Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104795 articles
Browse latest View live

KHA! Shehe Yamkuta, Picha Zake na Mchepuko Bofya Hapa!

$
0
0

Kamati ya Mashehe Mkoa wa Mwanza, wiki iliyopita ilimsimamisha huduma Shehe Mkuu wa Wilaya ya Sengerema, Ahmad Ally Jaha ambaye pia ni mfanyakazi ‘mtingaji’ wa Mgodi wa Geita Gold Mine ‘GGM’ kwa madai ya kukutwa na picha kwenye simu yake ya mkononi akiwa anabadilishana mate ‘denda’ na mwanamke ambaye si mke wake.

ALIYENASA PICHA HIZO

Tukio hilo lilijiri hivi karibuni baada ya mke mkubwa wa Shehe Jaha kubaini uwepo wa picha za mumewe na mwanamke mwingine ‘mchepuko’ wakila denda, jambo lililomkasirisha na kumsikitisha kwa kuwa, mumewe ni kiongozi wa dini na hakustahili kufanya hivyo kulingana na maandiko.

MTIRIRIKO WA TUKIO

“Ni kweli Shehe Jaha amesimamishwa baada ya mkewe kukuta picha chafu za mwanamke mwingine na mumewe wakiwa wanakula denda.

“Kimsingi mkewe alikasirika sana na kuamua kwenda kutoa malalamiko yake kwenye ngazi husika.

“Yale malalamiko yalitua kwenye Baraza Kuu la Waislam Tanzania (Bakwata) Wilaya ya Sengerema na wao kutokana na uzito wake, wakayawasilisha kwenye ngazi ya juu kabisa, yaani taifa.

“Inasemekana kwamba, mwanamke aliyenaswa kwenye picha na Shehe Jaha ndiye anayeishi naye kule kazini kwake, mgodini Geita ambaye kimsingi ni mchepuko,” kilidai chanzo chetu.

SHEHE ANA WAKE WATATU!!

“Kinachonishangaza, inadaiwa Shehe Jaha ana wake watatu, lakini aliyenaswa naye kwenye picha si miongoni mwa hao wake zake watatu.

“Kwa hiyo wake watatu mbali, huyo ni mchepuko wake. Hivi unadhani hata kama ni wewe ungefanyaje?” kilihoji chanzo chetu ndani ya Bakwata wilayani Sengerema.

KATIBU WA BAKWATA

Akizungumza na Wikienda baada ya tukio hilo la aina yake, Katibu wa Wilaya ya Sengerema, Shehe Madaraka Zubery, alithibitisha kusimamishwa kwa Shehe Jaha kwa kupewa barua iliyotolewa kutokana na maamuzi ya uongozi wa juu wa Bakwata Mkoa wa Mwanza.

Kwa mujibu wa katibu huyo, maamuzi hayo yaliidhinishwa na Shehe Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Salum Fereji kutokana na Jaha kukiuka misingi na maadili ya Kiislam na kutumia vibaya madaraka yake na kuwatia aibu Waislam.

Hivyo, alisema kuwa, kamati hiyo ilimteua Shehe Hassan Nuhu kukaimu nafasi yake hadi pale taarifa rasmi itakapotamkwa na Makao Makuu ya Bakwata Taifa jijini Dar es Salaam kama anastahili kuondolewa kabisa au lah.

MTUHUMIWA HUYU HAPA

Baada ya kumsikia Shehe Zubery, Wikienda lilimtafuta Shehe Jaha anayetuhumiwa na alipopatikana alielezwa kila kitu kuhusu sakata hilo kuanzia kusimamishwa huduma, kuwa na wake watatu na madai ya kuishi na mchepuko mgodini, Geita.

Hata hivyo, katika kujibu madai hayo, Shehe Jaha alionesha kushtushwa zaidi na taarifa za kusimamishwa kuliko maswali mengine kwani alionesha kama mtu ambaye alikuwa hajui kinachoendelea kisha akasema yeye hana taarifa kuhusu hatua zilizochukuliwa dhidi yake.

Alisisitiza kuwa, hajui kama amechukuliwa hatua ya kusimamishwa huduma hivyo anaendelea na kazi zake kama kawaida hadi atakapojulishwa rasmi kwa maandishi.

“Sina hizo taarifa, sijui kama nimechukuliwa hatua na mimi naendelea na kazi zangu kama kawaida, sijapewa barua rasmi, nasikia tu kwa watu,” alisema Shehe Jaha kisha akakata simu bila kufafanua mengine.

UKWELI Mchungu ..Wasiposhtuka… Naliona Kaburi la Bongo Fleva Kama Bongo Muvi..!!!

$
0
0

SEHEMU yoyote kunapokuwa na ushindani, kunakuwa na maendeleo chanya. Kila mtu hujaribu kufanya mambo ‘unique’ ili kumfanya kuwa na mvuto zaidi kwa kile anachokifanya. Lengo kuu huwa ni kuteka hisia za watu juu ya bidhaa inayokwenda sokoni au kwa mlaji.

Kunapokuwa hakuna ushindani, watu huchoka kula bidhaa ya aina moja. Matokeo yake ni anguko.

Hicho ndicho kilichojiri kwenye Bongo Muvi kulipokuwa na ushindani mkubwa wa mastaa wawili, marehemu Steven Kanumba na Vincent Kigosi ‘Ray’. Hapana shaka kuwa, kuondoka kwa Kanumba kuliua ushindani na matokeo yake ni kama ulivyosikia. Bongo Muvi inaaminika kuwa tuendako kama hakutakuwa na mabadiliko makubwa basi kaburi hilooo…

Wakati kelele zikiwa nyingi kwenye Bongo Muvi na kila mmoja akisema lake, uchunguzi wa gazeti hili umebaini kwamba, kama Bongo Fleva nako hakutakuwa na mshtuko au kuzinduka, basi nako kuna kishindo cha kifo kinafuata. Nitafafanua na kutoa tahadhari ya nini kifanyike ili tuendako kuwe salama.

Miaka kadhaa iliyopita kulikuwa na shoo nyingi mno zilizosababisha kumbi za starehe na viwanja mbalimbali vya burudani kufurika hadi pomoni. Wakati fulani kumbi zilijaa hadi kukawa na tatizo la hewa kukata.

MTAZAMO WA MWANA-FA 
Kinachotokea sasa ni kwamba shoo hizo hakuna tena. Katika mazungumzo yangu na wanamuziki wakubwa wa Bongo Fleva kwa nyakati tofauti, kila mmoja alieleza dhamira yake ya kwenda kimataifa zaidi isipokuwa Hamis Mwinjuma  ‘Mwana-FA’ ambaye anaamini kwamba bado mashabiki wake wa Bongo na Afrika Mashariki wanamuhitaji zaidi kuliko huko kwingine.

