Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live

Nafasi za Kazi Zilizotangazwa Leo

$
0
0

HOTUBA ya Kiingereza ya Rais Magufuli na Wafanyabiashara wa Afrika Kusini..!!!

$
0
0

Rais Magufuli alikutana na wafanyabiashara wa Afrika Kusini walioambatana na Rais Zuma kuhusu fursa za kuwekeza Tanzania na ushirikianao baina yao na wafanyabiashara wa Tanzania
Hotuba hiyo aliitoa kwa kiingereza ili aeleweke na wote kiurahisi


RAMBIRAMBI za Waliokufa wa Shule ya Lucky Vincent, Arusha Zadaiwa Kuchezewa Rafu na Kutafunwa....!!

$
0
0

Familia za Wanafunzi, Waalimu/Dereva zilizopoteza wapendwa wao kwenye ajali ya gari la shule ya Lucky Vincent huko Arusha zimepatiwa kila moja kiasi cha shilingi Milioni 3.6, (Pesa Zingine zilizotolewa zimetumika kugharamia gharama Zingine. Millions 60, 400,000) zipi?

Kwa mujibu wa mkuu wa mkoa wa Arusha,jumla ya shilingi milioni 190 zimetumika kwenye gharama zote.

Kimahesabu jumla ya shilingi Milioni 129,600,000 ndizo walizopewa wafiwa kama Rambirambi baada ya matumizi mengine.Kiasi cha shilingi milioni 60,400,000 ndizo zilizotumika kwa matumizi mengineyo.

Swali langu moja tuu,
"Serikali ilitangaza itagharamia Mambo yoote ya Msiba mpaka kuzika, sasa hii ya kusema tena kiasi flani cha fedha ya Rambi rambi kilichotolewa kimetumika kwa mambo mengine ni yapi hayo? Ili kuondoa utata vichwani mwa wengi, ingependeza endapo yangetajwa.

BAADA ya Bunge Live, Wasanii, Magazeti, Sasa Mwakyembe Asema Mitandao ya Kijamii ni Hatari Lazima...!!!

$
0
0

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe amesema watumiaji wa mitandao ya kijamii Tanzania ni wengi sana hivyo mitandao hiyo kama haitadhibitiwa mapema huenda ikaleta matatizo katika nchi.

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe.

"Watanzania ambao wapo kwenye mitandao ni mamilioni kwa sasa, lakini tunachosema tatizo hapa ni matumizi mabaya ya hiyo mitandao, mwanasiasa maarufu wa Marekani nafikiri Clinton alisema mwaka jana kuwa matumizi mabaya ya mitandao ni ugonjwa hatari unaoweza kuteketeza dunia, kwa kweli mitandao ya jamii kama hatujaiangalia vizuri au kuithibiti inaweza kutuingiza katika matatizo makubwa sana" alisisitiza Mhe. Dkt Harrison Mwakyembe 

POLISI Asombwa na Mafuriko, Afariki..!!!

$
0
0

MVUA kubwa inayoendelea kunyesha mfululizo katika maeneo mbalimbali nchini imeendelea kuleta madhara ikiwamo kufariki dunia askari wa Jeshi la Polisi aliyekumbwa na mkasa wa kusombwa na maji yaendayo kasi wakati akiwa na pikipiki visiwani Zanzibar.

Aidha, mvua hizo zilizosababisha mafuriko katika maeneo mbalimbali, yakiwamo ya Tanga na Zanzibar na kusababisha maafa makubwa kwenye baadhi ya maeneo nchini, zimewashtua wabunge ambao jana walitaka kusitishwa kwa shughuli za Bunge ili kupata taarifa kamili na kujadili hatua za kuchukua.

KIFO CHA POLISI
Licha ya kuendelea kuharibu miundombinu kama ya barabara na kubomoa nyumba, mafuriko yatokanayo na mvua yaliendelea kuleta vilio baada ya jana kusababisha kifo cha askari wa Jeshi la Polisi, Sajenti Abbas Anas Haji (55). Marehemu alikumbwa na umauti baada ya kusombwa na maji katika barabara ya Fuoni Kibonde Mzungu, Mkoa wa mjini Unguja, Zanzibar.

Akizungumza eneo la tukio, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mjini Magharibi, Hassan Nassir Ali, alisema tukio hilo lilitokea majira ya saa 5:30 asubuhi wakati askari huyo akiwa na usafiri wa pikipiki (Vespa), akitokea kazini Makao Makuu ya Jeshi la Polisi, kuelekea nyumbani kwake.

Alisema alipofika katika eneo hilo, aliteleza na kuanguka kabla ya kusombwa na maji hayo.

Mwandishi wa Nipashe alifika katika eneo la tukio na kukuta umati wa watu waliokuwa wakiendelea na shughuli za uokozi wa mwili wa marehemu ambao ulikuwa hauonekani kutokana na maji mengi yaliyokuwapo.

Hata hivyo, vikosi vya uokoaji vilifanikiwa kuupata mwili wa askari huyo majira ya saa 9:30 jioni.

Kamanda Ali alisema marehemu ni wa kitengo cha picha Makao Makuu ya Jeshi hilo, Zanzibar.

Alisema eneo hilo ni hatari kutokana na barabara kufunikwa na maji ambapo pembezoni mwa barabara hiyo kuna bonde kubwa la mpunga na maji huwa mengi, yakipita barabarani kwa kasi na mengine kutuwama pembezoni.

“Hivi sasa haturuhusu waenda kwa miguu wala vyombo vya moto kupita eneo hilo kwa sababu maji yana kasi kubwa na yanaweza kusababisha maafa mengine,”alisema.

Alisema mwili wa marehemu umeshakabidhiwa kwa ndugu zake kwa ajili ya mazishi ambayo yanatarajiwa kufanyika kwao, Fuoni Kibondeni.

Alisema Jeshi la Polisi limepokea kwa masikitiko makubwa kifo cha askari huyo na kuwataka wananchi kuchukua tahadhari, hasa katika kipindi hiki cha mvua kubwa zinazoendelea kunyesha.

Mkuu wa Wilaya ya Magharibi ‘B’,Unguja, Silima Ali Haji, alisema hali ya mafuriko ya mvua si nzuri na maeneo mengi yameathirika na mvua hizo, ikiwamo nyumba kujaa maji na pia barabara kutopitika kwa kufunikwa na maji.

Aliyataja baadhi ya maeneo hayo kuwa ni barabara ya Mwanakwerekwe Sokoni ambayo hivi sasa haipitiki, barabara ya Fuoni Kibonde Mzungu na eneo la Tomondo Ziwa Maboga ambako nyumba nyingi hivi sasa zimejaa maji na wananchi waliokuwapo kukosa mahala pa kuishi.

“Bado hatujafanya tathmini katika wilaya yangu familia ngapi zimekosa makazi. Lakini athari za mvua ni kubwa na niwasihi wananchi wachukue tahadhari kwani bado mvua zinaendelea kunyesha”alisema.

