya Mrema Kuibuka na Mpya Hii Kuhusu Rais Magufuli..!!!

$
0
0

Mwenyekiti wa Bodi ya Parole Tanzania, Augustine Mrema amesema kuwa  uhalifu unaoendelea kujitokeza hapa nchini unafanywa kwa makusudi na watu wenye nia mbaya na Serikali ya awamu ya Tano.

Amesema kuwa uhalifu kama huo haukubaliki hivyo unatakiwa kupigwa vita na kila mtu mwenye mapenzi mema na nchi kwani haijawahi kutokea mauaji ya askari Polisi kama yaliyotokea hivi karibuni.

Ameyasema hayo alipokuwa akifanya mahojiano na kituo kimoja cha redio Jijini Dar es salaam kuhusu hali ya nchi ilivyo kwa sasa, amesema kuwa kwa sasa ana mpango wa kuonana na Rais Dkt. Magufuli ili aweze kumuomba amruhusu kutoa wafungwa wenye sifa ya kupata msamaha ili waweze kusaidia kutoa taarifa za watu wanaofanya uhalifu huo.

“Kuwatoa wafungwa wenye sifa ya kupata msamaha itakua ni moja ya mkakati ambao utawezesha kukamatwa kwa wahalifu wanaondelea kufanya mauaji nchini, hawa wafungwa lazima watakuwa wanajua walipo wahalifu,” amesema Mrema.

Aidha, Mrema ameongeza kuwa atatumia mbinu zote na uzoefu alionao ili kuweza kupambana na uhalifu huo, kwani kulingana na uzoefu wake amegundua kuna kampeni za makusudi zinazofanywa kwa ajili ya kumchafua Rais Dkt. Magufuli.

Hata hivyo, katika hatua nyingine amemtaka Rais Dkt. Magufuli kuwashughulikia wale wote wanaoleta viashiria vya uvunjifu wa Amani hapa nchini.

CHANJO ya Malaria Kutolewa 2018...!!!

$
0
0

Chanzo ya kwanza kabisa duniani dhidi ya ugonjwa wa Malaria inatarajiwa kutolewa katika nchi tatu za Ghana, Kenya na Malawi kuanzia mwaka 2018.

Chanjo hiyo ya RTS,S inafundisha mfumo wa kinga mwilini, kushambulia vimelea vya Malaria vinavyosambazwa na mbu, ambapo kwa mujibu wa Shirika la Afya Duniani, chanjo hiyo ina fursa kubwa ya kuokoa makumi kwa maelfu ya maisha.

Lakini haijafahamika kama chanjo hiyo itaweza kutumika kwa nchi ambazo zina huduma duni za afya. Chanjo hiyo inatakiwa kutolewa mara nne yaani mara moja kila baada ya miezi mitatu na dozi ya nne miezi 18 baadaye.

Mkurugenzi wa WHO Kanda ya Afrika, Dk. Matshidiso Moeti, amesema chanjo hiyo inatarajiwa kutolewa kwa zaidi ya watoto 750,000 wenye umri wa kati ya miezi 5 hadi 17.

Licha ya mafanikio hayo makubwa, bado kuna visa vipya milioni 212 vya Malaria kila mwaka na vifo 429,000

JOH Makini Afunguka Haya Baada ya Mashabiki Kumfananisha na Jay Z wa Marekani..!!!

$
0
0

Msanii wa miondoko ya 'Hip hop' kutoka kampuni ya Weusi, Joh Makini amefunguka ya moyoni na kusema anajisikia faraja kwa mashabiki zake kumfananisha na msanii Jay Z.

Joh Makini amesema ufananisho huo uko wazi kwa kuwa kiwango cha muziki wake ni mkubwa kiasi ambacho watu wanaomzunguka na wapenzi wa kazi zake hawaoni mtu mwingine wa kumfananishia naye isipokuwa msanii huyo kutoka Ughaibuni.

"Jay Z ni 'role model' wangu...mimi naimba maisha ya sinoni daraja mbili na Tanzania na Jay Z anaimba maisha ya Brooklyn na Marekani, nafikiri nipo katika 'level' ambayo hawaoni mtu mwingine wa kunifananisha naye...Kwahiyo mimi naona poa kwa sababu kama unanifananisha na Jay z 'yeah i like it' kuliko ungenifananisha na mtu mwingine". Alisema Joh Makini

Kwa upande mwingine msanii huyo amedai changamoto na vikwazo anavyokutana navyo katika kufanya kazi zake za kila siku huwa ndiyo vinamfanya aweze kutengeneza mambo mazuri zaidi.