Atakapoamini kuwa amekata kiu yao, automatic, hali itamlazimisha kwenda kimataifa kutokana na mahitaji na wakati.

KWA NINI SHOO ZA NYUMBANI ZIMEKATA? 
Uchunguzi huo ulibaini kuwa, wasanii wenyewe wanaamini kuwa, shoo za nyumbani za kuwaweka karibu na mashabiki wao, ambao kimsingi ndiyo waliowapa sapoti hadi kufikia hapo walipo, hazilipi na kwamba hazina mashiko! Nakataa!

Wengine wanasema hakuna wadau wanaondaa shoo hizo na kwamba wenyewe au msanii mmojammoja hawezi kuandaa shoo yake mwenyewe bila wafadhili, makampuni, mapromota na wadau wengine.

Wanachoshindwa kujua ni kwamba, mashabiki wao wa nyumbani waliowapa sapoti na majina makubwa, wanahitaji kuwaona wakiwaburudisha kwa namna yoyote ile bila kujali sababu au visingizio wanavyovitoa. Wakiwa-puuza, basi ndiyo kwaheri ya kuonana!

ZIKO WAPI SHOO ZA WIKI-ENDI?
Kama nilivyoeleza awali, miaka kadhaa iliyopita kulikuwa na ‘events’ au shoo nyingi za kila wikiendi, Ijumaa, Jumamosi na Jumapili. Kumbi za burudani au klabu za usiku zilisheheni mashabiki wao.

Ulikuwa ni msisimko wa hali ya juu kwani mbali na kuwaona, kulikuwa na ushindani wa nani anayejua kutawala jukwaa na nani anayetoa shoo nzuri kuliko mwingine! Kwa sasa hilo halipo na ni vigumu mno kusikia msanii fulani ndiye mkali stejini kwa sasa.

NAY YUPO TOFAUTI 
Katika mazungumzo yangu na Mwanamuziki Emmanuel Elibariki ‘Nay wa Mitego’, yeye anaamini kuwa ndiye msanii pekee ambaye yupo karibu zaidi na mashabiki wake kwani huwa hajali kama ni wikiendi au ni siku ya kawaida kwani hugonga shoo nyingi zaidi hasa mikoani, wilayani na kwenye miji midogo vijijini.

Siyo kwamba hataki kuwa kimataifa, la hasha! Lakini bado anaamini kuwa mashabiki wake waliomkuza na kumpa jina kubwa wanahitaji burudani kutoka kwao na tena kwa viingilio vya chini kabisa vinavywawezesha watu wake wa hali ya chini kuhudhuria.

Na kiukweli kwa kufanya hivyo, Nay anakimbiza mwizi kimyakimya kwani anazichanga tu mdogomdogo.

KURUDISHA KWA JAMII NI TATIZO 
Kosa lingine kubwa linalofanywa na wanamuziki hawa ni kutorudisha fadhila kwa jamii. Tunaishi kwenye jamii zenye matatizo mengi kuanzia magonjwa, mazingira, uchumi mbaya na matatizo mengine ya msingi.

Ni nadra sana kumuona msanii akianzisha au akiwa mstari wa mbele kwenye kampeni ya janga fulani au kuhamsisha jamii kuondokana na janga hilo. 
Siyo lazima kutoa fedha nyingi, lakini kuonesha mashabiki kuwa yupo pamoja nao katika maisha yao ya kila siku.

Hili wanaliona ni jambo dogo lakini ni kubwa mno kwa mashabiki wao. Kwa msanii yeyote anayejitolea kwa jamii, hata anapopata tatizo hasa la ugonjwa akihitaji kuchangiwa, huwa ni ishu ndogo. Lakini kwa yule asiyekuwa karibu na watu wake huwa ni shughuli nzito. Mifano ipo mingi.

NINI KIFANYIKE KWA HARAKA KUNUSURU KIFO? 
Nimefungua mjadala huu mpana kwa ajili ya kuchukua tahadhari ya huko tuendako yasiwakute ya Muziki wa Dansi, Taarab na yale tunayoshuhudia kwenye Bongo Muvi. Kwa mtazamo wangu, ni muda muafaka sasa kwa mastaa wa Bongo Fleva kuanza kuwa ‘selfish’, yaani wang’ang’anie kwanza kuwaridhisha mashabiki wao wa nyumbani, waliowanyanyua kabla ya kukimbilia shoo za nje ambazo mara nyingi wenyewe hukiri kuwa hazina masilahi zaidi ya sifa kwamba wanakwenda kufanya shoo ughaibuni.

Mfano mzuri ni msanii Omary Nyembo ‘Ommy Dimpoz’ ambaye uchunguzi ulionesha kuwa hajafanya shoo kwa mashabiki wake wa Bongo au mkoani kwake, Kigoma tangu mwaka uanze.

Mastaa wa Bongo Fleva lazima wakubali kuwa wamekuwa hapo walipo kwa sababu ya sapoti waliyopewa nyumbani hivyo wawape burudani. Ni lazima waamini katika kurudisha kwa jamii, bila hivyo Bongo Fleva hiyooo…kaburini!

NAY wa Mitego Afungukia Maajabu ya Wapo..Adai BBC na CNN Wameucheza..!!!!

$
0
0

MWANAMUZIKI Emmanuel Elibariki ‘Nay wa Mitego’ anayesumbua na Wimbo uitwao Wapo, hivi karibuni amefunguka namna wimbo huo ulivyomletea mafanikio ndani ya muda mfupi tangu auachie jambo ambalo kwake ni kama maajabu.

Akichonga na Over Ze Wikend, Nay alizidi kufunguka kuwa miongoni mwa mafanikio ambayo wimbo huo uliyompa misukosuko umempatia ni kubadilishwa lugha na ‘media’ mbalimbali za nje zikiwemo BBC na CNN ili dunia nzima iweze kuupata ujumbe alioulenga lakini pia shoo ambazo hazikatiki.

“Tofauti na nyimbo zangu zote, Wapo umenipa mafanikio sana. Naona ni kama maajabu maana kila wiki napiga shoo kuanzia tatu lakini pia umenifanya kuwa karibu na viongozi wa kiserikali na ambao hawapo serikalini. Lakini pia ni kujulikana zaidi nje ya nchi maana media za nje zimenizungumzia sana,” alimaliza

TUNDA Aanika Kila Kitu Juu ya Mahusiano Yake Na Young D..!!!

