Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live

NAY wa Mitego Amjibu Shombo Yusuph Mlela..Adai Hawezi Kupigana Naye Kwakuwa Ametolewa 'Marinda'...!!!

$
0
0

Msanii Nay Wa Mitego Amesema Hayo Kufuatia Kauli Ya Msanii Wa Bongo Movie Yusuphu Mlela Kutangaza Kuwa Anataka Vita Na Nay Wa Mitego Kwa Kuingilia Masuala Yao Ya Maandamano Kupinga Cd Za Nje Kuuzwa Bei Rahisi Kuliko Kazi Zao.Hata Hivyo Nay Wa Mitego Hakuishia Hapo Naye Akajibu Kwakusema Hawezi Kupigana Na Wanaume Wa Bongo Movie Waliotolewa Marinda

HIMID Mao wa Azam Aitangazia Simba Sc Vita..Awaambia Waje Tu Kichwakichwa Wale za Uso..!!!

$
0
0

Nahodha msaidizi wa Azam FC Himid Mao amesema, kikosi kizima kinamorali kubwa ya kupata matokeo mazuri kuelekea mchezo wa Kombe la Shirikisho (FA) Tanzania Bara dhidi ya Simba mchezo utakaopigwa Jumamosi ya Aprili 29 Uwanja wa Taifa jijini DSM.

Himid amesema, kikosi kipo vizuri na watanufaika na urejeo wa wachezaji muhimu waliokuwa majeruhi.

“Morali iko juu, timu ipo vizuri bahati nzuri wachezaji wenzetu karibia asilimia 90 wapo vizuri na wapo fiti na wako tayari kwa mchezo na naamini kocha atakuwa na nafasi nzuri ya kuchagua timu yake ya kwenda kucheza mchezo huo,” amesema Himid Mao

Kiungo huyo anayesifika kwa ukabaji na mwenye mashuti makali, aliongeza kuwa mchezo huo utakuwa mgumu licha ya kufanikiwa kuwafunga mara mbili katika mechi mbili zilizopita.

“Usidhani kama mchezo huu wa tatu utakuwa mrahisi kama mara mbili zilizopita tulizoshinda, kwani Simba nayo inajipanga, lakini naamini sisi tutajipanga vizuri zaidi ili kuweza kushinda mechi hiyo inayokuja,” alisisitiza Himid Mao 

Himid ambaye amekulia kwenye timu hiyo kwa takribani miaka tisa sasa, alitoa wito kwa mashabiki wa Azam FC kujitokeza kwa wingi kwenye mchezo huo ili kuwapa sapoti kwani wao ni sehemu muhimu sana katika timu na uwepo wao utawaongezea nguvu zaidi uwanjani ya kuibuka kidedea.

Kikosi cha Azam FC kipo kwenye maandalizi makali kuelekea mchezo huo, ambapo tayari kimeshaingia kambini hapo jana.

CUF-Maalim Yaiuliza Maswali CUF-Lipumba..!!!

$
0
0

Mkurugenzi wa Habari, Uenezi na Mahusiano wa CUF –Maalim, Salim Bimani ameshangazwa na kauli ya wafuasi wa CUF-Lipumba kuwa waliovamia mkutano wa Vina wiki iliyopita ni walinzi wa chama hicho waliokuwa doria.

Pia Bimani amewahoji CUF –Lipumba maswali mawili. La kwanza ni kwa nini wafanye doria ghorofa ya nne wakati wao sio askari? Swali jingine alilolihoji Bimani ni kwa nini walikuja na bastola?

Jana, Mkurugenzi wa Habari wa CUF-Lipumba, Maulid Kambaya alisema aliyekatwa kisigino ni mlinzi wa chama aliyekwenda kufanya doria na kuwa hakupigwa na wananchi bali wafuasi wa CUF-Maalim.

  Lakini Bimani alisema:

“Umesema Kambaya anasema walikuwa katika doria? Mngemuuliza doria gani inafanyika floor ya nne wakati wao siyo askari huu ni uongo wa mchana kweupe,”alisema Bimani.

Alisisitiza kuwa upande wa Profesa Lipumba ndiyo unao husika na tukio hilo, kwani siyo mara kwanza kutuma kundi kama hilo kufanya vurugu wakiwa na silaha mbalimbali

Kwa mujibu wa Bimani, kundi hilo lilishafanya vurugu katika mahakama kuu hivyo hakuna cha kujitetea badala yake mamlaka husika ziwachukulie hatua kwa kitendo hicho.

“Yule kijana aliyejeruhiwa na wananchi ambao walimdhibiti, siyo upande wa Maalim kama anayodai Kambaya.Hivi Kambaya kusoma hajui hata picha haoni kujua nani aliyehusika,”alihoji Bimani.   

Jinsi Masaju, Jenista Walivyohangaika na Lissu bungeni

$
0
0

WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Ajira, Kazi, Vijana na wenye Ulemavu), Jenista Mhagama na Mwanasheria Mkuu wa Serikali, George Masaju jana walikuwa na kazi ya ziada ya kumwongoza Msemaji Mkuu wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni kwa Wizara ya Katiba na Sheria, Tundu Lissu kuisoma hotuba yake iliyoonekana kuwa na dosari kutokana na kuwa na maneno yenye ukakasi. 