KIMENUKAA..Mbunge wa Cuf Temeke Amsasambua Prof Lipumba Hadi Aibu..!!!

$
0
0

Mbunge wa Temeke Mh. Abdallah Mtolea amefunguka na kudai kuwa aliyekuwa Mwenyekiti wa CUF Prof . Ibrahim Lipumba ni msomi ambaye amejishushia heshima kwa kufanya jambo la ajabu  la kuagiza vijana wake kuvamia mkutano wa CUF.

Mh. Mtolea amefunguka hayo alipohojiana na EATV  na kudai kuwa Lipumba amefanya vitu vya ajabu ambavyo jamii iliyokuwa inamuheshimu sasa itampuudha na yeye atapunguza heshima aliyoitengeneza kwa muda mrefu.

"Mimi Lipumba ni kama kaka yangu kwa jinsi nilivyokuwa namuheshimu, lakini pia alikuwa kiongozi wangu bado namheshimu ila kwa kitendo kilichofanyika pale VINA nimeishusha heshima yangu kwake kwa kiasi kikubwa sana na niseme tu amekuwa mtu wa ajabu sana, elimu yake yotee na heshima aliyonayo amekuja kuiharibu kwa mambo ya ajabu kama yaliyofanyika"- Mh. Mtolea alifunguka.

Aidha katika hatua nyingine Mh. Mtolea amekiri kusikitishwa na kitendo cha jeshi la polisi kuzuia mkutano wake uliopangwa kufanyika  jana kujadili jinsi ya kuzitatua kero za wananchi na kuhusisha mkutano wake na masuala ya kisiasa kitu ambacho kinaweza kurudisha maendeleo nyuma.

" Ni kweli  nilipanga kufanya mkutano na wadau wa maendeleo kujadili changamoto za wananchi wa Temeke haswa wale wanaoishi Kilakala ambao eneo lote limejaa maji, kwenye eneo lile tumelazimika kuweka pump inayonyonya maji lakini tulikuwa na changamoto kama mafuta na mambo mengine hivyo nilikuwa nimepanga kukutana na wadau mbalimbali kwenye ukumbi wa Temeke Executive  lakini ghafla nashangaa nakuja kupewa taarifa nisifanye mkutano wowote kwa vile eti wamesikia nataka kukutana na vijana wa CUF ya Lipumba niwashawishi"- aliongeza Mh. Mtolea.

Mh. Mtolea ameendelea kusikitika kwa kudai kuwa kuzuia vikao kufanyika ni kuwanyima wananchi kutimiziwa haki zao za msingi.

"Mimi huwa ni mstaarabu nikitaka kufanya mkutano huwa nawajulisha jeshi la polisi na wao mara nyingi wamekuwa wakinipatia ulinzi tunashirikiana vizuri lakini hili la leo nilivyoenda kuwataarifu ni kama nimeenda kuwambia nizuieni. Hichi kitendo cha kutubana upinzani naona ndicho kinachoendelezwa zaidi, walitunyima mikutano ya hadhara wakaruhusu mikutano ya kujadili maendeleo na mimi siku zote huwa nafanya hivyo sasa nashangaa wamekuja na hii ya kuzuia vikao vya ndani  bila kuuliza kikao kinahusu nini  na wakati  vinaruhusiwa. Hata kama ni kweli nilikuwa nakutana na watu wa CUF mimi ni Mbunge katiba ya chama inaniruhusu kufanya mkutano kwa sababu tayari kwenye chama nina uongozi"- alimaliza Mh. Mtolea.

CCM Wamshitaki Nape ..Habari Vichwa vya Magazeti ya Leo 25/4/2017..!!!

DIAMOND Aelezea Jinsi Young Killer Alivyopagawa Baada ya Kumpa Biti Wafanya Collabo

$
0
0
Msanii wa muziki wa Hiphop Tanzania anaewakilisha vema rock city Young killer Msodoki alipagawa baada ya kupewa taarifa ya kuwepo kwenye wimbo wa pamoja na Boss wa wasafidotcom Diamond Platinumz.

Diamond Platinumz amesema kuwa anayo kolabo na rapa @Youngkillermsodokii na siku aliyomuita studio kumpa taarifa za kuwa watafanya kazi pamoja rapper huyo alipagawa na hakuamini alichokisikiana.