$
0
0

VIDEO queen matata Bongo, Tunda Sebasita ‘Tunda’ hivi karibuni ameibuka na kumkana aliyewahi kuwa mpenzi wake David Ganzi ‘Young D’ kuwa si mwanaume hasa aliyewahi kutamani kuwa naye huko nyuma na juu ya uhusiano wao ni jambo ambalo lilitokea tu.

Akichonga na Uwazi Showbiz, baada ya kuulizwa ni mwanaume gani alitamani kuwa naye Bongo huko nyuma na hakupata bahati ya kuwa naye, Tunda alisema hayupo maana mwanaume aliyetamani kuwa naye amekwisha kuwanaye lakini si Young D.

“Siwezi kulitaja jina lake wazi, lakini kiukweli mwanaume ambaye nilitamani sana kuwa naye tayari nilikwishakuwanaye na tukaachana lakini naweka wazi kuwa si Young D,” alimaliza Tunda.

UBUYU wa Moto Moto...Kumbe Lulu Diva Ashea’ Penzi na Shangazi Yake..!!!!

$
0
0

Ubuyu wa kutisha! Jipu limepasuka mjini kuwa muuza nyago na msanii wa Bongo Fleva, Lulu Abbas ‘Lulu Diva’ amekiri kushirikiana ‘kushea’ penzi la bwana mmoja na shangazi yake pamoja na shosti yake wa karibu.

Kwa mujibu wa Lulu Diva, jambo hilo limekuwa likimtesa moyoni lakini kwa kuwa anataka kuwa huru, basi ameona ni vyema akalipasua.

MSIKIE LULU DIVA

“Kila mtu anapitia mambo mengi sana kwenye uhusiano wa mapenzi na maisha kwa jumla. Nimeamua kufunguka kuhusu jipu nililonalo moyoni mwangu. Ni kuhusu jamaa mmoja ambaye nilikuwa ninampenda sana katika maisha yangu.

UKIMSEMA VIBAYA…

“Kwa jinsi nilivyokuwa ninampenda yule jamaa, yaani ulikuwa ukiniambia kitu kibaya kuhusu yeye, basi ujue ni lazima nitaenda kumwambia na kukutaja. Nilikuwa sisikii wala siambiliki kwake.

AENDA KUMTAMBULISHA

“Kutokana na kudumu kwenye mapenzi kwa muda mrefu na kumuelewa, nilimuomba aje home (nyumbani) ajitambulishe ili tuwe huru, akafanya hivyo.

KUMBE ALISHA-DATE NA SHANGAZI

“Nilishangaa nilipomfi kisha pale nyumbani, watu wote wanamfahamu kama bwana’ke shangazi yangu. “Nilichoka sana kusikia vile, yule shangazi yangu, umri ni kama wangu kwa sababu tunatofautiana kama miaka minne au sita.

NDUGU WAMKATALIA

“Kutokana na hali hiyo, ndugu walikataa katakata mimi kuwa na uhusiano na mwanaume huyo kwa sababu ya kuwa na uhusiano na shangazi yangu. Familia yangu ilikataa kabisa nisiwe na uhusiano naye.

AZIBA MASIKIO

“Kiukweli nilikuwa ninampenda sana yule jamaa, niliumia, lakini nikaziba masikio na kuwaambia kuwa mimi ninampenda na siwezi kuishi bila yeye.

AVISHWA PETE

“Basi nilivyowachomolea kuachana naye, jamaa alinivisha pete ya uchumba na tukaendeleza penzi letu.

ACHEZEA KICHAPO

“Pamoja na upendo niliokuwa nao kwa jamaa, lakini bado alikuwa akinidunda sana, nilikuwa nalia, nilivumilia kwa kuhisi labda ni sehemu ya mapenzi, lakini jamaa alikuwa ananipa kichapo.

AMFUMANIA NA SHOSTI WAKE

“Nahisi jamaa alikuwa kicheche sana kwani siku moja nilimkuta anazini na rafi ki yangu, tena kwenye kitanda changu. Niliumia kwani yule rafi ki yangu alikuwa ni kila kitu kwangu, nilimuamini na kumpenda kwa dhati.

JAMAA AFUNGWA

“Baadaye yule jamaa alipata matatizo akafungwa nchini Israel, tangu kipindi hicho sijawahi kuonana wala kuwasiliana naye.

MIAKA 2 BILA KUCHEPUKA

“Kutokana na maumivu yale na misukosuko ya mapenzi, niliamua kukaa kwanza bila kujiingiza kwenye uhusiano hadi miaka miwili ilipofi ka.

HANA RAFIKI WA KIKE

“Kutokana na kile kilichotokea nikawa sina imani tena na marafi ki kwani wao wanaweza kukuharibia maisha yako, ndiyo maana mimi sina rafi ki kihivyo,” alifunguka Lulu. Lulu ambaye kwa sasa amegeukia kwenye Bongo Fleva, anatamba na Wimbo wa Malele na Usimwache.

KUTOKA KWA MHARIRI

Yapo mambo mengi mabaya na mazuri ambayo yanafanywa na watu wengi kila siku, ingawa kuna mengine yanatesa kubaki moyoni hadi pale mtu anapoamua kuyatoa na kuwa huru kama alivyofanya Lulu.

KESI ya Wema Sepetu ya Kukutwa na Madawa ya Kulevya Yafikia Hatua Hii Mahakamani..!!!

$
0
0

Malkia wa filamu , Wema Sepetu, Jumanne hii amepanda tena katika mahakama ya hakimu mkazi kisutu, Dar es salaam, kusikiliza kesi ya tuhuma za kutumia na kukutwa na madawa ya kulevya, ambapo upande wa Jamhuri umekamilisha upelelezi wa kesi inayomkabili msanii huyo.

Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba, ameahirisha kesi hiyo mpaka June 1, mwaka huu ambapo mahakama itasikiliza maelezo ya awali ya upelelezi huo.

Muigizaji huyo, ambaye yupo nje kwa dhamana baada kusota mahabusu kwa siku 7, anadaiwa kukutwa na msokoto wa bangi nyumbani kwake, kufuatia msako mkali wa kupambana na dawa za kulevya uliofanywa na ofisi ya mkoa wa Dar es salaam.

ALICHOKISEMA Zitto Kabwe Baada ya Halima Mdee Kuchukua Hatua Dhidi Yake..!!

$
0
0

Mbunge wa Kigoma mjini, Zitto Zuberi Kabwe, ametoa shukrani kwa Bunge la Tanzania kwa kumsamehe Mbunge wa Kawe, Halima Mdee kwa kuendelea na vikao vya Bunge.

