Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104807 articles
Browse latest View live

DC wa Iringa Richard Kasesela Aamua "Kulipa" Pozi la Picha ya Kikwete

$
0
0
Mzee wa "Mapicha",Mkuu wa Wilaya ya Iringa Kasesela,ameamua kumlipa JK kwa pozi la kwenye sofa.

Siku mbili hizi katika mitandao ya kijamii,kulienea picha ya Rais Mstaafu JK akiwa amepozi kwenye sofa huku anaperuzi na kudadisi kilongalonga chake.

Kasesela akaona isiwe tabu,ngoja na yeye alipe pozi la swahiba wake JK ili waende sambamba.
Pichani ni JK na Kasesela katika picha yenye mfanano wa mapozi

Unampa Maksi ngapi kwa Kupatia pozi?

EMMANUEL Mbasha Amvua Nguo Hadharani Mzazi Mwenzie ‘Flora Henry’

$
0
0
Muimbaji  wa nyimbo za Injili nchini Tanzania, Emmanuel Mbasha ambaye alikuwa mume wa Mwanamama Flora Henry amefunguka na kuweka wazi kwa kila kitu kuwa Mrembo huyo ni mtu wa kuruka kuruka kwa Wanaume kwani anaendeshwa na tamaa.

Image result for flora mbasha na emmanuel mbasha
Enzi za uhai wa ndoa yao Emannuel na Flora Mbasha katikati ni Mtoto wao.

Mbasha amesema Flora amezoea maisha ya kurukaruka na wanaume kwani hata yeye licha ya kumtoa kijijini na kumleta mjini bado alimkimbia kwa tamaa ndogo ndogo.

“Unajua Flora amechaguwa kuwa na maisha ya kurukaruka, kwani hata baada ya mimi alikuwa na wanaume wengine kadhaa, saizi kaolewa  tena akiona maisha magumu huko aliko atakwenda kwa mwingine hayo ndiyo maisha aliyochagua.“Alisema Emannuel Mbasha na kusisitiza kuwa, Flora hakumuacha kwa sababu ya Kuporomoka kiuchumi.

“Mimi nilikuwa na pesa muda mrefu ndiyo maana nilimchukua  Flora na kumleta mjini, tukaanza maisha pamoja, nikamuuingiza studio akaanza kurekodi na Watanzania kumjua, hivyo pesa nilikuwa nazo maana ningekuwa sina pesa sidhani kama angekubali kuolewa na mimi,“Alisema Emannuel Mbasha kwenye Mahojiano yake na EATV.

Flora Henry aliachana na Emannuel Mbasha kwa mvutano kwenye ndoa yao ambayo ilibarikiwa kupata mtoto mmoja wa kike na tayari mrembo huyo ameshafunga ndoa nyingine ya pili wikiendi iliyopita na Mwanaume mwingine huko Jijini Mwanza.

FREEMAN Mbowe Agonga Mwamba Kortini

$
0
0

MAHAKAMA Kuu Tanzania, Kanda ya Dar es Salaam, imefuta maombi ya kesi ya kikatiba yaliyofunguliwa na Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe.

Kutupwa kwa kesi hiyo kumetokana na mahakama hiyo kukubali pingamizi la walalamikiwa kwamba mahakama hiyo haina mamkala ya kuyasikiliza.

Walalamikiwa katika maombi hayo ni  Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam (kwa sasa Paul Makonda), Kamishna wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam (Simon Siro) na Mkuu wa Upelelezi Kanda Maalum ya Dar es Salaam (ZCO) (Camillius Wambura).

Uamuzi huo ulitolewa jana na jopo  la majaji watatu, likiongozwa na Mwenyekiti wake Jaji Sekiet Kihiyo, akisaidiana na Pellagia Khaday na Dk. Lugano Mwandambo.

Akisoma uamuzi huo kwa niaba ya jopo, Jaji Khaday alisema upande wa walalamikiwa uliwasilisha pingamizi la awali kwamba mahakama hiyo haina mamlaka ya kusikiliza maombi hayo kwa sababu mlalamikaji alitakiwa kuwasilisha katika mamlaka husika.

Pia sheria za haki za msingi kifungu cha 8 kidogo cha (2) sura ya 3, inakataza mahakama hiyo kusikiliza maombi kama hayo na kwamba kuna mamlaka zinazoshughulikia kabla ya kufikishwa mahakamani kwa sababu si kesi ya kikatiba.

Aidha, mahakama imetoa uamuzi huo baada ya mlalamikaji kushindwa kufika mahakamani kuwasilisha majibu ya pingamizi la awali la walalamikiwa hata baada ya kupewa muda wa kufanya hivyo.

Katika kesi ya Msingi ya Kikatiba Mbowe alikuwa anapinga kitendo cha polisi kumtaka afike kituoni kwa madai kuwa ni utekelezaji wa amri ya Mkuu wa Mkoa.

Mbowe katika kesi hiyo alidai kuwa sheria inayompa Mkuu wa Mkoa mamlaka ya kutoa amri ya kumkamata na kumweka ndani mtu, yako kinyume cha katiba kwa madai kuwa ilitungwa katika mazingira ambayo hapakuwa na vituo vya polisi vya kutosha.

Kutokana na madai hayo, Mbowe alidai kuwa kwa mazingira ya sasa sheria hiyo imeshapitwa na wakati na anaiomba mahakama itamke kuwa ni kinyume cha katiba.

Kadhalika alidai kuwa hata kama Mkuu wa Mkoa alikuwa anatekeleza mamlaka yake kwa mujibu wa sheria hiyo, hakutimiza matakwa ya kisheria, ambayo ni pamoja na kutoa taarifa kwa Hakimu wa Mahakama ya Wilaya au ya Hakimu Mkazi na kwamba mahakama kama itaona alikuwa sawa kutoa amri hiyo, imwamuru afuate matakwa ya kisheria, ikiwa ni pamoja na kulinda haki za binadamu katika kutekeleza madaraka yake hayo.

DOGO Asley Atoa Kitchenpart kwa Wanawake..!!!

$
0
0

Msanii wa muziki kutoka Mkubwa na Wanawe, Aslay amedai wimbo wake mpya ‘Usiitie Doa’ ni maalum kwaajili ya kuwafunda akina dada ambao wanaingia kwenye maisha ya ndoa.

Muimbaji huyo ambaye ni baba wa mtoto mmoja, amesema ndani ya wimbo huo amevaa uhusika wa baba ambaye anamweleza mwanaye namna ya kuishi vizuri na watu.

“Wimbo ‘Usiitie Doa’ nimemwongelea msichana ambaye anaenda kuolewa, yaani nimekuwa kama namfunda japo kuwa namfunda kiume kama baba. Mwanangu ukienda huko ishi vizuri na mumeo, angalia maisha yako vizuri, fuatilia nyendo zako vizuri, ogopa marafiki wabaya,” alisema Aslay.