Msikilize diamond platinumz hapo juu akieleza zaidi:

JB: Simfahamu Ney wa Mitego Wala Sisikilizagi Bongo Fleva

$
0
0
JB amedai hamfahamu mwanamuziki huyo na wala hasikilizagi bongo fleva, ila kwa kauli yake hiyo amesema anampenda sana japo amemdiss.

Yeye pamoja na kusema hasikilizi Bongo Flevaila hawachukii wanamuziki wa Bongo Fleva
Pia amesema sio kwamba hawataki movie za nje zisije ila wanataka zilipe kodi kama wao wanavyofanya, kwa kuwa mtu anadownload movie ya nje kisha anaizalisha copy nyingi na kuiuza bila kulipa kodi na amesema hii ikiendelea na wao hawatalipa kodi kwa movie zao pia

RAIS Magufuli Amteua Profesa Chibunda, Atua Dodoma Kuwafunda Wabunge wa CCM..!!!

$
0
0

Rais John Magufuli amemteua Profesa Raphael Chibunda kuwa Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA).

Taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi, Ikulu Jijini Dar es Salaam jana imeeleza kuwa uteuzi wa Profesa Chibunda unaanza jana tarehe 24 Aprili, 2017.

Kabla ya uteuzi huo Profesa Chibunda alikuwa Mkurugenzi Msaidizi, Idara ya Sayansi na Teknolojia katika Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia.

Profesa Raphael Chibunda anachukua nafasi ya Profesa Gerald Monela ambaye amemaliza muda wake.

Wakati huo huo, Rais Magufuli amewasili mjini Dodoma ambako pamoja na mambo mengine atakuwa mgeni rasmi katika sherehe za maadhimisho ya miaka 53 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.

POLEPOLE Afunguka ya Moyoni Kuhusu Samatta..Afichua Kuwa Yeye ni Yanga Damudamu..!!!

$
0
0

Katibu wa itikadi, siasa na uenezi wa chama cha mapinduzi (CCM), Humphrey Polepole amemtaja mshambuliaji wa RCK Genk, Mbwana Samatta kama mwanasoka pekee anayemvutia hapa nchini.

Akizungumza katika mahojiano maalum katika ofisi za gazeti la Mwananchi, Tabata Relini,  Polepole alisema juhudi za Samatta ambaye ni nahodha wa timu ya taifa,  Taifa Stars ndizo zinazofanya avutiwe naye.

"Napenda kuona vijana wetu wanapata mafanikio kwenye soka hivyo mchezaji wa soka ambaye ninampenda ni Mbwana Samatta.

Huyo tu kwa upande wangu ndiye anatosha kwa ndani na nje ya nchi na hakuna mwingine anayenivutia zaidi yake," alisema Polepole.

Polepole alifichua kuwa yeye ni shabiki wa kutupwa wa klabu ya Yanga.

Credit - mwananchi

AUAWA kwa Kupigwa na Wananchi Akituhumiwa Mchawi..!!

$
0
0

MKAZI mmoja wa kijiji cha Mwenge kata ya Kate wilayani Nkasi mkoani Rukwa Joseph Songaleli (56) amefariki dunia baada ya kupigwa na watu wasiojulikana akituhumiwa kuwa ni mshirikina.

Akizungumza  Mwenyekiti wa kijiji hicho, Medadi Kitinsi, alisema marehemu alivamiwa nyumbani kwake majira ya saa 6:00 usiku na watu wasiojulikana huku wakiwa na silaha za jadi na kuvunja mlango wa nyumba kwa kutumia jiwe kubwa aina ya fatuma na kumshambulia mtu huyo.

Alisema kuwa awali mke wa marehemu baada ya mlango kuvunjwa alikimbia na kutokea dirishani ndipo wauaji hao walipopata nafasi ya kumkamata marehemu na kuanza kumshambulia kwa silaha hizo za jadi.

Alidai kuwa kulitokea mapambano makali kati yao ambapo marehemu alijitahidi kujiokoa lakini alizidiwa nguvu  na watu hao walimuamuru marehemu alale kifudifudi na ndipo alipoanza kukatwa mapanga kichwani hadi kufikia kifo chake.

Mwenyekiti huyo wa kijiji amedai kuwa mauaji hayo chanzo chake kikuu ni imani za kishirikina ambapo inasemekana marehemu aliingia mgogoro na mmoja wa ndugu zake akidai kuwa marehemu alikua akimroga.

Habari za Kipolisi zinadai kuwa mpaka sasa wanamshikilia mtu mmoja kuhusika na tukio hilo na kuwa uchunguzi zaidi unaendelea ili kuweza kuwakamata wale wote waliohusika katika tukio hilo.