Akizungumzia kuhusu tukio la Mafuriko Bwejuu Mkoa wa Kusini Unguja ambalo limeenea katika mitandao ya kijamii ya kwamba watu wanatembea mitaani kwa mitumbwi, mkuu huyo wa wilaya alisema kuwa mafuriko yapo katika baadhi ya maeneo lakini siyo makubwa ya aina hiyo na kwamba, video inayosambazwa haiakisi uhalisia wa eneo husika.

Akizungumzia kuhusu maafa ya mvua zinazoendelea kunyesha, Rais wa Zanzibar, Dk. Ali Mohamed Shein, alisema serikali yake imekuwa ikifanya juhudi mbalimbali za kuimarisha miundombinu ili kuhimili maafa hayo kwa kuzuia maji yasituwame pasipostahili.

“Nimeshuhudia eneo la Tomondo Ziwa Maboga pamejaa maji. Nyumba nyingi zimefukiwa na maji lakini kila wananchi wakitakiwa waondoke hawataki,” alisema Dk. Shein, akisisitiza wananchi kuzingatia tahadhari zinazotolewa kipindi hiki.

Aidha, imeelezwa kuwa mvua kubwa zinazoendelea kunyesha katika maeneo mbalimbali ya visiwa vya Unguja na Pemba zimeathiri nyumba 325 katika Mkoa Kusini Pemba, nyumba 667 kukimbiwa na wakazi wake ndani ya Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja pamoja na kubomoka kwa miundombinu ya barabara na baadhi ya madaraja.

WABUNGE WASHITUSHWA
Katika mjadala wa jana bungeni, wabunge waliitaka serikali kueleza athari za mvua kubwa zinazoendelea kunyesha katika maeneo mengi nchini na hatua inazozichukua kuwapa unafuu wa maisha wananchi waliokumbwa na mafuriko hayo.

Mjadala huo ulisababisha Mwenyekiti wa Bunge, Andrew Chenge, aliyekuwa anaongoza kikao cha Bunge, kuitaka serikali itoe tamko kuelezea jambo hilo na hatua zilizochukuliwa.

Chenge alilazimika kuamua hivyo baada ya wabunge watatu kusimama kuomba mwongozo wa Kiti cha Spika, huku baadhi yao wakitaka shughuli za Bunge zisitishwe ili kujadili hoja hiyo waliyotaka ichukuliwe kuwa ni ya dharura.

Wabunge walioomba mwongozo wa Kiti cha Spika ni Stephen Ngonyani 'Prof. Majimarefu' (Korogwe Vijijini-CCM), James Mbatia (Vunjo-NCCR Mageuzi) na Rashid Shangazi (Mlalo-CCM).

Akiwasilisha hoja yake, Prof. Majimarefu alitumia Kanuni ya 68(7) akisema kuna athari kubwa nchini zilizosababishwa na mafuriko nchini.

“Kwenye mkoa wangu wa Tanga kumekuwa na maafa. Leo (jana) hii tunavyoongea kuna watu 1,000 hawana chakula, mahali pa kuishi na hawana msaada wowote," alisema.

"Serikali itawasaidiaje hawa watu wakati kamati za afya zikiendelea na utaratibu?" Alihoji.

Katika kujenga hoja yake, Shangazi aliyesimama kwa kuzingatia Kanuni ya 47(1), alitaka shughuli za Bunge ziahirishwe ili wabunge wajadili kuhusu mafuriko hayo.

“Sasa hivi katika Mkoa wa Tanga kuna mafuriko makubwa sana. Na jana (juzi) yametokea maporomoko katika Milima ya Usambara, eneo la barabara za Lushoto-Arusha-Mombo, Pangani-Tanga, Mombo kwenda Lushoto na Kilindi-Morogoro zote zilifungwa,” alisema Shangazi.

Alisema Mkoa wa Tanga umegeuka kuwa kisiwa ghafla na umepata athari kubwa na kuiomba serikali ilione jambo hilo ni la kimkakati na Wakala wa Barabara (Tanroads) umezidiwa.

Mbatia alisema hali ni tete katika mikoa mingi nchini ikiwamo Kilimanjaro, Dar es Salaam, Pwani, Tanga na Zanzibar kufuatia mafuriko yaliyojitokeza na kuomba utu kuzingatiwa miongoni mwa wabunge kwa kuamua kutenga walau robo saa kujadili suala hilo na kupendekeza hatua za kuchukua.

“Tutenge muda wa dakika 15 ama 20 ili tujadili suala hili ambalo ni la maafa. Tunaweza tukatoa majibu sahihi kwa wapigakura wetu," alisema.

Akijibu maombi ya wabunge hao, Chenge, akirejea kanuni, alisema kwa hali anayoiona, haoni kama suala hilo linahitaji kujadiliwa bungeni kwa kipindi hicho.

“Ni kweli tukio hili limegusa maeneo mengi, nawapa pole walioguswa kwa namna moja hata nyingine. Naamini Serikali iliyoko humu ndani, itaitolea maelezo wakiangalia nchi nzima,”alisema Chenge.

Alisema anaamini serikali italizungumzia vizuri suala hilo kuliko kila mbunge kujisemea katika eneo lake.

Akijibu ombi la Prof. Majimarefu, Chenge alisema Kanuni ya 68(7) kuhusu kuomba mwongozo wa Kiti cha Spika, ina sharti la lazima mwongozo huo uombwe kwa tukio ambalo limetokea mapema bungeni na si nje ya chombo hicho cha kutunga sheria.

HALI YA TANGA
Kutoka Tanga, inaelezwa kuwa mvua zinazoendelea kunyesha mkoani humo zinaendelea kuleta athari na hivyo kukata mawasiliano kati ya mikoa ya Kiliamanjaro na Arusha.

Zaidi ya magari yameharibika vibaya baada ya kupondwa na mawe makubwa yaliyoporomoka kutoka juu ya milima kwenda barabarani .

Mawe hayo yalifunika baadhi ya magari na kufunga kabisa barabara zinazoelekea wilayani Lushoto lakini kwa mujibu wa serikali mpaka jana hali imerudi shwari na magari yameanza kupita.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga, Benedict Wakulyamba, alisema jana kuwa magari hayo yameharibika baada ya kuangukiwa na udongo ambao umetoka juu ya milima katika barabara kuu ya kutokaka wilayani Korogwe kuelekea Soni Wilaya ya Lushoto.

Alisema katika ajali hiyo watu nane walijeruhiwa vibaya na walipelekwa katika Hospitali ya Wilaya ya Lushoto kwa matibabu na wameruhusiwa kurudi nyumbani baada ya kutibiwa.

Kamanda Wakulyamba alisema kuwa magari yaliyoharibika kwa kuangukiwa na udongo wa mawe kutoka milimani kuwa ni Toyota Coaster mbili, Toyota
Carina, Noah na Toyota Hilux na kwamba barabara ya kutoka Mombo kwenda Lushoto iliyokuwa imefungwa, sasa imefunguliwa na magari yameanza kupita kwa tahadhari kubwa.