Katika hatua nyingine muimbaji huyo amedai hakuwa na mpango wa kumtumia Stan Bakora kwenye video ya wimbo huo.

“Stan ni mwanangu kinoma, wakati naangaika kutafuta nguo nilimfuata huyu jamaa akanitengenezea nguo kali sana. Pia akaniambia mimi nitakuwa kama mwanaume wa ukweli. Kwa hiyo jamaa amenionyesha upendo wa hali ya juu na namshukuru sana,”

BASHITE Aufyata Bungeni..Awampooleee na Kukiri Makosa Yake..!!!

$
0
0

PAMOJA na majigambo na lugha za kejeli, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, amesalimu amri mbele ya Bunge na hatimaye chombo hicho kumsamehe baada ya kuomba radhi na kuonyesha unyenyekevu, alipoitwa kuhojiwa.

Mbali na kiongozi huyo, bunge pia limewasamehe Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe na Mkuu wa Wilaya Arumeru, Alexander Mnyeti, baada ya kufuata nyayo za Makonda kwa kukiri kutekeleza na kuomba radhi kwa kutoa lugha isiyofaa.

Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge, Almas Maige akiwasilisha bungeni mjini hapa jana taarifa kuhusu mashauri yanayowahusu watatu hao, alipendekeza Bunge liwasamehe kutokana na uungwana wao wa kukiri, kuomba radhi na kujutia makosa yao walipofika mbele ya kamati hiyo kwa ajili ya kuhojiwa.

Akizungumzia shauri la kigogo huyo, aliyekuwa anatuhumiwa kusema wabunge wanasinzia bungeni, Maige alisema kamati yake ilikuwa na hadidu mbili za rejea, kama ni kweli alitamka maneno hayo yaliyolalamikiwa na wabunge na hatua za kisheria zinazopaswa kuchukuliwa dhidi ya yake kama alitenda kosa hilo.

Alisema chanzo cha malalamiko dhidi yake ni hatua aliyoichukua ya kutaja majina ya watu wanaojihusisha na dawa za kulevya.

Alisema katika mkutano wake na waandishi wa habari ofisini kwake jijini Dar es Salaam, kiongozi huyo wa serikali aliulizwa hatua anazozichukua dhidi ya baadhi ya wabunge wanaotuhumiwa kujihusisha na dawa za kulevya na wengine walikuwa wameanza kutajana wao wenyewe bungeni.

Kwa mujibu wa Maige, katika kujibu swali hilo, alisema: "... zingine ni mbwembwe tu, unajua mle ndani (bungeni) wakati mwingine wanachoka na kusinzia lazima kuwe na watu kidogo akili zao zinawasaidia kuamka, kucheka na kufurahi maisha yanaendelea."

Maige alisema kiongozi huyo alifika mbele ya kamati yake Machi 29, mwaka huu, majira ya saa nne asubuhi kwenye Ukumbi wa Spika na kusomewa tuhuma dhidi yake na kukiri kwamba ni kweli alitoa kauli hiyo.

Alisema katika maelezo yake alionyesha kujutia kauli hiyo ambayo iliwakwaza na kuwavunjia heshima wabunge, hivyo aliomba radhi na kueleza kuwa hata kabla ya kuitwa mbele ya kamati, tayari alikuwa ameandika barua kwa Spika ya kuliomba radhi Bunge.

Maige alinukuu sehemu ya maelezo ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam kuomba radhi kuwa ni: "... najisikia vibaya kusimama mbele yenu kwa kuwakwaza na kuwavunjia heshima ambayo sikupaswa kufanya hasa kwa watu ambao mmekuwa walezi na ni watu ambao mnanitegemea nifanye vizuri kwa ajili ya kuwawakilisha vijana wengine.

"Itakumbukwa baada ya kauli yangu, nilichukua jukumu la kuandika barua kwa Mheshimiwa Spika, baada ya kusikiliza mjadala katika Bunge na kumwomba radhi kwa kitendo cha kauli yangu niliyoitoa wakati nikijibu swali pale ambapo mwandishi alitaka kujua mambo kadhaa yaliyofanyika.

"Kwa hiyo, akili yangu ilikuwa na mtazamo wa namna hiyo, haikuwa na mtazamo wa kulidharau Bunge, haikuwa na mtazamo wa kumvunjia heshima mbunge yeyote yule na kwa kweli najisikia vibaya sana kusimama mbele yenu na ninaomba radhi sana sana kwa kauli niliyoitoa na tafsiri iliyopatikana."

Kutokana na maelezo hayo, Maige alisema kamati yake imejiridhisha bila shaka yoyote kwamba maneno ya Mkuu wa Mkoa huyo yalivunja haki na kudharau mamlaka ya Bunge.

Alisema kitendo cha kutamka maneno hayo ni cha kudharau, kudhalilisha na kulifedhehesha Bunge.

Hata hivyo, licha ya kukiuka masharti ya kifungu cha 26(e) cha Sheria ya Kinga, Haki na Madaraka ya Bunge (Sura ya 296), Maige alisema Bunge limeazimia Mkuu wa Mkoa huyo asamehewe kutokana na kitendo chake cha kiungwana cha kukiri na kujutia kosa lake na kuliomba radhi Bunge mbele ya kamati yake.

Alisema kamati yake imezingatia ukweli kwamba Mkuu wa Mkoa huyo hakuisumbua kwa namna yoyote ile bali alikuwa mtii na alitoa ushirikiano mkubwa kwa kamati.

Alisema kamati pia imezingatia kuwa kiongozi huyo wa serikali hakuwa na dhamira ya kulidharau wala kulidhalilisha Bunge kama ambavyo ilichukuliwa.

Mbunge huyo wa Newala (CCM) alisema kamati imezingatia kuwa Mkuu wa Mkoa huyo alikuwa hajawahi kutenda kosa kama hilo na kufikishwa mbele ya kamati na pia amekiri kosa lake na kuomba radhi.

Alisema msamaha wake pia umezingatia kitendo cha Mkuu wa Mkoa huyo kuandika barua kwa Spika kuomba radhi, uzoefu wa mabunge mengine ya Jumuiya ya Madola kuhusu adhabu kwa mtu ambaye amekiri kosa la kudharau Bunge na kuomba msamaha.

SHAURI DC MNYETI
Akizungumzia shauri la DC Mnyeti, Maige alisema chanzo cha malalamiko hayo ni taarifa ya Kamati ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa iliyowasilishwa Februari 3, mwaka huu na kuanisha changamoto za mapendekezo ya kuzitatua ikiwa ni pamoja na suala la Wakuu wa Mikoa na Wilaya kutumia vibaya mamlaka yao.

Maige alisema kuwa katika taarifa hiyo, kamati ilipendekeza waziri mwenye dhamana awapatie semina viongozi hao wa serikali namna ya kutekeleza majukumu yao.