Mbunge Zitto ametumia ukurasa wake wa Facebook kutoa shukrani hizo kwa bunge. Ameandika hivi:

Hatimaye Waziri Kivuli wa Fedha ndg. Halima Mdee amesamehewa na ataendelea na vikao vya Bunge. Hii ndio haki. Mtu aliomba radhi hadharani, kwanini aadhibiwe. Shukran Kwa Bunge.

Halima Mdee alituhumiwa kutumia lugha chafu bungeni wakati wa uchaguzi wa Bunge la Afrika Mashariki, Aprili 14 mwaka huu.

NEC Yatangaza Nafasi ya Ubunge Viti Maalumu Chadema..!!!

$
0
0

Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imetangaza nafasi  ya mbunge wa viti maalumu kwa tiketi ya Chadema.

Nafasi hiyo imetangazwa baada ya kifo mbunge aliyekuwa anashikilia wadhifa huo, Dk Elly Macha kufariki dunia Machi 31, mwaka huu.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo (Jumanne) na Mwenyekiti wa NEC, Jaji Semistocles Kaijage ni kuwa kwa mujibu wa Kifungu cha 37 (3) cha Sheria ya Taifa ya Uchaguzi, Sura ya 343, Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania amemjulisha kuwepo kwa nafasi hiyo.

“Kutokana na kuwepo kwa nafasi wazi ya Ubunge wa Viti Maalum, taratibu za kujaza nafasi hiyo zinaendelea kwa kuzingatia Ibara ya 78 (4) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977, ikisomwa pamoja na kifungu cha 86A (8) cha Sheria ya Taifa ya Uchaguzi, Sura ya 343,”amesema.

WANAWAKE wa Haya makabila Kitandani ni Wabovu Sana

$
0
0


Hiyoooooooooooooo ndo habari kwani kuna baadhi ya makabila ukiwa una mgegeda hata hatingishiki yeye ni kutulia kama gogo tu wala hawezi hata kukukuruka kwanza wachaga, wapare, waha, wasukuma, wangoni, wakikuyu, wakurya, waluguru, wagogo, wamasai na mengine kibao yani ni shida hadi wanafanya papuchi zao kua za baridi sana jaman badilikeni, haya toeni uzoefu wenu na ninyi mie nimechokoza tu hapo ila kuna ukweli

SHILOLE - Harusi Yangu Utafungwa Kwenye Helkopta ..Sherehe Itafanyika Uwanja wa Taifa..!!!!

$
0
0

Shilole amesema lengo lake sio tuu kuweka rekodi au kuonyesha ana uwezo mkubwa kifedha la hashaa!! Lengo lake ni kutaka kila shabiki yake kuhudhuria kwenye tukio hilo la kihistoria ambalo litafanyika angani kabla ya helkopita kutua uwanja wa mpira wa Taifa ambako mashabiki wake watakutana kushuhudia harusi hiyo.

“Ndoa yangu nitafungia juu ya Ndege (Helkopita),Tukishuka nashukia uwanja wa taifa…,hivi unategemea mimi nitaolewa tuu halafu watu waone picha zangu tuu? Mimi nataka watu waje kushuhudia.Ujue mimi nina mashabiki wengi na wote nataka waje waone Dada Mwajuma aking’olewa“Alisema Shilole kwenye mahojiano yake na Clouds Fm.

Shilole ambae hakutaka kuweka wazi jina la mchumba wake huyo mpya ambae watafunga nae ndoa kwa kuhofia kuporwa na walimwengu alisema mipango ya ndoa ipo ingawaje bado kwanza kuna vitu havijakaa sawa na ikifika muda atawatangazia mashabiki wake.

BASHITE Abebwa, Abebwa Tena..Habari Vichwa vya Magazeti ya Leo 3/5/2017..!!!

ZIJUE Sifa na Majukumu ya Mkuu wa Mkoa Kisheria Hapa Tanzania

$
0
0
Tuanze kwa kutazama majedwali haya na ufafanuzi wake kwa lugha ya kiswahili utafuata..



SEHEMU YA KWANZA: KUHUSU MKUU WA MKOA

- Ni sehemu ya Wizara ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI)

- Ofisi za Mkuu wa Mkoa zitakuwa kwenye Makao Makuu ya Mkoa husika

- Mkuu wa Mkoa atawajibika chini ya Waziri wa TAMISEMI

2. DHIMA YA KAZI HII

Kuhakikisha kuwa maendeleo ya kiuchumi na kijamii yanapatikana kutokana na huduma bora za ushauri na uratibu ambazo zinajenga mazingira bora kwa Serikali za Mitaa na wadau kutoa huduma inayotarajiwa.

3. MAJUKUMU NA KAZI ZA MKUU WA MKOA

- Kuhakikisha uwepo wa Haki na Sheria kk mkoa

- Kuongoza na kusimamia operesheni za Maafa na Kufariji

- Kama Mwenyekiti wa Kamati ya Ushauri ya Mkoa(RCC), Mkuu wa Mkoa atawajibika kufanya jitihada za kuhakikisha kutimizwa kwa sera za serikali juu ya Mkoa husika.

- Kufanya yale yote yatakayosaidia kuimarisha ulinzi na usalama wa mkoa kwa ushirikiano na serikali za mitaa.

4. ELIMU

Mkuu wa Mkoa itampasa awe na Elimu Ngazi ya Shahada(Degree) au inayoshabihiana na hiyo kutoka kwenye Taasisi ya Elimu inayotambulika.

5. UELEWA

Mkuu wa Mkoa atapaswa awe ni mwenye ufahamu kuhusu Utawala wa Sheria, Utawala bora, Kanuni za Haki Asilia (Natural Justice), Sera na taratibu zake, Uongozi na Utawala pamoja na masuala yote ya msingi ktk utekelezaji wa Mipango ya Maendeleo.

6. UJUZI

Kimsingi Mkuu wa Mkoa anapaswa kuwa na stadi zote za uongozi;

Ujuzi wa kujenga umoja, ujuzi wa kutatua changamoto, ujuzi wa kutoa ushauri nasaha, ujuzi wa maridhiano, ujuzi wa kuhimili msongo/mihemuko, sambamba na ujuzi kuhusu mahusiano ya umma na uwezo wa kuzungumza vizuri mbele za watu.

7. SIFA BINAFSI

Aonyeshe uwezo wa kutunza siri, kufanya maamuzi yenye tija, kufanya kazi pasipo mashinikizo, uelewa kuhusu mwenendo wa siasa na tamaduni za jamii, awe na heshima, mbunifu, mtenda haki, bila kusahau kuheshimu miiko ya kazi.

8. UZOEFU

Ni lazima Mkuu wa Mkoa awe ni mtu mwenye uzoefu kuhusu masuala ya utawala/siasa usiopungua Miaka 10.