Hata hivyo, mawasiliano kati ya Pangani na Tanga mjini yamekatika baada ya daraja kubomoka eneo la Neema jijini Tanga.

PICHAAZZ..Pamoja na Mafuriko Kukita Kila Kona..Hivi Ndivyo Watu Walivyoamua Kupambana Nayo..!!!

Yanga Wamtamani Kocha Maxime wa Kagera Sugar, Hivi Ndivyo Watakavyofanya

$
0
0

KWELI ukijituma neema zinakuja, Kocha wa Kagera Sugar, Mecky Maxime amepigiwa simu na Yanga wakimtaka akae katika benchi lao la ufundi msimu ujao. 

Bosi mmoja wa Yanga ameliambia Championi Jumamosi kuwa, wapo katika mchakato wa kumchukua Maxime ili aweze kuchukua mikoba ya Kocha Msaidizi Juma Mwambusi katika msimu ujao wa Ligi Kuu Bara. 

Yanga imevutika na utendaji wa Maxime tangu alipokuwa Mtibwa Sugar ikiwemo jinsi alivyoweza kuibua vipaji vya wachezaji kadhaa wanaofanya vizuri Simba na Yanga sasa. 

Miongoni mwa wachezaji hao ni Juma Abdul, Andrew Vincent na Hassan Kessy wa Yanga na Mzamiru Yassin, Mohammed Ibrahimu ‘Mo’, Jamal Mnyate na Shiza Kichuya wote wa Simba. 

“Tayari tumeshaanza mazungumzo na Maxime, msimu ujao tunataka kufanya mapinduzi makubwa ndani ya timu yetu, siyo kwa wachezaji tu hata katika mechi la ufundi. 

“Tuna mpango wa kutaka kumchukua Maxime ili awe kocha wetu msaidizi kwani tunaamini atakuwa na mchango mkubwa katika kikosi chetu kutokana na kazi nzuri anayoifanya, tumeshazungumza naye juu ya hilo kwa hiyo muda ukifika tutamalizana naye,” alisema bosi huyo. 

Alipotafutwa Maxime kuhusu dili hilo, alisema: “Bado hatujazungumza lakini endapo watakuja, nitawasikiliza na baada ya hapo ndipo nitakapojua nini cha kufanya lakini kwa sasa siwezi kusema lolote.” 

Katibu Mkuu wa Yanga, Charles Mkwasa kuhusu hilo, alisema: “Hakuna kitu kama hicho pia hivi sasa si muda muafaka wa kuanza kuzungumzia mambo hayo, akili yetu ipo katika mbio za ubingwa.”

Wenye Vyeti FEKI Kulipwa Mafao Yao

$
0
0

Watumishi waliobainika na vyeti feki, watalazimika kusubiri mafao yao hadi utaratibu wa kuwalipa utakapofanyika. 

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejmenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Angela Kairuki alitoa kauli hiyo jana bungeni wakati akijibu swali la nyongeza lililoulizwa na Mbunge wa Viti Maalum (CCM) Amina Mollel. 

Amina alitaka kujua ni hatua gani zitachukuliwa ili kuwalipa mafao yao wafanyakazi waliobainika na vyeti feki.

Waziri Kairuki alisema, ofisi yake itaandaa utaratibu wa mafao ya wafanyakazi hao na pindi utakapokamilika, watajulishwa na kulipwa haki zao. 

Aidha,  Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera , Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Watu wenye ulemavu, Anthony Mavunde, alisema kwamba seeikali inaendelea na mchakato wa kuunganisha mifuko ya jamii. 

Mavunde alisema hayo alipojibu swali la msingi la Mbunge wa Tabora Kaskazini (CCM), Almas Maige, aliyetaka kujua mchakato wa kuunganisha mifuko ya hifadhi ya jamii, umefikia hatua gani. 

Mavunde alisema, serikali kwa sasa inafanya tathmini ya mifuko ya hifadhi ya jamii ambayo imetoa mapendekezo kuhusu namna bora na mambo ya kuzingatiwa katika mchakato wa kuunganisha mifuko hiyo. 

Alisema, wadau vikiwemo vyama vya waajiri, vimeshirikishwa ili kutoa maoni na mapendekezo kwa serikali na kutoa maamuzi

SERIKALI Kuwafuta Machozi Watumishi Wenye Vyeti Feki..!!!

$
0
0

Baada ya kilio kikuu kuhusu hatima ya maisha ya watumishi waliobainika kuwa na vyeti feki hivyo kuondolewa kazini, hatimae serikali imekisikia na inaandaa mpango wa kuwalipa watumishi hao kwa kuwa wamehudumu katika nafasi mbalimbali serikalini kwa muda mrefu, Waziri ofisi ya Rais menejimenti ya utumishi wa umma na utawala bora Angellah Kairuki ameeleza hayo kwa kuthamini michango ya watumishi hao.

Aidha Katibu Mkuu Utumishi Dr Laurean Ndumbaro anategemea kutangaza majina wengine ya watumishi wa serikali kuu wenye vyeti feki ifikapo tarehe 15.5.2017 siku ya jumatatu.

NASISITIZA: Tusijifananishe na Rwanda, Siyo Saizi Yetu Kabisaaa...!!

$
0
0

Unakuta mtu analeta mada za ajabu juu ya ulinganifu wa Tanzania na Rwanda kimaeendeleo!
Huku ni kufikiri sawa kweli?

Ni sawa na kulinganisha usafi wa nyumbani kwangu na usafi wa kijiji chetu, baada ya hapo nikaanza kujisifia eti mimi niko vizuri hapa kwangu kwani nimemshinda Mwenyekiti wa kijiji kwa usafi.
Ndugu zangu kwa wale msioijua Rwanda vizuri; ni nchi ndogo mno! 
Sawa na mkoa mmoja au baadhi ya wilaya moja kubwa!

Huku kutakuwa ni kukosea shabaha sana kujaribu kufanya maendeleo kwa mtazamo wa kile Rwanda wanachofanya!

Kimsingi kwa wao watakuwa sahihi kulingana na mazingira yao, ila sisi tutakuwa tumekosea sana!

Hata kama sisi tungekuwa tumeendelea kuliko wao; endapo wao wangetaka kututazama sisi wangekuwa wanakosea sana!
Tanzania ina rasirimali nyingi kuliko Rwanda hivyo hawawezi kujifananisha na sisi kivyovyote vile.
Tunafanana rangi tu! lakini mazingira yetu ya kiuchumi na wao ni tofauti sana!
Nchi ambazo zinapaswa kujifunza toka kwa Rwanda hapa afrika mashariki ni Burundi, Uganda na pengine na Sudani ya kusini.

Sisi tunazo baadhi ya nchi za kuzitama hapa afrika ila sio za aina ya Rwanda.
Kama Kenya tu kujilinganisha nayo ni uzembe, na aibu kubwa kwetu! itakuwa Rwanda?

KWA Maoni Haya ya Raia wa Afrika Kusini, Bora Zuma Asingekuja Tanzania..!!!