Kutokana na masuala mbalimbali yaliyojadiliwa bungeni kuhusiana na jambo hilo, Maige alisema ndipo Mnyeti alipoandika katika ukurasa wake wa mtandao wa Facebook akiyaita mapendekezo hayo ni ya upuuzi mtupu na kwama wabunge hawajielewi na anawashauri wafanye kazi zao.

Akinukuu maneno hayo, Maige alisema: "Upuuzi mtupu. Wabunge hawa hawajielewi. Nawashauri fanyeni kazi zenu za wengine waachie wenyewe."

Alisema kuwa Mnyeti aliitwa mbele ya kamati hiyo Aprili 6, mwaka huu na kuhojiwa kuhusu tuhuma zilizomkabili na alikiri kuandika maneno hayo na kumiliki akaunti ya Facebook iliyoandika maneno yaliyolalamikiwa.

Alisema kuwa baada ya maelezo, shahidi aliomba radhi kwa Bunge na kusema hana ubavu wa kushindana nalo.

Maige alinukuu maneno ya Mnyeti akisema: "...Mheshimiwa Mwenyekiti, basi naomba sasa kamati yako itumie busara na ninaomba radhi kwamba limekuwa kubwa lakini halikuwa kusudio langu tangu awali kwamba sasa nilikwaze Bunge kwa 'style' (mtindo) hiyo.

"Mimi naomba radhi kamati yako, itumie busara zake lakini lengo kutoka moyoni kwangu halikuwa katika hali hiyo ambayo limechukuliwa... Nikiri kuwa ni madhaifu yangu sikutenda kiungwana, naomba kamati inisamehe kuanzia sasa na kuendelea haitajirudia tena. Kwa hiyo, binafsi niiombe kamati yako kwa nafasi ya kipekee ione umuhimu wa kunisamehe..."

Kutokana na maelezo hayo ya Mnyeti, Mkuchika alisema kamati yake imethibitisha kuwa Mkuu wa Wilaya huyo aliingilia uhuru na kuvunja haki za Bunge kinyume cha kifungu cha 26(e) cha Sheria ya Kinga, Haki na Madaraka ya Bunge.

Alisema kitendo cha kuandika maneno hayo ni cha dharau, kudhalilisha na kulifedhehesha Bunge lakini kwa kuzingatia kwamba Mnyeti hakuisumbua kamati na alikuwa mtii na kutoa ushirikiano na hajawahi kutenda kosa jingine la aina hiyo, Bunge limeazimia kumsamehe.     
      
Februari 8, mwaka huu, Bunge lilipitisha maazimio ya kuwaita bungeni na kuwahoji Makonda na Mnyeti kutokana na hoja ya Mbunge wa Ukonga, Mwita Waitara (Chadema) aliyewatuhumu viongozi hao wa serikali kuudharau mhimili huo na ikithibitika, wachukuliwe hatua kwa mujibu wa sheria zilizopo.

SHAURI LA MBOWE
Akizungumzia shauri la Mbowe, Mkuchika alisema lilianzia Aprili 4, mwaka huu wakati wa mkutano wa kwanza wa Bunge la Bajeti ambao ulikuwa na uchaguzi wa wabunge wa Bunge la Afrika Mashariki (EALA) ambapo baadhi ya wabunge walionekana kufanya vitendo vya utovu wa nidhamu.

Alisema Mbowe alinukuliwa na vyombo vya habari akitoa maneno ya utovu wa nidhamu kwa kudharau Mamlaka ya Spika na kutoa maneno ya kuudhi dhidi ya wabunge wengine, kitendo ambacho alikifanya akiwa nje ya ukumbi wa Bunge baada ya uchaguzi huo.

Katika uchunguzi wa kamati yake, Mkuchika alisema walijiridhisha kuwa Mbowe alitamka maneno: "... Spika amevunja Kanuni za Bunge, sheria hazikuheshimiwa, ubabe umetumika... ni mkakati wa kiserikali, tunajua Rais anahusika, Waziri Mkuu anahusika, viongozi wa chama chao wanahusika...

"...tumeleta wagombea wazuri sana wawili 'very competent', wamepigiwa kura za hapana kwa sababu ulikuwa mkakati wa Chama Cha Mapinduzi, tumeona ujinga na upumbavu mtupu... uchaguzi huu umekuwa wa kijinga"

Mkuchika alisema kuwa baada ya kumuita mbele ya kamati, Mbowe alikiri wazi kuwa alitamka maneno hayo na akaliomba radhi Bunge.

Licha ya kumtia hatiani kiongozi huyo wa upinzani kwa kudharau mamlaka ya Spika, Mkuchika alisema Bunge limeazimia kumsamehe kutokana na kitendo chake cha kuonyesha ushirikiano na kuomba radhi huku likimkumbusha kuwa anatakiwa kuwa mfano kwa wengine anaowaongoza.

Mbowe ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) na Mbunge wa Hai, alitakiwa na Spika kufika mbele ya kamati hiyo mwanzoni mwa mwezi uliopita baada ya Mbunge wa Mwibara, Kangi Lugola (CCM) kulamika bungeni kuhusu kauli zake hizo zilizomtia hatiani.

MBOWE Agonga Mwamba Kortini..Kesi Aliyomfungulia Makonda Yafutwa..!!!

$
0
0

MAHAKAMA Kuu Tanzania, Kanda ya Dar es Salaam, imefuta maombi ya kesi ya kikatiba yaliyofunguliwa na Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe.

Kutupwa kwa kesi hiyo kumetokana na mahakama hiyo kukubali pingamizi la walalamikiwa kwamba mahakama hiyo haina mamkala ya kuyasikiliza.

Walalamikiwa katika maombi hayo ni  Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam (kwa sasa Paul Makonda), Kamishna wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam (Simon Siro) na Mkuu wa Upelelezi Kanda Maalum ya Dar es Salaam (ZCO) (Camillius Wambura).

Uamuzi huo ulitolewa jana na jopo  la majaji watatu, likiongozwa na Mwenyekiti wake Jaji Sekiet Kihiyo, akisaidiana na Pellagia Khaday na Dk. Lugano Mwandambo.

Akisoma uamuzi huo kwa niaba ya jopo, Jaji Khaday alisema upande wa walalamikiwa uliwasilisha pingamizi la awali kwamba mahakama hiyo haina mamlaka ya kusikiliza maombi hayo kwa sababu mlalamikaji alitakiwa kuwasilisha katika mamlaka husika.

Pia sheria za haki za msingi kifungu cha 8 kidogo cha (2) sura ya 3, inakataza mahakama hiyo kusikiliza maombi kama hayo na kwamba kuna mamlaka zinazoshughulikia kabla ya kufikishwa mahakamani kwa sababu si kesi ya kikatiba.

Aidha, mahakama imetoa uamuzi huo baada ya mlalamikaji kushindwa kufika mahakamani kuwasilisha majibu ya pingamizi la awali la walalamikiwa hata baada ya kupewa muda wa kufanya hivyo.