9. MSHAHARA

Mkuu wa Mkoa atalipwa kiwango cha mshahara kwa taratibu zilizoainishwa na Ofisi ya Utumishi (kwa sasa salary scale yake ni LSS(P) 4).

Asanteni.

HIVI Ndivyo Jinsi Siasa za Matukio zinavyozorotesha Upatikanaji wa Ben Saanane

$
0
0
Kama tujuavyo Beni amepotea sasa ni takribani miezi sita haifahamiki ni upi mustakabali wake na kinachosikitisha si tu vyombo vya dola kutokupata majibu kwa haraka,ama raia wenye mapenzi mema bali hata viongozi wa chama ambacho Beni alikiwa ni miongoni mwa kiongozi mwenzeo wanalifuatilia jambo hili kwa mtindo wa siasa za matukio.

Ndugu wanachadema mchezo wa kuwa busy kwenye siasa za matukio kunasababisha sakata la Beni kusahaulika kila itokeapo agenda mpya ionekanayo kama mtaji wa kisiasa.

Nafahamu mtasema kwamba CDM sio chombo cha Dola ila ifahamike sakata la Roma ni kama hili la beni lakini nadiriki kusema wasanii wameonesha mfano mzuri kuliko CDM kwani walisimama imara mpaka Roma akapatikana.

Juzi sakata hili lilionesha kufufuliwa na wanasiasa kama ZZK,Lissu na Mbowe lakini inasikitisha jambo hili kusahaulika kwa kuibuka isue ya Bashite.

Hivi ni sawa kuhangaika na kutumia nguvu kubwa kwa isue ya Bashite kuliko mustabali wa wapi alipo Beni Saanane?

Siku chache hapo nyuma kila mtu ni lazima kila aandikapo aweke#Tunamtaka Beni saanane akiwa hai,lakini kwa sasa watu wameshasahau kabisa.

Ni lazima CDM wakajifunza kupendana si tu wakati wa siasa bali hata wakati wa matatizo

MAGUFULI Ampa Tano Dk Mengi kwa Uwekezaji Nchini..!!!

$
0
0

RAIS John Magufuli amempongeza Mwenyekiti Mtendaji wa Makampuni ya IPP, Dk. Regnald Mengi kwa kufanya uwekezaji wa Kiwanda cha Kutengeneza Vinywaji Baridi Jamii ya Coca Cola cha Bonite Bottlers Limited (BBL) cha Moshi mkoani Kilimanjaro.

“Nimemuona Dk. Mengi yuko pale na kwa kweli naomba nimpongeze kwa kile Kiwanda chake cha Bonite alivyowekeza, hongera sana. Wazawa wengine wa Kilimanjaro rudini nyumbani muwekeze. Huyu Dk. Mengi anapiga kote kote Dar na Moshi,”alisema.

Rais Magufuli alitoa pongezi hizo  wakati wa sherehe za maadhimisho ya sikukuu ya wafanyakazi duniani (Mei mosi) zilizofanyika kitaifa mjini Moshi kwenye viwanja vya Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi.

Pongezi hizo za Rais, ziliamsha hisia za furaha za maelfu ya wakazi wa mkoa wa Kilimanjaro waliofurika katika sherehe hizo na kumshangilia Dk. Mengi, baada ya Rais Magufuli kumsimamisha na kumtaka awapungie mkono.

Dk. Mengi ambaye pia ni Mwenyekiti wa Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania (TPSF) amekuwa akisisitiza suala la uwezeshaji wananchi kiuchumi kuwa ni njia pekee duniani iliyoonesha mafanikio katika kukuza uchumi wa nchi mbalimbali,kupunguza umaskini na kudumisha amani na utulivu.

MRISHO Mpoto Awacharukia Wanaomsema Vibaya kwa Kumuunga Mkono Rais Magufuli..!!!

$
0
0

Msanii wa muziki wa asili nchini, Mrisho Mpoto amedai kuwa amekuwa akitukanwa matusi pamoja na kutupiwa maneno ya kejeli tangu aonyeshe nia yake ya kumuunga mkono Rais John Pombe Magufuli.

Msanii huyo ambaye huwa anafanya sho nyingi za Ikulu, amesema yeye ataendelea kumuunga mkono Rais huyo kwa kuwa ni kiongozi ambaye anawapigania wananchi wa chini.

“Nimepokea matusi mengi, kebehi, na maneno machafu juu ya mimi kuunga mkono utendaji wa Rais Magufuli, kitu ambacho nakiamini kuna “KUKUBALIANA KWA KUTOKUBALINA” lakini kumtukana mtu mwingine sio busara hata kidogo, kwa kuwa tu hakusema au hakufanya ambacho nafsi yako ilipenda kusikia,” ameandika Mpoto kupitia mtandao wa Instagram.

“Kilichonifanya niandike ujumbe huu ni kuwa nisiwekewe maneno mdomoni yakuwa nimesema Rais Magufuli ni Mungu, kwa wale ambao hawakuangalia sherehe za MEI MOSI jana, naomba niseme kuwa hayo maneno siyo kweli na yamebadilishwa kutoka kwenye ukweli wa nilioyasema. Mimi ni mtu mwenye hofu na Mungu siwezi kusema hivyo,” ameongeza.

Mpoto amedai kuwa imekuwa ni tamaduni kwa baadhi ya watu kuwashambulia watu ambao wameonyesha nia ya kumsapoti Rais Magufuli.

“Kumekuwa na utamaduni ikitokea mtu anauunga mkono utendaji wa Rais kunaibuka kundi la wapinga maendeleo na kuanza kutukana. Naomba ijulikane kuwa sababu za kumunga mkono Rais, yale niliyokua nayaongea huko nyuma naona yanafanyiwa kazi hivi sasa!! MRISHO MPOTO mpaka sasa namuunga mkono Rais MAGUFULI.  Iwe nachumia tumbo kama inavyosemwa au nimevimbilwa kwa shibe,” ameongeza Mpoto.

WAZIRI Lukuvi Atishia Kumpasua KITAMBI Mkurugenzi

$
0
0
Waziri  wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi, amemtahadharisha Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela, John Wanga, kwamba endapo atashindwa kusimamia vema agizo la urasimishaji makazi holela na uandaaji wa hati miliki kwa wananchi, atatumbuliwa.

Alitoa tahadhari hiyo juzi baada ya kusomewa taarifa ya utekelezaji wa   urasimishaji na uandaaji wa hati za ardhi ambako Halmashauri ya Ilemela imetekeleza kwa asilimia moja kwa kuandaa hati 834 huku viwanja  vingine 16,000  vikiwa vimepimwa bila kuandaliwa hati.