$
0
0

Kama wanafika hatua ya kutudharau hivi basi hata ziara ya huyu Rais wao haikuwa na maaana tena kwetu


WATOTO Majeruhi wa Lucky Vicent Wapata Visa ya Kwenda Marekani..!!!

$
0
0

Mbunge wa Singida Kaskazini,Lazaro Nyalandu amesema Ubalozi wa Marekani umetoa hati ya kusafiria (visa)  kwa ajili ya kuwawezesha wanafunzi watatu wa Shule ya Lucky Vincent kupata matibabu nchini Marekani.

Katika ukurasa wake wa Facebook leo Nyalandu  amesema waliopata Visa ni wazazi,watoto na wataalamu wawili wa afya ambao watasafiri kwenda Marekani.

"Wote wamepewa visa asubuhi ya leo Ubalozi wa Marekani Dar es Salaam. Akina Mama watatu, watoto wote watatu, na Daktari Moja na Nurse Moja. Kansela wa Ubalozi wa Marekani alinipigia simu asubuhi akiwasubiri katika siku ambayo haikuwa ya kazi,” amesema  Nyalandu  na kuongeza:

“Mungu ambariki sana kwa moyo huu. Napenda pia kutoa taarifa kuwa ndege yao aina ya DC 8 inatarajiwa kutua Leo usiku saa 2:15 majira ya Afrika Mashariki katika uwanja wa KIA. Mungu wa Watanzania awabariki wote kwa sala na dua zenu kwa ajili ya hawa watoto. Sifa na utukufu kwa Mungu wetu.”

Katika taarifa ya awali kwa vyombo vya habari Nyalandu amesema safari ya kuelekea Marekani itakua kesho  asubuhi na ndege itatua Charlotte,New York na kisha wagonjwa pamoja na waliowasindikiza wataingia katika ndege nyingine maalumu ya kubeba wagonjwa hadi katika mji wa Sioux City,Iowa

Watoto hao watatu walijeruhiwa wakati wakiwa katika safari ya masomo wilayani Karatu mkoa wa Arusha jumamosi iliyopita na kusababisha vifo vya wanafunzi 32,walimu wawili na dereva wao.

BREAKING News..Ajali ya Tren Yatokea Morogoro..Mabehewa Matatu Yalaliana..!!!

$
0
0

Treni ya abiria imepata ajali usiku saa 5 eneo la Stesheni ya Mazimbu Morogoro ambapo mabehewa manne yameegama na matatu yameacha reli.


Ashura Mrisho aliyekuwa anakwenda Tabora amejeruhiwa kwa kuangukiwa na mizigo. Mabehewa 13 yamerejeshwa Morogoro kuwapangia usafiri mbadala 

Sakata la Diamond Kudaiwa Mil 400 na TRA lafika Hapa

$
0
0

Siku chache tangu Mbunge wa Jimbo la Mikumi Professa Jay kupaza sauti yake kuhusu makadirio makubwa ya kodi anayotakiwa kulipa Mwanamke anayewika nje na ndani ya nchi  katika muziki wa bongo Flavor Diamond  Platnum Mamlaka ya Mapato nchini (TRA) imekanusha kumlipisha kwa makadirio nyota huyo. 
  

Mkurugenzi  wa Huduma na Elimu kwa Mlipa Kodi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA),  Richard Kayombo, ameendelea kukanusha kwamba, Mamlaka hiyo haijamkadiria msanii wa muziki wa kizazi kipya,Nassib Abdul ( Diamond Platnamuz) kulipa kodi ya shilingi Milioni 400. 

Hayo ameyasema leo wakati akifafanua hoja mbalimbali kwa waandishi wa habari wanaoshiriki semina ya siku moja iliyoandaliwa na TRA ili kutoa elimu ya ulipaji kodi kwa waaandishi. 

“Tuko kwenye hatua za awali za mazungumzo bado hatujakadiria kiasi kodi anayopaswa kulipa Diamond, na kwa bahatio nzuri tumekaa naye na bado tuko kwenye mazungumzo na sio kweli kwamba tumemkadiria shilingi Milioni 400,”, 

“Tunajaribu kujua vyanzo vyake vya mapato, lakini hata kama imetokea mtu umekadiriwa kulipa kodi kwa kiasi Fulani na hujaridhika unayo nafasi ya kukata rufaa kwa Kamishna Mkuu wa TRA, na ndapo hujaridhika na rufaa hiyo ipo Mamlaka nhyingine ambayo iko nje ya TRA, Tax Tribunal, na bodi ya Rufaa za kodi.” amesema Kayombo. 

Kongamano lililotaka kuwakutanisha Kinana,Mbowe, Lowassa meza moja lapigwa sarakasi

$
0
0

Kongamoanamo la kidenmokrasia lilikudiwa kuwakutanisha viongozi mbalimbali wa kisiasa jijini Dar es Salaam lashindwa kufanyika. 

Kamati ya Maandalizi ya kongamano lililoandaliwa na Chadema imesema serikali ya mkoa wa Dar es Salaam imewazuia kutumia ukumbi wa Anatouglou waliouomba kwa ajili ya kongamano hilo. 

Taarifa iliyotolewa na Mwenyekiti wa kamati hiyo, Makongoro Mahanga imeeleza kuwa wamepewa taarifa ya ghafla na serikali ya mkoa ya kuwazuia kufanya kongamano hilo leo Mei 13. 

 “Hata hivyo kwa mshangao mkubwa, usiku huu tumepata taarifa kwamba Serikali ya Mkoa wa Dar es Salaam imezuia matumizi ya ukumbi huo kwa ajili ya  kongamano hilo kwa kile tulichoambiwa ni kujitokeza kwa shughuli nyingine za Mkoa kwenye Ukumbi huo hiyo kesho,” imesema  taarifa hiyo na kuongeza: 

 “Kutokana na hali hiyo na muda uliopo, tunalazimika kuahirisha kongamano hilo hadi litakapotangazwa tena. Tunaahidi kutoa taarifa kamili ya jambo hili kwa vyombo vya habari mapema iwezekanavyo.” 

Kadhalika taarifa hiyo imesema kuwa mwaliko wa kongamano hilo ulipelekwa pia kwa viongozi wakuu wa Vyama vyote vikubwa vya siasa nchini vikiwemo CCM, CHADEMA, CUF, NCCR Mageuzi, ACT Wazalendo na CHAUMMA.

VUMBI la Makonda Lamkumba Lowassa..Alia Kutoruhusiwa Kuingia Kwenye Kongomano la Demokrasia..!!!

$
0
0

Waziri mkuu wa zamani, Edward Lowassa amesema amesikitishwa na hatua ya Serikali ya Mkoa wa Dar es Salaam ya kuzuia kongamano la demokrasia lililopangwa kufanyika leo katika ukumbi wa mikutano wa  Anatouglou.

Lowassa ambaye ni mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema alitoa kauli hiyo leo (Jumamosi) wakati akizungumza na wanahabari ofisi kwake Mikocheni.