Mkuu wa wilaya Nkasi Said Mtanda amesikitishwa na mauaji hayo na kuwa serikali inachokifanya ni kuhakikisha wale waliohusika wamnakamatwa na sasa wataanza kupita kila kijiji na kuanza kuielimisha jamii juu ya imani hizo potofu.

STEVE Nyerere Azidi Kuwachamba Wasanii Walioandamana..Adai Nay wa Mitego Alikuwa Sahihi Kuwatukana..!!!

$
0
0

Muigizaji na mchekeshaji maarufu nchini Steve  Nyerere amemuombea msamaha msanii wa muziki Nay wa Mitego kwa kuwaita wasanii wa filamu wote walioandamana kupinga uingizwaji wa filamu kutoka nje ya nchi kuwa ni 'Matahira'

Akizungumza  kwenye Planet Bongo ya East Africa Radio, Steve Nyerere amesema kwamba yawezekana  Nay wa Mitego alikuwa na hasira hivyo akashindwa kutumia lugha sahihi ya kuwaelekeza wasanii wenzake walivyokuwa wanakosea ndio maana alitoa lugha yenye maneno makali ijapokuwa alikuwa sahihi kukosoa maandamano yale.

"Kwanza naomba nimuombee msamaha ndugu yangu Nay wa Mitego, hakuwa na nia mbaya lakini hakutumia maadili kufikisha ujumbe wake, Unajua sisi watanzania hatupendi kuambiwa ukweli na hata tukisemana tuna lugha zetu laini za kusemeshana. Nay wa Mitego mpaka kutoa maneno makali vile ujue anaipenda tasnia yetu ya filamu alikuwa kaaumia, si unajua hata yeye alishawahi kuwa huku anatuonea huruma na anatupenda mimi niseme mumsamehe tuu" - alisema Steve.

Aidha Steve Nyerere ameongeza kuwa kwa hali ilivyo katika tasnia ya filamu Tanzania hakuna haja ya maandamano pamoja na kurushiana maneno kwenye mitandao bali kinachotakiwa ni kukalishana chini waigizaji wote na kuangalia mahali walipojikwaa na kufanya marekebisho.

"Mtandaoni hatutaweza kumaliza hili tatizo kinachotakiwa hapa ni tukae chini na tuongee tunataka nini. Msibague kuandamana kwa ajili ya faida yenu wenyewe ila tujenge hoja ambayo tukubaliane wote tuiombe serikali itusaidie wote kwa ujumla na siyo watu wachache wanaojifanya manabii hawataki kukosolewa" Steve Nyerere alisistiza.

HAJI Manara - Kama Mbwai na Iwe Tu..Niko Tayari kwa Mapambano na TFF ya Malinzi..!!!

$
0
0

Mkuu wa  Idara ya Habari na Mawasiliano wa Klabu ya Simba, Haji Manara amesikitishwa na uamuzi uliotolewa na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) huku akidai yupo tayari kwa mapambano kwa kuwa hakupewa nafasi ya kusikilizwa. 

Haji Manara amesema hayo baada ya kutolewa  hukumu na Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Nidhamu, Jerome Msemwa ya kumfungia kujihusisha na masuala ya soka kutokana na makosa matatu ambayo ni kuituhumu na kuidhalilisha TFF, kueneza chuki za ukabila kwa kudai Rais wa TFF, Jamal Malinzi na Katibu wake Selestine Mwesigwa kuwa ni Wahaya na viongozi wa zamani wa Yanga na la mwisho kuingilia utendaji wa shirikisho hilo.

Kufuatia maamuzi hayo ya TFF Manara amefunguka haya 

"Unazuia na kutonipa nafasi ya kusikilizwa, unanipa hukumu kwa makosa nisiondikiwa katika mashtaka yao..Nipo tayari kwa ajili ya mapambano, tukutane juu". Alisema Manara kupitia ukurasa wake wa Instagram

Haji Manara amesimamishwa kutojihusisha na masuala ya soka kwa mwaka mmoja na pia kutakiwa kulipa faini ya Shilingi Milioni tisa.

AKIMBIZWA Hospitali Baada ya Kukaa ‘Airport’ Siku 10 Akimsubiri Mpenzi wake

$
0
0
Mwanaume mmoja raia wa Uholanzi amejikuta akilazwa hospitalini baada  ya kukaa katika Uwanja wa Ndege kwa siku 10 nchini China alipoenda kwa lengo la kukutana na mrembo aliyekuwa akiwasiliana naye mtandaoni, ambaye hakutokea.