Hali hiyo iliibuka baada ya Mwenyekiti wa Bunge, Andrew Chenge kumwita Lissu kuwasilisha hotuba yake. Kabla ya kuanza kusoma, Jenista ambaye pia ni Mnadhimu Mkuu wa Serikali alimuomba Mwenyekiti kuizuia hotuba hiyo kwa kuwa imejaa maneno ambayo masuala yake yapo mahakamani na pia amezungumzia mwenendo wa Rais, jambo ambalo ni kinyume cha Kanuni za Bunge. 

Alisema hotuba hiyo ina mambo mengi yanayokiuka kanuni. Alisema katika hotuba hiyo kuna mambo ya mienendo ya kesi ambazo zipo mahakamani, jambo ambalo ni kinyume na kanuni na pia, kuna mambo yanayozungumzia mwenendo wa Rais, jambo ambalo ni kinyume cha Kanuni Kifungu 64 (1) (e). “Naomba nitoe utaratibu ni kwanini hoja hii irudishwe mezani kwako na maeneo yanayokiuka kanuni hizi yaweze kuondolewa na ndipo iweze kuwasilishwa ndani ya Bunge hili,” alisema Waziri Mhagama. 

Hata hivyo, Chenge alimruhusu Lissu kusoma hotuba yake huku akimtaka Waziri Mhagama kuainisha maeneo yaliyokuwa na maneno yenye ukakasi. Wakati huo Lissu alianza kusoma hotuba yake, lakini Chenge alimkatisha na kumtaka kuyafuta maneno hayo, kwa kuwa hayapo kwenye hotuba yake na kumtaka kwenda moja kwa moja kwenye hotuba. 

Akisoma hotuba hiyo, Lissu alisema hiyo ni mara yake ya saba kusimama mbele ya Bunge kutoa maoni ya kambi rasmi ya upinzani kuhusu Wizara ya Mambo ya Katiba na Sheria na ameshangaa kuona Wizara hiyo imekuwa ikiongoza kwa kuwa na mabadiliko mengi ya mawaziri kuliko wizara nyingine. Alisema baada ya Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2010, alianza Celina Kombani (sasa marehemu) kisha wakafuata Mathias Chakawe, Dk Asha-Rose Migiro, Dk Harrison Mwanyembe na sasa Profesa Palamagamba Kabudi. 

Alisema ingawa Profesa Kabudi anaweza kuwa mgeni bungeni, lakini si katika uelewa wa matatizo makubwa ya kisiasa na kikatiba nchini. Alimkumbusha majukumu makubwa na mazito anayolazimika kuyabeba kwa nafasi yake hiyo.

UNGA Wamchanganya Zitto Kabwe..!!!

$
0
0

Mbunge wa Kigoma mjini kwa tiketi ya ACT Wazalendo Mhe. Zitto Kabwe amefunguka na kusema bei ya unga wa ugali sasa ni juu kuliko hata bei ya mafuta ya magari jambo ambalo linafanya wananchi kuumia na gharama hizi za chakula.

Zitto Kabwe amesema hayo kupitia mtandao wake wa Facebook na kusema bei hizi za chukula zipo juu sana na kufanya wananchi kuingia kwenye umasikini  

"Bei ya Unga wa Sembe 1kg TZS 2,300/= ( wastani ). Bei ya Mafuta ya Petroli 1lita TZS 2,060/= ( wastani). Kwa mara ya kwanza Ugali umekuwa ghali kuliko mafuta ya gari. Gharama hizi za maisha Kwa wananchi ni kubwa mno, hazistahmiliki na zinaingiza raia wengi kwenye umasikini. Serikali ipo kimya kana kwamba kila kitu kipo sawa" alisema Zitto Kabwe 

Haya Ndio Madhara 12 ya Kujichubua Ngozi

$
0
0

Tabia ya kujichubua ilianza kupata umaarufu kwanzia mika ya 1980 mpaka miaka ya hivi karibuni, hii hasa kwenye nchi za watu ambao hawana ngozi nyeupe kabisa kama waarabu, wahindi na waafrika. biashara hii imewafanya watu wanaotengeneza bidhaa hizi kua matajiri sana huku zikiacha madhara makubwa kwa watumiaji.
kitaalamu  matibabu dawa kujichubua yalitakiwa yatolewe kitaalamu kwa ajili ya kuondoa mabaka ya ngozi na kuondoa makunyazi ya uzee lakini chini ya usimamizi maalumu wa daktari na matumizi yake yawe ya muda fulani tu kama dozi ya dawa lakini hali hii imekua tofauti kwani kemikali hizi zimekua zikitumika bila usimamizi na kusababisha madhara makubwa kwa watumiaji.
kwa hapa tanzania tafiti zinaonyesha zaidi ya asilimia 70 ya wanawake hutumia dawa za kujichubua na huku asilimia mbili mpaka tano ya wanaume hutumia pia.
kuna aina tatu ya madawa hayo, dawa za kumeza, dawa za kupaka, dawaza kuchoma sindano na njia ya upasuaji lakini kwa hapa kwetu wengi hutumia za kupaka na wachache za kunywa.
watu wengi wamekua wakiiga wasanii wa nje kama marekani huku wakishindwa kujua kwamba wale pale wanafanya vile kwa usimamizi wa madaktari bingwa wa ngozi na kwa  dozi maalumu ili wasipate madhara yeyote.
serikali imekua ikijitahidi kuyapiga marufuku madawa hayo bila mafanikio kwani watu wengi huyapitisha na kuyatumia kwa magendo wakidhani wanaikomoa serikali bila kujua wanajiua wenyewe.
yafuatayo ni madhara yatokanayo na kujichubua ngozi..
kansa ya ngozi;dawa za kujichubua zina kemikali kuu mbili yaani hydroquinone na mercury, lakini dawa nyingi zinazopatikana mtaani zina mchanganyiko wa steroids, tretinion, na hydroquinone. kemikali hizi ni moja ya vyanzo vikuu vya kansa ya ngozi na kuharibu maini.