 Amesema amelaani kitendo hicho na kusema kongamano hilo halikuwa na nia mbaya bali lilikuwa limelenga kujadilia mambo mbalimbali kwa mustakabali wa Taifa.

 "Nimesikitishwa na kitendo hiki na nimeshangaa kwa jambo hili halikemewi.Nchi hii ni moja na kila mtu ana haki.

 "Walituzuia mikutano ya hadhara tumetii, tumeamua kufanya mikutano ya ndani wanatufuata fuata,"amesema Lowassa ambaye aliwahi Mbunge wa Monduli kwa nyakati tofauti.

 Katika mkutano huo Lowassa aliambatana na mwenyekiti wa kamati ya Maandalizi ya kongamano hilo Dk Makongoro Mahanga ambaye alishangazwa na hatua hiyo ya Serikali ya mkoa wa Dar es Salaam

MAKUSANYO ya Bilioni 76 Yavunja Rekodi Wizara ya Ardhi..!!!

$
0
0

Serikali imefanikiwa kukusanya Sh76bilioni cha makusanyo ya kodi ya pango la ardhi hadi kufikia tarehe 13 Mei 2017 kiwango ambacho hakijawahi kufikiwa.

Akiongea katika mkutano wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi leo,  Katibu Mkuu wa Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi,   Dk Yamungu Kayandabila amesema kiwango cha makusanyo ya kodi ya ardhi hakijawahi kufikiwa ukilinganisha na miaka ya nyuma ambapo kwa sasa Wizara imekusanya Sh76 bilioni cha kodi ya pango la ardhi.

 “Juhudi za kukusanya kodi ya pango la ardhi kwa viwanja vilivyopimwa zinaendelea vizuri licha ya changamoto iliyopo hususan mwamko wa wananchi katika kulipa kodi.” amesema Dkt. Kayandabila.

MSUKUMA(Mb) Awaponda Nape na Kitwanga, Ataka Kitwanga Ahakikiwe Vyeti..!!!

$
0
0

Mbunge Joseph Kasheku maarufu kama Musukuma amewaponda mawaziri waliotumbuliwa na Magufuli Nape Nnauye na Charles Kitwanga kwa kuiponda serikali baada ya kutolewa kwenye uwaziri na kumtaka waziri wa elimu ahakiki vyeti vyao.

Amemshangaa Kitwanga kwa kusema sasa ameondoka kwenye uwaziri na ataanza kuisema serikali akiuliza kwenye baraza la mawaziri wanaambiwa nini.

Amemponda kauli ya kitwanga ya ku mobilize wananchi 10,000 kuharibu mtambo wa maji na kuhoji vyeti vyake vipi? 

Kuhusu kauli ya Nape kusema CCM haitarudishwa endapo haitatekeleza bajeti ya maji amesema sio kwdeli kwa kuwa miaka mingi hawatekelezi ilani na wanachaguliwa na wananchi hawawategemei kwa maji tu na bado muda upo

Pia amesema hela ya bajeti ya maji ni nyingi iwapo itatoka yote. amesema bajeti liyopita ilipangwa kutolewa bilioni 915 lakini mpaka leo ni 181 tu ndio imetoka

ATTENTION...Uvamizi Hatari wa Kimtandao Watokeoa Duniani..Unasababishwa na Kirusi Hatari cha Kompyuta ..Kimeshasambaa Katika Nchi 100 Duniani Kote..!!!

$
0
0

Jana usiku nimetoa taadhari kwenye moja ya taasisi za umma juu ya Global Cyberattack - Uvamiszi wa kutisha wa udukuzi wa mifumo ya kompyuta - uliotokea jana nikiwataka wachukue hatua za haraka kujilinda. 

Hata hivyo nimeona niweke maelezo na ushauri wangu kwenye public maana jambo hili ni utishio kubwa kwa usalama wa taifa na hadi ninapoandika ujumbe huu udukuzi huu unaendelea kusumbua mifumo ya computer duniani kote nanimepata taarifa waathirika toka Tanzania. 

Kwa kifupi huu ni udukuzi wa kimtandao ambao umeathiri nchi takribani 100 duniani kwa siku ya jana tu. Nchi zenye wataalamu wa hali ya juu, mifumo ya kisasa, na uwezo mkubwa wa ulinzi na udukuzi wa mitandao kama Uingereza, Urusi, Ujerumani, na Ukrain wameathiriwa sana. Kama hawa wamedhurika ni wazi kwamba sisi tuko kwenye hatari kubwa na tunalazimika kuchukua hatua za haraka kama nchi na kama mtu mmoja mmoja.

Pamoja na kwamba hakuna taarifa nyingi kutoka Tanzania na Afrika kwa ujumla juu ya uvamizi huu, ukweli ni kwamba nchi za kiafrika zimeshavamiwa.asubuhi ya leo nimeshatapa taarifa za watu walikumbwa na kadhia hii nchini. Mfumo huu mpya wa udukuzi unaendeshwa na majangili wenye utalaamu mkubwa wa mitandao na wamejificha nyuma ya pazia la chuma lisilopenyeka kirahisi.

Udukuzi wa kimtandao (Cyberattack)

Udukuzi wa mifumo ya computer uliozoeeleka kama hacking ni kitendo cha wavamizi kuingilia mifumo ya computers hufanya mojawapo ya haya:

Kuiba taarifa toka kwenye mifumo kwa malengo ya kwenda kuzitumia kudanganya, kuiba, kazi za kiusalama, ugaidi, nk.

Huingilia mifumo kuratibu mawasiliano ya watu ambayo wana interest naoi li kufuatilia mienendo yao.

Kuingilia mifumo kwa lengo la kuharibu tu kama aina ya ukorofi, ubaya, ubabe, nk.

Kuingilia mifumo kwa lengo la kufuta ushahidi fulani.

Hata hivyo udukuzi huu ulioivamia dunia jana ni wa ujambazi wa aina yake kwani wahusika pamoja na malengo mengine ambayo wanaweza kuwa nayo, kikubwa wanchotaka ni fedha. Wanapoivamia computer yako wanaitawala wao kwa kufunga programme na mafaili yote (encrypting your computer). 

Unapojaribu kuifungua unapata ujumbe wa kitendo walichokifanya ambacho hukupa maelezo kwamba njia pekee ya kuirudisha computer yako katika hali ya kawaida ni kulipa kiasi cha dola 300 za kimarekani ($300) ndani ya muda maalum waliokupa. Usipolipa ndani ya muda huo, dau linaongezeka au wanafuta mafaili yote kwenye computer yako.

Udukuzi wa huu Unaitwaje?

Mfumo huu wa udukuzi unaitwa Ransomware kwa sababu umelenga kushambulia mifumo kwa madhumuni ya kujipatia fedha. Njia ya kujikomboa kwa mauathirika ni kulipa fedha pekee (you get back access to your computer after paying a sum of money demanded –ransom – hence the name Ransomware). Kirusi anayefanya shambulio hili la sasa anaitwa WannaCry na uharibifu aliofanya kwa siku moja tu ya jana ni mkubwa kuliko yote ambayo imewahi kutokea. 