Mwanaume huyo aliyetajwa kwa jina la Alexander Peter Cirk mwenye umri wa miaka 41, alisafiri kutoka Uholanzi na kutua katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Changsha Huanghua kukutana na mrembo aliyemfahamu kwa jina la Zhang.

Hunan TV imeripoti kuwa Cirk alikataa kuondoka katika uwanja huo wa ndege, lakini hali yake ya afya ilizorota kwa kukosa maji ya kutosha na chakula, hivyo maafisa walilazimika kumkimbiza hospitalini.

Baada ya tukio hilo kuripotiwa kwenye vyombo vya habari, mrembo huyo alijitokeza na kufanya mahojiano na Hunan TV wakati mwanaume huyo alikuwa tayari amesharushwa nchini kwao.

Mrembo huyo alieleza kuwa alidhani mwanaume huyo anatania pale alipomwambia anaenda nchini China kwa ajili yake. Aliongeza kuwa wakati wote huo yeye alienda kufanya upasuaji (plastic surgery), hivyo simu yake ilikuwa imezima.

“Siku moja alinitumia picha ya tiketi za ndege ghafla na nilidhani alikuwa anatania. Hakuwahi kuwasiliana na mimi tena baadae,” alisema mrembo huyo.

Hata hivyo, mwanaume huyo alipoulizwa wakati anarudishwa Uholanzi baada ya kutibiwa, alieleza kuwa anaamini atakaporudi nchini kwao wataendelea na uhusiano wao wa mapenzi mtandaoni.

JB Amchana Wema Sepetu na Wengine Ambao Hawakuandamana na Makonda Kariakoo

$
0
0

Muigizaji mkongwe nchini Jacob Stephen 'JB amefunguka na kudai hawakufanya maandamano ya kuzuia movie za nje ya nchi kuuzwa nchini bali waliandamana kuzitaka zilipiwe kodi au serikali itoe msamaha kwenye filamu za ndani.

JB amezungumza hayo alipokuwa akifanya mahojiano na wanahabari wakati wa uzinduzi wa filamu ya Tunu na kudai kuwa watu wengi wamehusisha maandamano yao na siasa kitu ambacho hakina ukweli na kuongeza kuwa tasnia ya filamu kwa sasa inahitaji watu watakaowasaidia kumaliza kilio chao. "Sisi hatupingi movie za nje kuingia nchini, mimi mwenyewe nazipenda na ninaziangalia. Hapa ugomvi uliopo ni wao watozwe kodi au na sisi tuondolewe hizo kodi, wakifanya hivyo hakuna mtu ambaye atapiga kelele tena. Sasa hivi nakatwa asilimia 30 lakini bado natakiwa nitoe asilimia tano na wakati huo huo, nikitaka kutoa movie mpaka nikaombe kibali kama ni wewe ungekubali? Na jambo hili lisihusishwe na siasa kwani sisi mtu yoyote ambaye ataweza kutusaidia kutusemea tutamsikiliza hata akiwa wa upinzani hatuna shida" Alisema Jb

Aidha msanii huyo ameongeza kuwa wasanii wenzao wanaowakejeli kwa kuandamana wengi wao hawategemei movie kuwaingizia kipato na ndio maana wanaongea maneno ya ajabu huko nje. "Msanii yoyote ambaye filamu ndiyo chakula chake hawezi kuwa nje ya hili kwa sababu hataweza kuishi. Mimi niseme tu siwezi kuishi bila filamu ndiyo maana tunapiga kelele. Sitaki kuwataja majina lakini angalia tu wewe mwenyewe huyo mtu ambaye hataki kupiga kelele anaishi bila filamu?" JB alimaliza

JIPATIE Water Dispenser Mpya Kwa Bei Nafuu Mnoo

$
0
0

JIPATIE WATER DISPENSER MPYA kwa bei Nafuu sanaa,Kwa matumizi ya OFISINI NA NYUMBANI, Upate Maji baridi na Moto.

Tunakuletea Oda yako kwa Wakati na Mikoani tunatuma Oda zenu pia.

Tunatoa DHAMANA ya Mwaka 1.

BEI 195000/= TU HAINA FRIJI.

BEI 290000/= INA FRIJI CHINI

TUPIGIE SASA 0743757575

More Items/Products follow us Instagram
@beinafuu_shop
@beinafuu_shop
@beinafuu_shop
@beinafuu_shop

TARIME, Mara: Afungwa Mwaka Mmoja kwa Kuua Polisi kwa Bastola..!!!