 Lukuvi  ambaye alionekana kukasirishwa na hali hiyo alisema kushindwa kuandaliwa    hati hizo  ndani ya Halmashauri ya Ilemela ambayo ina maofisa ardhi  na watathmini zaidi ya 40 kmeisababishia  hasara   Serikali.

Alisema kazi hiyo ingefanyika ilivyotarajiwa serikali ingepata  mapato ya  Sh bilioni 2.5 kwa mwaka lakini kilichopatikana  ni Sh bilioni 1.3 tu.

“Hakuna halmashauri nchini iliyo na watumishi  wengi wa idara ya ardhi kama Ilemela na Nyamagana mara zote nimekuwa nikifikiria kuwahamishia wilaya nyingine kama Geita kwa Mheshimiwa Rais, Dk. John  Magufuli ambako hakuna hata mmoja.

“Lakini  leo pamoja na wingi wenu mnaandaa hati 834 huku viwanja 16,000 mkishindwa kuvikamilisha kwa muda niliotoa.

“Sasa Mkurugenzi nakuambia kwamba Serikali imewavumilia  vya kutosha na sasa kama hautabadilika kwa muda ambao nimekuongezea kuanzia sasa hadi Juni 30, mwaka huu   tambua kwamba kitambi chako kitapata pancha.

“Wewe mwenyewe utajua namna ya kuiziba pancha hiyo, hatuwezi kuimba wimbo huo huo kila mwaka.

“Kuna  vitu vidogo vidogo vya hapa halmashauri  mnavifinyia kazi lakini suala ambalo ni la muhimu    mnashindwa kukamilisha.

“Nilikuwa namuona mkurugenzi ni mjanja   lakini anachokifanya hapa ni kama kutwanga maji kwenye kinu kwa sababu kodi ya ardhi haikusanywi,” alisema.

 Waziri alisema Halmashauri za Ilemela na Nyamagana  zinatakiwa zikamilishe hatua hiyo  Juni 30, mwaka huu atakapoifunga rasmi na kutangaza ‘masterplan’ ya Jiji la Mwanza ifikapo Agosti.

Aliwataka wananchi kutambua kuwa baada ya kufungwa  urasimishaji makazi haitatokea    tena  fursa ya namna hiyo.

Alisema wananchi ambao hawatakuwa na hati ya eneo analoishi watahesabika kama wavamizi, hivyo watapoteza haki yao na maeneo hayo yatachukuliwa na Serikali kwa shughuli nyingine.

Lukuvi alisema Serikali kuu imetenga Sh bilioni 22 kwa ajili ya masterplan ya   Mwanza ambayo itaanza kutekelezwa Agosti mwaka huu,  kazi ambayo  itafanywa na wataalamu kutoka China.

RAIS wa Zamani wa Nigeria Goodluck Jonathan Amshushia Lundo la Lawama Obama kwa Kusababisha Kushindwa Kwenye Uchaguzi..!!!

$
0
0

RAIS wa zamani wa Nigeria Goodluck Jonatham amemshutumu Rais wa zamani wa Marekani Barack Obama kwa kushindwa katika uchaguzi mkuu dhidi ya Rais wa sasa wa nchi hiyo Muhammadu Buhari, akidai kwamba aliongoza njama za ulimwengu dhidi yake ili kumwondoa madarakani.

Jonathan alitoa shutuma hizo katika kitabu kipya kilichotolewa Ijumaa iliyopita kinachoitwa Against The Run of Play, ambacho kinaeleza namna alivyokuja kuwa rais wa kwanza wa Nigeria aliyeko madarakani kushindwa katika uchaguzi.

Kuzuia machafuko

Alisema Obama na maafisa wake “waliweka wazi kwangu kimatendo kwamba walikuwa wanataka mabadiliko ya serikali nchini Nigeria na walikuwa tayari kufanya lolote kufanikisha nia yao hiyo. Waliweza hata kutuma meli za kivita kwenda katika Guba ya Guinea siku chache kabla ya uchaguzi,” alinukuliwa akisema katika kitabu hicho chenye kurasa 204, na mwandishi wa habari Olusegun Adeniyi.

Jonathan alipata sifa duniani baada ya kukubali kushindwa kabla ya matokea ya mwisho ya uchaguzi huo kutangazwa, jambo ambalo lilizuia machafuko makubwa ambayo yamewahi kutia dosari chaguzi za nyuma katika taifa hilo lenye idadi kubwa zaidi ya watu barani Afrika.

Alimshutumu Obama kwamba alimshawishi aliyekuwa Waziri Mkuu wa Uingereza David Cameron na Rais wa sasa wa Ufaransa Francois Hollande kufanya kazi dhidi yake. “Nilikuwa napatana vizuri na Cameron lakini ilifika wakati, niligundua kuwa Wamarekani walikuwa wanamshinikiza na alilazimika kuungana nao dhidi yangu,” alisema.

“Lakini niligundua ni kwa kiasi gani Rais Obama alikuwa tayari kufanya ili kuniondoa mimi hadi Ufaransa nayo ikakubali kutokana na shinikizo kutoka kwa Marekani.” Jonathan alisema kuwa alikuwa na uhusiano mzuri na Hollande, ambaye alikuwa ni mtu wa kwanza kuwasiliana nae iwapo kunatokea matatizo katika nchi ya jirani ya Cameroon kuhusu kundi la Boko Haram.

Baada ya kutekwa kwa zaidi ya wanafunzi 200 wa kike kaskazini mashariki mwa mji wa Chibok nchini Nigeria, Hollande aliandaa mkutano wa usalama jijini Paris akizihusisha Nigeria pamoja na mataifa ya jirani.

Mazungumzo hayo yalikuwa ni muhimu katika kuunda jeshi la ukanda huo, ambalo limefanya kazi kubwa katika kudhoofisha sehemu hiyo ya kundi la Islamic State.

“Lakini wiki kadhaa kabla ya uchaguzi, aliungana na Wamarekani katika kuunga mkono upinzani dhidi yangu,” aliongeza, kulingana na kitabu hicho ambacho kimeonekana na shirika la habari la AFP.

Shutuma za rushwa

Chama cha Buhari cha All Progressives Congress (APC) kilimshutumu Jonathan kuwa alikuwa hafanyi inavyopasa katika kupambana dhidi ya tatizo la rushwa nchini humo. “Hilo ni jambo ambalo pia nilikuwa nikilisikia kwa Wamarekani bila kuwepo kwa shutuma za moja kwa moja dhidi yangu,” aliongeza, akipinga kwamba hakuwa amefanya lolote katika kupambana na tatizo hilo.