Pamoja na kukutisha kufuta maifaili yako iwapo utashindwa kulipa fedha wanayotaka, wadukuzi hawa pia wanakutisha kutumia picha na mafaili waliyoyamiliki kwenye computer yako kukuaibisha kwa maana ya kukuanika mitandaoni. Wanachukua taarifa za siri kam amafaili, picha, na video ulizonazo na kuziweka hadharani ili kukudhuru au kukudhalilisha. Hivyo wanakupa chaguo dogo sana la kulipa au vinginvyo.

Nini kimetokea?

Mamlaka ya Usalama wa Taifa ya Marekani (National Security Agency – NSA) ni taasisi yenye nguvu kubwa ya intelligence kuliko zote. Pamoja na kazi zingine, taasisi hii ina kitengo maalumu cha cybersecurity chenye wataalamu wa hali ya juu kabisa. Pamoja na kazi za kujilinda dhidi ya uvamizi wa kimtandao, kitengo huki hutengeneza tools/software za kushambulia au kujipenyeza kwenye mifumo mingine duniani kwa lengo la kutafuta taarifa, kujua watu wanafanya nini kwenye computers zao, na kuwafuatilia wale wanaowashuku kiusalama kama vile magaidi, wezi, wauza madawa, na kuingilia mifumo ya nchi maadui. 

Mwezi wa nne mwaka huu, mifumo ya taasisi ya NSA ilivamiwa na wadukuzi (hackers) wasiojulikana ambao waliwaibia taarifa nyingi sana ikiwa ni pamoja na software yao walioyoitengeneza kwa lengo nililolitaja hapo juu. Software hiyo inaitwa Eternal Blue na ina uwezo wa kupenyeza knye Microsoft Windows computers (Windows XP, Windows 8, Windows 10) na kumruhusu muhusika kutizama unachokifanya na taarifa zako. Kwa kifupi, software hii inafungua mlango wa nyumba na vyumbai na kuiacha wazi kwa aliyefungua kufanya atakacho.

Majambazi hao wa kimtandao ambao hawajajulikana bado, walipoipata software hii inasemekana walioiweka Eternal Blue kwenye website moja iliyofichika tarehe 4 mwezi wan ne. baada ya kufanya hivyo, kundi linguine la kijambazi wa kimtandao wakaipata na wakaanza kuitumia kupenyeza kwenye computers za watu duniani kote walizokua (huend ana yako wameiingilia). Baada ya wao kuiona wana uwezo wa kuingilia computer za watu bila wao kujua, wakatengeneza kirusi aitwaye WannaCry ambaye ndiye anayefanya kazi ya kuiteka nyara computer yako. Hivyo Eternal Blue akishafungua milango ya computer yako, 

WannaCry anaingia na kuiratibu hivyo anafunga maifaili na programme zote usiwe na uwezo wa kufanya lolote. Njia pekee unayoachiwa ni kufuata maelekezo ya majangili hawa kwamba ni lazima ulipe ($300) ili waweke kukurudishia funguo za milango na madirisha ya nyumba yako (computer). Kwenye taasisi nyingine WannaCry amehitaji kulipwa kwa mamilioni ya dola ili arudishe access. 

Huu ni utekaji nyara wa kiwango cha juu sana kwani huna njia nyingine kwa vile uwezo wa kumtoa virusi mtu anakua nao tu pale ambapo computer inafanya kazi na sasa huna. Iwapo hutalipa kiwango wanachotaka kwa muda waliokupa, fedha inongezeka na wanaanza kudelete mafaili yako.

Unalipaje na kwa nini wameshindwa kufunga njia ya malipo?

Njia pekee ya kuwalipa hawa wadukuzini kupitia mfumo wa malipo wa siri ujulikanao kama BitCoin. Bitcoin ni mfumo wa malipo wa kielekroniki kama ilivyo PayPal ila mlipaji halipi gharama za huduma hiyo kwa kuwa mfumo huu unakwepa mifumo ya kiserikali inayotoza kodi. BitCoin iluitengenezwa na mtu alijitambulisha kama Satoshi Nakamoto mwaka 2008 na aliuweka mtandaoni mwaka 2009. Hata hivyo biidi zote za kumtambua Satoshi ni nani hazijafanikiwa hadi leo. Mfumo wa malipo wa BitCoin una uwezo wa kufanya mchakato wa malipo bila mifumo ya kibenki na serikali kutoza tozo (charges) hivyo hutumiwa sana na watu wanaoficha utambulisho wao kama magaidi, wauza madawa ya kulevya, na wengine wanaoendesha magenge ya kiuhalifu. Kwa kuwa mfumo huu unafanya kazi kwenye layer ya ndani/giza ya mtandao wa internet (Dar Web), imekua vigumu kuwakamata wahusika n ahata kufuatilia malipo yanayofanywa yanakwenda wapi. Hata hivyo wataalamu wanaonesha kwamba kuna uwezekano wakaanza kuweza kujua malipo yanapokwenda na hivyo kuwakamata wahusika.

Unawezaje kujilinda na udukuzi wa Ransomware?

Moja, usifungue kabisa email yoyote ambayo humjui mwandishi ni nani wala hukua unasubiri ujumbe wa aina hiyo. Emails zinazokuja na kirusi huyu zina ushawishi mkubwa wa kukufanya uone imetoka kwenye taasisi au mtu unayemjua hivyo umakini mkubwa unatakikana haya kwa kutokudownload file lolote au kubonyeza link itakayoonekana kwenye email hiyo. 

Pili, hakikisha umefanya windows updates kwenye kompyuta yako haraka iwezekanavyo. Mifumo iliyoshambuliwa zaidi ni za computer za Microsoft windows hivyo kila anayetumia windows XP, Windows 8, Windows Vista, na Windows 10 yuko kwenye hatari hii. Hata hivyo kwa kuwa Microsoft walishajulishwa na NSA baada ya tool yao kuibiwa mwezi wa tatu, wametengenza update patches za windows ambazo zinamzuia Eternal Blue kupenyeza na hivyo kujikinga na WannaCry. Watu wote waliofanya windows updates siku za karibuni wamejikinga na udukuzi huu kwa sehemu kubwa.

Tatu, kirusi huyu anakuja kama pop-ups kwenye browser yako hivyo usiruhusu pop-ups (don’t unblock pop-ups). Zikijika wakati una-browse zikatalie (Block them)

Ukiona dalili ya computer yako kushambuliwa, ondoa computer yako mara moja kwenye internet ili uwe salama bila kujali chanzo cha internet unachotumia.

Hakikisha computer yako ina antivirus imara na thabiti. Kumbuka free antivirus software wanazotumia watu wengi, hazina uwezo kabisa wa kupambana na udukuzi huu.

Zingatia kwamba uvamizi huu sio kwa computer na mifumo ya computer tu bali unahusu vifaa vyote vinavyotumia internet ikiwa ni pamoja na simu yako ya mkononi, tablets, PDAs, nk.