$
0
0

MFANYABIASHARA anayemiliki duka la vipuri vya magari mjini Tarime, Tumaini Wankyo (28) maarufu Zuma, amehukumiwa kifungo cha mwaka mmoja jela baada ya kupatikana na hatia ya kumuua bila kukusudia askari wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi (JWTZ) Kikosi cha Nyandoto, Rojar Elias kwa kumpiga risasi wakati wakigombea mwanamke wakiwa hoteli na baa ya NK mjini Tarime mkoani Mara.

Jaji Joaquine De-Mello alitoa hukumu hiyo jana katika kesi namba 9/2016 katika kikao cha Mahakama Kuu inayoendesha vikao vyakeMahakama ya Wilaya Tarime. Awali, Mwanasheria wa Serikali, Harry Mbogoro alidai kuwa Agosti 17, 2015 saa 7 usiku Wankyo akiwa katika Hoteli ya NK iliyopo mjini Tarime akiwa na mpenzi wake wakila chakula na vinywaji, alifika askari wa JWTZ, Elias akiwa na wenzake wawili na kutaka kumchukua mwanamke aliyekuwa naye Jacob.

Alidai alimshambulia kwa kumpiga ngwala na kumwangusha chini, na mtuhumiwa alitaka kujiokoa akiwa ameangushwa chini huku akiwa na silaha yake na risasi iliyokuwa ndani ya bastola yake anayomiliki kihalali, ilifyatuka na kumjeruhi Elias aliyekimbizwa Hospitali ya Wilaya Tarime kisha kuhamishiwa Hospitali ya Bugando jijini Mwanza ambako alifariki wakati akipatiwa matibabu.

“Mtuhumiwa baada ya tukio hilo usiku huo alifika Kituo cha Polisi Tarime akiwa na majeraha aliyopigwa wakati wa ugomvi na askari hao na kupewa PF 3 ya kupatiwa matibabu na kusalimisha silaha yake na baadaye kuwekwa chini ya ulinzi na kushitakiwa kwa kuua bila kukusudia amekaa rumande kwa miezi sita na kupewa dhamana,” alidai mwanasheria huyo wa serikali.

Wakili wa upande wa utetezi, Deus Mgengeri alimtetea mteja wake kuwa mtuhumiwa walikuwa hawana chuki wala fitina yoyote na marehemu, bali ni ugomvi uliotokana na kugonganishwa na mwanamke na kumshambulia Tumaini kwa kumpiga ngwara na kumuangusha chini akiwa na wenzake ambapo mtuhumiwa alitaka kujiokoa na kipigo kutoka kwa askari hao.

Hana rekodi mbaya ya makosa ya jinai na ni kosa lake la kwanza, hivyo akaomba Mahakama kumpa adhabu ndogo mteja wake. Jaji De-Mello alimhukumu mshitakiwa kwenda jela mwaka mmoja ili iwe fundisho kwa watu wengine.

Chanzo: Habari leo

UNAMTONGOZA, Anasema Anakuchukulia Kama Rafiki, Unajua Kwanini?

$
0
0

"Hataki muwe zaidi ya hapo, anakuchukulia kama rafiki!"