Kuongezeka kwa weusi wa ngozi;matumizi ya kemikali kama hydroquinone 2% kwa muda wa miezi mitatu mfululizo huweza kusababisha ngozi kua nyeusi zaidi na kukataa matibabu yeyote ya kuirudisha kwenye hali yake ya kawaida. lakini pia matumizi makubwa ya vipodozi hivi husababisha sehemu kama za vidole, miguu na masikio kua nyeusi zaidi kuliko sehemu zingine.
                                                      


Ngozi kua nyembamba sana; hii husababishwa na kemikali ambazo hupunguza sana unene wa ngozi, ngozi hii honyesha mishipa ya ndani ya damu na ni rahisi sana kuumia na kuvuja damu kirahisi.                                 
Vidonda visivyopona; kawaida ngozi ya mtu wa kawaida huweza kupona yenyewe ikiumia bila kutumia dawa yeyote lakini matumizi ya kemikali za kujichubua husababisha ngozi kupoteza uwezo wake wa kupona wenyewe.

Kuungua na mapele ya ngozi;kemikali hizi huweza kuunguza ngozi na kufanya iwe na mabaka baka, chunusi, harara na ngozi isiyokua na afya. kemikali ya hydroquinone hufanya kazi ya kuzuia ngozi kutengeneza kitu kinachoitwa melanin ambacho ni muhimu kwa ajili ya kuleta rangi ya ngozi.
                                          
Magonjwa ya ngozi; tafiti nyingi zilizofanywa na madaktari wa ngozi zimegundua kwamba watu wengi wanaosumbuliwa na magonjwa mbalimbali ya ngozi kama upele, miwasho, fangasi na aleji ni watu wanaotumia kemikali hizi hatari za kujichubua.
                                         

Huingiza sumu za ndani ya mwili; moja ya madhara makubwa ya kutumia kemikali za kuchubua rangi ya ngozi ni kuingiza sumu mwilini. sumu hizi huingia ndani ya mwili kupitia ndani ya ngozi, kwa vidonge vya kujichubua au sindano zinazotumika kwa kazi hii. madhara yake ni kuharibika kwa figo, kuharibika kwa ngozi, kinga ya mwili kushuka, kupata ngazi sehemu mbalimbali za mwili.
                                                      

Kubadilika kwa ngozi ya uso; hali hii hutokea pale ngozi ya uso inakua nyembamba sana kuliko sehemu zingine za mwili na husababisha kubadilika kwa ngozi ya uso na kua na hali tofauti kabisa.
                                                    

Kuathirika kisaikolijia; watu wengi waliojichubua na kupata madhara wanakosa amani wakiwa mbele za watu kwa kuhisi kwamba wanasemwa sana kulingana na hali yao ya sasa ilivyo, hii huwanyima uhuru na kuwafanya wawe watu wa kukaa ndani tu au kuvaa nguo za kuficha sura zao muda mwingi.
                                            
Kuharibu watoto tumboni; kemikali za kujichubua zina uwezo wa kuingia mpaka kwenye kizazi cha mama mjamzito, hali hii huweza kusababisha kuzaliwa kwa mtoto mwenye upungufu wa viungo fulani vya mwili kama mkono mmoja au mguu mmoja.


Upofu; kemikali za kuchubua ngozi ambazo hupakwa usoni zina uwezo wa kuharibu macho na kumfanya mtu awe kipofu kabisa, mimi binafsi nimeshuhudia watu waliopata upofu sababu ya kujichubua ngozi.



michirizi ya ngozi; kwasasa kuna wanawake wengi sana wanasumbuliwa na tatizo la michirizi ya ngozi, japokua michirizi hii huletwa na unene auujauzito lakini kujichubua pia moja ya vyanzo vikuu vya hali hii.

mwisho; kama wewe ndio unaanza kujichubua basi ujue uko kwenye hatari kubwa, inawezekana kwa sasa mambo yako ni safi kwamba umeshakua mweupe na kila mtu anakusifia lakini naomba nikwambie mbio zako za sakafuni zina ukingo..... kama umeshaathirika tayari basi ni wakati wa kuacha na kuomba msaada wa matibabu ili urudi kwenye hali yako ya kawaida. sasa hivi kuna kampuni nyingi za nje zinauza dawa kwa ajili ya matibabu ya waathirika wa hali hii.pia unaweza ukawasilaina na sisi na ukapata matibabu popote ulipo.

YAJUE Majina ya Wanaume na Sifa Zao Katika Mapenzi..Tazama Jina Lako Kisha Utuambie Kama Uko Hivyo..!!!