Hakikisha umefanya backup ya mafaili yako yote kwenye computer ili ukishambuliwa n ahata usipolipa bado uwe salama kwa maana ya taarifa zako.

Ushauri kwa Serikali na taasisi zake

Ninaishauri serikali hasa vyombo vyake vyote vya ulinzi na usalama wakiongozwa na usalama wa Taifa na TCRA wachukue hatua madhubutu na za haraka kulinda nchi yetu na uvamizi huu. Jambo hili ni la hatari sana kuliko maelezo na hasara yake ni kubwa. Vyombo husika vilipe tatizo hili status ya tishio la usalama wa taifa na tusingoje hadi tusikie mifumo ya BOT, TRA, Polisi, Usalama na mingine imeingiliwa ndio tuanze kutafutana. Nini wafanye?

Wataalamu wa cybersecurity wa taasisi zote za serikali na mashirika ya umma wafanye kazi ya ziada kuhakikisha serveres ziko salama na ulinzi umeimarishwa

Wataalamu wote wa ICT wa taasisi wahakikishe computers zaote kwenye ofisi na za watu bianfsi zinazotumika kwenye network zao zimefanyiwa windows updates haraka iwezekanavyo. Ninashauri serikali ichukue hatua kuwaita wataalamu wake wote wa ICT kwenda makazini kuanzia leo na kesho ili kufanya kazi hii na kusaidia mifumo kuwa salama Jumatatu watu wakiingia kazini

Computers au mifumo ambayo sio lazima kuunganishwa kwenye internet, itolewe mara moja wakati jambo hili la kiusalama linashughuliwa

TCRA wakishirikiana na vyombo vingine na media houses, watoe elimu kwa umma kwa haraka iwezekanavyo ili watu wachukue taadhari husika.

Imeandikwa na Mathew Mndeme (Mwalimu MM)
MM ni Mchambuzi wa mifumo ya kompyuta na Mtafuiti wa mifumo ya TEHAMA katika huduma za afra
Brua Pepe: mmmwalimu@gmail.com

FAHAMU Njia 16 za Kuondoa Sumu Mbalimbali Mwilini...!!!

$
0
0

Mwili unaweza kupatwa na sumu au takataka zisizohitajika na mwili kwa namna mbili, ama kupitia mazingira tunayoishi (viwanda, migodi nk) au kupitia vyakula na vinywaji ambavyo tunatumia kila siku. Sumu au taka pia zinaweza kuingia mwilini kupitia dawa mbalimbali hasa za kizungu tunazotumia kujitibia magonjwa mbalimbali.

Mwili huzalisha hizi sumu au takataka (free radicals) kila mara kunapofanyika mmeng’enyo wa chakula mwilini mwako.

Njia 16 za kuondoa sumu mbalimbali mwilini

1. Fanya mlo wako mmoja wa siku kuwa ni matunda pekee

Amua moja ya mlo wako kwa siku uwe ni matunda pekee bila chakula kingine zaidi. Unaweza kuamua ama chakula cha asubuhi au cha jioni kuwa ni matunda pekee, ndiyo kwenye sahani yako unajaza matunda tu mbalimbali sahani ijae na ule hayo tu kama ndiyo mlo wako ukimaliza unaweza kunywa juisi ya matunda au maji pekee.

2. Kula vyakula vya asili zaidi kuliko vya viwandani

Kama unataka kuepuka sumu au takataka nyingine kirahisi kuingia katika mwili wako basi pendelea zaidi kula vyakula vya asili vinavyopikwa nyumbani kuliko kula vya kwenye makopo au vya dukani au vya kwenye migahawa (fast foods).

3. Fanya masaji

Kwa bahati mbaya waTanzania wengi hawajuwi kuwa masaji ni sehemu ya tiba au ni dawa pia kwa magonjwa mengine mengi mwilini. Wengi tunaichukulia masaji kama kitu cha starehe tu (relaxation) lakini unaweza kutumia masaji kama njia mojawapo ya kuondoa sumu mwilini na utafanikiwa kwa muda mfupi sana.

4. Kunywa maji mengi kila siku

Sababu kubwa ya watu wengi kutengeneza sumu au taka mwilini mwao ni kutokunywa maji mengi kila siku. Maji ni uhai, bila kunywa maji mengi kila siku ni sawa na kwenda dukani bila hela mfukoni. Haijalishi upo mazingira gani kama ni ya baridi au ni ya joto ni LAZIMA UNYWE MAJI YA KUTOSHA KILA SIKU IENDAYO KWA MUNGU.

Unahitaji maji glasi 8 mpaka 10 kila siku. Watu wengi wanahangaika namna ya kuondoa sumu kusafisha miili yao bila kujua kuwa maji pekee ya kunywa yanatosha kwa kazi hiyo. Kumbuka asilimia 94 ya damu yako ni maji, asilimia 85 za ubongo wako ni maji, hivyo ili kusafisha damu na mwili kwa ujumla ni lazima unywe maji ya kutosha kila siku.

5. Acha chai ya rangi na Kahawa

Kama tayari imethibitika una sumu au takataka nyingi mwilini nakushauri uache kunywa chai ya rangi na kahawa. Badala yake hamia kutumia chai yenye tangawizi au mdalasini au mchaichai. Chai ya rangi na kahawa vina kaffeina ambayo kwanza huyasukuma maji nje ya mwili kwa haraka na kuuacha mwili bila kuwa na maji ya kutosha kwa ajili ya kazi zake. Kaffeina pia ni madawa ya kulevya kundi la madawa yanayosisimua mwili (stimulants drugs).

6. Fanya mazoezi ya viungo

Inashangaza sana kuona waTanzania wengi hawaoni umhimu wa kufanya mazoezi ya viungo. Mazoezi ya viungo ni jambo la lazima kama ilivyo chakula. Iwe unaumwa au huumwi, iwe una uzito kuzidi au una uzito wa kawaida hakikisha unapata muda wa kufanya mazoezi.

Mazoezi yanakusaidia kukufanya ujisikie vizuri na hivyo kukuondolea mfadhaiko au stress kirahisi zaidi, sambamba na hilo mazoezi ni dawa tosha na nzuri ya kuondoa sumu mwilini haraka zaidi. Hakikisha jasho linakutoka la kutosha na iwe ni jambo la kila mara na siyo unaenda jumamosi na jumapili (weekend) tu, hiyo haitoshi, fanya mazoezi mara 4 mpaka mara 5 kwa wiki.

7. Kula zaidi vyakula vyenye nyuzinyuzi (faiba)

Umesikia mara nyingi kwamba unahitaji kula zaidi vyakula vyenye nyuzinyuzi kwa ajili ya kuwa na afya bora, mmeng’enyo wa chakula wenye afya na hata kukusaidia kupunguza uzito. Kile ulikuwa hujuwi pengine mpaka sasa ni kuwa vyakula hivi vyenye nyuzinyuzi ni vizuri pia katika kusafisha mwili na kuondoa sumu au takataka mbalimbali.