Stori inakwenda hivi; baada ya kumwangalia kwa muda mrefu, huyumwanamke anambae anakuuwa pole pole kwa mvuto wake, ambae anakila kitu ambacho wewe macho yako kwako unaona ndo kile kinachoitwa na kutengeneza uzuri usiopimika, ubongo wako unaamini ya kuwa mnaendana kwa kila kitu ila kinachokuchanganya ni wewe kutokua na uhakika iwapo na wewe unampendeza yeye, Kijana wa watu unajituma na kupiga moyo konde, leo hii unajikaza kiume na kwenda kumwambia yale yote yaliyo moyoni mwako... mara... 'kwaaa...' anakujibu, "Oho, lakini mbona mie siku zote huwa nakuona na kukuchukulia kama rafiki, kama rafiki.. rafiki tu!", moyo unapigwa na radi ya maumivu, na huamini kilichokupata, huku kichwani sauti ya "kama rafiki" ikijirudia rudia!.
Kama kungekua na kitu cha kuzuia hii dhihaka, ungetumia na kurudisha muda nyuma, kiume.com tumekusanya dalili zote za kuangalia kabla ya kupiga moyo kode na kwenda kumwambia yanayokusibu moyoni...
Anajiamini sana akiwa na wewe mpaka mazoea yake yamepitiliza...Msichana akiwa anajiamini sana kwako, ujue hapo umeshapoteza unachotamani na umeishia kunawa, kwa msichana akimuona mtu anayempenda kweli, utaona dalili...!, utaona hatulii, mara akae vizuri, na anakua anajihisi tu mda wote, atashika nywele zake kuangalia kama ziko vizuri, mapenzi asikuambie mtu kaka, mapenzi yanaleta kutokujiamini, na iwapo anajiamini sana kwako na ashtuki akikuona, wala atikisi hata ukucha basi hapo tafuta kitu kingine tu cha kufanya.
Anakupa hadithi za wanawake wengine... Msichana ambae yupo singo hana mpenzi, halafu ukiwa nae anakua anakupa stori za wasichana wengine, hapo anatumia janja ya nyani, hapo anakubadilisha akili usimwazie yeye na uwawazie hao wasichana wengine anaokupigisha stori, achana kabisa na haya maongezi, anaweza kukwambia.. "ooho, unaonaje nikikupigia pande kwa rafiki yangu Janeti, si ni mzuri eeh?", kaka hapo unapoteza mda tu.
Hafanyi kile unachotaka...Ukiona msichana hasikilizi kile unachotaka, yeye siku nzima anakuomba umsaidie hichi, twende pale.., we ukimwambia ya kwako anaruka maili tisa, ujue hapa huna chako, we upo pale ili akutumie tu na kwa sababu hana hisia nawe hajiulizi hata huyu jamaa anajisikiaje!.
Anatukana bila kujari uwepo wako...Maneno anayotumia ni kama yupo namwanamke mwenzie, na wala hashituki!, kaka hapa umeshakwenda na maji, mapenzi yana heshima na anayekupenda huwa anashituka akiona tu uwepo wako, na aibu yake sikuzote hua ipo karibu.
Hataki kuonekana na wewe sehemu za wazi...Ukimwambia tutoke wote, anakua na visingizio. Ukimwambia twende wote nikusindikize uendako, hata kama ni sokoni... utamsikia "ohhoo, mi nilishazoea kutembea mwenyewe wakati wote, mama atanielewa vibaya". Hapa ni kwamba anaogopa utamwalibia chansi ya kukutana na mwanaume wa ukweli achana na wewe masuruali tu, mama gani ambae hapendi mwanae aolewe?.
Anakuomba misaada mda wote...  Msichana mwenye hisia nawe hawezi kukuomba misaada ovyo hovyo, kwanza atakua hajiamini na hujiuliza maswali kama "Hivi atanionaje na atajifikiliaje nikimuomba hiki?".
Anakufanya kama spea tairi...Siku akikubali kutoka mtoko nawe, utashangaa kaja na mashoga zake!, hii anakua anafahamu kabisa kwa hio anakua anajihami ili usije ukapata chansi ya kuwa wewe na yeye. Yeye saa zote ni vicheko tu..., kidogo tu mara anaenda chooni, mwisho wa siku mbaba unaagwa usiku umeingia sie tunaenda.
hafanyi michezo yeyote ya kuwa karibu nae...Mwanamke akikupenda anatamani saa zote awe karibu nawe, mara mjikute mmeshikana mikono mda mrefu mpaka jasho, sasa huyu yeye atakua anakulia taimingi, anakua anahakikisha hakuna mguso wa ajabu ajabu, kaka mguso huleta hisia, na kama hana hisia kwako hawezi kufanya hivyo.
Anaongea na wanaume wengine mbele yako...Hivi hili si linaonekana kabisa, hili halina haja hata la kuliongelea, ila mtu akiwa amependa inawezekana kabisa asilione hata hili, anakua anajipa matumaini hewa!, huku kichwani akilipa sababu nyingine kabisa, "Oooh yuko sosho sana!".Kaka hapo kama msemo wa kiumeni.com usemavyo, "umeshaliwa kekundu".
 Hakutambulishi kwa rafiki zake...Hana hisia nawe atakutambulisha kwa nini?, labda kwa sababu vocha zote zinatoka kwako!, samahani kwa kuongea hivi najua nakukera ila ndo ukweli wenyewe, na hata ukitambulishwa, utatambulishwa kama rafiki tu, na hivyo ndo utabaki kuwa.
Cha kufanya jiongeze, na hata kama yeye ndo huwa anakupigia simu au anakufata na anaonyesha hisia ujue kuna kitu zaidi ya wewe kinachoendelea kumweka kwako.