Buhari alimshutumu Jonathan na chama chake cha Peoples Democratic Party (PDP) kwa kuondoka serikalini na kuacha hazina ya nchi hiyo ikiwa “haina kitu”na kusema kuwa fedha nyingi za umma ziliibiwa.

Maafisa wa ngazi za juu wa PDP na utawala wa Jonathan, wakiwemo watu wa familia yake, kwa sasa wanakabiliwa na mashtaka ya rushwa.

Buhari, ambaye aliwahi kuongoza serikali ya kijeshi katika miaka ya 1980, ameshuhudia oparesheni zenye mafanikio dhidi ya Boko Haram, kundi ambalo limeua kiasi cha watu 20,000 nchini Nigeria pekee.

Rekodi mbaya ya haki za binadamu

Jonathan, ambaye utawala wake ulishutumiwa kwa kushindwa kuunga mkono na kutoa silaha nzuri kwa jeshi la nchi hiyo katika mapambano dhidi ya kundi la Boko Haram, anadai kwamba utawala wa Obama ulikuwa unadhoofisha jitihada za nchi yake dhidi ya Boko Haram.

Balozi wa Nigeria huko Washington mwaka 2014 aliishutumu Marekani hadharani kwa kukataa kuiuzia nchi yake helikopta za kivita. Jonathan alisema kwamba sheria za Marekani zinapiga marufuku mauzo ya silaha kwenda kwa mataifa ambayo yana rekodi mbaya ya haki za binadamu “kusababisha vita dhidi ya Boko Haram kuwa ngumu sana.”

Afisa wa ubalozi wa Marekani huko Abuja alisema kwa njia ya taarifa kwa vyombo vya habari kwamba “inashangaza” kwamba Jonathan anaonekana kuwa anabadili mtazamo wake katika uchaguzi. Sera za Washington kabla ya kura ilikuwa ni uchaguzi ambao ni huru, haki na wenye uwazi, alisema, na kuongeza kwamba Marekani iliamini kwamba matokeo yalikuwa ni “maoni na matakwa ya watu wa Nigeria.”

BAYERN Munich Watwaa Bundersliga kwa Mara ya Tano Mfululizo..!!!

$
0
0

KLABU ya Bayern Munich imefanikiwa kutangazwa ubingwa wa Ligi Kuu nchini Ujerumani kwa mara ya tano mfululizo, baada ya juzi kuibuka na ushindi wa mabao 6-0 dhidi ya wapinzani wao, Wolfsburg.

Mabingwa hao wapya wameweza kutangaza ubingwa ikiwa ni saa chache baada ya wapinzani wao kwenye msimamo wa Ligi, Leipzig, kutoka suluhu dhidi ya Ingolstadt na kuwafanya Bayern Munich watangaze ubingwa kwa tofauti ya pointi 10, huku ikiwa imebaki michezo mitatu kumalizika kwa Ligi.

Katika mchezo huo, dakika 45 za kipindi cha kwanza Bayern Munich walikuwa mbele kwa mabao 3-0, yaliyowekwa wavuni na David Alaba, Robert Lewandowski akifunga mawili kabla ya Arjen Robben, Thomas Muller na Joshua Kimmich kuongeza mabao matatu kipindi cha pili.

Kiungo wa zamani wa Bayern Munich, Luis Gustavo, raia wa nchini Brazil ambaye kwa sasa anakipiga katika kikosi cha Wolfsburg, alioneshwa kadi nyekundu kutokana na utovu wa nidhamu na baadaye kutaka kumshambulia mwamuzi.

Kocha wa klabu ya Bayern Munich, Carlo Ancelotti, amejiwekea historia katika klabu kubwa barani Ulaya kutwaa mataji ya Ligi, ikiwa pamoja na nchini Italia, England na Ufaransa.

Ancelotti, ambaye alifukuzwa na klabu ya Real Madrid, Mei 25, 2015, amewashukuru mashabiki wa Bayern Munich kwa ushirikiano waliouonesha tangu kujiunga kwake ndani ya kikosi hicho Julai 2016.

“Ni muda wa kufurahia ubingwa, ni kazi ambayo imefanywa na wote, ikiwa pamoja na mashabiki, wachezaji, viongozi pamoja na wadau mbalimbali wa soka ndani ya klabu hii, tunayo furaha kubwa msimu huu kwa hapa tulipofikia.

“Nawashukuru mashabiki kwa sapoti yao kwa kipindi chote hadi kufikia hapo, umoja wao umewafanya wachezaji kujisikia kuwa na furaha mara kwa mara katika michezo yao kutokana na sapoti waliyopata,” alisema Ancelotti.

KUU la Wauza Madawa ya Kulevya Tanzania Lasafirishwa Kimya Kimya Kwenda Nchini Marekani

$
0
0
ANAYEDAIWA kuwa Kiongozi wa Taasisi ya Kusambaza Dawa za Kulevya nchini, Ally Haji, maarufu Shikuba na wenzake wawili, wamesafirishwa kimya kimya kwenda nchini Marekani usiku wa kuamkia jana.

Pamoja na rufaa iliyokatwa Mahakama Kuu ya Tanzania kupinga uamuzi huo, Serikali imewaondoa bila kutoa taarifa kwa mawakili wala ndugu wa watuhumiwa hao.

Taarifa za kupelekwa Marekani Shikuba na wenzake; Iddy Mfuru na Tiko Adam, zilipatikana jana kutoka vyanzo mbalimbali vya kuaminika, akiwamo mke wa mfanyabiashara huyo na mawakili wao.

Aprili 12, mwaka huu, Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam, ilikubali maombi ya aliyekuwa Waziri wa Katiba na Sheria, Harrison Mwakyembe ya kutaka Watanzania hao washikiliwe na kusafirishwa kwenda Marekani kujibu mashtaka ya kusafirisha na kusambaza dawa za kulevya yanayowakabili nchini humo.

Baada ya uamuzi huo, Aprili 13, mwaka huu, mawakili wa Shikuba na wenzake; Hudson Ndusyepo, Majura Magafu na Adinani Chitale, waliwasilisha katika mahakama hiyo nia ya kukata rufaa na tayari waliwasilisha sababu za kukata rufaa Mahakama Kuu ya Tanzania kama sheria inavyowataka endapo hawakuridhika.

Akizungumza na MTANZANIA, mtoa taarifa mmoja ambaye hakutaka kutajwa jina lake, alisema watuhumiwa hao wameshasafirishwa kuelekea Marekani tangu juzi saa sita usiku.

Mke wa Shikuba, Munira Ally, alipoulizwa kwa simu, alikiri kwamba mumewe alishasafirishwa na hawakupewa taarifa kuhusu kuondoka kwao.