Vyakula vyenye nyuzinyuzi nyingi ni pamoja na parachichi, ndizi, peazi, karoti, pilipili hoho, mchele wa brown (ule wanashauriwa watu wa kisukari wautumie), maharage meusi, njegele, tende, viazi vitamu, tufaa (apple), machungwa, ugali wa dona pia mkate wa unga wa ngano ambao haujakobolewa.

8. Funga kula

Ndiyo, kama ulikuwa hujuwi namna nyingine rahisi ya kuondoa au kupunguza sumu mwilini ni kufunga kula kabisa kutwa nzima. Ukifunga kula mwili unalazimika kuvitumia vile vilivyomo ndani yake bila kushughulika kuvisaga vingine vipya unavyokula. Kunapokuwa hakuna shughuli ya kuvisaga na kumeng’enya chakula kipya mwilini ndipo mwili unaweza kuondoa sumu na taka nyingine kirahisi zaidi.

Amua kufunga kula kabisa kwa wiki mara 2 hata 3 ili kuondoa au kupunguza sumu, hii inaweza kuwa pia ni njia mojawapo ya kufanya maombi na kujiweka karibu na muumba wako.

9. Pata usingizi wa kutosha kila siku

Moja ya vitu vinaweza kukupelekea kuwa na sumu mwilini au takataka nyingi ni pamoja na kutokulala muda wa kutosha kila siku. Usingizi haukopwi na huwezi kuwa na ufanisi katika kazi zako kama hupati usingizi wa kutosha kila siku.

Usingizi siyo jambo la starehe tu, ni sehemu mhimu sana katika afya yako ya kila siku. Bila kupata usingizi wa kutosha unaweza kuwa karibu na matatizo kama kuongezeka uzito, kushuka kwa kinga ya mwili na nguvu zako za mwili kwa zinaweza kushuka.

Unapopata muda wa kutosha wa kulala masaa 7 mpaka 8 kwa siku unaupa mwili wako nafasi ya kutosha ya kupumzika na kujiripea upya na hivyo ndivyo sumu na takataka nyingine zinavyoweza kukutoka kirahisi. Ingia kulala mapema walau saa tatu usiku ingia kulala siyo unakaa unaangalia tamthiliya au mpira mpaka saa sita za usiku!

10. Epuka mazingira hatarishi kwa sumu

Kuna mazingira yanajulikana wazi kuwa ni vyanzo vya sumu mwilini. Maeneo ya migodi ya madini, maeneo yenye viwanda vingi, maduka yanayouza dawa za kilimo nk

Maeneo haya yanafaa kukaa mbali na makazi ya binadamu kwa usalama wa afya zetu.

11. Tumia mtindi

Moja ya njia nyingine ya kuondoa sumu na takataka nyingine ni kutumia vyakula vyenye bakteria wazuri (probiotics). Mtindi ndicho chakula pekee kinajulikana kuwa na bakteria hawa wazuri kwa ajili ya tumbo lako. Pata mtindi kikombe kimoja kila siku na utabaki na mwili msafi muda wote. TUmia mtindi wa nyumbani ndiyo mzuri zaidi ingawa hata wa dukani nakuruhusu utumie hasa ule ambao haujaongezwa kingine chochote ndani yake (flavors and additives).

12. Epuka vyakula vilivyokobolewa

Ili kuwa na mwili msafi kabisa epuka kula mkate mweupe, sukari na vyakula vinavyopikwa katikati ya mafuta mengi kama vile chipsi, maandazi na vingine vyote vinavyochomwa katikati ya mafuta mengi.

Mkate upo mkate mweusi (brown bread), sukari ipo asali mbichi, vyakula vinavyopikwa katikati ya mafuta mengi unaweza kuamua kuwa unavioka (bake) au uvichemshe (boiling). Uchaguzi ni wako.

13. Ondoa mfadhaiko (stress)

Kile tayari unajuwa ni kuwa mfadhaiko au stress ni jambo baya kwa afya yako. Kile unatakiwa kujua kuanzia sasa ni kuwa ili kubaki na afya bora kabisa yenye TBS basi ukae mbali na stress. Kama utaruhusu stress kutawala maisha yako basi ujuwe mwili wako hauwezi kufanya kazi zake vizuri ikiwemo ya kuondoa taka au sumu mbalimbali mwilini.

Stress peke yake inaweza kupelekea magonjwa mbalimbali mwilini zaidi ya 50. Unapokuwa na mfadhaiko mwili wako hauwezi kutoa taka nje kirahisi na kinga yako ya mwili inashuka matokeo yake unakuwa karibu na magonjwa mengine mengi.

Watu wengine wenye uelewa mdogo wakiwa na stress hukimbilia kutumia vilevi wakidhani zitapungua kumbe ndiyo wanazidi kuongeza tatizo bila kujua. Vitu viwili vinaondoa stress bila kulazimika kutumia njia mbaya kwa afya yako ni mazoezi ya viungo na tendo la ndoa. Siku nyingine ukijiona umefadhaishwa sana nenda kafanye mazoezi ya kufa mtu ikiwezekana baadaye tafuta mtu shiriki tendo la ndoa.

14. Tumia dawa za asili badala ya zile za kizungu

Dawa nyingi za hospitali huwa zina matokeo chanya (positive) na matokeo hasi (negative) pia ambayo ndiyo matokeo mabaya. Kama unalazimika kutumia antibiotic kila mara au unameza dawa za kuondoa maumivu kila mara unaweza kuwa unaongeza sumu na taka mwilini bila kujua na bila sababu yoyote ya lazima.

Kuepuka hilo jaribu kutumia mitishamba au mimea ya asili kwa baadhi ya magonjwa ambayo si lazima uende hospitali. Siyo mafua tu mtu ameenda kuchoma sindano!

15. Acha vilevi

Moja ya vitu vinavyoweza kuleta sumu au taka mwilini moja kwa moja ni vilevi. Vilevi kama pombe, madawa ya kulevya, sigara, bangi na vinginevyo ni vitu vinavyopelekea mwili kuwa na taka moja kwa moja.

Namna pekee ya kuondoa sumu kutokana na vilevi ni kuviacha hivyo vilevi, ndiyo kuviacha. Usitegemee asubuhi utumie dawa kuondoa sumu mwilini halafu jioni ukanywe pombe au ukavute sigara utegemee tu ile dawa uliyotumia asubuhi kwamba itafanya kazi, hapana unajidanganya, dawa ni kuacha vilevi moja kwa moja.

Vingine vya kuacha kama tayari imegundulika una sumu nyingi mwilini ni pamoja na vinywaji baridi vyote, juisi zote za dukani, chai ya rangi na kahawa.

16. Tumia vifuatavyo kuondoa sumu zaidi

Vifuatavyo vinaondoa sumu kirahisi zaidi mwilini; kitunguu swaumu, unga wa majani ya mlonge na mbegu zake na mbegu za maboga au unga wake. Kitunguu swaumu  Mlonge  Mbegu za maboga
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live




Latest Images