$
0
0

1. Andrew-mapenzi ya tamthiliya
2. Nicolas-muongo
3. Albert-domo zege ila mjanja mjanja
4. Mathias-anapenda mwanamke kwa muda mrefu
5. Joseph/Josephat/yusuph-kicheche
6. Jeryson-anapenda mademu ila wanawake wanamkataa
7. Shadrack-anapenda sifa kwa mademu
8. Richard-ana wapenzi wengi ila msiri
9. Mathew-anapendwa na wanawake ila domo zege
10. Thomas-anapendwa na mademu ila hajatulia
11. Prosper-hajui habari za mapenzi
12. Fidelis-mtaalam wa kutongozea mademu wenzie (kuwadi)
13. Aaron-maneno mengi ila vitendo sifuri
14. Costantine-wanapenda kutongoza hovyo ingawaje wana mpenzi mwaminifu
15. Elvis-handsome ila hapendwi na mademu
16. Edward-serious sana kwenye mapenzi
17. Moses/Mussa-mwepesi kutongoza na mwepesi kuwacha
18. Ally/Elly-wasiri sana kwenye mapenzi
19. Mohammedy-anapenda watu waliomzidi umri
20. Nickson-wakiingia kwenye mapenzi wanatendwa vibaya
21. Alpha-wanapenda sifa kwa wanawake ili wapendwe
22. Jimmy-wana mapenzi ya kejeli
23. Elias-wanapenda mademu ila wanaogopa kuwaambia
24. Frank-huyu mpole wanawake wanajitongozesha wenyewe
25. Joachim-hana habari na mademu,anaamini ipo ataoa tu
26. Omary-anapenda achape tu atembee
27. Steven-hana habari kabisa na wanawake ila ana bahati ya kupendwa
28. Gerald-mpole na antulia na mpenzi mmoja kwa mda mrefu
29. Elisha-anapenda wanawake wanaochukiwa katika jamii
30. Benard-akipenda kapenda
31. Juma-hawa kazi yao ni kuchafua wanawake wa mtaani na jamii inayozungukwa
32. Kassimu- anapend utukufu na kusifiwa hata na mkewe
33. Khalid -msumbufu na anapenda kupedwa kuliko kupenda wanawake
34. Daniel-anawivu sana mjanja na anapenda kujua mambo yaliyojuu ya uwezo wake.
35. Said-hajui kupenda na huwa anatamaa hasa kwa bint weupe.
36. Rajabu-mgumu kumuamin mwenza wake.
37. David-Kupenda kujionesha mbele ya wanawake kwamba anauwezo mkubwa hata kama hana.
38. Farid-Mpenda wanawake warefu wenye mwanya na shepu.
39. Rama-hupenda kusikilizwa yeye tuu na anapenda wanawake wenye makalio makubwa hasa wanene.
40. Seleman-anapenda ngono.
41. Issa -huwa na msimamo hasa katika maamuzi yake hat kwa mwenza wake
42. Fadhili- vitu vyake ni vya siri saana na hata mwenza wake ni ngumu kujua
43. Charles -Hapend kudumu katika mahusiano na hupenda kuwa pek yake
44. Karimu- hupenda kuwa na wanawake weupe
45. Laurence-hunyanyasika kwenye mahusiano hata huweza kulia hovyo
46. Masoud- anajua kujali na kuheshimu ndoa yake ila mkali sana.
47.Hamad-mpole pia hapend kutoa siri zake kwa mwenza wake pia hupend kunyenyekew na mpenz wake
48. Hasani -hupenda kupewa kuliko kutoa hata kwa wenza Wap
49. Alen-hupenda kulaumu hata kwa jambo dogo na hupend wanawak weupe
50. Luka- wanapenda kwa mda ukijichanganya utaumia ukiwa nae.
51. Jafari- Hupenda wake za watu.

Je wewe jina lako lipi?

MAMBO 5 Yakumfanya Mwanamke Avumilie Kwenye Ndoa..!!!

$
0
0

Mahusiano mazuri kwa wanandoa au watu walio kwenye mahusiano ya kimapenzi ni moja ya mambo yanayochangia wahusika pia kuwa na afya njema na hata kuepuka baadhi ya matatizo kiafya.


Leo nmeona nikuletee mambo matano muhimu ambayo mwanamke hupenda atimiziwe na mume wake.

1. Kudekezwa & Kubembelezwa
Wanawake hupenda kubembelezwa pale wanapokuwa na huzuni, lakini pia wengi hupenda kuungwa mkono katika maamuzi yao au mawazo yao. Hivyo basi ili mwanaume uweze kumteka mwanamke wao ni lazima ujitahidi kuwa mkarimu na mwenye lugha nzuri za kubembeleza kwa mkeo.


2. Kusikilizwa shida

Wanawake hupenda pale wanapoeleza shida zao wasikilizwe vizuri na kutatuliwa matatizo yao. Inawezekana hayo matatizo yakatatuliwa kwa kuwezeshwa kifedha au hata ushari pia wakati mwingine.

3. Kuwa mstari wa mbele

Wanawake muda wote hupenda kuoneshwa kuwa wao ni wathamani kuliko wengine hivyo huhitaji kuwekwa mstari wa mbele katika mambo yao. Hali ambayo huwafanya wao kuhisi wanapendwa zaidi.

4. Kufurahishwa kwenye ndoa

Hakikisha wewe kama ni mwanaume basi katika sekta hii uwe umekamili kiasi cha kutosha yaani hata kama huna fedha, lakini hakikisha eneo hili unaliweza vizuri na unalifanya kwa ufanisi zaidi kila unapokutana na mkeo. Kwani uwapo dhaifu eneo hili basi ni rahisi sana kuyumbisha mahusiano yenu au ndoa yenu.

Kimsingi wewe kama mwanaume ni lazima utambue kuwa unawajibu wa kuhakikisha unamridhisha mpenzi/mke wako katika tendo hilo.