Katika kesi ya Msingi ya Kikatiba Mbowe alikuwa anapinga kitendo cha polisi kumtaka afike kituoni kwa madai kuwa ni utekelezaji wa amri ya Mkuu wa Mkoa.

Mbowe katika kesi hiyo alidai kuwa sheria inayompa Mkuu wa Mkoa mamlaka ya kutoa amri ya kumkamata na kumweka ndani mtu, yako kinyume cha katiba kwa madai kuwa ilitungwa katika mazingira ambayo hapakuwa na vituo vya polisi vya kutosha.

Kutokana na madai hayo, Mbowe alidai kuwa kwa mazingira ya sasa sheria hiyo imeshapitwa na wakati na anaiomba mahakama itamke kuwa ni kinyume cha katiba.

Kadhalika alidai kuwa hata kama Mkuu wa Mkoa alikuwa anatekeleza mamlaka yake kwa mujibu wa sheria hiyo, hakutimiza matakwa ya kisheria, ambayo ni pamoja na kutoa taarifa kwa Hakimu wa Mahakama ya Wilaya au ya Hakimu Mkazi na kwamba mahakama kama itaona alikuwa sawa kutoa amri hiyo, imwamuru afuate matakwa ya kisheria, ikiwa ni pamoja na kulinda haki za binadamu katika kutekeleza madaraka yake hayo.

UTOTO Wamtesa Tunda Kimapenzi..Afunguka ya Moyoni Jinsi Anvyotamani Kulala na Staa wa Nigeria Wizkid..!!!

$
0
0

UTOTO unaonekana kumtesa muuza sura kwenye video za wasanii wa Kibongo, Tunda Sebastian ambaye licha ya kuwa katika uhusiano wa kimapenzi na mtu mwingine, ameibuka na kudai anampenda ‘kufa mtu‘ msanii wa Nigeria, Wizkid.

Akizun-gumza na Risasi Vibes, mwanadada huyo alisema kuwa amekuwa akimzimia jamaa huyo kwa muda mrefu na ndoto zake ni siku moja kuwa naye kwenye uhusiano wa kimapenzi.

“Msema kweli mpenzi wa Mungu. Kiukweli ninampenda Wizkid. Ni bora niweke wazi maana hata nisiposema nitabaki naumia tu moyoni,” alisema Tunda.

TONY Blair Atangaza Kurudi Kwenye Siasa za Uingereza..!!!!

$
0
0

WAZIRI Mkuu wa zamani wa Uingereza, Tony Blair ametangaza kuwa anarejea tena kwenye siasa za Uingereza ili kupambana dhidi ya uamuzi wa kujiondoa kutoka Umoja wa Ulaya, maarufu Brexit.

Blair ambaye alikiongoza Chama cha Labour kuanzia mwaka 1994 hadi 2007, hata hivyo hatagombea katika uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Juni 8.

Lakini ataunda vuguvugu la kisiasa juu ya majadiliano ya Uingereza kujiondoa Umoja wa Ulaya.

Blair (63), ambaye alikuwa Waziri Mkuu wa Uingereza kwa muongo mmoja kuanzia mwaka 1997, alisema anafahamu uamuzi wake huu utakumbwa na ukosoaji mkali.

Lakini alisema si sawa kwake kuachia suala la Brexit liende kama liendavyo, bila kutoa mchango wake.

Soma Nafasi za Kazi Zilizotangazwa Siku ya Leo...

UKWELI Mchungu...Narudia Tena Kukwambia Maalim Seif Jitazame Nyuma Usiogope Kivuli Chako Mwenyewe..!!!

$
0
0

Mgogoro uliopo ndani ya Cuf ni mkubwa sana. 
Maalim Seif unaushawishi mkubwa ndani ya Cuf, pia fahamu kwamba Lipumba nae anaushawishi mkubwa tu kama ulivyo wewe. 

Habari ya mashabiki ndani ya mitandao ya kijamii si suluhu ya kumaliza mgogoro huu.

Umesikika ukisema ni Bora uzungumze na CCM, lakini si Lipumba. Mimi nasema hapana. 

Mgogoro huu Utamalizwa kwa wewe na Lipumba kukaa mezani na kujadiliana Nini kifanyike ili muendelee na ujenzi wa Chama chenu. 
Shirikisheni wanataaluma mbalimbali wa masuala ya kisiasa, kisheria, kijamii na kitamaduni katika maridhiano yenu. 

Wapambe walio nyuma yenu si wema hata kidogo. 
Msipo kubali kukaa na kuyamaliza kwa majadiliano hakika hata patikana mshindi. Matokeo yake mnaiua CUF kwa mikono yenu wenyewe. 

Mmeijenga kwa jasho na Damu nyingi za wanachama wenu lakini haya hamkumbuki hata kidogo kwa kua kuna misukumo nyuma yenu isio salama. 

Namalizia kwa kusema kwamba mchawi wa CUF ni wewe Maalim Seif na Lipumba. 
Mtasingizia kila kundi, kila Raia. 

Kubalini kukaa mezani na kuyamaliza.

KIMENUKAA..JB,Ray na Rich Wafunguka Mazito Juu ya Tuhuma za Kuhongwa Viwanja na Pesa Ili Waongoze Maandamano ya Wasanii wa Bongo Movie..!!!!

$
0
0

Baada ya kuwepo kwa madai kuwa mastaa wa filamu Bongo, Jacob Steven (JB), Single Mtambalike (Rich) na Vincent Kigosi (Ray) walihongwa fedha na viwanja ili ‘kuinjinia’ maandamano ya hivi karibuni kupinga sinema za nje, mastaa hao wamebanwa na hatimaye kufungukia ishu hiyo inayowatafuna, Risasi Mchanganyiko lina mkanda kamili.

Chanzo kilicho karibu na tasnia hiyo kililiambia Risasi Mchanganyiko kuwa kampuni moja ya usambazaji filamu (jina kapuni kwa sasa), iliwapa fedha baadhi ya waigizaji ili wafanye maandamano ya kuziondoa sokoni filamu hizo za nje, zinazodaiwa kukingiwa kifua na Rais wa Shirikisho la Filamu Tanzania, Simon Mwakifwamba.

Inadaiwa kuwa baada ya kampuni hiyo ya usambazaji ‘kupenyeza sumu hiyo’ waigizaji hao walikwenda kwa kigogo mmoja wa kisiasa na kumshawishi kuwaunga mkono, ambaye naye alikubali na kuwaomba waigizaji hao kufanya kila wawezalo, kumtoa kwenye kiti chake, Simon Mwakifwamba, kwani ana ukaribu na hasimu wake wa siasa.

“Kuna watu wamevuta huku na huku katika hii ishu, wale wasambazaji hawazitaki kabisa filamu za ndani kwa sababu zinaharibu soko lao, ingawa wana kisingizio cha kodi, hawana lolote, watu hawataki sinema za Bongo kwa sababu hazina ubora,” kilisema chanzo hicho.