Mume wa Shamsa Ford afunguka baada ya kudaiwa kumpiga

$
0
0


Shamsa Ford alidai kupigwa bila kukusudia wakati akiamulia ugomvi wa msichana wake wa kazi, lakini zipo taarifa zinasema majeraha hayo yametokana na kupigwa na mume wake Chidi Mapenzi baada ya kufumwa akinywa pombe. 

Ili kuujua ukweli wa tukio hilo Soudy amepiga story na Chidi Mapenzi na haya ndiyo aliyoyasema:”Siwezi kumpiga mke wangu. Wewe mwenyewe unanijua mimi siyo mgomvi. Nilitoka ofisini, nikamkuta mke wangu ameumia, nilipomuuliza nini tatizo, akanielezea. Nilipomuuliza unamjua mtu mwenyewe, akasema tumeyamaliza. Basi nikampeleka hospitali.” – Chidi Mapenzi.

HIZI Hapa Faida Za Maharage Meusi Mwilini..!!!

$
0
0

Baadhi  ya watu hawapendi kutumia maharage kama mboga kutokana na kuonekana kama ni chakula cha kimaskini, lakini kiafya maharage ni miongoni mwa mboga zenye faida kubwa mwilini na hutoa ahueni kubwa kwa watu wenye matatizo mbalimbali ya kiafya kama tutakavyoona leo katika makala haya;

Kwa mujibu wa utafiti mbalimbali, maharage, hasa meusi ni chanzo kizuri cha kirutubisho aina ya faiba kinachoshusha kiwango cha kolestro mwilini, vilevile kiwango cha faiba kilichomo kwenye maharage meusi, huweza kudhibiti kiwango cha sukari kisipande haraka baada ya chakula, hivyo kufanya maharage kuwa lishe nzuri kwa wagonjwa wa kisukari na shinikizo la juu la damu.

Iwapo utapata mchanganyiko wa maharage meusi na ule mchele ‘mweusi’ ambao haujakobolewa na kuondolewa virutubisho vyake muhimu brown rice, basi utaweza kupata kiasi kikubwa cha protini na faiba ambacho huwezi kupata kutoka katika chakula kingine.

Aidha, utafiti wa muda mrefu uliofanywa na jarida moja lijulikanalo kama Journal of Agriculture and Food Chemistry, unaonesha kuwa mbali ya maharage kuwa na kiwango kikubwa cha faiba, pia maharage yana virutubisho vingine vinavyojulikana kama Anthocyanins ambavyo hutoa kinga mwilini Antioxidant.

Kiwango cha virutubisho hivyo kilichomo kwenye maharage, kinaelezwa kuwa ni kikubwa kuliko hata kinachopatikana kwenye matunda kama zabibu ambayo inaaminika kuwa na kiwango kikubwa zaidi.

Inaelezwa pia kuwa, watafiti walipofanya tathmini ya ziada kwenye maharage, waliweza kubaini kuwa maharage yanapokuwa meusi zaidi, ndivyo ambavyo kiwango kikubwa cha kinga kinavyoweza kupatikana, yakifuatiwa na maharage ya rangi nyekundu, kahawia, njano na mwisho meupe.

Hii ina maana kwamba maharage meusi ndiyo yana virutubisho vingi zaidi kuliko maharage meupe na rangi nyingine.

RANGI Za Nyumba Zinazobamba Kwa Sasa..!!!

$
0
0

Ukuaji wa teknolojia umeongeza kwa kasi mabadiliko katika ujenzi wa nyumba zetu miaka ya nyuma wengi walipaka rangi cream au nyeupe kwa ndani tofauti na siku hizi ambapo rangi huchanganywa kwa teknolojia ya kisasa ya kutumia kompyuta na kupelekea kuongeza wigo mpana wa uchaguzi wa rangi za kupaka ndani na nje ya nyumba zetu.

Muhimu kuzingatia ni kuwa rangi hizi zinazong’aa kwasana mfano rangi ya machungwa “Orange” zinapendeza kupakwa katika ukuta mmoja tu kwa ndani na kwingine zinabaki rangi zisizo na kelele yaani zilizotulia zaidi.

kwenye vyumba vya watoto wa kiume wengi hupendelea blue wakati kwa wakike pink,purple na rangi ya machugwa “orange” au rangi ya kijani “green” hupendeza zaidi.

Utakapohitaji kununua rangi za nyumba yako ni muhimu kujua ni rangi ipi ipo katika wakati, siku hizi rangi hata gypsum zinapendeza ukiweka tofauti na nyeupe kama wengi walivyozoea.
Viewing all 104795 articles
Browse latest View live




Latest Images