5. Nafasi ya kuzungumza

Kwa kawaida wanawake hupenda zaidi kujieleza kuhusu hisia zao au mambo yao kwa wale wanaohisi wanawapenda, hivyo mwanaume lazima uhakikishe unatenga muda wa kuzungumza na mpenzi wako na kumsikiliza kuhusu mambo yake na kuyafanyia kazi pale yanapoonekana yanawezekana.

Kimsingi mambo hayo yote au machache kati ya hayo yakitokea yakakosekana ndani ya ndoa kwa mda wa kipindi fulani huweza kupelekea mwanamke kuondoka na ndoa kuvunjika hivyo ni muhimu kwa wanaume kuyazingatia hayo.


HIZI Hapa Sababu Zitakazokufanya Usiache Kula Ndizi Kamwe..!!!

$
0
0

Mara kadhaa tumekuwa tukizungumza faida za matunda kiafya, lakini leo napenda tuzungumze tena kuhusu sababu hizi muhimu ambazo zitakufanya utumie ndizi kama tunda muhimu kwa afya yako.

Sababu zifuatazo zitakufanya usiache kutumia ndizi kama tunda.

Ni tunda ambalo limesheheni madini ya potassium ambayo huweza kusaidia kuweka uwiano katika kiwango cha msukumo wa damu ndani ya mwili na hivyo kulinda afya ya moyo kwa ujumla.

Aidha ndizi zinaelezwa kuwa na uwezo wa kupambana na matatizo ya kupooza yaani stroke endapo tunda hilo litatumika mara kwa mara.

Kwa mujibu wa utafiti uliochapishwa kwenye jarida la 'American Heart Association' lilieleza kuwa ndizi zinauwezo wa kupunguza tatizo la kupooza kwa asilimia 20 ikiwa tunda hilo litaliwa mara kwa mara.

Pamoja na hayo ndizi zinasifika kwa kuongeza nguvu kwa haraka ndani ya mwili, hivyo ni tunda ambalo linashauriwa kutumiwa na wanamichezo pia.

Ndizi pia huboresha mfumo wa umeng'enyaji chakula tumboni kwa sababu tumbo hilo lina kiwango cha fiber pia.

Mbali na hayo ndizi pia ni nzuri kwa wenye vidonda vya tumbo pamoja na matatizo ya kiungulia cha mara kwa mara.

AINA za Vyakula Vinavyoongeza Uhodari kwa Wanaume..!!!

$
0
0

Vyakula jamii ya nafaka ni miongoni mwa vyakula ambavyo vimejaa nishati nyingi ikiwa ni pamoja na nyuzinyuzi na sukari. Hivyo unaweza kuweka kwenye orodha ya vyakula anavyopaswa kula mwanaume.

Nafaka husaidia kuzalisha homoni ya testosterone kwenye damu hivyo kumuwezesha mtu kuwa na nguvu na hivyo kuepuka tatizo la upungufu wa nguvu za kiume.

Ulaji wa vyakula vya nafaka visivyokobolewa ni muhimu zaidi kwani husaidia kutokupa mwili wa mafuta mengi kwani mafuta mengi ndani ya mwili huweza kuchangia kuharibu mishipa ya damu ikiwamo mishipa uume.

Moja ya viungo muhimu kwa wanaume ni pamoja na tangawizi ambayo husaidia kusisimua mfumo wa mzunguko wa damu mwilini ieleweke kwamba mzunguko wa damu unapokuwa vizuri ndani ya mwili husaidia hata damu kwenda vizuri sehemu za viungo vya uzazi pia (uume).

Aidha, ulaji wa karanga ni muhimu pia kwani ndani ya karanga kuna madini ya magnesium,zinc ambayo ni muhimu sana katika uzalishaji wa mbegu za kiume pamoja na kuamsha hisia za tendo la ndoa.

Pia matumizi ya tunda la komamanga huweza kumsaidia mwanaume kujenga afya ya kimahusiano kutokana na tunda hilo kusaidia kuamsha mishipa ya fahamu na hivyo kumuongezea mtu uwezo wa kushiriki tendo hilo.

TABIA 3 za Wanawake Zinazochangia Mwanaume Kuwa na Upungufu wa Nguvu za Kiume..!!!

$
0
0

Upungufu wa nguvu za kiume huweza kuchangiwa na sababu mbalimbali, ikiwa ni pamoja na magonjwa. 

Wanaume wanaougua maradhi ya kisukari huweza kuwa katika hatari kubwa ya kukubwa na upungufu wa nguvu za kiume kuliko wanaume wasio na maradhi hayo. 

Inapotokea sukari haikudhibitiwa katika damu huweza kusababisha kuharibika kwa neva na misuli midogo inayodhibiti kusimama kwa uume.

Hata hivyo, mbali na sababu hizo za magonjwa pia kuna sababu nyingine za kibinadamu ambazo huweza kuchangia tatizo hilo la upungufu wa nguvu za kiume ikiwemo hizi zifuatazo ambazo huchangiwa na wanawake.

Usafi kwa mwanamke:
Hali ya usafi ni muhimu hasa zile sehemu muhimu ambazo huusika kwenye tendo la ndoa endapo mwanamke atakuwa si msafi basi huweza kumsababishia mwanaume matatizo ya upungufu wa nguvu za kiume. 

Naamini kwamba kila mtu hupenda usafi na wengi wetu tunafahamu kero za uchafu wakati wa tendo, kwa mantiki hiyo ni wazi kuwa mwanamke akiwa mchafu huweza kusababisha mwanaume kupoteze msisimko na uwezo wa tendo la ndoa. 