“Waliondoka jana (juzi) saa tano na dakika kumi na ndege ya KLM kuelekea Marekani, sisi tumepata taarifa wakiwa wameshaondoka, hatuna jinsi walishaondoka.

“Baba mkwe hali yake ni mbaya baada ya kupata taarifa hizi, pale nyumbani watu wanajua wanazungumza anasikia… huwa anasumbuliwa na ugonjwa wa sukari na shinikizo la damu.

 “Tunataka tukutane na mawakili tuzungumze nini cha kufanya, gerezani atakuwa kaacha vitu vyake, napanga utaratibu niende Gereza la Ukonga kufuata vitu mbalimbali zikiwemo nyaraka za rufaa,” alisema Munira.

Wakili Ndusyepo, akizungumzia hilo, alisema amesikia wateja wao wameondoka nchini juzi usiku, huku Serikali ikijua kwamba kuna rufaa Mahakama Kuu.

“Serikali inajua kuna rufaa imekatwa kupinga uamuzi wa Mahakama ya Kisutu, inaacha kuheshimu, sheria inadharauliwa, Katiba haifuatwi, leo wamefanyiwa hawa kesho watafanyiwa wengine, kuna haja ya kupiga kelele,” alisema.

Wakili Magafu alipotakiwa kuzungumzia suala hilo, alisema alipata taarifa ya kuondoka kwao kutoka kwa Ndusyepo.

Awali Aprili 10, mwaka huu, Serikali iliwasilisha maombi katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu pamoja na vielelezo mbalimbali, ikiomba watuhumiwa wazuiliwe na kusafirishwa kwenda Marekani kujibu tuhuma za kujihusisha na biashara ya dawa za kulevya.

Mahakama ilisikiliza maombi hayo Aprili 11, mwaka huu na kutoa uamuzi Aprili 12, ikibariki watuhumiwa hao kwenda nchini humo baada ya kujiridhisha kwa ushahidi uliotolewa mahakamani.

Hakimu Mkazi Mfawidhi, Cyprian Mkeha aliposoma uamuzi baada ya kusikiliza hoja za pande mbili, alisema mahakama kabla ya kuamua ilijiuliza maswali kadhaa, ikiwamo kama mashtaka wanayohusishwa nayo wajibu maombi yako katika utaratibu wa kubadilisha wahalifu.

Pia mahakama ilijiuliza na kubaini kuwa kuna makubaliano ya kubadilishana wahalifu kati ya nchi hizo mbili.

Hakimu Mkeha alisema kama wajibu maombi watakuwa wanapingana na uamuzi huo, mahakama inawapa nafasi ya kukata rufaa ndani ya siku 15 na walifanya hivyo.

Mwakyembe aliwasilisha maombi Februari 15, mwaka huu, akiomba mahakama hiyo kuamuru Shikuba, Mfuru na Adam washikiliwe wakati wakisubiri kibali cha kuwasafirisha kwenda Marekani kujibu tuhuma za kula njama, kusafirisha na kusambaza dawa za kulevya nchini humo.

Jamhuri ikiwakilishwa na Wakili wa Serikali Mkuu, Edwin Kakolaki, katika kuiridhisha mahakama iliwasilisha maombi na ushahidi dhidi ya wajibu maombi, kuonyesha kujihusisha kwao katika matukio hayo.

Ushahidi ulionyesha kwamba Marekani iliwachunguza wajibu maombi kwa miaka minne na walitumia Dola 10,000 kununua dawa hizo kutoka kwa taasisi yao ili kubaini ukweli.

Wajibu maombi ilibainika walikuwa wakisafirisha heroin na cocaine kwa kutumia magari, na wakifikisha dawa hizo Marekani huwatumia watu kusambaza kwa kutumia ndege binafsi na Shikuba ndio kiongozi wa taasisi hiyo.

Kakolaki alidai maombi yaliambatana na kiapo kilichoapwa na Richard Magnes ambaye anadai wajibu maombi wanatuhumiwa kuingiza dawa za kulevya zaidi ya kilo 1.78 Marekani.

Shikuba, ambaye amekuwa akihusishwa na biashara kubwa ya usafirishaji dawa za kulevya kati ya Afrika Mashariki, Asia, Ulaya na Marekani, alikamatwa mwaka 2014 nchini, akihusishwa na shehena ya kilo 210 za heroin zilizokamatwa mkoani Lindi mwaka 2012.

Serikali ya Marekani iliamua kutaifisha mali za mfanyabiashara huyo na kupiga marufuku kampuni za nchi hiyo kujihusisha na biashara zake.

Taarifa iliyotolewa na Kitengo cha Udhibiti wa Mali za Nje cha Wizara ya Fedha ya Marekani, ilieleza kuwa Shikuba ametambuliwa kama kinara wa usafirishaji wa dawa za kulevya kwa mujibu wa Sheria ya Utambuzi wa Vinara wa Dawa za Kulevya wa Nje ya nchi hiyo.

Kwa mujibu wa gazeti la The New York Times, sheria hiyo imekuwa ikitumiwa na Marekani kufuatilia wahalifu kadhaa wanaojihusisha na biashara hiyo duniani na kwamba Shikuba amekuwa akijaribu mara kadhaa kurubuni viongozi wa Serikali za Afrika kuepuka kukamatwa na kufunguliwa mashtaka kutokana na biashara zake haramu.

Imeelezwa kuwa tangu mwaka 2006, Shikuba amekuwa akiongoza wanachama wa mtandao wake kutuma shehena za dawa za kulevya kwenda sehemu kadhaa duniani kama China, Ulaya na Marekani.

AJALI: Tazama Video ya Mwanamke Akigongwa na Gari Wakati Likirudi Nyuma na Kumbamiza Ukutani..Inasikitisha

$
0
0
Video ambayo ilichukuliwa kwa kamera za CCTV imeonyesha ajali mbaya ambayo imetokea nchini Kenya ambapo imehusisha gari aina ya Vitz, mlinzi alikuwa akimuelekeza dereva wa Vitz sehemu ya kupaki ambapo pembeni palikuwa na mwanamke amekaa pembezoni mwa barabara lakini kilichotokea baada ya hapo kinaweza kukuvunja moyo...

Dereva wa gari hiyo ambae ni mwanamke inavyosemekana alikuwa lena hivyo gari likamshinda kurudisha nyuma na kujikuta amemparamia mwanamke aliyekaa na kumbamiza ukutani..Haijajulikana bado kama mwanamke huyo alipona ama la...

Tazama video Hapa chini:
Viewing all 104795 articles
Browse latest View live




Latest Images