Kiliendelea kudai kuwa katika kuhakikisha lengo hilo linafanikiwa, kigogo huyo wa kisiasa anadaiwa kutoa hongo ya viwanja kwa mastaa hao, ambavyo vinadaiwa viko Kigamboni jijini Dar.

Ili kuujua ukweli juu ya tuhuma hizo, Risasi Mchanganyiko liliwatafuta waliotajwa na kuwabana ili wafungukie ishi hiyo.

Ray alipoulizwa alijibu akisema; “Hiyo ishu ya kupewa viwanja hainiingii akilini, kwanza ili iweje, mimi nilienda kwenye maandamano maana ni ishu iliyokuwa inanihusu kama msanii wa filamu, huyo Mwakifwamba ambaye anapinga suala hilo atakuwa ana mambo yake ya kisiasa, kwanza yeye mara ya mwisho kutoa filamu sijui ni lini.

“Sisi tunapigania haki yetu maana filamu za nje hazitozwi kodi, ndiyo maana zinauzwa bei rahisi kitu ambacho kinaathiri soko la filamu zetu nzuri na zenye ubora tunazozitengeneza.”

Kwa upande wa JB alipoulizwa kuhusiana na hilo alijibu; “Ili iweje? Kwani (anamtaja kigogo huyo) anapata wapi viwanja? Uongo huo wa kijinga. Mimi nilienda pale kushiriki maandamano kwa sababu ni mdau, si vinginevyo.

“Hebu fikiria, hivi unaona tofauti za bei za bia? Bia za nje na ndani ziko sawasawa? Zinatofautiana kwa sababu ya kodi na ili kulinda viwanda vya ndani,” alisema muigizaji huyo maarufu.

Kwa upande wa Rich, naye kama walivyo wenzake, alisema madai ya kupewa hongo ya viwanja na fedha ni ya uongo, kwani yeye alianza kushiriki kampeni za kukamata filamu za nje tangu enzi zile Nape Nnauye akiwa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo.

“Kwanza mimi siyo timu (kigogo), nilienda pale kama mdau na wala sikwenda pale kupinga kazi za nje, nilienda pale kutaka filamu zote zilipe kodi. Tatizo la filamu zetu siyo zile za nje, bali ni ubovu wa kazi zetu.

“Kama tutatengeneza kazi nzuri zitauzika tu sokoni, lakini kama kila mtu mwenye fedha anadhani anaweza kutengeneza filamu, hiyo ndiyo inayoharibu soko letu. Ninakubali kuna udhaifu katika filamu za ndani, ambazo nadhani ndiyo zinachangia kuua soko, si filamu za nje,” alisema.

MWAKYEMBE Apiga Marufuku Tv na Redio Nchini Kusoma Magazeti..!!!

$
0
0

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk Harrison Mwakyembe amepiga marufuku Runinga na Redio kusoma habari nzima katika magazeti huku akivitaka kusoma vichwa vya habari tu.

Dkt. Mwakyembe ametoa agizo hilo, jijini Mwanza ambapo amesema kutekelezwa kwake kunaanza kesho (Alhamisi) tarehe 04/05. Leo ikiwa ni siku ya uhuru wa vyombo vya habari duniani, Mwakyembe amesema ataendelea kutetea na kulinda haki za waandishi wa habari huku akiwahakikishia ulinzi katika kazi zao.

Mwakyembe amesema amepiga marufuku kusomwa kwa magazeti kwenye runinga na redio, ili magazeti yaweze kuuzwa kwani punde habari yote inaposomwa kwenye chombo cha habari na watu wakasikiliza maeneo yote, hakuna mtu atakayenunua gazeti hilo.

SPIKA Ndugai Afunguka Maana ya Tusi 'FALA' Alilotukanwa na Halima Mdee Bungeni..!!!

$
0
0

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Job Ndugai jana ameonyesha aliumizwa na kitendo cha Mbunge wa Kawe kwa tiketi ya CHADEMA Mh. Halima Mdee kumwambia 'fala' bungeni na kusema hata kama mtu humpendi lakini si vyema kumtusi matusi.

Job Ndugai alisema hayo alipokuwa akitoa maana ya neno fala bungeni ambapo ilibidi arejee maana hiyo kwa kusoma kupitia kamusi ya Kiswahili ambayo ilitoa maana kuwa fala ni mtu ambaye akili zake hazifanyi kazi vizuri.

"Kwa neno ambalo alilisema Halima Mdee humu ndani, kamati imeenda kwenye tafsiri ikachukua Kamusi kwa neno lile alilosema ambalo maana yake kwa yule unayemwambia 'Fala' ni mtu ambaye akili zake hazifanyi kazi vizuri, ni mtu mpumbavu, ni mtu bwege, ni mtu mjinga, ni mtu bozi, ni gulagula. Ndiyo maana nikasema sisi Waafrika hata kama humpendi namna gani mwenzako huwezi kumfanyia hivyo" alisisitiza Job Ndugai 

KAULI za Hatari Kwenye Migogoro ya Mapenzi

$
0
0

WAKATI fulani kwenye uhusiano suala la migogoro ni la kawaida. Inaelezwa kwamba, wapenzi wanapoingia kwenye kuhitilafiana ndiyo uimara wa penzi unapotokea. 


Yeah! Matatizo hukomaza akili. Mkikaa bila kugombana ni vigumu kujua namna mwenzako alivyo hasa kama ikitokea kutoelewana baadaye.

Rafiki zangu, kugombana hakuna maana ya kumalizika kwa uhusiano hasa kwa wale walio kwenye ndoa. Mambo yanatokea, yanatatuliwa na mwisho wake maisha yanaendelea kama kawaida.


Kwa bahati mbaya sana ni kwamba, wengine wanapokuwa kwenye migogoro na wenzi wao, badala ya kutafuta njia za utatuzi, wanazalisha tatizo lingine!

Jambo la kusikitisha ni kuwa, tatizo jipya linalozaliwa linaweza kusababisha matatizo makubwa zaidi katika uhusiano huo na mwisho wake kusababisha kuachana kabisa.

Ngoja tupanue mawazo yetu leo hapa kwenye All About Love. Zipo kauli ambazo ukizitoa kwa mpenzi/mke/mume wako wakati mkiwa kwenye ugomvi, zinaweza kuzalisha tatizo kubwa zaidi mbeleni.

Tutaona tu. Tuendelee kuwa pamoja.

KWA NINI KAULI?

Inawezekana ukajiuliza; ni kwa nini nimesema kauli? Rafiki zangu, kwa kawaida, watu wakiwa kwenye ugomvi, jambo kubwa linalotokea ni kutupiana maneno.

Katika hali hiyo basi, kwa wenzi au wanandoa ni vyema kuchunga ndimi zao maana zinaweza kusababisha matatizo makubwa siku zijazo. Sasa twende tukaone... 