Mwanamke kuwa msafi ni muhimu sana, kuanzia mavazi na mwili pia hii itasaidia kuleta msisimko zaidi katika mapenzi.

Kutokuwa na uhodari na ujuzi
Wanawake wengi huhofia sana kuonesha ujuzi wao wa kimapenzi wanapokuwa na wapenzi wao, huku wengi wakiogopa kuhisiwa huenda ni wazoefu zaidi katika masuala hayo ya kimapenzi, lakini si kweli ujuzi na uhodari kwa mwanamke ni muhimu zaidi kwani huleta hamasa kwa mwanaume na hivyo kumsaidia kuepukana na shida ya upungufu wa nguvu za kiume.

Tatizo hili lipo zaidi kwa wanawake ambao tayari wapo ndani ya ndoa, wengi wao huwa hawajishughulishi kumsaidia mwanaume kupata mihemko zaidi na wala hawana ubunifu jambo ambalo humfanya mwanaume kushiriki tendo kwa kutegemea hisia zake mwenyewe pekee, hali ambayo si nzuri kwani mwanaume ikitokea atakuwa na mawazo au kuchoka hatoweza kupata mhemko kwasababu hapati ushirikiano toka kwa mwenzake (mwamke).

Karaha za maneno
Pale inapotokea mwanamke akawa ni mwingi wa maneno ya kashfa, dharau na matusi basi hali hiyo huweza kumfanya mume amchukie na kutopenda kushiriki naye tendo. Jambo ambalo baadaye husababisha wanaume wengi kuanza kutoka nje ya ndoa zao.

MAAJABU ya Dunia… Binti Darasa la 7 Aota Matiti Manne..!!!!

$
0
0

Ukistaajabu ya Musa utayaona ya Firauni! Hivyo ndivyo unavyoweza kusema kufuatia familia moja kukumbwa na mauzauza baada ya watoto wa mama aliyefahamika kwa jina la Hawa Hassan Ngonyani kupatwa na mabadiliko ya maumbile ambapo mmoja ameota matiti na mwingine kuanza kuotwa na uvimbe shingoni.

Hawa anaishi na wanaye watatu maeneo ya Kinzudi Kata ya Goba, jijini Dar ambapo waandishi wetu walifika na kujionea hali halisi ya watoto hao.

Mara baada ya waandishi wetu kufika katika nyumba hiyo, walipokelewa na Hawa aliyeonekana kukata tamaa ya maisha kutokana na jinsi anavyoishi kwa malumbano na mumewe anayedaiwa kuitelekeza familia yake.

Akizungumza na mwandishi wetu nyumbani hapo, Hawa alisema aliolewa ndoa ya mkeka miaka kadhaa iliyopita huku mwanaume akimzalisha ‘fastafasta’.

Alisema mwanaye mwenye umri wa miaka kumi na mbili anayesoma darasa la saba katika Shule ya Msingi Kinzudi, alizaliwa mzima huku akiwa na chuchu mbili tu hadi mwaka jana mwanzoni ndipo alipokumbwa na balaa hilo la kuota chuchu zingine sehemu za juu ya titi za kawaida ambazo hadi sasa zinazidi kukua siku hadi siku.

Akizidi kufafanua, mama huyo alisema mara baada ya kuona hali hiyo, aliamua kumshirikisha baba watoto wake ambaye ni kama amehama kabisa nyumbani, lakini alikosa ushirikiano kwa mumewe huyo kwani hadi sasa mtoto hajapelekwa hospitali kufanyiwa uchunguzi, kwani zile chuchu zinazidi kukua pamoja na kumkosesha amani mtoto huyo anayejiandaa na mitihani ya kuhitimu darasa la saba.

Hawa alisema wakati akihangaika na mwanaye huyo wa kwanza namna ya kumpeleka hospitali bila msaada, mtoto wake mwingine ameanza kuota uvimbe shingoni ambao unahitaji jitihada za haraka kuutibu kabla haujawa mkubwa.

Na alipomueleza tena mumewe, pia hakumpa ushirikiano.

“Yaani alichonijibu ni kuwa yeye kwa sasa ana madeni mengi hivyo hana fedha, nifanye michakato mingine nikawatibu yeye hana hela kwa sasa,” alisema bi mkubwa huyo huku akibubujikwa na machozi.

Hata hivyo, dada huyo alisema mumewe ni mkorofi kwani pia amewahi kumpiga hadi kusaidiwa na majirani.

Mwanamke huyo alihitimisha kuomba msaada kwa taasisi na mashirika ya utetezi wa haki za binadamu wamsaidie kumuachanisha na mwanaume huyo ambaye pia inadaiwa hutumia kilevi.

Hawa alisema anahofia usalama wake kutokana na kupigwa mara kwa mara na mbaya zaidi wakati anampiga huwa anamvua nguo zote na kumdhalilisha mbele ya watoto hivyo kukimbilia kwa majirani akiwa mtupu.

Aidha, pia mtoto huyo mwenye tatizo la kuota matiti ya ziada, alisema anaamini manyanyaso ya kutopewa huduma na mama yake kudhalilishwa vinatokana na mchepuko wa baba yake ambapo kuna siku alinasa mazungumzo live ya baba yake akiongea na mchepuko wake, lakini kikubwa kinachomuuma ni kulala na njaa au kunywa uji ambao hauna sukari.

Kufuatia tuhuma hizo, gazeti hili lilimsaka baba wa watoto hao aliyefahamika kwa jina la Abdul Liloka ili kuelezea kwa nini amekuwa akiinyima haki za msingi familia yake na hapa anaelezea tuhuma hizo:

“Ndugu mwandishi kwanza ni kweli mke wangu alinipatia taarifa za wanangu kuumwa lakini hali ya Magufuli sasa ni ngumu, mimi nilikuwa na madeni kibao ila kwa sasa nimemaliza nikipata hela nitampeleka hospitali huyu mdogo mwenye uvimbe.”

Kuhusu huyu mwingine mwenye matiti manne pia alisema: “Jamani hayo maziwa yaliyoota huo ndiyo utamaduni wa familia yetu, wapo dada zangu wengi wameota pia kwa hiyo hapo hamna tatizo tena bora hata yeye ni madogo yupo shangazi yake mmoja anayo makubwa balaa.”

Alipoulizwa kuhusu tuhuma za kuitesa familia yake kutokana na kuwa na mchepuko, Liloka alisema:

“Jamani mimi ni Muislam nina haki ya kuoa hata wanawake kumi si uwezo wangu, ni kweli nina mchumba mwingine nje hata huyo aliyewapa taarifa kwa maana ya mke wangu anamjua sana na kuhusu kumpiga ni kweli kuna siku nilimpiga kofi moja tu!”




JUKWAA la Wahariri (TEF) Lamkaa Koo Profesa Ibrahim Lipumba......Lamtaka Atoe Maelezo Sakata la CUF Kuvamiwa na Waandishi Kupigwa..!!!

$
0
0

Jukwaa la Wahariri nchini (TEF) limelaani kitendo cha waandishi wa habari kujeruhiwa katika tukio la uvamizi lililotokea katika mkutano wa CUF katika hotel ya Vina kata ya Mabibo ambapo waandishi wa habari walipigwa na kujeruhiwa

Katika taarifa hiyo ya (TEF) imemtaka Profesa Lipumba kujitokeza na kukiri na kuomba radhi kwa waandishi wa habari pamoja na Watanzania kufuatia tukio hilo kama alivyofanya Maalim Seif

"Tunamtaka Profesa Lipumba binafsi atoe kauli kuhusu tukio hili kama alivyofanya Maalim Seif ambaye binafsi aliandika barua rasmi kwa uongozi wa TEF akilaani kupigwa kwa waandishi wa habari na kutoa pole kwa wale waliomizwa na kupata mshtuko" Walisema viongozi wa TEF

Taarifa hiyo ya TEF ilikwenda mbali zaidi na kuwatahadharisha waandishi wa habari, wahariri kuwa wanapaswa kuwa makini pindi wanapokuwa wanaitwa na kundi hili la Lipumba kwa ajili ya kutoa habari zao 

MFAHAMU Rais Mpya wa Ufaransa Emmanuel Marcon..Amemuoa Mwalimu Wake Aliyemzidi Zaidi ya Miaka 24..Alianza Kutembea Naye Toka Akiwa na Miaka 17..!!

$
0
0

EMMANUEL MARCON mwenye umri wa miaka 39 ndiye anayetarajiwa kuwa rais ajaye wa Ufaransa.

Pamoja na hayo, Marcon ambaye ameoa mke mwenye umri wa miaka 64 ,ana mambo mengi ya kufurahisha na kuvutia maishani mwake hususan kuhusiana na mkewe huyo ambaye anamzidi umri kwa kiasi cha miaka  zaidi ya 24.

Mkewe huyo alikuwa ni mwalimu wake wa darasa miaka ipatayo 24 iliyopita ambapo mwalimu wake wa darasa wakati huo alikuwa na binti ambaye alikuwa mwanafunzi mwenzake darasa moja.  Wakati huo, kila mtu, wakiwemo wazazi wake Marcon, walifikiri binti huyo wa mwalimu alikuwa rafiki yake, wakati hawakuwa hivyo.

Katika mlolongo huo wa vituko, Marcon alijikuta katika mapenzi na mwalimu wake wakati yeye akiwa na umri wa miaka 15 ambapo wakati huo, mwalimu huyo alikuwa ameolewa akiishi kwa furaha na akiwa na watoto watatu

Alipofikisha umri wa miaka 17, aliamua kumuoa mwalimu huyo, wakati huo akiwa na umri wa miaka 42.

apendanao hao walifunga pingu za upendo mwaka 2007 wakati huo ‘mlume’ huyo akiwa na umri wa miaka 30 na ‘mrembo’ wake akiwa anapiga hodi katika umri wa miaka 55.

Mwanandoa huyo wa kiume anatarajiwa kuapishwa kuwa Rais wa Ufaransa mwezi ujao akiwa amebakiza miezi sita kufikisha umri wa miaka 40 wakati ambapo kipenzi chake, yaani mkewe,  ana watoto  (watu wazima) watatu na wajukuu saba sasa.

Ni vyema pia kufahamu kwamba mtoto wa kwanza wa mkewe huyo anamzidi Marcon kwa umri wa miaka miwili, wakati ambapo mtoto wake wa pili, aliyekuwa kipenzi na mwanafunzi mwenzake  na Marcon wakiwa darasa moja, wanalingana umri.

KAULI ya Waziri wa Viwanda Kuhusu Kenya Kupiga Marufuku Gesi ya Tanzania..!!!

$
0
0

Jana Waziri wa Viwanda na Biashara Charles Mwijage amekiri kupokea taarifa za katazo lililotolewa na serikali ya Kenya juu ya uuzwaji wa gesi zinazotumika majumbani zinazotoka Tanzania na kusema wataalamu wa wizara wanazifanyia kazi taarifa hizo.