‘HUNA AKILI’

Wako baadhi ya watu wakigombana (hasa wanaume) wamekuwa na tabia ya kuwaambia wanawake wao: “Wewe huna akili kabisa...yaani hutumii akili kabisa katika kufanya mambo yako.

“Unakurupuka tu. Sasa ishu kama hii, hata mtoto mdogo anajua ni makosa, inakuwaje wewe unakosea?”

 

Hili ni jeraha la moyo. Mwanamke ukimwambia hana akili anajisikia vibaya, unampa kovu kubwa moyoni mwake. Anajiona wa hali ya chini na anahisi ameshuka thamani yake.

Kwake, kumwambia hana akili, ataanza kuwaza kuwa yupo mwanamke mwingine ambaye kwako ana akili kuliko yeye. Ni maumivu makali sana kwake.

‘NITAKUACHA’

Baadhi ya wanaume wana ulemavu huu. Ugomvi kidogo tu, atamwambia mwenzake: “Endelea na tabia zako za hovyo, ipo siku utajuta. Nimevumilia mengi sana lakini kuna siku nitachoka.

“Hutaamini macho yako. Siyo lazima niishi na wewe. Siwezi kuendelea kuteseka nikiwa na wewe. Nitakuacha nakuambia ukweli.”

Hii ni kauli mbaya ambayo inapandikiza chuki ndani ya moyo wa mwanamke. Kwanza kwa kumwambia hivi, hata kama alikuwa hakusaliti, unamfanya aanze kufikiria kutafuta mtu mwingine wa kumliwaza.

 

Kauli hii hasa kama ukiirudia zaidi ya mara mbili, humkaa akilini mwake na huanza kuwaza kuhusu kuwa na mwanaume mwingine nje ili apate mahali ambapo hata kama ukimuacha, atapata pumziko la uhakika.

‘NAKUVUMILIA TU’

Ni kweli mapenzi ni uvumilivu. Kuvumiliana ni siri ya uhai wa ndoa nyingi lakini hilo linapaswa kubaki moyoni.

Kugombana na mwenzako halafu umwambie kuwa unamvumilia tu, inamaana kwamba kuna siku uvumilivu wako utaondoka na utafanya maamuzi magumu – kuachana!

Si kauli njema kwa mwenzi wako. Mbaya zaidi humfanya aanze kufanya maandalizi ya mtu wa kuziba nafasi yako hata kama ni kwa usaliti. 

‘KUNA SIKU UTAJUTA’

Kauli hii haina tofauti kubwa sana na iliyotangulia maana kinachofanyika hapa ni kumuandaa mwenzi wako kwa ajili ya matatizo siku zijazo.

Kumwambia: “Kuna siku utajuta, endelea na mambo yako tu, utaona.” Hii inamaanisha kwamba, uamuzi ulio ndani yako si mzuri kwake lakini ni suala la muda tu.

Ataamini (na ndivyo ilivyo mara nyingi) kuna muda ambao atajuta sana kwa sababu yako. 

Hiyo ni sawa na kutengeneza bomu unaloliandaa kulilipua muda ujao.

Bado zipo kauli zaidi ambazo zina maudhi lakini pia zinaweza kusababisha matatizo zaidi kwa mwenzi wako

Afande Sele Ampa Makavu Msanii Wakazi..Adai Anajifanya Mjuaji

$
0
0

Mwanamuziki mkongwe wa Hip Hop Tanzania Afande Sele amesema kupitia 255 ya XXL ya Clouds FM akidai kuwa hamjui msanii wa Hip Hop Wakazi baada ya msanii huyo kuwataja wasanii wanaoandika mashairi na kusema Afande Sele hayupo technically. 

Baada ya kauli hiyo ya Wakazi, Afande Sele aliitumia account yake ya Twitter akiandika kuwa hamjui Wakazi kabla ya leo May 3, 2017 kuirudia kauli hiyo kupitia 255 akisema: 

“Naapa mbele za Mungu kwamba Wakazi simfahamu kwa sura na sijawahi kumuona. Kazi zake sijawahi ...kuzisikiliza, isipokuwa jana jioni mshikaji mmoja alinikumbusha na kusema alishawahi kuimba kama Mangwea. Kwa hiyo, alijivisha umangwea baada ya kufariki, ila sijui kazi yake hata moja. 
a
“Kuna kipindi nilijitoa kwenye Group ambalo tulikuwa wote, kwa sababu anajifanya anajua kila kitu wakati hajui kitu chochote. Sasa sioni kama kuna tija yoyote ya yeye kuniona labda mimi nafanya nini maana ni mtu ambaye hata ukisema uitishe show Manzese, hakuna anayemjua. Mimi mwenyewe simjui.” – Afande Sele.

KULA Vyakula Hivi Ili Kurudisha Heshima ya Ndoa Nyumbani Kwako..!!!

$
0
0

Tangawizi

Ndoa nyingi zimekuwa zikivunjika kutokana na mmoja wa wanadoa hoa kukosa hamu ya kushiriki tendo la ndoa bila kujua kuwa vipo vyakula tunavyokula vinavyoweza kuchangia chemistry ya miili yetu kuhusiana na suala la hamu ya kushiriki tendo la ndoa.Miongoni mwa vyakula hivyo ni pamoja na :

KARANGA

Karanga huhusika moja kwa moja na kutunza mfumo wa mzunguko wa damu kuwa na afya (vascular system).Pia mfumo wenye afya (mzunguko wa damu) katika uke na uume huwezesha mwanaume na mwanamke kupata msisimko wa mapenzi haraka hatimaye tendo la ndoa kuwa zuri na kulifurahia.
Pia karanga zina madini muhimu kama vile magnesium, asidi ya folic na zinc ambayo ni muhimu sana katika uzalishaji wa mbegu za mwanaume.

TANGAWIZI

Tangawizi ni chakula ambacho husisimua sana mfumo wa mzunguko wa damu mwilini, na tangawizi zinajulikana sana kwa kusukuma damu kwenda sehemu za viungo vya uzazi yaani uke na uume.
Inaweza kuliwa mbichi, au kupikwa au kuanikwa na kuwa kama unga.

PILIPILI

Kama tunavyojua chakula ambacho kimeungwa na pilipili hufanya hata mapigo ya moyo kuwa tofauti na wakati mwingine hata jasho kutoka au kamasi kutoka.

Kwenye pilipili kuna kitu kinaitwa capsaicin ambacho hufanya pilipili iwe na hali ya ukali ambao huwezesha ubongo kutoa homoni ya endorphins ambayo katika hali ya juu huleta mguso wa hisia za raha.

Pia pilipili husisimua mfumo wa ufahamu (nerves) wa ubongo na katika kufanya hivyo huwezesha kuamsha haraka hisia za mapenzi na pia usaidia mwili kuwa na hisia za haraka zaidi kwa kuguswa na kadhalika.