Waziri Mwijage ametoa taarifa hiyo wakati alipozungumza na mwandishi wahabari wa Azam Two mjini Dodoma baada ya kuzagaa kwa taarifa za serikali ya kenya kupiga marufuku ya gesi zamajumbani za Tanzania kuuzwa Kenya na kukiri kuwa Kenya wamekuwa na chokochoko kadhaa lakini watahakikisha wanakaa chini kutafuta suluhu ikiwa ni pamoja na kuwashirikisha viongozi wa juu wa nchi hizi mbili.

DIWANI wa CHADEMA Akamatwa kwa Kudharau Mwenge..!!!

$
0
0

Diwani wa CHADEMA Kata ya Kitwiru katika Manispaa ya Iringa Ndugu. Baraka Kimata, alishikiliwa kwa muda na Jeshi la Polisi baada ya kutoa maneno yaliyotafsiriwa kwamba ni kashifa kwa mbio za Mwenge. Kimata ambaye pia ni Katibu Mwenezi wa CHADEMA Iringa Manispaa aliitwa Jukwaani kuongea kwa niaba ya chama chake baada ya Katibu wa CCM wilaya kuongea.

Kimata pamoja na mambo mengine aliyoongea, alimalizia hotuba yake kwa kusema kwamba kama CHADEMA ikipewa ridhaa ya kuongoza nchi basi wataupumzisha Mwenge wa Taifa. Baada ya hapo wasemaji wote waliofuatia akiwamo Mkuu wa Wilaya ya Iringa na Mkimbiza Mwenge Kitaifa walimshambulia Kimata na chama chake kwa msimamo huo wa kupinga Mbio za Mwenge.

Baadaye Kimata alikamatwa na kupelekwa Kituo Kikuu cha Polisi kuhojiwa na kuachiwa. Habari toka kwa watu walio karibu naye wanadai kwamba Kimata ametakiwa kuandika barua ya kuomba radhi kabla ya kesho saa kumi jioni.

MAWAZIRI Waanzisha Chama Kipya..Wajipanga Kuiondoa CCM Madarakani..Habari Vichwa vya Magazeti ya Leo 27/4/2017..!!!

STEVE Nyerere: Harakati za Makonda kwa Bongo Movie ni Batili na za Kujitafutia Umaarufu..!!!!

$
0
0

Steve Nyerere amedai kuwa kupigania Bongo movie dhidi ya maharamia wa filamu feki ni batili na za kujitafutia umaarufu kwa kuwa hilo ni suala la kitaifa linalotakiwa kuratibiwa nchi nzima na wakuu wote wa mikoa na polisi na sio Dar tu kwa kuwa vitu vingi vinavyovyoanzishwa hapa Dar vinafeli,

Pia alisema pia Makonda aliwaita watu watano, na tasnia ya filamu haiongozwi na watu hao

MAGUFULI Atoa Onyo Kali Watakaotishia Muungano..!!!

$
0
0

RAIS Dk. John Magufuli ameonya kuwa mtu yeyote atakayethubutu kutaka kuvunja Muungano atavunjika yeye.

Ametoa onyo hilo jana wakati akizungumza na mamia ya wananchi katika uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma kwenye maadhimisho ya miaka 53 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.

Dk. Magufuli amesema kwa kutambua kuwa Muungano ndio silaha, jembe na ushindi wetu, atahakikisha yeye (Magufuli) na Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Dk. Ali Mohamed Shein wanaulinda kwa gharama yeyote.

Amewataka Watanzania kuendelea kudumisha amani na kuitunza ili muungano nao uweze kudumu milele. Mbali na Dk. Magufuli na Dk. Shein, viongozi wengine wandamizi waliohudhuria sherehe hizo ni marais wastaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Ali Hassan Mwinyi na Jakaya Kikwete.

Wengine ni Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa na Makamu wa Rais Serikali ya Mapunduzi ya Zanzibar Balozi Seif Ali Idd.

MALKIA Elizabeth wa Uingereza Aanza Kugawa Majukumu Yake..Ni Baada ya Hali ya Afya Yake Kuanza Kuzorota..!!!

$
0
0

MALKIA Elizabeth II wa hapa, ambaye wiki iliyopita aliadhimisha miaka 91 ya kuzaliwa ameagiza wanafamilia wake wa kifalme kumwakilisha katika baadhi ya majukumu yake.

Kuna ripoti afya ya kiongozi huyo aliyezaliwa Aprili 21, 192 inaendelea kuzorota.

Kwa kawaida Malkia husherehekea siku yake ya kuzaliwa kwa awamu mbili; Kwanza katika tarehe ambayo alizaliwa na katika sherehe rasmi ya mwezi Juni.

Hiyo ni kuendana na mila na utamaduni wa kale kwa lengo la kuepuka machafuko ya hali ya hewa.

Hivi karibuni wakati akiwa katika ziara Ireland Kaskazini,  Malkia Elizabeth alizungumzia afya yake akisema kuwa bado yu salama.

“Bado niko hai,” alisikika akitania Malkia huyo.

Malkia Elizabeth ndiye mtawala aliyeongoza muda mrefu zaidi katika historia ya Uingereza, akiwa amekaa miaka 64 madarakani.

Na amekuwa kwenye ndoa kwa kipindi cha miaka 68, akiwa ametembelea nchi 117 duniani na kufanya kazi na mawaziri wakuu 12 wa Uingereza.
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live




Latest Images