ASALI

Asali ina madini yanayoitwa boron, ambayo husaidia mwili kutumia homoni ya estrogen ambayo ni homoni inayohusika na viungo ya uzazi na mapenzi kwa mwanamke.

Pia utafiti unaonesha kwamba asali huongeza nguvu, kitendo ambacho kitapelekea mwanamke kuwa na uwezo wa hamu ya tendo la ndoa.

MATUNDA NA MBOGA ZA MAJANI.

Mlo wenye matunda na mboga za majani una matokeo makubwa sana katika hamu ya tendo la ndoa kwa njia nyingi.

Kwanza matunda na mboga za majani hupunguza kiwango cha mafuta na unene (cholesterol), kuongezeka kwa mafuta mwilini huzuia mzunguko wa damu kwa kubana mishipa ya damu.

Pia kula matunda na mboga za majani huhakikisha balance ya uzito kwani unene (obesity) kwa wanaume kuna matokeo mabaya katika kuzalisha homoni za testoeterone na hatimaye jogoo kushindwa kuwika na kuwa na tatizo la kukosa hamu ya tendo.

Na pia wanandoa wanapozidi kunenepeana ndipo na hali ya kufurahia, kutaka au kuwa na hamu ya tendo la ndoa huzidi kupungua.

NAFAKA

Nafaka zina nyuzinyuzi (fibre) na sukari ngumu (complex sugar) ambazo kusaidia kutunza uzito wa mwili.

Nafaka husaidia katika kuzalisha homoni za testosterone kwenye damu.

Na pia nafaka huwezesha mtu kuwa na nguvu hatimaye kwenda masafa marefu wakati wa tendo.

Kula nafaka kama vile brown bread badala ya white bread, pia kula nafaka halisi badala ya cornflakes ni jambo zuri linalokuhakikishia afya njema na mahusiano mazuri ya ndoa yako.

CHOCOLATE

Chocolate ina phenylethylamine, kemikali ambayo husababisha hisia (feelings) za furaha wakati mwanamke au mwanaume anapofika kileleni (orgasm)

OYSTERS

Huwa na kiasi kikubwa sana cha madini ya zinc na haya madini ndiyo huhusika zaidi na uzalishaji wa homoni ya testosterone kwa wanaume.

Pia imethibitika kwamba wanaume wenye ukosefu wa madini ya zinc huwa na matatizo ya nguvu za kiume na wakati huohuo kuwa na madini mengi ya zinc mwilini huongeza kiwango cha shahawa.

SOYA

Pamoja na kuwa na kiwango kidogo sana cha fat na pia kuwa na kiwango kizuri cha protein, soya zina phytoestrogens ambayo husaidia sana wanawake ambao wamefikia menopause kutengeneza homoni estrogen ya ziada.

Husaidia uke kuwa laini (wet, lubricated) hali inyomfanya mwanamke kufurahia tendo bila maumivu  wakati wa tendo la ndoa.

KAMA Unafanya Mambo Haya Lazima Utaishi Maisha Mafupi..!!!

$
0
0

Kwa kawaida maisha ya kibinadamu mwisho wake huwa ni kufa, hivyo kila mwenye pumzi hii leo mwisho wa maisha yake huishia kaburini.

Hata hivyo, kumekuwepo na viashiria fulani fulani ambavyo huweza kuashiria baadhi ya makundi fulani ya watu huenda wanaweza kuwa na muda mfupi wa kuishi duniani kutokana na sababu tofauti tofauti.

Miongoni mwa dalili ambazo huweza kuashiria mhusika anaweza kuwa na maisha mafupi duniani ni pamoja na hizi zifuatazo.

1. Watu wenye kupenda maisha ya anasa na starehe
Watu wa aina hii huwa katika hatari ya kupoteza maisha haraka hata kabla ya siku zao kutokana na kuwa na hatari kubwa ya kupatwa na magonjwa mbalimbali yakiwemo ya zinaa.

2. Wavutaji wa sigara.
Watu wanaovuta sigara huwa katika hatari ya kuishi maisha mafupi zaidi kuliko wale ambao hawatumii sigara kwani watu wa aina hii huwa katika hatari ya kukumbwa na saratani ambayo huweza kukatisha uhai wa mhusika hata kabla ya siku zake.

3. Kushinda umekaa siku nzima
Wale ambao huwa miili yao haina mazoezi kabisa nao huwa katika hatari ya kupoteza maisha mapema kutokana na kushambuliwa na magonjwa yasiyoambukiza kama vile shinikizo la damu, kisukari nk.

4. Unywaji wa pombe
Watumiaji wa vileo na huwa katika hatari ya kupoteza maisha yao mapema kutokana na mambo mawili makuu

a) Kupata ajali kutokana na kutumia vyombo vya moto wakati wakiwa wamelewa na baadaye kujikuta wanapoteza maisha.

b) Ugomvi ambao huweza kuibuka kutokana na mihemko ya vilevi wanavyokuwa wamekunywa na kuweza kusababisha ugomvi mkubwa. Mfano kupigana na chupa na baadaye kupoteza uhai.

5. Ulaji wa vyakula vya viwandani
Kuna wale ambao mara nyingi wamekuwa wakila vyakula vya makopo ambavyo vinapotumiwa mara kwa kwa mara huweza kuwa na madhara kadhaa likiwemo tatizo la saratani. Hivyo kundi hili nalo linaweza kuwa katika hatari ya kupoteza maisha kabla ya siku zao

MaATATIZO 2 ya Kiafya Ambayo Dalili Zake Huanza kwa Kuhisi Uchovu..!!!

$
0
0

Kila mtu huhitaji kuwa mwenye nguvu na mchangamfu kila siku ili kuweza kuendelea kufanya shughuli za uzalishaji mali za kila siku.

Lakini tatizo linakuja pale ambapo kila siku utajikuta ukiamka ukiwa mchovu na usiyetamani kufanya chochote kabisa zaidi ya kukaa tu.

Hata hivyo ni vyema ikafahamika kuwa unapokumbwa na hali hiyo basi huwa kuna sababu na zifuatazo ni baadhi tu ya sababu ambazo huweza kumfanya mtu kuhisi uchovu.

Upungufu wa damu (anemia)
Upungufu wa damu ni mojawapo ya chanzo cha mtu kuweza kuhisi hali ya uchovu wa mara kwa mara hususani kwa wanawake, 

Ikiwa unapata muda mzuri wa kutosha na unapata virutubisho vyote muhimu na bado unapatwa na hali ya kuhisi uchovu basi ni vyema uende ukafanye uchunguzi kuona kama hauna tatizo la anemia.

Tatizo la upungufu wa damu mwilini ni rahisi sana kukabiliana nalo ambapo mgonjwa atatakiwa kupata virutubisho na vyakula vyenye madini chuma ndani yake.

Kisukari (Diabetes)
Kuhisi uchovu wa kila siku na mara kwa mara huweza kuwa ni kiashiria cha ugonjwa wa kisukari. Hivyo ikiwa unahisi hali hiyo kila siku na unapata haja ndogo mara kwa mara na uoni wako unakuwa hafifu basi unaweza kuonana na wataalam ili kufanya vipimo zaidi.

Magonjwa ya moyoKama unapata uchovu wa mara kwa mara huenda ikawa ni dalili ya matatizo ya moyo, hivyo pia ni nzuri ukaonana na wataalam kwa ajili ya uchunguzi zaidi.

ORODHA ya Vyakula Vinavyosaidia Kulinda Afya ya Figo..!!!

$
0
0

Afya ya figo ni muhimu kama ilivyo afya ya moyo, hii ni kwa sababu figo ni moja ya kiungo ambacho husaidia kuchuja sumu mbalimbali ndani ya mwili na baadaye kutoa taka mwili kwa njia ya haja ndogo (mkojo)

Matatizo ya figo huweza kuchangia ugumu wa upatikanaji wa haja ndogo (mkojo) au miguu na mikono kuvimba.

Pia mtu mwenye shida ya figo huwa katika hatari kubwa ya kukumbwa na matatizo ya moyo.

Ulaji unaofaa mara zote husaidia sana kulinda afya ya viungo vyote muhimu ndani ya mwili ikiwa ni pamoja na figo na kuifanya iweze kufanya kazi zake vizuri ndani ya mwili.

Hata hivyo, kuna baadhi ya vyakula ambavyo tunaweza kusema ni vyakula rafiki kwa afya ya figo ndani ya mwili ni vyema ukafahamu hapa leo. Karibu>>>

Kabeji, hii ni mboga ambayo wengi wetu tunaifahamu sana na tumekuwa tukiitumia katika maisha yetu ya kila siku, lakini ni vyema msomaji wangu ukatambua kwamba mboga hii nayo inauwezo mzuri wa kulinda afya ya figo yako.

Samaki pia ni muhimu sana kwa afya ya figo, hii ni kwa sababu kitoweo hiki kina kirutubisho kiitwacho omega 3 ambayo huwa na nafasi nzuri ya kulinda afya ya figo, lakini pia samaki ni chanzo kizuri cha protini ndani ya mwili.

Pamoja na hayo, mafuta ya mzaituni nayo ni mazuri sana kwa kuboresha afya ya figo na kuikinga dhidi ya magonjwa mbalimbali.

Mafuta haya ya mzaituni ndani yake yana virutubisho mbalimbali kama 'oleic acid', anti-inflammatory fatty acids ambavyo vyote kwa pamoja hutetea afya ya figo ndani ya mwili, halikadhalika mafuta haya ni mazuri pia kwa afya ya moyo.

FIKIRI na Ujiulize Unaanzaje Kumponda Anayekupigania?

$
0
0

NIMEKEREKA hadi nimepoteza siku yangu, yaani kanikera hasa mtoto wa Kidigo, kama ningekuwa na uwezo ningemzabua vibao nijue moja, lakini nikifikiria jela, naona bora tu ninyamaze, ila nyie wenzie niwapashe mpashike!

Yaani mtoto wa kike kweli unathubutu kumwambia mumeo maneno ya kumkatisha tamaa, yanayomuonyesha yeye kuwa siyo mchakarikaji na kwamba anachokifanya kazi bure? Kweli? Hivi, jamani, unaanzaje sasa kusema maneno hayo?

Khaaa! Ona sasa, mihasira imenifanya hadi nimeshindwa kuwasabahi, mtanisamehe ndugu zangu, maana huyu mtu kaniudhi haswaaa.

Kaja barazani, nimempokea kama kawaida, najua hawa ndo wateja wangu, wapashkuna wenzangu, lakini mwisho wa siku tunapataga kitu cha maana cha kufanya au cha kuwaambia wenzetu huko mliko, sasa nimekaa mkao wa kula si ndiyo kaja na kimbwanga?

Kaanza, eti oooh nimefukuzwa kwa mume, kisa, nimemsimanga! Hee, umemsimangaje? Eti nimemwambia mume wangu hana akiba hata shilingi benki, hela yetu inaishia tumboni tu, hatuna cha kujidai!

Mh, nikamuuliza unaujua mshahara wa mumeo, kasema ndiyo, nikamuuliza unajua matumizi yenu yalivyo? Kasema najua, nikauliza tena, kwa hiyo unaona matumizi yetu hayamalizi mshahara wake, eti ooh, yanazidi!

Nikajua hapa naongea na juha, nikamu-uliza tena, hivi pale kwako na mumeo, wewe una ndugu wangapi

 na mumeo ana ndugu wangapi wanawategemea, kasema eti yeye anao watatu, mumewe hana ndugu!

Jamani, sasa mtu kama huyo wewe humchapi kibao kweli? Yaani mshahara wa mumewe anaujua, anafahamu kwamba kama siyo hela ya ziada anayotafuta, pasingetosha hapo nyumbani. Haya, achana na hiyo, humo ndani ya nyumba, ndiyo kwanza mke kajaza ndugu, halafu unamwambia mumeo eti huna hata akiba, fyuuutu!

Alinikera, nikamwambia nenda kwanza, hali yangu imebadilika ghafla, uje baadaye tuzungumze. Pale mwanzo nilikuwa sitaki kabisaa kuzun-gumza naye, maana nilimuona kama mchawi, lakini baada ya kufikiria sana, nikaona hapana, huyu anahitaji kufunzwa, ajielewe ili asije akaendelea na ujinga wake akajikuta anapoteza mume kizembe.

Lakini pia nikaona hili jambo lazima na nyie mlipate, maana inavyoonekana au huenda tabia hii mnayo pia.

Sikia, katika maisha ya ndoa, kitu cha msingi sana kwa mwanamke ni kuhakikisha mumewe ana amani naye kwa asilimia zote mia moja. Asiwe mtu mwenye kujisikia aibu, kinyaa, hasira au kinyongo kwa mke wake. Lazima tuwe na kauli ambayo siku zote inamuongezea hamasa na nguvu katika kutafuta uhai wa familia yenu.

Unapompa maneno ya kukatisha tamaa au kuudhi, unampa muda wa kukufikiria kwa mabaya. Atajiuliza amewasaidia ndugu zako wangapi, halafu wewe umewasaidia nini ndugu zake, ataangalia jinsi unavyoishi na nduguze hao, akiona kuna tofauti, basi lazima kichwa kitamuuma na kufikiria vitu vingine vibaya.

Hata kama hupendezwi na baadhi ya vitu kwa mumeo, kuna namna yake ya kumweleza ili uso wake uendelee kupambwa na furaha, amani na matumaini. Kauli za kuvunjana nguvu zinachangia sana migogoro katika ndoa.
Viewing all 104807 articles
Browse latest View live


Latest Images